the_legend
JF-Expert Member
- Jan 14, 2019
- 1,611
- 7,063
- Thread starter
- #161
RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI.
MTUNZI : ALEX KILEO.
SEHEMU YA THELATHINI NA TATU.
______________
ILIPOISHIA...
______________
Mchungaji Wingo aliporudi nyumbani kwake, akakuta mlango wa mbele uko wazi, video sebuleni inawaka, akamuita binti yake, lakini hakupata jibu, akaamua aende akamuangalie chumbani kwake, alipokaribia mlango wa chumba cha binti yake, alisikia mlio wa kitanda cha binti yake kikilalamika kwa fujo,
"mh..", mchungaji Wingo aliguna...
______________
ENDELEA.....
_______________
...mh", mchungaji aliguna, kisha akagonga mlango, mlio wa kitanda ukakoma, kisha ukimya ukatawala,
we happy", Mchungaji Wingo akamuita binti yake,
"abee baba", happy akaitika,"una shughuli gani umo ndani?", Mchungaji Wingo akamuuliza, kimya kikatawala tena, ila cha sasa hivi kilikuwa kirefu kidogo,
"mbona hujibu?", Mchungaji Wingo akauliza baada ya ukimya,
"nilikuwa naa...naa...naa.., sijakusikia ulichosema baba", Happy akashindwa kujibu akawa anajiuma uma tu,
"nimekuuliza una shughuli gani umo ndani, mbona kitanda kinapiga kelele hivyo?", Mchungaji Wingo akarudia swali katika sauti ya ukali,
"nafunga neti baba", happy akajibu huku sauti ikiwa na wasiwasi,"neti tu, ndo kitanda kipige kelele namna hiyo?", Mchungaji Wingo aliongea huku akiwa anarudi sebuleni, pia alionekana hakuridhishwa na jibu la binti yake
.***************
Ndani baada ya kusikia mtu anagonga hodi, wote walishtuka, ila hawakukurupuka, wakatulia tuli, baada ya kugundua kuwa anaegonga ni mchungaji, happy aliteremka chini taratibu kisha akavaa kanga yake, akawa anamjibu baba yake, kipindi hicho chote, Omari alikuwa anajing'ang'aniza kupita dirishani bila mafanikio, baada ya majibizano ya muda mfupi, kati ya happy na baba yake, Mchungaji aliondoka mlangoni kwa happy, hapo ndipo Omari akapata sauti,
"Sasa nitatokaje nje?", Omari alimuuliza happy kwa sauti ya chini sana,
"subiri kidogo, sasa hivi anaenda kuoga", Happy alimtoa Omari hofu.
"Happy umeniponza mwenzio" Omary aliongea huku akitaka kulia,
"Acha ujinga wewe, kwani baba amejua kinachoendelea?" Happy aliuliza kwa ukali,
"Hata kama hajui, wewe unadhani nitatokaje nje?" Omary aliuliza huku akiwa anafunga vifungo vya shati yake,
"Si nimekwambia ataenda kuoga muda si mrefu" Happy aliongea,
"Sasa mimi nitaaminije?" Omary alijikuta anauliza swali la kipuuzi,
"Mimi hapa ni kwetu, najua ratiba za watu wote hapa, ebu niamini acha ujinga" Happy alimuelewesha Omary.
"Dah, tamaa nyingine mbaya sana" Omary aliongea peke yake huku akijifuta jasho ingawa ndani hakukuwa na hali ya joto,
"Unasemaje" Happy alimuuliza Omary baada ya kumuona akiongea ingawa hakumuelewa,
"Sijasema kitu bwana" Omary alijibu huku akionekana ana hasira I logic hang any in an a na hofu.
"Mwenzangu ushaanza kuwa chizi" Happy aliongea huku akimcheka Omary chinichini.
*********************
Mchungaji Wingo alipotoka mlangoni kwa binti yake, alienda sebuleni, kisha akazima luninga, alafu akamuita happy,
"Umeshamaliza kufunga chandarua?" Mchungaji Wingo alimuuliza binti yake,
"Tayari, alafu sijisikii vzuri" Happy alimwambia baba yake,
"Kwa hiyo umehisi itakuwa malaria na ndio maana ukafunga chandarua?" Mchungaji Wingo aliuliza huku akitabasamu,
"Ndio hivyo, mimi nadhani itakuwa ni malaria tu" Happy alijibu huku nae akitabasamu,
"Kuna maji ya moto?" Mchungaji Wingo aliamua kubadili mada,
"Ndio, yapo...yatakosaje wakati najua watumiaji mpo?" Happy aliuliza,
"Ebu niandalie nikaoge mie" Mchungaji Wingo aliongea huku akinyanyuka,
"Sawa mzee" Happy alijibu,
"Mama bado hajarudi?" Mchungaji Wingo aliuliza huku akisimama,
"Wakiendaga mjini wanawahigi kurudi kwani?, hiyo ni mpaka saa kumi na mbili jioni" Happy alijibu baba yake,
"Huyu nae bwana, si ahache kwenda uwage unaenda wewe?, yeye ameshaanza kuzeeka" Mchungaji Wingo aliongea kwa kulalamika,
"Wivu tu huo, muache aendage yeye, maana ndio anajua mahitaji ya watoto" Happy aliongea wakati baba yake anaelekea chumbani.
Happy akaenda bafuni akachukua ndoo na kwenda nayo jikoni ambapo aliiwekea maji ya moto na kuirudisha tena bafuni.
"Maji yapo tayari baba" Happy alipaza sauti kumwambia baba yake aliyekuwepo chumbani,
"Oooh nakuja, umeshayachanganya na maji ya baridi?" Mchungaji Wingo aliuliza huku bado akiwa ndani,
"Utachanganya mwenyewe, maana Jana nilivyokuchanganyia ulilalama nimezidisha ubaridi" Happy alimwambia baba yake,
"Bora hujachanganya, maana Sikh hizi nahitaji maji ya uvugu vugu mkali kidogo" Mchungaji Wingo aliongea huku bado akiwa chumbani,
"Umeshaanza kuzeeka ndio maana unataka maji yenye joto Kali" Happy alimwambia Baba yake huku akiwa bado amesimama mlangoni,
"Kweli aisee, naona umri unanitupa mkono" Mchungaji Wingo aliongea huku akitoka ndani akiwa amejifunga taulo lake kiunoni na moja kwa moja akanyoosha mpaka bafuni.
Alipoingia, akatoa taulo lake mwilini,
"mh..kumbe sabuni imeisha?", mchungaji aliongea peke yake, baada ya kuangalia sehemu ya kuwekea sabuni ikiwa tupu mule bafuni,
Mchungaji Wingo akakata shauri la kurudi kutoka bafuni na kurudi chumbani ambapo ndipo huifadhi sabuni nyingine.
********************
Happy Binti Mchungaji alipoona kuwa baba yake kaingia bafuni, akaingia chumbani haraka,
"Tayari baba ameingia bafuni, twende nikutoe nje" Happy aliongea kwa sauti ya chini ambayo ilisikika vyema masikioni mpwa Omary,
''Sasa njia tunayotokea si ndipo lilipo bafu, akisikia hatua za watu wawili zinatembea si atagutuka?" Omary alimuuliza happy Binti Mchungaji,
"Hawezi kugundua bwana, twende acha uoga" Happy aliendelea kumwambia Omary,
"Sasa si bora nisubiri Stoke bafuni aende chumbani?" Omary aliuliza,
"Acha ujinga, mama anarudi sasa hivi na wadogo zangu, wakikukuta humu, je itakuwaje?" Happy nae aliuliza,
"He!!!! Leo kweli siku yangu, haya twende" Omary aliongea kinyonge huku akisikitika.
Happy akamshika mkono Omary, kisha akaanza kutoka nae nje kwa mwendo wa kunyata, yaani mwendo wa taratibu usiokuwa na vishindo.
Walipofika usawa wa mlango wa baf na ndio muda huo Mchungaji Wingo alikuwa anafungua mlango ili akachukue sabuni chumbani.
Ghafla tu Omary na Happy binti Mchungaji wakashuhudia mlango wa bafu ukifunguliwa na wote macho yakawatoka pima mithili ya mtu aliekwamwa na kitu kooni...
********ITAENDELEA********
the Legend☆
MTUNZI : ALEX KILEO.
SEHEMU YA THELATHINI NA TATU.
______________
ILIPOISHIA...
______________
Mchungaji Wingo aliporudi nyumbani kwake, akakuta mlango wa mbele uko wazi, video sebuleni inawaka, akamuita binti yake, lakini hakupata jibu, akaamua aende akamuangalie chumbani kwake, alipokaribia mlango wa chumba cha binti yake, alisikia mlio wa kitanda cha binti yake kikilalamika kwa fujo,
"mh..", mchungaji Wingo aliguna...
______________
ENDELEA.....
_______________
...mh", mchungaji aliguna, kisha akagonga mlango, mlio wa kitanda ukakoma, kisha ukimya ukatawala,
we happy", Mchungaji Wingo akamuita binti yake,
"abee baba", happy akaitika,"una shughuli gani umo ndani?", Mchungaji Wingo akamuuliza, kimya kikatawala tena, ila cha sasa hivi kilikuwa kirefu kidogo,
"mbona hujibu?", Mchungaji Wingo akauliza baada ya ukimya,
"nilikuwa naa...naa...naa.., sijakusikia ulichosema baba", Happy akashindwa kujibu akawa anajiuma uma tu,
"nimekuuliza una shughuli gani umo ndani, mbona kitanda kinapiga kelele hivyo?", Mchungaji Wingo akarudia swali katika sauti ya ukali,
"nafunga neti baba", happy akajibu huku sauti ikiwa na wasiwasi,"neti tu, ndo kitanda kipige kelele namna hiyo?", Mchungaji Wingo aliongea huku akiwa anarudi sebuleni, pia alionekana hakuridhishwa na jibu la binti yake
.***************
Ndani baada ya kusikia mtu anagonga hodi, wote walishtuka, ila hawakukurupuka, wakatulia tuli, baada ya kugundua kuwa anaegonga ni mchungaji, happy aliteremka chini taratibu kisha akavaa kanga yake, akawa anamjibu baba yake, kipindi hicho chote, Omari alikuwa anajing'ang'aniza kupita dirishani bila mafanikio, baada ya majibizano ya muda mfupi, kati ya happy na baba yake, Mchungaji aliondoka mlangoni kwa happy, hapo ndipo Omari akapata sauti,
"Sasa nitatokaje nje?", Omari alimuuliza happy kwa sauti ya chini sana,
"subiri kidogo, sasa hivi anaenda kuoga", Happy alimtoa Omari hofu.
"Happy umeniponza mwenzio" Omary aliongea huku akitaka kulia,
"Acha ujinga wewe, kwani baba amejua kinachoendelea?" Happy aliuliza kwa ukali,
"Hata kama hajui, wewe unadhani nitatokaje nje?" Omary aliuliza huku akiwa anafunga vifungo vya shati yake,
"Si nimekwambia ataenda kuoga muda si mrefu" Happy aliongea,
"Sasa mimi nitaaminije?" Omary alijikuta anauliza swali la kipuuzi,
"Mimi hapa ni kwetu, najua ratiba za watu wote hapa, ebu niamini acha ujinga" Happy alimuelewesha Omary.
"Dah, tamaa nyingine mbaya sana" Omary aliongea peke yake huku akijifuta jasho ingawa ndani hakukuwa na hali ya joto,
"Unasemaje" Happy alimuuliza Omary baada ya kumuona akiongea ingawa hakumuelewa,
"Sijasema kitu bwana" Omary alijibu huku akionekana ana hasira I logic hang any in an a na hofu.
"Mwenzangu ushaanza kuwa chizi" Happy aliongea huku akimcheka Omary chinichini.
*********************
Mchungaji Wingo alipotoka mlangoni kwa binti yake, alienda sebuleni, kisha akazima luninga, alafu akamuita happy,
"Umeshamaliza kufunga chandarua?" Mchungaji Wingo alimuuliza binti yake,
"Tayari, alafu sijisikii vzuri" Happy alimwambia baba yake,
"Kwa hiyo umehisi itakuwa malaria na ndio maana ukafunga chandarua?" Mchungaji Wingo aliuliza huku akitabasamu,
"Ndio hivyo, mimi nadhani itakuwa ni malaria tu" Happy alijibu huku nae akitabasamu,
"Kuna maji ya moto?" Mchungaji Wingo aliamua kubadili mada,
"Ndio, yapo...yatakosaje wakati najua watumiaji mpo?" Happy aliuliza,
"Ebu niandalie nikaoge mie" Mchungaji Wingo aliongea huku akinyanyuka,
"Sawa mzee" Happy alijibu,
"Mama bado hajarudi?" Mchungaji Wingo aliuliza huku akisimama,
"Wakiendaga mjini wanawahigi kurudi kwani?, hiyo ni mpaka saa kumi na mbili jioni" Happy alijibu baba yake,
"Huyu nae bwana, si ahache kwenda uwage unaenda wewe?, yeye ameshaanza kuzeeka" Mchungaji Wingo aliongea kwa kulalamika,
"Wivu tu huo, muache aendage yeye, maana ndio anajua mahitaji ya watoto" Happy aliongea wakati baba yake anaelekea chumbani.
Happy akaenda bafuni akachukua ndoo na kwenda nayo jikoni ambapo aliiwekea maji ya moto na kuirudisha tena bafuni.
"Maji yapo tayari baba" Happy alipaza sauti kumwambia baba yake aliyekuwepo chumbani,
"Oooh nakuja, umeshayachanganya na maji ya baridi?" Mchungaji Wingo aliuliza huku bado akiwa ndani,
"Utachanganya mwenyewe, maana Jana nilivyokuchanganyia ulilalama nimezidisha ubaridi" Happy alimwambia baba yake,
"Bora hujachanganya, maana Sikh hizi nahitaji maji ya uvugu vugu mkali kidogo" Mchungaji Wingo aliongea huku bado akiwa chumbani,
"Umeshaanza kuzeeka ndio maana unataka maji yenye joto Kali" Happy alimwambia Baba yake huku akiwa bado amesimama mlangoni,
"Kweli aisee, naona umri unanitupa mkono" Mchungaji Wingo aliongea huku akitoka ndani akiwa amejifunga taulo lake kiunoni na moja kwa moja akanyoosha mpaka bafuni.
Alipoingia, akatoa taulo lake mwilini,
"mh..kumbe sabuni imeisha?", mchungaji aliongea peke yake, baada ya kuangalia sehemu ya kuwekea sabuni ikiwa tupu mule bafuni,
Mchungaji Wingo akakata shauri la kurudi kutoka bafuni na kurudi chumbani ambapo ndipo huifadhi sabuni nyingine.
********************
Happy Binti Mchungaji alipoona kuwa baba yake kaingia bafuni, akaingia chumbani haraka,
"Tayari baba ameingia bafuni, twende nikutoe nje" Happy aliongea kwa sauti ya chini ambayo ilisikika vyema masikioni mpwa Omary,
''Sasa njia tunayotokea si ndipo lilipo bafu, akisikia hatua za watu wawili zinatembea si atagutuka?" Omary alimuuliza happy Binti Mchungaji,
"Hawezi kugundua bwana, twende acha uoga" Happy aliendelea kumwambia Omary,
"Sasa si bora nisubiri Stoke bafuni aende chumbani?" Omary aliuliza,
"Acha ujinga, mama anarudi sasa hivi na wadogo zangu, wakikukuta humu, je itakuwaje?" Happy nae aliuliza,
"He!!!! Leo kweli siku yangu, haya twende" Omary aliongea kinyonge huku akisikitika.
Happy akamshika mkono Omary, kisha akaanza kutoka nae nje kwa mwendo wa kunyata, yaani mwendo wa taratibu usiokuwa na vishindo.
Walipofika usawa wa mlango wa baf na ndio muda huo Mchungaji Wingo alikuwa anafungua mlango ili akachukue sabuni chumbani.
Ghafla tu Omary na Happy binti Mchungaji wakashuhudia mlango wa bafu ukifunguliwa na wote macho yakawatoka pima mithili ya mtu aliekwamwa na kitu kooni...
********ITAENDELEA********
the Legend☆