the_legend
JF-Expert Member
- Jan 14, 2019
- 1,611
- 7,063
- Thread starter
- #121
RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI.
MTUNZI : ALEX KILEO.
SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE.
______________
ILIPOISHIA...
______________
"nibusu basi ili nishinde vizuri mwenzio" mtoto wa mchungaji akaongea kwa mahaba.
"kesho rafiki yangu, hivi huogopi kusema hayo maneno katika nyumba takatifu kama hii?" kayoza akamjibu kwa busara,
"si unibusu jamani wewe." yule binti akakomalia kwa sauti ya juu kidogo.
"unamwambia nani akubusu?" Mchungaji Wingo aliuliza huku akiwa anaingia Sebuleni.....
____________
ENDELEA..,.
_____________
..."hakuna kitu baba" binti mchungajibu akajibu.
"kwa hiyo nimesikia vibaya?" Mchungaji Wingo akauliza huku anamuangalia binti yake.
"nilikuwa namsimulia filamu moja hivi ilioneshwa jana ." binti wa Mchungaji akajibu huku akiangalia chini kwa aibu,
"Umekalia kuangalia filamu tu, badala ukazane kusoma biblia ili uongeze imani unakalia kuongeza ujinga tu" Mchungaji Wingo alimwambia binti yake aliyekuwa amesimama mbele yake
"Nisamehe baba, ila hiyo filamu ilikuwa na Mafundisho tu mazuri" Binti Mchungaji alijitetea,
"Ebu tupishe bwana" Mchungaji Wingo akamwambia mwanae na binti akaondoka haraka,
"Huyu mwanangu ni muongeaji sana, yupo tofauti na wenzake kabisa" Mchungaji Wingo aliongea huku akimgeukia Kayoza na usoni akikunjua tabasamu,
"Ila ni mcheshi sana, yaani amenizoea muda mfupi sana" Kayoza nae alijibu,
Kisha mchungaji na kayoza wakawa wanaongea, ila jambo kubwa ambalo mchungaji alimsisitiza Kayoza asikose katika maombi ya usiku.
Kayoza akarejea kwao kujumuika na mama yake.
"vipi mwenzetu, mchungaji alikuwa anakuambia nini?" mama kayoza alimuuliza mwanae.
"tulikua tunaongea mambo ya kawaida tu" kayoza akajibu.
Kisha mama kayoza akaenda jikoni kutayarisha chakula.
"eh, mwana leo nimekutana na vituko" Kayoza alianza namna hiyo kumuelezea Omari.
"wapi tena shee" Omari akauliza kwa shauku .
"si kwa mchungaji mwanangu, kuna binti yake mkubwa amedata na flag yangu"Kayoza aliongea huku akitabasamu
"kwa hiyo unataka kufanyaje?" Omari akauliza huku amekunja sura.
"nitafanyaje ndugu yangu, na hili dubwana linanibana" Kayoza alijibu kwa upole
"aah, ok, we mshiti au kama ana mahamu nitajaribu kumseti mimi" Omari aliongea, na kusababisha wote wakacheka.
"Poa mi ntakupigia pande, we si mwanangu bwana" Kayoza aliongea huku akicheka...
*****************
Sajenti Minja hakwenda kupima, alimfuatilia mkubwa wake mpaka alipomuona anapanda gari na kuondoka, naye akarudi ndani moja kwa moja hadi katika kitanda cha msaidizi wa mganga..
"vipi, unaweza kukaa" Sajenti Minja alimuuliza yule msaidizi wa mganga.
"kwanini nisiweze?, naweza tu" Msaidizi wa mganga akajibu,
"kuna maswali machache nataka nikuulize" Sajenti Minja akaongea kwa upole.
"kwani wewe ni polisi" Msaidizi wa mganga aliuliza ili apate uhakika, kwa sababu alimuhisi.
"ndio" sajenti Minja alijibu.
"sasa unataka kuniuliza nini wakati tulikuwa wote kuanzia mwanzo hadi mwisho" Msaidizi wa mganga alijibu huku akionekana akimshangaa Sajenti Minja,
"najua ndugu yangu, ila naomba unisaidie kitu kimoja" Sajenti Minja aliongea huku akisubiri sauti itakayomruhusu aendelee .
"endelea" Msaidizi wa mganga alijibu.
"naomba polisi yeyote atakaekuuliza kuhusu yale mambo yaliyötokea kule, mjibu hujui chochote, sawa?" Sajenti Minja aliwasilisha ombi lake huku akiwa hana uhakika wa kukubaliwa,
"kwanini tufiche ukweli?" Msaidizi wa mganga aliuliza kwa mshangao,
"Ukiongea ukweli utakuwa umeniharibia kila kitu katika maisha yangu, yaani hata kufungwa nitafungwa" Sajenti Minja aliongea kwa huruma ili kumshawishi Msaidizi wa Mganga akubaliane nae,
"Kwa maana hiyo wewe umependa lile tukio lililotokea siku ile?" Msaidizi wa Mganga alimuuliza Sajenti Minja,
"Tukio sasa, maana yalikuwa mengi" Sajenti Minja aliuliza,
"La wenzangu kuuawa kinyama?" Msaidizi wa Mganga aliuliza,
"Hapana, nitalifurahia vipi wakati lilikuja kuharibu tiba ya ndugu yangu na nikampoteza mtu ambaye ndiye nilikuwa nategemea yeye atamponya ndugu yangu?" Sajenti Minja aliongea kwa upole na machozi yakimtoka kwa mbali ili kumshawishi tu Msaidizi wa Mganga asiseme ukweli mbele ya Polisi wengine,
"Sasa kwanini nifiche?" Msaidizi wa Mganga akauliza tena ila kipindi hiki aliuliza kwa upole,
"Kuwa na utu ndugu yangu, maana unachotaka kukifanya ni kuniharibia maisha tu" Sajenti Minja aliendelea kumlalamikia Msaidizi wa Mganga,
"Sio nakuharibia maisha, mbona mimi maisha yangu yameshaharibika?" Msaidizi wa Mganga aliongea huku anamkodolea macho Sajenti Minja,
"Yameharibikaje sasa wakati upon hai na upon huru?" Sajenti Minja alimuuliza,
"Hill sio tatizo, tatizo ni kwamba yule Mganga nilimchukulia kama mkombozi wangu kutokana na maisha yangu" Msaidizi wa Mganga aliongea,
" kivipi yaani?" Sajenti Minja alimuuliza,
"Yaani nilikuwa sina mbele wala nyuma, ila yule mzee aliniokota tu mjini na kunichukua kisha akawa ananifundisha uganga na akawa ananipa kipato kidogo angalau nikajiona mtu" Msaidizi wa Mganga aliongea,
"Hilo sio tatizo, ngoja upone tutaongea zaidi, mimi nitakusaidia" Sajenti Minja aliongea kwa huruma huku akichomoa noti nyingi kutoka katika mfuko wake wa suruali na kumpa msaidizi wa Mganga,
"Za nini hizi?" Msaidizi wa Mganga aliuliza huku akiwa anaziangalia zile hela akiwa hataki kuzipokea,
"Zitakusaidia kununua vitu vidogo vidogo kipindi upo hapa Hospitali" Sajenti Minja aliongea huku akiwa bado amezishikilia zile pesa,
"Wewe ni ndugu yangu bwana, tusaidiane" Sajenti Minja aliongea kwa upole,
"Ngoja nitoke hospitali tutaongea vizuri ndugu yangu" Msaidizi wa Mganga aliongea huku akizitia pesa zile mfukoni,
"Nikununulie chakula gani kabla sijaondoka" Sajenti Minja alimuuliza,
"Chochote tu, mimi mswahili bwana sichaguagi chakula" msaidizi wa Mganga aliongea,
"Wewe mgonjwa bwana, itabidi ule minyama nyama, ngoja nikakutafutie kuku bosi" Sajenti Minja aliongea kwa furaha huku akitoka nje na akiamini tayari ameshamteka hisia yule Msaidizi wa Mganga.
**"***********
Babu wa monchwari alivyopigwa ule mtama ile asubuhi kumbe aliteguka mguu maeneo ya nyuma ya paja chini ya kiuno ila alivumilia na hakuwaambia kitu chochote wale polisi kwa sababu walikuwa na hasira muda ule, ila ilivyofika jioni maumivu yalimzidia na Babu wa monchwari akawaambia polisi ila walimpuuza tu, masikini Babu wa watu maumivu yalimzidia mpaka akawa Amalia kwa sauti kubwa kama mtoto, kilio kikamfikia mkuu wa polisi na kuja kuangalia kuna nini,
" mbona huyo mzee analia?" Mkuu wa polisi aliwauliza askari aliowakuta hapo ambayo walibaki wakitazamana bila kutoa jibu,
"Anamaumivu nadhani" Askari mmoja alijibu,
"Babu una tatizo gani?" Mkuu wa Polisi aliamua amuulize mwenyewe,
"Mguu nahisi umevunjika, nawaambia wanisaidie ila wananitukana" Babu alijibu huku akiendelea kulia,
"Umevunjikaje, umeanguka?" Mkuu wa Polisi aliuliza,
"Hao wenyewe walinipiga asubuhi" Babu alijibu,
"Hata mambo ya kuwapiga watuhumuwa si tulishawakataza?, tena mnampiga mzee kabisa..ebu chukueni gari ya doria mumpeleke hospitali" Mkuu wa Polisi aliongea kwa ukali na vijana wake wakanyanyuka haraka,
"Kwani yupo hapa kwa kosa gani" Mkuu wa polisi akauliza,
"Huyu ndiye yule mlinzi wa monchwari" Askari mmoja akajibu,
"Hata mumpeleke hospitali akapatiwe matibabu na mumrudishe hapa," Mkuu wa polisi aliongea na kuondoka huku akiwaacha vijana wake wakimbeba Babu monchwari na kumpeleka kwenye gari na safari ya hospitali ikaanza.
Iliwachukua dakika chache kufika hospitali, walimshusha Babu na kumpeleka kupata matibabu.
Babu akapatiwa huduma kisha kwa Saa nzima na akaonekana ni mfupa tu ulikuwa umehama eneo lake, madaktari wakafanya jitihada na kumtibu bila tatizo na kuwaruhusu askari waondoke nae.
Askari walipotoka nje walienda moja kwa moja mpaka kwenye gari yao, wakapanda gari ili warudi kituoni, kwa bahati mbaya gari yao ilipata itilafu ikawa haiwaki, ikabidi wapige simu kwa mkuu wao ili wapate msaada, mkuu wao akawapa namba ya sajenti Minja na kuwaambia yuko pale hospitali kwa hiyo wampigie awape msaada wa kuwarudisha kituoni kwa maana Sajenti ana gari.
Sajenti Minja baada ya kupigiwa simu akawaelekeza mahali gari lake lilipo, wale askari na Babu wa mochwari wakafika mahali gari lilipo, kisha wakawa wanamsubiri sajenti Minja atoke ndani ili awarudishe kituoni, na Babu wa monchwari ndio kabisa alikuwa anaangalia katika mlango wa kutokea hospitali ambayo ndio njia anayokuja nayo Sajenti Minja..
***"***"ITAENDELEA******""
*Kwa Mara nyingine tena Sajenti Minja anakutana na mtihani wa kukutanishwa na Babu wa monchwari, je nini kitatokea?
the Legend☆
MTUNZI : ALEX KILEO.
SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE.
______________
ILIPOISHIA...
______________
"nibusu basi ili nishinde vizuri mwenzio" mtoto wa mchungaji akaongea kwa mahaba.
"kesho rafiki yangu, hivi huogopi kusema hayo maneno katika nyumba takatifu kama hii?" kayoza akamjibu kwa busara,
"si unibusu jamani wewe." yule binti akakomalia kwa sauti ya juu kidogo.
"unamwambia nani akubusu?" Mchungaji Wingo aliuliza huku akiwa anaingia Sebuleni.....
____________
ENDELEA..,.
_____________
..."hakuna kitu baba" binti mchungajibu akajibu.
"kwa hiyo nimesikia vibaya?" Mchungaji Wingo akauliza huku anamuangalia binti yake.
"nilikuwa namsimulia filamu moja hivi ilioneshwa jana ." binti wa Mchungaji akajibu huku akiangalia chini kwa aibu,
"Umekalia kuangalia filamu tu, badala ukazane kusoma biblia ili uongeze imani unakalia kuongeza ujinga tu" Mchungaji Wingo alimwambia binti yake aliyekuwa amesimama mbele yake
"Nisamehe baba, ila hiyo filamu ilikuwa na Mafundisho tu mazuri" Binti Mchungaji alijitetea,
"Ebu tupishe bwana" Mchungaji Wingo akamwambia mwanae na binti akaondoka haraka,
"Huyu mwanangu ni muongeaji sana, yupo tofauti na wenzake kabisa" Mchungaji Wingo aliongea huku akimgeukia Kayoza na usoni akikunjua tabasamu,
"Ila ni mcheshi sana, yaani amenizoea muda mfupi sana" Kayoza nae alijibu,
Kisha mchungaji na kayoza wakawa wanaongea, ila jambo kubwa ambalo mchungaji alimsisitiza Kayoza asikose katika maombi ya usiku.
Kayoza akarejea kwao kujumuika na mama yake.
"vipi mwenzetu, mchungaji alikuwa anakuambia nini?" mama kayoza alimuuliza mwanae.
"tulikua tunaongea mambo ya kawaida tu" kayoza akajibu.
Kisha mama kayoza akaenda jikoni kutayarisha chakula.
"eh, mwana leo nimekutana na vituko" Kayoza alianza namna hiyo kumuelezea Omari.
"wapi tena shee" Omari akauliza kwa shauku .
"si kwa mchungaji mwanangu, kuna binti yake mkubwa amedata na flag yangu"Kayoza aliongea huku akitabasamu
"kwa hiyo unataka kufanyaje?" Omari akauliza huku amekunja sura.
"nitafanyaje ndugu yangu, na hili dubwana linanibana" Kayoza alijibu kwa upole
"aah, ok, we mshiti au kama ana mahamu nitajaribu kumseti mimi" Omari aliongea, na kusababisha wote wakacheka.
"Poa mi ntakupigia pande, we si mwanangu bwana" Kayoza aliongea huku akicheka...
*****************
Sajenti Minja hakwenda kupima, alimfuatilia mkubwa wake mpaka alipomuona anapanda gari na kuondoka, naye akarudi ndani moja kwa moja hadi katika kitanda cha msaidizi wa mganga..
"vipi, unaweza kukaa" Sajenti Minja alimuuliza yule msaidizi wa mganga.
"kwanini nisiweze?, naweza tu" Msaidizi wa mganga akajibu,
"kuna maswali machache nataka nikuulize" Sajenti Minja akaongea kwa upole.
"kwani wewe ni polisi" Msaidizi wa mganga aliuliza ili apate uhakika, kwa sababu alimuhisi.
"ndio" sajenti Minja alijibu.
"sasa unataka kuniuliza nini wakati tulikuwa wote kuanzia mwanzo hadi mwisho" Msaidizi wa mganga alijibu huku akionekana akimshangaa Sajenti Minja,
"najua ndugu yangu, ila naomba unisaidie kitu kimoja" Sajenti Minja aliongea huku akisubiri sauti itakayomruhusu aendelee .
"endelea" Msaidizi wa mganga alijibu.
"naomba polisi yeyote atakaekuuliza kuhusu yale mambo yaliyötokea kule, mjibu hujui chochote, sawa?" Sajenti Minja aliwasilisha ombi lake huku akiwa hana uhakika wa kukubaliwa,
"kwanini tufiche ukweli?" Msaidizi wa mganga aliuliza kwa mshangao,
"Ukiongea ukweli utakuwa umeniharibia kila kitu katika maisha yangu, yaani hata kufungwa nitafungwa" Sajenti Minja aliongea kwa huruma ili kumshawishi Msaidizi wa Mganga akubaliane nae,
"Kwa maana hiyo wewe umependa lile tukio lililotokea siku ile?" Msaidizi wa Mganga alimuuliza Sajenti Minja,
"Tukio sasa, maana yalikuwa mengi" Sajenti Minja aliuliza,
"La wenzangu kuuawa kinyama?" Msaidizi wa Mganga aliuliza,
"Hapana, nitalifurahia vipi wakati lilikuja kuharibu tiba ya ndugu yangu na nikampoteza mtu ambaye ndiye nilikuwa nategemea yeye atamponya ndugu yangu?" Sajenti Minja aliongea kwa upole na machozi yakimtoka kwa mbali ili kumshawishi tu Msaidizi wa Mganga asiseme ukweli mbele ya Polisi wengine,
"Sasa kwanini nifiche?" Msaidizi wa Mganga akauliza tena ila kipindi hiki aliuliza kwa upole,
"Kuwa na utu ndugu yangu, maana unachotaka kukifanya ni kuniharibia maisha tu" Sajenti Minja aliendelea kumlalamikia Msaidizi wa Mganga,
"Sio nakuharibia maisha, mbona mimi maisha yangu yameshaharibika?" Msaidizi wa Mganga aliongea huku anamkodolea macho Sajenti Minja,
"Yameharibikaje sasa wakati upon hai na upon huru?" Sajenti Minja alimuuliza,
"Hill sio tatizo, tatizo ni kwamba yule Mganga nilimchukulia kama mkombozi wangu kutokana na maisha yangu" Msaidizi wa Mganga aliongea,
" kivipi yaani?" Sajenti Minja alimuuliza,
"Yaani nilikuwa sina mbele wala nyuma, ila yule mzee aliniokota tu mjini na kunichukua kisha akawa ananifundisha uganga na akawa ananipa kipato kidogo angalau nikajiona mtu" Msaidizi wa Mganga aliongea,
"Hilo sio tatizo, ngoja upone tutaongea zaidi, mimi nitakusaidia" Sajenti Minja aliongea kwa huruma huku akichomoa noti nyingi kutoka katika mfuko wake wa suruali na kumpa msaidizi wa Mganga,
"Za nini hizi?" Msaidizi wa Mganga aliuliza huku akiwa anaziangalia zile hela akiwa hataki kuzipokea,
"Zitakusaidia kununua vitu vidogo vidogo kipindi upo hapa Hospitali" Sajenti Minja aliongea huku akiwa bado amezishikilia zile pesa,
"Wewe ni ndugu yangu bwana, tusaidiane" Sajenti Minja aliongea kwa upole,
"Ngoja nitoke hospitali tutaongea vizuri ndugu yangu" Msaidizi wa Mganga aliongea huku akizitia pesa zile mfukoni,
"Nikununulie chakula gani kabla sijaondoka" Sajenti Minja alimuuliza,
"Chochote tu, mimi mswahili bwana sichaguagi chakula" msaidizi wa Mganga aliongea,
"Wewe mgonjwa bwana, itabidi ule minyama nyama, ngoja nikakutafutie kuku bosi" Sajenti Minja aliongea kwa furaha huku akitoka nje na akiamini tayari ameshamteka hisia yule Msaidizi wa Mganga.
**"***********
Babu wa monchwari alivyopigwa ule mtama ile asubuhi kumbe aliteguka mguu maeneo ya nyuma ya paja chini ya kiuno ila alivumilia na hakuwaambia kitu chochote wale polisi kwa sababu walikuwa na hasira muda ule, ila ilivyofika jioni maumivu yalimzidia na Babu wa monchwari akawaambia polisi ila walimpuuza tu, masikini Babu wa watu maumivu yalimzidia mpaka akawa Amalia kwa sauti kubwa kama mtoto, kilio kikamfikia mkuu wa polisi na kuja kuangalia kuna nini,
" mbona huyo mzee analia?" Mkuu wa polisi aliwauliza askari aliowakuta hapo ambayo walibaki wakitazamana bila kutoa jibu,
"Anamaumivu nadhani" Askari mmoja alijibu,
"Babu una tatizo gani?" Mkuu wa Polisi aliamua amuulize mwenyewe,
"Mguu nahisi umevunjika, nawaambia wanisaidie ila wananitukana" Babu alijibu huku akiendelea kulia,
"Umevunjikaje, umeanguka?" Mkuu wa Polisi aliuliza,
"Hao wenyewe walinipiga asubuhi" Babu alijibu,
"Hata mambo ya kuwapiga watuhumuwa si tulishawakataza?, tena mnampiga mzee kabisa..ebu chukueni gari ya doria mumpeleke hospitali" Mkuu wa Polisi aliongea kwa ukali na vijana wake wakanyanyuka haraka,
"Kwani yupo hapa kwa kosa gani" Mkuu wa polisi akauliza,
"Huyu ndiye yule mlinzi wa monchwari" Askari mmoja akajibu,
"Hata mumpeleke hospitali akapatiwe matibabu na mumrudishe hapa," Mkuu wa polisi aliongea na kuondoka huku akiwaacha vijana wake wakimbeba Babu monchwari na kumpeleka kwenye gari na safari ya hospitali ikaanza.
Iliwachukua dakika chache kufika hospitali, walimshusha Babu na kumpeleka kupata matibabu.
Babu akapatiwa huduma kisha kwa Saa nzima na akaonekana ni mfupa tu ulikuwa umehama eneo lake, madaktari wakafanya jitihada na kumtibu bila tatizo na kuwaruhusu askari waondoke nae.
Askari walipotoka nje walienda moja kwa moja mpaka kwenye gari yao, wakapanda gari ili warudi kituoni, kwa bahati mbaya gari yao ilipata itilafu ikawa haiwaki, ikabidi wapige simu kwa mkuu wao ili wapate msaada, mkuu wao akawapa namba ya sajenti Minja na kuwaambia yuko pale hospitali kwa hiyo wampigie awape msaada wa kuwarudisha kituoni kwa maana Sajenti ana gari.
Sajenti Minja baada ya kupigiwa simu akawaelekeza mahali gari lake lilipo, wale askari na Babu wa mochwari wakafika mahali gari lilipo, kisha wakawa wanamsubiri sajenti Minja atoke ndani ili awarudishe kituoni, na Babu wa monchwari ndio kabisa alikuwa anaangalia katika mlango wa kutokea hospitali ambayo ndio njia anayokuja nayo Sajenti Minja..
***"***"ITAENDELEA******""
*Kwa Mara nyingine tena Sajenti Minja anakutana na mtihani wa kukutanishwa na Babu wa monchwari, je nini kitatokea?
the Legend☆