WAKALA WA SIRI 13
Mtunzi; Robert Heriel
0693322300
ILIPOISHIA
Alipanda ghorofa ya pili akiwa kashika bastola yake mkononi, alipofika juu ghafla akasimama baada ya kusikia sauti ya watu wakizungumza. Alitulia kisha akasikiliza;
“ Haiwezekani mpaka sasa hivi hatujaipata Chipu ya Darubini, mwezi sasa umeisha bado mnahangaika bila mafanikio yoyote. Ingekuwa bora kama mngekosa hizi sampo na Cadava kuliko kukosa chipu ya darubini ya hospitalini” Maneno hayo yalimchanganya sana Sajenti akiwa kajificha kwenye korido pembeni ya mlango wa kuingilia kwenye chumba ambacho kulikuwa na kikao cha siri.
INAENDELEA
“ Nafikiri kuna mchezo tumechezewa, na mwenye uwezo wa kucheza mchezo huu ni mtu mmoja. Sasa naweza kuelewa” Sauti nyingine ya mwanaume ilizungumza, Sajenti akiwa makini kusikiliza bila ya kuwaona watu wale.
“ Mtu gani huyo Dokta Binamungu? Nakuahidi donge nono zaidi ikiwa utatufungulia njia ya kumfahamu huyo adui ambaye anavuruga mipango yetu. Tuambie ni nani mtu huyo?” Sajenti aliamini sauti hiyo ilikuwa ya kiongozi wa kikao hicho. Alishtuka pia kusikia jina la Dokta Binamungu, alikuwa akimfahamu kama Daktari wa hospitali ya Boreti ingawaje alikuwa hanamazoea naye. Kufikia hapo Sajenti akaanza kuona mwanga wa kile kinachoendelea, tayari aligundua kuwa Dokta Binamungu ni miongoni mwa wasaliti waliowageuka na kutoa siri za taifa kuhusu hospitali ya Boreti.
“ Nadhani Dokta Beatus atakuwa anafahamu chochote kuhusu kupotea kwa Chipu, yeye ndiye mhusika tuu” Dokta Binamungu alisema.
“ Sidhani..! Ile siku nilivyomzimisha akazirai hakuwa na ujanja mwingine, nilichukua hiyo chipu kwenye darubini na kuondoka” Sauti ya mwanamke iliongea. Sajenti alishtuka kusikia sauti ya kike. Kilichomchanganya zaidi ni kusikia kuwa kumbe Yule mtu aliyevaa kininja aliyemuona siku ile alikuwa ni mwanamke. Sajenti hakudhani kama mtu Yule waliyemuona kwenye Kamera siku ile wakiwa room 66 angekuwa mwanamke. Jinsi alivyokuwa akitembea, alivyomvamia Dokta Beatus na pia alivyoibeba ile Cadava hakuna ambaye angeamini mtu Yule alikuwa ni mwanamke. Watu wote walijua ni mwanaume. Sajenti alitaka kumuona Yule mwanamke aliyekuwa akiongea angalau sura yake.
Habari za Dokta Beatus kutajwa kwenye kile kikao kilimfanya akili yake ikose utulivu. Aliona ipo haja ya yeye kumuwai Dokta Beatus kabla hajafikiwa na wale watu wabaya. Hakutaka kuchelewa kama alivyochelewa kwenye hospitali ya Boreti mpaka Mateka wa Ushahidi akatoroshwa.
Ghafla akiwa bado pale mlangoni alisikia mtu akipanda ngazi kuja ghorofa ya pili kule alipokuwa amesimama. Akajua ni Yule Mzee mlevi aliyekuwa amelala pale sebuleni ndiye aliyekuwa anakuja. Upesi alifyatuka kumfuata kulekule alipokuwa akija, hamadi! Walikutana kwenye ngazi Yule mlevi akiwa anapanda akiwa kashika chupa yake. Mlevi alishtushwa kwa uwepo wa Sajenti mule ndani, alikuwa kama kaona jini wa kaburini aliyesimama mbele yake. Mlevi hakutarajia kutokea kwa Sajenti. Sajenti hakutaka kumchelewesha alimpiga teke la kifua akadondoka na kuanza kubilingita mpaka chini ilipo ngazi ya kwanza. Masikini Mlevi wa watu kabla hajafikiri cha kufanya Sajenti alimzima kwa buti la kifua kama Mjeshi anayepiga guu pande. Hapo hapo Mlevi akapoteza fahamu.
Sajenti alitoka akaenda sebuleni, akakagua kagua lakini hakuona la maana, akatoka nje na kuondoka.
Moja kwa moja aliazimia kwenda nyumbani kwa Dokta Beatus, alichukua pikipiki yake na safari ya Sinza Mori ikaanza. Njia zilikuwa nyeupe pasipo na magari, ilikuwa tayari imehitimu saa kumi na nusu. Ndani ya Lisaa limoja alikuwa kashafika Sinza Mori yapata saa kumi na moja na nusu kukiwa kumekucha, Daladala na magari yakiwa yameshaanza kutembea barabarani. Alipaki pikipiki yake mbele ya geti la Nyumba ya Dokta Beatus. Bila kupoteza muda alizunguka kwa nyuma akaruka ukuta na kuzama ndani. Nyumba ya Dokta Beatus ilikuwa kimya, hii ikamfanya Sajenti kuwa makini zaidi. Alichungulia kwenye dirisha la sebuleni, hakuona mtu yeyote ingawaje taa ya sebuleni ilikuwa inawaka. Punde Sajenti alishtuka kumuona msichana akitokea pale sebuleni, Yule msichana alikuwa akipikicha macho yake yaliyozingirwa na utando wa tongo tongo za usingizi. Msichana Yule bila ya kujua kuna mtu anamtazama alifunua kanga yake ambayo aliifungia kwenye shingo kwa mtindo wa mtu anayetoka kuoga. Woooh! Sajenti soni ilimshika kuona msichana Yule akiwa uchi kama alivyozaliwa. Sajenti hakutaka kuona mambo kama yale, alificha macho yake kwa aibu ili asiuone uchi wa Yule msichana mdogo ambaye kwa umri alionekana anamiaka kumi na nane.
Ghafla Sajenti akiwa kaficha macho yake na viganja vyake, alisikia sauti ya viatu ndani ikitembea, akachungulia. Hapo akamuona Dokta Beatus akitokea chumbani akiwa kavaa kwa umaridadi, Yule msichana alivaa kanga haraka lakini alikuwa ameshachelewa kwani Dokta Beatus alikuwa amemuona. Kwa aibu Yule msichana alifunga kanga yake huku akizuga kwa kuitengeneza sebule. Chakushangaza Dokta Beatus alipofika pale sebuleni alimfuata moja kwa moja Yule msichana na kusimama nyuma yake huku akimkumbatia kwa nyuma. Jambo hili lilimshangaza sana Sajenti. Iweje Dokta mwenye elimu kubwa, na anayeheshimika kwenye jamii afanye mambo kama yale. Jambo hili lilimchukiza sana Sajenti lakini hakuwa na lakufanya zaidi ya kushuhudia aibu ile.
Aliwaona Wakinyonyana ndimi huku wakishikana kwa mahaba mazito, Sajenti aligundua kuwa ule ndio ulikuwa mchezo wao kwani kila mmoja wao alimfurahia mwenzake. Walipinduana mpaka kwenye sofa huku kanga ya Yule binti ikianguka, na hapo akawa uchi kama alivyozaliwa. Hii ilimpa nafasi Dokta Beatus kuufaidi mwili wa msichana Yule ambaye Sajenti alihisi kuwa ni Mfanyakazi wa ndani. “Mtoto mdogo lakini anamambo makubwa jamani” Sajenti alijisemea kimoyo moyo huku uhondo ule ukizidi kupamba moto.
Punde jambo lakushangaza lilimshtua Sajenti, alimuona Yule msichana akiingiza mkono wake kwenye mfuko wa Suruali ya Dokta Beatus, hapa Sajenti akawa macho kushuhudia kile anachotaka kukifanya Yule binti, lakini kabla Yule binti hajatoa mkono wake ndani ya mfuko wa Dokta ghafla sauti ya mlango wa chumbani ikasikika, na wote wakakurupuka huku Yule binti akiiwahi kanga yake pale chini na kujifunga. Dokta Beatus alijiweka sawia na kitambo kidogo alisimama mke wa Dokta Beatus akiwa kavaa nguo za kiofisi na mkoba wake begani huku akijiangalia kwenye kioo. Mke wa Dokta hakuwashtukia, ni wazi alikuwa hajawaona. Waliondoka na kumuacha Yule msichana pale sebuleni akiwa haamini kama hajafumaniwa.
Sajenti alimlaumu sana kimoyomoyo Yule binti kwa yale aliyokuwa anayafanya lakini hata hivyo alimtetea kuwa huenda alikuwa amelazimishwa na Dokta. Hivyo wakulaumiwa ni Dokta Beatus. Bado akiwa dirishani kwa nje alishangaa kuona Yule binti akijibwaga kwenye sofa huku akichekelea kama mtu aliyefanikisha jambo Fulani. Hii iliongeza umakini kwa Sajenti, alitaka kujua ni kwanini Yule binti anacheka kwa namna ile. Hapo akakumbuka muda ule Yule binti akiwa anaingiza mkono katika mfuko wa Dokta Beatus. Akili ya udadisi ikabisha hodi, na macho ya uvumbuzi yakachomoza kama jua la wakati wa kiangazi.
Yule msichana akiwa kakaa pale Sofani alitoa kifaa kilichofanana na Chipu. Sajenti alipagawa alipokiona. Akili yake ilimuambia ndio ileile chipu wanayoitafuta, ndio ileile chipu ambayo kama ataipata inaweza kumfanya akawa huru. Mapigo ya moyo yalienda upesi kama kimbunga, mwili ulimsisimuka mno. Akili yake ilikosa utulivu huku ikipiga kite. Angeachaje kupagawa ikiwa chipu hiyo ndiyo inayodaiwa kuwa yeye ndiye kaiiba. Chipu iliyomgeuza kuwa mkimbizi katika nchi yake mwenyewe. Ingawaje kulikuwa kuna kupotea kwa Cadava, lakini aliona kama angepata ile chipu ingempunguzia mzigo kwa kiasi Fulani. Lakini iweje Yule msichana aibe ile chipu kwenye mfuko wa dokta Beatus, anakazi nayo gani? Kama ametumwa, nani aliyemtuma? Mbona ni msichana mdogo lakini jambo alilolifanya ni kubwa?
Sajenti alivamiwa na msururu wa maswali yasiyo na majibu. “Huyu msichana anamuda gani katika nyumba ya Dr. Beatus? “ Sajenti alinong’ona Wakati huo Yule binti akinyanyuka na moja kwa moja akaelekea chumbani jambo ambalo lilimfanya Sajenti kuangalia anaelekea chumba kipi. Basi baada ya kujua chumba alichoingia Yule msichana, Sajenti akazunguka mpaka lilipodirisha la kile chumba. Alipofika dirishani alimsikia Yule msichana akiongea na simu.
”Ilikuwa kazi rahisi sana tofauti na nilivyotegemea, nilimlaghai na penzi zito mpaka likampofusha, likamlewesha akili yake ikawa chakari. Mke wake ndio alitaka kuwa kigagula lakini kabla hajatokea tayari nilishaiweka mikononi chipu ya Darubini. Nasubiri maelekezo yenu” Yule Binti aliongea kwa wasiwasi huku akiangalia huku na huku kama mtu asiyejiamini licha ya kuwa pekee yake. Hakutaka mtu yeyote ajue yale aliyokuwa akizungumza kwenye simu.
“ Mfanye haraka kabla hajarudi, maana ninauhakika atarudi muda mfupi ujao atakapogundua hana ile chipu. Sawa nawasubiri” Yule Binti aliongea kisha akakata simu. Akaichukua bahasha akaiweka ile chipu kisha akaiingiza ndani ya begi lake la nguo. Kisha akatoka kwenda sebuleni kuendelea na shughuli zake.
Basi Sajenti hakutaka kupoteza muda, hapohapo aliondoka upesi na kwa umakini wa ajabu aliingia sebuleni bila ya Yule binti kumuona wakati huo Yule binti alikuwa akipiga deki, kilichomshtua Yule binti ni mlango wa sebuleni kujigonga lakini alipoutazama aliukuta umefungwa.
ITAENDELEA
OFA hii isikupite!
MLIO WA RISASI HARUSINI
Kitauzwa Kwa Tsh 10,000 badala ya Tsh 15,000.
Mwisho WA OFA ni tarehe 14/10/2021
TUMA PESA KWA NAMBA
0693322300
Airtelmoney
Robert Heriel