Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #121
SEHEMU YA 90
Kila mmoja alianza kupiga kelele mule ndani na kuogopa.
Maiko hakuwa na wasiwasi wowote na kile kichwa mkononi na hiyo ikawathibitishia na kufanya waamini kuwa kweli Maiko ni muuaji.
Patrick hakushangazwa sana kumuona Maiko ameua ila kitu kilichomshangaza ni kuwa Maiko amempata wapi Mashaka.
Patrick akainuka na kuanza kumsogelea Maiko.
PATRICK: Umempata wapi Mashaka?
MAIKO: Tafadhari usinisogelee.
Deborah kusikia vile akainuka na kuanza kumvuta Patrick kwani alihofia nae kupatwa na matatizo kama yale. Ila Patrick alikuwa mbishi, bado alihitaji kujua Maiko kamtoa wapi Mashaka.
PATRICK: Nataka uniambie ulipomtoa Mashaka.
MAIKO: Yote nitasema ila usinisogelee.
Deborah akazidi kumvuta mwanae na kumuomba warudi kukaa. Ndio Patrick akarudi kwani hata yeye hakujua hatma yake ni nini.
Mwita pale nje hakutaka kujiuliza mara mbili mbili akachukua simu yake na kuwapigia maaskari kisha akawaelekeza eneo la tukio ili waje kumkamata muharifu yule halafu akaingia ndani, alitamani hata muujiza utokee kuwa muongeaji wa yale maneno asiwe baba yake, alitamani hata awe ni mtu mwingine.
Mwita alipoingia tu ndani, Maiko aliweza kumsikia na kumuona.
Maiko akatoa bastola na kumuwahi nayo Mwita kuwa akae chini, Maiko hakuwa kama binadamu wa kawaida. Wote walibaki kushangazwa na ile hali.
Mwita aliamua kukaa huku akivizia namna ya kumnyang'anyanya silaha hiyo baba yake kwani alijua wazi kuwa kitendo cha kumsogelea ni kuhatarisha maisha yake.
Maiko akawaelezea tena vile anavyojielewa yeye.
"Sikufikiria kama ninachokifanya ni kitu kibaya na kuwa ipo siku itanigharimu, kuhusu kukamatwa na polisi sikuwa na shaka nao haswa kwa vijana wanaopenda rushwa kama Taifa letu.
Sitaki mtu anisogelee kwavile nataka kueleza niliyonayo jambo kwa ufupi na kwa kuruka ruka ili wote mpate kunielewa.
Mtoto wa Deborah huyo Jasmine ni mimi kweli niliyetoa oda kwa vijana wakammalize mtoto huyo, sio kwamba nilikuwa na ugomvi na mume wa Deborah au Deborah mwenyewe hapana!! Ila nilifanya kwa kuifurahisha nafsi yangu, ila mwanzoni sikujua kama mtoto huyo ni wa Deborah, nilitoa sifa za mtoto na badae nikaletewa. Nilikuja kugundua wakati mtoto mwenyewe tushamteka ila nikaamua kuipotezea tu, Laiti kama ningejua kuwa Jumanne ni ndugu yangu nisingethubutu kufanya vile.
Vijana wangu walinipa taarifa juu ya kukamatwa kwa yule binti aliyetuletea mtoto, nikafanya mpango hadi yule binti akawa huru kabisa hakuwa na kesi tena hapo pesa yangu ndio iliyoongea.
Nilipomkuta Deborah tena na mtoto nilishangaa sana nikajua labda kipindi tunamteketeza mwanae alikuwa mjamzito. Sikuhisi hata kidogo kama Patrick si mtoto wa Deborah.
Huyu mwanamke ana moyo wa kijasiri sana anahitaji kuigwa.
Ni kweli mimi ni mume gaidi, Deborah hajakosea kuniita hivyo sikuwa na huruma kwa mke wala mtoto.
Nilimtenda vibaya Fausta tena bila hata ya kujua ni dada yangu. Halafu kibaya zaidi ni kitendo cha kumbaka mwanangu Tina.
Sifai kuigwa na yeyote, nilipandikizwa roho mbaya na ya kikatili moyoni mwangu ila hadi nitakapoingia kaburini nitakuwa namlaumu huyu mwenye kichwa hiki.
Msimuhukumu Patrick kwa chochote, najua vyote alivyofanya mimi ndiye chanzo. Nimemuharibu sana Patrick kimawazo na kitabia.
Ni mimi niliyempa mbinu za kumpata Tusa kwa urahisi na kumfanya atakavyo.
Patrick si mtu mbaya kwani kuna kipindi huwa anajirudi.
Patrick alimteka Mashaka, mimi nilikuwa nikimfatilia.
Patrick alimfunga Mashaka huko porini nami nimeitumia nafasi hiyo kummaliza Mashaka kwani tushamaliza watu wengi sana ila Mashaka hakuacha kutamani kuendelea kumaliza watu wasio na hatia.
Mashaka hafai tena hafai kabisa, najua hapa hakuna wa kumsamehe Mashaka wala mimi.
Narudia tena msimuhukumu Patrick, akili yake ilivurugwa.
Deborah ni mwanamke mwema, yani mateso yote yale hakuthubutu kumtupa Patrick.
Laiti kama ningerudi ujanani basi ningemfanya Deborah kufurahia maisha yake duniani.
Kifo cha baba yangu mzazi kimeniumiza sana, ni mengi nimeyafanya bila huruma. Kwangu mimi mwanamke hakuwa na thamani yoyote.
Pole mama yangu bi.Rehema najua hukutarajia kitu cha namna hii ila ndio hivyo mwanao sio mtu wa kawaida kabisa.
Mkienda Arusha mtaweza kuona uajabu wangu humo ndani.
Pole na wewe Deborah kwani uliponitoroka niliitumia nafasi hiyo kummaliza baba yako mdogo. Mimi ndiye niliyemuua.
Wote niliowaumiza nawaambia pole, poleni sana kwa kuumizwa na Maiko.
Sitaki kufungwa na siko tayari kwenda jera.
Najua hakuna wa kunisamehe, ila nawaomba kitu kimoja.
Patrick anakujua nyumbani kwangu Arusha.
Mwende huko, mkateketeze kila kitu cha ndani haswa viungo vya binadamu na mali zangu zote nawaachia nyie mtajua cha kufanya ila nawaomba myasikilize mawazo ya Deborah.
Najua kuna maswali bado mnayo ya kuniuliza ila hiyo barua itawajibu kila kitu. Nimemaliza ila sitaki mtu wa kunisogelea"
Akachukua bastola yake, mara gafla mule ndani mkavamiwa na kundi la maaskari ambao Mwita aliwapigia simu.
Wakataka kumsogelea Maiko, akawanyoonyea bastora.
MAIKO: Atakayenifata nakwenda nae na maji, siko tayari kwenda jela. Kweli nimeamini, mwisho wa ubaya ni aibu.
Wale mapolisi wakikazana kutafuta mbinu ya kumkamata Maiko hakupoteza muda, akaweka ile bastora kichwani mwake na kusema neno moja tu.
MAIKO: Kwaheri mama.
Kisha akajifyatua kwenye ubongo na kuanguka chini huku kichwa cha Mashaka kikiwa mkononi.
Ilikuwa ni tukio la kushtua sana mule ndani.
Polisi wale wakamfata Maiko pale chini aliyeonyesha kuwa bado hajakata roho vizuri,
Polisi mmoja akainama ili amsikilizie akashangaa akivutwa kwa chini.
Itaendelea kesho....!!!
Kila mmoja alianza kupiga kelele mule ndani na kuogopa.
Maiko hakuwa na wasiwasi wowote na kile kichwa mkononi na hiyo ikawathibitishia na kufanya waamini kuwa kweli Maiko ni muuaji.
Patrick hakushangazwa sana kumuona Maiko ameua ila kitu kilichomshangaza ni kuwa Maiko amempata wapi Mashaka.
Patrick akainuka na kuanza kumsogelea Maiko.
PATRICK: Umempata wapi Mashaka?
MAIKO: Tafadhari usinisogelee.
Deborah kusikia vile akainuka na kuanza kumvuta Patrick kwani alihofia nae kupatwa na matatizo kama yale. Ila Patrick alikuwa mbishi, bado alihitaji kujua Maiko kamtoa wapi Mashaka.
PATRICK: Nataka uniambie ulipomtoa Mashaka.
MAIKO: Yote nitasema ila usinisogelee.
Deborah akazidi kumvuta mwanae na kumuomba warudi kukaa. Ndio Patrick akarudi kwani hata yeye hakujua hatma yake ni nini.
Mwita pale nje hakutaka kujiuliza mara mbili mbili akachukua simu yake na kuwapigia maaskari kisha akawaelekeza eneo la tukio ili waje kumkamata muharifu yule halafu akaingia ndani, alitamani hata muujiza utokee kuwa muongeaji wa yale maneno asiwe baba yake, alitamani hata awe ni mtu mwingine.
Mwita alipoingia tu ndani, Maiko aliweza kumsikia na kumuona.
Maiko akatoa bastola na kumuwahi nayo Mwita kuwa akae chini, Maiko hakuwa kama binadamu wa kawaida. Wote walibaki kushangazwa na ile hali.
Mwita aliamua kukaa huku akivizia namna ya kumnyang'anyanya silaha hiyo baba yake kwani alijua wazi kuwa kitendo cha kumsogelea ni kuhatarisha maisha yake.
Maiko akawaelezea tena vile anavyojielewa yeye.
"Sikufikiria kama ninachokifanya ni kitu kibaya na kuwa ipo siku itanigharimu, kuhusu kukamatwa na polisi sikuwa na shaka nao haswa kwa vijana wanaopenda rushwa kama Taifa letu.
Sitaki mtu anisogelee kwavile nataka kueleza niliyonayo jambo kwa ufupi na kwa kuruka ruka ili wote mpate kunielewa.
Mtoto wa Deborah huyo Jasmine ni mimi kweli niliyetoa oda kwa vijana wakammalize mtoto huyo, sio kwamba nilikuwa na ugomvi na mume wa Deborah au Deborah mwenyewe hapana!! Ila nilifanya kwa kuifurahisha nafsi yangu, ila mwanzoni sikujua kama mtoto huyo ni wa Deborah, nilitoa sifa za mtoto na badae nikaletewa. Nilikuja kugundua wakati mtoto mwenyewe tushamteka ila nikaamua kuipotezea tu, Laiti kama ningejua kuwa Jumanne ni ndugu yangu nisingethubutu kufanya vile.
Vijana wangu walinipa taarifa juu ya kukamatwa kwa yule binti aliyetuletea mtoto, nikafanya mpango hadi yule binti akawa huru kabisa hakuwa na kesi tena hapo pesa yangu ndio iliyoongea.
Nilipomkuta Deborah tena na mtoto nilishangaa sana nikajua labda kipindi tunamteketeza mwanae alikuwa mjamzito. Sikuhisi hata kidogo kama Patrick si mtoto wa Deborah.
Huyu mwanamke ana moyo wa kijasiri sana anahitaji kuigwa.
Ni kweli mimi ni mume gaidi, Deborah hajakosea kuniita hivyo sikuwa na huruma kwa mke wala mtoto.
Nilimtenda vibaya Fausta tena bila hata ya kujua ni dada yangu. Halafu kibaya zaidi ni kitendo cha kumbaka mwanangu Tina.
Sifai kuigwa na yeyote, nilipandikizwa roho mbaya na ya kikatili moyoni mwangu ila hadi nitakapoingia kaburini nitakuwa namlaumu huyu mwenye kichwa hiki.
Msimuhukumu Patrick kwa chochote, najua vyote alivyofanya mimi ndiye chanzo. Nimemuharibu sana Patrick kimawazo na kitabia.
Ni mimi niliyempa mbinu za kumpata Tusa kwa urahisi na kumfanya atakavyo.
Patrick si mtu mbaya kwani kuna kipindi huwa anajirudi.
Patrick alimteka Mashaka, mimi nilikuwa nikimfatilia.
Patrick alimfunga Mashaka huko porini nami nimeitumia nafasi hiyo kummaliza Mashaka kwani tushamaliza watu wengi sana ila Mashaka hakuacha kutamani kuendelea kumaliza watu wasio na hatia.
Mashaka hafai tena hafai kabisa, najua hapa hakuna wa kumsamehe Mashaka wala mimi.
Narudia tena msimuhukumu Patrick, akili yake ilivurugwa.
Deborah ni mwanamke mwema, yani mateso yote yale hakuthubutu kumtupa Patrick.
Laiti kama ningerudi ujanani basi ningemfanya Deborah kufurahia maisha yake duniani.
Kifo cha baba yangu mzazi kimeniumiza sana, ni mengi nimeyafanya bila huruma. Kwangu mimi mwanamke hakuwa na thamani yoyote.
Pole mama yangu bi.Rehema najua hukutarajia kitu cha namna hii ila ndio hivyo mwanao sio mtu wa kawaida kabisa.
Mkienda Arusha mtaweza kuona uajabu wangu humo ndani.
Pole na wewe Deborah kwani uliponitoroka niliitumia nafasi hiyo kummaliza baba yako mdogo. Mimi ndiye niliyemuua.
Wote niliowaumiza nawaambia pole, poleni sana kwa kuumizwa na Maiko.
Sitaki kufungwa na siko tayari kwenda jera.
Najua hakuna wa kunisamehe, ila nawaomba kitu kimoja.
Patrick anakujua nyumbani kwangu Arusha.
Mwende huko, mkateketeze kila kitu cha ndani haswa viungo vya binadamu na mali zangu zote nawaachia nyie mtajua cha kufanya ila nawaomba myasikilize mawazo ya Deborah.
Najua kuna maswali bado mnayo ya kuniuliza ila hiyo barua itawajibu kila kitu. Nimemaliza ila sitaki mtu wa kunisogelea"
Akachukua bastola yake, mara gafla mule ndani mkavamiwa na kundi la maaskari ambao Mwita aliwapigia simu.
Wakataka kumsogelea Maiko, akawanyoonyea bastora.
MAIKO: Atakayenifata nakwenda nae na maji, siko tayari kwenda jela. Kweli nimeamini, mwisho wa ubaya ni aibu.
Wale mapolisi wakikazana kutafuta mbinu ya kumkamata Maiko hakupoteza muda, akaweka ile bastora kichwani mwake na kusema neno moja tu.
MAIKO: Kwaheri mama.
Kisha akajifyatua kwenye ubongo na kuanguka chini huku kichwa cha Mashaka kikiwa mkononi.
Ilikuwa ni tukio la kushtua sana mule ndani.
Polisi wale wakamfata Maiko pale chini aliyeonyesha kuwa bado hajakata roho vizuri,
Polisi mmoja akainama ili amsikilizie akashangaa akivutwa kwa chini.
Itaendelea kesho....!!!