popie
JF-Expert Member
- May 28, 2016
- 801
- 577
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mie ninacho nilikinunua kariakooUnacho?
Hadithi hii ilitungwa na mtunzi nguli aliyekuwa akijulikana kama Eddie Ganzel miaka ya 90 mwishoni na 2000's mwanzoni..kuna nyingine kama MSAKO WA MR X mtunz n huyo huyo zilikuwa zikichapishwa kwny majarida ya BongoKAMBI YA NDALA.
MWANGAZA hafifu wa mapambambazuko
uliwafanya Luten Dennis Raymond Makete na wenzeke waonekane kama vivuli.Walikuwa katikati ya msitu wa Ndala wakienda mbio za mchakamchaka.
Wote walikua katika vazi kamili la kombati,bunduki mkononi ,mkoba mgongoni.
Rekuruti au 'Kuruta' wanaochukua mafunzo ya Uwanajeshi wa kawaida huamushwa mapema kuanza mazoezi.Lakini wanajeshi wanaojitayarisha kuchukua kozi ya ukomandoo huamushwa mapema zaidi -aghalabu hukesha na kufanya mazoezi usiku na mchana.
Na mazoezi yao huwa magumu kupindukia .Kwani lengo kuu ni kumkomaza mwanajeshi afikie kiwango cha hali ya juu kabisa ya ukakamavu na ujasiri ili awe tayari wakati wowowte ule kuhimili mazingira ya aina yoyote,hata mateso.Kwani iwapo atakuja shikwa na adui hapaswi kutoa siri.Anachopaswa kufanya ni moja wapo tu kati ya mambo matatu:Kuhimili mateso,kutoroka au kujiua.
Sehemu kubwa ya mazoezi yenyewe kwa kweli ni mateso matupu,Kwanza kabisa,mwanajeshi hutakiwa aishi maisha magumu kadri iwezekanzvyo.Kula kwa taabu,kunywa kwa taabu,kulala kwa taabu .Jua liwe lake ,mvua yake,baridi yake.Hakuna cha kukwepa .
Na juu ya hayo,kuna amri za ajabu ajabu ambazo lazima zitiiwe bila ya kusita .Kama vile kutembea au kukimbia msituni usiku wa manane .Kuchimba handaki katika muda mfupi usio wa kawaida .Pengine kwa kutumia zanz zisizo za kawaida,bakuli la mesi au hata vidole vitupu.Kupanda mti ambao pengine hata Nyani asingeweza kupanda.Kuvuka mto ambao mtu wa kawaida asingeweza kuuvuka ,tena na mzigo mgongoni na bunduki mkononi. Na kadhalika.
Baada ya mazoezi hayo ambayo huchukua takribani miezi mitatu,na ambayo hudhihirisha ukakamavu na ujasiriwa mutukabla ya kuchaguliwa kuanza kozi yenyewe ya ukomandoo,mwanajeshi hutakiwa adhihirishe pia kiwango cha hali ya juu cha werevu,busara,maarifa,ujanja utundu.
Kwa hiyo si ajabu kuona idadi ya makomandoo ni ndogo sana katika jeshi lolote lile duniani.Kwani hatimaye,idadi ya wanaofaulu kuteuliwa kuchukua kozi yenyewe huwa aghalabu haifikii asilimia hamsini.Na kati yao, wanaohotimu na kuwa makomandoo kamili huwa wachache zaidi..Mmoja au wawili-wakati mwingine zaidi ,kufia mafunzoni ni jambo la kawaida kabisa.Kwani mtihani wa mwisho ni wa kupambana kwa kutumia silaha za kweli kweli.
katika hali kama hiyo ,si ajabu pia kuona kuwa mwanajeshi huwa kwa kawaida halazimishwi kuchukua mafunzo ya ukomandoo.kila mmoja hujitolea yeye mwenyewe.
Na kawaida ,hakuana anaelazimishwa kumaliza kozi yote.Ye yote ,wakati wowote,anapoona imetosha huinua mokono juu na kurudia uanajeshi wa kawaida.
Na hakuna anayemcheka .Huwa kinyume chake.Hupongezwa na kila mmoja .Kwani yeye angalau ameweza kujaribu kuishi jehannam kwa siku chache,wiki chache au miezi michache.
*************
Dakika chache kabla ya saa nne kamili Dr.Raymund Makete aliliegesha gari lake aina ya Bentley kwenye uwanja wa kuegeshea magari nyuma ya Benki ya wakulima .Akateremka na kuelekea barabara ya Nkurumah ,uliko mlango wa mbele wa benki hiyo.
Dr.Makete alkua mtu mzima wa zaidi ya miaka sitini.Nywele zake zilikua nusu nyeupe nusu nyeusi.Lakini hata hivyo,hakuwa mkongwe aliekongoka .Akiwa na mwili wa wastani na wajihi mtulivu wa kiungwana .Alikuwa angali imara,nadhifu,alietembea kwa hatua madhubuti za uhakika.Si za pupa wala si za kinyonga .Suti yake ya kiafrika-ya mikono mifupi na kola pana -ilimkubali kikamilifu.
Aliumaliza uchochoro wa benki akaingia mtaa wa Nkurumah na kupinda kushoto.Hatua chache zaidi zikamfikisha kwenye mlango wa mbele wa Benki ya Wakulima.
Alipousukuma mlango huo ukamgonga mtu aliekuwa anataka kutoka ambaye macho yake yalikuwa kwenye karatasi alizozishika mkononi.
Alkua mrefu ,aliyenawili vizuri,wa umri wa kati ya miaka hamsini na tano,mwenye haraza kubwa lililotenganisha nywele kama matuta .Suti yake ya kunguru ilionyesha wazi kuwa ni ya thamani,Na yeye mwenyewe alionyesha wazi hakuwa na tatizo la ukwasi.
"Kumradhi,"Mzee Makete alisema haraka kama vile kosa la kumgonga mtu huyo lilikuwa lake peke yake.Mtu huyo alipoinua uso,macho yake na ya Mzee Makete yakafungamana.Macho yake yalikua makubwa kuliko kawaida,tena makali,ya dharau na jeuri.Ya mtu ayenata.Mtu anaeaminianaweza kupata chochote akitakacho au kufanya lolote apendalo.
Mzee Makete akaganda,macho yake mapole ameyafinya ,mdomo nusu wazi kwa mshangao na msituko .Kumbukumbu ya mambo ya kutisha ikamjia akilini.Akauliza kwa sauti kama si yake,"Wewe siye Kassim?"
"Nani?" Ingawa mtu huyo aliuliza kijeuri lakini uso ulikwishambadilika ghafla .Ulimwiva,na alikua akipumua kwa nguvu .Macho yake makubwa yaliingiwa na kila dalili ya hofu.Mshituko wake ulikua mkubwa zaidi kuliko wa Dr Makete.
Ingawa walitazamana kwa nukta moja au mbili tu,lakini ilikuwa kama muda mrefu zaidi ulipita kabla ya Dr.Maketekusema "Kassim Ha....."
Mkuu hizi Hadithi zote nitazipata Wapi???Hadithi hii ilitungwa na mtunzi nguli aliyekuwa akijulikana kama Eddie Ganzel miaka ya 90 mwishoni na 2000's mwanzoni..kuna nyingine kama MSAKO WA MR X mtunz n huyo huyo zilikuwa zikichapishwa kwny majarida ya Bongo
Hata mie nazitafta sana..nilibahatisha kitabu kimoja k'kooMkuu hizi Hadithi zote nitazipata Wapi???
Kwa ruhusa yenu jumamosi nitaleta hapa toka tulipoishia Ila kwa picha za kurasaKitabu ninacho mwenye kuhitaji au anayeweza kuandika aje inbox
Litakuwa jambo la msingi sana mkuuKwa ruhusa yenu jumamosi nitaleta hapa toka tulipoishia Ila kwa picha za kurasa
Karibu MkuullKwa ruhusa yenu jumamosi nitaleta hapa toka tulipoishia Ila kwa picha za kurasa
Itakuwa labda kaokokaaHuyo Hayawani Badoooo