Riwaya: Kijijini kwa Bibi

Riwaya: Kijijini kwa Bibi

Wakuu kuna episodes 4 za hii riwaya nimejaribu kuzitafuta leo bila mafanikio, hiyo ndio sababu iliyofanya nichelewe kupost mpaka muda huu. Nazo ni episode ya 35-38. Nyingine zote zipo. So tutaendelea na episode ya 39. Samahanini kwa usumbufu utakaojitokeza

the Legend☆
 
RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI.
MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA THELATHINI NA TISA.

__________________
ILIPOISHIA....
-----------------------------
"Ebu mtaje, ni upuuzi huu" Mkuu wa Polisi aliongea na kumfanya Babu wa monchwari atulie kidogo kwa maana alikuwa amelisahau jina la Sajenti Minja,

"Mbona humtaji?" Mkuu wa Polisi aliuliza kwa hasira na kumgutusha Babu wa monchwari aliyekuwa bado analitafuta jina la Sajenti Minja,

Baada ya muda akalikumbuka jina, na akaona haina haja ya kuuficha uovu, akaamua kulitaja jina sasa. Kabla hajalitaja kwanza akaamua atabasamu, akatoa tabasamu la ushindi kwa maana alijua akimtaja Sajenti Minja ndio utakuwa mwisho wa mchezo na yeye ndio utakuwa mwanzo wa utajiri wake,

Babu wa monchwari akaendelea kutabasamu....

*********ENDELEA*********

...Babu wa mochwari akaendelea kutabasamu,

"Mzee acha mzaa, nimekwambia umtaje huyo askari" Mkuu wa polisi aliuliza kwa ukali na kumfanya Babu wa monchwari ashtuke,

"askari mwenyewe si yule mwenye nanii, nini ile, ha, nimemsahau, ila nikimuona nitamjua", Babu wa mochwari aliendelea kuongea kwa kujiamini, ila hakutaka kumtaja moja kwa moja Sajenti Minja kwa kuwa alitaka kumfanyia jambo la kushtukiza Mkuu wa Polisi,

"mzee usinichanganye, maana sikuelewi", Mkuu wa polisi aliongea kwa ukali,

"niamini mwanangu, huyo muuaji napajua hadi anapokaa", Babu wa monchwar aliendelea kumwaga sera zake za kumshawishi Mkuu wa Polisi amuamini,

"Anakaa maeneo gani?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"Anakaa maeneo ya kota, karibu na kanisani" Babu wa monchwari alijibu huku akitabasamu,

"Mzee unachoongea ni kweli au leo umeamua kunichezea akili tu?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akimuangalia kwa jicho kali Babu wa monchwari,

"Kama itabainika nakudanganya, niweke ndani hata miaka mitatu" Babu wa monchwari alijibu kwa kujiamini,

"Na wewe ulimjuaje huyo mtuhumiwa, au mna mahusiano naye ya kindugu, ujirani au urafiki?" Mkuu wa Polisi alimuuliza Babu wa monchwari,

"Mi naona kama maswali yako yanapoteza muda vile, cha msingi ulichotakiwa kufanya ni kutuma vijana wako wakamkakate alafu ndio mahojiano yaanze" Babu wa monchwari alimshauri Mkuu wa polisi,

"Usinifundishe kazi mzee, ninachokifanya hapa ninakijua" Mkuu wa Polisi aliongea kwa hasira,

"Sawa mkuu, aya endelea na maswali" Babu wa Monchwari alijikuta ananywea na kuwa mtumwa kwa muda ule mfupi,

"Je kwa ujuzi wako, mtuhumiwa anaweza kuwa na silaha ya moto kama bastola au bunduki?" Mkuu wa polisi aliendelea kuhoji,

"Mimi ninapajua anapokaa tu, hayo mengine siyajui" Babu wa monchwari alijibu lakini sura yake ilionesha hakuyapenda kabisa hayo maswali, kwa maana aliona kama yanamchelewesha tu,

"Nimekuuliza hivyo ili nijue tumuingiliaje tutakapoenda kumkamate" Mkuu wa polisi alimuelesha Babu wa monchwari baada ya kugundua hapendi kuulizwa,

"Ana mwili wa kawaida tu, ni kakijana tu kachekibobu ambacho hakawezi kushika hata jembe" Babu wa monchwari alijibu,

Mkuu wa polisi akalainika, akatoka nje, kisha akawatafuta askari watatu aliowaamini, akawapa bunduki, kila mmoja risasi thelathini, kisha akawapa yule Babu kama dira ya safari yao,

"Mwanangu unanipa askari watatu!? hivi unamchukuliaje yule kijana?" Babu wa monchwari aliongea huku anasikitika,

"Wana bunduki hao, kwa hiyo usiwe na shaka, watafanikisha tu hiyo misheni" Mkuu wa polisi aliongea huku akimtazama Babu wa monchwari,

"Ujue awa wanaenda kupambana na dubwana, sio mtu wa kawaida, sasa unapowapeleka watatu tu itakuwa unafeli" Babu wa monchwari aliongea kwa sauti tulivu,

"Lakini si uliniambia ni kijana tu wa kawaida?" Mkuu wa polisi alimuuliza Babu wa monchwari,

"Ni kijana wa kawaida, ila anabadilika na kuwa likitu moja la ajabu sana, linatisha hakuna mfano" Babu wa monchwari alijibu,

"Nitakuongezea askari wawili wengine wawili" Mkuu wa polisi aliongea na kuagiza askari wengine wawili wenye silaha na walipofika, Mkuu wa polisi aliwapa maelekezo.

Baada ya hapo, mkuu wa polisi aliwaruhusu kuondoka, kisha akarudi ofisini kwake, akachukua simu yake ya kiganjani, akabonyeza namba anazojua yeye, inaonekana hakupata majibu anayoyataka, akarudia tena na tena kuipiga ile simu lakini ilionekana inaita muda mrefu mpaka inakatika bila kupokelewa,

"minja nae ana matatizo sana, anajijua yeye ni mtu muhimu, alafu hapokei simu", Mkuu wa polisi alijiongelesha na nafsi yake huku akiiweka simu yake mezani.

*******************

Hiyo siku sajenti Minja aliamka mapema, na katika ratiba zake, zilionesha ofisini kwao anaitajika mchana wa saa sita, wazo alilolipata ni kwenda nyumbani kwa Babu wa mochwari, maana tokea wameachana pale kwa sheikh hajajua Babu ana hali gani.

Ilipofika saa nne, Sajenti Minja alijipakia kwenye gari na kwenda nyumbani kwa Babu wa monchwari.
Hakupata tabu sana kufika kwa maana alishawahi kufika hapo Siku za nyuma.

"leo sijisikii hata hamu ya kupika, ila nitaenda kula kwa dada, ningewajulisha ila simu nimeiacha kwenye chaji", Sajenti Minja alijisemea peke yake, wakati gari yake inapaki mbele ya kajumba kamoja kaudongo, akatelemka kutoka katika gari, na kwenda kugonga katika mlango wa kale kajumba, akatoka mtoto mdogo wa kike, mwenye umri kati ya miaka kati ya miaka kumi na mbili na kumi na nne,

"karibu, shikamoo", yule mtoto akamsalimia Sajenti Minja,

"marahabaa, Babu yako nimemkuta?",Sajenti Minja alimuuliza yule mtoto,

"yupi, yule anaefanya kazi hospitali?", kale kabinti nako kalimuhoji Sajenti Minja,

"ndio huyo huyo", Sajenti Minja akajibu kwa kifupi,

"yule ni baba yangu na sio babu yangu kama unavyodhani", kale kabinti kalimtaharifu sajenti Minja,

"alah, we ni mtoto wake wa ngapi?", Sajenti Minja alimuuliza yule binti,

"wa tisa", yule binti akajibu,

"kwani nyie mmezaliwa wangapi?", akakatupia swali jingine, inavyoonekana kalimvutia katika kupangua maswali,

"kumi na nne, ila watatu wamefariki", kale kabinti kalijibu,

"oooh, haya, baba yuko wapi?",Minja akarudi katika topic iliompeleka pale,

"ameenda polisi", yule binti akajibu jibu lilomshtua kidogo Sajenti Minja,

"polisi?!",Sajenti Minja akauliza kwa mshangao,

"ndio, nilimsikia anamwambia mama kuwa, eti anaenda kutoa taharifa za mnyonya damu",yule binti aliendelea kupasua moyo wa Sajenti Minja bila kufahamu,

"ha!, sasa si kuharibiana uko!", Sajenti Minja aliongea bila matarajio yake,

"kwani nini kaka?", yule binti akamuuliza Sajenti Minja huku akiwa na wasiwasi,

"hakuna, shika hii kanunue soda", Sajenti Minja aliongea katika hali ya kuchanganyikiwa huku akimpa yule binti noti ya shilingi elfu mbili (2000).

Sajenti Minja akapanda gari, kisha akaliondoa gari kwa mwendo wa kasi sana,

"ngoja nikawape taharifa kule kwa dada, kisha tujue cha kufanya", Sajenti Minja aliongea kwa sauti ya chini ambayo ilijawa na kitetemeshi kutokana na habari mbaya alizozipokea muda mfupi uliopita.

Alitumia dakika kumi na tano mpaka kufika jirani na mtaa wa wakina kayoza, kulikuwa kuna kona kama tatu, ndio afike katika nyumba ya dada yake.

Kona ya kwanza aliikata vizuri huku akiwa katika mwendo ule ule wa kasi, kwenye kona ya pili ndo kulikuwa na shughuli, gari ya polisi ambayo alikuwemo Babu wa monchwari na askari nayo ilikua katika spidi ya juu, ndio ya mwisho, nao walibakia mita chache waifikie nyumba ya mama kayoza, ile kukata kona tu, ili gari lishike barabara ya nyumba ya wakina kayoza, na Sajenti Minja nae ndio alikuwa anaingia katika hiyo hiyo barabara inayoelekea kwa dada yake, basi kikasikika kishindo kikubwa sana ambacho hakikuwai kutokea pale mtaani, ni gari ya polisi iliivaa gari ya Sajenti Minja kwa ubavuni, ilikuwa ni ajali ya kutisha sana.

Ni damu pekee ndizo zilionekana vizuri katika eneo lile na gari ya Sajenti Minja ilibondeka vibaya sana, haswa upande wa dereva. Hakuna mtu aliyeweza kuiangalia Mara mbili gari ya Sajenti Minja na hakuna mtu aliyekuwa na akili timamu aliyedhani katika ile ajali kuna mtu yupo hai....

**********ITAENDELEA**********

the Legend☆
 
RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI.
MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA AROBAINI.

__________________
ILIPOISHIA....
-----------------------------

Kona ya kwanza aliikata vizuri huku akiwa katika mwendo ule ule wa kasi, kwenye kona ya pili ndo kulikuwa na shughuli, gari ya polisi ambayo alikuwemo Babu wa monchwari na askari nayo ilikua katika spidi ya juu, ndio ya mwisho, nao walibakia mita chache waifikie nyumba ya mama kayoza, ile kukata kona tu, ili gari lishike barabara ya nyumba ya wakina kayoza, na Sajenti Minja nae ndio alikuwa anaingia katika hiyo hiyo barabara inayoelekea kwa dada yake, basi kikasikika kishindo kikubwa sana ambacho hakikuwai kutokea pale mtaani, ni gari ya polisi iliivaa gari ya Sajenti Minja kwa ubavuni, ilikuwa ni ajali ya kutisha sana.

Ni damu pekee ndizo zilionekana vizuri katika eneo lile na gari ya Sajenti Minja ilibondeka vibaya sana, haswa upande wa dereva. Hakuna mtu aliyeweza kuiangalia Mara mbili gari ya Sajenti Minja na hakuna mtu aliyekuwa na akili timamu aliyedhani katika ile ajali kuna mtu yupo hai....

*********ENDELEA**********

..eneo lote liligubikwa na harufu ya damu, watu wakaanza kujisogeza mmoja mmoja, dakika mbili tu zilitosha kujaza watu eneo la tukio.

Wasamalia wema wakatoa taharifa polisi baada ya kugundua kuwa gari moja lilikuwa na polisi.

Kwa jinsi hali ilivyoonekana, ilikuwa vigumu kujua kama watu waliohusika katika ajali ni wazima, ilionesha wote wamekufa. Kwenye gari ndogo ambayo ndani alikuwepo Sajenti Minja peke yake, yeye aliganda pale pale huku damu zikimtoka puani na mdomoni, wakati katika gari ya polisi, dereva, babu wa mochwari na askari mmoja aliekuwepo mbele, wote walitokea kupitia kioo cha mbele na kuangukia juu ya gari la Sajenti Minja, wote watatu walikuwa wamepoteza maisha, na nyuma ya gari, hakukuwa na dalili yoyote iliyoonesha bado kuna mtu ana hati miliki ya pumzi yake, wote walikuwa wamepoteza uhai.

Baada ya dakika kadhaa, gari ya polisi ilifika huku ikiongozana na ambulance ya hospitali ya mkoa wa Shinyanga.

Mkuu wa polisi alishtuka sana baada ya kugundua kuwa lile gari dogo ni la Sajenti Minja, aliakikisha kila jambo linafanyika haraka.

Madaktari waliofika pale waligundua kuwa yule aliyekuwepo katika gari dogo ni mzima, baada ya kumpima na kugundua kuwa mapigo yake ya moyo yanapiga kwa mbali sana.

Wakamwekea mashine ya kusukuma hewa safi (oxygen) puani kwake, pamoja na dripu, kisha gari ya hospitali ikaondoka kwa kasi sana, huku ikipiga king'ora kumuwahisha hospitali majeruhi.

Kisha gari ya polisi nayo iliubeba mwili wa Babu wa monchwari na wale askari waliopoteza maisha na kuwapeleka monchwari kuwahifadhi.

Masikini Babu wa monchwari, toka kulinda maiti mpaka kulindwa kama maiti.
Ndivyo dunia ilivyo, kifo chake kilifanya aukose utajiri aliokuwa anaenda kuupata Siku chache zijazo. Kifo chake kimeacha majonzi kwa ndugu, marafiki na familia yake. Na zaidi kifo chake kimeacha tabu sana kwa watu waliokuwa wanamtegemea.

Alazwe pema peponi babu wa monchwari.

*****************

Mama kayoza na wanae walikuwa wanaongea maongezi yao ya kawaida pale nyumbani, ghafla wakasikia kishindo kikubwa sana,

"mh!, na huku kuna kambi ya jeshi karibu nini?", Kayoza alimuuliza mama yake,

"hakuna, ila iko kishindo inaweza kuwa tairi la gari limepasuka", mama Kayoza alijibu,

"Sio tairi ya gari hilo mama, mlio wa tairi naujua" Omary alimbishia Mama Kayoza na kisha Omari peke yake ndio aliamua kwenda nje kuangalia kilichotea.

Baada ya kusikia kelele za watu, nae alitoka tu mlangoni akamuuliza mtu mmoja aliekuwa anapita pale nje, akamjibu kuwa kuna ajali, baada ya kuridhika na jibu, Omari akarudi ndani.

"vipi, umeshaangalia?",Kayoza akamuuliza Omari,

"yah, ni ajali imetokea pale kwenye kona", Omari akamjibu,

"mtu kagongwa nini?", Kayoza akaendelea kudadisi,

"mimi sijafika, ila kwa kile kishindo, itakuwa gari imeikuta gari pale", Omari alijibu,

"madereva wa siku hizi hovyo kabisa, enzi zetu hizi ajali zilikuwa ni nadra sana", mama Kayoza aliongea kwa manung'uniko,

"mama ile kona mbaya sana", Kayoza aliongea kuwatetea madereva wa siku hizi,

"hata kama", mama Kayoza alishikilia msimamo wake,

"Wewe mama hushangai Sikh hizi magari yapo chungu mzima lakini ajali ni chache sana?" Kayoza aliendelea kuwatetea madereva wa kisasa,

"Zamani magari yalikuwa machache ndio, ila miundombinu ilikuwa mibovu na ajali zilikuwa chache pia" Mama Kayoza aliongea,

"Mimi nafikiri madereva wa Siku hizi ndio chanzo cha ajali nyingi, kwanza hata leseni zenyewe hawasomei, ila wanazipata kiujanja ujanja tu kwa kununua kwa rushwa" Omary aliongea kwa kumuunga mkono Mama Kayoza,

"Bora wewe mwanangu umeongea, hili likayoza bishi sana, kama marehemu Baba yake vile" Mama Kayoza aliongea,

"Basi yaishe, maana mmeamua kunichangia sasa" Kayoza aliamua kumaliza mada,

"Sio yaishe tu, kwanza kubali madereva wa sasa si madereva ila washika usukani tu" Mama Kayoza aliongea kwa utani,

"Sawa, kwa hiyo hata Mjomba Minja ni mshika usukani tu?" Kayoza aliuliza huku akicheka,

"Sasa yule udereva ni Nazi yake?, yule ni polisi bwana" Mama Kayoza alimjibu mwanaye,

"Tunapozungumzia madereva tunajumuisha wote, wanaobeba abiria na wanaoendesha magari yako binafsi" Kayoza aliamua kuipa nguvu point yake,

"Haya sawa umeshinda, maana unachotaka ni kubishana tu na mimi sitaki" Mama Kayoza aliongea,

Na katika kipindi hicho hicho kuna mtu alikuwa akigonga hodi mlangoni, kwa hiyo hodi iliyokuwa inapigwa ndio iliwakatisha maongezi yao,

"pita, mlango uko wazi", Mama Kayoza aliongea kwa sauti ili mgonga hodi amsikie,

"hodi tena, jamani salama hapa?", Kijana mmoja ambae anakaa nyumba ya pili kutoka pale, aliwasalimia huku akionekana mwenye wasiwasi,

"kumbe ni wewe Tino, sisi wazima, we hujambo?", mama Kayoza akamuuliza yule kijana,

"jambo ninalo mama yangu", yule kijana alijibu,

"haya tuambie hilo jambo sasa", mama Kayoza aliongea kwa sauti ya ucheshi,

"yule bro polisi, white white hivi, anaekujaga hapa amepata ajali pale kona", Yule kijana alitoa taharifa iliyowapa mshtuko wote waliopo pale,

"ah!, kagonga mtu", Omari aliuliza huku akisahau kuwa yeye ndiye aliyesema kile kishindo sio cha kugongwa mtu, ila ni magari yamegongana,

"gari yake imegongana uso kwa uso na gari ya polisi", Yule kijana aliendelea kuelezea alichokiona,

"ile gari ya polisi wote wamekufa, ila yule bro kabebwa hajielewi, sijui hata kama atafika hospitali", Yule kijana alipigilia msumari wa mwisho katika maumivu ya mama kayoza na wanae, kisha akawaaga, ila hakujibiwa kutokana na hali iliyokuwepo.

"Mama sasa tunafanyaje?" Kayoza aliuliza kwa sauti tulivu,

"Twendeni tu hospitali, hatuna muda wa kupoteza" Omary alijibu na kipindi chote mama Kayoza alikuwa amefumba macho anasali, hali aliyokuwa nayo ni dhahiri alikuwa amechanganyikiwa.

"Haya twendeni" Mama Kayoza aliongea huku akisimama,

"Sasa mama tunaenda hospitali gani?, au unajua hospitali aliyopelekwa?" Kayoza alimuuliza mama yake huku akimshangaa,

"Acha kuuliza maswali ya kijinga, wewe unadhani atapelekwa hospitali gani zaidi ya hospitali juu ya mkoa?" Mama Kayoza aliuliza huku akijitanda khanga,

"Mama tunapoteza muda bure, twendeni tuwahi" Omary aliongea huku akiwa amesimama mlangoni,

"Si huyu mpumbavu anauliza uliza vitu visivyokuwa na maana" Mama Kayoza aliongea kwa hasira huku akiuelekea mlango wa kutokea.

***********************

Majira ya saa sita mchana, mama Kayoza na wanae walikuwa wameshafika hospitali, moja kwa moja wakaenda kujitambulisha kwa madaktari, kisha wakaambiwa mgonjwa wao alipowekwa,

wakatoka tena hadi katika chumba cha wagonjawa mahututi(I.C.U), walizuiliwa mlangoni na manesi, wakaambiwa bado madaktari wako ndani wanapigania uhai wa mgonjwa.

Wakarudi kukaa katika benchi lililo jirani na kile chumba na wote wakakaa kimya huku kila mtu akiwaza jambo lake.

Mama Kayoza ndiye aliyeonekana amechanganyikiwa zaidi kuhusu hali aliyokuwa nayo Sajenti Minja.

Baada ya nusu saa, Daktari alitoka kutoka katika kile chumba alichokuwa amelazwa Sajenti Minja.
Mama kayoza na wanae wakamkimbilia, kisha wakajitambulisha, yule Daktari akawaangalia sekunde kadhaa, kisha akatingisha kichwa,

"Aya baba tuambie hali ya mgonjwa wetu ikoje?" Mama Kayoza aliuliza huku machozi yakianza kumtoka,

"Sasa mama unalilia nini, usilie bwana unakuwa unaleta uchuro" Kayoza alimwambia mama yake,

"Ebu ngojeni kwanza, wewe mama ni nani yake?" Daktari alimuuliza Mama Kayoza,

"Mimi ni dada yake, tumezaliwa baba mmoja na mama mmoja, baada ya kuzaliwa mimi ndio akafuata yeye" Mama Kayoza alijibu na kumfanya Daktari akili kuwa Mama Kayoza hayupo katika akili zake za kawaida,

"Na nyie vijana ni zake?" Daktari aliuliza huku akiwageukia Kayoza na Omary,

"Awa ni wanangu kabisa, yule ni mjomba wao" Mama Kayoza aliamua kuwajibia, maana aliona kama watachelewa vile kutoa jibu,

"Basi kama ni hivyo, mama nakuomba utusubiri nje, acha niongee na awa watoto wa kiume" Daktari aliongea huku akimtazama Mama Kayoza,

"Sasa utawaeleza nini awa watoto? Nieleze mimi mama yao, awa watoto wenyewe wananitegemea mimi" Mama Kayoza aliongea kwa hasira huku akianza kulia,

"Mama msikilize daktari, unapopayuka unakuwa unakosea mama" Kayoza alimwambia Mama Yake,

"Kaa kimya, tena funga mdomo wako, hujui uchungu ninaousikia hapa" Mama Kayoza alimkaripia mwanae huku akilia,

"Basi usilie, unalilia nini sasa?" Omary aliuliza baada ya kuona hakuna maelewano kutokana na kilio cha Mama kayoza,

"Muache alie, anastahili kulia kwa maana hata nyinyi mtalia muda mchache ujao" Daktari alimjibu Omary na kisha akawaambia habari mbaya ambayo ilipelekea mama Kayoza kupiga mueleka wa nguvu na kupoteza fahamu palepale...

**********ITAENDELEA**********

the Legend☆
 
RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA AROBAINI NA MOJA.

__________________
ILIPOISHIA....
-----------------------------
"Muache alie, anastahili kulia kwa maana hata nyinyi mtalia muda mchache ujao" Daktari alimjibu Omary na kisha akawaambia habari mbaya ambayo ilipelekea mama Kayoza kupiga mueleka wa nguvu na kupoteza fahamu palepale...

************ENDELEA**********

...wakina Kayoza pamoja na manesi, wakambeba juu juu Mama Kayoza na kumkimbiza wodini haraka. Kayoza na Omari wakaambiwa watoke nje, mgonjwa anatakiwa kupewa huduma ya haraka.

Wakina kayoza ikawabidi waende nje wakasubiri.

"Aisee, mbona mitihani inaongezeka hivyo?" Kayoza alimuuliza Omary huku wakiwa wamesimama nje ya jengo la wodi aliyolazwa mama yake,

"Ila hatupaswi kukata tamaa, mjomba ataamka tu, Mimi nina imani hiyo" Omary aliongea kwa ujasiri,

"Ni ngumu sana, si umesikia daktari alivyosema?" Kayoza alimuuliza Omary,

"Kuna daktari, lakini kumbuka kuna Mungu pia" Omary alijibu,

"Sawa, ngoja tuone" Kayoza alijibu na kisha ukimya ukatawala huku wakiendelea kusubiri nje, ingawa hawakuwa wanachosubiri. Kila mmoja alikuwa kimya.

Baada ya robo saa wakarudi ndani ya eneo la hospitali, wakaruhusiwa kwenda kumuona mama yao, wakamkuta amekaa kitandani huku dripu ikiwa inahesabu matone yake,

"pole mama", Kayoza na Omari waliongea kwa pamoja,

"mh, mmeongea tena na daktari", Mama Kayoza badala ya kuitikia, akawauliza swali,

"hapana, nafikiri kama kuna mabadiliko yoyote yametokea atatuambia",Kayoza alimjibu mama yake,

"Atawaambiaje wakati hamjamtafuta?" Mama Kayoza aliuliza,

"Si angekuja hata hapa wodini ulipolazwa" Kayoza aliongea,

"Bado akili zako hazijakomaa, sasa hata kama angekuja unadhani angeongea nini na Mimi wakati Mimi ni mgonjwa?" Mama Kayoza aliuliza,

"Sasa hivi unajisikiaje mama?" Omary alimuuliza Mama Kayoza,

"mh, naisi mwili hauna nguvu kabisa",Mama Kayoza alimjibu Omary,

"mama nawe una presha ya ajabu, je ungeambiwa amekufa, si na wewe ungekufa!", Kayoza alimwambia mama yake,

"we Kayoza acha ujinga, sasa tumeambiwa uhakika wa kuishi ni asilimi 30, wa kufa asilimia 70, huoni ni jambo la kuogopa sana?",Mama Kayoza aliongea kwa ukali kidogo,

"mama wewe ni mlokole, ulichotakiwa kufanya ni kumuomba Mungu na si kukata tamaa", Kayoza alimwambia mama yake,

"Kwani mlokole sio binadamu? kuna hisia za kibinadam uwa zipo kwa kila mtu" Mama Kayoza aliongea,

"Hata kama, mbona sisi hatujapoteza fahamu baada ya kusikia hiyo habari?" Kayoza alimkazania mama yake kwa maswali,

"Kwanza nyie ni watoto wa kiume, alafu pia inawezekana upendo wenu kwa Minja sio mkubwa kama niliokuwa nao Mimi" Mama Kayoza alieleza,

"Kwa hiyo sisi hatumpendi mjomba?" Kayoza aliuliza,

"Sijui wenyewe, kwanza tuachane na hayo, kamtafute daktari aje kunipa ruhusa mimi", Mama Kayoza akamwambia mwanae.

Kayoza akaenda kumtafuta Daktari, baada ya muda kidogo, akarudi na daktari, daktari akampima pima mama Kayoza, kisha akamuuliza maswali mawili matatu, akamuandikia maelezo katika kikaratasi, alafu akamruhusu.
Walichofanya wakina Kayoza ni kumrudisha mama yao nyumbani, kisha wao wakarudi hospitali.Hata wenyewe hawakuelewa pale hospital wanasubiri nini, ilimradi walikuwa wanakaa tu ili kumridhisha mama yao ambae aliwataka wasiondoke eneo la hospitali.

*****************

Mkuu wa polisi kazi kubwa aliyokuwa anafanya ni kuwajulisha ndugu na jamaa wa marehemu juu ya ajali iliyotokea, na kuwapa taharifa za kifo, ila hakutaka kabisa kuwaambia askari wengine kuwa, yeye ndio aliwaagiza, maana angewaambia ni lazima angewajulisha kuwa aliwatuma kumkamata mtuhumiwa wa mauaji ya kunyonya damu na yeye hakutaka ijulikane, kwa sababu angetangazia uma, basi huyo muuaji angeshtuka na kuhama mkoa, ila alichoamua ni kufanya upepelezi wake wa kimya kimya. Alipekua makabrasha yake na kutoa gazeti ambalo lilionekana la siku nyingi, kisha akalikunjua, mbele kulikuwa na picha ya Omari, akaiangalia ile picha kwa muda mrefu sana, akajikuta anatabasamu mwenyewe,

"Yule mzee wa monchwari alimuona kweli muuaji, na kama alimuona alimjuaje, au lao lilikuwa moja?" Mkuu wa polisi alijiuliza huku akiwa bado anaitazama picha ya Omary iliyopo katika kipande cha gazeti.

"kama yupo hapa shinyanga, nitamkamata tu, huu mkoa ni mdogo sana", Mkuu wa polisi aliongea huku akiwa bado anaendelea kuitazama ile picha ya Omari.

Kisha akaikunja vizuri kama mwanzo, na kuirudishia katika droo ya meza yake ya pale ofisini, kisha akainuka na kwenda kabatini kisha akaitoa kofia yake na kuibandika kichwani.

Baada ya hapo, akamwita dereva wake na kumuamuru ampeleke hospitali.

Walipofika hospitali, Mkuu wa polisi alitelemka, kisha akaenda katika wodi alipokuwepo Sajenti Minja, ila alizuiliwa mlangoni na daktari,

"mimi nataka nimuone tu ili nijue hali yake", Mkuu wa polisi alimwambia daktari,

"hali yake sio nzuri kamanda", yule Daktari alimjibu mkuu wa polisi, alionekana kumfahamu haswa,

"kuna mtu yeyote aliyekuja kumuona?", Mkuu wa polisi alimuuliza daktari,

"ndio, kuna mwanamama mmoja, alikuja na vijana wawili, walijitambulisha ni ndugu zake", yule Daktari alimjibu Mkuu wa polisi,

"walikwambia wanapokaa?", Mkuu wa polisi alimuhoji Daktari,

"hapana, ila wameondoka mida hii hii, kwa sababu yule mwanamama alipoteza fahamu baada ya kumwambia hali ya mgonjwa",yule Daktari alijibu,

"kama mpaka alipoteza fahamu, basi anamuhusu",Mkuu wa polisi aliongea hivyo.

"Ila kiukweli inahitajika sala kweli ili huyu jamaa apone" Daktari alimwambia Mkuu wa polisi,

"Kwa maana hiyo nyie uwezo umefika mwisho?" Mkuu wa polisi alimtupia swali Daktari,

"Nikisema hapana, nitakuwa nadanganya, kwa hata ile tuliyofikia hakuna hata nyingine ambayo tunaweza kuipiga, sasa hapo ni uwezo wa Mungu tu ndio utamuweka hai" Daktari aliendelea kuongea anachokijua,

"Sasa kama ni hivyo si ni bora mmuandikie barua ya kumuhamishia hospitali nyingine zenye uwezo" Mkuu wa polisi alitoa maoni yake,

"Hata tuna uwezo, tungekuwa hatuna uwezo tungeshamuandikia barua hata ya kumpeleka india" Daktari alimjibu Mkuu wa polisi,

"Kwani tatizo ni hasa?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"Uti wa mgongo umepata itilafu kidogo, kwa hiyo mawasiliano ya mwili hayapo na pia kichwa chake inaonesha kilipigizwa sana" Daktari alimjibu Mkuu wa Polisi,

"Tuweke imani tu atapona, tusiwe tunavunjika moyo kwa kitu ambacho kipo nje ya uwezo wetu" Mkuu wa polisi aliongea,

"Na hata akipona kuna mawili, anaweza kupata ulemavu wa maisha kutokana na tatizo la uti wa mgongo, au anaweza akapoteza kumbukumbu kwa muda mrefu au pia vyote vinaweza kumtokea" Daktari aliendelea kutoa Maelezo,

"Cha muhimu uzima, hayo mengine ni kuendelea kumuomba Mungu" Mkuu wa Polisi aliongea,

Wakiwa bado katika maongezi yao, mbele yao walikuja Kayoza na Omari,

"vipi Dokta?" Kayoza alimuuliza Daktari,

"vijana wenyewe ambao ni ndugu wa mgonjwa ni awa hapa",Daktari hakumjibu Kayoza, ila alimtaharifu mkuu wa polisi kuhusu wakina Kayoza, lakini Mkuu wa polisi hakuonekana kumsikiliza Daktari kabisaaa, badala yake, alimtumbulia macho Omary huku ile picha iliyopo katika kipande cha gazeti ikimjia....

********ITAENDELEA**********

the Legend☆
 
RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI.
MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA AROBAINI NA MBILI.

__________________
ILIPOISHIA....
-----------------------------

Wakiwa bado katika maongezi yao, mbele yao walikuja Kayoza na Omari,

"vipi Dokta?" Kayoza alimuuliza Daktari,

"vijana wenyewe ambao ni ndugu wa mgonjwa ni awa hapa",Daktari hakumjibu Kayoza, ila alimtaharifu mkuu wa polisi kuhusu wakina Kayoza, lakini Mkuu wa polisi hakuonekana kumsikiliza Daktari kabisaaa, badala yake, alimtumbulia macho Omary huku ile picha iliyopo katika kipande cha gazeti ikimjia....

***********ENDELEA**********

aliendelea kumuangalia Omari kwa dakika nzima mpaka Omari akapata wasiwasi na lile jicho kali la Mkuu wa Polisi,

"we kijana unaitwa nani?",Mkuu wa polisi alimuuliza Omari, tena aliuliza kwa sauti ya ukali,

"remmy, naitwa Remmy", Omari akataja jina la uongo, alikuwa na wasiwasi ila alijitahidi kuficha hofu yake mbele ya Mkuu wa Polisi,

"Minja ni nani kwako?", Mkuu wa polisi akamuuliza tena Omari,

"ni mjomba wangu", Omari akajibu huku akikwepesha macho yake yasigongane na macho ya Mkuu wa polisi,

"Mjomba ako kivipi?" Mkuu wa polisi akamtupia swali lingine Omary,

"Mimi ni mtoto wa Dada ake" Omary akajibu,

"unamfahamu Omari Mkwiji?",Mkuu wa polisi akamtupia swali lingine tena, ila hili swali la kipindi hiki ndilo lililokuwa gumu kuzidi yote aliyoulizwa kabla, na hata jasho lilianza kumtoka,

"hapana", Omari akajibu, wakati huo wote, Kayoza moyo ulikuwa unamuenda mbio sana, mpaka jasho likawa linamtililika mgongoni kuelekea sehemu za makalio,

"mh!, kweli duniani wawili wawili", Mkuu wa polisi aliongea huku akimgeukia Daktari,

"vipi kamanda, umemfananisha na ndugu yako nini?",Daktari alimuhoji mkuu wa polisi,

"hapana, kafanana na mtu mmoja hatari sana"Mkuu wa polisi aliongea kitu ambacho kilimpelekea Omari atoe ushuzi kwa mbali kwa ajili ya uoga,

"kama ni mtu hatari, basi asingekuwepo eneo hili",Daktari aliongea kauli iliyompoteza kabisa mkuu wa polisi.

"Kweli kabisa, kama angekuwa mtu mbaya basi asingesogea eneo hili" Mkuu wa polisi aliamua kumuunga mkono Daktari.

"Na wewe ni nani yake Minja?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akimuangalia Kayoza,

"Na mimi ni mjomba wake pia, mtoto wa Dada yake" Kayoza alijibu huku akijitahidi kujiamini,

"Kwa hiyo nyinyi ni ndugu?" Mkuu wa polisi aliwauliza huku akiwaangalia kwa zamu,

"Ndio" Omary alijibu,

"Mnakaa na mama yenu?" Mkuu wa polisi aliwauliza,

"Ndio tunakaa nae" Kayoza alijibu,

"Basi baadae nitarudu hapa, naomba niwakute ili mnipeleke nyumbani kwenu nikapajue na pia nimjue mama yenu" Mkuu wa polisi aliongea,

"Sawa haina shida, tena itakuwa vizuri sana" Omary alijibu huku akijitahidi kutabasamu,

"Alafu inaonesha wewe ni muongeaji sana kuliko mwenzako" Mkuu wa polisi alimwambia Omary huku nae akitabasamu,

Baada ya maongezi ya hapa na pale pamoja na kutambulishana, Mkuu wa polisi aliagana na wakina Kayoza kwa ahadi ya kuwafuata baadae pale hospitali na wampeleke akapajue wanapoishi.

"pppfffuuuu", wakajikuta wanashusha pumzi nzito baada ya Mkuu wa polisi kuondoka,

"duh!, mwana mi makalio yameloana hapa", Kayoza ndiye alieanza kuongea,

"dah!,we acha tu, ebu twende tukatafute maji ya baridi nje, maana naisi moyo uko kasi sana",Omari aliongea huku akitanguliza mguu wa kulia mbele, hali iliohashiria waondoke.

*************

Wakina Kayoza walirudi kwao muda huo huo, ila hawakutaka kumwambia mama yao kama wamekutana na mkuu wa polisi na kukubaliana nae kuwa jioni atakuja hapo nyumbani, walitaka kumfanyia kama kitu cha kushtukiza.

Kibaya ambacho hawakukijua ni kuwa kwa kufanya ujinga wao huo wa kutaka kumshtukiza mama yako, ni kitu ambacho kinaweza kuja kuwagharimu wao wenyewe.

"Haya nipeni habari za hospitali" Mama Kayoza aliongea huku akijibwaga katika kochi lilokuwepo hapo sebuleni,

"Hakuna mabadiliko yoyote mama, bado hali ya mjomba ipo vile vile" Kayoza alijibu kwa masikitiko,

"Jamani mfunge na kusali, mmuombee mjomba wenu, kwa ile hali aliyokuwa nayo ni hatari sana" Mama Kayoza aliongea kwa huzuni,

"Mke wake umempa taharifa?" Kayoza alimuuliza Mama yake,

"Hapana, ila nimeongea na baba na yeye amesema tusimwambie mke wa Minja kwanza, tuvute subira huku tukiangalia ni namna gani tumueleze" Mama Kayoza alijibu mwanae,

"Mimi naona hakuna haja ya kumficha, mwambieni tu ukweli ili kama likitokea la kutokea, asimlaumu mtu" Kayoza alimshauri mama yake,

"Hakuna anayemficha, ila tunatafuta wakati sahihi wa kumwambia hilo tatizo" Mama Kayoza alijibu,

"Na kama make wake anampigia simu na hampati hewani? Huoni na hiyo itampa wakati mgumu?" Kayoza aliendelea kuuliza,

"Kwanza unachotakiwa kujua ni kwamba Minja anapoondoka nyumbani kwake kikazi uwa habebi simu, hii simu anayotumia aliinunua kwa ajili ya hii kazi tu, alipanga akimaliza hii kazi na ile simu na laini yake anachoma moto" Mama Kayoza aliwaambia kitu wasichokijua,

"Sasa inawezekanaje muda wote huo asiwasiliane na mke wake?" Omary aliuliza huku akionekana kutokubaliana na Maelezo ya mama Kayoza,

"Kwani imewezekanaje wewe kutowasiliana na wazazi wako kipindi chote hiki?" Mama Kayoza alimtupia swali Omary,

"Sasa mama mimi si Nina matatizo, ni hatari sana nikiwasiliana na ndugu zangu, naweza kuwaingiza matatizoni pia" Omary alijibu, ila alijibu kinyonge,

"Ebu tuachane na hayo, pumzikeni ili jioni mrudi hospitali" Mama Kayoza aliongea huku akielekea chumbani kwake.

***********************

Jioni, Mkuu wa polisi aliwafuata wakina Kayoza pale hospitali, Kisha akawachukua, ili wampeleke wanapoishi.
Njia nzima walikuwa wanapiga stori za hapa na pale, walipofika katika eneo ambalo ajali ilitokea, Mkuu wa polisi akashtuka,
"mhm, wanakaa huku, yule Babu nae si alikuwa anakuja huku, mh, bado nina wasiwasi na huyu Remmy, ntaendelea kumchunguza taratibu", mkuu wa polisi aliongea kimoyo moyo.
Wakafika kwa wakina Kayoza.
"karibu nyumbani", Kayoza alimkaribisha mkuu wa polisi,
"asante mheshimiwa, kumbe mlikuwa karibu sana na eneo la ajali?", Mkuu wa polisi aliuliza kinafki,
"hata kile kishindo tulikisikia",Kayoza akamjibu.
Wakamkaribisha ndani, kisha wakamtambulisha kwa mama yao, mama Kayoza akafurahi sana kutembelewa na mtu mkubwa pale nyumbani kwake. Mama yao alipata faraja kutembelewa na mkuu wa polisi,

"Sasa mbona hamkunitaharifu kama ugeni?" Mama Kayoza aliwauliza wanae,

"Tulitaka kukufanyia shambulizi la kushtukiza" Kayoza alijibu huku aki tabasamu,

"Siku nyingine muwe mnasema bwana, ili tumuandalie mgeni chakula" Mama Kayoza alimwambia mwanae,

"Kweli lakini, mlitakiwa mseme bwana, sasa si mnaona mmenikosesha chakula?" Mkuu wa polisi aliongea kwa utani huku akicheka,

"Ila hakuna ubaya kaka yangu, ngoja nikuandalie" Mama Kayoza aliongea,

"Hapana usiangaike, nitakula siku nyingine" Mkuu wa polisi aliongea kwa ucheshi,

"Mama sisi yupo ndani" Kayoza aliongea huku akiinuka pamoja na Omary,

"Mlitakiwa mkae tuongee na mgeni" Mama Kayoza aliwaambia wanae,

"Nyie ongeeni tu, sisi tunarudi muda si mrefu" Kayoza alijibu huku wakielekea ndani na Omary na kuwaacha Mkuu wa Polisi na Mama yao wakiongea.

Wakaongea sana kuhusu Sajenti Minja, undugu wa Mama kayoza na Sajenti Minja.

Mwishowe, Mkuu wa Polisi aliamua kuaga, ila Omari na Kayoza walikuwepo wako ndani, ikabidi Mama Kayoza hawaite, ila alikuja Kayoza peke yake,

"Naam mama, nimeitikia wito" Kayoza aliongea alipotoka ndani,

"mgeni anataka kuwaaga", Mama Kayoza alimwambia mwanae,

"sawa, karibu tena", Kayoza alimwambia Mkuu wa polisi,

"Sio karibu tena, unatakiwa umsindikize" Mama Kayoza alimwambia mwanae,

"Amekuja na gari" Kayoza alijibu mama yake,

"Hata kama amekuja na gari, unatakiwa umtoe nje, ndio uungwana upo hivyo" Mama Kayoza alimwambia mwanae,

"Yule mwenzio yupo wapi, yeye hataki kuniaga?" Mkuu wa polisi alimuulizia Omary,

"Alafu kweli, ebu kamuite na Ommy, aje amuage", mama Kayoza aliongea huku akimuangalia Kayoza,

"OMMY?", Mkuu wa polisi aliuliza kwa mshangao....

*******ITAENDELEA*******

the Legend☆
 
RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI.
MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA AROBAINI NA TATU.

__________________
ILIPOISHIA....
-----------------------------

Mwishowe, Mkuu wa Polisi aliamua kuaga, ila Omari na Kayoza walikuwepo wako ndani, ikabidi Mama Kayoza hawaite, ila alikuja Kayoza peke yake,

"Naam mama, nimeitikia wito" Kayoza aliongea alipotoka ndani,

"mgeni anataka kuwaaga", Mama Kayoza alimwambia mwanae,

"sawa, karibu tena", Kayoza alimwambia Mkuu wa polisi,

"Sio karibu tena, unatakiwa umsindikize" Mama Kayoza alimwambia mwanae,

"Amekuja na gari" Kayoza alijibu mama yake,

"Hata kama amekuja na gari, unatakiwa umtoe nje, ndio uungwana upo hivyo" Mama Kayoza alimwambia mwanae,

"Yule mwenzio yupo wapi, yeye hataki kuniaga?" Mkuu wa polisi alimuulizia Omary,

"Alafu kweli, ebu kamuite na Ommy, aje amuage", mama Kayoza aliongea huku akimuangalia Kayoza,

"OMMY?", Mkuu wa polisi aliuliza kwa mshangao....

*******ENDELEA*******

.."we Remmy njoo mgeni akuage",Kayoza aliita kwa sauti ya juu ili kumvuruga mkuu wa polisi.

Mkuu wa polisi ikambidi anyamaze, maana hakuna aliejibu swali lake, na isitoshe hata mama Kayoza alihisi kuna kitu, haiwezekani Omary aitwe Remmy ghafla kiasi mile.

Baada ya sekunde chache, Omary alitoka ndani na kujongea sebuleni kujumuika na wengine waliokuwako eneo hilo.

"bwana mdogo mi naenda, nawakimbia bwana",Mkuu wa polisi alimwambia Omari huku akiwa amemkazia macho na pia alikuwa anatabasamu tabasamu moja la kinafki sana, ila hakuna aliegundua jambo hilo,

"haya, karibu tena",Omari akamuitikia huku nae akilazimisha tabasamu lake halisi,

"Mama ukiwa na shida ndogo ndogo kipindi hiki Minja mgonjwa, usisite kuniambia" Mkuu wa polisi alimwambia Mama Kayoza,

"Hata usiwe na shaka baba angu, tushakuwa kama ndugu sasa" Mama Kayoza alijibu Mkuu wa Polisi

Baada ya maongezi hayo machache, wakamtoa mpaka nje, kisha Mkuu wa polisi akajipakia kwenye gari, gari ikaondoka.

Mama Kayoza na wanae wakarudi ndani.

"ehe mwenzetu, hilo jina umeliokota wapi?",Mama Kayoza alimuuliza Omari kwa utani,

"jina gani hilo",Omari nae aliuliza kanakwamba hajui,

"si hilo la Remmy Ongala!",Mama kayoza akajibu.

"Kwanza mama bado kidogo tu uharibu" Kayoza aliongea huku akijitupia katika kochi,

"Niharibu nini tena,!!?" Mama Kayoza aliuliza kwa mshangao,

"Ujue huyu mkuu wa polisi alivyomuona omary Kyle hospitali alimtilia shaka, na alipomuuliza jina lake, omary ndipo alipodanganya anaitwa Remmy. Sasa wewe tena ukamuita ommy" Kayoza alimlalamikia mama yake,

"Sasa huo ni ujinga wa nani?, huo ni ujinga wenu, kama mlitambua huyu mkuu wa polisi atakuja hapa, kwanini hakunitaharifu?" Mama Kayoza aliuliza kwa ukali,

"Sasa sisi tungejuaje kama yangetokea haya?" Kayoza nae aliuliza,

"Sasa ndio yameshatokea, ujinga wenu utawaponza, sijui mkuu wa polisi ameyaacha hapa hapa au ameenda nayo?" Mama Kayoza aliongea kwa hasira,

"atakuwa ameyaacha" Kayoza alijibu,

"Atakuwa ameyaacha" Mama Kayoza alirudia maneno ya mwanae, ila yeye alirudia kwa kebehi huku akiwa amebana pua.

Baada ya hapo Mama Kayoza akaenda sake ndani kwa hasira huku akiwaacha wakina Kayoza wakiwa wamekaa wanatazamana kwa jicho la kulaumiana,

"Hakuna haja ya kumtafuta mchawi, sisi sote tumehusika" Omary aliongea huku macho yake yakielekea kwenye runinga,

"Kweli, tulikosea kumficha mama, ila hakuna kilichoharibika" Kayoza aliongea huku akijilaza katika kochi.

********************

Mkuu wa polisi hakuridhika kabisa na hali aliyokutana nayo, tayari akili yake ilimwambia kuwa kuna kitu kinafichwa katika familia ya wakina kayoza.

"yule Babu alisema kuwa kuna mwenzetu anatuzunguka, alikua anamaanisha Sajenti Minja au?",Mkuu wa polisi alijiuliza mwenyewe, kisha akaendelea,"na huyu Remmy nae....simuelewi kabisa, nilisikia kwa masikio yangu mwenyewe yule mama kasema OMMY, mara yule kijana akabadilisha akaita Remmy, mh.., kuna kitu kinaendelea hapa, ngoja nichunguze mwenyewe", Mkuu wa Polisi alikata shauri na kuamua kuifatilia mwenyewe ile kesi.

"Ila kama yule babu alisema amemsahau jina huyo askari anaetuzunguka, inawezenaje amsahau Minja?, ila hapana, hii kesi ngoja niichukue Mimi mwenyewe kimya kimya, nitaujua tu ukweli.

Hata yule kijana atakuwa ndio Omary Mkwiji, sasa sitokurupuka kumkamata, nitaangalia kwanza namna ya kupata ushahidi, hii kesi imeshakuwa nyepesi tayari. Hapa ni kuendelea kujifanya sijui kitu, alafu nakuwa nawachunguza pole pole" Mkuu wa polisi aliendelea kuongea peke yake ndani ya gari.

*******************

Jumapili tulivu, Omari na Kayoza, huku wakiongozana na happy binti mchungaji, walikuwepo katika maeneo ya hospitali pembeni ya kitanda cha Sajenti Minja,

Hapo Happy hakuvaa kistara kama anavyovaaga na badala yake alivaa suruali ya jeans iliyombana na juu alivaa fulana nyeupe iliyomkaa vema, ukiwa nae mbali huwezi kumjua ni kama yeye, labda ungepata bahati ya kumsogelea ndio ungemjua.

Pembeni ya kitanda alichokuwa amelazwa Sajenti Minja, hakuna aliyeruhusiwa kuongea neno lolote kutokana na hali ya Sajenti Minja.

Walimuangalia kwa dakika tano na kisha wakaenda kwenye eneo la kupumzikia watu walioenda kuwaangalia wagonjwa wao. Lilikuwa eneo safi lenye bustani na miti kadhaa kwa ajili ya kivuli, ila wao walijitenga sana na watu kwa ajili ya kuwa na Happy binti mchungaji.

"Kumbe mjomba wenu ndio yule?" Happy alimuuliza Omary wakati wakikaa na kipindi hicho Kayoza yeye aliwaacha umbali kidogo, alikuwa bize na simu yake,

"Ndiyo yule, vipi unamjua?" Omary akamtupia swali Happy binti mchungaji,

"Yule ameshawahi kuzaba vibao yule, namkumbuka vizuri" Happy alijibu huku akicheka kutokana na tukio alilolikumbuka la kupigwa makofi na Sajenti Minja,

"Alikupigia nini sasa?" Omary aliuliza kanakwamba hajui, kumbe anajua kila kitu,

"Tuachane na hayo bwana, nunua ice cream tule" Happy aliamua kuipotezea hiyo mada,

"Hapa hospitali hawawezi kuuza Ice cream, labda tutoke nje ya hili eneo" Omary alijibu,

"Ngoja tupumzike kwanza, tutaenda baadae" Happy aliongea,

"Kayoza njoo utupige picha mshkaji wangu" Omary alipaza sauti kumuita Kayoza aliyekuwa amejitenga na wao.

*******************

Wakati wakina Kayoza wakiwa nje ya hospitali, ndicho kipindi ambacho mama Kayoza na Mchungaji Wingo walikuwa wanaenda kumuangalia Sajenti Minja pia,

walipofika, wakamtafuta Daktari, kisha wakaongea nae maneno machache kabla ya kuruhusiwa kwenda kumuangalia Sajenti Minja,

"ila nimeamua kuvunja kanuni tu, kwa ajili ya heshima yako na mchungaji, kwa sababu muda wa kuangalia wagonjwa umeshakwisha",Daktari aliwaambia huku akielekea sehemu ilipo wodi aliyolazwa Sajenti Minja,

"asante baba, maana nisingekuja leo, hakuna ambae angejua hali ya mgonjwa pale nyumbani",Mama Kayoza alimshukuru Daktari,

"kwani wale vijana ambao unakujaga nao hapa ukai nao?",Daktari akamtupia swali Mama Kayoza,

"kwanini baba?, wale ni wanangu, ninachokula ndicho wanachokula", Mama Kayoza alijibu baada ya kuuliza swali,

"Basi hao wanao wametoka hapa muda si mrefu", Daktari alijibu,

"alah!, basi mimi hawakuniaga",Mama kayoza alimaliza namna hiyo.

"Sasa hivi wameshaujua mji, kila kona wanaijua" Mchungaji Wingo aliongea,

"Tena wanazurura hao, alafu kibaya zaidi uwa hawaagi" Mama Kayoza aliongea,

"Sasa Mimi naona mtoke, muda umeisha wakubwa zangu" Daktari aliongea huku akiwaimiza watoke,

"Jamani baba angu ebu niongezee hata dakika mbili tu" Mama Kayoza alimuomba Daktari,

"Mama uje baadae, wakubwa zangu wakikuta nimewaruhusu kuingia muda huu, kibarua change kitakuwa mashakani" Daktari aliongea huku akiendelea kuwahimiza watoke,

"Mama tutoke tu, tuje baadae" Mchungaji Wingo aliongea huku akitangulia kutoka na Mama Kayoza akamfuata kwa nyuma.

Wakamuona mgonjwa wao, kisha wakatoka kuelekea sehemu ya kupumzikia, kwa mbali wakawaona wakina Kayoza wako na Binti ambae hawakumtambua, tena huyo binti alikua wanabusiana(kiss) mdomoni na Omari, kila baada ya dakika.

Mama kayoza na Mchungaji Wingo wakawa wameshika njia ya kwenda walipo wakina kayoza,

"Mungu wangu, awa watoto wapumbavu sana" Mama Kayoza alilalama baada ya kuona wanamdhalilisha mbele ya Mchungaji,

"Alafu hata yule binti waliekuwa nae ni mjinga, eneo la hospitali unavaaje vile kama huna wazazi?" Mchungaji Wingo aliuliza huku wakiwa bado wanaelekea sehemu walipo wakina Kayoza.


Wakiwa wanazidi kuwasogelea na wamebakiza hata zisizo nyingi sana, Mara pasipo kutegemea, Mchungaji Wingo akatoa sauti ya mguno,

"mh!"

"vipi mchungaji?",Mama Kayoza akauliza..

***********ITAENDELEA*********

the Legend☆
 
Back
Top Bottom