Riwaya: Kijijini kwa Bibi

Riwaya: Kijijini kwa Bibi

Wakuu kuna episodes 4 za hii riwaya nimejaribu kuzitafuta leo bila mafanikio, hiyo ndio sababu iliyofanya nichelewe kupost mpaka muda huu. Nazo ni episode ya 35-38. Nyingine zote zipo. So tutaendelea na episode ya 39. Samahanini kwa usumbufu utakaojitokeza

the Legend☆
Usiwaze kamanda. Tupo pamoja...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA AROBAINI NA SABA.

__________________
ILIPOISHIA....
-----------------------------

Omari na Kayoza waligundua mchezo anaocheza Mkuu wa Polisi, na wote walinyong'onyea kwa kujua kwamba wameumbuka, kwa maana anaefuata kutambulishwa ni Omari.

"huyu nae anaitwa nani?, taja majina yake yote matatu, ili nijue kumbukumbu yako imerudi",Mkuu wa Polisi alimuuliza Sajenti Minja huku akimsogeza Omary mbele ya macho ya Sajenti Minja....

**********ENDELEA**********

..."jamani waungwana muda wa kuangalia wagonjwa umekwisha",Daktari mmoja mwenye umri ulioenda kidogo aliingia ndani ya wodi na kutamka maneno hayo,

"ebu tufanyie subra kidogo, kama dakika tano za nyongeza",Mkuu wa polisi alimwambia Daktari zamu ambaye alikuwa nae muda mrefu ,

"haiwezekani kamanda, ni makosa makubwa sana kuongeza muda wa ziada wa kumuangalia mgonjwa",yule Daktari mwenye umri mkubwa kidogo aliongea huku akiwafungulia mlango ikiwa ni ishara ya kuwaruhusu watoke,


"Minja mimi nitakuja baadae",Mkuu wa polisi alimwambia Sajenti Minja, ambae muda wote alikuwa kimya huku akijaribu kuvuta kumbukumbu zake kuhusu Omary,

"sawa mkuu",Sajenti Minja alijibu kwa sauti ya uchovu,


"baadae tukuletee chakula gani anko?",Kayoza alimuuliza Sajenti Minja,

"mleteeni juisi au uji, msisahau maji, haya nendeni nje waheshimiwa",Daktari wa zamu alidakia, kisha akawaondoa wodini wakina kayoza.

Sajenti Minja akageukia ukutani na kutabasamu,

"Anaitwa Omary mkwiji, hilo ndilo jina lake mkuu" Sajenti Minja aliongea peke na kuendelea kutabasamu.

Kayoza, Omary na Mkuu wa Polisi Waliondoka wakiwa na furaha sana,
Kayoza alipata tumaini jipya la kupöna, kwa sababu mtu aliekuwa anamsaidia amepona.

Huku Mkuu wa polisi akipata zaidi imani ya kumchunguza Sajenti Minja, nae alijikuta anatabasamu,

"Naona leo umefurahi mjomba kupona" Kayoza alimwambia Mkuu wa polisi baada ya kumuona akitasamu, na kumfanya Mkuu wa polisi ashtuke maana alikuwa anatabasamu bila kujijua,

"Eeh, ndio...kwani nyie hamjafurahia?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akijifanya ni kweli anafurahia Sajenti Minja kupona,

"Kwanini tusifurahi, lazima tufurahi" Omary alijibu huku akicheka,

"Jambo la heri sana, bora ameamka maana akishatengemaa kabisa kila kitu kitakuwa sana" Mkuu wa polisi aliongea,

"Kweli kabisa" Kayoza alijibu,

"Mnaelekea wapi sasa?" Mkuu wa polisi aliwauliza wakina Kayoza,

"Ni nyumbani tu, tukampe taharifa mama" Kayoza alijibu,

"Atafurahi sana akisikia mdogo wake amefungua macho" Mkuu wa Polisi aliongea huku akitabasamu,

"Tena sana, anaweza hata kuchanganyikiwa" Omary alimsapoti mkuu wa polisi,

"Sasa Mimi leo siwapeleki, kuna sehemu kuna kikao natakiwa ndani ya dakika kumi hizi, chukueni hii hela mkapande bajaji" Mkuu wa polisi aliongea huku akitoa noti shilingi elfu kumi na kuwakabidhi,

"Asante, ila baadae naimani baadae tutakutana hapa hapa" Kayoza aliongea huku akiiweka pesa mfukoni,

"Lazima nine baadae, kikao kikiisha tu nitakuja kushinda hapa hapa" Mkuu wa polisi aliongea,

"Haya, sasa sisi acha twende tukatafute hiyo bajaji ya kutupeleka nyumbani" Kayoza alimwambia Mkuu wa polisi,

"Sawa wajomba, baadae" Mkuu wa polisi aliongea huku akiingia katika gari yake na kuwaacha wakina Kayoza wakienda upande wa pili wa barabara ambapo ndipo bajaji zilikuwepo.

*******************



BAADA YA WIKI MOJA

Sajenti Minja aliruhusiwa kutoka hospitali, ila Mkuu wa polisi alimuomba akae nae nyumbani kwake, mpaka pale Sajenti Minja atakapotengemaa kabisa ndipo arudi kwake. Ilo halikupingwa, Sajenti Minja aliamua akae kwa muda kwa Mkuu wa polisi kwa maana ndani ya nyumba ya Mkuu wa polisi alikuwa anaweza kupata kila kitu alichokitaka kutokana maisha mazuri aliyokuwa nayo Mkuu wa polisi ambayo yalikuwa tofauti na maisha ya kwa dada yake.

Maisha katika nyumba ya Mkuu wa polisi yalikuwa ni mazuri sana, wakina Kayoza walikuwa wanaenda kila siku kumtembelea Sajenti Minja katika nyumba ya Mkuu wa polisi, na watu wote pale katika nyumba ya Mkuu wa polisi waliwazoea, kuanzia wafanyakazi, mke wa Mkuu wa polisi na mtoto wa kike na wa pekee wa Mkuu wa polisi.

Sasa tatizo lilikuwa kwa mtoto wa pekee wa mkuu wa polisi, ambae alikuwa anaitwa Martha, huyu Martha toka aanze kuzoeana na Kayoza amekuwa akimuonesha dalili zote za kumpenda, ila Kayoza hakuelekea kabisa, sio kwamba hakuwa na hisia na huyo binti, la asha, aliohofia mzimu ambayo ungeweza kumletea matatatizo anapokuwa katika mahusiano ya kimapenzi. Kwa hiyo alimuwekea ngumu kabisa.

********************


Mkuu wa polisi alifanikiwa kumpata kijana mmoja pale mtaani kwa wakina Kayoza, yule kijana aliitwa Ismail, ila wengi walizoea kumuita Suma, huyo kijana aliambiwa mkanda mzima jinsi ulivyo, kwa hiyo kazi yake ilikuwa kumchunguza Omari.

Suma alikua ni kijana mchangamfu sana, na kwa kuanzia tu, alianza kwenda katika kijiwe cha mchezo wa drafti ambacho Omari alipenda sana kwenda, hatua ya kwanza alifanikiwa kujua kuwa Remmy sio jina halisi la Omari, ila hata hivyo hakujua jina halisi la Omari, maana pale walikuwa wanamuita mzee wa supa, ni kutokana na mtindo wa magoli anayowafunga wenzake. Ila suma hakukata tamaa, akajipa moyo kuwa lazima aifanikishe kazi aliyopewa, maana hata posho aliyoahidiwa kupewa na Mkuu wa polisi, ilikuwa ni posho nzito, ilimtosha kununua kila kitu cha ndani.

Na sifa nyingine ya ziada, Suma aliweza kujenga mazoea ya haraka sana, tena na kila mtu.



**************


Jioni moja tulivu, Kayoza na Omari wakiwa nyumbani kwao,

"Twenzetu basi, maana sioni kama una dalili za kutoka" Kayoza alimwambia Omary,

"Si nilishakwambia najisikia hovyo, sijui ni malaria?" Omary aliongea kinyonge huku akiwa kitandani,

"Sasa unaumwa alafu unakaa ndani?, si uende hospitali man" Kayoza alimwambia Omary,

"Hela hamna kaka" Omary alijibu kinyonge,

"Acha mambo yako bwana, si umuombe mama, usimuogope bwana, yule ni mama yako" Kayoza alimwambia Omary,

"Sijamzoea kama wewe, basi kaniombee" Omary alimwambia Kayoza,

"Ngoja nikamwambie, ila usirudie tena, utakuja kufa umelala" Kayoza alimwambia Omary,

"Kamwambie mama bwana, acha blah blah blah nyingi" Omary alimwambia Kayoza,

"Mi ndo natoka hivyo, sirudi tena huku chumbani, naenda kumcheki mjomba" Kayoza aliongea huku akitoka nje,

"Poa, mwambie naumwa na ndio maana sijafika" Omary aliongea,

"Poa" Kayoza aliongea huku akitoka.

Alipofika sebuleni alimwambia mama yake hali ya Omary, kisha akaaga kuwa anaenda kwa Mkuu wa polisi kumuangalia mjomba ake.

++++++++

Kayoza alifika nyumbani kwa mkuu wa polisi na kumkuta Martha yupo peke yake, na Martha alimwambia Kayoza kuwa Sajenti Minja na Baba yake ambae ni Mkuu wa Polisi wametoka, wameenda kunyoosha miguu kidogo.

Sasa Martha akaona kuwa huo ndio muda mzuri wa kufanya, anachotaka kwa kayoza, Martha akaaga anaenda ndani Mara moja kufanya usafi na kumuacha Kayoza akiwa sebuleni anaangalia runinga.

Baada ya dakika chache.......
"mama weee, jamani panya panya",Martha alipiga kelele ndani ya chumba chake, kisha akatoka nje huku anakimbia, akaenda alipokaa Kayoza,

"Yaani wewe mkubwa hivyo unaogopa panya?" Kayoza alimtania Martha huku akimcheka,

"Usiseme huvyo Kayoza, kwanza naomba ukanisaidie kuua panya",Martha alimwambia Kayoza,

"Sasa huyo panya atakuwa amekaa tu anakusubiri?" Kayoza alimuuliza Martha huku akiendelea kumcheka,

"Yupo kwenye kabati, alafu limefungwa, yupo kwa ndani. Twende bwana ukamuue, uwa ananisumbua sana" Martha alimwambia Kayoza, Kayoza bila kubisha akanyanyuka alipokaa na kwenda chumbani kwa Martha, huku Martha akimfuata kwa nyuma.

Kayoza alipoingia ndani, Martha akaubana mlango na funguo kisha funguo akaidumbukiza ndani ya kifua chake, kisha akamgeukia Kayoza,

"Kayoza hakuna panya, ila ninachotaka toka kwako unakijua, Kayoza unaumiza moyo wangu sana, nifanyaje ili ujue nakupenda, eee?",Martha aliongea huku machozi yakimtoka,

"Dah, Martha si nilishakuambia haiwezekani lakini?" Kayoza aliuliza baada ya kukaa muda mrefu akimuangalia Martha kwa hasira,

"Naomba tu iwezekane, mpaka Mimi kufikia hata hii ya kukutamkia maneno haya, ujue hisia zangu zimenishinda" Martha aliongea huku akipiga magoti,

"Sawa nimekuelewa, naomba unifungulie mlango nitoke nje" Kayoza aliamua kumkubalia ili amridhishe Martha,

"Hapana sitaki utoke" Martha aliongea kwa hisia huku akimtazama Kayoza...

mara sauti ya Mkuu wa Polisi ambaye ndiye Baba yake Martha ikasikika mlangoni,


"we Martha unaongea na nani uko chumbani? Ebu nifungulie mlango"

**********ITAENDELEA***********

the Legend☆
 
RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA AROBAINI NA NANE.

__________________
ILIPOISHIA....
------------------------------

Kayoza alipoingia ndani, Martha akaubana mlango na funguo kisha funguo akaidumbukiza ndani ya kifua chake, kisha akamgeukia Kayoza,

"Kayoza hakuna panya, ila ninachotaka toka kwako unakijua, Kayoza unaumiza moyo wangu sana, nifanyaje ili ujue nakupenda, eee?",Martha aliongea huku machozi yakimtoka,

"Dah, Martha si nilishakuambia haiwezekani lakini?" Kayoza aliuliza baada ya kukaa muda mrefu akimuangalia Martha kwa hasira,

"Naomba tu iwezekane, mpaka Mimi kufikia hata hii ya kukutamkia maneno haya, ujue hisia zangu zimenishinda" Martha aliongea huku akipiga magoti,

"Sawa nimekuelewa, naomba unifungulie mlango nitoke nje" Kayoza aliamua kumkubalia ili amridhishe Martha,

"Hapana sitaki utoke" Martha aliongea kwa hisia huku akimtazama Kayoza...

mara sauti ya Mkuu wa Polisi ambaye ndiye Baba yake Martha ikasikika mlangoni,

"we Martha unaongea na nani uko chumbani? Ebu nifungulie mlango"

**********ITAENDELEA***********

..."hakuna kitu daddy",Martha alimjibu Mkuu wa polisi,

"kwa hiyo unaongea peke yako uko"Mkuu wa polisi akamtupia mwanae swali jingine,

"si naongea na simu",Martha akajibu.

"Fungua basi mlango niingie" Mkuu wa polisi akamwambia mwanae,

"Daddy navaa bwana, kwani unataka nini huku?" Martha alimjibu baba yake huku akideka.

Hivyo ndivyo alivyolelewa na wazazi wake, amelelewa malezi ya kujibishana na wazazi wake kama rafiki zake,

"Si nilitaka nikuone mwanangu, au vibaya mama?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akiwa mlangoni,

"Nakuja sebulebi daddy, mammy umemuacha wapi?" Martha aliuliza,

"Nimerudi nae, ameenda kuoga" Mkuu wa polisi alijibu huku akiamua aondoke zake, na kurudi sebuleni kuongea na Sajenti Minja,


"naweza kupata juice",Sajent Minja alimuuliza Mkuu wa polisi alipokua anakaa,

"mhmm..sidhani kama ipo, ebu ngoja, we Martha, marthaa",Mkuu wa polisi alijibu kisha akamuita mwanae,

"nakuja daddy" Sauti ya Martha ilisikika kutoka chumbani kwake.

Baada ya sekunde chache Martha akawa mbele ya Sajenti Minja na baba yake,

"shikamoo anko",Martha alimsalimia Sajenti Minja,

"marhabaaa anko, kuna juisi?",Sajenti Minja aliitikia, kisha nae akauliza swali,


"ipo anko,",Martha alijibu,

"naomba unipe ya pera",Sajenti Minja aliwasilisha ombi lake, mmmh, ya pera hamna, ipo ya orange, strawberry,mango na passion",Martha alijibu,

"nipe ya chungwa na maji ya baridi",Sajenti Minja aliagiza na martha akamletea,

"Vijana wangu hawajaja leo?" Sajenti Minja alimuuliza Martha, alikuwa akiwaulizia wakina Kayoza,

"Hawajafika anko" Martha alijibu huku nafsi yake ikimsuta kwa maana aliongea uongo,

"Leo naona watakuwa wamechoka" Mkuu wa polisi alimwambia Sajenti Minja,

"Wamechoka wapi, itakuwa wameona nimeshapona kwa hiyo hawaoni umuhimu wa kuja kunijulia hali" Sajenti Minja aliongea,

"Acha wapumzike, maana wale watoto walikuwa wanashinda hospitali mpaka nikawa nawahurumia" Mkuu wa polisi aliwatetea wakina Kayoza,.

"Hakuna haja ya kuwahurumia, hilo ndilo lilikuwa jukumu lao, mama yao umri wake umeshakwenda, anatakiwa apumzike" Sajenti Minja aliongea,

"Wameshawahi kuishi Dodoma ee?" Mkuu wa polisi aliuliza swali lililomshtua Sajenti Minja,.

"Nani alikwambia?" Sajenti Minja aliuliza huku akijifanya anacheka ili kuuficha mshtuko wake, ila tayari Mkuu wa polisi alikuwa ameshamsoma,

"Waliniambia wenyewe, wakadai wamemaliza pale UDOM ila hawajachukua vyeti vyao" Mkuu wa polisi alizidi kutiririka na kuendelea kumshtua Sajenti Minja,.

"Yah ni kweli walimaliza pale" Sajenti Minja alijibu kifupi,

"Sasa ni kwanini hawajachukua vyeti?" Mkuu wa polisi aliuliza swali la kumtega Sajenti Minja ili zone kama jibu lake litafanana na la wakina Kayoza,

"Hawajachukua vyeti?, mbona Mimi hawajaniambia kama hawajachukua vyeti vyao?" Sajenti Minja alijifanya kushangaa huku akiuliza,

"Alah!!! Kumbe hujui?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"Aisee hawakuniambia, labda wamefanya makosa wanaogopa kuniambia, au wamekula ada?" Sajenti Minja aliamua kumuigizia sasa Mkuu wa polisi, alivyokuwa anaongea utasema kweli yaani,

"Wameniambia wameshindwa kulipa ada ndio maana hawajachukua" Mkuu wa polisi aliamua kumwambia ukweli,

"Wanekudanganya, niliwapa pesa yote, itakuwa wamefeli au wamekula ada...yaani awa watoto awa, utakuta hata mama yako hajui kama hawana vyeti" Sajenti Minja alijifanya kusikitika,

"Kwani walikuwa wanasomea nini?" Mkuu wa polisi aliuliza swali jingine lilimuweka mtegoni Sajenti Minja,

"Hawajakwambia?" Sajenti Minja alimuuliza mkuu wa polisi huku akijitahidi kuvuta kumbukumbu ya masomo waliyokuwa wanasoma wakina Kayoza,

"Hawakuniambia" Mkuu wa polisi alijibu huku akibonyeza controller ya runinga,

"Mi hata nilikuwa sifuatilii wanachukua kozi gani, ili mradi nilikuwa nawalipia ada wamalize tu chuo" Sajenti Minja alilipangua swali la Mkuu wa polisi,

"Ulikuwa unatakiwa uwafuatilie bwana" Mkuu wa polisi alimwambia Sajenti Minja,

"Shauri yao bwana kama walichezea masomo, ngoja nikajimwagie maji" Sajenti Minja alijibu huku akinyanyuka na kuondoka ili kuyakwepa maswali ya Mkuu wa polisi, maana yalimpa mashaka na akahisi inawezekana babu wa monchwari alimchoma.

Kuanzia hapo akaanza kuishi kwa wasiwasi akihisi kuwa inawezekana kabisa Mkuu wa polisi anawapeleleza wakina Kayoza pasipo wao kujua.

*******************

Baada ya Martha kumuhudumia Sajenti Minja, Martha alirudi chumbani kwake, usiku ulikuwa umeshaingia,


"sasa mimi nitatokaje humu?",Martha alipokelewa na swali la Kayoza ambae alikuwa yuko ndani ya kabati,

"subiri bwana, sasa hivi wanaenda kulala, sebule itakuwa haina mtu",Martha alimjibu Kayoza kwa kujiamini,

"Alafu mbona unajiamini sana, we huogopi kuniingiza mwanaume chumbani kwako?" Kayoza aliuliza huku akiwa ana hasira,

"Lazima nijiamini, sasa nimuogope nani wakati nipo kwetu?" Martha alijibu kwa nyodo huku akitandika vizuri kitanda chake,

"Usiwe unajiamini kwa kila kitu, vingine vitakutokea puani, shauri yako" Kayoza aliongea kwa hasira huku akichungulia dirishani,

"Nikuletee chakula?" Martha alimuuliza Kayoza,

"Hapana, sihitaji" Kayoza alijibu huku akionekana amesusa,

"Ukisusa sisi twala" Martha aliongea kwa madaha huku akielekea sebuleni.

Martha alibeba chakula kingi na kwenda kulia chumbani kwake kwa lengo la kula pamoja na Kayoza.

"Njoo rule bwana K, usiwe unasusa Susa kama mtoto wa kike" Martha alimwambia Kayoza huku akimpa kijiko, lakini Kayoza hakutaka hata kujisumbua kupokea, badala yake alikaa tu kitandani huku mkono ukiwa shavuni.

Baada ya masaa mawili, kila mtu aliyekuwa sebuleni alienda kulala, sebule ikabaki tupu.

Ilikuwa ni mishale ya saa nne usiku, katika chumba cha Martha kulikuwa na sauti za mabishano ambazo zilikuwa zinasikika kwa chini chini sana,

"Martha niachie niende, mama atakua na wasiwasi nyumbani",Kayoza alimlalamikia Martha,

"ni vigumu kutoka Kayoza, lazima mlinzi kesho atamwambia baba alafu iwe msala kwako",Martha alijibu akiwa na lengo la kumzuia Kayoza asiondoke ili atimize azma yake ya kufanya nae mapenzi,

"kulala na wewe ni kitu ambacho akiwezekani Martha, kwanza tulikubaliana kuwa watu wakienda kulala ndio unanitoa, ona sasa unaleta sababu nyingine",Kayoza aliongea kwa kulalamika,

"isiwe tabu mwenzangu, wewe lala kitandani mimi nitalala chini",Martha aliongea huku akikunjua godoro jingine alilolitoa juu ya kabati.

"Nani kakwambia anataka kulala hapa?" Kayoza aliuliza kwa jazba,

"Alafu usiongee kwa sauti kubwa, Baba akisikia itakuwa tabu kwako, shauri yako" Martha alimtisha Kayoza,

"Basi nitoe nje niende kwetu" Kayoza aliongea kwa sauti ndogo,

"We lala, ikifika saa saba au saa sita nitakutoa, mlinzi atakuwa amesinzia" Martha alimlaghai Kayoza, ikambidi alale, ila kwa sharti moja, wasilale pamoja, ambapo Martha alikubali na kutandika godoro chini na kitandani alilala Kayoza.


Ilimchukua saa moja tu Kayoza kupata usingizi, akalala fofofo huku akikoroma, saa sita ikafika, ikapita na saa saba ikafika na kupita na sasa ilikuwa saa Tisa usiku,

Martha akakurupuka kutoka katika godoro la chini, taratibu akavua nguo zake zote, kisha akapanda kitandani kwa hadhari ya kutomshtua Kayoza, akaingia ndani ya blanketi, kisha akaanza kufungua zipu ya suruali ya Kayoza,

"mmmh, mbona yuko hivi?",Martha aliguna baada ya kumuona Kayoza kalegea kama mtu aliepoteza fahamu, ila hiyo haikumzuia kuendelea na anachokifanya, akafanikiwa kuishusha suruali ya Kayoza hadi miguuni, sasa akawa anajiweka sawa ili atimize lengo lake, Kayoza aliinuka kama mshale, kwa kasi ya mwanga na meno yake yakapenya sawia katika shingo ya Martha,

"mamaaaaaaaa nakufaaaaaaaaa",sauti ya Martha ilisikika kwa nguvu na kuwaamsha watu wote waliolala mpaka majirani..............

****"*****ITAENDELEA************

*kwa Mara nyingine tena Kayoza ameharibu, tena ameharibu ndani ya nyumba ya Mkuu wa polisi, je kelele alizotoa Martha zitasababisha Kayoza akamatwe?

*Mkuu wa polisi amemtuma mtu ili amchunguze Omary huku na yeye akianza kumchunguza Sajenti Minja, je atafanikiwa kupata anachokitaka?

the Legend☆
 
RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA AROBAINI NA TISA.

__________________
ILIPOISHIA....
------------------------------

Martha akakurupuka kutoka katika godoro la chini, taratibu akavua nguo zake zote, kisha akapanda kitandani kwa hadhari ya kutomshtua Kayoza, akaingia ndani ya blanketi, kisha akaanza kufungua zipu ya suruali ya Kayoza,

"mmmh, mbona yuko hivi?",Martha aliguna baada ya kumuona Kayoza kalegea kama mtu aliepoteza fahamu, ila hiyo haikumzuia kuendelea na anachokifanya, akafanikiwa kuishusha suruali ya Kayoza hadi miguuni, sasa akawa anajiweka sawa ili atimize lengo lake, Kayoza aliinuka kama mshale, kwa kasi ya mwanga na meno yake yakapenya sawia katika shingo ya Martha,

"mamaaaaaaaa nakufaaaaaaaaa",sauti ya Martha ilisikika kwa nguvu na kuwaamsha watu wote waliolala mpaka majirani.............

****"*******ENDELEA************

...Ni kitendo cha dakika tano tu, familia nzima ilikuwa imeuzunguka mlango wa chumba cha Martha,

"we Martha fungua mlango, kuna nini?",Mkuu wa polisi aliita kwa sauti kubwa, lakini hakujibiwa na mtu, na kipindi hicho wale majirani wa karibu na nyumba ya Mkuu wa polisi walikuwa wameshafika kutoa msaada kwa tukio lolote haya ambalo lingetokea.

Aliendelea kuita kwa muda wa dakika tano, lakini hali ilikuwa ile ile.

Ndipo wakashauriana na baadhi ya majirani ambao walikuwa tayari wamefika kutoa msaada, kwa sauti moja wakakubaliana kuvunja mlango.

"Tunaweza kupata kisu au bisibisi?" Jirani mmoja aliuliza baada ya kugundua ule mlango wa kitasa ni mgumu sana, yule bwana aliuliza huku akimuangalia Mkuu wa polisi aliyekuwa ameganda tu,

"We Dada ebu tuletee kisu" Sajenti Minja alimwambia Dada wa kazi ambayo alikuwa jirani nae, kisha yule Dada akakimbilia jikoni haraka na kurudi visu viwili na kumpatia yule bwana jirani aliyeagiza hicho kifaa.

Kisha kwa kushirikiana watu wengine waliopo ple wakafanikisha zoezi lao la kutegua kitasa cha mlango na mlango ukafunguka.

Sasa walichokiona mbele yao ndicho kilikuwa kitu cha ajabu sana kilichopelekea mke wa Mkuu wa Polisi kupoteza fahamu pale pale.

Mkuu wa polisi yeye aliangalia mara moja tu, kisha akatoka nje huku macho yake yakiwa yametawaliwa na machozi, baadhi ya majirani wakaenda kumfariji na wengine wenye roho ngumu walichukua shuka lililokuwepo juu ya kitanda na kuusitiri mwili.

Ulikuwa mwili wa Martha ukiwa na chupi tu mwilini, ulikuwa umelala juu ya kitanda, na damu zikiwa zimemuenea shingoni zikiwa zimechirizika kwenda sakafuni, alikuwa tayari ni mfu, tayari mwili umetengana na roho kutokana na tamaa zake za mwili.

"Ni nini kimemkuta?" Jirani mmoja alimuuliza Sajenti Minja,

"Sasa Mimi nitajuaje ndugu yangu wakati mlango tumevunja wote na kuukuta mwili umelala?" Sajenti Minja alijibu huku moyoni mwake akiwa na mawazo ya kuwa inawezekana Kayoza ndiyo aliyefanya hill tukio.

Sajenti Minja aliamini hivyo baada ya kuona sehemu ya dirishani kulikuwepo na vioo vilivyopasuka, pamoja na nondo kadhaa kuondolewa, akakumbuka Kayoza alishawahi kuondoka kwa mtindo huo kipindi cha nyuma alipojaribu kumtegea askari ndani ya lodge kipindi anaanza kuipeleleza hii kesi ya Kayoza mjini Dodoma.

"Sasa kama ametoka akiwa kama mzimu si ataenda kupoteza fahamu maeneo ya jirani tu? Nitoke nikamuangalie nini? Nikitoka pia watu wa hapa si watanishangaa?, bora nibaki tu hapa hapa huku nikiomba Mungu amfikishe salama nyumbani" Sajenti Minja aliongea peke yake huku akielekea sebuleni alipokaa Mkuu wa polisi na majirani wengine waliokuwa wanamfariji.

Ila hakuridhika kukaa tu pale, kuna fikra zilimjia. Akanyanyuka taratibu na kuelekea nje ya nyumba lakini ndani ya geti. Akamtafuta mlinzi na kumkuta akiwa amekaa kimajonzi sana,

"Ni kitu kimefanya tukio hili?" Sajenti Minja alimuuliza mlinzi kwa ajili ya kutaka kujua kama ni kweli Kayoza alikuja hapo,

"Nashindwa hata kueleza, ila nimekiona kiumbe cha ajabu sana kikitokea chumbani kwa Martha, sijui ni nini lile" Mlinzi aliongea huku akiwa anasimumuka mwili,

"Kuna nani aliingia leo kipindi tumetoka?" Sajenti Minja alimuuliza tena huku akitaka kujua kama mlinzi atamtaja Kayoza ingawa tayari Sajenti Minja alishagundua kuwa yale mauaji yamefanywa na Kayoza, sasa hapo alitaka kujua kama Mlinzi anaweza kumtaja Kayoza ndio pekee aliyeingia kipindi hawapo au kuna wengine,

"Aliingia yule mjomba wako mpole mpole" Mlinzi alijibu na kumfanya Sajenti Minja aone hatari iliyopo mbele yao, maana kama Mkuu wa polisi akimbana mlinzi kuhusu watu waliokuja siku hiyo, basi lazima atajwe Kayoza,

"Huyo tupo nae ndani mbona, hakuna mwingine aliyekuja zaidi ya huyo?" Sajenti Minja alizuga ili kumfanya mlinzi asimuhisi vibaya Kayoza,

"Leo hakuna zaidi ya huyo" Mlinzi alijibu na kumfanya Sajenti Minja ahisi hatari kubwa iliyopo mbele yao,

"Sasa ndugu yangu, kwa usalama wako, ni bora tu ukimbie, kwa maana hii kesi unaangushiwa wewe, nimemsikia boss wako ndani akisema hivyo" Sajenti Minja aliongea baada ya kufikiria kwa muda, alifanya hivyo ili kumtisha mlinzi akimbie ili ushahidi wa Kayoza kuingia ndani kwa Mkuu wa polisi ufutike,

"Lakini Mimi sijaua, kwanini nikamatwe?" Mlinzi aliuliza huku akitetemeka,

"Haukamatwi kwa kuua, utakamatwa kwa uzembe wa kumuachia huyo muuaji apite" Sajenti Minja alizidi kumtisha mlinzi,

"Lakini utakuwa uonevu huo" Mlinzi alilalamika huku akitaka kulia,

"Acha ujinga, ni bora tu ukimbie kabla hujatiwa mikononi mpwa polisi, mpaka wake kujua wewe hujaua, itakuwa umeshakuwa mlemavu tayari kwa ajili ya mateso utakayopata" Sajenti Minja alizidi kumtisha mlinzi,

"Dah, sasa utanisaidiaje?" Mlinzi aliuliza baada ya kufikiria kwa muda,

"We mpumbavu nini, nikupe msaada gani zaidi ya huu niliokupa sasa hivi?" Sajenti Minja aliuliza huku akijifanya ana hasira,

"Takimbilia Wapi na sina hata pesa ya nauli?" Mlinzi aliuliza,

"Wewe mwanaume mwenzangu, nakusaidia huku nikiamini hata Mimi naweza kupata tatizo na wewe ndio unaweza kuna kuwa msaada" Sajenti Minja aliongea huku akiingiza mkono mfukoni na kutoa noti nyingi nyingi zilizokaa bila mpangilio na kumpatia mlinzi,

"Dah, asante sana" Mlinzi alipokea na kuzitia mfukoni,

"Sasa usikimbie hivyo kama Mbwa, hapa unatakiwa utoke kama unaenda kujisaidia nyuma ya nyumba, ukifika tu nje ya geti ndio uanze riadha" Sajenti Minja alimwambia mlinzi ambayo aliishia kujibu kwa kichwa tu, kisha akafanya kama alivyoelekezwa na Sajenti Minja na kutokomea nje ya geti na kumuacha Sajenti Minja akisikitika kwa mengi, kwanza kumpotezea hajira huyo mlinzi, pili kumpoteza Martha, msichana mdogo aliyekuwa mchangafu na waliyezoena kwa Siku chache tu, na tatu ni Kayoza.

***************

Majirani wengine wa mkuu wa polisi wakatoa taharifa polisi na hospitali,

gari ya wagonjwa ikaenda usiku ule ule kuuchukua mwili wa Martha.

Ambulance haikuchukua muda sana barabarani ilifika haraka sana nyumbani kwa Mkuu wa polisi, nadhani na cheo alichonacho kilichangia gari hiyo kuwahi kufika na sababu ya pili ni kutokana na kutokuwepo na magari mengi barabarani usiku ule.

Gari ya hospitali ilipofika, mwili wa Martha ulibebwa juu juu na kuingizwa ndani ya gari, kisha gari ikaondoshwa kwa kasi sana, utasema ndani amelazwa mgonjwa ambayo anahitaji matibabu ya haraka, kumbe amelazwa maiti ambayo hata useme ukimbize gari mpaka iruke hewani kama ndege lakini bado hutoweza kuurudisha uhai wake.

Ambulance ilikuwa inasindikizwa na gari mbili za polisi, moja walikaa askari wa kawaida wapatao sita, na nyingine alikuwepo Sajenti Minja na askari wawili, ila Sajenti Minja hapa alisimama kama mwanafamilia na wala hakuwa polisi.

Iliwachukua dakika ishirini gari ya wagonjwa kufika hospitali.

Walipofika walipokelewa haraka haraka, mwili wa Martha ukachukuliwa na kupelekwa chumba cha uchunguzi, baada ya uchunguzi, mwili ukapelekwa monchwari.



*******************


Kayoza alipomaliza kumnyonya Martha damu, alivunja nondo za madirisha na kutokea dirishani, mlinzi alimuona, ila kwa kuwa Kayoza alikuwa anatisha sana, yule mlinzi alichofanya ni kujificha katika bustani ya maua kwa kulala chini mpaka kayoza aliporuka ukuta na kutokomea pasipokujulikana.


Mzimu uliendelea kumshika Kayoza mpaka alipofika katika mlango wa kuingilia kwao, alipofika mlangoni, akadondoka chini, kisha akapoteza fahamu.

Mama Kayoza na Omari walikuwa hawajalala kwa sababu ya wasiwasi, walivyosikia kishindo mlangoni, wote wakashtuka,

"ebu chungulia kuna nini?",Mama kayoza alimwambia Omari,

"mh, mama",Omari alitoa mguno wa uoga baada ya kuambiwa achungulie nje kupitia dirishani,

"ebu acha uoga uko, chungulia hata kwa hapo dirishani",mama Kayoza alizidi kumuandama Omari,

Omari akafungua dirisha kidogo, kisha akachungulia,

"eh!",Omari akashtuka,

"Mbona umeshtuka hivyo, umeona nini?",mama Kayoza akahoji baada ya Omary kushtuka,

"Kayoza",Omari alijibu huku akiundea mlango, alipoufikia alifungua, wakatoka nje.

Omari na Mama Kayoza wakawa wanamuangalia Kayoza aliyekuwa amelala chini.

Mama Kayoza aliogopa sana, kwa sababu hakuwai kumuona Kayoza akiwa ametoka kunyonya damu, ila Omari alijua kila kitu.

"Mbebe basi umuingize ndani" Mama Kayoza alimwambia Omary,

"Sasa mama Mimi peke yangu nitamuweza?" Omary aliuliza huku akiwa anajaribu kumuinua,

"Tatizo lenu uwa mnajilegeza sana" Mama Kayoza aliongea huku akijaribu kuibeba miguu ya Kayoza na Omary akiwa upande wa kchwa cha Kayoza huku nae akiwa anajitahidi kukiinua.

Wakawa wanaangaika kumbeba ili wamuingize ndani.

Wakiwa bado wanaangaika kumuinua Kayoza, walishtushwa na gari iliyokuwa inakuja upande waliopo, ghafla hata kabla hawajaamua chochote, lile gari tayari lilikuwa mbele yao, likaenda kusimama pale pale walipokuwepo.

wote walishtushwa baada ya kugundua kuwa lile gari ni la polisi...

*********ITAENDELEA*********"*

the Legend☆
 
Back
Top Bottom