Road Trip yangu ya Kukumbukwa mwaka 2018

Road Trip yangu ya Kukumbukwa mwaka 2018

Wewe we have something in common nami, nami napenda sana hizo nyimbo, nikibadilisha hapo ni msondo, sikinde, vijana jazz ,tatunane etc etc,nikimpa lift mtu wa kuiga amapiano nitamshusha middle ya kitonga pass au kwa huruma katikati ya mikumi national park
safi sana
 
View attachment 2400731
Unatandika samaki wa kuchoma na ugali wa dona laini kidogo na mboga nyingi ya majani, samaki unamchapa limao ya kutosha, ukimaliza unakaa nusu saa unatandika maji ya kutosha then unaanza kuvuta shots za kitajiri za whiskey yako kama unalamba lips kumbe ndio unameza hivo, baadae unamsikiliza franco, unarudi kwa fally na ferre gola, ukiwa unasinzia unamtafuta mbilia bel nakei nairobi, unaweka celin dion sauti ya mbali sana hadi unasinzia huku ukiwaza mipango yako ya kesho.
Hahaha, inakua safi sanaaa..kinywaji murua kimenogesha story kabisa..nikajua wanasafiri hamna drinks, ingekua safari mbovuu haina haja ya uzi.
 
Sijawahi kuielewa supu ya samaki, huwa naona kama unakunywa maji yenye shombo hivi...
pole sana ndg yangu.
mwaka juzi nyumbani kwangu tuliwahi kuwa na dada wa kazi kutoka mkoa fulani.

alikuwa ni mchapakazi hodari, shida yake ilikuwa ni ulaji wa nyama ya kuku.

ukileta nyama ya kuku nyumbani, atapika na kuiunga vizuri, ila ikija mezani hali. cha ajabu mayai yake alikuwa anakula.

siku moja wife akamuuliza kwanini hali nyama ya kuku, akajibu ni sharti la huko kwao alikotoka, bibi yake alimwambia siku akila kuku ataugua ghafla homa kali.

basi tukawa tunaishinae kwa style hiyo.
View attachment 2401047
 
Hahaha, inakua safi sanaaa..kinywaji murua kimenogesha story kabisa..nikajua wanasafiri hamna drinks, ingekua safari mbovuu haina haja ya uzi.
hahaha
 
Ujue kuna pombe ukinywa huoti ndoto mbaya, katandike hizi za bukubuku uone koo linavoanza kuwasha, kichwa kinakua kizito kama ulibeba matofari basi tu dunia haina usawa
hii comment imenivunja mbavu sana. haya weekend ndio hii imeshaanza.
 
Huu uzi hauja utendea haki.
Naandika article hii baaada ya kupata inspiration kupitia uzi wa rrondo Wazee wa ‘road trip’ mpo?. Mimi ni subscriber wa uzi huu.

Ilikuwa december 2018 nikiwa na jamaa zangu watano wa idara fulani.Katika hao watano mmoja alikuwa dereva.

Gari tuliyotumia ni off-road toyota land cruiser 4.5 v8 dlx 2013. Mimi sio mtaalamu wa magari, watu wa magari mnajua speed yake na namna inavyoweza kuhimili mikimikiki ya safari ndefu.

Trip ilianzia dar mpaka musoma. We stayed at musoma for six days. Then we left for another roadtrip to Bukoba.

Tuliondoka Musoma saa 11 asubuhi. Around saa nne asubuhi tukafika kivuko cha Kigongo-Busisi Mwanza. Tukavuka na kuanza safari ya kuitafuta Geita Town.

Tulifika Geita na kupumzika kwa nusu saa. baada ya mapumziko tukaanza safari ya kuitafuta Chato.

Tulipita Buzirayombo, Itari then Chato. Tulisimama kidogo kwenye makazi ya marehemu Magufuli. Tukapiga story kidogo na jamaa zetu tuliowakuta pale nje kwenye Mgahawa wake. Sina hakika kama ule mgahawa bado unaendelea kutoa huduma au lah.

Wale jamaa zetu wakatukaribisha supu ya samaki Sato. Hatukulaza damu, supu ilikuwa tamu sana. Wale sato walikuwa ndio kwanza wametoka kuvuliwa ziwani, si unajua tena kanda ya ziwa.

Mwaka 2018 Magufuli alikuwa wa moto sana, he was in his prime time kiasi kwamba kama ulikuwa safarini na gari ukatize Chato jirani na makazi yake, unajikuta tu unakatiza kwa heshima na adabu(nimechomekea tu, hili sio jukwaa la siasa[emoji1787]).

Basi tukaamsha zetu kuitafuta Nyamirembe, Katemwa, pori la Biharamuro, Nyakabongo, Kyamyorwa, Muleba na hatimaye around saa tatu usiku tukaingia zetu Bukoba town.

Tulikuwa hatuna haraka, mwendo wetu ulikuwa very reasonable kama watalii vile. Tulisimama mara kwa mara njiani kupiga picha na simu zetu.

Kwangu hii ni trip ya kukumbukwa sana, ilijaa matukio mengi ya furaha, utani, vicheko na story za hapa na pale.

Kipande cha kutoka Geita kuitafuta Chato tulichangamka sana, kwasababu tukiwa Geita tulinunua chupa mbili kubwa za Jameson. Mimi na wenzangu wanne ndio tulikuwa tunazinywa.

Dereva wetu ni kijana wa kipemba, ustaadh fulani mjanja mjanja. Yeye na mambo ya ulevi tofauti. Starehe yake kubwa ni watoto wa kike[emoji1787].

Naambatanisha kipande cha video nilicho record siku hiyo. Ila sikumbuki exactly ni aneo lipi. Nadhani ni Nyamirembe au Nyakabongo. Nawaachia assignment wakali wa location.

NB:
Mmoja kati ya jamaa yangu niliyekuwanae kwenye hii road trip ameshatangulia mbele ya haki miezi mitatu iliyopita. I dedicate this thread to him. May his soul continues to rest in peace. We are dust and to dust we shall return.
Nilitarajiwa kuona V8 ikikata mbuga/lami Ila umeweka video ya miti na ziwa
 
Nilitarajiwa kuona V8 ikikata mbuga/lami Ila umeweka video ya miti na ziwa
niwie radhi ndg.
front view video ya hii roadtrip ipo, ila file ni kama limekuwa damaged maana ni siku nyingi sana(2018).kila nikijaribu ku transfer kutoka kwenye flash disk kuja kwenye simu, inakataa

badala yake nakuwekea hii. hapa ni 2020, nikiwa na jamaa zangu tuki drive toka singida kuelekea arusha. sikumbuki ni eneo gani nilirekodi hii video maana siko familia sana na barabara ya singida-arusha. ila ninachokumbuka tulikuwa tunaitafuta katesh.

ilikuwa ni miezi ya masika, bila shaka utaenjoy kutazama front view ikionyesha barabara, landscape na uoto wa asili.

NB:
ilikuwa ni trip ya kikazi, gari tuliyotumia ni toyota hiace wagon grand cabin, mali ya taasisi fulani.enjoy.
 
Naandika article hii baaada ya kupata inspiration kupitia uzi wa rrondo Wazee wa ‘road trip’ mpo?. Mimi ni subscriber wa uzi huu.

Ilikuwa december 2018 nikiwa na jamaa zangu watano wa idara fulani.Katika hao watano mmoja alikuwa dereva.

Gari tuliyotumia ni off-road toyota land cruiser 4.5 v8 dlx 2013. Mimi sio mtaalamu wa magari, watu wa magari mnajua speed yake na namna inavyoweza kuhimili mikimikiki ya safari ndefu.

Trip ilianzia dar mpaka musoma. We stayed at musoma for six days. Then we left for another roadtrip to Bukoba.

Tuliondoka Musoma saa 11 asubuhi. Around saa nne asubuhi tukafika kivuko cha Kigongo-Busisi Mwanza. Tukavuka na kuanza safari ya kuitafuta Geita Town.

Tulifika Geita na kupumzika kwa nusu saa. baada ya mapumziko tukaanza safari ya kuitafuta Chato.

Tulipita Buzirayombo, Itari then Chato. Tulisimama kidogo kwenye makazi ya marehemu Magufuli. Tukapiga story kidogo na jamaa zetu tuliowakuta pale nje kwenye Mgahawa wake. Sina hakika kama ule mgahawa bado unaendelea kutoa huduma au lah.

Wale jamaa zetu wakatukaribisha supu ya samaki Sato. Hatukulaza damu, supu ilikuwa tamu sana. Wale sato walikuwa ndio kwanza wametoka kuvuliwa ziwani, si unajua tena kanda ya ziwa.

Mwaka 2018 Magufuli alikuwa wa moto sana, he was in his prime time kiasi kwamba kama ulikuwa safarini na gari ukatize Chato jirani na makazi yake, unajikuta tu unakatiza kwa heshima na adabu(nimechomekea tu, hili sio jukwaa la siasa[emoji1787]).

Basi tukaamsha zetu kuitafuta Nyamirembe, Katemwa, pori la Biharamuro, Nyakabongo, Kyamyorwa, Muleba na hatimaye around saa tatu usiku tukaingia zetu Bukoba town.

Tulikuwa hatuna haraka, mwendo wetu ulikuwa very reasonable kama watalii vile. Tulisimama mara kwa mara njiani kupiga picha na simu zetu.

Kwangu hii ni trip ya kukumbukwa sana, ilijaa matukio mengi ya furaha, utani, vicheko na story za hapa na pale.

Kipande cha kutoka Geita kuitafuta Chato tulichangamka sana, kwasababu tukiwa Geita tulinunua chupa mbili kubwa za Jameson. Mimi na wenzangu wanne ndio tulikuwa tunazinywa.

Dereva wetu ni kijana wa kipemba, ustaadh fulani mjanja mjanja. Yeye na mambo ya ulevi tofauti. Starehe yake kubwa ni watoto wa kike[emoji1787].

Naambatanisha kipande cha video nilicho record siku hiyo. Ila sikumbuki exactly ni aneo lipi. Nadhani ni Nyamirembe au Nyakabongo. Nawaachia assignment wakali wa location.

NB:
Mmoja kati ya jamaa yangu niliyekuwanae kwenye hii road trip ameshatangulia mbele ya haki miezi mitatu iliyopita. I dedicate this thread to him. May his soul continues to rest in peace. We are dust and to dust we shall return.
R I p
 
Sijawahi kuielewa supu ya samaki, huwa naona kama unakunywa maji yenye shombo hivi...

Jiandae, nakuandalia trip ya kwenda kula samaki wa maziwa ya Tabora.

Samaki wanachemshwa supu kisha wanapakwa asali na kubanikwa....

Ukitengewa unapewa supu pembeni na samaki aliyebanikwa na asali....

Usijesema Tabora kuna ulozi, ni Mahaba na ukarimu tu kwa wageni...😊😊
 
Jiandae, nakuandalia trip ya kwenda kula samaki wa maziwa ya Tabora.

Samaki wanachemshwa supu kisha wanapakwa asali na kubanikwa....

Ukitengewa unapewa supu pembeni na samaki aliyebanikwa na asali....

Usijesema Tabora kuna ulozi, ni Mahaba na ukarimu tu kwa wageni...[emoji4][emoji4]

nilikuwa tabora december 2021 na hiyo ndio ilikuwa trip yangu ya kwanza kufika mkoa huo.

sijui kwanini sikuulizia kuhusu hao samaki wanaopakwa asali.
 
nilikuwa tabora december 2021 na hiyo ndio ilikuwa trip yangu ya kwanza kufika mkoa huo.

sijui kwanini sikuulizia kuhusu hao samaki wanaopakwa asali.

Wanapatikana kwa oda, Bi. Kalunde ndo mtaalamu wa kuwaandaa.

Hutojutia ukifika wakati mwingine.
 
Back
Top Bottom