Riwaya: Senyenge

Riwaya: Senyenge

SEHEMU YA ISHIRINI
Dokta McBannerman alikuwa bado ameweka mgomo kutoa taarifa binafsi za wateja wake. Kwahivyo alitoa anuani ya Bwana na Bibi Hobie, lakini namba zao za simu alizing’ang’ania. Jodie hakuona kama kuna utofauti. Hakuendelea kuuliza maswali. Alishikana naye mikono ya kwaheri na kutoka nje huku Reacher akimfuata kwa nyuma.

“Hali sio nzuri,” Jodie alisema. “Umewaona wale wagonjwa waliokuwa pale mapokezi?”

“Ndiyo,” Reacher alijibu. “Nusu watu nusu wafu.”

“Baba alikuwa kwenye hiyo hali pia dakika za mwishomwisho. Halafu walikuwa wanafuatilia nini hiki ambacho kimempa mtu hasira hadi anaanza kuua watu hovyo?”

Reacher hakujibu. Waliingia kwenye Bravada yao, Jodie akikaa kiti cha abiria na Reacher akikaa nyuma ya usukani. Jodie alipiga simu kuomba taarifa. Aliambiwa namba za simu za familia ya Mzee Hobie ambaya makazi yake yalikuwa kaskazini mwa Garrison. Aliandika zile namba kwenye karatasi aliyokuwa amechana kutoka kwenye notebook yake. Alipokata simu akaziandika na kupiga. Simu ililia kwa muda kidogo kabla upande wa pili haujabonyeza kitufe cha kupokea halafu sauti ya mwanamke ikasikika.

“Abee?” Sauti ilisema.

“Mrs. Hobie?” Jodie aliuliza

“Ndiyo?” Sauti ilijibu tena. Jodie akaanza kuwaza muonekano wa Mrs. Hobie – Mwanamke mzee mwenye mvi kichwani, mwembamba na pengine amevaa nguo zinazoonekana kumvaa zilizochoka huku akiwa kashika mkonga wa simu ya kizamani kwenye sebule ya nyumba ambayo imechoka pia.

“Mrs. Hobie, ninaitwa Jodie Garbar. Ni binti yake na Leon Garbar.”

“Ndiyo?”

“Amefariki siku tano zilizopita.”

“Ndiyo, ninafahamu.” Mrs. Hobie alisema na kuongeza, “Nimesikitishwa sana na hiyo taarifa. Baba yako alikuwa anatusaidia na alikuwa mtu mzuri sana. Sijui kwanini watu wazuri wanawahi kufa. Pole sana.”

“Nashukuru,” Jodie alijibu. “Lakini sijui kama unaweza kuniambia alikuwa anawasaidia jambo gani?”

“Kwa sasa hakuna umuhimu hata nikikuambia.”

“Kwanini?”

“Kwa sababu baba yako amekwishafariki,” Mrs. Hobie alisema. “Yeye ndiye alikuwa tumaini letu la mwisho.”

Kila neno alilosema lilikuwa limemaanishwa. Sauti yake ilikuwa ya chini. Kulikuwa na mchanganyiko wa hisia za kukata tamaa mwisho wa sentensi yake, kama mtu aliyeamua liwalo na liwe sitaki tena. Jodie akaiona tena picha ya Mrs. Hobie kichwani mwake. Mwanamke mzee – mifupa bila nyama na mashavu yaliyolowa kwa machozi yaliyokuwa yanadondoka kutoka machoni.

“Pengine ninaweza kukusaidia.” Jodie alisema.

Ukimya ukapita kabla sauti ya Mrs. Hobie haijarudi tena kwenye spika za simu. “Sidhani,” Alisema. “Sidhani kama hili ni tatizo linaloweza kushughulikiwa na mwanasheria.”

“Ni tatizo la aina gani?”

“Sidhani kama kuna umuhimu wa kuliongelea tena,” Mrs. Hobie alisema.

“Hauwezi kuniambia hata kidogo tu?”

“Hapana. Nadhani kila kitu kimeshaisha.” Mrs. Hobie alisema. Sauti yake ilikuwa bado ni ya mtu aliyekata tamaa.

Ukimya ulipita kidogo. Jodie akageuza macho na kuangalia jengo la ofisi ya Dokta Mcbannerman.

“Lakini baba yangu angeweza vipi kukusaidia? Ni kwa sababu alikuwa analijua tatizo lako? Au ni kwa sababu alikuwa jeshini?”

“Ndiyo. Na ndiyo maana nahofia hauwezi kunisaidia kwa vyovyote. Inahitaji mtu wa jeshini. Hata hivyo asante kwa kujali.”

“Huyo mtu yupo,” Jodie alisema. “Na nipo naye hapa. Alikuwa anafanya kazi na baba yangu jeshini na yupo tayari kuwasaidia.”

Ukimya ukapita tena kwenye simu. Kulikuwa na muungurumo wa spika unaotengenezwa na mgongano wa mawimbi kama simu nyingi zinavyosikika watu wawili wakiwa wanaongea halafu wakae kimya. Ni kama Mrs. Hobie alikuwa anafikiria. Akubali au abadilishe mada.

“Jina lake ni Reacher,” Jodie alisema. “Pengine baba aliwahi kulitaja hilo jina? Na baba ndiye aliyemtafuta awasaidie.”

“Alimtafuta?”

“Ndiyo. Nadhani alikuwa na uhakika huyu Reacher angewasaidia.”

“Huyo mtu alikuwa ni Polisi Jeshini?”

“Ndiyo. Kwani kama alikuwa mwanajeshi wa kawaida kuna tatizo?”

“Sina hakika,” Mrs. Hobie alisema. Halafu akanyamaza. Alikuwa anahema kwa nguvu. “Anaweza kuja nyumbani?” Aliuliza hatimaye.

“Nitakuja naye,” Jodie alimwambia. “Tunaweza kuja sasa hivi?”

Ukimya tena. Kuhema. Kutafakari.

“Mume wangu amemaliza kumeza vidonge muda sio mrefu na sasa hivi amelala. Hali yake sio nzuri.”

Jodie alitikisa kichwa kukubali. “Mrs. Hobie kwani wewe hauwezi kutuambia walikuwa wanafuatilia nini?”

Ukimya tena. Kuhema. Kutafakari.

“Nitamwachia mume wangu awaambie. Nadhani maelekezo yake yamenyooka tofauti na ya kwangu. Ni hadithi ndefu kidogo.”

“OK, atakuwa ameamka saa ngapi?” Jodie aliuliza. “Au tuje baadae?”

Ukimya mwingine.

“Huwa analala sana baada ya kumeza vidonge vyake, Mwambie Rafiki yako aje kesho asubuhi.”



HOBIE ALITUMIA NCHA ya chuma lake kubonyeza kitufe cha simu yake ya mezani. Aliinama kwa mbele na kumuita yule mwanaume wa mapokezi kwa jina lake. Hii haikuwa tabia yake isipokuwa kama alikuwa na jambo linalomsumbua kichwa chake.

“Tony,” Alisema. “Tunahitaji kuongea.”

Tony alikuja na kukaa kwenye sofa lililokuwa karibu kabisa na meza ya Hobie.

“Aliyeenda Hawaii ni Garber,” Tony alisema.

“Una uhakika?” Hobie aliuliza.

Tony alitikisa kichwa kukubali. “Alipanda ndege ya American hadi Chicago na kutoka Chicago hadi Honolulu. Halafu akarudi kesho yake, Aprili kumi na sita. Alilipa kwa Amex na taarifa zote hizo zipo kwenye kompyuta zao.”

“Lakini huko alienda kufanya nini?” Hobie aliuliza.

“Hatuna uhakika.” Tony alinong’ona. “Lakini tunaweza kubashiri.”

Ukimya ukapita. Tony akayakaza macho yake kwenye uso wa Hobie upande ambao haukuwa umeliwa na lile kovu kubwa.

“Nimesikia pia fununu kutoka Hanoi,” Hobie alisema.

“Mungu wangu, lini?”

“Dakika kumi zilizopita.”

“Mungu wangu, Hanoi,” Tony alisema. “Shit, shit, shit.”

“Miaka thelathini,” Hobie alisema. “Na hatimaye mwisho umefika.”

Tony hakujibu. Baadala yake alisimama akaenda kusimama kwenye dirisha na kufungua pazia. Nje kulikuwa na jua kali ambalo liliingiza mwanga kiasi mule ndani.

“Unatakiwa kuondoka sasa hivi. Mambo yamekwishakuwa mabaya.”

Hobie hakujibu. Alikuwa analipapasa chuma lake kwa vidole vyake vya mkono wa kushoto.

“Uliniahidi,” Tony alisema. “Onyo la kwanza, Onyo la pili utaondoka na onyo zote tayari zimekuja.”

“Bado itawachukua muda,” Hobie alisema. “Kwa sasa hivi hawawezi kufanya chochote.”

Tony alitikisa kichwa kukataa. “Garbar hakuwa mwehu. Lazima kuna kitu alikuwa anafahamu. Na kama alienda hadi Hawaii lazima kuna sababu nzuri iliyokuwa imempeleka huko.”

Hobie aliutumia mkono wake wa kushoto kuliongoza chuma lake la kulia hadi lilipotua juu ya uso wake. Alianza kulikandamiza kovu lake huku akisuguasugua sehemu ya kovu lake kupunguza mwasho.

“Na huyu Reacher?” Aliuliza. “Kuna Habari gani?”

“Nilipiga simu St. Louis,” Tony alisema. “Naambiwa alikuwa polisi wa wanajeshi pia. Alihudumu na Garbar kwa muda wa miaka kumi na tatu. Na wote walikuwa wamewasiliana na Costello.”

“Kwanini?” Hobie aliuliza na kujijibu, “Familia ya Garbar iliwasiliana na Costello kumtafuta Reacher. Kwanini? Kwanini?”

“Sina uhakika,” Tony alijibu. “Ninachojua alikuwa huko Keys akichimba mabwawa ya kuogelea.”

“Polisi wa wanajeshi mchimba mabwawa?”

“Usijiulize maswali,” Tony alisema. “Unatakiwa kuondoka.”

“Hakuna kitengo sikipendi kama polisi wa wanajeshi,” Hobie alisema.

“Ninafahamu hilo.”

“Kwahivyo huyo mjinga anafanya nini huku?”

“Usijiulize sana. Unatakiwa kuondoka.” Tony alisisitiza kwa mara ya tatu.

Hobie alitikisa kichwa kukubali. “Nadhani unanijua mimi ni mtu wa kubadilika kuendana na mazingira.”

Tony aliachia pazia. Chumba kikaingiwa tena na giza. “Sijasema ubadilike. Nimesema ukae kwenye mpango tulikuwa tumepanga.”

“Mpango upo palepale, lakini siwezi kuondoka kabla sijamalizana na Stone.”

Tony alirudi kukaa kwenye sofa lake lilelile. “Ninafahamu, lakini ni hatari sana kuendelea kubakia. Maonyo yote mawili yametokea. Moja Veitnam na linguine Hawaii. Ondoka.”

“Ni kweli, lakini mipango huwa inabadilishwa kidogo.”

“Kivipi?”

Hobie aliguna na kutikisa kichwa chake. “Tutaondoka ndiyo, lakini ni baada ya kumalizana na Stone.”

Tony aliguna na kuinua mikono yake kama anayeuliza kitu. “Wiki sita ni muda mrefu sana. Garbar alikuwa amekwishaenda Hawaii na alikuwa mmoja wa majenerali. Lazima kuna kitu atakuwa anafahamu.”

Hobie alitikisa kichwa kukubali, “Unachokisema ni kweli. Lakini huyohuyo Garbar aliugua na akafa na hivyo vitu alivyokuwa anavijua vilienda naye huko kuzimu.”

“Unajaribu kusema nini?”

Hobie alilishusha chuma lake chini na kuliweka mezani. Akakigusa kidevu chake kwa vidole vya mkono wake mzuri. Aliviacha vidole visambae kwenye kovu lake. Lilikuwa ni pozi alilolitumia , bila kujua, kila mara alipotaka kuongelea mpango muhimu.

“Siwezi kuondoka na kumuacha Stone,” Alianza kueleza. “Nikimuacha hicho kitendo kitanifanya nijute hadi siku ambayo nitaingia kaburini. Kukimbia, nakubaliana na wewe, ni jambo zuri. Lakini bado ni mapema kiasi kwamba tukikimbia sasa hivi tutakuwa ni waoga, Tony.”

“Sijakuelewa bado. Unataka kusema nini?”

“Tunatakiwa kuua ndege wawili kwa jiwe moja. Ni kweli wiki sita ni muda mrefu na tunatakiwa kuondoka kabla ya hizo wiki sita, lakini sio kabla hatujamalizana na Stone. Ndiyo maana inatakiwa tuharakishe mambo tufanye kila kitu harakaharaka.”

“Ok, Kivipi?”

“Ninaingiza hisa za Stone sokoni leo, sasa hivi.” Hobie alianza kueleza tena. “Haitachukua muda thamani yake itakuwa chini sana na mabenki yatashtuka. Kesho asubuhi Stone atakuja hapa jasho likiwa linamtoka. Mimi sitakuwepo. Kwahivyo wewe utamwambia sisi tunataka nini, na tutakipata vipi, na tutafanya nini kama asipotoa ushirikiano. Niamini mimi. Atatupa kila kitu chake ndani ya siku chache tu. Tutauza kila kitu halafu tunaondoka.”

“Ok, kivipi. Bado sijaelewa.”

Hobie aligeuza kichwa kuangalia kona za kwenye kile chumba.

“Wale wanaume mikia wawili hawatakuwa ni tatizo. Mmoja wao anamuua mwenzake usiku wa leo, na atakayebaki utashirikiana naye hadi tumpate Mrs. Jacob, ambapo wewe utawafuta wote. Tutauza boti, tutauza nyumba zote, tutaondoka, bila kuacha nyayo. Inaweza ikachukua wiki. Wiki moja tu. Nadhani tunaweza tukajipa wiki moja tu, sio?”

Tonny alitikisa kichwa kukubali. “Na vipi kuhusu Reacher?”

Hobie alitikisa kichwa pia, “Nina mpango tofauti kwaajili yake.”

“Hatuwezi kumpata,” Tony alisema. “Sisi tukiwa wawili tu hatuwezi kumpata ndani ya wiki moja.”

“Hakuna haja ya kumtafuta.”

Tony alitumbua macho. “Tusipompata tunaacha nyao.”

Hobie alitikisa kichwa chake. Halafu akaushusha mkono wake kutoka usoni. “Nitamshughulikia kwa makini sana. Hakuna haja ya kumaliza nguvu zangu kumtafuta. Nitamuacha anitafute. Ninajua atanitafuta na atanipata. Ni kawaida ya polisi wa wanajeshi.”

“Halafu nini.?”

Hobie alitabasamu. “Halafu ataishi maisha marefu na ya furaha,” Hobie alisema. “Pengine miaka thelathini tena.”

ITAENDELEA...
Nimetoka sasa hivi kucheck movie ya Jack Reacher muda sio mrefu ya tom cruise sijui ndo yenyewe
 
Ndugu wasomaji, nilipata matatizo ya kuharibikiwa na hard disk iliyokuwa inahifadhi vitu vyangu. So muda ambao nilikuwa kimya nilikuwa najaribu kuiandika tena hii riwaya kwa kumbukumbu - ninaendelea vizuri, naamini siku sio nyingi tutaendelea na burudani yetu. Naomba mniwie radhi.
 
Ndugu wasomaji, nilipata matatizo ya kuharibikiwa na hard disk iliyokuwa inahifadhi vitu vyangu. So muda ambao nilikuwa kimya nilikuwa najaribu kuiandika tena hii riwaya kwa kumbukumbu - ninaendelea vizuri, naamini siku sio nyingi tutaendelea na burudani yetu. Naomba mniwie radhi.
Nilipoona umePost nilijua umeweka vitu nikaja faster kumbe porojo!
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA
"Kwahivyo tunafanya nini sasa?" Reacher aliuliza.

Walikuwa bado wapo kwenye maegesho ya nje ya ofisi ya McBannerman, huku jua likiimulika ile Bravada ya Jodie. Kiyoyozi kilikuwa kimewashwa pia. Hii ilimfanya Reacher aisikie vyema harufu ya unyunyu aliokuwa ameuvaa Jodie. Kwa wakati huo, Reacher alikuwa ni mwanaume mwenye furaha kuliko wanaume wote akiishi kwenye kuimbukumbu ya zamani. Miaka ya nyuma, mara kwa mara angewaza ingekuwaje kama angekuwa na Jodie katika umbali wa kugusana siku akiwa mkubwa. Ni jambo ambalo hakuwahi kutarajia lingeweza kutokea. Alidhani wangepotezana tu na wasingewahi kuonana tena. Alidhani hisia zake zingeyeyuka na kufifia. Lakini leo alikuwa hapo, akivuta hewa ya unyunyu wake, akimuangalia miguu kwa jicho la wiziwizi. Zamani alidhani Jodie angekuwa akawa mwanamke wa kawaida tu, lakini sasa hivi alikuwa anajihisi mwenye hatia kwa kuuchukulia poapoa uzuri wa Jodie.

"Ni tatizo tayari," Jodie alisema. "Siwezi kwenda huko kesho muda hauniruhusu."

Miaka kumi na tano. Ilikuwa ni muda mrefu au muda mfupi? Huo muda unaweza kumbadilisha mtu? Kwa Reacher miaka kumi na tano aliiona kama muda mfupi. Hakujisikia kama amebadilika sana. Alikuwa ni mtu yuleyule, anaefikiria vilevile na mwenye uwezo wa kufanya vitu kama miaka kumi na tano iliyopita. Ni kweli alikuwa ameongeza uzoefu wa mawili matatu kwa muda huo, alikuwa amezeeka lakini kiujumla alikuwa ni mtu yuleyule. Lakini alihisi Jodie angekuwa amebadilika. Hakuna wasiwasi. Miaka yake kumi na tano iliyopita ilikuwa ni ya mazingira tofautitofauti. Shule ya sekondari, chuo, shule ya sheria, ndoa, talaka. Lazima angekuwa mtu tofauti. Reacher alihisi alikuwa anashughulika na mambo matatu kwa wakati mmoja: Uhalisia wa Jodie kama mtoto miaka kumi na tano iliyopita, halafu namna Reacher alivyotarajia atakuwa, na mwisho kabisa namna alivyomkuta amekuwa. Alikuwa na uhakika wa mambo mawili ya kwanza, ila sio jambo la tatu. Alikuwa anamjua Jodie kama mtoto, alikuwa anamjua Jodie kama mtu mzima aliyemuumba kwenye fikra zake. Lakini hakuwa anajua Jodie wa sasa jambo ambalo lilimtia mashaka kwasababu hakuwa tayari kufanya kosa lolote la ajabu mbele ya Jodie.

"Itabidi uende mwenyewe," Jodie alisema. "Ni sawa?"

"Ni kweli," Reacher alijibu. "Lakini hilo sio tatizo hapa, tatizo ni kwamba unatakiwa uwe makini sana."

Jodie alitikisa kichwa kukubali. "Sawa. Nitakuwa makini."

"Ofisi yako ipo wapi?"

"Wall Street na Lower Broadway."

"Lower Broadway ndipo unaishi?"

"Ndiyo. Huwa natembea kufika nyumbani. Navuka nyumba kama 15 tu."

"Kuanzia kesho nitakuwa nakuendesha kwa gari. Hautakiwi kutembea tena."

Jodie alionesha mshangao. "Utaniendesha?"

"Ndiyo." Reacher alijibu. " Kuvuka nyumba kumi na tano kwa mguu ni hatari zaidi. Wanaweza kukukwapua mtaani, vipi ofisi yako ipo salama kweli?"

Jodie alitikisa kichwa kukubali. "Hakuna mtu anaruhusiwa kuingia bila kitambulisho au bila kuwa na miadi na mtu wa mule."

"Ok, kwahivyo nitakuwepo nyumbani kwako usiku wote na asubuhi nitakuendesha mlango hadi mlango kabla sijaja kuonana na familia ya Hobie. Na wewe utatakiwa ubaki ofisini hadi nitakapokuja kukuchukua tena."

Jodie alibaki kimya. Reacher akayapitia maneno aliyoyasema.

"Namaanisha kwako lazima una chumba cha wageni?"

"Ndiyo," Jodie alijibu.

"Basi sawa."

Jodie alitikisa kichwa kukubali.

"Kwahivyo?" Reacher aliuliza.

Jodie aligeuza uso kumtazama halafu akatabasamu. "Tunaenda shopping."

"Shopping? Unataka kununua nini?"

"Siyo ninataka kununua nini," Jodie alisema. "Ila ni wewe unataka nini!"

Reacher alimtazama Jodie kwa jicho la wasiwasi. "Ninataka nini?"

"Nguo mpya," Jodie alisema. "Itakuwa jambo la ajabu kwenda kuwatembelea wale wazee huku unaonekana kama mzimu. Na tunahitaji kupita duka la dawa pia. Jeraha lako halitopona kwa muujiza."



"UNAFANYA UJINGA GANI?" Mkurugenzi wa fedha alifoka.

Alikuwa kwenye mlango wa ofisi ya Chester Stone, ghorofa ya juu ilipo ofisi yake mwenyewe. Alikuwa ameshikilia fremu ya mlango akihema kwa nguvu na uchovu. Hakuwa amekuja kwa lifti. Kuisubiria kungemchelewesha. Alikuwa amepanda ngazi kwa kukimbia. Stone alikuwa anamuangalia kwa mshangao.

"Wewe mwehu," alifoka tena. "Nilikuambia usifanye huu upuuzi."

"Nisifanye nini?" Stone aliuliza.

"Kuweka hisa sokoni. Nilikuambia usifanye huo upuuzi."

"Mbona sijaweka hisa sokoni," Stone alisema.

"Basi hisa zipo sokoni na watu wanazikimbia kama ni bomu au mvua ya tindikali."

"Nini?"

Mkurugenzi wa fedha alivuta pumzi ndefu. Akamkodolea macho mwajiri wake. Hapo akaona mwanaume mnyonge aliyevaa suti ya gharama ya uingereza akiwa amekaa kwenye dawati ambalo lilikuwa la bei ghali kuliko pesa zilizomilikiwa na kampuni.

"Wewe ni mjinga na nilikuambia usifanye huu upuuzi. Ni mara mia ungeita waandishi wa habari ukatangaza 'kampuni yangi haina thamani yoyote' kuliko huu upuuzi."

"Unaongelea nini. Sikuelewi."

"Mabenki yananipigia simu," Mkurugenzi wa fedha alianza kueleza. "Wanasema wanafuatilia kwa karibu. Hisa zako zimeingia sokoni lisaa limoja lililopita na bei inaporomoka tu. Haziuziki. Ni kama umetuma meseji kuwaambia wewe ni tatizo na wanakudai zaidi ya milioni kumi na sita kwa dhamana ya vitu ambavyo thamani yake hata senti kumi na sita haifiki."

"Sijaziweka hisa sokoni," Chester alisema.

Mkurugenzi wa fedha alitikisa kichwa kwa dharau. "Kwahivyo nani ameziweka. Mzimu wa Santa?"

"Hobie," Stone alisema. "Lazima ni yeye. Yesu wangu! Kwanini?"

"Hobie?" Mkurugenzi wa fedha alirudia.

Stone alitikisa kichwa kukubali.

"Hobie? Kwanini ulimpa hisa?"

"Sikuwa na jinsi." Stone alijitetea.

"Shit. Unaona anachokifanya sasa?" Mkurugenzi wa fedha alifoka.

Stone alitikisa kichwa kwa uoga. "Tunafanyaje sasa?"

Mkurugenzi wa fedha alishusha mikono yake chini kutoka kwenye fremu ya mlango. "Sahau kuhusu mimi. Hakuna neno tunafanyaje ni unafanyaje wewe, mimi ninaacha kazi. Hili tatizo utalimaliza mwenyewe."

"Lakini wewe ndiye ulimpendekeza huyu jamaa." Stone alifoka pia.

"Ni kweli, lakini sikupendekeza umpatie hisa wewe mwehu." Mkurugenzi wa fedha alifoka pia. "Wewe ni chizi kumbe. Inamaana nikipendekeza utembelee mbuga za Serengeti uwaone simba utaenda mbali zaidi kuwashika sharubu halafu unilaumu mimi?"

"Lakini nahitaji msaada wako," Stone alisema.

Mkurugenzi wa fedha alitikisa kichwa kukataa. "Mimi nimeacha kazi. Kwa sasa hivi ushauri wangu ni uende ilipo ofisi yangu ukapokee simu zinazoingia uwajibu maswali yao."

"Subiri," Stone alifoka tena. "Ninahitaji msaada wako."

"Dhidi ya Hobie? Endelea kuota rafiki yangu." Mkurugenzi wa fedha alisema.

Halafu akawa ameondoka. Aligeuka nyuma na kutokomea tu. Stone alinyanyuka kutoka kwenye dawati lake na kusimama mlangoni na kumtazama akiondoka. Ofisi ikawa kimya. Katibu muhtasi wake pia alikuwa ameondoka. Mapema zaidi ya alivyotarajia. Stone alitoka nje kusimama kwenye korido. Ofisi ya mauzo ilikuwa tupu. Mashine zilikuwa kimya. Akapanda kwenye lifti na kushuka ghorofa ya chini peke yake. Ofisi ya mkurugenzi wa fedha ilikuwa tupu. Droo zilikuwa tupu na baadhi ya vifaa binafsi vilikuwa vimeondolewa. Kompyuta ilikuwa imezimwa na simu ilikuwa inaita. Akaipokea.

"Hello?" Alisema kwenye maiki ya simu. "Mimi ni Chester Stone."

"Bwana Stone, tafadhali subiri uunganishwe na mkurugenzi."

Ukapita mziki kidogo kabla sauti ya Mkurugenzi haijaja kwenye spika za simu.

"Bwana Stone," ilikuwa sauti nzito. "Mkurugenzi hapa."

"Hello," ndilo neno pekee aliloweza kufikiria Chester.

"Nadhani unaelewa nafasi yetu kwa sasa, hatuna budi kuchukua hatua." Sauti ilisema.

"Ok," Chester alikuwa anawaza hatua zipi hizo. Jela? Mahakama?

"Tutatoka nje ya msitu pengine kuanzia kesho,"

"Nje ya msitu? Kivipi?"

"Tunaliuza deni." Sauti ilisema.

"Mnauza deni? Sijaelewa."

"Hatuhitaji kuendelea kukudai. Naamini unaelewa nafasi yetu, kwasababu hili suala limetoka nje ya mipaka. Kwahivyo tunaliuza deni. Na hicho ndicho watu hafanya, sio? Wakiwa na kitu ambacho hawakihitaji tena wanakiuza, sio?"

"Mnamuuzia nani?" Stone aliuliza.

"Kampuni moja inajiita Caymans. Wametoa ofa nzuri."

"Kwahivyo hilo suala linatuacha sisi wapi?"

"Sisi?" Sauti ilisema tena. "Haituachi popote kwa maana jukumu letu kwako limevunjwa. Hakuna sisi tena. Uhusiano wetu umekufa. Na ushauri wangu ni kwamba usiwahi kujaribu kuufufua. Tutauchukulia kama tusi kwa majeruhi. Umenielewa?"

"Kwahivyo nadaiwa na nani sasa hivi?"

"Kampuni ya Cayman," Sauti ilijibu kwa upole. "Nina uhakika anayehusika nayo atakutafuta muda sio mrefu."

SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI
 
Hongera mkuu Chachasteven.
Maneno ndio haya!
 
Okay! Changamoto za hapa na pale zimeisha. Nitakuwa naweka kila baada ya siku mojamoja yaani masaa 24 kuanzia kesho asubuhi saa 4 mapema mzigo unakuwa hewani....
Ahadi ni deni mkuu.Sasa hivi tunaelekea saa 7 mchana bado bilabila!
 
Back
Top Bottom