Mangungo II
JF-Expert Member
- Jul 6, 2012
- 18,133
- 26,766
Eddy ganzel hahahaha
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
SEHEMU YA NNE
Kassimu aliliangalia Benzi likitoka nje ya geti kisha akageuza kichwa na kumtazama mtunza bustani. Alikuwa kama hatua arobaini mbali naye,akimwagilia miwaridi. Akajiuliza kama ameweza kusikia kuyasikia mazungumzo yao. Alizungumza kwa sauti ndogo kwa ajili yake. Akaamua asingeweza kumsikia. Akageuka na kuingia ndani.
Vyumba vyote vya kulala vya jumba hilo vilikuwa ghorofani. Sehemu kubwa ya chini ilikuwa ukumbi mkubwa uliopambwa vilivyo. Sakafu yote ilifunikwa na zulia. Upande mmoja ulitawaliwa na meza iliyozungukwa na viti kumi na viwili. Upande mwingine ulikuwa na TV na rafu za vitabu,mapambo na vinywaji, hasa vikali na aina kadhaa za mvinyo aghali toka ng'ambo. Hapa na pale palikuwa na seti za sofa na vimeza vifupi. Ngazi za kwenda ghorofani zilikuwa mkabala na mlango wa mbele.
Kassim alikwenda moja kwa moja kwenye rafu ya vinyaji. Akatoa chupa ya kinywaji kikali na kjitilia robo glasi. Akaimeza kwa mkupuo.
Kisha akaenda kwenye simu iliyokuwa pembeni. Baada ya kubonyeza namba atakazo na kujibiwa, akasema "Nipatie Bwana Kembo." Punde sauti upande wa pili akasema, " Kembo hapa." Kassim akatamka neno moja tu, "Vipi?"
"Ohh, Bwana Kessy! Nahitaji kukuona. Tuna tatizo."
"Na mimi pia nina tatizo."
"Tatizo gani?" Kembo aliuliza kwa mashakamashaka.
"Tuna watu karibu sehemu zote mhimu."
"Vizuri. Kuna mtu alifikwa na ajali ya gari nyuma ya Benki ya Wakulima muda mfupi uliopita. Nataka kujua ni nani mtu huyo na hali yake ikoje. Unaweza kufanya hivyo?"
"Hakuna lisilowezekana, Bwana Kessy. Hakuna lisilowezekana."
"Fanya hivyo halafu njoo unione,"
***********************
Bessy hakua mgeni na Dk. Beka, Daktari Mkuu wa hospitali kuu ya serikali. Tangu avishwe uinspekta mwaka mmoja na nusu nyuma, alikwisha kutana nae mara kadhaa,kuhusiana na kesi mbalimbali.
Kwa hiyo alipofika hapo hospitalini alikwenda moja kwa moja ofisini kwake. Akabisha na alipoambiwa aingie, akaufungua mlango na kuingia.
"Ohh, ni wewe Inspekta." Alisema Dk. Beka kwa suti yake tulivu na ya chini. Leo Bessy aliona,ilikuwa ya chini zaidi - ya huzuni.
Akasema, "Ni kuhusu Dk. Makete." Naye pia alitumia sauti ndogo. Dk.Beka akaitikia kwa kichwa. akaivua miwani yake na kuyafikicha macho yake machovu.
"Ikoje hali yake?" Bessy aliuliza,akiketi na kukitoa kijitabu chake.
"Nasikitika kusema si nzuri. Bado yuko thieta anashughulikiwa na wataalamu wa hali ya juu."
"Uko uwezekano wake wa kuishi?"
"Kitu kama hamsini kwa hamsini,"
Bessy alikwishaizoea kauli hiyo. Dk. Beka hakupenda kumkatisha mtu tamaa,hata kama alijua kuwa mgonjwa huyo asingetoka thieta akiwa hai.
Akauliza, "Aliwai kurudiwa na fahamu?"
"Alizinduka thieta kwa nukta chache tu kabla ya ganzi kumkolea sawasawa."
"Aliwai kusema lolote lile katika nukta hizo chache?" Bessy aliuliza kwa matumaini kalamu ikisubiri mdomoni.
"Alisema maneno machache. Lakini hakusikika vizuri. Alikuwa kama anaeota - anaeweweseka. Sauti yake ilikuwa ya chini sana, na maneno hayakuwa ya kuleta maana. Nilichoweza kukidaka ni maneno mawili tu - kama tutayaita maneno - 'kassi hashi.' Aliyarudia maneno hayo mara mbili tatu."
Baada ya kuyaandika maneno hayo,Bessy akasema kwa sauti ya mkazo , "Dk. Beka, lazima nizungumze na Dk. Maketemapema iwezekanavyo - kabla....kabla mambo hayajawa mabaya zaidi. Dk. Makete aligongwa kusudi. Na kwa bahati mbaya hakuna aliewai kuzisoma namba za gari."
"Una maana haikuwa ajali ya kawaida?" Dk. Beka aliuliza kwa mshangao wa kutoamini.
"Hapana! Lilikuwa jaribio la kuua!" Sauti ya Bessy ilikuwa imepanda. Akavuta pumzi na kuendelea kwa sauti ya kawaida. "Nadhani Dk. Makete anamfahamu mtu aliemgonga. Na sababu yake. Huwezi kumgonga mtu kusudi bila sababu."
" Una uhakika haikuwa ajali? Madereva wengi wanapomgonga mtu...."
"Najua. Hukimbia. Hukimbilia polisi kujisalimisha. Lakini huyu hakufanya hivyo. Zaidi ya masaa mawili sasa yameshapita. Nina hakika hata jisalimisha. Isitoshe, uchochoro aliogongewa Dk. Makete hautumiwi na magari, na kama kuna gari litapita, basi si kwa kasi ya kuweza kusababisha ajali.
Dk. Beka akatikisa kichwa kwa majonzi.
Inspekta Bessy akaendelea, "Isitoshe tuna ushahidi. Ingawa kichochoro kile - kichochoro cha Benki ya Wakulima - hakina pilika za watu. Tumebahatika kupata watu wawili walioshuhudia tukio hilo. Wote wanaelekea kuwa watu wa kuaminika. Wote wapo tayari kuapa kuwa Dk.Makete aligongwa kusudi."
Dk. Beka alifumbua mdomo ili aseme neno lakini akabadili mawazo na kuufumba
Bessy akaendelea, "Mashahidi hao wanatoa sababu mbili. Kwanza. Dk Makete hakuwa katikati ya njia. Alikuwa pembeni. Alifuatwa. Pili, gari lililomgonga lilimnyemelea. Liliongezwa mwendo ghafla lilipomkaribia. Mmoja kati ya mashahidi hao aliwai hata kuguta. Hakumbuki alisema kitu gani. Bila ya shaka kitu kama 'Hey...! au 'Wewee...!' Hajui kama alikuwa anamkemea yule dereva au anamtahadharisha Dk. Makete. Anasema alikuwa katika mshituko wa kuruka akili. Ndiyo maana hakuweza kuzisoma namba za gari."
Dk.Beka akatikisa tena kichwa. Akasema, "Nashindwa kuamini."
"Amini usiamini, hivyo ndivyo mambo yalivyo. Dk. Makete amegongwa kusudi."
"Hukunielewa. Nina maana....." Beka alitafuta maneno ya kumalizia sentesi yake lakini hakuyapata. Akasema, "Namfahamu Dk. Makete vizuri sana. Nimefanya nae kazi kwa zaidi ya miaka ishirini. Miaka kumi nikiwa msaidizi wake mkuu. Ni rafiki yangu mkubwa. Tumekuwa kama ndugu. Siri yake ni yangu. Mkewe ananiita shemeji, na mwanae ananiita mjomba. Hata siku moja sijaona wala kusikia Raymond akikorofishana na mtu. Nakuhakikishia yeye si mtu wa kuweza kuwa na adui hata mmoja hapa duniani."
"Na mimi nakuhakikishia kuwa anao. Angalau mmoja. Na ni wajibu wangu kumtia mbaroni. Nina imani Dk. Makete anamfahamu mtu huyo. Kwa hiyo lazima nizungumze nae kabla hali yake haijawa mbaya zaidi."
Dk. Beka aliinua uso akauliza, "Unamaana iwapo hata .... hatarudiwa na kauli, mtu huyo hataweza kupatikana?"
Badala ya kujibu swali hilo Inspekta Bessy alisema kwa sauti kavu, "Dk. Beka tafadhali usinifiche niambie ukweli. Dk. Makete atatoka thieta akiwa hai au maiti?"
"Mimi siyo mtabiri! Wala siyo Mungu!" Ingawa maneno hayo yalitamukwa kwa sauti ndogo lakini ilikuwa sauti ya ukali. Iliyojaa uchungu na ghadhabu. Dk. Beka akapumua na kusema kwa sauti yake ya kawaida, "Bessy, hatuwezi kufanya miujiza, kufanya lisilowezekana. Hatuwezi kufufua maiti. Hakuna anaeweza kufanya hivyo zaidi ya Yesu."
"Ndiyo kusema Dk. Makete hana tumaini?"
"Sijasema hivyo. Raymond hajawa maiti. Hivi tunavyozungumza anashughulikiwana mabingwa. Wanaweza wakafaulu kuyaponya maisha yake, wanaweza wasifaulu. Ikishindikana, hakuna yeyote wa kuweza kufanya lolote."
Bessy alikunja uso na kusema. " Kuna sindano ya kuua ganzi na kumzindua mtu na kumfanya aweze kijibu swali moja au mawili kabla ya kukata roho.Kama Dk. Makete hana tumaini lazima sindano hiyo itumiwe ili atutajie mtu alie mgonga."
"Dk.Beka akamtazama Bessy kwa mshangao. Akamwuliza, "Umeisikia wapi hiyo sindano?"
"Katika kitabu."
"usiamini kila unachosoma kwenye vitabu vya hadithi."
"Hakikuwa kitabu cha hadithi."
Kimya kizito kikazagaa humo ndani kwa nukta kadhaa. Hatimaye Bessy akauliza "Sindano hiyo ipo au haipo?"
"Ndiyo - ipo."Dk. Beka alijibu kwa karaha. "Lakini haitumiwi ovyo. Kwa sababu humumaliza kabisa mgonjwa. Hata kama alikuwa asife atakufa."
"Kwa mtu asie na matumaini ....?"
"Ni nani wa kuamua kuwa hana matumaini? Si mimi. Ninavyoamini mimi, mtu anaepumua ni mzima, Hata kama tumaini la kupona ni moja katika milioni. Oh, tunapoteza bure wakati kuizungumzia sindano hiyo. Kwanza hatuwezi kuitumia bila amri toka juu. Ni nani wa kwenda ikulu? Wewe?
Na hata kama nitalazimishwa kuitumia sitaitumia. Nitajiuzulu. Kwa sababu moja tu. Siwezi kukubali kuua - kumwua mtu yeyote yule, achilia mbali mtu huyo kuwa rafiki yangu mkubwa."
Bessy alishusha pumzi ndefu akasema. "Nimekuelewa, Dk. Samahani."
Dk. Beka akapumua pia. Akasema, "Kuhusu swali langu?"
itaendelea.
SEHEMU YA SITA.
Sajini Bob alikazana kujipepea kwa gazeti. Yeye na Koplo Butu walikuwa wameketi ndani ya gari lao la polisi waliloliegesha pembeni, karibu na makutano ya barabaraya Wazawa.
Palikuwa mahali pa pirikapirika za magari. Taa za barabarani, ambazo zilikuwa za kisasa, za kuning'inia juu,zilikazana kuamuru maderevakusimama na kuondoka. Bob na Butu walikuwa wakisubiri mtu avunje sheria wamtoe upepo au wamchukulie hatua, mno hilo la kwanza.
Bob ambaye alikuwa mnene, na hasa sehemu ya tumbo alikuwa akitokwa jasho, pamoja na kujipepea kwa nguvu na kuuacha wazi mlango wa upande wake. Butu, aliekuwa mwembamba, alikuwa mkavu kabisa. Alikuwa anavuta sigara na kuuangalia kwa jicho moja moshi aliokuwa akiupulizia pembeni. La pili likiyavinjari magari yaliyosongamana barabarani, akiomba kimoyomoyo mojawapo livunje sheria.
"Unaweza kuvuta katika fukuto kama hili?" Bob alimwuliza. Yeye hakuwa mvutaji. Alikuwa mtu wa lawalawa. Hata dakika hiyo alikuwa akimung'unya moja. Alitaka kumuuliza, Na wewe unaweza kufutuka mtumbo katika usawa mgumu kama huu.? Lakini akajikuta akisema , "Ni mazoea, Bob mazoea." Akaongeza, "Wanasema mazoea ni kitu kibaya sana. Nadhani ni kweli. Kusema kweli, mimi hukushangaa wewe kuweza kumung'unya pipi wakati wote.Mdomo haochoki?"
Bob akaguna. Akaitazama saa yake na kusema, "Nadhani tunapoteza bure wakati wetu hapa." Kisha akatega masikio.
Wote wakausikia mvumo wa injini inayolalamika kwa kulazimishwa. Wakageuza kichwa. Wakaliona gari lenyewe. Lilikuwa Jeep la kijeshi likitokea upande wa Ndala na kuelekea mjini. Taa zote za gari hilo zilikuwa zikiwaka, honi ikihanikiza, likichenga magari mengine kama mchezaji wa mpira aliepania kufunga goli.
Bob akatikisa kichwa. Akasema kwa karaha, "Hawa wanajeshi wakati mwingine hujisahau kabisa. Huyu lazima tumfunze adabu. Ndio wanaosababisha ajali za kipumbavu kama ile iliyotokea nyuma ya benki leo asubuhi."
"Ile haikuwa ajali ya kawaida, Bob." Butu alimkumbusha. "Ilikuwa kusudi."
"Hata huyu akigonga itakua kusudi." Ingawa taa za barabarani zilimuamuru derva wa Jeep asimame lakini hakusimama. Huku matairi yakiuma lami na kulalama, akapinda kushoto na kuendelea na safari yake kwenye barabara ya Wazawa."
Bob akaufunga mlango wa gari kwa nguvu kupita kiasi na kuamuru, "Mwandame!" Butu akasita. Akasema, "Bob unadhani hakutuona?'
"Una maana gani?"
"Katuona!"
"Kwa hiyo?"
"Ametudharau!"
"Nimesema mwandame!" Bob alifoka kwa sauti yake ya kisajini. "Tutaona mwisho wa dharau yake!"
Butu alitia moto gari. Huku king'ora kikibweka na kimwelumwelu kikimetemeta,wakaliandama Jeep.Lakini hakuweza kulikamata.
Hatimaye likapinda kushoto na kutulizwa kwenye uwanja wa kuegesha magari wa Hospitali Kuu ya Serikali. Mwanajeshi aliekuwa akiliendesha akateremka na kuelekea lango kuu.
"Kamkamate!" Bob alimwamuru Butu,baada ya mwenzake kulisimamisha gari kando ya Jeep lililotapakaa vumbi.
Butu akasita. Akasema, "Bob yule ni Luteni," "Kwa hiyo?" Huoni kama ni bora uende wewe?" "Hapana! Nenda wewe. Akileta ukorofi nitakuja kukusaidia."
Kwa shingo upande, Butu akateremka na kumfuata mwanajeshi yule, ambaye alikuwa akilikaribia lango. Akamwita, "Luteni!"
Mwanajeshi akasimama na kugeuka taratibu. Akauliza, "Kitu gani?" "Kuhusu uendeshaji wako .... Butu akauhisi mdomo wake ukiwa mzito.
Akajikuta anaangalia macho ambayo hajapata kuyaona maishani mwake .Yalikuwa kama ya Nyoka alieghadhabika. Kama yanatoa cheche . Kama yanayosema , "Ropoka neno moja tu la kipuuzi na utaingizwa humu ndani kwa machela."
Ghafla, Butu akaanza kutokwa jasho jembamba .Mwanajeshi aligeuka na kuingia hospitalini.Kwa hatua nzito za kupwaya Butu akaanza kurudi kwenye gari lao. Akilini akishindwa kuamini kijana kama yule kuweza kuwa na macho kama yale, pamoja na kuwa mwanajeshi.
"Vipi?" Bob alimwuliza. Butu alijikuna kichwa na kusema, "Alikuwa na sababu ya kuendesha vile."
"Sababu?" Bob akauliza. "Sababu gani?"
"Eee. Ya usalama." Usalama? Usalama gani?"
"Usalama wa Taifa," Alijibu Butu huku akiingia garini. "Bob akauliza, "Usalama wa Taifa?"
"Bob, acha kuwa kama kasuku." Alisema Butu akilitia gari moto. "Kijana yule si wa kawaida. Achana naye. Twende zetu."
Itaendelea