Robert Amsterdam athibitisha kufungua mashitaka ya uhalifu dhidi ya binadamu kwa Tanzania ndani ya ICC jumatatu

Robert Amsterdam athibitisha kufungua mashitaka ya uhalifu dhidi ya binadamu kwa Tanzania ndani ya ICC jumatatu

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
11,795
Reaction score
36,704
Baada ya gwiji la sheria la kimataifa ndugu Robert Amsterdam kufanikiwa kuishawishi idara ya mambo ya nje ya Umoja wa Ulaya kuijadili Tanzania dhidi ya ukiukwaji wa haki za binadamu na hatimaye kusubiri hatua rasmi za kinidhamu kuchukuliwa, sasa Robert amethibitisha rasmi kuwa jumatatu anaenda ICC kufungua mashitaka dhidi ya uhalifu wa binadamu nchini Tanzania.

Kwa mujibu wa kanuni za ICC, endapo mashitaka yatafunguliwa basi Tanzania itahitajika kupeleka utetezi wake na kisha pande zote mbili kujadiliwa kwa kina.

Sasa mataifa mbalimbali yanaendelea kuchukua hatua dhidi ya Tanzania baada ya ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na uhuru kipindi cha uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.
 
Mkuu G Sam kama mlivyojifariji na nyomi za kutengenezwa mitandaoni kuwa NiYeyeee, ndivyo hivyo hivyo kesi ya kusadikika mnaipamba mitandaoni. Au mnasahau mauaji ya kutisha Kenya na viongozi wakafunguliwa kesi hukohuko isiyo na miguu wala kichwa!

Mtasubiri sana hao viongozi wenu, wanasiasa uchwara, wenye ulafi wa madaraka, kuiongoza Tanzania.
 
Mkuu G Sam kama mlivyojifariji na nyomi za kutengenezwa mitandaoni kuwa NiYeyeee, ndivyo hivyo hivyo kesi ya kusafikika mnaipamba mitandaoni. Au mnadmsahau mauji ya kutisha Kenya na vionhozi wakafunguliwa kesi hukohuko isiyo na miguu wala kichwa!

Mtasubiri sana hao viongozi wenu, wanasiasa uchwara, wenye ulafi wa madaraka, kuiongoza Tanzania.
Tuko pamoja na rafiki yetu mpendwa Bob Amsterdam. Mungu ambariki sana huyu mzungu!
 
Back
Top Bottom