Riwaya: Kijijini kwa Bibi

Riwaya: Kijijini kwa Bibi

KIJIJINI KWA BIBI--54.

...maneno aliyoyatamka Omari, watu wote ambao walikuwa jirani nae akuna hata alielewa alichokimaanisha, Sajenti Minja peke yake ndiye aliyekuwa anaelewa kinachoendelea,

Sajenti Minja alipogundua Omari amekufa, alilia sana. Na Kayoza ndio alichanganyikiwa zaidi, kwa maana alipata mapigo mawili kwa Mara moja, la kwanza ni kifo cha rafiki yake aliyetoka nae mbali toka mwanzo wa matatizo mpaka walipofikia, na pigo la pili ni kifo cha bibi yake ambaye ndio alikuwa msaada pekee wa kumsaidia mzimu umuachie.

Sasa ikawa misiba miwili ndani ya nyumba moja.

Misiba iliyoletwa na mkuu wa polisi, mmoja aliudhamilia ila mwingine hakuhudhamilia ila umetokea tu pasipo kutegemea na aliyesababisha hiyo misiba hana habari kama kitendo chake kimemuondoa mtu ambaye hausiki kabisa katika mipango yake.

Na jambo vzuri ni kwamba hakuna aliyemuona mkuu wa polisi wakati akifanya tukio hilo isipokuwa Omary pekee ambaye nae ameshamtaja aliyemuua.

Wanandugu walikaa na Sajenti Minja, na mwisho wakakubaliana kuwa Omari azikwe pale pale ili kuepusha gharama. Lakini Sajenti Minja alipinga na kusema yeye atagharamia kila kitu kuhusu mwili wa Omary, na alichofanya ni kuwasiliana na wazazi wa Omary na kisha ndugu wa Omary walifika Bukoba na wakauona mwili wa ndugu na wenye kulia wakalia.

Baada ya hapo ndugu hao waliondoka na mwili wa ndugu yako na kwenda nao Tanga kwa ajili ya maziko.

Huku kwa Bibi Kayozs Wakafanya maziko ya Bibi yake Kayoza.
Walifanya maziko ya heshima kwa bibi Kayoza kwa maana yeye nae alikuwa make wa chief ambaye ndiye Babu yake Kayoza ambaye ndiye inaesemekana ndio huo mzimu aliokuwa nao Kayoza.

Msiba ulipoisha, Sajenti Minja alimuita Kayoza na kumuweka kitako,

"yaliyotokea nafikiri umeyaona, ni kama ajali kazini na hakuna jinsi zaidi ya kujipanga upya, maana bibi yako tuliekuwa tunamtegemea kuwa msaada kwako, amekufa, na Omari nae amekufa",Sajenti Minja alimwambia Kayoza ambae muda wote alikuwa amekaa kimya,

"kwani huyo aliyempiga risasi Omari ulimuona?",Kayoza akamuuliza Sajenti Minja,

"sikumuona na wala sikubahatika kuongea na Omari, ila neno la mwisho aliloniambia ni MKUU WA POLISI",Sajenti Minja alimfahamisha Kayoza,

"ina maana Mkuu wa Polisi ndiye aliempiga risasi?",Kayoza akahoji,

"mimi ndio nimeelewa hivyo, na niliwaambia kuwa nilimuona Mkuu wa Polisi, nyie mkabisha, haya ndio matokeo yake sasa",Sajenti Minja aliongea kwa uchungu,

"nafikiri atakuwa bado hajaondoka pale Guest, na naimani ataondoka maiti",Kayoza aliongea huku akiwa anaondoka, hiyo kauli ikamshtua Sajenti Minja,

"njoo, unakwenda wapi?",Sajenti Minja alimzuia Kayoza,

"nipo hapa hapa",Kayoza alijibu huku akiwa amesimama mlangoni,

"sasa mbona unaondoka huku tukiwa bado hatujafikia muafaka?",Sajenti Minja alimuuliza Kayoza,

"muafaka gani tena?",Kayoza aliuliza kwa jazba,

"ya yaliyotokea na hatua za kuchukua",Sajenti Minja aliongea kwa kubembeleza,

"wewe uliniambia imetokea kama ajali na muafaka ulioniambia ni kujipanga upya, ila kwa kuwa huyu Mkuu wa Polisi amefanya ujinga kama kulipa kisasi kwa binti yake, ila akamuua Omari ambae hausiki na kifo cha binti yake, pia amesabisha zoezi la kutolewa mdudu mwilini kwangu lishindikane, basi adhabu anayostahili ni kifo, tena nitamuua nikiwa mzima kabisa, tena kwa mikono yangu miwili",Kayoza aliongea huku machozi yakimtoka, moja kwa moja akaamua kuenda nje kwa kuwa aliona kuendelea kuogelea hilo jambo ni kujiongezea hasira tu,

"hapa nisipokuwa makini, naweza kumpoteza na huyu Kayoza",Sajenti Minja aliongea huku akijilaza katika kajitanda cha pale chumbani.

"Mkuu wa polisi anachofanya ni kisasi, kama amemuua Omary, basi na Kayoza nae anahitajika kuuwawa, sio Kayoza peke yake, hata Mimi ni mmoja kati ya watu wanaowindwa na mkuu wa polisi, sasa sijui yupo peke yake au amekuja na watu wengine wa kumsaidia? Hii ni vita, tena vita ambayo tunapigana na adui aliye na silaha, cha muhimu ni kuwa makini, au tuondoke tu huku kwa maana hatuna cha kufanya tena, kilichotuleta kimeshindikana" Sajenti Minja alikuwa anawaza

******"***********

Mkuu wa Polisi aliamini kwa asilimia zote kuwa, pale alipofikia, hakuna aliegundua kati ya wakina Sajenti Minja.

"nimeanza na yule kibaraka, alafu anafata yule mshenzi Minja, Yuda Eskarioti, anaisaliti serikali?",Mkuu wa Polisi alijiuliza mwenyewe huku akijimiminia mzinga wa konyagi katika glass ndogo iliyokuwepo juu ya meza katika chumba chake.

"Hivi kwanini nilivyogonga mlango asingekuja Minja kufungua? angeanza yeye kufa kazi ingekuwa rahisi sana. Ila hata hivyo sawa tu, kwa maana wanapambana na adui wasiyemtambua, hata atumie mbinu zake za kijeshi sijui, hawezi kunijua" Mkuu wa polisi aliongea kisha akatoa cheko kubwa sana alilolishushia na tusi la nguoni kumuelekea Sajenti Minja kisha akagida tena ile konyagi iliyokuwa katika glass yake ndogo iliyopo juu ya meza.

"Alafu hii kazi imekuwa rahisi sana, kumbe naweza kuimaliza mapema kuliko hata nilivyodhani?, inawezekana, inawezekana kabisa, nataka Sikh ninayorudi shinyanga, nirudi nikiwa sina kisasi na mtu, nirudi nikaanze upya katika maisha yangu. Hivi utajisikiaje unapobahatika kupata mtoto mmoja, tena kwa tabu sana na miaka Mingi sana sana ya kusubiri huku ukivumilia maneno mengi sana kutoka katika jamii iliyokuzunguka?, alafu anatokea mpumbavu mmoja na kumuua huyo mtoto, ni lazima uchanganyikiwe, ni lazima uone dunia inakuelemea, dah jamani Martha wangu, my martha, baba yako nipo kwa ajili ya kukulipia kisasi, damu yako haijapotea bure mwanangu" Mkuu wa polisi aliongea huku akiwa anaiangalia picha ya Martha iliyokuwa katika simu yake ya mkononi.

Siku hiyo aliifanya kama sherehe kwake, maana alikuwa anakunywa tu, huku alitaja sana jina la Sajenti Joel Minja.

Saa moja baadae akawa hajitambui wala hajielewi, alizima huku akiwa amekaa katika kochi la chumba cha Guest.

*********************

"Hivi si naweza tu kummaliza huyu mtu, mbona hanishindi kabisa, au nitakuwa namuonea? Lakini mbona na yeye amemuonea Omary, Omary hana hatia, Omary alipaswa kufa kwa mipango ya Mungu na wala hakupaswa kufa kinyama namna hii tena ugenini. Ni vipi wazazi wake watajisikia? Haiwezekani kwa kweli, hii kitu kuivumilia ni sawa na kuacha matatizo yaendelee ingali una ufumbuzi wa kufumbua kinachokukabili" Sajenti Minja alikuwa akifikiri huku macho yake yakiangalia juu ambapo kulikuwa na paa ya nyumba ambayo ilijaa uchakavu kiasi.

Sajenti Minja baada ya kufikiria sana, akaamua kwenda katika Guest aliyofikia Mkuu wa Polisi, akupata tabu kuingia ndani, akaenda mpaka ulipo mlango wa chumba alichofikia Mkuu wa Polisi, kwa taratibu na tahadhali kubwa, huku akiwa ameweka chupa ya soda katika mfuko wake wa suruali, kwa ajili ya kummaliza Mkuu wa Polisi.

Tayari roho ya kinyama ilikuwa imefunika damu ya Sajenti Minja, roho iliyokuwa na imani ya kuwa njia nzuri ya kujilinda ni kumuua adui unayepambana nae.

Sajenti Minja ameamua kuua na hakutaka kwenda na bastola bali ameona silaha inayomtosha ni chupa ya soda tu.

Akashika kitasa cha mlango, kisha akaminya kwa chini...

**********ITAENDELEA***********

the Legend☆
 
KIJIJINI KWA BIBI - 55

..mlango haukufunguka,
"amejifungia kwa ndani huyu",Sajenti Minja aliongea peke yake.
Kisha akainamisha jicho lake mpaka kwenye tundu la ufunguo, pia hakuweza kumuona kwa ajili ya ufunguo uliokuwepo pale.
Sajenti akaamua kuahirisha hazma yake, akatoka nje na kuelekea nyumbani.

Kayoza muda wote alikuwa na mawazo tu, alikuwa hataki kuongea na yeyote zaidi ya Sajenti Minja. Nyele alikuwa hachani, mafuta hapaki, nguo moja aliweza kuvaa hata wiki, hakuwa mtanashati tena kama zamani, wageni wa eneo lile walikuwa wanamuona kama mvuta bangi.

"vipi anko?",Kayoza alishtuliwa na sauti ya Sajenti Minja,
"safi, ulikuwa wapi?, maana sijakuona muda mrefu kidogo",Kayoza alimuuliza Sajenti Minja,
"nilienda pale hotelini kumchunguza huyo bwana mkubwa",Sajenti Minja aliongea huku akikaa chini,
"umefanikiwa?",Kayoza akauliza kwa ufupi,
"nilifika pale hotelini, ila yeye alikuwa ndani na mlango alikuwa ameufunga kwa ndani",Sajenti Minja alimjibu Kayoza,
"kumbe ulitaka kuingia mpaka ndani!?",Kayoza akauliza kwa mshtuko,
"ndio",Sajenti Minja akajibu kwa kifupi,
"sasa ungefanikiwa kuingia ndani ungemfanya nini?",Kayoza alimuuliza Sajenti Minja,
"unaona hii chupa, ndio ingekuja kutoa ushaidi wa chochote ambacho ningemfanyia",Sajenti Minja alijibu huku akimuonyesha Kayoza chupa ya soda,
"na afadhali hukufanikiwa",Kayoza akaongea huku akikwepesha macho yake yasigongane na Sajenti Minja,
"alah!, kwanini!?"Sajenti Minja akahoji,
"nilishakuambia kuwa yule nitamuua kwa mikono yangu mwenyewe",Kayoza alijibu akiwa anaelekea ndani,
"mh, hii kasheshe",Sajenti Minja alijisemea peke yake.

Jioni ya siku hiyo, pale kwa bibi yake Kayoza kulikuwa na shughuli ya kutoa ng'ombe ambao ni wagonjwa, ili kesho alfajili wapelekwe mnadani, hiyo kazi ilifanywa na vijana wa pale, wakiwemo Kayoza na Sajenti Minja.

Mkuu wa Polisi baada ya kuzinduka, akaenda kuoga kisha akaenda kuagiza chakula, baada ya kula akaingia chumbani kwake, kisha akaibeba bastola yake na kuelekea walipofikia wakina Sajenti Minja, giza lilikuwa limeshachukuwa nafasi yake,
"afadhali wako nje",Mkuu wa Polisi alisema, baada ya kuona watu ndani ya zizi la ng'ombe.
Akaenda sehemu ambayo imejificha na pia karibu na zizi waliokuwemo wakina Kayoza, akatoa bastola yake na kumuweka Sajenti Minja katika shabaha yake, aliweza kumtambua kutokana na taa ya chemri ambayo Sajenti Minja alikuwa kainyanyua juu usawa wa kichwa chake kwa ajili ya kuwamulikia wenzake.
Mkuu wa Polisi akaikamata vizuri bastola yake,
"ukalale mahali pabaya motoni Minja, usaliti ndio umekuponza, moja..mbili...tatu",Mkuu wa Polisi aliongea kwa sauti ndogo, kisha akahesabu na kufyatua risasi kumuelekea Sajenti Minja

********ITAENDELEA*********

the Legend☆
 
KIJIJINI KWA BIBI--56
...ukafuata mlio mkali ulioambatana na risasi, kisha kwa macho yake, Mkuu wa Polisi akashuhudia giza limetanda ndani ya zizi la ng'ombe alilokuwamo Sajenti Minja, huku kukifatiwa na kelele za watu, na wengi wao walikuwa wakionekana wanakimbia huku wakitoka ndani ya zizi la ng'ombe na tena wakiomba msaada.

Kuona hivyo, Mkuu wa Polisi akaondoka katika lile eneo taratibu bila kuonekana na mtu, hata kama ungekutana nae njiani usingedhani kuwa ule mlio wa bastola uliosikika muda muchache uliopita ni yeye ndiye aliyefyatua, kwa maana nae alikuwa anakimbia hivyo kama watu wengine wa eneo lile walioshtuliwa na mlio wa risasi.

Alijitahidi kukimbia kwa dakika mbili kisha akaanza kutembea mwendo wa kawaida, ni baada ya kuiacha kwa mbali nyumba aliyoifanyia tukio muda mchache uliopita.

"asante Mungu, sasa nimebakiza kazi ndogo tu, kumuua yule anaejifanya shetani",Mkuu wa Polisi aliongea huku akiwasha sigara yake na kuvuta funda moja kisha apuliza taratibu na kuuangalia moshi uliokuwa unaelekea juu,

"Kama sinema vile au hadithi ya kisasi kwa jinsi ninavyofanya matukio yangu, au kama Rambo anavyowamaliza wavietnam" Mkuu wa polisi aliongea peke yake na kisha akatoa tabasamu moja haya sana.

Alikuwa kama hajitambui ni mtu wa aina gani? mtu anayeua na kufurahi hii inaonesha sio mzika, ila yeye hakujali wala hakufikiria hilo, baada ya kufanya tukio hilo la kinyama, alichokuwa akikiwaza muda huu ni pombe tu, tena alizidisha hatua zake za kutembea ili awahi kufika hotelini akanywe pombe, koo lilikuwa limemkauka.

**************

Baada ya Mkuu wa Polisi kufyatua risasi, ile risasi ilichomoka moja kwa moja na kulenga taa ambayo ilikuwa imeshikiliwa na Sajenti Minja usawa wa uso wake, risasi ikapasua kioo cha chemri na kusababisha baadhi ya vipande vya chupa kuingia kwenye macho ya Sajenti Minja hali ambayo ilisababisha maumivu makubwa sana machoni kwa Sajenti Minja, ila hakutaka kupiga kelele kwa kuhofia adui akimsikia amepiga kelele anaweza kusogea na kummalizia kabisa.

Sajenti Minja aliamua kutulia chini kimya kama amekufa huku maumivu akiyavumilia.

Baada ya muda mchache eneo lile lililokuwa na vurugu zilizotokana na mlio wa risasi lilitulia, ndipo wajomba zake Kayoza walipokuja sehemu aliyolala Sajenti Minja.

"Mjomba upo salama?" Kayoza alimuuliza baada ya kumuona akijigeuza,

"Nahisi nipo salama, ila macho yanauma sana, sijui kama yamesalimika" Sajenti Minja aliongea huku mikono yake ikiwa imeziba macho yake,

"Ebu toa mikono nikuangalie" Kayoza alimwambia mjomba wake,

"Hapana, bora nikishika hivi nasikia nafuu kidogo. Nipelekeni hospitali" Sajenti Minja aliongea,

Wakina Kayoza wakambeba Sajenti Minja ambae alikuwa anaugulia maumivu na kumkimbiza ndani,

"mjomba uko salama?",Kayoza alirudia tena kumuuliza Sajenti Minja,

"macho, macho yangu jamani, naomba mniwaishe hospitali",Sajenti Minja alijibu katika sauti iliyoashiria anataka kulia,

Bila kupoteza muda, wanaume wawili wakambeba juu juu na kumpeleka nje ambapo walienda barabarani na kukodi gari iliyompeleka hospitali.

Walipofika hospitali, wakapokelewa na wauguzi na kupelekwa katika chumba cha Daktari, ambae alimuangalia kwa dakika kumi, na kuwaambia wauguzi wampeleke theatre.

Baada ya Sajenti Minja kuingizwa katika chumba hicho, waliingia madaktari wapatao watano kwa ajili ya kumfanyia upasuaji mdogo wa macho Sajenti Minja,

"Vipi mgonjwa, ilikuwaje kuwaje mpaka ikawa hivyo?" Daktari mmoja alimuuliza Sajenti Minja aliyekuwa amelazwa kitandani,

"Hata sijui, sisi tulikuwa tunatoa mifugo zizini ndio tukasikia mlio wa risasi ghafla na inaelekea ilipiga taa niliyoibeba na vipande vyake vilinirukia machoni" Sajenti Minja alizungumza,

"Mlipitia polisi kuchukua PF3?" Daktari aliuliza,

"Uko ni kupoteza muda, kwa hiyo ningeendelea kupata maumivu kiss PF3?" Sajenti Minja aliuliza,

"Lakini ndio utaratibu huo, bila PF3 hakuna matibabu" Daktari aliendelea kutoa maneno yaliyomchukiza Sajenti Minja,

"Hata mimi ni polisi, kama hamtaki kunitibu niambieni" Sajenti aliongea kwa hasira huku akiingiza mkono mfukoni na kutoa kitambulisho chake,

"Tufanye kazi jamani, tuache malumbano" Daktari mwingine wa kike alizungumza huku akivaa mipira (gloves) mikononi,

"Mwenzako sio muelewa" Sajenti Minja aliongea,

"Mgonjwa nawe mtata sana, haya jiandae nakuchoma nusu kaputi" Daktari wa kike aliongea kisha akamchoma sindano Sajenti Minja na kisha Sajenti Minja akapoteza fahamu, matibabu yakaanza sasa usiku huo huo.

*****************

Mkuu wa Polisi alirudi katika guest aliyofikia, kisha akaoga vizuri, akaagiza konyagi, alafu akajifungia ndani kujipongeza kwa kazi aliyofanya.

Kama kawaida yake alikuwa anakunywa huku akitukana matusi kumuelekea Sajenti Minja, na safari hii kabla hajaweka jina Sajenti Minja, alikuwa anaanza na neno marehemu Sajenti Minja, kwa maana alikuwa anaamini amemuua kwa ile risasi moja aliyomlenga, hakujua kama imemkosa.

Baada ya kunywa pombe nyingi, Mkuu wa polisi alilala pale pale kwenye kochi kama kawaida yake, hii ni siku ya tatu hakijui kitanda.

Siku iliyofuatia, majira ya saa nne za asubuhi, Mkuu wa Polisi aliamua apitie katika maeneo ya karibu na nyumba waliyofikia wakina Kayoza kwa ajili ya kuangalia hali ilivyo, lakini alichotarajia kukiona hakukikuta, alitegemea kukuta msiba pale lakini akakuta hali ya kawaida ila kulikuwa na watu ambao walikuwa wamejitenga mafungu mafungu kuzungumzia tukio la siku iliyopita.

"kuna nini kijana, mbona mko kimafungu mafungu hivyo?",Mkuu wa Polisi alimuuliza kinafiki kijana ambae alikuwa jirani na yeye,

"ina maana hujui kilichotokea, au wewe mgeni hapa?",yule Kijana alihoji badala ya kujibu,

"sasa ningejua ningeuliza?, vijana wa Sikh hizi sijui mkoje?",Mkuu wa Polisi akarudishia swali,

"ni hivi mzee wangu, jana kuna mtu kapigwa risasi hapa ila kwa bahati nzuri hajafa, na wiki kadhaa zilizopita kuna mtu katika nyumba ile ile alipigwa risasi na kufa papo hapo",yule Kijana alimueleza Mkuu wa Polisi,

"umesema aliyepigwa risasi hajafa!?",Mkuu wa Polisi aliuliza kwa mshangao,

"ndio, kwani vipi mzee?",yule Kijana aliushangaa mshangao wa Mkuu wa Polisi,

"Hiyo risasi alipigwa wapi mpaka asife?, maana risasi sio kitu cha mchezo" Mkuu wa polisi alihoji huku akiwa ahamini kama ile risasi aliyopiga imemkosa Sajenti Minja,

"Nasikia haijampata, ila ilipiga taa ambayo alikuwa ameibeba" Kijana alijibu na kumfanya Mkuu wa polisi akunje Sura kwa kusikia kuwa ile risasi ilimkosa Sajenti Minja,

"Huu ujinga huu" Mkuu wa polisi aliongea kwa hasira na kujisahau kama na mtu mwingine,

"Kwani vipi mzee?" Kijana aliuliza huku akishangaa hali aliyokuwa nayo Mkuu wa polisi,

"hakuna kitu kijana, kwa hiyo kapelekwa hospitali?",Mkuu wa Polisi alihoji,

"ndio, kapelekwa hospitali ya mkoa",yule Kijana alijibu.

Mkuu wa Polisi akutaka hata kuaga, akageuka na kurudi guest,

"mh!, yule mbwa ana bahati gani?, hapana, lazima nikammalizie pale pale hospitalini",Mkuu wa Polisi aliongea kimoyo moyo, kisha akachukua bastola yake na safari ya kuelekea hospitali ikaanza.

Alipofika hospitalini, hakujua Sajenti Minja amelazwa wodi namba ngapi, ila baada ya kuuliza uliza kwa madaktari alifanikiwa kufika katika wodi aliyokuwepo Sajenti Minja, akaingia ndani ambapo alimkuta Sajenti Minja peke yake huku katika macho yake kukiwa na bandeji zilizomzuia kuona, alifungwa bandeji kubwa machoni make kutoka na upasuaji mdogo aliofanyiwa.

Mkuu wa Polisi aliingia ndani ya wodi na kisha akaanza kumsogelea taratibu Sajenti Minja, alipomfikia, akaichomoa bastola yake, kisha akawa anajitayarisha kummaliza Sajenti Minja, tena alidhamiria kabisa, hata sura na macho yalionesha hivyo.....

********ITAENDELEA**********

the Legend☆
 
KIJIJINI KWA BIBI 57

...mara mlango wa wodi ukafunguliwa, alikuwa ni Daktari, Daktari alishtuka sana baada ya kumkuta Mkuu wa Polisi kashika bastola, Mkuu wa Polisi aliliona hilo, akawai kutoa kitambulisho,

"alah, kumbe ni polisi, nimekuja kumpa huduma mara moja kwa hiyo nakuomba ukae nje kidogo",Daktari aliongea huku akitabasamu,

Mkuu wa Polisi akatoka nje bila hata kuongea neno huku akishukuru kwa daktari kutokujua kitu chochote na pia alilaani kwa daktari kuingia ghafla kwa maana alimuaribia mpango wake.

"polisi yuko wapi?",Sajenti Minja alihoji baada ya kusikia daktari akiongea na mtu aliyejitambulisha kuwa ni polisi,

"si mlikuwa nae hapa ndani",Daktari akajibu huku akimshangaa Sajenti Minja,

"hapana, hakuna aliengia na kuniambia yeye ni polisi",Sajenti Minja aliongea kwa mkazo huku akimbishia Daktari,

"Unachoongea ni kweli au unatania, kwa hiyo wewe unasema hujamuona!?",Daktari aliuliza kwa mshangao,

"amini nilichokuambia, huyo polisi yukoje, na umejuaje kuwa ni polisi?",Sajenti Minja aliendelea kuhoji,

"umri wake kati ya miaka 45 mpaka 50, alikuwa kashika bastola, aliponiona alinionesha kitambulisho ambacho kinaonesha ni polisi wa shinyanga",Daktari alieleza kwa urefu,

"umesema wa shinyanga!?",Sajenti Minja alihoji kwa mshangao,

"ndio, vipi unamjua?",Daktari aliuliza,

"mhm, hapana",Sajenti Minja alijibu lakini mawazo yake yote akayahamishia kwa Mkuu wa Polisi,

"ina maana amejua niko hospitali na amenifuata na bastola ili animalize?",Sajenti Minja aliongea kwa fikra.

"Au ana mpango gani na mimi? Nani amemwambia nipo hapa? Huyu mzee ni hatari aisee" Sajenti Minja aliendelea kuwaza,

"Mheshimiwa mimi natoka, nilikuja kukubadilishia drip tu" Daktari aliongea na kumfanya Sajenti Minja Stoke mawazoni,

"Jamani kuweni makini na watu wanaoingia humu, sasa kama huyo uliyesema amekuja na bastola hata simjui, angalieni wasije wakanidhuru" Sajenti Minja aliongea kwa kulalamika kwa maana yoga ulimuingia tayari,

"Sasa sisi hatuwezi kuzuia mtu, tunajua wote ni ndugu zako" Daktari alijibu Sajenti Minja,

"Nyie ndugu zangu si mnawajua, kwanza msimruhusu mtu yoyote kuingia humu mpaka awepo yule kijana mwenye nywele nyingi zisizochanwa" Sajenti Minja aliongea huku akimaanisha ni Kayoza,

"Lakini hata wewe si ni polisi?, hata huyu aliyeingia nae ni polisi mwenzako" Daktari alimwambia Sajenti Minja,

"Atakuwa sio polisi, usikute amegushi tu kitambulisho, msimruhusu tena" Sajenti Minja aliongea,

"Inaelekea una maadui wengi sana bosi" Daktari aliongea,

"Fuata nilichokuambia, sitaki maneno mengi" Sajenti Minja aliongea huku zile bandeji zikiwa bado katika macho yake,

"Sawa bosi, lakini kumbuka huwezi kuna alafu unaniletea ubabe" Daktari aliongea kwa utani huku akiondoka,

"Kwa kuwa sioni ndio mumuingize kila mtu humu ndani?" Sajenti Minja aliuliza lakini hakuna aliyemjibu, Daktari alikuwa ameshatoka ndani kitambooo.

Baadae wakina Kayoza walipofika, Sajenti Minja alimsimulia Kayoza kila kitu, Kayoza alishtuka, na kuahidi hatoondoka katika eneo la hospitalini mpaka Sajenti Minja apone.

"Sasa wewe ukikaa hapa muda wote ni Mani ataniletea chakula?" Sajenti Minja alimuuliza Kayoza,

"Sasa unadhani ni nini kifanyike kukulinda kipindi hiki ambacho una bandeji machoni?" Kayoza alimuuliza Sajenti Minja,

"Mi nadhani tumtafute mtu awe analeta chakula, alafu wewe ushinde hapa mpaka usiku alafu unaondoka" Sajenti Minja alimwambia Kayoza,

"Sio kushinda tu, itanibidi nilale kabisa" Kayoza aliongea,.

"Kulala na mgonjwa hawaruhusu" Sajenti Minja alimwambia Kayoza,

"Itabidi waruhusu tu, kwa maana hawajaweka ulinzi wa kutosha" Kayoza aliongea huku hasira zikianza kumtawala,

"Muda mwingine kuvunja sheria za mahali penye uongozi wake, unaweza kujitafutia matatizo, ni bora ufanye kama nilivyokuagiza" Sajenti Minja alimwambia Kayoza ambaye hakutaka kuendelea na mabishano badala yake alikitoa kwenye kikapu chakula walichomletea Sajenti Minja,

"Hicho chakula mbona kinanukia vizuri, inaelekea kitakuwa kitamu sana" Sajenti Minja aliongea baada ya kusikia harufu ya chakula.

"We ongea yote, ila usiku wa leo itanibidi niwe eneo hili" Kayoza aliongea kisha akatoka nje kwenda kununua maji na kumuacha Sajenti Minja akiongea mwenyewe

******************

Mkuu wa Polisi baada ya kushindwa kufanikisha azma yake, alirejea katika Guest aliyofikia na kujipanga upya, baada ya kupita pita katika kichaka cha fikra zake, akaamua kuwa usiku lazima arudi kule hospitalini.

Nae alishajua inawezekana asubuhi ile alishtukiwa baada ya kuondoka, na yeye sasa akaongeza akili za ziada ili usiku aweze kufanikisha lengo lake, na ilimbidi siku hiyo asiguse hata pombe kabisa. Chakula alichokula Sikh hiyo ni matunda tu, ndio alliamini kufanya hivyo kutaifanya akili yake ifanye kazi vizuri.

Baada ya kula alipumzika nusu saa kisha akaenda kuoga, alipotoka kuoga alipanda kitandani na kulala ili kujiandaa na misheni aliliyopo mbele yake. Kumbuka hapo ilikuwa ni saa name mchana.

Aliamka saa mbili usiku na kwenda kuoga tena, kisha akavaa nguo zake za mazoezi na raba nyeusi, kisha akaichukua bastola yake na kuifanyia ukaguzi kidogo na kisha aliipachika kibindoni, alafu akachukua kisu kidogo kiasi na kukitia mfukoni kisha akanywa maji mengi sana na kushusha pumzi ndefu,

"Mwenyezi Mungu naomba unilinde kwa kila hatua ninayopiga" Mkuu wa polisi aliongea na kutoka chumbani kwake na kuelekea nje.

Safari ya hospitali ilikuwa inaanza sasa.

Usiku wa saa tano na dakika zake, mkuu wa Polisi alikuwa katika maeneo ya hospitali, akajipenyeza mpaka mahali ilipo wodi aliyolazwa Sajenti Minja, kipindi hicho chote Kayoza alikuwa anamuona, Kayoza nae akawa anafuata kila hatua iliyokuwa inafanywa na Mkuu wa Polisi.

Mkuu wa polisi alifanikiwa kupenya penya na mpaka kuingia katika wodi aliyolazwa Sajenti Minja.

Mkuu wa Polisi baada ya kuingia katika wodi aliyolazwa Sajenti Minja, aliingia kisha akafunga mlango kwa ndani, akachomoa kisu kilichokuwa katika mfuko wake. Aliamua kutumia kisu kwa maana aliona akitumia bastola inaweza kutoa sauti kubwa na kusababisha watu kujaa eneo lile, kwa hiyo kufanya hivyo ni kujiweka hatarini.

Kwa hiyo maamuzi aliyofikia ni kutumia kisu tu ili kutimiza dhamira yake.

"Nani wewe?" Sajenti Minja aliuliza baada ya kusikia vishindo vya mtu vikimsogelea,

"Mimi ni mtu mbaya" Mkuu wa polisi alijibu kwa sauti kavu iliyojaa utulivu,

"Usiku huu unataka nini kwangu?"Sajenti Minja aliuliza huku akijitahidi kupapasa engo za kitanda,

"Minja nimekuja kukuua, nimekuja kukuua Minja",Mkuu wa Polisi aliongea kwa hasira, wakati Sajenti Minja anataka kunyanyuka ili ajiokoe ilihali haoni, Mkuu wa Polisi alikishusha kishu katika jicho la kushoto la Sajenti Minja, na kujikuta Sajenti Minja akipiga kelele ambazo ziliwashtua wagonjwa wa wodi za jirani ambao wenye ahueni walienda katika mlango wa wodi ambako walimkuta Kayoza anaangaika kufungua, huku akilia kwa maana alihisi tayari mjomba wake yupo katika hatua za kupigania uhai wake kutokana na kelele alizozitoa.

Wakashirikiana na kufanikisha kuuvunja mlangp, walipofika ndani kila mtu mwenye moyo mwepesi aliishia kulia au kuzimia, Sajenti Minja alikuwa amelala kitandani huku akiwa amejaa damu mwili wote, na kisu kikubwa kiasi kikiwa kimeshindiliwa katika jicho lake la kushoto, ila ndani hawakumkuta mtu mwingine zaidi ya Sajenti Minja peke yake na hakukuwa na dalili ya dirisha kuvunjwa wala njia nyingine iliyoonesha kuna mtu alitumia kutokea mule ndani.

Watu wakawa wanashangaa lile tukio, wengine walidai ni mambo ya kishikirina, wengine wakasema alitaka kujiua, ila Kayoza yeye aliamini mule ndani kuna mtu, kwa hiyo akawa anaangaika kuangaza angaza kila mahali huku akiendelea na kilio kilichoambatana na chuki zilizojaa hasira.

**********************

Mkuu wa Polisi baada ya kumchoma visu visivyo na idadi Sajenti Minja, alisikia watu wakijaa mlangoni, alichoamua ni kupanda juu na kuingia kwenye singboard, lengo lake lilikuwa ni kutembea juu mpaka katika eneo ambalo atakuwa salama, ili atoke.

Alitembea juu ya Dari mpaka alipofika usawa wa choo, akashuka na kuanza kuelekea nje, alitoka salama kabisa na alifanikiwa kwenda katika guest aliyofikia salama salmini, akiwa na imani kuwa kazi yake imekamilika, na sasa anadili na Kayoza pekee.

Alipofika chumbani kwake aliingia bafuni na kunawa mikono, kisha akarudi ndani na kujitupa juu ya kochi, akajijiminia konyagi katika glass yake na kuigida yote kwa fujo...

*********ITAENDELEA***********

the Legend☆
 
KIJIJINI KWA BIBI--58

Mkuu wa polisi akainuka katika kiti na kuelekea tena bafuni, akaoga na kutoka kisha akavaa suruali ya kitambaa na shati, kichwani akavaa kofia ya uviringo maarufu kama parma au watu was miaka ya themanini na tisini uwa wanaziita Marlboro kutokana na nembo moja maarufu ya sigara ambayo ilikuwa na picha ya mtu akiwa juu ya farasi huku akiwa amevaa kofia ya namna hiyo, pia baadae hiyo picha iliweza kuweka kwenye picha za mifuko ya Tanzania na hiyo mifuko ikapewa jina hilo, yaani mifuko ya Marlboro.

Mkuu wa polisi akatoka na kuelekea mitaa ya nyumba ya bibi yake Kayoza ili aone kama atakutana na habari za msiba wa Sajenti Minja.

Aliweza kufika kwenye mtaa huo ila hakubahatika kusikia habari yoyote, ikaendelea kuzunguka zunguka pale bila mafanikio yoyote na mwisho akaamua arudi zake katika ile nyumba ya wageni huku akiamini kuwa tayari Sajenti Minja ameshakufa, aliamua kuamini hivyo tu ingawa hakusikia habari yoyote, aliamua tu kuamini kutokana na ule unyama alioutenda kule hospitali.

Aliingia ndani ya chumba chake na kuvua shati lake na kofia, kisha akajitupa kitandani na kuwasha runinga na kuangalia vipindi vilivyokuwa vinaoneshwa kipindi hicho.

*******************

Ndani hospitali kulikuwa na patashika, madaktari walimuweka Sajenti Minja katika kitanda cha magurudumu na kuanza kusukuma kile kitanda kitanda mpaka chumba cha upasuaji, walipofika ndani ya chumba kile, walimuondoa nguo zote mwilini na kuanza kumfuta damu iloyokuwa imemtapakaa mwili mzima, walipomaliza kumfuta damu walikuta mwili wake una majeraha matatu tu, walikuta amechomwa kisu mbavuni, kifuani na katika jicho lake la kushoto.

Walichofanya ni kuangalia kama hivo visu alivyochomwa kama vina madhara makubwa, mwisho waligundua kisu cha mbavuni na kifuani havina madhara sana, walichofanya ni kusafisha vidonda hivyo na kuvipaka dawa kisha wakavifunga na bandeji laini, ila tatizo kubwa lilikuwa katika kisu alichochokwa katika jicho lake la kushoto, ilionekana ndio kina madhara makubwa sana.

"Ni nani mwenye ujasiri huu was kuingia hapa na kufanya unyama wa namna hii?" Daktari mmoja aliuliza,

"Hapa kwetu usalama hakuna, huo ndio ukweli, na kama hii habari itafika ngazi za juu, basi tutakuwa mashakani" Daktari mwingine alijibu,

"Ila mtu aliyefanya hivi inaelekea ana kiasi na huyu bwana, haiwezekani atoke uko na kuja moja kwa moja katika wodi aliyolazwa huyu bwana" Daktari mwingine alijibu,

"Hilo sio jukumu letu, tunachotakiwa ni kumtibu tu mgonjwa, hayo mengine ni ya walinzi" Daktari wa tatu aliongea,

"sasa itakuaje?", Daktari mmoja aliuliza huku akitegemea jibu kutoka kwa wenzake, lakini ilikua tofauti, kwa sababu hakuna hata mmoja alienyanyua mdomo wake kujibu,

"ina maana hamjanisikia au?", yule Daktari aliuliza tena baada ya kuona kimya,

"hapo mkuu hamna jinsi, itabidi aondolewe tu!",Daktari mmoja aliyevaa suruali ya jeans alijibu hivyo,

"kwa hiyo inabidi afanyiwe uperation, si ndio?", yule Daktari ambae ndio alionekana mkuu aliuliza tena.

"Hamna jinsi, itabidi iwe hivyo" Daktari mwingine aliongezea,

Na makubaliano waliyofikia ilikua ni kumuondoa Sajenti Minja jicho lake.

Na ndipo jicho lake la kushoto likaondolewa, na kupata kilema cha milele kilichotokana na shambulio lililofanywa na mkuu wa polisi.

Kipindi chote, Kayoza alikuwa amekaa nje ya wodi huku machozi yakimtoka, mara ghafla Kayoza akashuhudia mlango wa wodi ukifunguliwa na wakatoka wauguzi wawili ambao walikuwa wanakisuma kitanda chenye magurudumu manne, huku wakifuatiwa na Madaktari wawili, Kayoza nae akaamka, kisha akaongozana nao mpaka katika mlango wa chumba cha wagonjwa mahututi, Madaktari wakaingia ndani, Kayoza alibaki nje, muda wote Kayoza alikua hatulii, mara akanyanyuka kwenda katika mlango wodi aliyolazwa Sajenti Minja, akawa anatafuta upenyo ili aweze kuona kinachoendelea ndani, lakini bado hakufanikiwa, mwisho akaamua kusimama tu! kama mtu aliyekosa matumaini.

Baada ya dakika kadhaa za kusubiri pale nje, Daktari mmoja akatoka ndani huku akiwa anaelekea maeneo zilipo ofisi za hospitali, ila alipofika usawa wa viti vya watu wanavyokaa watu wanaosubili wagonjwa wapo, Kayoza akasimama na kumkimbilia daktari,

"Samahani Daktari, mgonjwa wangu ana hali gani?" Kayoza aliuliza huku akimuangalia Daktari aliyekuwa anatembea,

"Mgonjwa wako yupi?" Daktari aliuliza huku akiendelea kutembea,

"Yule aliyevamiwa na kuchomwa visu" Kayoza alijibu,

"Ooooh. kijana, mgonjwa ni ndugu yako?",Daktari alimuuliza Kayoza,

"ndio dokta",Kayoza alijibu,

"mbona uko peke yako, hakuna watu wakubwa ulioongozana nao?",Daktari akauliza swali lingine,

"hakuna, kwani vipi?",Kayoza akauliza huku akiwa na wasiwasi,

"ok, nifuate ofisini",Daktari aliongea huku akiwa anaondoka.

Kayoza akaongozana na Daktari mpaka katika ofisi ya huyo Daktari, akakaribishwa kiti, akakaa,

"bila kupoteza muda kijana, hali ya ndugu yako umeiona na hakuna jinsi zaidi ya kuondolewa jicho, kwa hiyo tunasubiri azinduke, maana amepoteza fahamu, fahamu zikimrudia itambidi asaini kitabu cha upasuaji ili tumuondoe lile jicho",Daktari alikuwa anampa maelezo Kayoza,

"hakuna shida Dokta",Kayoza alijibu,

"sio unasema hakuna shida tu, je pesa ipo?",Daktari alimuuliza Kayoza,

"kwani inahitajika shilingi ngapi?",Kayoza akauliza,

"laki tatu",Daktari akajibu,


"hakuna tatizo, pesa ipo",Kayoza alimwambia Daktari.

"Wewe unafanya kazi?" Daktari akamtupia swali lingine Kayoza,

"Hapana, mimi ni mwanafunzi" Kayoza alijibu,

"Sasa pesa utazitoa wapi?" Daktari aliuliza,

"pesa ipo kaka" Kayoza alijibu kwa kifupi,

"Basi wewe nenda kalete hela" Daktari alimwambia Kayoza,

"Je naweza kumuona mgonjwa wangu?" Kayoza aliuliza,

"Hapana, utamuona akishafanyiwa upasuaji?" Daktari alijibu,

"Sawa" Kayoza alijibu kwa unyonge.

Kisha Kayoza akatoka katika ofisi ya Daktari, na kuelekea nyumbani, njia nzima alikuwa anawaza mtiririko wa matukio yanayomtokea, ila kwa sasa aliamini adui yake mkubwa ni Mkuu wa Polisi.

Kayoza akaondoka na kwenda katika bar iliyo jirani na pale hospitali, akanywa soda, kisha akaondoka huku akiwa na mawazo mengi sana,


"lazima nimuue yule mzee, ameniharibia tumaini langu la kupona na sijui hatma yangu ya maisha mpaka sasa, Mjomba minja anakuwa mlemavu kwa sababu yangu mimi, Omari rafiki yangu kipenzi nisamehe, umenisaidia sana ila mwisho umekuwa maiti kwa sababu yangu mimi, Denis nilikupenda sana jamaa yangu, ila...",Kayoza akashindwa kuendelea machozi yakawa yanamtoka, akasimama pembeni ya barabara huku machozi yakimtoka.

Akashindwa hadi kutembea, akakodi taxi ya kumfikisha nyumbani.

Kayoza alipofika nyumbani, aliwaambia waanze kutayarisha chakula cha mgonjwa, kisha Kayoza akaenda kuoga, alipotoka akaenda kuvaa, kisha akala chakula, alafu akachukua chakula cha mgonjwa na safari ya kuelekea hospitali ikaanza ingawa hakuwa na uhakika kama Sajenti Minja ataweza kula ila ilibidi abebe tu hivyo hivyo.

alipokuwa anatoka nje, ndipo macho yake yalimshuhudia mtu ambae alikuwa anaelekea katika nyumba aliyokuwepo yeye.

Kayoza machozi yakaanza kumtiririka katika mashavu yake, sababu ya uchungu wa yaliyomtokea, aliamua kulia kwa sauti kubwa huku akimuangalia yule mtu anaekuja, mwisho akaamua kuweka chakula chini na kukimbia kumuelekea yule mtu, yule mtu nae alikua anakimbia kumuelekea Kayoza....

*****ITAENDELEA******

the Legend☆
 
Back
Top Bottom