SIN 204
Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)
Age ……………………………………………………18+
Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188
Website………………………………………………
www.storyzaeddytz.com
ILIPOISHIA
“Baba na ana jua kwamba wewe ulimua yule mpelelezi kwa kutuma vijana na kumuwekea bomu ndani ya gari lake”
“Nabii Sanga akayatumbua macho yake huku akiwa haamini anacho kisikia kwa mwanaye huyo”
“Una sema kweli?”
“Ndio maana nika kuambia kwamba ana full details zangu, zako, za mama na familia yetu kwa ujumla”
“Ohoo Mungu wangu. Kamsikilize na atakacho kihitaji sisi tuta fanya ila kwa sharti moja”
“Sharti gani”
“Ahakikishe ana zika kila kitu anacho kijua endapo hato fanya hivyo haijalishi yeye ni balozi au hizi data zipo ndani ya nchi yao, tuta hakikisha kwamba tuna rudisha mapambano kadri ya uwezo wetu. Ume nielewa?”
“Ndio nime kuelewa baba”
Maneno ya nabii Sanga yakampa ujasiri mkubwa sana Julieth na kujikuta akijiwa na nguvu mpya huku wasiwasi na mashaka ambayo yalimtawala yakimuisha moyoni mwake na yupo tayari kukutana na balozi huyo wa nchi ya Marekani.
ENDELEA
“Uta nijulisha ukitoka huko”
“Sawa baba”
Nabii Sanga akamshika Julieth kiganja cha mkono wake wa kulia na kukiminya kidogo ikiwa ni ishara ya kumpa ujasiri wa kwenda kuonana na balozi huyo. Julieth akashuka kwenye gari lake. Akaelekea moja kwa moja katika hoteli ya Serena. Akaelekezwa na mlinzi ni wapi asimamishe gari lake na akafanya hivyo. Akatazama saa yake ya mkononi na ina onyesha zime salia sakika kumi na nne kabla ya kufika saa nane kamili mchana. Akaa ndani ya gari hadi ilipo timu saa nane kamili akashuka na kuelekea mapokezi. Akapiga namba iliyo mpigia na ika pokelewa.
“Nime fika”
“Waoo ni jambo zuri. Ata kuja mwanaume mweupe ana upara kichwani mwake na amevalia suti nyeusi na katika upande wa kushoto wa koti lake la suti kuna kibendera kidogo. Ata kuleta sehemu nilipo”
“Sawa”
Julieth akakata simu na baada ya dakika tatu akamuona mwanaume huyo ambaye akampa ishara ya kuongozana naye kueleka alipo balozi huyo. Wakaingia kwenye lifti na kupandisha hadi gorofa ya saba. Wakatembea kwenye kordo hiyo yenye walinzi sita walio valia suti nyeusi. Mwanaume huyo akamnyooshea Julieth mkono wa kulia kamaishara ana omba kitu.
“Nini?”
Julieth aliuliza huku akimkazia macho.
“Simu yako”
Julieth akamkabidhi mwanaume huyo simu yake. Mlango uka gongwa wa chumba kilichopo mbele yao uka gongwa mara mbili na akatoka mlinzi wa kike.
“Nyoosha mikono”
Julieth akatii hivyo na akanyosha mikono yake upande wa kulia na kushoto. Akakaguliwa na msichana huyo alipo onekana hana silaha ya kumdhuru kiongozi huyo akaingia ndani ya chumba hicho kikubwa sana.
“Kaa hapo”
Mlinzi huyo wa kike alizungumza huku akimuonyesha Julieth sofa zilizopo eneo hilo. Julieth akaketi kwenye moja ya sofa na balozi huyo akatoka chooni huku akiwa ana jifuta futa mikono yake na kitaulo cheupe.
“Karibu sana Julieth Sanga”
“Nashukuru”
Julieth alijibu huku akimtazama mwana mama huyo aliye jawa na tabasamu pana usoni mwake. Mwana mama huyo akaka kwenye sofa linalo tazamana na Julieth. Akampa ishara mlinzi wake huyo wa kike na akaleta faili lenye rangi nyeusi na kumkabidhi balozi Trump.
“Nchi yangu ime weza kujitosheleza kwenye kila aina ya nyanja, ukianzia kiuchumi, kisiasa, kipesa na kijasusi pia. Ume weza kuchukua nafasi katika white house ya Tanzania ila mikono yako na familia yako ikiwa ni michafu sana tena sana.”
Balozi huyo alizungumza huku akiwa ame lifunua faili hilo.
“Ila nina imani kwamba tuna uwezo wa kuwachukulia hatua za kisheria wewe, mama yako na baba yako na kila aina ya pesa haramu muliyo ipata basi tuna weza kuzizuia katika mabeki yote duniani mulipo zificha.”
Balozi Trump aliendela kuzungumza kwa vitisho ila kwa sauti ya upole sana na kana kwamba maneno anayo yazungumza hapo ni mazuri kwa Julieth.
“Nime jaribu kushangaa ni kwa nini nchi ya Tanzania hadi sasa hivi haijui upande wa giza wa baba yako pamoja na familia yake. Isitoshe nina shangaa raisi wa nchi hajui chochote kuhusiana na nyinyi. Una kula naye una shinda naye ila hajui”
“Tukiachana na baba yako. Mama yako pia ni muuaji, alimuua kimada wake baada kwa sumu kali, ila nchi yenu haijui, ila sisi tuliopo mbali kwa maelfu ya miles tuna jua. Hii inaonyesha dhahiri nchi yenu ina ongozwa kwa maono pasipo kufanya upelelezi wa kina”
Julieth akaendelea kukaa kimya huku akimkazia macho mwana mama huyo. Balozi Tramp akamkabidhi faili hilo na akaanza kulipitia taratibu na kuona picha zake, za familia yake. Akastuka sana kuiona meli ambayo ndipo kilipo kikosi chao. Akaona biashara zote haramu, wanazo zifanya huku picha zake kwa baadhi ya mikutano anayo ifanya na kikundi chake nacho ikiwemo hapo.
“Tuna kujua vizuri sana. Baba yako ni mtenda dhambi mkubwa anaye tumia jina la Mungu kuficha dhambi zake.”
“Muna hitaji nini kwetu”
Julieth aliona ni heri ajue nia na lengo la nchi hiyo.
“Muna vitu viwili tunavyo hitaji kutoka kwenu”
“Vitu gani?”
“Mkataba wa makubaliano ya nchi yetu na kundi la Bokoharamu na endapo mkataba huo tukiupata ni lazima uhakikishe kwamba una mua baba yako mkwe, raisi Mtenzi”
“Jambo la pili tuna hitaji uhakikishe kwamba tuna ipata hadhina ya dhahabu kupitia watu wako. Ukikamilisha hayo, kila unacho kiona hapo na tunacho kijua sisi tuta kwenda kukisahau.”
Julieth akaka kimya kwa dakika mbili huku akimkazia macho mwana mama huyo.
“Ni hivyo tu?”
“Yes Julieth ni hivyo tu ndio tunavyo vihitaji”
Taratibu Julieth akasimama, mlinzi akatoka kusogea karibu ila balozi Trump akampa ishara ya kumzuia.
“Nisikilize vizuri sana na uni elewe. Mume kosea mtu wa kublack mail. Labda nikupe siri moja ambayo wewe na watu wako hamuijui. Nipo tayari kufa kwa ajili ya nchi yangu na si familia yangu na sinto kuwa kibaraka wa nchi yako kwa sasabu hata nikifa mimi basi hadhina iliyopo katika nchi yangu ita kwenda kuupita uchumi wa nchi yako na muta kuwa chini ya nyayo zetu na nina iona Tanzania yenye nguvu mara mbili ya Marekani.”
Julieth alizungumza kwa ujasiri hadi balozi Trump akastuka kidogo kwa maana aliamini kwa kutumia vielelezo alivyo kuwa navyo basi wana weza kumtumia Julieth kutekeleza mipango yao.
“Waoo ume jiamini vizuri sana Julieth”
“Mimi ni mtoto wa Simba, kamwe siwezi kuja kuwa fisi au paka”
Julueth mara baada ya kuzungumza hivyo akaanza kutembea kuelekea mlangoni.
“Ume sahau jambo moja Julieth”
Kauli hiyo ikamfanya Julieth kusimama, akashusha pumzi kisha akamgeukia balozi Trump.
“Una weza kwenda na hili faili uka muonyeshe baba yako. Nina imani kwamba wewe bado una akili za kitoto na wala hujui mambo yana kwenda vipi. Ila baba yako na mama yako wakiona hivi basi wata elewa nini tuna maanisha. Mchana mwema”
Balozi Trump akamkabidhi Julieth faili hilo lenye rangi nyeusi huku juu likiwa limeandikwa kwa maandishi mekundu TOP SECRETY. Julieth akalitazama kwa sekunde kadhaa kisha akatoka ndani hapo. Akakabidhiwa simu yake na moja kwa moja akaelekea kwenye gari lake. Machozi yakaanza kumtoka huku woga mwingi ukiwa ume mtawala. Hakika masharti aliyo pewa ni magumu sana, hapo ndipo akaanza kuyakumbuka maono ya Josephine alipo muambia raisi Mtenzi kwamba ana paswa kuwa makini sana kwani Wamarekani wana uwinda mkataba ambao waliingia na kundi la Bokoharamu na endapo mkataba huo uta toka au kufichuliwa na nchi ya Tanzania, basi una weza kusababisha nchi ya Marekani kuongeza maadui ambao hajui wata kuwa ni nani na nani. Julieth akampigia baba yake.
“Baba upo wapi?”
“Nipo nyumbani mwanangu, vipi mbona una lia”
“Nina kja baba”
“Kwa hali hiyo una weza kuendesha gari?”
“Ndio”
“Sawa nakusubiria”
Julieth akakta simu na kuwasha gari na kuondoka hotelini hapo kwa mwendo wa taratibu.
***
“Baba Julieth vipi?”
Mrs Sanga aliuliza huku akiwa na wasiwasi mwingi.
“Mtoto ana kuja”
“Ehee Mungu huyo balozi ata kuwa ame mueleza nini?”
Mrs Sanga aliuliza huku akiwa na wasiwasi mwingi sana. Chumbani hapo hakukulika hata mgeni waliye muacha sebleni hakika wame msahau kwani tukio hilo liliweza kuvuruga amani yao.
‘Baby njoo unichukue bwana, watu wenyewe wame niacha sebleni, sijui kuna tatizo gani lime wapata’
Leila alituma meseji hiyo kwa Evans.
‘Ume shindwa kumpagawisha huyo mzee?’
‘Hawaeleweki kwa kweli, sijui wame kumbwa na nini. Njoo bwana tuondoke zetu’
‘Poa nina kuja’
Macho ya Leila yakatazamana na Juieth anaye ingia mlangoni hapo. Kwa kumtazama tu una weza kugundua kwamba hayupo sawa kwani macho yake yame tawaliwa na uwekundu mithili ya mvuta bangi anaye jifunza.
“Habari yako”
Leila alimsalimia Julieth ila hakujibu chochote zaidi ya kuendelea kuanza kupandisha ngazi kuelekea gorofani huku mkono wake wa kulia akiwa ameshika faili lenye rangi nyeusi.
‘Mmmm ana nini huyu?’
Leila alijiuliza na wala hakushangaa sana kwa maana sura ya Julieth sio ngeni kwake kwani alisha wahi kuiona kwenye tv kwa mara kadhaa. Julieth akagonga mlango wa chumba cha wazazi wake na nabii Sanga akafungua mlango. Julieth akapitiliza hadi ndani pasipo kuzungumza chochote, akajitupa kitandani huku akiwa na mawazo mengi sana.
“Julieth kime tokea nini?”
Mrs Sanga aliuliza huku akimtazama mwanaye.
“Yaani sijio ita kuwaje baba”
“Ita kuwaje nini?”
Taratibu Julieth akakaa kitako na kumkabidhi baba yake faili hilo. Nabii Sanga kaanza kulifungua na kuanza kutazama kilicho ndani. Mwili mzima ukaanza kumtetemeka kwa woga mwingi sana. Mrs Sanga akamsogela mume wake naye macho yakamtoka.
“Wamejuaje?”
Nabii Sanga aliuliza huku akiwa ametawaliwa na woga mkubwa sana.
“Hata sijui baba”
Julieth alijibu kwa sauti ya unyonge mkubwa sana. Katika siku ambazo familia ya nabii Sanga ime tawaliwa na hofu kubwa ni siku hii. Kila mmoja akahisi kama mwisho wao ume wadia. Mlio wa gari ukamfanya nabaii Sanga kutembea kwa kasi hadi dirishani na kuchungulia na kuona gari lake likiingia na George(Evans) akashuka kwenye gari.
“Amerudi”
Nabii Sanga alizungumza huku akifunika dirisha hilo.
“Nani?”
Julieth aliuliza huku akimkazia macho baba yake.
“Kuna kijana mmoja ni bilionea wa kimarekani. Ametufwata na kutuomba tuweze kumpatia idea ya biashara hapa Tanzania kwa maana ana hitaji kuwekeza dola bilioni mbili na nusu za Kimarekani katika mradi wowote hapa nchini”
“Mmmmm!!”
Julieth akaguna tu kwa maana akili yake kwa sasa haiwazii kabisa maswala ya biashara.
“Mume wangu ngoja kwanza. Hili swala tuna limaliza vipi?”
“Hilo sio jambo la kuzungumza juu juu. Tutulize kwanza vichwa, kwa sasa twende tuka zungumze na wageni”
Nabii Sanga na mke wake wakatoka ndani hapo na kuelekea sebleni.
“Nime rudi jamani, nina shukuru sana kwa kila jambo”
“Usijali kijana wetu, nina imani tuta zidi kuwasiliana. Ukiwa tayari wewe nipigie tu simu tuta panga”
“Usijali mzee wangu. Ila mbona kama sura zenu zina wasiwasi?”
“Aha….hakuna kitu George kila jambo lipo vizuri”
Macho ya Evans yakaanza kumtazama Julieth anaye shuka kwenye ngazi huku akionekana kuchoka sana.
“Ahaa Julieth njoo ukutane na George Sanga”
Nabii Sanga alizungumza huku akijitahidi kutengeneza furaha usoni mwake. Julieth akatembea kwa hatua za kinyonge hadi sehemu walipo kaa wazazi wake na kujibwaga kwenye sofa. Kitendo cha Julieth kumtazama Evans usoni mwake akajikuta akistuka sana hadi kila mtu akagundua kwamba ame stusha na jambo hilo lika mfanya Evans kuanza kuhisi kwamba Julieth atakuwa amemgundua.
***
“Baba una muda tuzungumze?”
Jery alizungumza huku akiwa amekaa kwenye kiti kilichopo mbele ya meza ya baba yake.
“Kuna nini tena kwa maana mke wako ameondoka hapa masaa mawili yaliyo pita na ana onekana ana wasiwasi mwingi sana. Vipi tayari umesha muudhi?”
“Hapana, sija gombana naye. Ame kwenda wapi?”
“Ameniambia ana kwenda kuonana na baba yake. Sasa kama kuna jambo ambalo ume muudhi mtoto wa watu ni heri ukazungumza mapema Jery.
“Hapana baba, sija mkera. Ila nina hitaji tuzungumze kama watu wazima”
Raisi Mtenzi akatabasamu kwa maana hakuwahi kumsikia mwanaye huyo akizungumza kauli kama hiyo.
“Watu wazima?”
“Ndio baba nina hitaji tuzungumze kikubwa”
“Ehee nina kusikiliza mtu mzima”
Jery akaka kimya kwa sekunde kadhaa kisha akashusha pumzi nyingi.
“Baba una jua sisi ni wanaume”
“Ndio nina litambua hilo”
“Hivyo tukiwa kama wanaume, kuna mambo mambo huwa tuna yafanya ili mradi kukidhi haja za miili yetu”
“Usitake kuniambia kwamba bado una mahusiano na yule mfagiaji?”
“Baba najua hichi kitu ninacho kizungumza ni kwa ajili ya mstakabali wa familia yetu.”
“Nenda kwenye pointi yako acha kuzunguka sana”
“Baba Shani ni mjaumzito na ana mimba yangu”
Raisi Mtenzi macho yakamtoka na uso wake ukajaa ndiza zilizo mfanya Jery atambua kabisa amesha likoroga kwa baba yake. Ukimya wa dakika mbili uka pita huku raisi Mtenzi akiwa katika hali hiyo ya kukasirika.
“Hichi ndio ulicho kuwa una kitafuta si ndio?”
“Hapana baba, ime tokea tu akapata ujauzito”
“Kwani huwezi kutumia Condomu wewe?”
Raisi Mtenzi alizungumza kwa kufoka huku akimtazama Jery.
“Baba nime fanya hivi kwa ajili ya mke wangu wa ndani hataki kuzaa kwa kipindi hichi ambacho mimi nina hitaji mtoto. Nilimvumilia sana tena sana kiasi kwamba nikashindwa kwa maana jukumu la mwanamke ndani ya familia yake ni kuzaa na kulea familia. Yeye anakazi ya kuhangaika huku ofisini akidhani kwamba hii ofisi ndio ime muoa. Nime angali what best for my future famili. Sina kaka, sina dada sina ndugu ambaye hata siku wewe ukifa ata weza kuwa karibu yangu. Ila mtoto aliyopo tumboni mwa Shani ndio rafiki yangu mimi”
Jery naye alizungumza kwa kufoka huku akimkazia macho baba yake. Raisi Jery akasimama huku macho ya hasira yakimtawala.
“Nime ishi na mama yako na wala sikuwahi kumleta mtoto wa haramu. So na wewe usiniletee wajukuu haramu ndani ya ukoo wangu wa Mtenzi. Umenielewa wewe?”
Raisi Mtenzi alizungumza huku akipiga piga ngumi mezani na kuwafanya walinzi wake wawili walio simama nje ya mlango wake kuingia ndani, ila akawanyooshea ishara ya mkono kuwaomba watoke ndani hapo na wakatii agizo hilo.
“Ohoo kwa hiyo mwanangu atakapo zaliwa ata kuwa ni haramu?”
“Ndio ni mjukuu haramu na unazaaje na wafagiaji wa ikulu wewe. Tume kuoezesha kwa binti ambaye wazazi wake ni wacha Mungu na yeye ni mcha Mungu, ana heshima ana pesa ana kila aina ya sifa ya uzuri isitoshe alikutunzia bikra hadi ukampata. Alafu wewe una una kwenda kutembea na wafagiaji kweli Jery?”
Raisi Mtenzi alizungumza kwa kufoka.
“Mapenzi sio pesa sio uzuri na kama umemuoana mkwe wako ni mzuri sana kuliko wanawake wote nenda kamuoea wewe”
“Una semaje wewe”
Raisi Mtenzi kwa haraka akapanda juu ya meza yake na kumrukia Jery, akamuanguka chini na kuanza kumtandika ngumi mvululizo ambazo zilizo mfanya Jery kukikinga na mikono yake ili asiumizwe moyo wake.
“Nita kuua wewe, sijawahi kuzaa mtoto haramu na mpumbavu kama weweee”
Raisi Mtenzi alizunguma kwa hasira huku akiendelea kumshushia kipigo Jery. Uvumilivu ukawashinda walinzi wake na wakaingia ndani, hali hiyo ikawaogopesha sana na kuwalazimu kuamua ugomvi huo.
“Niacheni niweze kumuaa mwana haramu mkubwa huyu”
“Hapana muheshimiwa upo ofisini na tena ni ikulu hapa. Hupaswi kufanya hivyo”
Mlinzi wake mkuu alizungumza kwa sauti ya ustarabu huku akimzuia raisi Mtenzi kumendelea na mapambano hayo. Jery akanyanyuka huku chini ya jicho la kushoto akiwa ana mwagikwa na damu kwa maana kuna ngumi ilimpata eneo hilo.
“Nina uwezo wa kukupiga wewe mzee ila siwezi kunyanyua mkono wangu na kukupiga kwa maana wewe ni baba yangu. Ila nilioa mwanamke mwenye bikra feki hakuwa na bikra halisi na ndio maana niliamua kwenda kuzaa nje ya ndoa yangu na kama amenidanganya kuhusiana na bikra yake. Je kuna mambo mangapi ambayo ana nidanganya. So nina mchukua mfagiaji wangu na kutoweka naye pasipo julikana na usijaribu kunitafuta na kuanzia hivi sasa nina hesabia sina baba wala mama”
Jery mara baada ya kuzungumza maneno hayo akajitoa mikononi mwa mlinzi aliye mshika na kutoka ofisini hapo na kumfanya sekretari kushangaa kwa maana Jery aliingiaa kiwa na tabasamu pasana usoni mwake, ila ana toka ofisini humo akiwa ana mwagikwa na damu kwenye shavu lake na inavyo onyesha ndani ya ofisi ya baba yake hakna usalama kabisa.
****************************************************************************************************************
u
ITAENDELEA
Haya sasa, raisi Mtenzi amemtembezea kipondo mtoto wake, Jery kuanzia hivi sasa ana hesabu raisi Mtenzi sio baba yake tena kisa ame kataa mimba ya Shani. Familia ya nabii Sanga nayo kwa sasa ipo kwenye kipindi kigumu cha hofu ya siri zao kujulikana na serikali ya nchi ya Marekani je nini kitatokea.? Usikose sehemu ya 205.