RIWAYA: Tai kwenye mzoga

RIWAYA: Tai kwenye mzoga

SAA TATU KASORO USIKU ule msafara wa magari ya UN ulianza kuondo-
ka pale hotelini. Kulikuwa na malori makubwa sita na magari madogo mawili
na yote yakiwa na nembo za UN ubavuni.
Niliwasha gari na kujiunga na msafara ule kwa nyuma na wakati nikifanya
vile nikagundua kuwa sikuwa peke yangu kwani nyuma yangu kulikuwa na
magari mawili mengine ya watu binafsi yaliyonifuata kwa nyuma yangu.
Wakati tukiondoka eneo lile la Hotel des Mille Collines nilisikia vilio vya
akina mama na watoto waliokuwa wakilia kwa kuachwa na wale askari wa UN
bila ulinzi na hali ivileinihuzunisha sana hata hivyo sikuwa na namna yaku-
wasaidia ingawaje niliumia sana.
Tulitembea kwa umbali mrefu nyuma ya msafara ule wa UN na tukiwa
tunaendelea na safari njiani niliweza kuziona maiti nyingi zikiwa zimetelekez-
wa ovyo barabara na kuna wakati tulilazimika kukanyaga juu ya maiti hizo
pale tulipokuta zimelundikwa barabarani.
Kwa kweli hali ilikuwa inatisha sana na kadiri usiku ulivyokuwa ukizidi
kuingia ndiyo mashaka nayo yalivyokuwa yakizidi kuongezeka.
Yale malori ya UN yalikuwa yakizidi kutokomea mbele yetu na mimi siku-
taka yaniache. Drel Fille ambaye alikuwa ameketi pembeni yangu tulikuwa
tumekubaliana kuwa endapo kungetokea rabsha yoyote njiani awe tayari kuji-
bu mashambulizi haraka ili lengo letu litimie. Diane alikuwa akilia na Mutesi
alijitahidi kwa kila hali kumfariji na hali hiyo ilinipa faraja kidogo.
Wakati tukiendelea na safari tuliona baadhi ya nyumba zikiwa zinateketea
kwa moto huku sauti za vilio na mayowe ya hofu zikihanikiza. Nchi nzima ya
Rwanda ilikuwa ikinuka damu na hadi pale tulipofika kuziona maiti za watu
halikuwa jambo la kushangaza tena.
Tulikuwa tumeziona maiti za kila aina na zenye majeraha yasiyo tazamika
kwa urahisi na hapo nikayakumbuka maneno ya Jaji Makesa juu ya umwagaji
damu wa kutisha uliokuwa mbioni kutokea kwenye nchi hii.
Hali ya mambo ilivyokuwa ilikuwa imenichanganya na kunikatisha tamaa
sana. Niliona ni kama lilikuwa tukio la kufikirika lakini haikuwa vile kwani
lilikuwa ni tukio la kweli na lililonishangaza sana.
__________
TULIKUWA TUMESAFIRI umbali wa zaidi ya kilometa ishirini pale tuli-
poyaona yale malori ya UN yakipunguza mwendo na hapo nikahisi kule mbele
kulikuwa na rabsha.
Akili yangu ikaanza kufanya kazi haraka, nilimtazama Drel Fille pembe-
ni yangu nikamuona kuwa alikuwa amejiandaa kwa lolote hivyo na mimi
nikaisunda vizuri bastola yangu mafichoni tayari kwa lolote.
Muda mfupi baadaye yale malori ya UN mbele yetu yalisimama na hapo
tukasikia makelele ya watu wakishangilia kama wehu. Mle ndani ya gari nili-
wasihi watu wasiwe na hofu ila wawe tayari kukabiliana na lolote.
Haukupita muda mrefu mara niliwaona madereva wa yale malori ya UN
wakishuka chini na hapo nikawaona vijana wenye bunduki, mapanga na
marungu wakija kukagua kwenye yale malori.
Ukaguzi ule ulipoisha niliwaona baadhi ya watu wakishushwa chini toka
kwenye yale malori kisha yale malori yakaruhusiwa kuendelea na safari. Wale
watu walioshushwa walihojiwa kidogo na kisha wakakusanywa barabarani na
hapo kilichofanyika kilinitia simanzi sana.
Mtu wa kwanza alikabidhiwa panga na kulazimishwa amfyeke mwenzake
na mtu yule aliyefekwa alipokufa mwingine alikabidhiwa tena lile panga
amuue yule muuaji wa awali. Zoezi hilo liliendelea hadi pale alipobakia mtu
wa mwisho na yule mtu wa mwisho aliuwawa kwa risasi huku wauaji wale
wakishangilia.
Zoezi lile lilipomalizika wale wauaji walihamia kwetu na mimi sikutaka
kuonesha ukaidi wa namna yoyote mbele yao kwani nilipanga kutumia akili
zaidi kabla ya nguvu kutumika baadaye.
Kilikuwa kikundi cha watu ishirini na nane na ishirini na sita kati yao wali-
kuwa na silaha za jadi kama marungu, mapanga na visu na wawili waliosalia
ambao ndiyo walioonekana kuwa ni viongozi wa kizuizi kile walikuwa na
bunduki mikononi mwao.
Niliwatazama watu wale wakati wakilikaribia gari letu na hapo nikapiga
moyo konde na kumtaka Drel Fille akae tayari wa lolote.
“Wote shukeni chini” mmoja alituamrisha kwa lugha ya kinyarwanda na
hapo nikashusha kioo cha gari na kuwatazama. Ila kwa kuwa ilikuwa usiku
wale watu wakawasha tochi na kuanza kutumulika mle ndani, mmoja baada ya
mwingine na kitendo kile kilinikera sana hata hivyo sikuwa na namna.
“Mnaenda wapi? mwingine aliuliza
“Ngara, mkoani Kagera, Tanzania” niliwajibu
“Nyinyi ni watanzania?
“Ndiyo”
“Tunataka kuona vitambulisho vyenu” kiongozi wao mmoja mwenye bun-
duki aliongea na hapo nikatoa kitambulisho changu cha bandia toka kwenye
wallet na kuwapa. Tule kiongozi wao alikipokea kitambulisho kile kisha aka-
kitazamatazama na kunirudishia lakini niligundua kuwa hakuwa ameridhika.
“Na hao wengine vitambulisho vyao viko wapi?
“Huyu ni mke wangu, huyu ni shemeji yangu na huyu ni mtoto wetu. Vitam-
bulisho vyao wamevisahau kwenye begi wakati tulipokuwa tukifanya haraka
kuondoka” nilijaribu kutunga uongo na yule kamanda akacheka kwa kejeli.
“Kwanini mlifanya haraka kuondoka? mwenzake aliuliza huku akicheka
“Ubalozi wetu umefungwa kwa muda kwa hiyo hakuna shughuli inayoen-
delea kwa sasa ndiyo maana nikaonelea nirudi na familia yangu nyumbani
Tanzania”
“Mbona hawa siyo watanzania hata wewe mwenyewe ukiwatazama tu una-
gundua” mmoja alidakia.
“Unatudanganya siyo eh” yule kiongozi wao aliuliza kwa hasira
“Hapana si hivyo mnavyodhani”
“Inyenzi...! ’’ mmoja alisikika akisema na hapo wote wakacheka
“Wote shukeni chini” kiongozi wao mmoja aliongea kwa hasira
Niliwatazama wale watu na nilipoona kuwa hawaelekei kunielewa nikafun-
gua mlango wa gari na kushuka. Drel Fille aliwahi kunishika mkono akinizuia
lakini nilimuonesha ishara kuwa asiwe na wasiwasi.
Niliposhuka kwenye gari wale watu walinizingira wakinizongazonga na
hapo nikaona hali ilikuwa ikielekea kuwa mbaya zaidi.
Nikiwa pale nje niligeuka kumtazama Drel Fille na hapo akaelewa kuwa
nilikuwa nikimaanisha nini. Sasa akili yangu yote ilikuwa kwa wale viongozi
wao wawili wenye bunduki.
Kwa kuzingatia kuwa nilikuwa komandoo niliyehitimu vizuri katika medani
za mapambano ya kivita wale watu walipokuwa wakinizongazonga nilijisoge-
za kwa hila karibu na yule kiongozi wao mmoja mwenye bunduki huku niki-
jidai kuwasihi watuache.
Nilipofika kwenye usawa mzuri wa kufanya mashambulizi kufumba na ku-
fumbua nikawa nimemdhibiti yule kiongozi wao mmoja kwa kabari ya nguvu
huku bastola yangu ikiwa kichwani mwake.
“Wekeni silaha zenu chini kama mnapenda kumuona mwenzenu anaendelea
kuishi” wale watu walitaharuki na muda uleule Drel Fille akamchakaza kwa
risasi yule kiongozi wao mwingine mwenye bunduki.
Kuona vile wale wenzake wakaanza kurudi nyuma na hapo Drel Fille
akashuka na kuikota ile bunduki ya yule kiongozi wao aina ya AK-47. Yule
mtu niliyemdhibiti nikamshona risasi ya kichwa na aliponguka chini nikaic-
hukua ile bunduki yake.
Wale vijana kuona vile wakataka kukimbia lakini hakuna aliyefika mbali
kwani wote tuliwafyeka kwa risasi na hapo tukarudi haraka kwenye gari na
safari ikaanza.
Mutesi na Diane walikuwa wameshangazwa sana na tukio lile hata hivyo
hatukuwa na muda wa kupoteza.
Yale malori ya UN yalikuwa yameisha tuacha hivyo hatukuwa na namna
tena badala yake Mutesi ndiyo akawa anatueleza sehemu ya kupita.
Wakati tukiendelea na safari njiani bado tuliendelea kuziona maiti nyingi
sana zikiwa zimetawanywa ovyo barabarani. Nilijitahidi kuzikwepa nisizikan-
yage lakini wakati mwingine nilishindwa hivyo nikapita juu yake ingawa roho
iliniuma sana.
Safari iliendelea usiku mzima na kuna wakati tulilazimika kubadili njia pale
tulipoona kuwa kulikuwa na vizuizi vya Interahamwe mbele yetu.
Kwa mujibu wa maelezo ya Mutesi ni kuwa katika uelelekeo ule hatukuwa
mbali sana na ulipo mpaka wa Rwanda na Tanzania na hilo lilinitia moyo sana.
Wakati tukiendelea na safari nilianza kushawishika kumueleza Drel Fille
juu ya mashaka niliyokuwa nayo kwa mratibu wangu wa safari za kijasusi,
Brigedia Masaki Kambona.
Sikufahamu haraka ni nini kilinishawishi kufanya vile lakini huenda niliona
ni wakati sahihi wa kueleza hisia zangu.
__________
NAKUMBUKA KUWA ILIKUWA SAA KUMI USIKU kasoro dakika
chache pale tulipokutana na kizuizi kingine cha Interahamwe barabarani. Na
wakati huo tulikuwa peke yetu kwani ile yale magari mengine yaliyokuwa
yakitufuata nyuma yetu tulikuwa tumeyaacha kule nyuma na hatukuwa tuki-
fahamu habari zake.
Kizuizi hiki kilikuwa kikubwa zaidi na chenye watu wengi wenye bunduki.
Wakati tukisimamishwa nilitazama pembeni ya kizuizi kile na hapo nikao-
na maiti nyingi zikiwa zimelundikwa kando yake. Nilikata tamaa zaidi baada
ya kuona kulikuwa na kichwa mtu kilichokuwa kimekatwa na kuchomekwa
kwenye mti uliokuwa pembeni yake.
Hofu ikiwa imetushika safari hii sikutaka kushuka kwenye gari na badala
yake nilimwambia Drel Fille ajiweke tayari kwa lolote. Niliposimamishwa
tu viongozi wa vizuizi vile walioonekana kuwa makatili zaidi walilisogelea
gari letu na wakati wakilisogelea walisita halafu nikamuona mmoja akim-
nong’oneza jambo mwenzake na ile kwangu ilikuwa ishara mbaya.
“Shukeni chini wote” kiongozi wao aliyevaa suruali ya jeshi na fulana
nyekundu alituamrisha huku akisogea mbali na gari lile na wakati akifanya
vile niliongeza mwanga wa taa kumulika mbele huku nikijidai natafuta mae-
gesho mzuari, na hapo nikaziona picha zetu, mimi na Drel Fille zikiwa zi-
mening’inizwa mbele ya kizuizi kile kama watu hatari tunaotafutwa.
Drel Fille alikuwa ameziona picha zile hivyo alianza kunionya juu ya hatari
ya kusimama eneo lile.
Nilipokuwa najidai kujiandaa kusimama Drel Fille akasogeza kioo cha gari
kwa siri na kuupenyeza mtutu wa bunduki na hapo mvua ya risasi ikaanza
kusikika. Mimi kuona vile nikaingiza gia na kukanyaga mafuta na kwa kuwa
mbele yetu kulikuwa na kizuizi ikanibidi nipite katikati ya kile kizuizi na kuki-
bomoa hali iliyopelekea taa za mbele na kioo cha mbele cha gari letu kupa-
suka.
Sikutaka kusimama hata hivyo nikaanza kusikia tukitupiwa risasi kwa nyu-
ma na hapo nikawaambia watu wote mle ndani ya gari walale chini.
Risasi zile zilipasua kioo cha nyuma cha gari letu na baada ya muda gu-
rudumu la nyuma la upande wa kushoto nalo likapasuliwa kwa risasi lakini
sikusimama badala yake nikatia moto nikiliendesha lile gari vilevile.
Hatukufika mbali sana pale niliposikia mshindo mkubwa wa ajabu na hapo
nikaliona gari letu likinishinda nguvu huku likiyumbayumba ovyo. Nilijitahidi
kulidhibiti lakini haikuwa kazi rahisi hivyo nililiona gari lile likiacha barabara
na kuingia vichakani na hapo nikasikia watu wote mle ndani wakipiga mayowe
ya hofu. Hata hivyo tukio lile lilikuwa nje ya uwezo wangu.
Muda mfupi baadaye tuligonga kitu ambacho sikukitambua haraka kutoka-
na na giza la usiku na baada ya hapo sikufahamu kilichoendelea.
____________
KAMBI YA WAKIMBIZI YA BENACO wilayani Ngara, mkoani Kagera il-
ikuwa imefurika watu waliokata tamaa sana. Wengi wao walikuwa wakimbizi
wa kitutsi na baadhi ya wahutu wenye msimamo wa wastani.
Drel Fille aliwasili kwenye kambi hiyo ya wakimbizi huku akiwa amembe-
ba Luteni Venus Jaka begani na Diane akiwa anamfuata kwa nyuma.
Ilikuwa safari ndefu ya masaa yasiyopungua saba na njiani waliongozana na
kundi kubwa la watu waliokuwa wakikimbia mapigano na kuelekea kwenye
kambi ile.
Wapo baadhi ya wazazi ambao waliwaacha watoto wao njiani baada ya ku-
choka kuwabeba na kuna wengine walipoteana kabisa na ndugu zao.
Drel Fille akiwa amembeba Luteni Venus Jaka njiani alikuwa amekutana na
Jèrome Muganza ambaye kwa haraka alipomtazama Luteni Venus Jaka alim-
kumbuka. Hivyo akaamua kufanya hisani kwa kumsaidia Drel Fille kumbeba
kuelekea kwenye kambi ile ya wakimbizi.
Mutesi alikuwa amekufa kule kwenye lile gari walilolitelekeza kule porini
kwani zile risasi zilizokuwa zikifyatuliwa nyuma yao muda mfupi kabla hawa-
japata ile ajali, moja ilikuwa imepenya mgongoni na kupotelea kwenye moyo
wake na jeraha hilo lilikuwa limempelekea apoteze damu nyingi na hatimaye
kuaga dunia akiwa ndani ya lile gari.
Mara baada ya ajali ile kutokea Drel Fille alimchukua Luteni Venus Jaka
na kumbeba begani na kisha wakapotelea kule msituni na Diane kabla ya baa-
daye kuja kukutana na barabara yenye wakimbizi wengi na hapo ikawa salama
kwao. Wakajichanganya na wakimbizi wale wakielekea kambi ya wakimbizi
ya BENACO.
Wakati wakivuka daraja la Rusumo waliziona maiti nyingi sana zikielea juu
ya maji ya mto ule huku zikiwa zimeharibika vibaya.
Mvua kubwa iliyokuwa ikiendelea kunyesha ilikuwa ikizisomba maiti hizo
na kuzisafirisha hadi kwenye mto Rusumo, zikiendelea mbele na safari na kwa
hakika hali ile ilitisha.
__________
KAMBI YA WAKIMBIZI YA BENACO ilifurika vilio vya watu wenye ma-
tatizo ya kila namna. Shirika la kuhudumia wakimbizi la umoja wa mataifa la
UNHCR lilikuwa limeweka mahema kwa ajili ya makazi ya wakimbizi hao
kwa muda na pia kulikuwa na msaada wa kitabibu kwa watu wenye majeraha.
Vilevile kulikuwa na msaada wa chakula na ushauri nasaha juu ya macha-
fuko yale ingawaje mahitaji bado yalikuwa madogo ukilinganisha na idadi ya
watu. Hivyo uharibufu wa mazingira nao uliongezeka kwa vitendo vya watu
kukata miti ovyo kwa ajili ya kujengea nyumba na matumizi ya kuni.
Kulikuwa na utaratibu kuwa kila mkimbizi alipaswa kujiandikisha jina lake
na sehemu anayotoka huko nchini Rwanda kwenye kambi ile ili iwe rahisi kwa
ndugu kutafutana.
Mara tu walipowasili kwenye kambi ile Jèrome Muganza aliamua kujichan-
ganya kivyake akiwaacha Drel Fille, Luteni Venus Jaka na Diane huku akidai
kuwa kuambatana kule kungemponza kwani yeye alikuwa akitafutwa sana na
washirika wa Interahamwe. Jèrome Muganza pia alimtaka Drel Fille amu-
ombee msamaha kwa Luteni Venus Jaka pale ambapo afya yake ingeimarika
kwa kumwambia kuwa alishawishika kumtoroka kule mapangoni baada ya
kuwa na wasiwasi naye lakini baadaye alikuja kugundua kuwa alifanya ma-
kosa.
Mwisho wakapeana anwani za kutafuta na kisha wakaagana kila mmoja aki-
shika hamsini zake.
Kabla ya yote mara tu walipoingia kwenye kambi ile ya wakimbizi Drel
Fille aliichukua ile bahasha yenye vielelezo vya ushahidi waliyoipata kwa Jaji
Makesa na kiasi cha pesa walichokuwa nacho, kisha kwa njia za panya akavi-
tuma vitu hivyo kwenye sanduku la posta la Luteni Venus Jaka kwenye ofisi
za posta iliyokuwa karibu na eneno lile.
Baadaye alimkutanisha Luteni Venus Jaka na baadhi ya maafisa wa jeshi la
Tanzania waliokuwa wakitoa msaada kwenye kambi ile huku Luteni Venus
Jaka akiwa bado hajitambui.
Maafisa wale walimshukuru sana Drel Fille kwa kuyaokoa maisha ya Lu-
teni Venus Jaka hadi kumfikisha kwao. Baadaye kwa msaada wa helikopta ya
kijeshi Luteni Venus Jaka alisafirishwa hadi Dar es Salaam kupewa matibabu
kwenye hospitali ya kijeshi.
Drel Fille hakuishia pale bado aliwaeleza maafisa wale juu ya mashaka aliy-
okuwa nayo Luteni Venus Jaka juu ya kiongozi wake wa operesheni za kijeshi
Brigedia Masaki Kambona, na maafisa wale kuona vile wakamshukuru sana
Drel Fille na kuamua kuongozana naye pamoja na Diane kama sehemu ya
ushahidi wa kuaminika.
Hivyo Drel Fille na Diane wakawa wameingia kwenye orodha watu wali-
omsindikiza Luteni Venus Jaka hadi jijini Dar es Salaam hospitali.
MIAKA MIWILI BAADAYE
JOPO LA MADAKTARI WA KIJESHI lilijiridhisha kuwa Luteni Venus Jaka
alikuwa amepona kabisa ugonjwa wa kupoteza kumbukumbu uitwao AMNE-
SIA baada ya kichwa chake kuwa kimepata misukosuko mikubwa hadi ile ajali
iliyompelekea apoteze fahamu na kumbukumbu zote
Maelezo ya Luteni Venus Jaka yalisaidia kwa kiasi kikubwa kukamatwa
kwa Brigedia Masaki Kambona. Na hapo ndiyo ikajulikana kuwa Brigedia
Masaki Kambona hakuwa mtanzania ila mnyarwanda wa kabila la kihutu ali-
yejipenyeza nchini miaka mingi iliyopita. Akajifunza vizuri lugha ya kiswahili
na kupata elimu yake katika shule na vyuo vya Tanzania kabla ya kujiunga na
jeshi akiaminika kuwa ni mtanzania. Hivyo basi alikuwa akiwasaidi wahutu
wenzake katika ule mpango mchafu wa umwagaji damu kwa kuvujisha siri,
kuwasaidia pesa na hata mbinu za kijeshi kwa siri.
Vielelezo hivyo vikamtika hatiani Brigedia Masaki Kambona pamoja na
ushahidi wa nyaraka alizokutwanazo baada ya kufanyiwa upekuzi wa kina
nyumbani na ofisi kwake.
Baadaye alihukumiwa kifungo cha maisha na mahakama ya uhalifu wa ki-
vita na uvunjifu wa haki za binadamu huko The Hague nchini Uholanzi. Na
baada ya kesi ya Brigedia Masaki Kambona kuisha, Luteni Venus Jaka akawa
amepata picha kamili juu ya mambo yalivyokuwa, kwamba Brigedia Masaki
Kambona hakuwa Mtanzania. Lakini vilevile kwa kuwa Luteni Venus Jaka ali-
kuwa ndiye mpelelezi mahiri sana ambaye angeweza kutumwa nchini Rwanda
na kurudi na majibu sahihi hivyo ulikuwa ni mpango wa Brigedia Masaki
Kambona kummaliza Luteni Venus Jaka kabla hajaileta ripoti yake na baada
ya hapo ukweli wa mambo usingejulikana na hivyo wahusika wa mauaji yale
ya Rwanda wasingekamtwa.
_________
AKIWA NA VIELELEZO VYA KUTOSHA, jopo la mawakili wa kesi za
mauaji ya Rwanda zilizokuwa zikisikilizwa katika mhakama ya ICTR-Inter-
national Criminal Tribunal for Rwanda mkoani Arusha, Tanzania. Lilimtaka
Luteni Venus Jaka kwenda kutoa ushahidi wake kwa baadhi ya washukiwa
wa mauaji hayo waliokamatwa ambao Luteni Venus Jaka alikuwa na ushahidi
dhidi yao.
Mawakili hao walituma ombi hilo baaada ya kupata uthibitisho toka kwa
madaktari kuwa Luteni Venus Jaka alikuwa amepona kabisa, mwenye afya
njema na fahamu zake zote zilikuwa zimerudi.
Luteni Venus Jaka alilipokea ombi hilo kwa mikono miwili akapewa tiketi
ya ndege na kusafiri hadi mkoani Arusha ambapo alishiriki kikamilifu katika
kutoa ushahidi wake.
Kwa kuwa vielelezo vingi alikuwanavyo washukiwa waliingizwa hatiani
kwa kuhusika kwa namna moja au nyingine katika mauaji yale.
Akiwa ndani ya ukumbi wa mahakama ya ICTR, Luteni Venus Jaka alipata
bahati ya kuonana na Dr. Amanda Albro lakini wakati huu daktari huyo akiwa
kwenye kiti cha magurudumu kwani alikuwa tayari amepoteza miguu yake
miwili na baadaye kubakwa baada ya kutekwa na wale askari wa Kanali Bosco
Rutaganda.
Hivyo Dr. Amanda Albro na yeye alikuwa amefika pale kwenye mahakama
ya mauaji ya Rwanda kutoa ushahidi wake dhidi ya Marceline na Kanali Bos
co Rutaganda baada ya kusikia kuwa walikuwa amekamatwa na wanajeshi wa
RPF-Rwandese Patriotic Front ambao baadaye walifanikiwa kuirejesha hali
ya amani nchini Rwanda.
Vikosi vya jeshi la RPF vilikuwa vimeingilia kati na kutuliza machafuko
yale nchini Rwanda na hivyo kufanya kazi nzuri ambayo kwa hakika vilistahili
kupewa pongezi kwani huenda bila vikosi hivyo vya kijeshi machafuko yale
yangeendelea zaidi.
Kipindi cha mwezi mmoja cha kutoa ushahidi katika mahakama ya ICTR
kilikuwa kimemfanya Luteni Venus Jaka ajione tena kama binadamu wa
kawaida lakini aliyepungukiwa na kitu fulani.
Baada ya kufikiria sana Luteni Venus Jaka akamkumbuka Drel Fille, msi-
chana aliyetokea kumpenda sana na hapo ndiyo akajua kuwa kutokuwepo kwa
Drel Fille ndiyo kitu pekee ambacho kilishindwa kuikamilisha furaha moyoni
mwake.
_________
ILIKUWA JIONI MOJA na manyunyu ya mvua hafifu yalikuwa yakianguka
kutoka angani sambamba na baridi ya wastani iliyokuwa mkoani Arusha.
Luteni Venus Jaka alikuwa ndiyo amemaliza kutoa ushahidi wake wa
mwisho kwenye mahakama ile ya ICTR, na alikuwa akitoka kwenye ukumbi
ule kuelekea hotelini alipokuwa amefikia wakati alipokutana na mwanamke
fulani nje ya geti la kuingilia kwenye jengo lile la mahakama.
Alikuwa mwanamke mzuri wa ajabu, mwenye weusi wa asili na alikuwa
amembeba mtoto mdogo wa mwaka mmoja, na pembeni ya mwanamke huyo
alisimama binti wa makamo.
Luteni Venus Jaka ilikuwa bado kidogo awapite watu hao pale aliposikii
akiitwa
“Luteni!...” alipogeuka kumtazama yule mwanamke moyo wake ukapoteza
utulivu kabisa, hisia kali zikamchota akili huku ameachama mdomo wazi kwa
mshangao.
“Drel Fille...oh! my God ni wewe? Luteni Venus Jaka aliongea kwa sauti
kubwa ya mshangao kiasi cha kuwafanya watu waliokuwa jirani na eneo lile
wageuke kumtazama. Yule mwanamke aliyebeba mtoto hakusema kitu badala
yake alibaki amesimama tu huku akitabasamu.
“Drel Fille mpenzi wangu oh! siamini...”
“Ndiyo mimi mpenzi na nimefurahi sana kukuona kuwa umepona hadi
kunikumbuka namna hii” Drel Fille aliongea huku akitabasamu.
“Diane...? Luteni Venus Jaka alimuita yule binti aliyesimama pembeni ya
Drel Fille na hapo yule binti akaitika
“Bhee!”
“Na huyu ni nani mpenzi? Luteni Venus Jaka aliendelea kuuliza huku akim-
tazama yule mtoto mchanga aliyebebwa na Drel Fille huku akishangaa.
“Mtoto wako, ...mama mpelelezi na baba naye mpelelezi, sijui huyu mtoto
atakuwaje” Drel Fille aliongea huku akiangua kicheko hafifu.
“Yaani siamini mpenzi, mbona ilikuwa haraka sana vile?
“Haraka lakini ilitosha kupata mtoto, sakafuni, kwenye kochi, kitandani na
bafuni”
“Loh! safi sana, jina lake je? Luteni Venus Jaka aliuliza huku akiwa hajiwezi
kwa furaha.
“Tanzania” Drel Fille aliongea
“Kwanini aitwe Tanzania mpenzi?
“Nitakwambia?
Halafu wote wakakumbatiana kwa furaha huku mchozi yakiwatoka
“Twendeni” baadaye Luteni Venus Jaka aliwaambia huku akijifuta machozi
“Wapi?
“Hoteli niliyofikia hakika leo nina furaha sijawahi kuona”
Muda mfupi baadaye walikuwa kwenye teksi wakielekea hotelini na njiani
maongezi ya furaha hayakuisha baina yao.
LA FIN

Safi sana...

Chapter Closed...


Cc: mahondaw
 
Ni moja ya riwaya bora kuwahi kusoma. Hongera kaka. vipi kitabu
 
Ahsante sana,stori ilikuwa tamu lkn bado haijaisha,ongea na mtunzi aiendeleze,yaani dhumuni lá huyu mcongo mke wa luteni awe bado anaitumikia serikali ya Congo na amfundishe upelelezi kisiri Diane bila luteni kujua,waweze kumuibia siri Luteni na kuzipelekwa kwao kwa msaada wa Diane,wawili hao wafanikiwe kurudi kwao na luteni arudi tena Rwanda akamuue Diane,halafu aende Congo kumuua Drel Fille,nadhani itanoga zaidi,nachoamini mimi Drel Fille alikuwa na ajenda yake ya siri kuipeleleza Tz
Nalog off
 
Hii kitu nikichelewa kuinyaka ila nahisi ni kama kuna vipande vya HOTEL RWANDA
 
Back
Top Bottom