idawa
JF-Expert Member
- Jan 20, 2012
- 25,284
- 38,364
- Thread starter
-
- #81
SEHEMU YA KUMI NA TATU.
Pombe ikampalia Kikoti. Radio ilikuwa inasema, "Dk. Makete aligongwa kusudi nyuma ya Benki ya Wakulima. Gari lililomgonga ni Benzi jeupe, likiendeshwa na mtu alievaa koti au jaketi la kunguru. Zawadi ya milioni moja iliyochangwa na wafanyakazi wa hospitali itatolewa kwa yoyote atakaesababisha mtu huyo kukamatwa."
Kikoti akaanza kutetemeka. Kila kitu kilikuwa waziwazi. Yule bwana kulitazama gari lake upande wa mbele, kumuonyesha Isidori,kumpa koti lake la kunguru .....kila kitu.
Hata yale maneno aliyoyadaka - 'ajali ...faini..heshima.' yalidhibitisha kitu kimoja tu. Tajiri yake ndie aliyetaka kumwua Dk. Makete. Sasa afanyeje? Alijiuliza. Lazima apate ushauri. Akawatazama wenzake. Akasema, "Bob! Butu! Mmesikia ajali iliyotangazwa?"
"Ndiyo." Alijibu Bobu.
"Inasemekana Dk. Makete amegongwa kusudi."
"Mmesikia zawadi iliyotangazwa?"
"Ndiyo."
"Namfahamu aliemgonga Dk. Makete."
"Unaleta masihara?"
"Hapana. Ni kweli."
Butu akauliza kidharau. "Sasa unataka tukusaidie kuibeba hiyo milioni?"
"Kikoti!" Alisema Bob kwa sauti yake ya kisajini, "Unasema kweli au umelewa? Maana wisk hii si......"
"Naapa. Nasema kweli. Mtu huyo ndiye tajiri yangu. Ana Benzi jeupe. Alirudi nyumbani boneti na bampa vikiwa vimeharibika. Alivaa koti la kunguru. Akaligawa haraka sana."
Bob na Butu wakatazamana. Kisha Butu akamwambia Kikoti, "Unataka tukusaidie kuipata hiyo milioni? Utatumegea?
"Ndiyo."
"Subirini." Bob akainua mkono. Si ulisema tajiri yako ni kizito?"
"Ni kizito kwelikweli."
"Basi hii nafasi ambayo mtu hawezi kuipata mara mbili katika maisha yake."
"Bob, unazungumza nini?" Butu aliuliza.
"Huyo Makete anatuhusu nini sisi?"
"Bob, mbona sikuelewi!"
"Hii ni nafasi ya kuokota mamilioni, na sio kimilioni kimoja, tena cha kugawana watu watatu." Butu akatikisa kichwa. Akasema, "Naona unakuja na mawazo ya hatari Bob."
"Hatari gani. Toka lini kuukacha umaskini, ulofa, ikawa hatari? Eti Kikoti, huyo tajiri yako hawezi kutupa milioni tatu ili tufumbe mdomo?"
"Anaweza kutoa hata zaidi."
"Unaona?" Bob aliumuuliza Butu.
"Hapana, Bob, mimi simo.Tumefanya mengi ya kipuuzi, lakini hili litakuwa la kichizi." "Butu, utakuja juta. Utakufa bila kushika milioni mkononi mwako."
"Potelea mbali."
"Lakini....lakini...utatufichia siri yetu?"
"Sina ninachokijua. Na hivi naondoka. Nakuacheni mwendelee na mipango yenu."
*************************************
"Mama, Kassim Hashir ndiye nani?"
Walikuwa katika chumba cha mgonjwa. Bi mkubwa aliketi kwenye sofa, Bessy na Denny vitini. Bi mkubwa akashusha pumzi. Akasema "Denny, pengine babako amekosea."
"Umeshamwona akisema neno au akitenda jambo bila ya kuwa na uhakika nalo?"
"Basi tusubiri apate fahamu atakueleza mwenyewe ni nani huyo Kassim Hashir - iwapo ataamua kukueleza."
"Mama, hatuna muda. Huyo hayawani anaweza kuihama tena nchi na kutoweka."
"Yaani umeshapata habari zake!"
"Ndiyo, za kijuujuu. Polisi wana faili lake, na mwandishi mmoja aliwekwa kizuizini kwa kufuatilia kifo cha babake. Inasemekana alimwua. Huyo mwandishi amesema wewe na baba mnakijua kisa hicho. Ni kweli?"
Mama Denny akasita.
"Mama, ni kweli au si kweli?"
"Ni kweli."
"Ndicho kilichomfanya atake kumwua baba?"
"Sikioni kinahusika vipi." Bessy akaingilia, "Tueleze kisa hicho. Sisi tutaamua kama kina uhusiano na tukio la leo."
Baada ya kusita tena, mama Denny akawasimulia kisa hicho......
Wakati huo, zaidi ya robo karne iliyopita, hospitali hiyo ilikuwa ndogo tu. Dk. Makete na mama Denny walikuwa ndio kwanza waoane.
Siku hiyo kama kawaida yao, walikuwa sehemu ya wagonjwa wapya,machela ilipoletwa, ikifuatiwa na msichana wa miaka kumi na mbili, aliyekuwa analia. Wakati mama Denny anamfariji msichana huyo, Dk. Makete alilifunua blanketi akaitazama maiti. Ilikuwa ya mzee wa kati ya miaka hamsini na sitini. Shingo yake ilikuwa imevunjika.
Akaifunika tena na kusema, "Hakuna cha kufanya. Amesha kufa. Amevunjika shingo. Apelekwe chumba cha maiti."
Mama Denny akasema, Rey, unamfahamu marehemu?"
"Hapana. Ni nani?"
"Othman Hashir."
Dk. Makete akaifunua tena maiti na kuitizama sura. Akasema, "Oh, my God! Ndiye. Imekuwaje?"
Msichana akasema huku akiendelea kulia, "Amesukuma."
"Ni nani aliyemsukuma?"
"Kaka Kassim, alimsukuma ghorofani, akabiringika kwenye ngazi."
"My God! Lazima turipoti polisi."
Dk. Makete alipofika Kituo cha Kati, akawekwa benchi asuburi karibu saa nzima. Hatimaye akapelekwa kwenye ofisi ya afisa mmoja wa cheo cha juu.
"Ndiyo, Dk. Makete?" Hakuambiwa aketi. Akasema, "Nimekuja kutoa taarifa ya kifo cha Mzee Othman Hashir. Binti yake anasema kaka yake Kassim Hashir alimsukuma kusudi kwenye ngazi. Kifo kimesababishwa na kuvunjika shingo."
"Dk. Makete," Alisema afisa huyo wa polisi, "Unataka kuyatia maanani maneno ya mtoto mdogo? Nimeambiwa hafiki hata miaka minane."
"Ana zaidi ya miaka kumi."
"Oh, sawa. Tutafanya uchunguzi. Ila ningekushauri uzingatie zaidi kazi yako kuliko kujihusisha na mambo mengine, mambo yasiyokuhusu."
"Ni wajibu wangu kuripoti mauaji." Dk. Makete alisema.
"Sawa. Umesharipoti. Ni juu yetu kuamua kama ilikuwa ajali au mauaji kama unavyodai. Kwisha."
Cc Joharia chiko18 gspace
Pombe ikampalia Kikoti. Radio ilikuwa inasema, "Dk. Makete aligongwa kusudi nyuma ya Benki ya Wakulima. Gari lililomgonga ni Benzi jeupe, likiendeshwa na mtu alievaa koti au jaketi la kunguru. Zawadi ya milioni moja iliyochangwa na wafanyakazi wa hospitali itatolewa kwa yoyote atakaesababisha mtu huyo kukamatwa."
Kikoti akaanza kutetemeka. Kila kitu kilikuwa waziwazi. Yule bwana kulitazama gari lake upande wa mbele, kumuonyesha Isidori,kumpa koti lake la kunguru .....kila kitu.
Hata yale maneno aliyoyadaka - 'ajali ...faini..heshima.' yalidhibitisha kitu kimoja tu. Tajiri yake ndie aliyetaka kumwua Dk. Makete. Sasa afanyeje? Alijiuliza. Lazima apate ushauri. Akawatazama wenzake. Akasema, "Bob! Butu! Mmesikia ajali iliyotangazwa?"
"Ndiyo." Alijibu Bobu.
"Inasemekana Dk. Makete amegongwa kusudi."
"Mmesikia zawadi iliyotangazwa?"
"Ndiyo."
"Namfahamu aliemgonga Dk. Makete."
"Unaleta masihara?"
"Hapana. Ni kweli."
Butu akauliza kidharau. "Sasa unataka tukusaidie kuibeba hiyo milioni?"
"Kikoti!" Alisema Bob kwa sauti yake ya kisajini, "Unasema kweli au umelewa? Maana wisk hii si......"
"Naapa. Nasema kweli. Mtu huyo ndiye tajiri yangu. Ana Benzi jeupe. Alirudi nyumbani boneti na bampa vikiwa vimeharibika. Alivaa koti la kunguru. Akaligawa haraka sana."
Bob na Butu wakatazamana. Kisha Butu akamwambia Kikoti, "Unataka tukusaidie kuipata hiyo milioni? Utatumegea?
"Ndiyo."
"Subirini." Bob akainua mkono. Si ulisema tajiri yako ni kizito?"
"Ni kizito kwelikweli."
"Basi hii nafasi ambayo mtu hawezi kuipata mara mbili katika maisha yake."
"Bob, unazungumza nini?" Butu aliuliza.
"Huyo Makete anatuhusu nini sisi?"
"Bob, mbona sikuelewi!"
"Hii ni nafasi ya kuokota mamilioni, na sio kimilioni kimoja, tena cha kugawana watu watatu." Butu akatikisa kichwa. Akasema, "Naona unakuja na mawazo ya hatari Bob."
"Hatari gani. Toka lini kuukacha umaskini, ulofa, ikawa hatari? Eti Kikoti, huyo tajiri yako hawezi kutupa milioni tatu ili tufumbe mdomo?"
"Anaweza kutoa hata zaidi."
"Unaona?" Bob aliumuuliza Butu.
"Hapana, Bob, mimi simo.Tumefanya mengi ya kipuuzi, lakini hili litakuwa la kichizi." "Butu, utakuja juta. Utakufa bila kushika milioni mkononi mwako."
"Potelea mbali."
"Lakini....lakini...utatufichia siri yetu?"
"Sina ninachokijua. Na hivi naondoka. Nakuacheni mwendelee na mipango yenu."
*************************************
"Mama, Kassim Hashir ndiye nani?"
Walikuwa katika chumba cha mgonjwa. Bi mkubwa aliketi kwenye sofa, Bessy na Denny vitini. Bi mkubwa akashusha pumzi. Akasema "Denny, pengine babako amekosea."
"Umeshamwona akisema neno au akitenda jambo bila ya kuwa na uhakika nalo?"
"Basi tusubiri apate fahamu atakueleza mwenyewe ni nani huyo Kassim Hashir - iwapo ataamua kukueleza."
"Mama, hatuna muda. Huyo hayawani anaweza kuihama tena nchi na kutoweka."
"Yaani umeshapata habari zake!"
"Ndiyo, za kijuujuu. Polisi wana faili lake, na mwandishi mmoja aliwekwa kizuizini kwa kufuatilia kifo cha babake. Inasemekana alimwua. Huyo mwandishi amesema wewe na baba mnakijua kisa hicho. Ni kweli?"
Mama Denny akasita.
"Mama, ni kweli au si kweli?"
"Ni kweli."
"Ndicho kilichomfanya atake kumwua baba?"
"Sikioni kinahusika vipi." Bessy akaingilia, "Tueleze kisa hicho. Sisi tutaamua kama kina uhusiano na tukio la leo."
Baada ya kusita tena, mama Denny akawasimulia kisa hicho......
Wakati huo, zaidi ya robo karne iliyopita, hospitali hiyo ilikuwa ndogo tu. Dk. Makete na mama Denny walikuwa ndio kwanza waoane.
Siku hiyo kama kawaida yao, walikuwa sehemu ya wagonjwa wapya,machela ilipoletwa, ikifuatiwa na msichana wa miaka kumi na mbili, aliyekuwa analia. Wakati mama Denny anamfariji msichana huyo, Dk. Makete alilifunua blanketi akaitazama maiti. Ilikuwa ya mzee wa kati ya miaka hamsini na sitini. Shingo yake ilikuwa imevunjika.
Akaifunika tena na kusema, "Hakuna cha kufanya. Amesha kufa. Amevunjika shingo. Apelekwe chumba cha maiti."
Mama Denny akasema, Rey, unamfahamu marehemu?"
"Hapana. Ni nani?"
"Othman Hashir."
Dk. Makete akaifunua tena maiti na kuitizama sura. Akasema, "Oh, my God! Ndiye. Imekuwaje?"
Msichana akasema huku akiendelea kulia, "Amesukuma."
"Ni nani aliyemsukuma?"
"Kaka Kassim, alimsukuma ghorofani, akabiringika kwenye ngazi."
"My God! Lazima turipoti polisi."
Dk. Makete alipofika Kituo cha Kati, akawekwa benchi asuburi karibu saa nzima. Hatimaye akapelekwa kwenye ofisi ya afisa mmoja wa cheo cha juu.
"Ndiyo, Dk. Makete?" Hakuambiwa aketi. Akasema, "Nimekuja kutoa taarifa ya kifo cha Mzee Othman Hashir. Binti yake anasema kaka yake Kassim Hashir alimsukuma kusudi kwenye ngazi. Kifo kimesababishwa na kuvunjika shingo."
"Dk. Makete," Alisema afisa huyo wa polisi, "Unataka kuyatia maanani maneno ya mtoto mdogo? Nimeambiwa hafiki hata miaka minane."
"Ana zaidi ya miaka kumi."
"Oh, sawa. Tutafanya uchunguzi. Ila ningekushauri uzingatie zaidi kazi yako kuliko kujihusisha na mambo mengine, mambo yasiyokuhusu."
"Ni wajibu wangu kuripoti mauaji." Dk. Makete alisema.
"Sawa. Umesharipoti. Ni juu yetu kuamua kama ilikuwa ajali au mauaji kama unavyodai. Kwisha."
Cc Joharia chiko18 gspace
Last edited by a moderator: