Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
SEHEMU YA KUMI.
"Ni nani mtu huyo?" Bessy aliuliza kwa sauti kali. Lakini mama Denny alikwishageukia ukutani na kuanza kulia kimya kimya.
Bessy akainuka na kumfanyia Dennis ishara ya kichwa kutaka watoke nje. Wakati wakitoka nje. Dk. Beka alijongea kitandani kumfariji mke wa rafiki yake.
Mara tu baada ya kutoka na kufunga mlango, Bessy akauliza kwa matuamaini makubwa. "Ni nani huyo Kassim Hashir?"
"Sijawai hata kumsikia katika maisha yangu." Dennis alijibu uso ukiwa umemnywea. Bessy akakunja uso.
"Itakuwaje usimfahamu na hali wazazi wako wote wawili wanamfahamu?"
"Unategemea kuwa nawafahamu watu wote wanaofahamiana na wazazi wangu? Mimi ni mwanajeshi, wakati mwingi huwa sipo nyumbani."
"Inalekea babako na mamako wanamfahamu vizuri mtu huyo. Nadhani mama yako anaufahamu uhasama uliopo kati ya babako na mtu huyo. Lakini katika hali aliyonayo hawezi kutueleza lolote. Ni vyema tumwache atulie."
Dennis akakubali kwa kichwa.
Baada ya kuwaza kidogo, Bessy akasema. "Twende zetu Makao Makuu ukachukue gari la babako. Na tukapekue mafaili. Pengine huko Kassim Hashir si mgeni nasi."
"Itabidi nifike Makao Makuu yetu kwanza nikarudishe gari lao na kuomba likizo ya dharura. Ikiwa nimeweza kuchokoa vikaragosi vya vichakani hakitanishinda cha mjini."
*********************
Siku hiyo Kikoti 'aliokota' nusu chupa ya wiski iliyosahauliwa chini ya meza,kando ya bwawa la kuogelea. Aliiona chupa hiyo kwa macho yake makali mara tu alipotokeza nyuma ya jengo hilo, akitokea kwenye stoo ya kuhifadhia zana za kazi yake.
Alipoina na kuikota na kuifutika kotini, mwenyewe alidhani hakuna mtu aliemwona. Lakini Kassim Hashir alikuwa dirishani, ghorofani, akimtazama. Hakujali. Si kwa vile alikuwa na mambo makubwa zaidi akilini, bali nusu chupa ya wiski ilikuwa si chochote kwake. Aliona kama vile mtumishi wake amefanya jambo zuri kuondoa takataka. Kwa upande mwingine, kitendo hicho kilimwongezea fahari, furaha,na utamu wa ukwasi - kuona kuna watu dhalili wanaodiriki kuiba hata chupa karibu tupu.
Nje ya geti, Kikoti alielekea kwenye kituo cha basi akiwa ameridhika kabisa na vuno la siku hiyo. Alijua nini cha kufanya. Atakwenda moja kwa moja kwa Shangazi suzy anakokunywa mapuya kila siku. Hapo asingekosa mtu wa kuelewana naye kwa namna moja ama nyingine.
*******************************
Alasiri hiyo, ulifanyika mkutano mfupi katika ofisi ya Daktari Mkuu. Kama kawaida, mwenyekiti alikuwa Dr.Beka mwenyewe. Wengine walikuwa madaktari bingwa wanne waliomshughulikia Dk. Makete thieta.
Baada ya wote kuketi, Dk.Beka akasema, "Sawa. Nipeni mawazo yenu."
"Ana matumaini makubwa." Alisema bingwa wa kwanza. "Tumejitaidi kadri ya uwezo wetu. Sidhani kama kuna mtu angeweza kufanya zaidi ya tulichokifanya. Naweza kusema tumefanya kazi nzuri."
Dk,Beka kakubali kwa kichwa. Akamtazama bingwa mwingine.
"Jambo zuri ni kwamba alifikishwa hospitali haraka." Alisema bingwa huyo. "Hakuwai kuvuja damu ndani kwa undani. Na vitu viwili mhimu, moyo na ubongo, havikuathiriwa."
"Na alikuwa na bahati nzuri," Alisema bingwa wa tatu. "Sisi sote tulikuepo na hatukuwa na shughuli mhimu."
"Likini itamchukua muda kupona sawasawa."
Alisema bingwa wa mwisho. "Na hata hivyo hatakuwa kama alivyokuwa zamani. Ninashuku itabidi atembelee kiti cha magurudumu maisha yake yote yaliyosalia."
"Cha mhimu ni uhai," Alisema Dk.Beka. "Ninachoombea, apone." "Tuna imani atapona. Tumefanya kazi nzuri sana."
*********************
Masjala ya Makao Makuu ya Polisi ilikuwa kubwa. Ilijaa rafu na makabati ya mafaili. Pia mlikuwa na meza mbili tatu, lakini Bessy na Dennis walipoingia, meza moja tu - ile kubwa kuliko zote ndiyo ilikuwa na mtu. Alikuwa amevaa kiraia.
Alisema, "Karibu Inspekta." "Asante Robby."
Bessy akajibu, akivuta kiti. Akaketi na kumwashiria Dennis aketi kando yake.
"Mbona umeadimika, Bessy?" Robby aliuliza.
"Siku nyingi sijawa na kesi mhimu. Leo nimeamua kujipa moja. Wengine walikataa. Walidhani ni ajali ya kawaida."
"Sasa nikusaidie nini?"
"Tuna habari zo zote kuhusu mtu aitwaye Kassim Hashir?"
Robby akabonyeza vibatani, akaliandika jina 'Hashir' kwenye kompyuta iliyokuwa mezani pake. Mashine ile ikaanza kuchakarika,ilipotulia Robby akasema, akisoma kwenye kioo. "Tuna Hashir mmoja tu. Kassim Ismail Hashir. Namba ya faili yake ni 997/69...."
"Sitini na tisa!?" Bessy aliuliza kwa mshangao. "Una maana faili hilo lilifunguliwa miaka ishirini na nne iliyopita?"
"Ndiyo na likafungwa mwaka 1974"
"Baada ya miaka mitano? Ilichukua muda huo kuikamilisha kesi yake?"
"Hapana. Kesi yake haikuwai kukamilika. Kassim hakuwai kukamatwa. Afariki."
Bessy akamtazama Dennis,macho yake yakimsaili. Alipokosa jibu akayarudisha kwa Robby. Akamwuuliza, "Kesi yake ilihusiana na nini?"
"Kwa hilo, maka tulipekue faili lake."
"Unaweza kutupatia,tafadhali?"
"Bila ya tabu." Robby akainuka na kuelekea kwenye rafu za mwisho. "Inaweza kuwa mzee amekosea - si Kassim aliemgonga?"
"Sijui." Alijibu Dennis."Lakini kadri niwezavyo kukumbuka, sijawai kumwona akikosea."
"Kumbuka hakuwa katika hali ya kawaida."
Kabla ya Dennis hajajibu, Robby alirejea mezani akiwa na faili ambalo halikuonyesha dalili yoyote ya kuwa na umri wa miaka ishirini na nne. Bessy akalipokea na kulifungua. Lilikuwa na ukurasa mmoja tu na picha ya kijana wa kati ya mika ishirini na mitano na thelathini mwenye uso wa duara na macho makubwa. Baada ya Bessy na Dennis kuitazama kwa muda, wakausoma ukurasa huo.
Kifupi,ulieleza kwamba Kassim Hashir alituhumiwa kutorosha kiasi kikubwa cha fedha za kigeni, dhahabu, almasi, na madini mengine ya themani, na vipusa, pembe za tembo na ngozi za chui. Vyote hivyo alivitorosha wakati wa utawala wa fasishti Ibrahim Mbwelwa. Kassim aliyeyuka muda mfupi kabla ya Mbelwa kuangushwa.Ilihisiwa alikimbilia Ulaya alikolimbikizia utajiri mkubwa. Alifia Kenya, mwaka 1974 katika ajali ya gari.Chini ya maelezo hayo palikuwa na saini.
Bessy akauliza, "Hii siyo sahii ya Mzee Maliki?"
"Ndiyo, ni yake." Robby alijibu. Lakini wakati huo hakua Kamishna Msaidizi."
Bessy akaitazama saa yake. Akaunyakua mkono wa simu na kusema. "Nipatie Mzee Maliki, kama angalipo ofisini mwake."
"Tangu lini akaondoka kabla ya taa kuwashwa?"
Aliuliza opareta. Kisha akasema, "Zungumza nae."
"Mzee? Ni Bessy hapa.Nataka kukuona."
"Kuhusu?" Ilikuwa sauti nzito, tulivu."
"Kassim Hashir."
"Kassim Hashir? Sidhani kama namfahamu."
"Si ajabu. Ni miaka mingi imekwishapita. Ulimfungulia faili mwaka 1969. Nitakuja nalo faili hilo."
"Sawa."
Faili mkononi, Bessy akainuka na kumwambia Dennis, "Twende kileleni."
mkuu ukimalizia sehemu ya 11 utakuwa umenisaidia sana jioni hii ya baridi kali.NAWASILISHA MAOMBI
SEHEMU YA KUMI NA MOJA.
Kwa Shangazi Suzy palikuwa na mambo. Mojawapo lilikuwa ni lile la watu kutengwa kufuatana na daraja. Wateja wa daraja la kwanza - 'maofisa' waliwekwa chumbani, ambamo mlikuwa na kitanda maridadi, seti ya sofa, viti na meza. Labda waliwekwa humo kwa vile hawakuwa wengi. Na walikuwa wasafi. Na hawakupendelea sana mapuya. Zaidi walikunywa bia na konyagi.
Wateja wa daraja la pili - 'waungwana,' waliwekwa ukumbini kwenye mabenchi. Hakuna alieweza kukisia sababu ya wao kuwekwa hapo. Wengi wao walikuwa wa umri mkubwa. Mno walikunywa mapuya. Waliagiza konyagi kwa nadra. Bia - mwaka mara moja. Sikukuu hadi sikukuu.
Wateja wa daraja la tatu na la mwisho - vichwa vya panzi - waliwekwa uani, ambako walikalia chochote kile, kuanzia matofali hadi chini aridhini.
Sababu za wao kuwekwa huko zilikuwa wazi. Kwanza walikuwa wengi, na wengi wao walioga na kufua kauka nikuvae, Jumapili hadi jumapili. Pili walikuwa hususani watu wa mapuya. Tatu, walikuwa wadoezi na wagandaji - yaani nusu lita ilimfanya mtu agande hapo tangu asubuhi mpaka usiku wa manane. Na nne walilipata jina lao 'vichwa vya panzi' - kwa sababu walikuwa hawakawii kulewa . Na hapo huwa wenye kelele, wagomvi, waimbaji na wachezaji.
Lakini ajabu ni kwamba hakuna hata mmoja, hata siku moja, alielalamikia ubaguzi huo. Kila mmoja alipajua mahali pake na aliridhika napo.
Lakini kwa Kikoti alikuwa tofauti kidogo. Yeye alijipandisha ngazi moja moja. Alianzia kwa 'vichwa vya panzi' alipokuwa hana kazi maalum, ndiyo kwanza aingie jijini.
Akahamia kwa 'waungwana' alipopata kibarua katika kampuni moja ya ujenzi. Akahamia kwa 'maofisa' alipota kazi ya kuhudumu huko Buffalo Hill.
Hata huvyo, kwa kuwa hakuwa mgeni mahali popote, na alikuwa 'memba' kila siku,ilikuwa juu yake mwenyewe kuchagua pa kuketi - aghalabu kutokana na mfuko wake au mwaliko.
Siku hiyo, mfuko wa karatasi mkononi, alipitiliza moja kwa moja hadi chumbani akawakuta 'maofisa' wawili wa kudumu, Bob na Butu, wamekwisha fika,walikuwa wakinywa konyagi.Bob, kwa sababu ya kitambi chake, katika nguo za kawaida alionekana kama meneja wa benki.
Bila ya kusema neno, Kikoti aliitoa chupa ya wiski na kuikita mezani. Bob akaitazama kwa makini. Akainua uso na kuuliza. "Umeipata wapi wiski hii, Kikoti? Ni ya thamani sana!"
"Kanipa tajiri yangu." Kikoti aliongopa, macho makavu. "Huyo ndie tajiri wa kumtumikia. Nikichoka kufokeana na madereva wakorofi, nitakwambia unipeleke na mimi nikaombe kazi."
"Shangazi yupo wapi utupe glasi?" Kikoti akauliza. "Atakuwa wapi kama sio kwa vichwa vya panzi?" Butu alimwuliza.
**********************
"Karibuni." Mzee Maliki aliwakaribisha. Alikuwa mtu wa makamo alietazamia kustaafu muda wowote. Sare yake ya Ukamishna Msaidizi ilimpendeza sana. Ofisi yake ilikuwa pana na nadhifu.
"Ketini." Wakaketi. "Ni nani mwenzako Bessy?"
"Luteni Dennis Makete. Baba yake, Dk.Raymond Makete, aligongwa na gari leo asubuhi nyuma ya Benki ya Wakulima. Aliemgonga hakusimama na hakuna mtu aliwahi kuzisoma namba za gari. Tunaamini mtu huyo ni Kassim Hashir na alimgonga Mzee Makete kusudi."
"Simkumbuki..."
"Ulimfungulia faili hili mwaka 1969 na kulifunga mwaka 1974, ukiamini amekufa."
Mzee Maliki akalipokea lile faili na kulifungua. Baada ya kuupitisha macho ukurasa uliokuwemo, akasema, "Ndiyo, nakumbuka sana. Nilipokea telegram kutoka Polisi ya Kenya ikieleza Kassim Hashir alifikwa na ajali mbaya ya gari na kufariki papo hapo. Sijui kwa nini telegram hiyo haimo humu! Ukweli ni kwamba kesi yake ilikuwa dhaifu sana. Kila mtu aliidharau, pamoja na kuhusiana na mamilioni ya pesa za kigeni. Kwa nini mnadhani yuko hai na ndiye aliemgonga Dk.Makete?"
"Mzee Makete alizinduka kwa nukta chache alipokuwa thieta na kulitaja jina lake."
"Hawezi kuwa amekosea?"
"Hatujui. Lakini kwa vile hatuna fununu yoyote nyingine..."
"Ikoje hali ya babako, Denny?"
"Niliarifiwa amejeruhiwa vibaya. Lakini Dk.Beka anaamini hayuko katika hali ya kutisha." Alijibu Denny. "Huwezi kufanya chochote kile kuhusu mtu huyo?"
" Hatujui chochote kile zaidi ya kulijua jina lake na kuiona picha iliyomo humo, ambayo sidhani kama itatusaidia sana,ni ya zamani mno - tuko gizani kabisa."
"Mmmh, labda nianze toka mwanzo." Alisema Mzee Maliki, akiwaza. "Kama unavyofahamu, nchi hii ilipata uhuru mwaka 1960. Bwana Nelson Benjamin Nseloa akawa Rais wa kwanza. Watu wote walifurahi jinsi alivyopigani uhuru, wote tulimpenda Nselo.
"Lakini kadri miaka ilivyozidi kupita bila ya yeye kutimiza kile ambacho wananchi wengi walitamazamia angetenda, mapenzi yakaanza kupungua. Wananchi wengi walitazamia kuwa baada ya uhuru, Nselo angewafukuza wageni wote - wazungu na waasia na mali zao kugawiwa kwa wazawa. Yeye hakufanya hivyo. Kinyume chake, aliwatetea na kuwalinda. Kwa vile tangu mwanzo walikuwa ndio wafanyabiashara wakubwa na wenye kumiliki mashamba makubwa na mazuri, wakazidi kutajirika. Wananchi wakaishiwa furaha."
Mzee Maliki alitoa mtemba akaanza kuujaza tumbaku kabla hajauwasha na kuukoleza.
"Mkuu wa majeshi wakati huo, Meja Jenerali Ibrahim Mbelwa,akaamua kuutumia mwanya huo. Akaipindua serikali ya Nelson Benjamin Nselo,ambaye alikuwa ng'ambo, na kutwaa madaraka."
Baada ya kuuwasha mtemba kwa kutumia njiti tatu,akaendelea, "Hiyo bila shaka, ni historia mnayoifahamu vizuri. Inasikitishwa vile watu wanavyofurahishwa na kitendo cha Mbelwa, hasa alipowafukuza wageni na kugawa mali zao kwa wananchi. Lakini haukupita muda mrefu kabla ya hulka ya kweli ya Mbelwa kudhihirika. Kwa vile hakuwa na elimu, aliwachukia wasomi, kwa vile alikuwa Mwislam ,aliwachukia wakristo. Kwa vile alikuwa Mshongwe, aliwachukia watu wa makabila mengine,hasa kabila la Nelson Nselo. Si tu aliuteketeza uchumi wa nchi, bali aliteketeza watu karibu milioni. Kwa vile wakati huo tulikuwa miloni chache tu, idadi hiyo ilikuwa kubwa ya kutisha. Watu wakaanza kujuta."
Mtemba ulikuwa umezimika. Akauwasha tena kabla ya kuendelea. "Kwa sababu moja au nyingine, maelfu ya wananchi wakaihama nchi na kuomba hifadhi katika nchi jirani. Nelson Nselo akaweza kuwaunganisha na kuwapa mafunzo ya kijeshi. Wakati ulipowadia wakaingia nchini. Wakashinda kirahisi askari wa Ibrahim, ambao hawakuwa na moyo hata na moyo wa kupigana. Yeye mwenyewe aliuliwa wakati akijaribu kutoroka nchi. Risasi zangu zilikuwa miongoni mwa risasi zilizomtoa roho."
Kikapita kimya cha muda, Dennis akajikuta anamtazama Mzee Maliki kwa matazamo mpya. Mzee huyo akaendelea, "Sasa kuhusu Kassim Hashir. Yeye na Ibrahim walikuwa marafiki, licha ya kutokuwa rika moja. Akampa Kassim pasipoti ya kibalozi na kumtumia kutorosha mali. Katika kipindi cha utawala wa miaka mnne ya utawala wake, Kassim alitorosha mamilioni kwa mamilioni. Alikwenda Ulaya karibu kila wiki kupeleka pesa za kigeni na chochote kile ambacho kilikuwa mali. Kazi hiyo inasemekana aliimudu vizuri. Pia inasemekana alikuwa na kichwa cha biashara. Hakuyaacha mamiloni hayo yalale benki, aliyazalisha katika vitega uchumi mbalimbali.
"Alipoona mambo yanaanza kuharibika hapa nyumbani, akayeyuka. Kwanza alikimbilia Ulaya, baadaye akawa hatulii mahali pamoja. Akawa mfanyabiashara wa kimataifa. Bila ya shaka aliposikia Ibrahim amekufa aliinua mikono mbinguni. Hakuwa na mtu wa kumghasi na wala kugawana nae tena. Na kama ni kweli angali hai atakuwa tajiri mkubwa sana - tajiri wa kuweza kushindana na serikali yoyote ya nchi ya Kiafrika."
Bessy akashusha pumzi. "Sioni kitendo chake cha kurosha mali kinaweza kuhusiana na Dk.Makete."
"Hata mimi sioni." Alikubali Mzee Maliki. Dennis akauliza, "Kwa nini ulisema kesi yake ilikuwa dhaifu - hamkujali sana?"
"Mara tu baada ya Ibrahim kung'olewa, niliteuliwa kuongoza skwadi ya kuwasaka, kuwakamata na kuwapeleka mahakamani wote waliotenda makosa wakati wa utawala wa fasishisti huyo. Walikuwa wengi, zaidi ya elfu. Wengine walikuwa wamefanya makosa madogo tu, lakini wengi walikuwa wametenda unyama kweli kweli. Kwa wengine palikuwa na ushaidi, na kwa wengine hapakuwa na ushaidi wa kutosha. Ilikuwa kazi kubwa kupata majina yao na makosa yao kuwafungulia mafaili, kuwasaka, kuwakamata, kutafuta ushaidi na hatimae kuwapeleka mahakamani. Kadhaa tuliwanasa na walihukumiwa kunyongwa au kufungwa. Lakini wengi pia ilibidi waachiwe na makama kwa uhaba wa ushaidi."
" Wote tuliona Kassim angekuwa mmojawapo wa kuachiwa. Kwanza, kwa vile alikuwa na pesa, angeweka mawakili kabambe. Pili, hatukuwa na ushahidi madhubuti kumtia hatiani. Mashahidi tuliowapata ni maafisa wa forodha na uhamiaji, ambao walikiri kuwa hawakuwa wakimpekua Kassim aendapo ng'ambo kwa sababu ya pasi yake ya kibalozi, ingawa walishuku mizigo yake. Huo sio ushahidi kitu mahakamani. Walishindwa hata kusema kwa hakika ni vitu gani alivitorosha.
"Ushahidi mwingine ulikuwa wa minong'ono tu, wa watu waliokuwa wakimtafutia bidhaa,ambao hatimae akawadhulumu. Unadhani wangekubali kusimama mahakamani na kutoa ushaidi? Wao na wao walikuwa wanavunja sheria. Hata kama wangekubali ili kumkomoa Kassim,wakili yoyote yule angewachakaza vibaya sana."
"Bessy akauliza, "Kwa hiyo hakuna juhudi zozote zilizofanywa za kutaka akamatwe huko Ulaya na kumrudisha nyumbani?"
Tunasubili