SASA NILIKUWA NA HAKIKA KUWA yule mtu aliyekufa kwa kuanguka
kutoka juu ya lile jengo la ghorofa la shirika la nyumba la taifa kule mtaa wa
Nkurumah,kuwa kifo chake kilikuwa na mahusiano ya namna fulani na yule
msichana niliyekuwa nikimfuatilia usiku wa jana kutoka kule Vampire Casino. Ingawaje
hadi hapa nilipofikia tukio lile bado lilikuwa halina uhusiano wowote wa kile
nilichokuwa nikiendelea kukichunguza.
Niliendelea kuwaza wakati nilipokuwa nikiegesha gari langu kwenye viunga
vya maegesho ya magari vya Vampire Casino baada ya kutoka kwenye ile nyumba
alipoingia yule msichana usiku wa jana kule mtaa wa Nkurumah na kumkosa. Nilikuwa
nimepitisha msako wa kina kwenye ile nyumba na hatimaye kuja na hitimisho moja
kuwa ile myumba ilikuwa ikikaliwa na mwanaume askari wa jeshi la wananchi wa
Tanzania baada ya kuiona picha yake uliyovunjika mle ndani ya ile nyumba sebuleni
sakafuni na sare za jeshi zilizokuwa kabatini chumbani kwake. Bado sikuweza
kumtambua yule msichana kuwa alikuwa nani hata hivyo niliampa kumfuatilia.
Niliegesha gari langu na nilipoitazama saa yangu ya mkononi nikagundua
kuwa dakika chache zilikuwa zimetoweka tangu ilipotimia saa nne asubuhi. Magari
yaliyoegeshwa mbele ya Vampire Casino hayakuwa mengi na miongoni mwa magari
hayo zilikuwepo teksi za abiria.
Kabla ya kushuka kwenye gari niliyatembeza macho yangu tena nikitathmini hali
ya mandhari yale kisha nikafungua mlango na kushuka nikielekea sehemu ya mlango
wa mbele wa casino ile kulipokuwa na ofisi ya mapokezi na huduma kwa mteja.
Kwa namna nyingine nilifurahi sana kwa kutowaona wale mabaunsa wa mlangoni
waliyonichachafya usiku wa jana wakati nilipokuwa nikitaka kuingia ndani ya casino
ile na badala yake msichana mzuri na mrembo akanipokea kwa bashasha zote huku
akiniweka kwenye kundi la Status conscious customer kutokana na mwonekano wangu nadhifu wenye sura ya kirafiki.
‘Kumbe wasichana warembo bado wapo duniani’ nilijisemea moyoni wakati nikilifikia lile
dawati la mapokezi mbele yangu lililomwifadhi msichana mlimbwende mwenye kila
kionjo cha uzuri.
“Karibu kaka” dada yule alinikaribisha kwa bashasha zote.
“Ahsante sana pole na kazi” nilimwambia huku nikiumba tabasamu la kirafiki
usoni mwangu.
“Nishapoa” dada yule aliongea kwa sauti tamu ya kumtoa nyoka pangoni huku
tabasamu lake usoni likikataa kwenda likizo.
“Tafadhali! naomba nikusikilize” hatimaye yule dada alivunja ukimya baada ya
kuniona nikiendelea kumkodolea macho ya mshangao uliotokana na uzuri wake.
Kabla ya kumjibu yule dada nikageuka nyuma kutazama kule kwenye maegesho
ya magari ya ile casino baada ya kuona gari dogo aina ya Nissan March likiingia eneo lile
na kutafuta maegesho. Kitendo cha kuwaona mwanamke na mwanaume wakishuka
kwenye gari lile kikanifanya niyarudishe macho yangu kumtazama tena yule dada
mbele yangu.
“Nahitaji kuwa mwanachama wa casino” nilimwambia yule dada kwa utulivu huku
tukitazamana.
“Oh! karibu sana na ondoa shaka kaka” yule dada aliniambia huku akivuta
mtoto wa meza yake na kuchukua karatasi fulani na kuziweka juu ya ile meza mbele
yangu. Niliposogea karibu na kuzitazama vizuri karatasi zile nikagundua kuwa
zilikuwa ni fomu kwa ajili ya usajili wa uanachama wa casino ile. Fomu zile zilikuwa
na vitu kama;nembo kubwa ya ile casino,anwani zake zote kama namba za simu za
uongozi,namba za nukushi,tovuti na barua pepe. Chini ya fomu zile kulikuwa na
sehemu za kujaza taarifa ya mtu anayeomba uanachama.
“Jaza taarifa zako humo ndani” yule dada akaniambia huku akinipa kalamu ya
wino.
“Naomba unijazie wewe mimi sijui kusoma wala kuandika” nilimwambia yule
dada nikichombeza utani huku nikimrudishia zile fomu. Tukio lile likampelekea
yule dada anitazame kwa mshangao hata hivyo macho yetu yalipokutana kila mmoja
akajikuta akitabasamu.
Yule dada akaipokea ile fomu na muda mfupi uliyofuata akaanza kuniuliza taarifa
zangu na kila nilipomjibu akawa akinijazia taarifa zile za uongo kwenye ile fomu.
Baada ya muda mfupi tukawa tumemaliza zoezi lile.
“Bado ada ya mwanachama” yule dada akaniambia huku akimalizia kujaza taarifa
zangu kwenye ile fomu.
‘‘Ada ni pesa kiasi gani?” nilimuuliza yule dada na aliponiambia nikatumbukiza
mkono mfukoni kuchukua wallet yangu kisha nikachukua kiasi cha pesa nilizopaswa
kulipa kutoka kwenye wallet ile na kumkabidhi yule dada.
Taratibu za ule usajili zilipokamilika nikakabidhiwa kadi ndogo ya utambulisho
wangu ambayo ningekuwa nikiitumia kuingia kwenye casino. Niliipokea kadi ile na kuitia mfukoni huku nikifurahi kufanikiwa kwa zoezi lile ndani ya muda mfupi.
Hatimaye nikaagana na yule dada na kuelekea sehemu nilipoegesha gari langu
kwenye yale maegesho ya ile casino.
Muda mfupi baadaye niliyaacha maegesho yale na kurudi ofisini kwangu ambapo
asubuhi ile nilikuwa nimemwacha Mwasu akiendelea kuandaa ripoti ya upelelezi wa
mkasa wa MIFUPA 206.
_____
KITENDO CHA KUEGESHA GARI LANGU chakavu aina ya Peugeot 504 toleo
la zamani katikati ya magari mawili ya kifahari na kisasa katika viunga vya maegesho
ya magari vya Vampire Casino usiku huu kilinifanya nijihisi mnyonge wa kipato.
Ningeweza kutafuta sehemu nyingine katika maegesho haya ambayo ingeendana na
hadhi ya gari langu lakini kwa wakati huu nilifahamu kuwa hilo lisingewezekana.
Magari mengi yaliyoegeshwa kwenye eneo lile bila shaka yangeweza kwendana na
thamani ya kiinua mgongo cha wakurugenzi wa kampuni kubwa za hapa nchini na
mgeni yeyote kutoka nje ya Tanzania ambaye ingekuwa ndiyo mara yake ya kwanza
kufika eneo lile huwenda angeshangazwa sana na ile kauli ya kuwa Tanzania ni nchi
masikini.
Eneo la maegesho yale lilikuwa mbioni kufulika magari ya kifahari hata hivyo hali
ile haikunitia mshawasha wowote badala yake nikautia mche wa sigara mdomoni na
kuiwasha huku nikiendelea kutathmini hali ya mandhari yake.
Niligeuka na kuitazama saa ndogo ya gari iliyokuwa kwenye dashibodi na saa ile
ilionesha kuwa dakika chache zilikuwa zimetokomea baada ya kutimia saa mbili usiku.
Nikajishauri kuwa nishuke na kuelekea ndani ya casino ile au niendelee kukaa mle
ndani ya gari huku nikilisubiri lile gari refu na jeusi aina ya Texas Longhorn Tailgate Van
lililombeba yule mlimbwende wa jana liwasili eneo lile.
Hata hivyo baada ya kufikiri kwa kitambo lile wazo la kulisubiri lile gari refu na
jeusi aina ya Texas Longhorn Tailgate Van lifike eneo lile hatimaye nikaliweka kando
kwani sikutaka kutengeneza aina yoyote ya kivutio eneo lile.
Hatimaye nikaichukua bastola yangu na kuichimbia kwenye maficho mazuri mle
ndani ya gari kisha nikafungua mlango na kushuka. Kupitia kitabu kidogo chenye
maelekezo ya taratibu zinazopaswa kuzingatiwa na mwanachama wa casino ile
ambacho nilikuwa nimepewa na yule dada aliyenisajili kuwa mwanachama wa casino ile
asubuhi iliyopita. Nilikuwa nimekumbuka kuwa kuingia na silaha mle ndani ya casino
lilikuwa ni jambo lililokatazwa kwa herufi kubwa. Hivyo sikutaka kujiingiza matatani
kwa kuikiuka sheria ile na ndiyo kisa nikaamua kuiacha bastola yangu mle ndani ya
gari.
Nililisubiri gari moja lililokuwa likija ule upande wangu linipite kisha nikavuka
eneo lile na kuanza kutembea taratibu nikielekea kwenye ule mlango wa mbele wa
casino.
Nilifika eneo la mbele la casino ile na kuanza kupanda ngazi zilizokuwa eneo lile na mara tu nilipomaliza kuzipanda ngazi zile njemba mbili matata,mabaunsa wa
mlangoni pale zikajitokeza kunikabili. Niliwatazama mabaunsa wale waliokuwa tayari
kukabiliana na aina yoyote ya ukorofi wangu na hapo nikafurahishwa na utendaji
wao. Hivyo pasipo kupoteza muda nikazama mfukoni kuichukua ile kadi yangu ya
utambulisho wa mwanachama wa casino ile na kuwaonesha. Zile njemba kuona vile
zikanywea na kufungua njia zikiniruhusu niendelee na safari yangu.
Niliirudisha ile kadi yangu mfukoni kisha nikaendelea na safari yangu na baada ya
muda mfupi nikawa nimeufikia ule mlango wa mbele wa vioo wa ile casino ambapo
niliusukuma na kuzama ndani huku nikiwa na hakika kuwa macho ya njemba zile
mbili zenye nguvu za kipigo yalikuwa yakinisindikiza nyuma yangu.
Sasa nilikuwa nimeingia ndani ya Vampire Casino kisima cha starehe chenye bidhaa
zote za kishetani.
Wakati nikipiga hatua zangu kuendelea na safari mle ndani ya ile casino nikajikuta
nikijiuliza kama bado nilikuwa jijini Dar es Salaam au nilikuwa kwenye jiji lingine
mashuhuri duniani. Kwani kwa namna moja au nyingine nilikuwa nimeshangazwa
sana na mambo niliyoanza kuyaona mle ndani.
Kwa tathmini yangu ya haraka ni kuwa idadi kubwa ya watu waliokuwa
mle ndani ya ile casino walikuwa ni watu wa kutoka mataifa yenye afya kiuchumi
kama;wazungu,wachina,waarabu na wahindi. Idadi ndogo ya watu waliosalia mle
ndani walikuwa ni watu weusi kama mimi.
Katika korido fupi na pana niliyoingia niliziona jozi kadhaa za wapenzi wakiwa
wamekumbatiana wakinyonyana ndimi na kufanya matendo mengine ya kishetani.
Nilipowatazama watu wale nikagundua kuwa wanaume walikuwa wa rika tofauti
wadogo kwa wakubwa lakini wale wasichana walikuwa ni mabinti wadogo sana kwa
umri huku wakiwa wamevaa nguo fupi nusu uchi na mienge ya sigara mikononi
mwao.
Hata hivyo watu wale hawakuonekana kushtushwa sana na ugeni wangu mle
ndani badala yake walionekana kuendelea na hamsini zao. Wasichana wawili wadogo
walinisogelea na kujaribu kuniwekea ukuta njiani wakijaribu bahati zao lakini mwendo
na sura yangu viliwaonya hivyo wakawahi kunipa mgongo huku wakiachia misonyo
ya hasira.
Hatimaye nikawa nimetokezea kwenye ukumbi mpana na ndani ya ukumbi ule
kulikuwa na taa za aina tofauti zikimulika huku na kule katika namna ya kupokezana.
Upande wa kushoto wa ukumbi ule kulikuwa na makochi ya sofa yaliyopangwa katika
namna ya kuzizunguka meza fupi za vioo zilizokuwa katikati. Pia kulikuwa na meza
na viti vya kisasa ambavyo baadhi yake vilikuwa vimekaliwa na watu huku juu ya meza
hizo kukiwa na aina tofauti za vinywaji.
Sehemu ya katikati casino ile ndipo palipokuwa pakifanyika mambo ya ajabu.
Wasichana wawili wenye maumbo mazuri ya mvuto wa ngono walikuwa wamevaa
chupi nyekundu za bikini zenye mikanda myembamba zilizokuwa zimeacha wazi
baadhi ya sehemu nyeti za miili yao.
Wasichana wale walikuwa wakinyonyana ndimi na kushikana sehemu zao nyeti
katika namna ya kuwapandisha ashki wanaume waliokuwa wakiwatazama. Wasichana
wale walikuwa juu ya jukwaa dogo la umbo duara lililokuwa likimulikwa kwa mwanga
mkali wa taa tofauti zilizokuwa sehemu ya juu ya eneo lile.
Katika jukwaa lile kulikuwa na bomba moja refu lililokuwa limeshikiliwa na
sehemu ya juu ya paa la ile casino huku sehemu ya chini ya bomba lile ikiwa imejikita
katikati ya lile jukwaa la umbo duara.
Wasichana wale juu ya lile jukwaa walikuwa wakilitumia bomba lile kucheza
muziki uliokuwa ukipigwa mle ndani kwa kujibinua binua katika mitindo tofauti huku
wakizishika nyeti zao. Kwa kufanya watu wengi wa mle ndani walitulia wakiwatazama
wasichana wale katika namna ya kuhamasika na matendo ya ngono
Niliyatembeza macho yangu mle ndani na upande wa kulia wa ule ukumbi
sehemu kulipokuwa na giza hafifu nikaona kuwa kulikuwa na makochi ya sofa na
baadhi ya makochi yale yalikuwa yamekaliwa na watu. Niliutazama vizuri upande
ule na hapo nikawaona baadhi ya mabinti wadogo wakiwa uchi wa mnyama huku
baadhi yao wakiwa wamevaa sketi fupi bila nguo za ndani. Wasichana wale baadhi
yao walikuwa wamepakatwa na wanaume wadogo kwa wakubwa na nilipochunguza
vizuri nikagundua kuwa walikuwa wakifanya ngono na wanaume wale bila wasiwasi
wowote kama sodoma na gomola. Kwa kweli niliwahurumia sana wabinti wale wadogo
lakini sikuwa na namna ya kufanya.
Niligeuka na kutazama mbele ya ukumbi ule na hapo nikaona kaunta kubwa ya
vinywaji ikiwa na wahudumu waliovaa sare. Baadhi ya wahudumu wale walikuwa
wakipishana huku na kule na masinia yao mikononi kupeleka vinywaji kwa wateja na
kuchukua chupa za vinywaji zilizokwisha tumika.
Nilitembea nikikatisha kando ya ukumbi ule wa casino na nilipofika sehemu
fulani upande wa kushoto nikaona ukumbi mwingine mkubwa. Ndani ya ukumbi
ule kulikuwa na mashine nyingi za kamari zilizopangwa katika mtindo unaovutia.
Nilisimama na kutazama eneo lile na hapo nikawaona baadhi ya watu wakiwa
wanaendelea kucheza kamari katika mashine zile.
Upande wa kulia wa ukumbi ule kulikuwa na milango mitatu iliyoongozana.
Katika ile milango mitatu milango miwili ilifanana kwa ukubwa lakini ule mlango
mmoja wenyewe ulikuwa tofauti na mkubwa. Juu ya mlango ule kulikuwa na
maandishi makubwa yakisomeka Bulk transaction Only . maelezo yale yakanitanabaisha
kuwa ndani ya mlango ule kulikuwa na chumba kilichokuwa kikitumiwa cha wacheza
kamari wenye pesa nyingi. Katika ile milango miwili iliyolingana juu yake kulikuwa
na vibandiko vyenye kuelekeza sehemu za maliwato kwa wanaume na wanawake.
Muziki laini uliokuwa ukipigwa kupitia spika fulani zilizokuwa mle ndani uliwaacha
watu katika viwango vya juu vya starehe zao.
Hatimaye nikaendelea na safari yangu nikielekea kwenye eneo la ile kaunta
ya vinywaji ambapo baada ya kufika ningetafuta sehemu nzuri ya kuketi ambayo
ingeniwezesha kuona vizuri kitu chochote ambacho kingekuwa kikiendelea mle ukumbuni. Hata hivyo wakati nikiendelea kutembea mle ndani nikagundua kuwa
kulikuwa na wanaume wawili waliokaa nyuma ya ule ukumbi ambao walikuwa
wakinitazama kwa makini sana.
Nilifika pale kaunta kisha nikavuta stuli moja ndefu na kupanda juu. Watu
wachache waliokuwa kwenye kaunta ile wakijipatia kinywaji wakageuka kunitazama
kidogo kabla ya kuendelea na hamsini zao.
Mhudumu wa kaunta ile mwanaume mrefu mweusi mwenye mwili uliojengeka
vizuri na sura ya ucheshi akiwa amevaa suruali nyeusi,shati jeupe na tai ndogo nyeusi
shingoni alinisogelea haraka na kunisikiliza haja yangu.
“Leapfrog cocktail baridi tafadhali!” nilimwambia mhudumu yule huku nikigeuka
kutazama kule nyuma ya ule ukumbi sehemu walipokuwa wamekaa wale wanaume
wawili. Sikuwaona wale watu hata hivyo hali ile haikunitia mashaka.
Muda mfupi baadaye yule mhudumu wa ile kaunta alinisogezea bilauri ya
kinywaji baridi cha Leapfrog cocktail yenye mrija mrefu na karatasi nyeupe ya tishu
iliyozungushiwa kwa nje.
Niliisogeza bilauri ile karibu yangu na kupitia mrija ule nikavuta funda moja la
kinywaji kile kikali na kukiacha kikiteremka taratibu kifuani kwangu na kutengeneza
starehe ya aina yake.
Kabla ya kuja kwenye casino hii nilikuwa nimetoka mtaa wa Nkurumah kwenye ile
nyumba huku nikitarajia kumuona tena yule msichana niliyemfuatilia kutoka Vampire
Casino usiku wa jana. Hata hivyo juhudi zangu zilikuwa zimegonga mwamba.
Nilikuwa nimejibanza kwa muda mrefu mle ndani ya ile nyumba huku nikimsubiri
yule msichana arudi lakini kitendo cha kuyaona masaa mengi yakitoweka bila msichana
yule kujitokeza nikaamua kutoka nje ya nyumba ile na kuendelea na hamsini zangu
huku nikipanga kurudi tena baadaye.
Bado akili yangu ilikuwa ikiendelea kusumbuka katika kutaka kufahamu kuwa
msichana yule alikuwa nani na kwani alihusika katika kifo cha yule mtu kule ghorofani
mtaa wa Nkurumah. Hata hivyo bado nilijipa matumaini kuwa hatimaye ukweli wa
mambo ungejulikana.
Mara kadhaa nilijikuta nikishawishika kutaka kuwasaidia polisi juu ya muuaji yule
kwani hadi wakati huu ushahidi nilikuwanao ingawa haukuwa wa moja kwa moja.
Lakini nilijikuta nikiachana na mpango hule pale nilipoanza kuhisi kuwa huwenda
msichana yule alikuwa akihusika kwa namna fulani na kile nilichokuwa nikikipeleleza.
Nilivuta tena funda moja la kinywaji kuupoza mtima wangu huku nikiyatembeza
tena macho yangu mle ukumbini. Kutoka pale nilipoketi niliweza kuziona ngazi
upande wa kushoto wa ukumbi ule zilizokuwa zikielekea ghorofa ya juu. Tukio lile
likanipelekea nianze kuhisi kuwa kule ghorofani ngazi zile zilipokuwa zikielekea
kulikuwa na shughuli nyingine za casino ile zilizokuwa zikiendelea. Nilipotazama vizuri
upande ule wenye zile ngazi mara nikakiona kibao kingine kidogo chenye maandishi
ya V.I.P hall and accommodation na hapo nikajua kuwa kule juu kulikuwa na ukumbi
mkubwa wa starehe na sehemu za kulala zilizokuwa zikitumika na watu wa daraja la juu. Kwa kweli ule ulikuwa ni uwekezaji wa aina yake. Niliendelea kuyatembeza
macho yangu mle ndani huku nikivuta sigara yangu taratibu mdomoni.
Niliitazama tena saa yangu ya mkononi kisha nikavuta funda jingine la kinywaji.
Bado kulikuwa na muda mfupi wa kusubiri kabla ya Milla Cash hajaingia mle ndani na
hicho ndiyo nilichokuwa nikikisubiri.
“Vipi hujisikii upweke?” mwanamke mmoja aliyeketi jirani yangu pale kaunta
aliniuliza kwa lugha safi ya kiingereza pengine baada ya kushochwa na ukimya wangu.
Mwanamke yule alikuwa amevaa suruali nyeusi ya jeans na blauzi nyepesi ya rangi ya
cream chafu. Katika vidole vya mkono wake alikuwa amevaa pete mbili za madini ya
Tanzanite na Almasi nyeupe. Nywele zake za rasta alikuwa amezizungusha na kuzifunga
kichwani kwa kitambaa cha rangi nyeusi. Mara nilipotulia na kumsikiliza vizuri yule
mama nikagundua kuwa namna ya matamshi ya kiingereza chake alifaa kufananishwa
na raia wa kutoka nchini Nigeria.
Mwanamke yule alikuwa akivuta sigara ya brand ya kifahari na juu ya meza ile ya
kaunta mbele yake alikuwa na kinywaji baridi cha Cocktail aina ya Manhattan. Kwa
tathmini yangu ya haraka nikahitimisha kuwa mwanamke yule alikuwa ni mtu mwenye
kipato cha kueleweka.
“Nilidhani unahitaji utulivu kidogo bibie” nilimwambia mwanamke yule kwa
lugha yangu safi ya kiingereza kisicho cha kubabaisha huku nikigeuka kumtazama na
kutabasamu.
“Kwa nini unapenda Cocktail ya Manhattan?” nilimchokoza mwanamke yule huku
nikimtupia macho ya udadisi.
“Ni kama wewe unavyopenda Cocktail ya Leapfrog” mwanamke yule aliongea huku
akitabasamu kisha akaendelea
“Hapo zamani nilikuwa mpenzi wa Cocktail aina ya Leapfrog,Negroni naSpritz lakini
nilijikuta nikiachana nazo baada ya kupata company nzuri ya wanywaji wa Manhattan
Cocktail. Hata hivyo sizichukii ingawa kwa sasa sizipendelei sana” mwanamke yule
aliongea huku akiitia sigara yake mdomoni.
Nilimtazama kwa udadisi mwanamke yule na hapo nikagundua kuwa alikuwa
akionekana kuzimudu vizuri starehe za dunia kwa namna yake.
“Mimi huwa ni mpenzi wa Manhattan Cocktail ingawa siyo mnywaji wa mara kwa
mara” niliongea kwa utulivu na baada ya kitambo kifupi cha ukimya nikaendelea.
“Lafudhi yako inaonesha kuwa wewe siyo mwenyeji waTanzania”
“Mimi ni raia wa Nigeria lakini maskani yangu kwa sasa yapo Capetown nchini
Afrika ya kusini” mwanamke yule aliniambia kwa utulivu huku akivuta funda la
kinywaji chake pale juu ya kaunta.
“Umekuja hapa Dar es Salaam kwa safari ya kikazi?” nilimuuliza yule mwanamke
huku taratibu kisha nikaipeleka sigara yangu mdomoni.
“Hapana! nipo hapa Dar es Salaama kwa ajili ya mapumziko mafupi ya likizo
yangu” yule mwanamke akaniambia huku akinitazama na hapo nikapata nafasi ya
kuiona vizuri sura yake.Alikuwa mwanamke wa makamo umri wake huwenda ulikuwa kati ya miaka
ishirini na nane na thelathini na mbili. Macho yake imara yenye nguvu makubwa na
legevu kiasi yalikuwa na kila kitu mwanaume alichopenda kukiona. Tulitazamana
na macho yetu yalipokutana kila mmoja akatabasamu na hapo haraka nikajua kuwa
alikuwa ni mwanamke wa aina yangu.
“Kwa nini ukaichagua Dar es Salaam kama sehemu ya mapumziko ya likizo
yako badala ya miji mingine ya Afrika mashariki kama Nairobi,Kigali,Bujumbura au
Kampala?” nilimuuliza mwanamke yule baada kuvuta funda la kinywaji.
“Nimewahi kufika huko kote lakini mtindo wa maisha ya hapa jijini Dar es Salaam
naweza kusema umenivutia sana” mwanamke yule aliongea huku akitabasamu na
hapo uzuri wake ukajitokeza.
“Kwa vipi?” nikamuuliza.
“Watanzania ni watu wakarimu mno!” yule mwanamke aliongea huku akiangua
kicheko hafifu kilichoniacha njia panda na hapo nikashindwa kuelewa kama kweli sisi
watanzania tulikuwa wakarimu kiasi cha kusifiwa na wageni au tulikuwa waoga katika
kufanya maamuzi ya msingi.
Nilipozikumbuka kashfa mbali mbali zilizokuwa zikiibuka nchini Tanzania kila
kukicha kama;EPA,Richmond,Escrow,kusafirishwa kwa wanyama wetu kwenye ndege kwenda
nchi za nje,kauli za viongozi wakwapuaji wa mamilioni ya pesa zetu bila huruma,chokochoko
za itikadi za kidini,mauaji ya wapigania haki na usawa na ubabe wa vingozi wetu,nikabaki
nikimeza funda kubwa la mate kuitowesha hasira yangu kifuani.
“Karibu sana!” hatimaye niliongea huku nikitabasamu.
“Ahsante!” yule mwanamke akaitikia huku akivuta funda la kinywaji.
Nilivuta funda moja la kinywaji kisha nikayatembeza macho yangu mle ukumbini
kabla ya kuyarudisha kwa yule mwanamke na hapo nikamuuliza huku nikimtazama
usoni.
“Jina lako?”
“Iko–ojo Obaje” mwanamke yule aliongea huku akiitia sigara yake mdomoni na
alipoitoa akaupuliza moshi wake pembeni kisha akaisogeza ile bilauri yake ya kinywaji
na kuvuta mafunda kadhaa kisha akageuka tena na kunitazama.
“Na wewe je?” akaniuliza.
“Naitwa Stephen Masika” nikamdanganya
“Wewe ni mwenyeji wa hapa Dar es Salaam?”
“Ndiyo! nimezaliwa na kukulia hapa”
“Oh! vizuri sana bila shaka sasa nitakuwa nimepata mwenyeji wa kufikia hapa jijini
Dar es Salaam” mwanamke yule akaongea huku akiangua kicheko hafifu cha furaha
nami nikaungana naye kwa kutabasamu kidogo kisha nikavunja ukimya.
“Umekuja na familia yako?” nilimuuliza lakini nikashangaa kumuona akitabasamu
na hatimaye kuangua kicheko.
“Mimi sina familia wala sijaolewa” mwanamke yule aliongea huku akiitia sigara
yake mdomoni huku kicheko chake kikiwa bado hakijafika tamati.
“Kwanini mwanamke mzuri kama wewe hujaolewa na umri wako unakuruhusu?”
nilimuuliza.
“Wanaume wanataka wake zao wawe ni watu wa kukaa nyumbani,wawafulie nguo
zao na kuwapigia pasi,wawapikie vyakula vitamu na kuwazalia watoto. Mimi najiona
kuwa siyo mwanamke wa aina hiyo” yule mwanamke akaongea baada ya kuitua bilauri
yake ya kinywaji pale juu ya kaunta na hapo nikamtazama huku nikimlinganisha na
maneno yake.
“Huna mpango wa kupata mtoto?” nikamuuliza na kuitia sigara yangu mdomoni
huku nikapambana na taswira ya matiti yake yaliyokuwa nusu wazi kifuani mwake.
Harufu nzuri ya manukato yake ikazipumbaza kwa muda hisia zangu. Hata hivyo
nilishangaa kumuona akitabasamu.
“Hujui kuwa mtoto ni sawa na mume wa pili. Itabidi umlishe,umfulie
nguo,umuogeshe,umpeleke hospitali,umpeleke shule. Kwa kweli nawahurumia sana
wanawake wenzangu”
“Mh! basi wewe utakuwa mwanamke wa aina yake” nilimwambia yule mwanamke
huku nikiipeleka bilauri ya kinywaji mdomoni na wakati nikifanya vile mara nikajikuta
nikivutiwa na tatoo iliyokuwa shingoni mwake. Mchoraji wa tatoo ile bila shaka alikuwa
fundi stadi mno ingawa hata hivyo tatoo ile haikunivutia hata kidogo.
Ilikuwa ni tatoo ya kichwa cha nyoka mwenye sumu kali huku akiwa ameachama
kinywa chake wazi na ulimi wake mrefu wenye pacha mbili ukiwa nje. Nikiwa
nimeduwaa kuitazama ile tatoo yule mwanamke ni kama ambaye hakuvutiwa na angalia
yangu hivyo aligeuka katika namna ya kunifanya nisiweze kuiona vizuri ile tattoo. Kwa
kutaka kumpa uhuru zaidi nikatumbukiza hoja mpya.
“Hapa Dar es Salaam umefikia wapi?” nilimuuliza yule mwanamke na hapo
nikamuona akiupeleka mkono wake kwenye pochi yake ndogo ya mkononi.
Alipoifungua ile pochi akatoa kadi ndogo na kunipa. Niliipokea ile kadi na kuitazama
kwa makini. Ilikuwa ni kadi ndogo yenye maelezo ya namba ya chumba cha hoteli
moja ya kifahari iliyopo jijini Dar es Salaam na chini ya kadi ile kulikuwa na namba
za simu.
“Ukipata nafasi unaweza kuja kunitembelea kwani bado nina siku kadhaa za kukaa
hapa jijini Dar es Salaam” yule mwanamke akaniambia huku akivuta tena funda la
kinywaji pale kaunta.
“Ninaweza kukutembelea wakati gani?” nilimuuliza na baada ya kufikiria kidogo
akaniambia
“Muda wowote utakapopata nafasi”
“Nashukuru sana,nitajitahidi” niliichukua ile kadi na kuitia mfukoni na wakati
nikifanya vile macho yangu yakajikuta yakivutwa na msichana aliyekuwa akiingia mle
ndani. Nikageuka na kutazama upande ule wa ukumbi na mara nikamuona Milla Cash
akiingia mle ndani.
Mshangao kidogo ukiwa umenishika nikayapelekea macho yangu nikimtazama
msichana yule kwa udadisi na mara hii niliweza kuubaini vizuri uzuri wake. Alikuwa mwanamke mzuri mno niliyewahi kumuona katika kipindi chote cha maisha yangu.
Nikiwa na hakika kuwa pale nilipokuwa nimekaa isingekuwa rahisi kwake
kunitambua niliyapa macho yangu utulivu huku ubongo wangu ukifanya usajili makini
wa taarifa nilizokuwa nikizihitaji.
Milla Cash alikuwa akitembea kwa madaha katika ule mtindo wa catwalk huku
mwili wake ukinesa taratibu kama mtu aogopaye kukanyaga ardhi. Alikuwa amevaa
gauni jepesi na fupi la rangi nyekundu iliyoiva vizuri lenye utepe mweupe kiunoni
na kulifanya umbo lake adimu lijichore vizuri na kuamsha hisia kwa mwanaume
yeyote ambaye angethubtu kumtazama. Gauni lile fupi liliyaanika wazi mapaja yake
laini yenye minofu ya misuli. Uwazi mdogo ulioachwa na gauni lile kifuani mwake
uliyaacha wazi matiti yake makubwa ya wastani yenye chuchu imara.
Milla Cash aliendelea kutembea kwa madaha huku akiyaacha macho ya wanaume
waliokuwa mle ukumbuni yakimsindikiza kila alipozisimika chini hatua zake. Wale
walinzi wake wawili walimuwekea ngome imara ya ulinzi upande wa kulia na kushoto
huku wakiwa wameshika mabegi mikononi mwao. Nilipowachunguza walinzi wale
vizuri nikatambua kuwa walikuwa walinzi mahiri wasiokuwa na mzaha. Suti zao
nyeusi ziliwakaa vyema na miili yao ilikuwa imejengeka vizuri kuwakabili wakorofi.
Bado macho yangu yalikuwa kwa Milla Cash huku moyoni nikijiuliza kwanini
alikuwa akilindwa namna ile na kwa kweli tukio lile lilinishangaza sana. Nikautia tena
mche wangu wa sigara mdomoni huku nikiupisha utulivu kichwani mwangu.
Niliendelea kumtazama Milla Cash huku nikitambua kuwa subira na uvumilivu
ndiyo silaha kubwa katika mafanikio yangu. Nilipoitoa sigara yangu mdomoni
nikaupuliza moshi pembeni kisha nikainama na kuvuta funda la kinywaji huku
nikiyatembeza macho yangu mle ukumbini.
Sasa nilimuona Milla Cash na wale wapambe wake wakipanda zile ngazi kuelekea
ile ghorofa ya juu yenye kile kibao cha V.I.P hall and Accommodation. Nikaendelea
kuwatazama hadi pale walipopotea kabisa machoni mwangu na hapo nikabaki
nikitafakari.
Baada ya kitambo kifupi kupita tangu Milla Cash na wale walinzi wake kupanda
kule ghorofani. Mara nikamuona mtu mmoja aliyekuwa ameketi pale kwenye makochi
ukumbini akisimama na kuelekea kule juu ya ghorofa. Kilipita kitambo kirefu huku
macho yangu yakiendelea kutazama juu ya zile ngazi na hatimaye nikamona yule mtu
aliyeelekea kule juu hapo awali akishuka tena zile ngazi.
Yule mtu alipofika pale chini hakurudi tena pale alipokuwa ameketi hapo awali
na badala yake aliambaa na ukuta wa ukumbi ule akielekea nje huku akiwa ameushika
mkoba mweusi wa ngozi mkononi.
Muda mfupi baada ya yule mtu wa awali kutokomea mara nikamuona mtu
mwingine akisimama kutoka pale ukumbini na kuelekea kule juu ghorofani alipotoka
yule mtu wa awali huku akiwa na mkoba mkononi. Hali ikawa kama kwa yule mtu
wa kwanza kwani baada kitambo kifupi kupita mara nilimuona yule mtu akirudi na
mkoba wake mkononi na alipomaliza kushuka zile ngazi hakurudi pale alipokuwa ameketi hapo awali badala yake nilimuona akielekea nje. Mtu wa tatu naye akafanya
vilevile kabla ya kufuatiwa na mtu mwingine. Kwa kweli hali ile ilinishangaza sana.
Niliendelea kuitazama mienendo ya watu wa mle ndani huku nikiendelea kuupisha
utulivu akilini mwangu. Hata hivyo nilishindwa kabisa kuelewa kilichokuwa kikiendelea
mle ndani. Hatimaye nikainama tena na kuvuta mafunda kadhaa ya kinywaji hadi pale
bilauri ile ilipobaki tupu.
Fikra zangu ziliporudi eneo lile nikakumbuka kuwa uchunguzi wangu ulikuwa
umeniweka mbali na maongezi ya Iko-Ojo Obaje aliyekuwa kando yangu pale kaunta.
Hivyo nikageuka na kumtazama Iko-Ojo Obaje huku nikiona aibu kwa kutokuwa
makani na uwepo wake. Yule mwanamke hakuwepo pale alipokuwa ameketi na kiti
chake kilikuwa wazi. Loh! nikaanza kujilaumu kuwa nilikuwa nimepoteza umakini kwa
kiwango cha juu huku nikijiuliza kuwa mwanamke yule angekuwa ameelekea wapi.
Hatimaye nikaitoa wallet yangu kutoka mfukoni ambapo niliifungua na kuchukua kiasi
fulani cha pesa kwa ajili ya kulipia kile kinywaji. Hata hivyo nilishangaa sana kumuona
yule mhudumu wa kaunta ya vinywaji akikataa kuipokea pesa yangu.
“Bro! umeshalipiwa” yule mhudumu wa kaunta akaniambia huku akiondoa bilauri
za vinywaji zilizokuwa pale kaunta halafu kwa kitambaa chake kidogo mfano wa taulo
alichokuwa amekining’iniza begani akaanza kufuta ile meza ya kaunta.
“Una maana gani?” nilimuuliza yule mhudumu wa kaunta kwa makini huku
nikimtazama usoni.
“Umeshalipiwa kinywaji na yule dada aliyekuwa ameketi kando yako” yule jamaa
akaniambia huku akitabasamu. Sikuwa namna hivyo nikaichukua pesa yangu pale juu
ya kaunta na kuitia mfukoni.
“Alikueleza kuwa anaelekea wapi?” nikamuulia yule mhudumu wa kaunta
“Hapana!” yule mhudumu akanijibu huku akiendelea kutabasamu na hapo
nikajua kuwa kile kitendo cha mimi kulipiwa kinywaji na yule mwanamke kilikuwa
kimemfurahisha sana. Nilimuacha yule mhudumu akiendelea kufurahi kisha nikashuka
kutoka kwenye ile stuli ndefu ya kaunta na kushika uelekeo wa upande wa kulia wa ile
kaunta nikielekea eneo la maliwato la ukumbi ule.
Wakati nikitembea kuelekea eneo la maliwato la ukumbi ule nikajikuta nikivutiwa
na ubora wa casino ile. Mikono ya mafundi ujenzi ilikuwa imeitendea haki taaluma
yao. Kila eneo la ndani ya casino ile lilivutia kulitazama na kuta zake zilikuwa safi na
zilizonyooka vizuri na kupambwa kwa nakshi tofauti za kupendeza. Mwanga wa taa za
mle ndani uliakisiwa vizuri na marumaru za kisasa zilizokuwa sakafuni na kutengeneza
mandhari nzuri inayovutia sana kutazama.
Baada ya hatua chache za safari yangu hatimaye niliingia upande wa kushoto
sehemu iliyokuwa na milango miwili. Mlango mmoja ulikuwa kwa ajili ya sehemu
ya maliwato ya wanaume na mlango mwingine ulikuwa ni kwa ajili ya sehemu ya
maliwato ya wanawake.
Nilishika kitasa cha mlango wa maliwato ya kiume kisha nikaufungua mlango ule
na kupotelea ndani. Mara baada ya kuingia mle ndani nikawa nimetokezea kwenye korido pana iliyotazama na milango kumi na mbili ya vyoo. Baadhi ya milango ile
ilikuwa wazi huku mingine ikiwa imefungwa. Hata hivyo hakukuwa na dalili za uwepo
wa mtu yoyote mle ndani. Vyoo vyote vilionekana visafi na kwenye ule ukuta wa
korido iliyokuwa ikitazamana na ile milango ya vyoo kulikuwa na kioo kipana cha
kujitazama.
Pembeni ya kioo kile kulikuwa na masinki ya ukutani kwa ajili ya haja ndogo
pamoja na mifereji midogo ya chini iliyojengewa vizuri kwa marumaru nyeupe kwa
ajili ya kukusanya maji taka na kuyasafirisha nje.
Nilichagua choo kimoja kilichokuwa mwishoni mwa ile korido kisha nikafungua
mlango na kuingia ndani. Nilitaka kwenda haja ndogo kwani kile kinywaji kilikuwa
kimekijaza vibaya kibofu changu.
Wakati nilipokuwa nikijiandaa kwenda haja ndogo mara nikaanza kuhisi kuwa mle
ndani kwenye korido ya vile vyoo kulikuwa na mtu na mtu huyo alikuwa akitembea
taratibu kuvikagua vile vyoo.
Nikiwa nimeanza kuhisi jambo baya sikutaka kumshtua mtu yule hivyo kimiminika
changu nikakitupia ukutani na hapo kikawa kikishuka chini kwa utulivu katika ukimya
wa kifo huku masikio yangu yakifanya kazi ya ziada kusikiliza hatua za mtu yule.
Hatimaye ile sauti ya hatua za yule mtu ikakoma na eneo lote la vile vyoo likawa
kimya. Niliendelea kuyatega masikio yangu na kwa kweli sikuweza kuhisi kitu chochote
eneo lile. Baada ya muda mrefu wa kusubiri hatimaye hisia zikanijia kuwa nje ya ule
mlango wa choo changu kulikuwa na mtu aliyesimama.
Hali ile ikanipelekea nikatishe haraka kile nilichokuwa nikikifanya huku nikiudhika
sana na hali ile. Niligeuka taratibu na kutazama chini ya ule mlango sehemu kulipokuwa
na uwazi mdogo kati ya ule mlango na sakafu ya kile choo. Kupitia mwanga wa taa
iliyokuwa nje ya ile korido ya vile vyoo niliweza kukiona kivuli cha miguu ya mtu na
hapo koo likanikauka ghafla. Muda mfupi uliyofuata mara nikaanza kuona kitasa cha
ule mlango kikizungushwa taratibu na hapo nikajua kuwa sikuwa salama tena.
Nikiwa bado nafikiria kitu cha kufanya ule mlango wa kile choo ulifunguliwa kwa
kasi kisha mkono uliyoshika bastola ukatangulizwa mbele. Niliwahi kuudaka mkono
ule kisha nikaupigiza ukutani kwa nguvu zangu zote na hivyo kuifanya ile bastola
ianguke chini. Hata hivyo yule mtu alikuwa makini sana hivyo akatupa ngumi mbili
zenye kasi ya upepo. Niliwahi kujibanza pembeni hivyo pigo moja la ngumi lilinikosa
na kukata hewa bila majibu.
Pigo la pili lilipotupwa nilichelewa kidogo hivyo ngumi yake makini ikaitandika
vibaya shingo yangu na kunifanya nihisi kichefuchefu huku maumivu makali
yakisambaa mwilini mwangu na kunipelekea mfadhaiko wa aina yake. Halafu
nikapokea mapigo mawili ya ngumi kavu za tumboni zilizolikoroga vibaya tumbo
langu na kunifanya nianze kuhema ovyo. Nilikuwa nimejitahidi kuyadhibiti mapigo
yale bila mafanikio kwani yule mtu alikuwa fundi sana wa mapigano.
Pigo la teke alilolirusha mtu yule huku dhahiri akioneka kudhamiria kuzitawanya
kama siyo kuzipasua vibaya korodani zangu nikalipangulia chini kwa mikono yangu imara. Tukio lile likampelekea yule mtu apoteze mhimili na kuanza kupepesuka ovyo
lakini alikuwa mwepesi sana. Akapepesuka kidogo hadi pale alipopata mhimili wa
ukuta wa kile choo na bila kusubiri akarusha pigo jingine matata la ngumi ya chembe
ya moyo.
Mara hii nilikuwa mtulivu na makini hivyo nikaipangua ngumi ile kama mchezo
huku nikiisukumia kwenye koki ya bomba la maji la mle ndani na hapo nikasikia sauti
kali ya mvunjiko wa mfupa wa mkono wa yule mtu. Yule mtu akapiga yowe kali na
kubweka kama mbwa mwizi lakini hakukata tamaa mapema.
Pigo jingine la teke alilolirusha yule mtu niliwahi kuliona hivyo nikalikwepa kwa
kusogea kidogo pembeni na hapo pigo lile la teke likapita bila shabaha na kujipigiza
ukutani. Mguu wa yule mtu ukavunjika kwenye kifundo na kumpelekea yule mtu
apige yowe kali la aina yake.
Hata hivyo yule mtu alikuwa mkaidi hivyo kwa ule mkono wake mmoja mzima
akawahi kuikota ile bastola yake mle ndani sakafuni hata hivyo alichelewa kwani
ulikuwa ni kama mchezo wa paka na nyoka. Niliwahi kumshika miguu yule mtu na
kumvuta nyuma hivyo ile bastola akawa anaiona kwa mbele yake lakini hakuweza
kuifikia.
“Wewe ni nani na una shida gani na mimi?” nikamuuliza yule mtu huku nikiwa
nimemkwida shati lake mkononi. Yule mtu akaendelea kulalama kutokana na
maumivu makali ya majeraha yake. Alikuwa mwanaume mrefu na mweusi mwenye
mwili uliojengeka vyema. Alikuwa amevaa suruali nyeupe ya jeans na fulana nyekundu
na miguuni alikuwa amevaa buti za askari. Kijana wa makamo mwenye umri wa miaka
thelathini na kitu.
“Nakuuliza bwana wewe ni nani na una shida gani?”
Yule mtu hakunijibu badala yake akaendelea kugugumia maumivu na hapo
nikamchapa makofi mawili ya nguvu usoni kumuweka sawa.
“Nakuuliza wewe una shida gani na mimi mbona tunafuatana fuatana chooni
kama mainzi?” nilimuuliza tena yule mtu na nilipomchunguza vizuri nikagundua
kuwa alikuwa miongoni mwa wale watu wawili waliokuwa wakinitazama kule nyuma
ukumbini.
“Sikufuati wewe bwana” yule mtu akaongea kwa hofu huku akilalama kwa
maumivu.
“Kwani vyoo vyote humu ndani vina watu?” nilimuuliza huku nikizidi kumkwida.
“Hapana!”
“Sasa mbona huna msimamo wewe bwege na yule mwenzako yuko wapi?”
nikamuuliza kwa hasira
“Mwenzangu yupi?” yule mtu akaniuliza huku akinitazama kwa mshangao.
“Mwenzako uliyekuwanaye kule nyuma ya ukumbi”
“Mbona sikuelewi?”
“Hivi nyinyi mna shida gani na mimi?” nilimuuliza yule mtu na kumchapa kofi
jingine usoni na hapo akalalama kwa maumivu.
“Unanionea bure tu mimi sifahamu chochote” yule mtu akazidi kulalama lakini
alikuwa ni mtu mwenye hila kwani wakati akinisemesha kumbe alikuwa akiupeleka
haraka mkono wake nyuma kiunoni mwake ili kuichukua bastola yake nyingine ya
ziada na hapo mshipa wa huruma ukanikatika.
Nilikuwa kwenye nafasi nzuri hivyo lengo lake halikufanikiwa kwani haraka
niliwahi kukipigiza kichwa chake kwenye sinki la choo cha mle ndani. Kichwa chake
kikafumuka na ubongo wake ukaruka na kutapakaa kwenye marumaru za mle ndani.
Yule mtu akahangaika kidogo kabla ya kutulia huku roho yake ikiwa mbali na mwili.
Nilimaliza kumfanyia upekuzi yule mtu pasipo kupata kitu chochote cha maana
kwake hivyo nikanawa vizuri kwenye bomba la mle ndani na nilipomaliza nikarudi na
kumalizia haja yangu kwenye kile choo.
Sikutaka mtu yoyote anikute mle ndani hivyo mara tu nilipomaliza shida zangu
nikatoka na kuufunga ule mlango wa choo halafu kwa msaada wa kalamu niliyokuwa
nayo mfukoni nikaandika kwa maandishi makubwa juu ya mlango ule wa choo kuwa.
CHOO HIKI HAKITUMIKI.
Dakika chache zilizofuata nilikuwa mbali na choo kile huku taratibu sigara yangu
ikiteketea mdomoni.
Mara hii nilijikuta nikimkumbuka tena Milla Cash na wale wapambe wake wakiwa
ubavuni. Hata hivyo macho yangu bado yaliendelea na kazi ya kutathmini sura na
mienendo ya watu waliokuwa mle ndani.
Mambo yangu sasa yalitakiwa kwenda haraka kabla ya uwepo wa yule mtu kule
chooni haujashtukiwa. Niliendelea kutembea mle ndani huku nikikatisha kando ya ile
kaunta ya vinywaji kisha nikapita pembeni ya ule ukumbi wa casino kama mwenyeji.
Sikumuona mtu yeyote akinitazama au kunifuatilia hivyo nikaamini kuwa hali ilikuwa
shwari.
Nilipofika mwisho wa ule ukumbi nikashika uelekeo wa upande wa kulia na muda
siyo mrefu nikawa nimezifikia zile ngazi na kuanza kuzipanda nikielekea kule juu.
Wakati nikiendelea kuzipanda zile ngazi njiani nikapishana na mwanaume mmoja
mwarabu akishuka zile ngazi na mkoba mweusi mkononi. Niligeuka na kumtazama
yule mwarabu huku nikiwa nimevutiwa sana na ule mkoba wake mkononi.
Ule mkoba ulikuwa ukifanana na ile mikoba ya wale watu waliokuwa wakipanda
kule juu ghorofani muda mfupi wakati ule baada ya Milla Cash kufika.
Katika zile ngazi kulikuwa na kamera mbili zilizopandwa katika namna ya kunasa
taswira za watu wanaopanda na kushuka kwenye zile ngazi. Nilizitazama kamera zile
kwa hila hata hivyo nilifurahi kuwa nilikuwa nimevaa kofia yenye kuikinga vizuri sura
yangu.
Wakati nikiendelea kuzipanda zile ngazi mawazo fulani yalikuwa yakipita kichwani
mwangu. Bado nilikuwa nikimkumbuka yule mtu niliyepambana naye kule chooni
muda mfupi uliyopita. Nilikuwa na kila hakika kuwa yule mtu alikuwa amedhamiria
kuniua. Ama kwa tafsiri nyingine ni kuwa uwepo wangu mle ndani tayari ulikuwa
ukifahamika na baadhi ya watu. Kwa kweli nilishindwa kabisa kuelewa kitu kilichokuwa kikiendelea mle ndani.
Nilipomaliza kuzipanda zile ngazi nikawa nimetokezea mbele ya korido nyingine
ya ghorofa ya pili lakini mandhari yale hayakuwa kama ya kule chini nilipotoka.
Nilisimama kidogo pale juu huku nikiyachunguza mandhari yale na hapo nikagundua
kuwa kulikuwa na korido mbili. Korido moja ilikuwa upande wa kushoto na korido
nyingine ilikuwa upande wa kulia. Korido zile zilikuwa zimelizunguka eneo kubwa
la ukumbi mwingine wa pale juu uliyofunikwa wenye umbo kubwa mfano wa koni.
Niliutazama ukumbi ule wenye kiwambo cha kuzuia sauti ama Sound proof na
haraka nikatambua kuwa mle ndani kulikuwa na mambo makubwa zaidi ya kishetani
yaliyokuwa yakiendelea. Nilirudia tena kuitazama korido ile na hapo kitu fulani
kikaanza kujengeka kichwani mwangu.
Kulikuwa na milango mingi iliyokuwa ikitazamana na zile korido na hapo mawazo
fulani yakaanza kujengeka kichwani mwangu. Milango ile mingi ilikuwa ikitazamana
na zile korido mbili kuuzunguka ule ukumbi.
Juu ya milango ile kulikuwa na namba na hapo nikawa na hisia juu ya nini
kilichokuwa kikiendelea mle ndani. Nikashawishika kuisogelea ile milango lakini
kwa kuwa eneo lile lilikuwa likitazamana na zile ngazi niliona kuwa yeyote ambaye
angeniona eneo lile angeweza kunitilia mashaka hivyo niliamua kuifuata ile korido ya
upande wa kulia.
Niliendelea kutembea huku nikiitazama ile milango ya vile vyumba ambapo
kwa wakati huu niliigundua kuwa yote ilikuwa ikifanana kwa mwonekano. Wakati
nikiendelea na safari yangu taswira ya yule msichana Milla Cash ikawa ikiendelea
kuumbika taratibu kichwani mwangu. Tatizo ni kuwa sikuweza kufahamu kuwa Milla
Cash alikuwa ameingia katika chumba kipi miongoni mwa vyumba vile.
Wakati nilipokuwa nikiendelea na uchunguzi wangu ghafla mlango wa chumba
kilichokuwa kikifuatia mbele yangu ulifunguliwa kisha mwanaume mmoja mwarabu
alitoka nje ya chumba kile na kunipita pasipo kunipa salamu huku marashi yake makali
yakiitesa pua yangu.
Niligeuka na kumtazama Mwarabu yule na hapo nikagundua kuwa mkononi
alikuwa ameshika mfuko mweusi uliyofanana na ile mifuko ya wale watu wa awali.
Kwa kweli nilishangazwa sana na hali ile hata hvyo niliendelea kumtazama mwarabu
yule hadi pale alipopotea kwenye zile ngazi za kushukia kule chini nilipotoka kisha
nikayarudisha tena macho yangu kuutazama ule mlango wa kile chumba ambacho
muda mfupi uliyopita yule mwanaume mwarabu alikuwa ametoka mle ndani.
Hatimaye nikazitupa hatua zangu kwa utulivu nikiuendea ule mlango wa kile
chumba huku nikitazama huku na kule kama kungekuwa na mtu yeyote aliyekuwa
akinitazama. Nilipofika nikakishika kitasa cha ule mlango na kuusukuma taratibu. Ule
mlango haukuwa umefungwa hivyo ulifunguka taratibu bila pingamizi lolote na hapo
nikaingia mle ndani na kuufunga kwa nyuma.
Nikiwa sasa nimeingia mle ndani ya kile chumba niliweza kuinusa vizuri ile harufu
kali ya yale marashi ya yule mwarabu aliyetoka mle ndani muda mfupi uliyopita.
Nilipomaliza kuzipanda zile ngazi nikawa nimetokezea mbele ya korido nyingine
ya ghorofa ya pili lakini mandhari yale hayakuwa kama ya kule chini nilipotoka.
Nilisimama kidogo pale juu huku nikiyachunguza mandhari yale na hapo nikagundua
kuwa kulikuwa na korido mbili. Korido moja ilikuwa upande wa kushoto na korido
nyingine ilikuwa upande wa kulia. Korido zile zilikuwa zimelizunguka eneo kubwa
la ukumbi mwingine wa pale juu uliyofunikwa wenye umbo kubwa mfano wa koni.
Niliutazama ukumbi ule wenye kiwambo cha kuzuia sauti ama Sound proof na
haraka nikatambua kuwa mle ndani kulikuwa na mambo makubwa zaidi ya kishetani
yaliyokuwa yakiendelea. Nilirudia tena kuitazama korido ile na hapo kitu fulani
kikaanza kujengeka kichwani mwangu.
Kulikuwa na milango mingi iliyokuwa ikitazamana na zile korido na hapo mawazo
fulani yakaanza kujengeka kichwani mwangu. Milango ile mingi ilikuwa ikitazamana
na zile korido mbili kuuzunguka ule ukumbi.
Juu ya milango ile kulikuwa na namba na hapo nikawa na hisia juu ya nini
kilichokuwa kikiendelea mle ndani. Nikashawishika kuisogelea ile milango lakini
kwa kuwa eneo lile lilikuwa likitazamana na zile ngazi niliona kuwa yeyote ambaye
angeniona eneo lile angeweza kunitilia mashaka hivyo niliamua kuifuata ile korido ya
upande wa kulia.
Niliendelea kutembea huku nikiitazama ile milango ya vile vyumba ambapo
kwa wakati huu niliigundua kuwa yote ilikuwa ikifanana kwa mwonekano. Wakati
nikiendelea na safari yangu taswira ya yule msichana Milla Cash ikawa ikiendelea
kuumbika taratibu kichwani mwangu. Tatizo ni kuwa sikuweza kufahamu kuwa Milla
Cash alikuwa ameingia katika chumba kipi miongoni mwa vyumba vile.
Wakati nilipokuwa nikiendelea na uchunguzi wangu ghafla mlango wa chumba
kilichokuwa kikifuatia mbele yangu ulifunguliwa kisha mwanaume mmoja mwarabu
alitoka nje ya chumba kile na kunipita pasipo kunipa salamu huku marashi yake makali
yakiitesa pua yangu.
Niligeuka na kumtazama Mwarabu yule na hapo nikagundua kuwa mkononi
alikuwa ameshika mfuko mweusi uliyofanana na ile mifuko ya wale watu wa awali.
Kwa kweli nilishangazwa sana na hali ile hata hvyo niliendelea kumtazama mwarabu
yule hadi pale alipopotea kwenye zile ngazi za kushukia kule chini nilipotoka kisha
nikayarudisha tena macho yangu kuutazama ule mlango wa kile chumba ambacho
muda mfupi uliyopita yule mwanaume mwarabu alikuwa ametoka mle ndani.
Hatimaye nikazitupa hatua zangu kwa utulivu nikiuendea ule mlango wa kile
chumba huku nikitazama huku na kule kama kungekuwa na mtu yeyote aliyekuwa
akinitazama. Nilipofika nikakishika kitasa cha ule mlango na kuusukuma taratibu. Ule
mlango haukuwa umefungwa hivyo ulifunguka taratibu bila pingamizi lolote na hapo
nikaingia mle ndani na kuufunga kwa nyuma.
Nikiwa sasa nimeingia mle ndani ya kile chumba niliweza kuinusa vizuri ile harufu
kali ya yale marashi ya yule mwarabu aliyetoka mle ndani muda mfupi uliyopita. Hata hivyo harufu ile ilikuwa imechanganyikana na harufu ya moshi wa sigara za kifahari
na marashi mengine ya kike. Hisia zikaniambia kuwa huwenda mle ndani kulikuwa na
mtu mwingine ambaye sikuweza kumfahamu mapema.
Nilisimama nikikichunguza chumba kile na mbele yangu nikaliona pazia jepesi la
kamba nyembamba zilizotungwa simbi za baharini. Kupitia uwazi mdogo uliyokuwa
baina ya zile kamba niliweza kuona mle ndani ya lile pazia.
Nyuma ya pazia lile kulikuwa na chumba kikubwa chenye makochi makubwa ya
sofa za kisasa kilichokuwa kikimulikwa kwa mwanga hafifu wa taa za rangi tofauti za
kupendeza na sehemu fulani katika chumba kile sauti ya muziki laini ilikuwa ikisikika.
Nilizitupa hatua zangu taratibu kulisogelea lile pazia na nilipolifikia nikalisogeza
pembeni kuchungulia mle ndani na hapo nikaiona taswira kamili ya mandhari ya kile
chumba.
Mbali na yale makochi ya sofa niliyoyaona pale awali mle ndani pia kulikuwa na
meza pana ya kioo na juu ya meza ile kulikuwa na bilauri mbili na chupa nne za
kinywaji cha kilevi aina ya Russian Standard. Chupa tatu miongoni mwa zile chupa
nne zilikuwa tupu. Pembeni ya chupa zile kulikuwa na kibeseni kidogo cha majivu ya
sigara chenye umbo mfano wa kifaranga cha bata na ndani yake kulikuwa na kipisi
kidogo cha sigara kilichokuwa kikiteketea.
Niliyatembeza macho yangu mle ndani na sehemu fulani kwenye kona ya chumba
kile kulikuwa na simu ya mezani juu ya meza ndogo yenye ua jekundu. Upande
wa kulia wa chumba kile kulikuwa na runinga kubwa ukutani na katika runinga ile
kulikuwa na filamu ya ngono iliyokuwa ikioneshwa lakini hapakuwa na mtu kwenye
kile chumba ambacho sasa nilianza kukifananisha na sebule ya aina yake. Pembeni
ya seti ile ya runinga kulikuwa na jokofu jembamba na refu lenye kuta za vioo zenye
kumuwezesha mtu yeyote kuona mle ndani ambapo kulikuwa na lukuki ya chupa za
vinywaji.
Chumba chote kilikuwa kimefunikwa kwa zulia zuri la manyoya laini lililodariziwa
kwa maua mazuri ya rangi tofauti za kuvutia. Nilisimama nikiyatazama mandhari yale
huku nikiendelea kushangazwa na uwekezaji ule wa aina yake.
Upande wa kushoto wa chumba kile kulikuwa na mlango. Mlango ule sasa ulikuwa
wazi ukitenganishwa na chumba kile cha sebule kwa pazia jepesi linalomwezesha mtu
yoyote kuona mle ndani ya kile chumba kwa shida.
Adha ya hali ya joto kali la jiji la Dar es Salaam ilikuwa imepelekwa likizo na
kiyoyozi makini kilichokuwa kikisambaza hewa ya baridi nyepesi isiyokinaisha.
Nilizitupa hatua zangu taratibu kukiendea kile chumba kilichokuwa upande wa
kushoto na mara hii nilijikuta nikivutiwa na kitu.
Katika kochi moja lililokuwa pale sebuleni nililiona vazi la kike aina ya sidiria
ya rangi ya pinki. Nilipoendelea kusogea mbele kidogo chini ya sakafuni usawa wa
kuelekea kwenye kile chumba nikaiona chupi ya bikini ya rangi nyekundu. Hatimaye
nikausogelea ule mlango na kulisogeza lile pazia nikichungulia mle ndani.
Msichana mzuri alikuwa amelala ndani ya beseni kubwa la kuogea huku baadhi ya sehemu za mwili wake kama magoti na mikono zikionekana bila kificho. Msichana
yule mzuri alikuwa amelala mle ndani ya lile beseni huku sehemu zake nyingine za
mwili wake zikishindwa kuonekana vizuri kutokana na mapovu ya sabuni nzuri ya
kunukia yaliyokuwa yametanda juu ya maji yale.
Kifua chake laini chenye mzigo wa matiti yenye ukubwa wa wastani yaliongeza
chachu nyingine katika uzuri wake. Msichana yule alikuwa amejilaza chali akitazama
juu huku kichwa chake chenye nywele ndefu,nyeusi na laini akiwa amekiegemeza
sehemu ya mbele kwenye ukingo wa lile beseni la kuogea. Mkono wake mmoja alikuwa
ameukunja na kuuegemeza upande wa kushoto kwenye lile beseni huku kiganja cha
mkono huo kikipotelea ndani ya lile povu la sabuni. Mkono wake mwingine ulikuwa
umeibana sigara katika pacha ya vidole vyake huku mkono huo ukibembea taratibu
nje ya beseni lile.
Mwanzoni nilidhani kuwa huwenda msichana yule alikuwa mfu kwa namna
alivyokuwa ameyatuliza macho yake kutazama juu kwenye dari ya chumba kile lakini
kitendo cha kumuona akiupeleka tena mkono wake mdomoni kuivuta ile sigara
kikanihakikishia kuwa msichana yule alikuwa hai na hapo nikatabasamu kidogo.
“Naomba unaniruhusu niingie mrembo” nilivunja ukimya na hali ile ikampelekea
msichana yule mrembo ashtuke na kugeuka akinitazama pale nilipokuwa nimesimama
huku akiwa ameshikwa na mshangao. Msichana yule aliendelea kunitazama kwa
mshangao halafu taratibu akalegeza uso wake na hapo tabasamu la kibiashara
likaumbika usoni mwake.
“Ondoa shaka unakaribishwa” msichana yule akaniambia huku akifanya jitihada
kidogo za kukaa vizuri kwenye lile beseni na hapo nikapata nafasi nzuri ya kuziona
chuchu zake imara zilizoupumbaza kwa muda mtima wangu.
Nilipoingia mle ndani nikaweza kuona vizuri mandhari ya kile chumba. Kilikuwa
chumba kipana chenye seti nyingine ya runinga pana ukutani na makochi ya sofa ya
ngozi nyeusi. Upande wa kulia kulikuwa na kioo kikubwa cha kujitazama na chini ya
kioo kile kulikuwa na chupa za mafuta mazuri ya kunukia pamoja na sabuni tofauti za
kuogea huku pembeni yake kukiwa kumening’inizwa mataulo mawili meupe. Sakafu
ya chumba kile kilichofaa kifananishwa na bafu la kisasa ilitengenezwa kwa marumaru
zenye rangi tofauti za kuvutia.
Niliyatembeza kwa utulivu macho yangu mle ndani na upande wa kushoto wa
chumba kile kulikuwa na sehemu ya kukaa iliyokuwa imetengenezwa kwa foronya
laini. Ile runinga ya kile chumba ilikuwa ikionesha filamu ya ngono kama ya kule
sebuleni na hapo nikajua runinga zote mbili za mle ndani zilikuwa zimeungwanishwa
na king’amuzi kimoja.
“Ahsante!” niliitikia kwa utulivu kisha taratibu nikapita na kwenda kukaa kwenye
ile sehemu yenye foronya laini huku nikiendelea kuyapeleleza mandhari yale.
“Yule rafiki yako ameenda wapi?” nilimuuliza yule msichana huku akiendelea
kunitazama.
“Rafiki yangu yupi?” yule msichana akaniuliza kwa mshangao.
“Mwarabu aliyetoka humu ndani muda mfupi uliopita!”
“Oh! sahau kuhusu yeye,huduma yake tayari imekwisha” msichana yule aliongea
kwa bashasha zote za kirafiki huku akiumba tabasamu usoni na nilipomchunguza
nikatambua alikuwa amelewa kidogo.
“Biashara inakwendaje?” nilimuuliza msichana yule huku nikimtazama.
“Dola mia moja kwa muda wa saa moja na huduma yangu utaifurahia” yule
msichana akaongea huku akiangua kicheko hafifu na hapo nikagundua kuwa alikuwa
akijitahidi kutengeneza mazingira ya kirafiki kama maadili ya kazi yake yalivyokuwa
yakimtaka. Kazi ya kuuza mwili wake.
“Haipungui?” nilimuuliza huku nikitabasamu hata hivyo umri wake mdogo
ukapeleka simanzi moyoni mwangu.
“Bei zetu ni nafuu sana ukifananisha na maeneo mengine hapa jijini Dar es
Salaam” msichana yule akaongea kwa kujiamini baada ya kuitoa sigara yake mdomoni
na nilipomchunguza nikagundua umri wake haukuwa zaidi ya miaka kumi na sita.
“Hakuna mkopo?” nilimuuliza yule msichana huku nikitumbukiza utani.
“Kama unataka mkopo nenda Pride au Faidika huko utapewa kwa masharti
nafuu” akaniambia kwa hasira huku akihisi kuwa nilikuwa nikitaka kuleta dharau
na kazi yake. Nilimtazama msichana yule huku nikimuonea huruma kwa namna
alivyokuwa mwathirika wa biashara ile ya ngono huku akiwa na umri mdogo ingawa
yeye mwenyewe hakuonekana kujali kitu.
“Dola mia moja ni pesa ndogo sana kwa mwanaume anayejua nini maana ya
starehe” yule msichana akaniambia huku taratibu akiipeleka mdomoni ile sigara
iliyokuwa mkononi mwake na kuanza kuivuta pasipo kunitazama. Alipoitoa akageuka
na kutabasamu huku akiniambia
“Napenda sana wanaume weusi wenye nguvu na warefu kama wewe” msichana
yule mdogo akaongea na hapo nikaanza kuilaani dunia kwa namna ilivyoharibika
namna ile. Hata hivyo nilitabasamu kidogo kuununua urafiki.
“Kwa nini?” nilimuuliza huku nikitabasamu.
“Huwa wananiacha nikiwa nimeridhika” yule msichana akaongea kwa sauti ya
mahaba.
“Jina langu naitwa Stephen Masika!” nilivunja tena ukimya.
“Mimi naitwa Zera”
“Jina lako tamu sana masikioni mwangu” niliongea kwa utulivu huku nikimtazama
msichana yule.
“Mh! kila mwanamume anaongea hivyo utasema mmeambizana” yule msichana
akaongea hukua akiipeleka sigara yake mdomoni na kuivuta taratibu.
“Unatumia kilevi gani?” hatimaye akaniuliza baada yakuitoa ile sigara mdomoni.
“Oh! usijali mrembo kilevi kwa sasa hapana!”
“Kwa nini?” akaniuliza kwa mshangao kidogo.
“Nina dozi ya Malaria” nilimwambia huku nikitabasamu na hapo akazidi kunikata
jicho kwa mshangao.
“Sasa kama unaumwa malaria unafanya nini humu ndani?. Si ungeenda hospitali
ya Ocean Road,Muhimbili au TMJ badala ya kuja hapa?”
“Kwani wagonjwa hatuna haki ya kununua huduma hii?” nilimuuliza kwa utulivu
huku nikimtathmini vizuri msichana yule.
“Nenda kauguze ugonjwa kwanza usije ukanifia kitandani” yule msichana
akaongea kwa dhihaka na hapo nikaingiza mkono mfukoni na kutoa kibunda cha
shilingi laki moja na kumrushia pale kwenye lile beseni la kuogea. Yule msichana
ambaye sasa nilimfahamu kwa jina la Zera akakidaka kibunda kile cha pesa kama
mbwa mwenye njaa adakavyo mfupa aliorushiwa kisha akaanza kuzihesabu zile noti
chapuchapu kwa vidole vyake virefu kama mashine ya ATM huku ile sigara yake
akiwa ameibana kwenye pembe ya mdomo wake. Alipomaliza kuzihesabu zile noti
akageuka na kunitazama kwa shauku kama atarajiaye maelekezo juu ya zile pesa.
Alipoona kuwa nakawia kuongea akavunja ukimya
“Nimesema dola mia moja ya kimarekani siyo shilingi laki moja ya kitanzania?”
Zera akaongea huku akinitazama kwa udadisi.
“Vuta subira mrembo haraka ya nini?” nilimwambia yule msichana hata hivyo
hakusema neno badala yake nilimuona akianza kutoka kwenye lile beseni la kuogea
na mara hii mapigo yangu ya moyo yakasimama huku akili yangu ikishindwa kufanya
kazi kwa sekunde kadhaa.
Uzuri wake ama kwa hakika ulikuwa umefanikiwa kuzichukua mateka hisia zangu.
Pamoja na kuwa niliwahi kukutana na wasichana wengi warembo na wazuri katika
harakati zangu lakini Zera alikuwa ni matokeo ya kazi bora kabisa ya mfinyanzi.
Alikuwa mrefu lakini nilimzidi kwa sentimita chache za hisabati. Nywele zake
ndefu laini na nyeusi ziliteleza taratibu kutoka kwenye yale maji ya povu la sabuni
kama samaki aina ya kambare kwenye tope jepesi la udongo mfinyanzi. Niliendelea
kumkodolea macho Zera na hapo nikamuona akizikamua maji zile nywele zake kwa
viganja vya mikono yake katika namna ya kuzichuja maji kistaarabu.
Macho yake makubwa meupe na legevu yalizungumza kuwa alikuwa tayari kwa
kazi. Pua yake ndefu na nyembamba na midomo yake yenye kingo laini na pana
viliutanabaisha vizuri uzuri wa sura yake nyembamba kiasi yenye mvuto wa kipekee
kuwahi kutokea duniani.
Matiti yake yaliyosimama wima yenye chuchu nyeusi katikati yalitikisika kidogo
wakati alipokuwa akiutua mguu wake wenye kikuku sakafuni mara baada ya kutoka
kwenye lile beseni la kuogea huku akiwa uchi bila ya nguo yoyote ya kujisitiri maungoni
mwake.
Zera aliposimama mwili wangu ukashikwa na ganzi na akili yangu ikayumba na
kupoteza uelekeo kama bondia aliyeshambuliwa kwa pigo la konde la nguvu kichwani
kutoka kwa mpinzani wake. Kiuno chake chembamba chenye aina tofauti za shanga
kilikuwa kimechongwa vizuri kuushikilia mzingo wa makalio yake usiokinaisha
kuutazama. Kitovuni alikuwa ametoga kipini kimoja cha dhahabu. Niliendelea
kumkodolea macho na hapo nikayaona yale mapovu ya sabuni nzuri ya kunukia kutoka kwenye lile beseni la kuogea mle ndani yakichuruzika taratibu na kutengeneza
ziada nyingine katika uzuri wake wa kustaajabisha.
Mikono yake mirefu,laini na yenye kucha ndefu zenye rangi ya kuvutia aliipeleka
kiunoni mwake na kujishikashika kisha akajitikisha kidogo katika namna ya kuzidi
kuzitaabisha vibaya hisia zangu ambazo tayari zilikuwa mahututi.
Zera alipoanza kutembea taratibu akinifuata pale nilipokuwa nimeketi mitetemo
ya mapaja yake laini na mang’avu yenye misuli imara yakaupelekea ule mzigo wake wa
makalio makubwa na laini uanze kuweweseka kama mshumaa unaopulizwa na upepo
mkali wa baharini.
Taswira ile mbele yangu ikanipelekea nianze kuhisi kuwa nilikuwa nimepotea njia
na hatimaye kujitumbukiza kwenye kiumbe kile kilichohitimu vizuri katika kucheza
na hisia za wanaume.
Zera alitembea taratibu na hatimaye kuketi pembeni yangu. Nilipogeuka
kumtazama mkono wake mmoja tayari ulikuwa umepenya ndani ya fulana yangu na
kuanza kufanya ziara ya taratibu tumboni na kifuani mwangu. Tukio lile likanifanya
nijihisi kama niliyepigwa na shoti kali ya umeme. Muda mfupi badaye nikaanza kuhisi
kuwa endepo ningeendelea kuiruhusu hali ile basi mawasiliano ya ubongo na kazi za
viungo vyangu mwilini yangekatika. Hivyo nikajitahidi kujinasua kwa jitihada zangu
zote.
“Subiri kidogo mpenzi” nilinong’ona taratibu kando ya sikio lake hata hivyo Zera
hakutaka kunisikia badala yake akaendelea kunipapasa maungoni mwangu.
“Mpenzi…!” nilimuita huku nikifanya jitihada za kujinasua mikononi mwake bila
mafanikio. Kufumba na kufumbua ulimi wake laini ulikuwa kwenye tundu la sikio
langu huku ukisababisha kiwango kikubwa cha hisia kuwahi kunitokoea mwilini.
Sikutaka kuendelea kuiruhusu zaidi hali ile hivyo hatimaye nikaamua kutumia nguvu
katika kujinasua mikononi mwake. Jitihada zangu zikafua dafu kwani hatimaye
nikafanikiwa kumshinda shetani na vishawishi vyake.
Zera akaondoa mikono yake haraka maungoni mwangu na kunikata jicho lenye
chuki na hasira halafu akanisukuma kando kiasi kwamba kama nisingekuwa makini
ningeweza kupiga mwereka mbaya.
“Wewe ni mwandishi wa habari?” hatimaye Zera akaniuliza kwa hasira.
“Habari zipi mpya huyo mwandishi wa habari anaweza kuzitafuta humu ndani
bibie?” nilimuuliza Zera huku nikijitahidi kuurudisha urafiki wetu ulionza kuingia
nyufa.
“Sasa umefuata nini humu ndani?” Zera akaniuliza kwa jazba.
“Tafadhali! hebu keti kwanza unisikilize mpenzi” nilimwambia Zera ambaye
wakati huu alikuwa tayari amesimama kwa hasira huku akinikata jicho.
“Sitokurudishia pesa zako” hatimaye Zera akavunja ukimya baada ya kitambo
kirefu cha ukimya kupita mle ndani huku tukitazamana.
“Ondoa shaka!” nilimwambia na hapo Zera akanitazama kwa mshangao na kuketi
taratibu kando yangu.
“Zungumza shida yako” hatimaye akaniuliza kwa sauti tulivu ya upole.
“Nitachukua dakika chache za muda wako” nilimwambia huku nikigeuka na
kumtaza wakati huo mkono wangu ukifanya ziara fupi kwenye sehemu za mapaja
yake.
“Zungumza!” akaniambia huku akiendelea kunitazama na hapo nikaichukua
ile sigara mkononi mwake na kuivuta mapafu kadhaa kisha nikamrudishia huku
nikiupuliza moshi taratibu katika namna ya kuipa utulivu akili yangu kisha nikavunja
ukimya
“Nahitaji kuonana na Milla Cash bila shaka unaweza kunisaidia kumpata”
nilimwambia Zera huku nikimtazama usoni na nilichokiona machoni mwake ni
mshangao wa hali ya juu.
“Hicho ndiyo kilichokuleta humu ndani?” hatimaye Zera akaniuliza kwa utulivu
huku akiutikisa mguu wake uliokuwa juu ya mwingine huku macho yake yakitazama
mbali na eneo lile kama mtu anayetafakari kitu.
“Nahitaji msaada wako” nilimwambia kwa utulivu.
“Sasa utamuuliziaje Milla Cash wakati upo na mimi. Huoni kuwa unanivunjia
heshima?” Zera aliongea kwa hasira kidogo lakini sauti yake bado ilikuwa na utulivu na
hapo nikacheka moyoni huku nikijiuliza kahaba kama yule ni heshima gani aliyokuwa
akiizungumzia.
“Sina maana hiyo mpenzi” nilimwambia kwa utulivu.
“Unadhani Milla Cash ni msichana mzuri na mrembo zaidi yangu?” Zera akaniuliza
na swali lake likanifanya nifahamu kuwa alikuwa akihisi wivu kwa kumuulizia Milla
Cash na siyo yeye na hapo nikatabasamu kidogo
“Ungekuwa hujathubutu kuzigaragaza vibaya hisia zangu huwenda ningekubaliana
na maneno yako” nilimwambia huku nikiangua kicheko hafifu cha kirafiki.
Zera akatabasamu kidogo huku akiipeleka sigara yake mdomoni. Nilipomtazama
usoni nikagundua kuwa maneno yangu yalikuwa yameukosha vizuri moyo wake.
Nijuavyo mimi ni kuwa ukitaka mwanamke akusikilize basi anza kwa kumsifia juu ya
uzuri wake lakini Zera alistahili sifa.
“Nina shida naye binafsi”hatimaye niliongea kwa utulivu
“Shida gani?”
“Binafsi”
“Sasa si ungemuulizia kule mapokezi badala ya kuja kwangu?”
“Nilihisi kuwa huwenda nisingepata ushirikiano wa kutosha” nilimwambia Zera
huku nikimtazama usoni.
“Wewe ni Njagu?” Zera aliniuliza kwa utulivu huku akigeuka na kunitazama na
hapo nikajua kuwa alitaka kufahamu kama mimi nilikuwa askari polisi au lah!
“Kwanini unaniuliza hivyo?” nilimuuliza kwa udadisi.
“Unaonekana kama polisi na sisi humu ndani polisi hatuwataki” maneno ya Zera
yakawa yamenivuta na hapo nikageuka na kumtazama kwa makini.
“Mimi siyo polisi lakini kwa nini hamuwapendi polisi na wakati wao ndiyo wanaolinda usalama wenu?” nilimuuliza Zera na hapo nikamuona akiupisha utulivu
kichwani mwake. Kitendo kile cha kuchelewa kunijibu kikanifanya nihisi kuwa
alikuwa akijipanga namna ya kukwepa kunieleza ukweli wa jambo fulani la mle ndani
ambalo mimi sikulifahamu.
“Polisi huwa wanatusumbua mara kwa mara wakidai biashara yetu ni kinyume na
sheria za nchi na wakati baadhi yao ni wateja wetu wa kuaminika”
Nilimsikiliza Zera pasipo kutia neno lolote badala yake nikatabasamu kidogo huku
nikifahamu fika kuwa lile halikuwa jibu sahihi la swali nililomuuliza huku mashaka
juu ya kilichokuwa kikiendelea ndani ya casino ile yakizidi kuniingia. Nilitulia kidogo
nikiikumbuka ile mifuko myeusi niliyowaona nayo wale watu mle ndani ya casino na
hapo akili yangu ikapoteza kabisa utulivu.
“Milla Cash yupo chumba namba ngapi humu ndani?” nilimtupia swali Zera
nikinuia kumrudisha kwenye msingi wa maongezi yetu. Zera aligeuka tena na
kunitazama kisha akaongea kwa utulivu baada ya kuitoa sigara mdomoni.
“Hakuna mtu yeyote miongoni mwetu anayefahamu. Humu ndani kuna idadi ya
vyumba vipatavyo sitini na nane na kila mmoja ana chumba chake kama unionavyo
mimi humu ndani na mbaya zaidi wengine hatufahamiani”
“Kwa nini msifahamiane?” nilimuuliza Zera kwa udadisi.
“Huwa tunaingia humu ndani kwa zamu. Kuna wanaoingia asubuhi saa mbili
asubuhi na kutoka saa mbili usiku na tupo wale tunaoingia saa mbili usiku na kutoka
saa mbili asubuhi ya siku inayofuata. Hivyo katika mazingira kama hayo unaweza
kuona mwenyewe kuwa ni kwa nini inakuwa vigumu kufahamiana miongoni mwetu”
Zera aliongea huku akiipeleka sigara yake mdomoni na hapo nikageuka na kumtazama
tena kwa udadisi. Kwa mara nyingine tena nafsi yangu ikajikuta ikiridhika kuwa Zera
alikuwa miongoni mwa wasichana wachache wazuri sana kawahi kuonekana kwenye
sayari hii. Niliupisha tena utulivu kichwani mwangu huku nikianza kuhisi ugumu wa
kazi iliyokuwa mbele yangu.
Wakati nikizama katika tafakuri ile mawazo juu ya yule mtu aliyenivamia kule
chooni yakaanza kuchipua upya katika fikra zangu huku nikijiuliza kuwa kwanini mtu
yule alitaka kuniua. Ina maana kuna watu waliokuwa wakifahamu sababu ya uwepo
wangu mle ndani?. Watu hao walifahamu vipi na nani aliyewaambia?. Nikaendelea
kujiuliza bila kupata majibu.
Nikajikuta nikizikumbuka pia sheria za casino ile kwenye kile kitabu kidogo
nilichopewa na yule binti asubuhi ile. Mojawapo ya sheria zile ni kuwa hakuna mtu
aliyekuwa akiruhusiwa kuingia na silaha mle ndani. Swali likabaki kuwa yule mtu
aliyenishambulia kule chooni aliwezaje kuingia na bastola humu ndani ya casino?.
Niliendelea kujiuliza bila kupata majibu huku mbele yangu nikihisi bado kulikuwa na
kiza kinene katika kuyapatia uvumbuzi maswali yangu.
Niliuinua mkono wangu na kuitazama saa yangu ya mkononi na hapo nikaridhika
na mwenendo wa majira yake. Baada ya muda mfupi ile maiti ya yule mtu kule chooni
ingeshtukiwa na sikutaka suala hilo litokee huku mimi nikiwa bado nipo mle ndani ya casino. Hivyo nikageuka kumtazama Zera kwa tabasamu langu la kichokozi.
“Wasichana wote wa humu ndani wanaofanya kazi kama yako huwekewa ulinzi
kama ilivyo kwa Milla Cash?” nilimuuliza Zera huku nikimtazama machoni. Zera
akanitazama kama anayefikiria jambo fulani na alipoitoa sigara mdomoni na kuupuliza
moshi pembeni akaongea kwa utulivu pasipo kunitazama.
“Hapana!”
“Wewe huwa unafikaje hapa casino?”
“Huwa tunapitiwa na basi dogo la hii casino kutoka majumbani mwetu tunapoishi”
Jibu la Zera likanifanya nimkumbuke Milla Cash na lile gari jeusi linalomleta
casino nyakati za usiku aina ya Texas Laghorn Tailgate Van na hapo hoja fulani ikaanza
kujengeka kichwani huku nikijiuliza ni kwa nini yeye peke yake ndiye aliyekuwa
akiletwa na gari lile pale casino. Bado jibu sikulipata hivyo nikayaacha mawazo yangu
yakielea hewani pasipo kupata mhimili mzuri wa hoja.
Nilipomtazama Zera pale pembeni yangu nikahisi kuwa huwenda alikuwa
akijiuliza maswali kadhaa juu ya uwepo wangu mle ndani.
“Unamuhitaji Milla Cash?” hatimaye Zera akaniuliza kwa utulivu huku macho
yake yakizitazama kuta za kile chumba.
“Ndiyo! nitafurahi sana endapo utanisaidia kuonana naye” nilimwambia Zera kwa
utulivu.
“Sifahamu mahali anapoishi hapa jijini Dar es Salaam hata hivyo bado ninaweza
kukusaidia mahali utakapoweza kuonana naye ingawa utalazimika kuwa na subira
kidogo” Zera alimaliza kuongea kisha akaipeleka sigara yake mdomoni. Niligeuka na
kumtazama Zera huku moyo wangu ukiwa umeanza kupata matumaini.
“Kweli?” nilimuuliza Zera kwa kutaka kuhakikisha maneno yake.
“Nakuahidi ondoa shaka kaka hata hivyo itabidi unilipe kwani ni kazi ya hatari“
Zera akaongea kwa msisitizo.
“Hatari iko wapi?” nilimuuliza Zera kwa shauku.
“Siwezi kukueleza chochote ila utakapofanikiwa kuonana na Milla Cash utamuuliza
swali hilo” Zera akaniambia kwa utulivu huku akionekana kutokuwa tayari kunieleza
chochote juu ya hatari hiyo nami sikutaka kumlazimisha.
“Utanitoza pesa kiasi gani?” hatimaye nikamuuliza
“Shilingi laki mbili” Zera akatamka haraka kama aliyekwisha kupanga kiwango
kile cha pesa hapo kabla.
“Usijali fanya kazi yangu pesa yako nitakulipa. Unadhani hadi lini utakuwa
umeikamilisha?” nilimuuliza Zera na baada ya kufikiria kidogo akanijibu.
“Mpaka kesho jioni kabla ya kuja hapa huwenda kazi yako tayari nikawa
nimeikamilisha”
“Nitafurahi sana” niliongea huku nikiingiza mkono mfukoni na kutoa kibunda
kingine cha pesa zenye thamani ya shilingi laki moja kisha nikampa Zera.
“Chukua pesa hii kama malipo ya awali ya kazi yangu” nikamwambia.
“Wala usihofu kazi yako nitaifanya” Zera akaniambia huku akizihesabu zile noti na alipomaliza akageuka na kunitazama
“Wapi tutakutana?” hatimaye akaniuliza.
“Hapa hapa kesho usiku muda na wakati kama huu” nilimwambia huku nikiumba
tabasamu.
“Hapana!” Zera akakataa na kunikazia macho
“Vipi kutakuwa na shida yoyote?” nilimuuliza Zera kwa mshangao.
“Hii ni sehemu ya kazi na kazi yako haihusiani na hapa” Zera akaniambia kwa
utulivu huku akinikata jicho la kunionya juu ya kuleta mazoea na kazi yake. Ukimya
ukapita kidogo huku nikiupisha utulivu kichwani mwangu kisha nikamuuliza tena
Zera.
“Mmiliki wa hii casino ni nani?”
Swali langu bila shaka lilimshangaza sana Zera na hapo akageuka na kunitazama
kabla ya kuangua kicheko cha kikahaba.
“Vipi unataka kuinunua?”
“Hapana! nilipenda tu kufahamu” nilimwambia Zera kwa utulivu huku
nikitabasamu.
“Hakuna anayemfahamu mmiliki wa casino hii kaka” Zera akaniambia huku
akiendelea kucheka na nilipoyatafakari maneno yake nikagundua kuwa alikuwa
akizungumza ukweli.
“Kwa hiyo tutakutana wapi?” Zera alipomaliza kucheka akaniuliza kwa utulivu.
Nilitulia kidogo nikifikiria juu ya sehemu ya kukutana halafu nilipokuwa mbioni kutoa
jibu ghafla nikapata wazo na hapo nikaichukua wallet yangu kutoka kwenye mfuko wa
suruali yangu na kuifungua. Nikatoa kadi ndogo ya biashara ama business card yenye
kila kitu feki kama;jina la kampuni,tovuti,barua pepe,jengo na mtaa wa kampuni hiyo
inapopatikana pamoja na nukushi isipokuwa namba ya simu tu ambayo ilikuwa mpya
kabisa ambapo nilimpa Zera.
“Utanipigia simu pale utakapokuwa umekamilisha kazi yangu” nilimwambia
Zera na hapo akaipokea ile kadi na kuitazama kwa makini huku wasifu wangu batili
wa mkurugenzi mkuu wa kampuni ya kukata na kusafisha madini ukiwa umeanza
kumzuzua. Zera alirudia kusoma wasifu wangu kwenye ile kadi huku akinitazama.
“Unaishi wapi hapa jijini Dar es Salaam?” nilimuuliza Zera.
“Naishi eneo la Kinondoni B mtaa wa Ukutavuka. Ukifika eneo la Biafra kituo cha
Kanisani unaingia upande wa kushoto ukiifuata barabara ya mtaa wa Bolingonanga halafu
mbele kidogo upande wa kushoto unaingia barabara ya mtaa wa Isere. Hutosafiri
sana na barabara ya mtaa huo mbele kidogo utakutana na barabara nyingine ya lami
inayoingia upande wa kulia kwako. Hiyo ndiyo barabara ya mtaa wa Ukutavuka.
Huwezi kupotea kwani kuna kibao cha barabara kinachoelekeza jina la mtaa huo.
Ukifika kwenye huo mtaa niulizie kwa jina la Zera utanipata kwani kila mtu wa mtaa
huo ananifahamu.
“Unaishi nyumba namba ngapi ya mtaa huo?” nilimkatisha Zera.
“Naishi nyumba namba 12 ina geti jekundu kwa mbele na ina tazamana na duka kubwa la madawa lenye jina la MM Pharmacy”
Mojawapo ya kigezo kilichotumika kunitunuku nishani ya juu ya masuala ya
upelelezi ni wepesi wa akili yangu katika kunasa na kuhifadhi taarifa za namna yoyote
kwa muda mrefu. Hivyo maelezo ya Zera nilikuwa nimeyanasa vyema kichwani.
Niligeuka na kumtazama Zera huku nikiyapapasa mapaja yake kisha nikatazama
muda kwenye saa yangu ya mkononi. Sikuwa na kitu kingine cha kufanya mle ndani
hivyo nikawa nimeamua kuondoka lakini wakati nikiwa kwenye hali ile mara simu
ya mezani iliyokuwa kule kwenye kile chumba cha awali ikaanza kuita. Mwito wa
simu ile ukamshuta Zera na hapo akageuka na kunitazama kwa mashaka kabla ya
kusimama haraka na kuelekea kule kwenye kile chumba kuipokea ile simu. Wasiwasi
niliouona machoni mwa Zera ukanisukuma na mimi kusimama na kumfuata Zera
kule kwenye kile chumba. Hivyo wakati Zera akiipokea ile simu mimi nilikuwa kando
yake nikimsikiliza.
“Haloo!” sauti ya upande wa pili iliita.
“Haloo nakusikia zungumza” Zera akaongea kwa utulivu huku akinitazama.
“Bila shaka naongea na chumba namba 26,sivyo?” ile sauti ya upande wa pili
iliuliza na niliweza kuihisi sauti ile kuwa ilikuwa ya kiume.
“Ndiyo chumba namba 26 hapa zungumza nakusikia” Zera akasisitiza.
“Kuna mwanaume yoyote chumbani kwako?” ile sauti ya upande wa pili iliuza tena
na niliweza kuisikia kwa mbali kutoka pale Zera aliposimama. Swali lile likamfanya
Zera ageuke na kunitazama kwa mashaka lakini niliwahi kumuonya kwa kumfanyia
ishara ya kukataa. Zera alikuwa mwepesi kunielewa.
“Hakuna mtu yoyote” hatimaye Zera akaongea kwa utulivu kwenye ile simu
“Una hakika?” ile sauti ya upande wa pili wa simu ikauliza kwa msisitizo
“Ndiyo! mteja wangu wa mwisho alikuwa ni yule mwarabu na naye ameshatoka”
“Okay! mwanaume yeyote atakayeingia chumbani kwako kuanzia sasa utanijulisha”
“Sawa!” Zera akaitikia kwa utulivu na ile simu upande wa pili ilipokatwa Zera
akairudisha mahala pake na hapo akageuka na kunitazama kwa wasiwasi.
“Mbona kama wanakuuliza wewe?” Zera akaniuliza huku uso wake ukionesha
mashaka,
“Bila shaka!” nikamjibu Zera huku nikifikiria uongo wa kumwambia utakao
karibiana na ukweli kwani endapo ningekataa kuwa siyo mimi niliyekuwa nikiuliziwa
kwenye ile simu Zera angeanza kuingiwa na mashaka na mimi.
“Sasa kwa nini ukanikataza nisiitikie?” Zera akaniuliza kwa mshangao.
“Kuna rafiki yangu nimekutana naye humu ndani sasa ananing’ang’ania na
anataka kunichomoa pesa ndiyo ikabidi nimtoroke nikamwambia kuwa nakuja huku
vyumbani kutafuta mrembo wa kustarehe naye. Sasa naona jamaa kapatwa na mashaka
baada ya kuona sipatikani kwenye simu kwani simu yangu nimeizima” niliongea huku
nikijichekesha mbele ya Zera katika namna ya kumzuga ingawa akilini nilishaanza
kuhisi kuwa huwenda ile maiti ya yule mtu kule chooni ilikwisha gundulika.
“Kama ni hivyo basi una haki ya kumkimbia” Zera akaongea kwa utulivu na nilipomtazama usoni nikafurahi kuwa angalau nilikuwa nimefanikiwa kumlainisha
hata hivyo sikutaka kuendelea kukaa mle ndani. Huku nikifahamu kuwa baada ya
muda mfupi polisi wangefika pale kwenye casino na kuanza uchunguzi wao nikaamua
kuagana na Zera kisha nikaelekea mlangoni ambapo niliufungua na kutoka nje.
Nilikuwa nimejiandaa kwa hali yoyote hivyo mara tu nilipotoka nje ya kile chumba
cha Zera niliigeuza kofia yangu nyuma kisha nikachukua miwani mfukoni na kuivaa
huku nikiharakisha kuelekea kwenye zile ngazi za kushukua ukumbi wa chini wa
casino. Lakini kabla sijashuka nilitazama kule chini kwenye ule ukumbi wa casino na hali
ya mambo haikuniruhusu kutimiza adhma yangu.
Watu wote mle ukumbini walikuwa wakielekea kule nyuma kwenye lile eneo la
maliwato ya casino na baadhi ya wanawake walikuwa wakilia. Nikajua ile maiti ya mtu
niliyepambana naye kule chooni ilikuwa tayari imegundulika na baadhi ya mabaunsa
wa casino ile walikuwa wakihaha haku na kule kumtafuta mtu aliyehusika na mauaji
yale.
Sikushuka tena kule chini ya ule ukumbi wa casino na badala yake nikashika uelekeo
wa kule nilikotoka nikitafuta njia nyingine mbadala ya kutokea nje ya jengo lile pasipo
kupitia kwenye ule mlango mkubwa wa mbele wa ile casino. Nilitembea kwa haraka
huku macho yangu yakizunguka huku na kule kutafuta sehemu ya kutokea.
Hatimaye nikakutana na milango miwili iliyokuwa upande wa kulia. Nilipoichunguza
milango ile nikagundua kuwa ilikuwa ni milango ya vyoo kama vile vya ule ukumbi wa
chini. Choo cha kiume na cha kike. Bila kupoteza muda nikaufungua ule mlango wa
choo cha kiume na kuzama ndani. Mandhari ya mle ndani hayakutofautiana kabisa na
vile vyoo vya kule chini kwenye ule ukumbi wa casino.
Nikaanza kuzunguka mle ndani nikitafuta sehemu ya kutokea nje lakini nilishindwa
kwani mle ndani hapakuwa na upenyo wa namna yoyote na kila sehemu ilikuwa
imezibwa kwa kuta nene. Sehemu ya juu ya dari ya kile choo ilikuwa imefunikwa kwa
ukuta wa zege kwa ajili ya sakafu ya ghorofa inayofuata. Nikiwa nimeridhika kuwa
nisingeweza kuitimiza adhma yangu ya kutoka nje ya lile jengo la casino kwa kupitia
mle ndani sikutaka kupoteza muda mle ndani. hivyo nikafungua mlango wa kile choo
na kutoka nje.
Mara tu nilipotoka nje ya kile choo nikawaona wanaume wawili mabaunsa wa
ile casino wakija upande wangu. Sikutaka wale mabaunsa wanifikie hivyo nikashika
uelekeo wa upande wa kushoto nikiharakisha kwenda mbele huku macho yangu
yakitazama huku na kule nikiendelea kutafuta sehemu ya kutokea. Hata hivyo kabla
sijafanikiwa wale mabaunsa walikwishanifikia na kunitahadharisha.
“Oyaa! braza hebu simama” baunsa mmoja alinionya hata hivyo niliendelea na
safari yangu huku nikijidai sijamsikia.
“Oyaa! vipi unajidai hutusikii au ndiyo unaleta kiburi?” mwenzake akasisitiza.
Haraka nikatazama kule mbele yangu na bado sikuona matumaini ya kutoka mle
ndani kwa hila hivyo ikanibidi nipunguze mwendo na kugeuka nyuma.
“Vipi mnaniongelesha mimi?” niligeuka na kuwauliza.
“Sasa unadhani tunamwambia nani mwingine kama siyo wewe!” mmoja akafoka
huku akiongeza hatua zake kunikaribia.
“Mimi siitwi wewe bwana hebu tumieni majina ya heshima basi” niliwaambia wale
mabaunsa huku nikizipima vizuri hatua zao kadiri walivyokuwa wakizidi kunikaribia.
“Huku unaelekea wapi?” mmoja aliniuliza pindi waliponifikia.
“Kwani nyinyi mnaenda wapi?” nikawarudishia lile swali.
“Oyaa mbona unajitia kiburi hebu jibu ulivyoulizwa” mwenzake akadakia huku
akizidi kunisogelea.
“Mna shida gani na mimi hadi mniulize mahali ninapoelekea wakati mnaniona
bado nipo humu ndani ya casino?” niliwauliza huku nikawatazama wale mabaunsa.
Miili yao ilikuwa mikubwa iliyotuna na yenye misuli iliyokaza na kugawanyika vizuri
kwa mazoezi makali yenye ratiba inayozingatiwa vizuri. Nguo walizovaa;fulana nyeupe
na suruali nyeusi za jeans hazikufanikiwa kuificha miili yao.
“Geuka nyuma na tunaenda na wewe” baunsa mmoja alinionya baada ya
uvumilivu wake kuonekana kufika kikomo na hapo kwa pamoja nikaanza kuwaona
wakinisogelea pale niliposimama.
”Niende wapi na nyinyi kwani mmekuja na mimi humu ndani?” niliwauliza kwa
jazba za kuchelewesha na hapo baunsa mmoja akawahi kunishika kwa nyuma na
kunikwida na kutokana na ukubwa wa mwili wake nikawa nimeenea vizuri kwenye
kabari matata ya mkono wake wenye nguvu.
“Mnanipeleka wapi nyie mabwege?” niliwauliza kwa hasira huku nikijitahidi
kufurukuta.
“Agh! sisi mabwege siyo eh! basi subiri uone kazi yetu” yule baunsa aliyenikwida
akaongea kwa hasira huku akizidi kunibana kwa nguvu kisha akamwambia mwenzake.
“Oyaa! Kibusta atatusumbua sana huyu fala hebu mlegeze kidogo”
Sikuelewa maana ya maneno yale hadi pale nilipoziona ngumi mbili za nguvu na za
chapuchapu zikitua tumboni mwangu na kunisababishia maumivu makali yasiyoweza
kusimulika huku nikianza kuhisi kichefuchefu. Tumbo lango lilikuwa limekorogeka
vibaya na kwa mbali ladha chungu ya nyongo ikaanza kutembea kwenye ulimi wangu
na hapo nikaanza kuifikiria roho yangu.
Ngumi nyingine zilipotupwa niliikaza vizuri misuli ya tumbo langu kukabiliana
na maumivu yake hata hivyo kuendelea kuruhusu kichapo cha namna ile tumboni
nilitambua kuwa kingezidi kuidhoofisha afya yangu. Hivyo nilikusanya nguvu za
kutosha kisha nikajipinda na kumtandika kichwa cha nguvu yule baunsa aliyenishika
nyuma yangu na hapo nikasikia kelele za yowe kali la maumivu. Yule baunsa akaniachia
mwenyewe bila kupenda. Kile kichwa nilichomtandika kilikuwa kimeupasua na
kuusaga vibaya mwamba wa pua yake huku sehemu ya mbele ya mdomo wake
ikichanika na kuvuja damu. Wale mabaunsa walikuwa na nguvu za ajabu lakini
walikuwa hawafahamu mbinu za mapigano hivyo hawakuweza kufua dafu mbele
yangu.
Wakati yule baunsa mwingine niliyemtandika kichwa akijishika usoni kuugulia maumivu yule mwenzake akasogea haraka kunikabili huku akirusha ngumi moja
ambayo niliiona mapema nikainama kidogo na kuikwepa kisha nikamtandika ngumi
moja ya nguvu mbavuni. Yule baunsa akapiga yowe kali la maumivu na kubweka kama
mbwa na kabla hajatulia vizuri nikamsindikiza na teke zito la mgongoni lililompekea
ajibamize vibaya kwenye ukuta wa ile korido na hapo tusi zito likamponyoka. Alipotaka
kugeuka nikamzaba ngumi kavu mbili za shingo zilizompotezea mawasiliano na
ubongo na hapo akaangua chini na kutulia.
Yule mwenzake niliyekuwa nimemtandika kichwa pale awali akaanza kunifuata
kwa hasira. Aliponifikia akarusha teke lakini nilikua makini kuishtukia dhamira yake
hivyo nikawahi kujitupa pale chini huku nikiliacha lile teke lake likikata hewa bila
mafanikio. Ilikuwa nafasi nzuri kwangu hivyo nikajizungusha na kumchota mtama
wa aina yake na hapo yule baunsa akapaa hewani mzobemzobe alipotua chini akatulia
kimya huku fahamu zikiwa mbali na nafsi yake.
Nikayumbayumba hadi pale nilipopata mhimili mzuri wa ukuta wa ile korido na
hapo nikajiegemeza huku nikihema ovyo kuirudisha pumzi mwilini mwangu. Yale
madubwana mawili yalikuwa yamelala pale chini sakafuni huku yakiwa hayajitambui.
Nikiwa bado nimeegemea ule ukuta huku nikiendelea kuhema ovyo mara nikasikia
sauti ya hatua za mtu mwingine akija upande ule. Sikutaka kusubiri hivyo nikaanza
tena kuharakisha nikielekea kule mbele ya ile korido ingawa sikuweza kufahamu kuwa
nilikuwa nikielekea wapi. Hatimaye bahati ikaangukia kwangu kwani mbele kidogo ya
korido ile upande wa kulia nikaziona ngazi nyembamba zinazoelekea sehemu ya juu
ya lile jengo la casino. Chini ya ngazi zile kulikuwa na mlango mdogo kwenye chumba
kidogo kisichoeleweka ujenzi wake. Ingawa sikuwa na utaalam wowote katika masuala
ya ujenzi lakini kuiona sehemu ile nikakumbuka kitu.
Kilikuwa chumba kidogo chenye Mainswitch ya umeme wa lile jengo lote la
casino. Ufundi umeme ulikuwa miongoni mwa fani zangu hivyo niliufungua ule
mlango mdogo wa kile chumba kisha nikaanza kufanya utundu wangu. Kufumba na
kufumbua jengo lote la ile casino likagubikwa na giza zito na hapo kazi iliyosalia ikawa
rahisi sana kwangu.
Haraka nikarudi kule chini kwenye ule ukumbi wa casino na kwa kuwa hakuna
mtu yeyote aliyeweza kuniona kutokana na giza la mle ndani hivyo ikawa rahisi sana
kwangu kujichanganya kwenye kundi kubwa la watu waliokuwa wakikimbilia mlango
wa kutokea nje ya ile casino huku wengi wao wakiwa ni wanawake waliokuwa wakipiga
makelele ya hofu.
Kwa uzoefu niliokuwanao nilifahamu fika kuwa jengo kama lile lisingekosa
jenereta kubwa la kusambaza umeme pale inapotekea kuwa ule umeme wa gridi ya
taifa umekatika. Hata hivyo nilikuwa na hakika kuwa kutokana na ukorofi niliyoufanya
kwenye kile chumba cha umeme wa jengo lile la casino hata jenereta hilo lisingeweza
kufua dafu.
Hapakuwa na namna ya kuwazuia watu wasitoke nje ya lile jengo la casino kwa
kuzingatia kuwa usalama wa watu lilikuwa zingatio la kwanza katika biashara za namna ile. Hivyo nikajichanganya katika kundi lile kubwa la watu waliokuwa wakikimbia
ovyo kwenda nje huku tabasamu maridhawa likifanya ziara usoni mwangu.
Kitu kilichozidi kuwachanganya watu ni kuwa majengo yote ya jirani na lile jengo
la ile casino yalikuwa na umeme. Hali ile ikampelekea kila mmoja aanze kuongea lake.
Baadhi ya watu niliwasikia wakiwashuku magaidia kuwa walikuwa wakihusika na
lile tukio la kifo cha yule mtu kwenye ile casino na baadaye kukatika kwa umeme.
Wengine nikawasikia wakiilaani miundo mbinu ya umeme wa jengo lile kuwa ilikuwa
mibovu tangu siku nyingi bila kubadilishwa.
Wengine nikawasikia wakidai kuwa umeme wa lile jengo la casino ulikuwa
umezimwa makusudi ili kufanikisha mpango wa mauji ya watu uliyoanza kutekelezwa
mle ndani. Ili mradi kila mtu alikuwa huru kuzungumza vile alivyojisikia lakini ukweli
wa mambo niliufahamu mimi.
Nje ya lile jengo la casino kila mtu aliharakisha kuliendea gari lake na wale wasiokuwa
na magari wao waliekea kwenye geti la kutokea nje ya eneo lile la casino kisha kila
mmoja akashika uelekeo wake.
Nililifikia gari langu nikafungua mlango na kuingia ndani kisha nikaipekua bastola
yangu na kuridhika kuwa bado ilikuwa kwenye maficho yake salama. Niliwaza kuwa
kuondoka kwangu eneo lile mapema kungeweza kutengeneza chanzo kizuri cha
upelelezi wa tukio lile la mauaji kwenye ile casino. Hivyo niliendelea kusubiri mle ndani
ya gari na baada ya magari manne kunitangulia kuondoka kwenye yale maegesho
na mimi ndiyo nikaunga mkia nyuma yao huku mche wa sigara ukiteketea taratibu
mdomoni mwangu.
Usiku ulikuwa mbioni kushamiri na kwa mbali manyunyu hafifu ya mvua yalianza
kuanguka kutoka angani nami nikayaondoa mbele yangu kwa kuwasha wiper za kioo
cha mbele cha gari langu. Mvua za masika bado zilikuwa zikiendelea kunyesha sehemu
mbalimbali za jiji la Dar es Salaam.
_____
MUDA MFUPI BAADAYE mafundi umeme kutoka kitengo cha dharura cha
shirika la umeme la Tanesco walikuwa ndani ya lile jengo la Vampire Casino wakifanya
kazi waliyoitiwa.
Kwa weledi wao na maarifa ya masuala ya umeme waliyokuwa nayo wakamtoa
hofu meneja wa casino ile mwanaume mrefu na mwembamba aliyeshindwa kabisa
kuitowesha hasira yake usoni tangu kugundulika kwa yale mauaji kule chooni na
hatimaye kukatika kwa umeme katika lile jengo la casino.
Mafundi wale wa umeme wakamuweka bayana meneja wa casino ile kwa kumueleza
kuwa tatizo lile la kukatika kwa umeme kwenye lile jengo la casino lilikuwa limetokana
na fyuzi chache muhimu zilizochomolewa kutoka kwenye Mainswitch iliyokuwa
ikisambaza umeme kwenye lile jengo la casino. Huku wakisisitiza kuwa hakukuwa na
uharibifu wowote uliokuwa umetokea katika miundo mbinu ya umeme wa lile jengo.
Hatimaye wakarudishia zile fyuzi na hapo umeme wa lile jengo ukawaka.
Wakati wale mafundi umeme wa kitengo cha dharura kutoka Tanesco wakiondoka
kwenye lile jengo la casino baada ya kukamilisha kazi yao mlangoni wakapishina na yule
mkuu wa kituo cha polisi cha mjini kati ASP O.J.Mkwaju Ngoma akiwa ameongozana
na askari wake watatu vijana wa kazi huku wote wakiwa wamevaa sare zao za polisi.
Taarifa za mtu aliyeuwawa katika choo cha Vampire Casino zilikuwa zimeifikia ofisi
yake kupitia simu ya mlinzi mmoja wa casino ambaye hakupenda kujitambulisha jina
lake. Askari wale walipoingia ndani ya casino wakafahamiana na baadhi ya uongozi wa
casino ile kisha wakaelekea moja kwa moja hadi kwenye eneo la tukio.
Kulikuwa na watu wachache waliosalia wakiitazama ile maiti ya yule mtu aliyeuwawa
kwenye kile choo cha casino. Miongoni mwa watu hao walikuwa ni wafanyakazi wa ile
casino ambao walikuwa wakimsikiliza kwa makini kijana mmoja ambaye alijinadi kuwa
yeye ndiye aliyekuwa shuhuda wa kwanza kulishtukia tukio lile la mauaji. Kijana yule
akaacha kusimulia mara baada ya kumuona ASP O.J.Mkwaju Ngoma akiingia eneo
lile huku ameongozana na askari wake.
“Poleni sana jamani!” ASP O.J.Mkwaju Ngoma akasimama na kuisalimia
kadamnasi ile.
“Tumeshapoa Afande” wote wakaitikia na hapo ASP O.J.Mkwaju Ngoma akaanza
kujitambulisha.
“Sisi ni askari tunaotokea kituo cha polisi cha mjini kati. Tafadhali! tunaomba
mtupishe kidogo tufanye kazi yetu. Hata hivyo tungeomba maelezo machache kama
kutakuwa na shuhuda yeyote mwenye taarifa za kutusaidia” ASP O.J.Mkwaju Ngoma
alimaliza kuongea kisha akachezesha sharubu zake na kujivika tabasamu la kirafiki.
Wale mashuhuda kuona vile wote wakageuka na kumtazama yule kijana aliyekuwa
mstari wa mbele akiwasimulia namna alivyokuwa wa kwanza kuishtukia ile maiti ya
yule mtu pale chooni na hiyo ikiwa ishara nzuri kwa ASP O.J.Mkwaju Ngoma kupata
kupata sehemu ya kuanzia mahojiano yake. Hivyo akageuka na kumtazana yule kijana
aliyekuwa akitazamwa na wale watu eneo lile huku akitengeneza tabasamu hafifu
usoni mwake.
“Ulikuwepo hapa wakati mauaji haya yalipofanyika?” ASP O.J.Mkwaju Ngoma
akauliza huku akimtazama kijana yule kwa makini.
“Sikuwepo ila nilikuwa shuhudua wa kwanza kuishtukia maiti hii” yule kijana
akaongea kwa kujiamini na hapo askari mmoja miongoni mwa wale watatu akasogea
na kuanza kuchukua maelezo yake.
“Nyinyi wengine mnaweza kwenda ili mtupe uhuru wa kufanya kazi yetu” ASP
O.J.Mkwaju Ngoma akawataka wale mashuhuda wengine waondoke eneo lile na
wakati wale watu wakiondoka akawaambia
“Naomba mtuitie na meneja wa hii casino”
Wakati wale mashuhuda wakitawanyika wale askari polisi wawili waliosalia
wao walikuwa wakishughulika na kuufungua ule mlango wa kile choo kwani wale
mashuhuda walikuwa wameitazama ile maiti ya yule mtu kwa kuchungulia kwa juu
kupitia choo cha jirani.Ule mlango ulipofunguka askari wote wakasogea karibu na kuitazama ile maiti
ya yule mtu. Kichwa cha ile maiti kilikuwa kimepasuka vibaya baada ya kubamizwa
kwenye sinki la choo cha mle ndani na hivyo kupelekea ubongo wake na damu nyingi
kutapakaa eneo lile huku mguu na mkono wake mmoja ukiwa umevunjika.
“Jina lako?” ASP O.J.Mkwaju Ngoma akamuuliza yule kijana huku yule askari
wake pembeni akiendelea kuchukua yale maelezo. Baada ya yule kijana kujitambulisha
mahojiano yakaendelea.
“Wewe ni mteja au mfanyakazi wa hii casino?”
“Mfanyakazi”
“Kazi yako?”
“Kusafisha vyoo vya hii casino” yule kijana akaendelea kutoa maelezo huku akianza
kuingiwa na woga wa kuhojiwa na polisi.
“Ilikuwa majira ya saa ngapi wakati ulipoishtukia maiti ya huyu mtu?”
“Kati ya saa tatu na nusu na saa nne kasoro usiku huu”
“Ilikuwaje?” ASP O.J.Mkwaju Ngoma akamuuliza yule kijana huku akimkazia
macho.
“Mimi kazi yangu ni kusafisha vyoo vyote vya hii casino hivyo mara kwa mara huwa
napita kufanya usafi. Sasa wakati naingia humu ndani kusafisha ndiyo nikashtuka
baada ya kuona damu nyingi ikitoka na kusambaa chini ya huu mlango wa choo” yule
kijana akamaliza kuongea huku akizitazama nyuso za wale askari.
“Sasa ulihisi nini baada ya kuiona hii damu?” ASP O.J.Mkwaju Ngoma akamuuliza
yule kijana huku akiyapeleka macho yake tena kuitazama ile maiti.
“Nilihisi jambo la hatari ndiyo nikatoka kwenda kuwaita wenzangu” yule kijana
akajibu kwa woga.
“Relax kijana wangu!” ASP O.J.Mkwaju Ngoma akamwambia yule kijana huku
akimpigapiga mabegani baada ya kumuona akianza kuongea kwa woga.
“Wakati ukiingia humu ndani hukumkuta au kupishana na mtu yeyote akitoka?”
“Hapana!”
ASP O.J.Mkwaju Ngoma akamtazama tena yule kijana kwa uyakinifu kisha
akayahamisha macho yake tena kuitazama ile maiti ya yule mtu pale chini kabla ya
kuuliza tena.
“Hiki choo ni kibovu?”
“Hapana!” yule kijana akajibu kwa kujiamini.
“Una hakika?”
“Kabisa!,humu ndani ya hii casino hatuna choo kibovu na kama kingekuwepo
ningekuwa tayari nimekiripoti kwenye uongozi”
“Sasa nani aliyeandika hapa kuwa CHOO HIKI HAKITUMIKI?”
“Hata mimi pia nashangaa” yule kijana akaongea huku akionesha kutofahamu
kabisa kilichokuwa kikiendelea juu ya maelezo yake kwenye ule mlango wa kile choo.
Kikafuatia kitambo kifupi cha ukimya huku yule askari mwingine akiendelea kuandika
maelezo ya kile walichokishuhudia pale chooni.Baada ya hapo kukafuatiwa na mahojiano mengine ya hapa na pale kisha yule
kijana akaruhusiwa aondoke ili akaendelee na kazi zake huku akisisitizwa kuwa awe
tayati kutoa ushirikiano kwa polisi pale atakapohitajika kufanya hivyo. Yule kijana
akaondoka.
Muda mfupi baada ya yule kijana kuondoka eneo lile ASP O.J.Mkwanju Ngoma
na vijana wake wakaanza kazi ya kuchukua vipimo vyote muhimu vya upelelezi eneo
lile.
Wakati ASP O.J.Mkwanju Ngoma na askari wake wakiwa wanaendelea na kazi
yao meneja wa casino ile akawa tayari amefika eneo lile huku akiwa ameongozana na
vijana watatu ambao miongoni mwao ASP O.J.Mkwaju Ngoma alimtambua mmoja.
Akajiuliza ni wapi alikutana na kijana yule na baada ya kufikiri kwa muda akakumbuka
na hapo mshangao ukamshika. Hata hivyo akajitahidi kuumeza mshtuko wake.
“Habari za kazi Afande?” mtu mmoja miongoni mwa wale watu wanne akamsalimia
ASP O.J.Mkwaju Ngoma huku uso wake ukishindwa kuonesha tashwishwi yoyote.
“Nzuri! wewe ndiye meneja wa hii casino?” ASP O.J.Mkwaju Ngoma akauliza
huku akimtazama yule mtu.
“Ndiyo!”
“Nahitaji kufanya mahojiano na wewe kufuatia hili tukio la mauaji” ASP
O.J.Mkwaju Ngoma akaongea kwa utulivu huku akimtazama meneja wa ile
casino,manaume mrefu na mweusi mwenye umri wa miaka arobaini na ushei.
“Mimi siyo msemaji wa hii casino” yule meneja wa casino akaongea huku akionekana
kukasirishwa na uwepo wa askari eneo lile.
“Wewe si ndiye meneja wa hii casino?” ASP akauliza huku akishindwa kumuelewa
vizuri yule mtu.
“Ndiyo! lakini kuzungumzia masuala ya hapa siyo kazi yangu” yule mtu akasisitiza
kwa kiswahili chake chenye kasoro na hapo ASP O.J.Mkwaju Ngoma akatulia kidogo
akimtazama yule mtu katika namna ya kushangazwa na maelezo yake.
“Sasa msemaji wa hii casino ni nani?” ASP O.J.Mkwaju Ngoma hatimaye akauliza
kwa udadisi.
“Yupo likizo!”
Jibu la mkato la yule meneja wa casino likazidi kumchanganya ASP O.J.Mkwaju
Ngoma na wale askari wake na hapo wakatazamana kwa muda huku ukimya ukichukua
nafasi. Ukimya ule ulipokuwa mbioni kushika hatamu kijana mmoja miongoni mwa
wale vijana watatu waliofika eneo lile huku wakiwa wameongozana na yule meneja wa
casino akavunja ukimya huku akipiga hatua kusogea mbele
“Mzee unanikumbuka?” yule kijana akauliza huku akitabasamu na ASP
O.J.Mkwaju Ngoma alipomtazama haraka akamkumbuka vizuri yule kijana. Alikuwa
ni Fulgency Kassy,yule kijana aliyekuja ofisini kwake kule kituo cha polisi cha mjini
kati akiulizia taarifa za upelelezi za kifo cha Guzbert Kojo kilichotokea kule mtaa wa
Nkurumah siku ya jana. Vijana wengine wawili waliosalia mmoja alikuwa Pweza na
yule mwingine alikuwa Kombe.
“Ndiyo nakukumba” ASP O.J.Mkwaju Ngoma hatimaye akaongea huku akili
yake ikisumbuka kutafuta sababu ya swali lile.
“Naomba hilo faili lenu lenye maelezo halafu wachukue askari wako mwondoke
eneo hili kwani hii kesi haiwahusu” Fulgency Kassy akaongea huku usoni akitabasamu
na wenzake nao wakafanya vilevile huku mikono yao wakiwa wameikunjia vifuani
mwao. Hata hivyo yule meneja wa ile casino hakuonesha kushtushwa hata chembe na
yale maneno ya Fulgency Kassy,tukio ambalo liliwastaajabisha sana ASP O.J.Mkwaju
Ngoma na askari wake.
“Mnaonekana kuwa mna ajenda yenu binafsi,sivyo?”ASP O.J.Mkwaju Ngoma
akaongea kwa jazba huku akiwakata jicho la hasira wale vijana.
“Hupaswi kulalamika Afande hiki tunachokifanya ni kukurahisishia kazi wewe
na askari wako. Huoni kuwa umri wako haukuruhusu kujishughulisha na masuala
magumu kama haya!” Pweza akadakia.
“Nyinyi vijana hamna mamlaka yoyote ya kunielekeza kitu cha kufanya na
mkiendelea na hiyo tabia yenu ya kunifuatafuata nitawafahamisha kwanini nilipewa
jina la Mkwaju Ngoma” ASP O.J.Mkwaju Ngoma akafoka kwa hasira lakini wakati
akifanya hivyo Fulgency Kassy alikuwa akimalizia kibonyeza kitufe cha tarakimu ya
mwisho kwenye simu yake kisha akaiweka simu yake sikoni. Ile simu ilipopokelewa
upande wa pili Fulgency Kassy akaongea kidogo kabla ya kuitoa sikioni mwake na
kumpa ASP O.J.Mkwaju Ngoma huku akiendelea kutabasamu.
“Afande zungumza na huyu mtu badala ya kuendelea kushikilia msimamo wako
usiyo na maana” Fulgency Kassy akaongea kwa ujivuni na hapo ASP O.J.Mkwaju
Ngoma akaipokea ile simu na kuiweka sikioni na baada ya mazungumzo mafupi na
mtu wa upande wa pili wa ile simu akatoa ile simu sikioni na kuirudisha kwa Fulgency
Kassy huku uso wake ukiwa umetahayari. Kisha akameza funda kubwa la mate
kuitowesha hasira iliyonasa kwenye koo lake kabla ya kuwageukia wale askari wake
na kuwaambia.
“Twendeni” wale askari wakiwa wameshajiweka tayari kusubiri jibu la namna ile
wakaacha kile walichokuwa wakikifanya. Yule askari aliyekuwa akiandika yale maelezo
ya awali ya lile tukio la mauaji ya yule mtu akamkabidhi Fulgency Kassy lile faili lenye
maelezo kisha wale askari wote kwa pamoja wakaanza kuondoka huku wameinamisha
vichwa vyao chini kama kondoo.
Taarifa juu ya mauaji yalitokea kwenye kile choo cha Vampire Casino zilikuwa
zimewafikia Fulgnecy Kassy,Pweza na Kombe kutoka kwa afisa mmoja wa usalama
wa ngazi ya juu serikalini mara baada ya afisa huyo kupokea simu kutoka kwa meneja
wa casino.
Mara baada ya ASP O.J.Mkwaju Ngoma na wale askari wake kuondoka Fulgency
Kassy akageuka na kumtazama meneja wa casino ile kabla kumuuliza.
“Una mfahamu huyu mtu aliyeuwawa?”
“Ndiyo!” yule meneja akaitikia huku akionekana kuanza kuchoshwa na mchokato
wa matukio yote yaliyokuwa yakitokea mle ndani ya casino.
“Unamfahamu vipi?”
“Ni mmoja wa walinzi wangu wa hapa casino”
“Una sababu yoyote unayodhani huwenda ikawa imepelekea kifo chake?” Pweza
akauliza huku akiziokota bastola mbili juu ya dimbwi la damu mle chooni ambapo
alipoanza kuzikagua akagundua kuwa zote zilikuwa zimejaa risasi.
“Taarifa nilizozipata kwa walinzi wenzake wa humu ndani ni kuwa yeye alikuwa
akimfuatilia huyo mtu aliyemuua baada ya kumtilia mashaka mtu huyo wakati
alipoingia kwenye hii casino. Sasa sijafahamu kipi kilichotokea hadi mlinzi wangu
akauwawa” meneja wa casino akaongea kwa masikitiko.
Kombe akaisogelea ile maiti ya yule mlinzi na kuanza kuifanyia uchunguzi kwa
ukaribu na baada ya muda mfupi akaja na hoja.
“Yeyote aliyehusika katika kumuua huyu mlinzi ni mtu mzoefu katika mapambano”
“Kwa nini?” Fulgency Kassy akauliza huku akiyapeleka macho yake kuitazama ile
maiti ya yule mlinzi pale chini.
“Inavyoonekana ni kuwa kulitokea patashika ya mapambano makali baina ya huyu
mlinzi na huyo mtu aliyemuua lakini huyu mlinzi hakuweza kufua dafu kwa huyo
mtu ingawa huyu mlinzi anaonekana kuwa alikuwa na bastola mbili na zote zilikuwa
zimejaa risasi” Kombe akaongea huku akizigeuzageuza zile bastola na kuzikagua kwa
makini.
“Ni kweli anavyosema Kombe” Pweza akadakia ”Inavyooneakana ni kuwa huyu
mlinzi ndiye aliyemvamia huyo mtu aliyemuua lakini alishindwa kuitumia nafasi hiyo
vizuri”
Flugency Kassy akageuka na kumtazama yule meneja wa casino kabla ya kumuuliza.
“Huwa mna utaratibu kuweka kumbukumbu za watu wote wanaoingia kwenye
hii casino?”
”Ndiyo!,mtu hawezi kuingia humu ndani mpaka awe na kadi ya mwanachama wa
casino” yule meneja akafafanua
“Nani aliyekueleza kuwa huyu mlinzi alikuwa akimfuatilia huyo mtu aliyepambana
naye hadi kufikia kuzidiwa na hatimaye kuuwawa?” Fulgency Kassy akaendelea
kuyaelekeza maswali yake kwa yule meneja wa casino.
“Nimeambiwa na mlinzi mwenzake”
“Tunaweza kuonana na huyo mlinzi?” Fulgency Kassy akauliza huku akimtazama
meneja yule kwa makini.
“Ondoa shaka!” meneja wa casino akaongea kisha akaichukua simu yake ya
kiganjani na kupiga namba fulani. Baada ya pale haukupita muda mrefu kijana
mwenye umri kati ya miaka ishirini na saba hadi thelathini akaingia mle ndani huku
akiwa ameongozana na mabaunsa wawili wenye sura za huzuni. Walikuwa ni wale
mabaunsa waliopambana na Chaz Siga kule kwenye ile korido ya ghorofa ya pili na
kuambulia kupigo kibaya hadi kupoteza fahamu.
Wale mabaunsa huku wakiwa wanaona aibu mara walipofika eneo lile wakaanza
kusimulia mkasa wote uliowapata juu ya yule mtu waliyepambana naye kule kwenye gorofa ya pili ya casino. Walipomaliza kusimulia Fulgency Kassy akageuka na
kumuuliza yule mlinzi mwingine aliyeitwa kutoa maelezo.
“Maelezo ya hawa wenzako juu ya huyo mtu waliyepambana naye yanawiana na
kile ulichotoka kutueleza?”
“Ndiyo!” yule mlinzi akaongea kwa unyonge
“Yupoje huyo mtu?” Pweza akadakia.
“Alikuwa mwanaume mrefu na mweusi mweupe mwenye mwili imara na alikuwa
amevaa suruali ya jeans na fulana nyeusi na kichwani alikuwa amevaa kofia” yule mlinzi
akafafanua.
“Atakuwa ndiye huyo huyo tu” Kombe akaongea kwa sauti tulivu.
“Unadhani ni kwa nini mlimtilia mashaka huyu mtu wakati alipokuwa akiingia
humu ndani ya casino?” Fulgency Kassy akamuuliza tena yule mlinzi.
“Alikuwa mgeni na alionekana kuchunguza mambo yaliyokuwa yakiendelea
humu ndani” maelezo ya yule mlinzi yakawapelekea wote wageuke na kumtazama
yule mlinzi kwa makini huku wakitafakari.
“Mnadhani ni kwa nini huyo mtu alipanda kule juu ghorofani?” Fulgency Kassy
akawatupia swali wale mabaunsa huku akiwatazama.
“Hatufahamu” wote wakaitikia
“Mimi nafikiri kitu cha kufanya hapa ni kupitia kamera zote za humu ndani na
hapo tutamfahamu huyo mtu ni nani” Pweza akasisitiza.
“Yes! hilo ni wazo zuri kwani kupitia kamera za humu ndani tunaweza kumuona
huyo mtu aliyehusika na haya mauaji” Fulgency Kassy akaongea akiunga mkono hoja
ya Pweza huku akionekana kufurahi na kabla yule meneja wa ile casino hajaondoka
eneo lile akawahi kumtahadharisha.
“Hakikisha hakuna mtu yeyote humu ndani atakayefungua mdomo wake
kuzungumza na waandishi wa habari kwani unafahamu madhara ya kufanya hivyo”
“Ondoa shaka!” meneja wa casino akaongea kwa utulivu kisha akafungua mlango
wa kile choo na kutoka nje huku akiwa ameongozana na wale walinzi wake.
Muda mfupi uliyofuata baada ya yule meneja wa casino kutoka Fulgency
Kassy,Pweza na Kombe walianza kuushughulikia mwili wa yule mlinzi wakichukua
vipimo ambavyo vingewasaidia katika uchunguzi wao. Zoezi lile lilipokamilika mwili
wa yule mlinzi wakautumbukiza ndani ya mfuko wa nailoni mkubwa na mweusi
uliokuwa na zipu ndefu. Kisha wakaisafisha ile damu iliyotapakaa pale chooni sakafuni
kama namna ya kuondoa vielelezo vyovyote kwa mtu au watu ambao wangefika eneo
lile baadaye.
Walipomaliza kazi yao majibu yaliyopatika kutoka kwenye kamera za mle ndani
na taarifa kutoka eneo la mapokezi la ile casino yalikuwa juu ya meza ya ofisi ya yule
meneja wa casino. Mshukiwa namba moja wa mauaji ya yule mtu kule chooni alikuwa
amefahamika kwa jina la Stephen Masika na hata uvaaji wake ulishabihiana na maelezo
ya walinzi wa mle ndani ya casino.
Baadhi ya kamera za ile casino zilionesha kuwa katika vipindi tofauti Stephen Masika alionekana akiwa amekaa eneo la kaunta huku akijipatia kinywaji. Kamera
hizo baadaye zilimuonesha akielekea kule sehemu ya maliwato ambapo yale mauaji
ndipo yalipokuwa yametokea.
Stephen Masika alipotoka kule sehemu ya maliwato akaonekana akipanda zile
ngazi za kule ghorofani na hatimaye kuingia chumba namba 26 ambapo humo
alikaa kwa muda na alipotoka akaonekana akipambana na wale walinzi wa casino na
hatimaye kuwadhibiti vizuri kwenye ile korido. Baada ya hapo mtu yule aliyejulikana
kwa jina la Stephen Masika haikufahamika alitoka vipi nje ya jengo lile la casino ingawa
hisia zilimuhusisha na kukatika kwa ule umeme mle ndani na huwenda alitoka kwa
kujichanganya na watu waliokuwa wakitoka nje ya casino muda mfupi baadaya ya ule
umeme kukatika.
“Nyinyi endeleeni na kazi yenu sisi tutajua nini cha kufanya” Fulgency Kassy
akamwambia meneja wa ile casino baada ya majadiliano ya hapa na pale kufika tamati
kisha wakasogeza viti vyao nyuma ya meza kubwa ya ofisini na kusimama wakiagana
na meneja wa casino ile kabla ya kutoka mle ndani. Muda mfupi baadaye walikuwa
ndani ya gari aina ya Landcruiser nyeupe na mwili wa yule mlinzi wakiupeleka mochwari
hospitali ya Muhimbili.