KIJIJINI KWA BIBI--58
Mkuu wa polisi akainuka katika kiti na kuelekea tena bafuni, akaoga na kutoka kisha akavaa suruali ya kitambaa na shati, kichwani akavaa kofia ya uviringo maarufu kama parma au watu was miaka ya themanini na tisini uwa wanaziita Marlboro kutokana na nembo moja maarufu ya sigara ambayo ilikuwa na picha ya mtu akiwa juu ya farasi huku akiwa amevaa kofia ya namna hiyo, pia baadae hiyo picha iliweza kuweka kwenye picha za mifuko ya Tanzania na hiyo mifuko ikapewa jina hilo, yaani mifuko ya Marlboro.
Mkuu wa polisi akatoka na kuelekea mitaa ya nyumba ya bibi yake Kayoza ili aone kama atakutana na habari za msiba wa Sajenti Minja.
Aliweza kufika kwenye mtaa huo ila hakubahatika kusikia habari yoyote, ikaendelea kuzunguka zunguka pale bila mafanikio yoyote na mwisho akaamua arudi zake katika ile nyumba ya wageni huku akiamini kuwa tayari Sajenti Minja ameshakufa, aliamua kuamini hivyo tu ingawa hakusikia habari yoyote, aliamua tu kuamini kutokana na ule unyama alioutenda kule hospitali.
Aliingia ndani ya chumba chake na kuvua shati lake na kofia, kisha akajitupa kitandani na kuwasha runinga na kuangalia vipindi vilivyokuwa vinaoneshwa kipindi hicho.
*******************
Ndani hospitali kulikuwa na patashika, madaktari walimuweka Sajenti Minja katika kitanda cha magurudumu na kuanza kusukuma kile kitanda kitanda mpaka chumba cha upasuaji, walipofika ndani ya chumba kile, walimuondoa nguo zote mwilini na kuanza kumfuta damu iloyokuwa imemtapakaa mwili mzima, walipomaliza kumfuta damu walikuta mwili wake una majeraha matatu tu, walikuta amechomwa kisu mbavuni, kifuani na katika jicho lake la kushoto.
Walichofanya ni kuangalia kama hivo visu alivyochomwa kama vina madhara makubwa, mwisho waligundua kisu cha mbavuni na kifuani havina madhara sana, walichofanya ni kusafisha vidonda hivyo na kuvipaka dawa kisha wakavifunga na bandeji laini, ila tatizo kubwa lilikuwa katika kisu alichochokwa katika jicho lake la kushoto, ilionekana ndio kina madhara makubwa sana.
"Ni nani mwenye ujasiri huu was kuingia hapa na kufanya unyama wa namna hii?" Daktari mmoja aliuliza,
"Hapa kwetu usalama hakuna, huo ndio ukweli, na kama hii habari itafika ngazi za juu, basi tutakuwa mashakani" Daktari mwingine alijibu,
"Ila mtu aliyefanya hivi inaelekea ana kiasi na huyu bwana, haiwezekani atoke uko na kuja moja kwa moja katika wodi aliyolazwa huyu bwana" Daktari mwingine alijibu,
"Hilo sio jukumu letu, tunachotakiwa ni kumtibu tu mgonjwa, hayo mengine ni ya walinzi" Daktari wa tatu aliongea,
"sasa itakuaje?", Daktari mmoja aliuliza huku akitegemea jibu kutoka kwa wenzake, lakini ilikua tofauti, kwa sababu hakuna hata mmoja alienyanyua mdomo wake kujibu,
"ina maana hamjanisikia au?", yule Daktari aliuliza tena baada ya kuona kimya,
"hapo mkuu hamna jinsi, itabidi aondolewe tu!",Daktari mmoja aliyevaa suruali ya jeans alijibu hivyo,
"kwa hiyo inabidi afanyiwe uperation, si ndio?", yule Daktari ambae ndio alionekana mkuu aliuliza tena.
"Hamna jinsi, itabidi iwe hivyo" Daktari mwingine aliongezea,
Na makubaliano waliyofikia ilikua ni kumuondoa Sajenti Minja jicho lake.
Na ndipo jicho lake la kushoto likaondolewa, na kupata kilema cha milele kilichotokana na shambulio lililofanywa na mkuu wa polisi.
Kipindi chote, Kayoza alikuwa amekaa nje ya wodi huku machozi yakimtoka, mara ghafla Kayoza akashuhudia mlango wa wodi ukifunguliwa na wakatoka wauguzi wawili ambao walikuwa wanakisuma kitanda chenye magurudumu manne, huku wakifuatiwa na Madaktari wawili, Kayoza nae akaamka, kisha akaongozana nao mpaka katika mlango wa chumba cha wagonjwa mahututi, Madaktari wakaingia ndani, Kayoza alibaki nje, muda wote Kayoza alikua hatulii, mara akanyanyuka kwenda katika mlango wodi aliyolazwa Sajenti Minja, akawa anatafuta upenyo ili aweze kuona kinachoendelea ndani, lakini bado hakufanikiwa, mwisho akaamua kusimama tu! kama mtu aliyekosa matumaini.
Baada ya dakika kadhaa za kusubiri pale nje, Daktari mmoja akatoka ndani huku akiwa anaelekea maeneo zilipo ofisi za hospitali, ila alipofika usawa wa viti vya watu wanavyokaa watu wanaosubili wagonjwa wapo, Kayoza akasimama na kumkimbilia daktari,
"Samahani Daktari, mgonjwa wangu ana hali gani?" Kayoza aliuliza huku akimuangalia Daktari aliyekuwa anatembea,
"Mgonjwa wako yupi?" Daktari aliuliza huku akiendelea kutembea,
"Yule aliyevamiwa na kuchomwa visu" Kayoza alijibu,
"Ooooh. kijana, mgonjwa ni ndugu yako?",Daktari alimuuliza Kayoza,
"ndio dokta",Kayoza alijibu,
"mbona uko peke yako, hakuna watu wakubwa ulioongozana nao?",Daktari akauliza swali lingine,
"hakuna, kwani vipi?",Kayoza akauliza huku akiwa na wasiwasi,
"ok, nifuate ofisini",Daktari aliongea huku akiwa anaondoka.
Kayoza akaongozana na Daktari mpaka katika ofisi ya huyo Daktari, akakaribishwa kiti, akakaa,
"bila kupoteza muda kijana, hali ya ndugu yako umeiona na hakuna jinsi zaidi ya kuondolewa jicho, kwa hiyo tunasubiri azinduke, maana amepoteza fahamu, fahamu zikimrudia itambidi asaini kitabu cha upasuaji ili tumuondoe lile jicho",Daktari alikuwa anampa maelezo Kayoza,
"hakuna shida Dokta",Kayoza alijibu,
"sio unasema hakuna shida tu, je pesa ipo?",Daktari alimuuliza Kayoza,
"kwani inahitajika shilingi ngapi?",Kayoza akauliza,
"laki tatu",Daktari akajibu,
"hakuna tatizo, pesa ipo",Kayoza alimwambia Daktari.
"Wewe unafanya kazi?" Daktari akamtupia swali lingine Kayoza,
"Hapana, mimi ni mwanafunzi" Kayoza alijibu,
"Sasa pesa utazitoa wapi?" Daktari aliuliza,
"pesa ipo kaka" Kayoza alijibu kwa kifupi,
"Basi wewe nenda kalete hela" Daktari alimwambia Kayoza,
"Je naweza kumuona mgonjwa wangu?" Kayoza aliuliza,
"Hapana, utamuona akishafanyiwa upasuaji?" Daktari alijibu,
"Sawa" Kayoza alijibu kwa unyonge.
Kisha Kayoza akatoka katika ofisi ya Daktari, na kuelekea nyumbani, njia nzima alikuwa anawaza mtiririko wa matukio yanayomtokea, ila kwa sasa aliamini adui yake mkubwa ni Mkuu wa Polisi.
Kayoza akaondoka na kwenda katika bar iliyo jirani na pale hospitali, akanywa soda, kisha akaondoka huku akiwa na mawazo mengi sana,
"lazima nimuue yule mzee, ameniharibia tumaini langu la kupona na sijui hatma yangu ya maisha mpaka sasa, Mjomba minja anakuwa mlemavu kwa sababu yangu mimi, Omari rafiki yangu kipenzi nisamehe, umenisaidia sana ila mwisho umekuwa maiti kwa sababu yangu mimi, Denis nilikupenda sana jamaa yangu, ila...",Kayoza akashindwa kuendelea machozi yakawa yanamtoka, akasimama pembeni ya barabara huku machozi yakimtoka.
Akashindwa hadi kutembea, akakodi taxi ya kumfikisha nyumbani.
Kayoza alipofika nyumbani, aliwaambia waanze kutayarisha chakula cha mgonjwa, kisha Kayoza akaenda kuoga, alipotoka akaenda kuvaa, kisha akala chakula, alafu akachukua chakula cha mgonjwa na safari ya kuelekea hospitali ikaanza ingawa hakuwa na uhakika kama Sajenti Minja ataweza kula ila ilibidi abebe tu hivyo hivyo.
alipokuwa anatoka nje, ndipo macho yake yalimshuhudia mtu ambae alikuwa anaelekea katika nyumba aliyokuwepo yeye.
Kayoza machozi yakaanza kumtiririka katika mashavu yake, sababu ya uchungu wa yaliyomtokea, aliamua kulia kwa sauti kubwa huku akimuangalia yule mtu anaekuja, mwisho akaamua kuweka chakula chini na kukimbia kumuelekea yule mtu, yule mtu nae alikua anakimbia kumuelekea Kayoza....
*****ITAENDELEA******
the Legend☆