Rodri ashinda Ballon d’Or 2024, kiungo mkabaji wa kwanza kushinda tuzo hiyo

Rodri ashinda Ballon d’Or 2024, kiungo mkabaji wa kwanza kushinda tuzo hiyo

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mshindi wa Ligi Kuu ya Uingereza na Euro, Rodri, ametangazwa kuwa mchezaji bora wa kiume duniani kwa mwaka 2024, akiwa kiungo mkabaji wa kwanza kushinda tuzo hiyo.
IMG_0434.jpeg

Kiungo wa Manchester City, Rodri, ametunukiwa tuzo ya Ballon d’Or baada ya msimu bora uliomletea mafanikio katika ngazi ya klabu na timu ya taifa. Alisaidia klabu yake kushinda taji la nne mfululizo la Ligi Kuu ya Uingereza mwezi Mei, akionesha kiwango bora baada ya msimu mzuri wa 2022/23.
IMG_0438.jpeg

Aidha, alitunukiwa tuzo ya Mchezaji Bora wa Mashindano ya UEFA EURO 2024 kutokana na uchezaji wake mzuri wakati Uhispania iliposhinda taji hilo nchini Ujerumani.
IMG_0435.jpeg

Rodri alikabidhiwa tuzo hiyo katika hafla iliyofanyika Paris siku ya Jumatatu, Oktoba 28 iliyoandaliwa na jarida la Ufaransa la France Football kwa ushirikiano na UEFA.
IMG_0437.jpeg

Soma, Pia:

Majina ya Vinicius Jr na Jude Bellingham yaondolewa kwenye Viti vyao katika Hafla ya Ballon d’Or usiku huu

Rodri atua na magongo ndani ya Paris kupokea Ballon d'Or aliyoporwa Vinicius Jr
 

Attachments

  • IMG_0433.jpeg
    IMG_0433.jpeg
    167.4 KB · Views: 9
Mshindi wa Ligi Kuu ya Uingereza na Euro, Rodri, ametangazwa kuwa mchezaji bora wa kiume duniani kwa mwaka 2024, akiwa kiungo mkabaji wa kwanza kushinda tuzo hiyo.
View attachment 3137744
Nyota huyo wa Manchester City alisaidia klabu yake kushinda taji la nne mfululizo la Ligi Kuu ya Uingereza mwezi Mei, akionesha kiwango bora baada ya msimu mzuri wa 2022/23.
View attachment 3137736
Ni DM wa kwanza kushinda toka 1996 sio DM wa kwanza ever.

Mwaka 1996 Mathias Sammer alishinda na ndio DM wa mwisho kushinda kabla ya Rodri.
 
Kushinda Ballin d'Or huku una rangi nyeusi ni sawa na ngamia kupenya kwenye tundu la sindano...
kina george weah , Gaucho mbona wameshinda. Hio sio sababu kama mtu ni bora ni bora tu usilete mambo ya colour.
Wakina mbappe, Vini jr na yamal miaka 2 or 3 ijayo wanaweza kushinda tuzo hio kama wakichafua vyakutosha.
Rodri kapewa tuzo sio kwasababu ya colour bali anastahili kubeba tuzo hio.
 
Miaka inavyokwenda hizi tuzo zinazidi kupoteza mvuto... Rushwa, siasa na ubaguzi ndio vimeshika hatamu...

Hongera kwa Rodrí by the way, amestahili pia.
Jidanganye!
Zinapoteza mvuto wakati wachezaji wengine bado wanaiota hiyo tuzo!
Juzi tu hapa AA Trent amesema ndoto yake ni kuwa right back wa kwanza kushinda Ballon d'or, wewe unang'atwa na mbu huku Tanganyika unaamini tuzo zinapoteza mvuto.
Wewe sema tu kuwa mchezaji unayetaka ashinde hajashinda, ila hadhi ya Ballon d'or bado ipo palepale.

Unafanya mchezo na golden ball wewe!
 
Hii tuzo kumpa Rodri alistahili kabisa... Wangempa Vini jr ingekuwa ni robery ya wazi kabisa.

Hata Lautaro Martinez alistahili kubeba au kuwa wa pili kwenye list lakini sio vinicious
Shida ni kwamba top 3 ilitawaliwa na wachezaji wa Madrid, na hivyo mashabiki wa Madrid walivyo wengi hapa duniani walifanikiwa kujazana ujinga kuwa mchezaji wao ndio anastahili kubeba tuzo ya mwaka huu.
 
Mimi binafsi sijawahi kuwa shabiki wa tuzo hizi, naamini mpira ni team hauchezwi kama Tennis hakuna mchezaji mmoja akawa bora anaweza kuwa ni special kuliko wenzake lakini ni team ndio mafanikio yanakuja ni kama music awards kama ni band bora inachaguliwa group bora hakuna mwanamziki bora atachaguliwa kutoka kwenye kundi hata kama yeye ni star wa Band. Mpira ndio hivyo bila wenzako 10 nyuma yako hata uwe na mabawa utakabika tu. Ila Madrid utoto mwingi unazira team nzima sababu hamjashinda?
 
Back
Top Bottom