Chachasteven
JF-Expert Member
- Jul 4, 2014
- 1,941
- 2,044
- Thread starter
-
- #81
SEHEMU YA KUMI NA TATU
"Wewe ndiye Mrs. Jacob?" Reacher aliuliza.
Jodie Graber alitikisa kichwa kukubali.
"Ndiye mimi, Nilikuwa," Jodie alijibu. "Ni Jina la mume wangu. Tumeachana, lakini bado nalitumia kazini."
"Alikuwa ni nani?"
"Wakili, kama mimi."
"Mmedumu kwenye ndoa kwa muda kiasi gani?"
"Miaka mitatu tu. Tulikutana chuo na kuamua kufunga ndoa tulipohitimu na kupata kazi kila mmoja. Mimi nilibaki Wall Street, Yeye akaenda DC. Nasikitika alipoondoka ndoa yetu aliiacha. Hakuondoka nayo na nilikuja kujua alipotuma karatasi za kuomba tuachane. Jina lake ni Alan Jacob."
Reacher alisimama na kumuangalia Jodie. Aligundua ilikuwa huzuni kwake kusikia Jodie alikuwa ameolewa na kuachika.
Jodie alikuwa mwembamba lakini mwenye mvuto tangu akiwa na miaka kumi na tano tu, alikuwa mwenye kujiamini na mwenye soni kidogo. Reacher alikuwa ameshuhudia mara nyingi vita kati ya haya na udadisi usoni pake kila mara walipoongea kuhusu kifo na uhai na mema na mabaya enzi hizo. Halafu wangebadilisha mada na kuongea kuhusu upendo na mapenzi na wanaume na wanawake. Halafu Jodie angeona aibu na kuaga kuondoka. Reacher angebaki mwenyewe akiwa kama barafu kwa ndani. Siku chache baadaye angemuona tena Jodie akizungukazunguka kwenye mazingira ya kambi. Na sasa miaka kumi na tano baadae alikuwa ni mwanamke mkubwa, mwenye elimu ya haja ya sheria, aliyeolewa na kuachika, mzuri na mwenye busara akiwa amesimama hapo mbele yake huku wameshikana mikono.
"Umekwishaoa?" Jodie alimuuliza Reacher.
Alitikisa kichwa kukataa, "Hapana."
"Lakini una furaha?"
"Mimi nina furaha kila siku," Reacher alijibu. "Ninayo furaha tangu zamani, na nitakuwa nayo kila siku."
"Unashughulika na nini sasa?"
Reacher aliinua mabega. "Sifanyi vingi," Alijibu.
Alianza kuzungusha macho yake kwa wale waombolezaji waliokuwepo kwenye ile kadamnasi. Watu ambao wako bize muda wote. Wana maisha ya kifahari. Kazi za heshima, wote wakiwa ni watu wanaojua wanapotoka na wanapoenda. Kama mtoto anayejua vyema kuimba alfabeti A mpaka Z kwa mpangilio. Aliwatazama kwa nukta na kuwaza kama wao ndiyo walikuwa wendawazimu, au yeye ndiye alikuwa mwendawazimu.
"Nilikuwa Keys," Alisema. "Nilikuwa nachimba mabwawa ya kuogelea kwa chepeo."
Mwonekano wa uso wa Jodie haukubadilika. Jodie alijaribu kuushika mkono wa Reacher kwa nguvu. Ilikuwa kazi bure. Mkono wake ulikuwa mdogo sana ukilinganisha na kiganja cha Reacher.
Costello alikupata huko?" Jodie aliuliza.
Hakuwa akinitafuta kunialika kwenye msiba, Reacher aliwaza. "Tunahitaji kuzungumza kuhusu Costello," Alisema.
"Ni mtu makini, sio?"
Hakuwa makini sana, Reacher aliwaza tena.
Jodie aliuachia mkono wa Reacher na kuanza kuwazungukia umati wa waombolezaji. Watu walikuwa wamesimama wanasubiri kutoa pole zao kwa mara nyingine tena. Hata hivyo, vinywaji walivyokuwa wamekunywa vilianza kuwaelemea na walikuwa wakiongea kwa sauti kubwa. Reacher naye aliteleza kutoka alipokuwa amesimama hadi kwenye meza iliyokuwa imefunikwa kwa kitambaa cheupe. Hapo alichukua sahani ya karatasi na kuiwekea kuku na wali na kuchukua glasi ya maji. Kulikuwa na kiti kilichoonekana kuzeeka. Pengine ndiyo maana watu wengi walikipuuza. Reacher aliketi kwenye hicho kiti peke yake.
Alikuwa akiyazungusha macho yake kwenye ule umati wa waombolezaji huku akila taratibu. Watu walikuwa wagumu kuondoka. Hii ilithibitisha upendo wao kwa Garber ulivyokuwa mkubwa. Jodie alikuwa akitoka kwa huyu na kwenda kwa yule akitoa na kupokea mikono, huku uso wake ukiwa na tabasamu la huzuni. Kila mmoja alionekana alikuwa na kisa cha kumwambia. Kisa kuhusu moyo wa dhahabu wa Garber kwa matendo yake. Reacher angeweza kumwambia Jodie visa vingine vingi vya Garber, lakini visingekuwa na umuhimu. Jodie hakuwa anahitaji kusikia kisa chochote kujua kwamba baba yake alikuwa mtu mbele ya watu. Ni kitu alichokuwa anakifahamu. Kwa muda wa uhai wa Garber hakuwahi kumficha Jodie kitu chochote. Watu wanaishi, halafu wanakufa, na kama watayaishi maisha yao katika njia nzuri hakuna kitu cha kujutia hata wakifa.
Waliipata sehemu ya kuhifadhi gari lao mtaa wa pili, Ilikuwa sehemu yenye ukimya bila watu. Waliliegesha gari yao nyuma ya gereji ambako isingeonekana kwa urahisi. Lakini walihakikisha inakaa katika mkao wa kuondoka. Walitoa bastola zao kwenye boksi lililokuwamo kwenye gari na kuzipachika kwenye mifuko ya mikoti ya suti zao. Wakaanza kutembea kurudi barabarani kwa uangalifu mkubwa kwa kutumia njia za pembeni kidogo.
Ilikuwa ni safari fupi, lakini ngumu. Ni kweli walikuwa maili sitini kutoka Manhattan, lakini ilikuwa ni sawa na kuwa katikati ya misitu ya Borneo. Kulikuwa na majani na miti iliyozagaa kila pahali ikiwa na matawai marefu. Waliamua kutembea kwa kutanguliza migongo. Walipofika karibu na barabara iliyokuwa inaelekea kwa Garber walikuwa wakihema kwa nguvu huku vumbi la kijani likiwa limewavaa. Walilala chini ambapo wasingeweza kuonekana wakitembea. Walianza kutambaa kwa matumbo yao kama nyoka kutafuta eneo ambalo lingewaruhusu kuona vyema nini kilikuwa kinaendelea kwenye mkusanyiko uliokuwepo hapo kwa Mrs. Jacob. Wale watu waliokuwa kwa Mrs. Jacob walikuwa wanaanza kuondoka. Ilikuwa imeanza kuwa dhahiri nani haswa alikuwa Mrs. Jacob. Kama Hobie alikuwa sahihi na hii ndiyo nyumba yake, basi Mrs Jacob alikuwa ni yule mwanamke mwembamba mwenye nywele asili za njano aliyekuwa akibadilishana mikono ya kwaheri hapa na pale na wageni wake. Walikuwa wanaondoka, Yeye alikuwa anabakia. Hakuna shaka yeye ndiye Mrs. Jacob.
Walimtazama bila kusemeshana. Yeye ndiye alikuwa sababu ya umati ule. Watu wengine walianza kuelekea walipoegesha magari yao mmojammoja na hata wawiliwawili. Halafu wakaanza kuondoka kwa makundi makubwamakubwa. Magari yalikuwa yakiwashwa. Msuguano wa matairi na barabara na miungurumo ya gari hili na lile ilitawala. Kazi ilikuwa inaenda kuwa rahisi kama kipande cha mkate kwa chai. Muda sio mrefu Mrs. Jacob angebaki akiwa amesimama pale peke yake akiwa na upweke na huzuni. Halafu angepata wageni wawili zaidi. Labda angewachukulia kama waombolezaji waliofika msibani wakiwa wamechelewa. Hata hivyo, walikuwa wamevaa suti za vitambaa vyeusi na tai zao zilikuwa nyeusi ambazo kiujumla zilichukuliwa kama nguo sahihi za msiba hapo Manhattan.
Reacher aliwafuata kuwasindikiza wageni wawili wa mwisho kuondoka. Mmoja alikuwa ni koloneli na mwingine alikuwa ni jenerali tu mwenye nyota mbili begani kwake. Wote walikuwa wamevaa sare za jeshi. Haikumshangaza. Sehemu yenye chakula na vinywaji vya bure wanajeshi ndiyo huwa watu wa mwisho kabisa kuondoka hapo. Hakuwa akimfahamu yule koloneli, lakini hisia zilimwambia alikuwa amewahi kukutana mahali na yule Jenerali. Walikuwa wakitazamana kila wakati. Hata hivyo, hakuna aliyethubutu kumuuliza mwenzake kuhusu mashaka yao hayo. Hakuna haja ya kujiingiza kwenye mijadala mirefu na migumu ya kujibu swali la kwahiyo-siku-hizi-unafanya-nini.
Wale wanajeshi wawili walipanda kwenye gari moja la mwisho lililokuwa limebaki kati ya mengi yaliyokwishaondoka. Wa kwanza kufika, wa mwisho kuondoka. Muda wa amani, Hakuna vita baridi, Hakuna kazi ya kufanya kwa siku nzima. Ndiyo maana Reacher alifurahi siku alipokatwa jeshini. Na alipolitazama lile gari la kijani likiondoka alijua alikuwa sahihi kufurahi.
Jodie alikuwa amesogea hadi alipokuwa amesimama na kuupeleka mkono wake tena kugusana na wa Reacher.
"Hatimaye," Alisema kwa ukimya. "Hili nalo limeisha."
Ulipita ukimya kidogo isipokuwa kwa kelele za lile gari la wale wanajeshi wawili likiwa linaishia zake.
"Amezikwa wapi?"
"Makaburi ya mjini," Jodie alisema. "Najua angepata nafasi ya kusema azikwe wapi angechagua Arlington. Unataka ukatembelee kaburi lake?"
Reacher alitikisa kichwa kukataa. "Hakuna haja. Haiwezi kuleta utofauti wowote kwake, au inaweza? Alikuwa anajua atakapokufa nitakuwa nimepoteza mtu muhimu. Inatosha."
Jodie alitikisa kichwa kukubali.
"Ni muda tuzungumze kuhusu Costello," Reacher alisema tena.
"Kwanini?" Jodie aliuliza. "Nadhani alikwishakupa ujumbe wake."
"Hakunipa ujumbe wowote. Ni kweli alinipata, lakini nilimwambia mimi sio Jack Reacher."
Jodie alimtazama kwa macho ya mshangao. "Kwanini?"
"Tabia yangu nadhani. Sitembei nikitafuta marafiki au mahusiano. Jina la Jacob sikuwa nalifahamu kwahivyo nilimpuuza tu. Nikaendelea na hamsini zangu."
Jodie alikuwa bado anamkodolea macho Reacher.
"Nadhani ningetumia jina la Garber," Jodie alisema. "Hata hivyo lilikuwa ni suala lililomhusu baba na mimi nilitumia jina la kazini, sikuwa nafikiria utalipuuza."
"Na?"
"Na hukupaswa kulipuuza au kuongopa kwa sababu haikuwa ni suala kubwa."
"Tunaweza kwenda ndani kuongea?" Reacher aliuliza.
Jodie alipata mshtuko tena. "Kwanini?"
"Kwasababu unachosema halikuwa suala kubwa limezua mambo mazito sana."
SEHEMU YA KUMI NA NNE
"Wewe ndiye Mrs. Jacob?" Reacher aliuliza.
Jodie Graber alitikisa kichwa kukubali.
"Ndiye mimi, Nilikuwa," Jodie alijibu. "Ni Jina la mume wangu. Tumeachana, lakini bado nalitumia kazini."
"Alikuwa ni nani?"
"Wakili, kama mimi."
"Mmedumu kwenye ndoa kwa muda kiasi gani?"
"Miaka mitatu tu. Tulikutana chuo na kuamua kufunga ndoa tulipohitimu na kupata kazi kila mmoja. Mimi nilibaki Wall Street, Yeye akaenda DC. Nasikitika alipoondoka ndoa yetu aliiacha. Hakuondoka nayo na nilikuja kujua alipotuma karatasi za kuomba tuachane. Jina lake ni Alan Jacob."
Reacher alisimama na kumuangalia Jodie. Aligundua ilikuwa huzuni kwake kusikia Jodie alikuwa ameolewa na kuachika.
Jodie alikuwa mwembamba lakini mwenye mvuto tangu akiwa na miaka kumi na tano tu, alikuwa mwenye kujiamini na mwenye soni kidogo. Reacher alikuwa ameshuhudia mara nyingi vita kati ya haya na udadisi usoni pake kila mara walipoongea kuhusu kifo na uhai na mema na mabaya enzi hizo. Halafu wangebadilisha mada na kuongea kuhusu upendo na mapenzi na wanaume na wanawake. Halafu Jodie angeona aibu na kuaga kuondoka. Reacher angebaki mwenyewe akiwa kama barafu kwa ndani. Siku chache baadaye angemuona tena Jodie akizungukazunguka kwenye mazingira ya kambi. Na sasa miaka kumi na tano baadae alikuwa ni mwanamke mkubwa, mwenye elimu ya haja ya sheria, aliyeolewa na kuachika, mzuri na mwenye busara akiwa amesimama hapo mbele yake huku wameshikana mikono.
"Umekwishaoa?" Jodie alimuuliza Reacher.
Alitikisa kichwa kukataa, "Hapana."
"Lakini una furaha?"
"Mimi nina furaha kila siku," Reacher alijibu. "Ninayo furaha tangu zamani, na nitakuwa nayo kila siku."
"Unashughulika na nini sasa?"
Reacher aliinua mabega. "Sifanyi vingi," Alijibu.
Alianza kuzungusha macho yake kwa wale waombolezaji waliokuwepo kwenye ile kadamnasi. Watu ambao wako bize muda wote. Wana maisha ya kifahari. Kazi za heshima, wote wakiwa ni watu wanaojua wanapotoka na wanapoenda. Kama mtoto anayejua vyema kuimba alfabeti A mpaka Z kwa mpangilio. Aliwatazama kwa nukta na kuwaza kama wao ndiyo walikuwa wendawazimu, au yeye ndiye alikuwa mwendawazimu.
"Nilikuwa Keys," Alisema. "Nilikuwa nachimba mabwawa ya kuogelea kwa chepeo."
Mwonekano wa uso wa Jodie haukubadilika. Jodie alijaribu kuushika mkono wa Reacher kwa nguvu. Ilikuwa kazi bure. Mkono wake ulikuwa mdogo sana ukilinganisha na kiganja cha Reacher.
Costello alikupata huko?" Jodie aliuliza.
Hakuwa akinitafuta kunialika kwenye msiba, Reacher aliwaza. "Tunahitaji kuzungumza kuhusu Costello," Alisema.
"Ni mtu makini, sio?"
Hakuwa makini sana, Reacher aliwaza tena.
Jodie aliuachia mkono wa Reacher na kuanza kuwazungukia umati wa waombolezaji. Watu walikuwa wamesimama wanasubiri kutoa pole zao kwa mara nyingine tena. Hata hivyo, vinywaji walivyokuwa wamekunywa vilianza kuwaelemea na walikuwa wakiongea kwa sauti kubwa. Reacher naye aliteleza kutoka alipokuwa amesimama hadi kwenye meza iliyokuwa imefunikwa kwa kitambaa cheupe. Hapo alichukua sahani ya karatasi na kuiwekea kuku na wali na kuchukua glasi ya maji. Kulikuwa na kiti kilichoonekana kuzeeka. Pengine ndiyo maana watu wengi walikipuuza. Reacher aliketi kwenye hicho kiti peke yake.
Alikuwa akiyazungusha macho yake kwenye ule umati wa waombolezaji huku akila taratibu. Watu walikuwa wagumu kuondoka. Hii ilithibitisha upendo wao kwa Garber ulivyokuwa mkubwa. Jodie alikuwa akitoka kwa huyu na kwenda kwa yule akitoa na kupokea mikono, huku uso wake ukiwa na tabasamu la huzuni. Kila mmoja alionekana alikuwa na kisa cha kumwambia. Kisa kuhusu moyo wa dhahabu wa Garber kwa matendo yake. Reacher angeweza kumwambia Jodie visa vingine vingi vya Garber, lakini visingekuwa na umuhimu. Jodie hakuwa anahitaji kusikia kisa chochote kujua kwamba baba yake alikuwa mtu mbele ya watu. Ni kitu alichokuwa anakifahamu. Kwa muda wa uhai wa Garber hakuwahi kumficha Jodie kitu chochote. Watu wanaishi, halafu wanakufa, na kama watayaishi maisha yao katika njia nzuri hakuna kitu cha kujutia hata wakifa.
Waliipata sehemu ya kuhifadhi gari lao mtaa wa pili, Ilikuwa sehemu yenye ukimya bila watu. Waliliegesha gari yao nyuma ya gereji ambako isingeonekana kwa urahisi. Lakini walihakikisha inakaa katika mkao wa kuondoka. Walitoa bastola zao kwenye boksi lililokuwamo kwenye gari na kuzipachika kwenye mifuko ya mikoti ya suti zao. Wakaanza kutembea kurudi barabarani kwa uangalifu mkubwa kwa kutumia njia za pembeni kidogo.
Ilikuwa ni safari fupi, lakini ngumu. Ni kweli walikuwa maili sitini kutoka Manhattan, lakini ilikuwa ni sawa na kuwa katikati ya misitu ya Borneo. Kulikuwa na majani na miti iliyozagaa kila pahali ikiwa na matawai marefu. Waliamua kutembea kwa kutanguliza migongo. Walipofika karibu na barabara iliyokuwa inaelekea kwa Garber walikuwa wakihema kwa nguvu huku vumbi la kijani likiwa limewavaa. Walilala chini ambapo wasingeweza kuonekana wakitembea. Walianza kutambaa kwa matumbo yao kama nyoka kutafuta eneo ambalo lingewaruhusu kuona vyema nini kilikuwa kinaendelea kwenye mkusanyiko uliokuwepo hapo kwa Mrs. Jacob. Wale watu waliokuwa kwa Mrs. Jacob walikuwa wanaanza kuondoka. Ilikuwa imeanza kuwa dhahiri nani haswa alikuwa Mrs. Jacob. Kama Hobie alikuwa sahihi na hii ndiyo nyumba yake, basi Mrs Jacob alikuwa ni yule mwanamke mwembamba mwenye nywele asili za njano aliyekuwa akibadilishana mikono ya kwaheri hapa na pale na wageni wake. Walikuwa wanaondoka, Yeye alikuwa anabakia. Hakuna shaka yeye ndiye Mrs. Jacob.
Walimtazama bila kusemeshana. Yeye ndiye alikuwa sababu ya umati ule. Watu wengine walianza kuelekea walipoegesha magari yao mmojammoja na hata wawiliwawili. Halafu wakaanza kuondoka kwa makundi makubwamakubwa. Magari yalikuwa yakiwashwa. Msuguano wa matairi na barabara na miungurumo ya gari hili na lile ilitawala. Kazi ilikuwa inaenda kuwa rahisi kama kipande cha mkate kwa chai. Muda sio mrefu Mrs. Jacob angebaki akiwa amesimama pale peke yake akiwa na upweke na huzuni. Halafu angepata wageni wawili zaidi. Labda angewachukulia kama waombolezaji waliofika msibani wakiwa wamechelewa. Hata hivyo, walikuwa wamevaa suti za vitambaa vyeusi na tai zao zilikuwa nyeusi ambazo kiujumla zilichukuliwa kama nguo sahihi za msiba hapo Manhattan.
Reacher aliwafuata kuwasindikiza wageni wawili wa mwisho kuondoka. Mmoja alikuwa ni koloneli na mwingine alikuwa ni jenerali tu mwenye nyota mbili begani kwake. Wote walikuwa wamevaa sare za jeshi. Haikumshangaza. Sehemu yenye chakula na vinywaji vya bure wanajeshi ndiyo huwa watu wa mwisho kabisa kuondoka hapo. Hakuwa akimfahamu yule koloneli, lakini hisia zilimwambia alikuwa amewahi kukutana mahali na yule Jenerali. Walikuwa wakitazamana kila wakati. Hata hivyo, hakuna aliyethubutu kumuuliza mwenzake kuhusu mashaka yao hayo. Hakuna haja ya kujiingiza kwenye mijadala mirefu na migumu ya kujibu swali la kwahiyo-siku-hizi-unafanya-nini.
Wale wanajeshi wawili walipanda kwenye gari moja la mwisho lililokuwa limebaki kati ya mengi yaliyokwishaondoka. Wa kwanza kufika, wa mwisho kuondoka. Muda wa amani, Hakuna vita baridi, Hakuna kazi ya kufanya kwa siku nzima. Ndiyo maana Reacher alifurahi siku alipokatwa jeshini. Na alipolitazama lile gari la kijani likiondoka alijua alikuwa sahihi kufurahi.
Jodie alikuwa amesogea hadi alipokuwa amesimama na kuupeleka mkono wake tena kugusana na wa Reacher.
"Hatimaye," Alisema kwa ukimya. "Hili nalo limeisha."
Ulipita ukimya kidogo isipokuwa kwa kelele za lile gari la wale wanajeshi wawili likiwa linaishia zake.
"Amezikwa wapi?"
"Makaburi ya mjini," Jodie alisema. "Najua angepata nafasi ya kusema azikwe wapi angechagua Arlington. Unataka ukatembelee kaburi lake?"
Reacher alitikisa kichwa kukataa. "Hakuna haja. Haiwezi kuleta utofauti wowote kwake, au inaweza? Alikuwa anajua atakapokufa nitakuwa nimepoteza mtu muhimu. Inatosha."
Jodie alitikisa kichwa kukubali.
"Ni muda tuzungumze kuhusu Costello," Reacher alisema tena.
"Kwanini?" Jodie aliuliza. "Nadhani alikwishakupa ujumbe wake."
"Hakunipa ujumbe wowote. Ni kweli alinipata, lakini nilimwambia mimi sio Jack Reacher."
Jodie alimtazama kwa macho ya mshangao. "Kwanini?"
"Tabia yangu nadhani. Sitembei nikitafuta marafiki au mahusiano. Jina la Jacob sikuwa nalifahamu kwahivyo nilimpuuza tu. Nikaendelea na hamsini zangu."
Jodie alikuwa bado anamkodolea macho Reacher.
"Nadhani ningetumia jina la Garber," Jodie alisema. "Hata hivyo lilikuwa ni suala lililomhusu baba na mimi nilitumia jina la kazini, sikuwa nafikiria utalipuuza."
"Na?"
"Na hukupaswa kulipuuza au kuongopa kwa sababu haikuwa ni suala kubwa."
"Tunaweza kwenda ndani kuongea?" Reacher aliuliza.
Jodie alipata mshtuko tena. "Kwanini?"
"Kwasababu unachosema halikuwa suala kubwa limezua mambo mazito sana."
SEHEMU YA KUMI NA NNE