Roho ni nini? inaenda wapi baada ya kufa?

Roho ni nini? inaenda wapi baada ya kufa?

Ubaya na uzuri ni kitu kimoja / like darkness and light /noise and silence..
You can't have one without the other.
Mwanga hutokea gizani.
Hujajibu swali langu, Mungu alishindwa kuumba ulimwengu ambao kuna uzuri lakini ubaya haupo na hauwezekani kuwepo?

Hili ndilo swali langu, ambalo hujalijibu.
 
Nimekaa hapa napiga ugali na mlenda na dagaa wakavu huku nasoma hii post yako na nimecheka hadi nimepaliwa...

Jamaa akaniuliza "sasa si hicho kisimu chako cha mchina utakidondoshea kwenye huo mlenda?" Nikamjibu nasoma "vurugu" za jamaa huku mtandaoni jombaa na hakidondoki kitu hapa iwe dagaa au haka ka mchina....

Huwa nasoma post zako maana unaandika kama mashairi hivi na inavutia sana kusoma...

Hiki ndicho nilichokibakiza....
Umeandika hadithi nzuri, lakini hujajibu swali nililouliza.

Mungu alishindwa kuumba ulimwengu ambao ubaya hauwezekani kufanyika?
 
Sasa hapo ndio ugumu wa biblia unapokuja. Yesu ni Mungu lakini Mungu huyo alikufa. Je alipokufa roho yake ilienda wapi?
.
Mungu ni Roho, Yesu ni mwili alimukaa Mungu(roho) hapa duniani ili kutenda yale aliyotenda.
Miili yetu irudiyo mavumbini tuna ahadi ya kufufuliwa siku ya mwisho na kuishi milele. Wa Yesu ulifufuka kama mtangulizi wetu kutuonyesha mfano ulio hai wa ile yetu itakavyofufuka na alipaa nao kuelekea mbinguni.

Huu ni mwili wa utukufu.
 
Umeandika hadithi nzuri, lakini hujajibu swali nililouliza.

Mungu alishindwa kuumba ulimwengu ambao ubaya hauwezekani kufanyika?
Umekisia tu kuwa nilikuwa na dhamira ya kujibu chochote hapa au una uhakika?

Nilichoandika ndicho nilitaka kuandika,hayo mengine ni yako wewe...
 
Umekisia tu kuwa nilikuwa na dhamira ya kujibu chochote hapa au una uhakika?

Nilichoandika ndicho nilitaka kuandika,hayo mengine ni yako wewe...
Nani kaongelea dhamira yako? Nani anakisia sasa wewe unayeongelea kwamba nimekisia kuhusu dhamira yako, ambayo siwezi kuijua - na hata nikiiongelea nitakuwa nakisia tu, hivyo wewe kusema nakisia nipointless, ingawa sikuwa naiongelea- au mimi niliyesema fact tu?

Mimi nimesema fact.

Fact ni kwamba hujajibu swali langu.

Au umejibu? Unataka kupinga hiyo fact?
 
.
Mungu ni Roho, Yesu ni mwili alimukaa Mungu(roho) hapa duniani ili kutenda yale aliyotenda.
Miili yetu irudiyo mavumbini tuna ahadi ya kufufuliwa siku ya mwisho na kuishi milele. Wa Yesu ulifufuka kama mtangulizi wetu kutuonyesha mfano ulio hai wa ile yetu itakavyofufuka na alipaa nao kuelekea mbinguni. Huu ni mwili wa utukufu.
Yooote hayo uliyoyaandika nisome andiko gani ili nielewe?
 
Kutokans na upotoshaji huo wa Shetani ndio maana hata Mfalme Sauli alimuendea yule mama mchawi wa Endor akimuomba amuinulie Nathan Nabii. Ni kweli yule mama mchawi wa Endor alimuinua 'Nathan' na aliweza kumtabiria Sauli kuwa yeye na watoto wake wangekufa kesho yake. Jambo hilo ni kweli lilitokea kwani Sauli aliuawa yeye na Watoto wake kama vile 'Nathan'alivyomtabiria.

Hata hivyo ambacho Mfalme Sauli hakufahamu ni kuwa yule aliyemuona hakuwa Nathan bali ni roho wa Shetani aliyevaa umbo la Nathan. Nabii Nathan alishakufa kitambo na pia roho wa Bwana alishamuacha Sauli.
.
Hizi tafsiri zilizo mawazo ya hisia zenu zinazojengwa juu ya itikadi ya madhehebu yenu ndio zimekua taabu kuu kwa wale wanaowasikia.
Nafikiri unamzungumzia Samweli na wala siyo Nathan. Biblia inasema kuwa aliyepandishwa kutoka kaburini ni Samweli. Wala haijawahi kutoa ufafanuzi popote wa aya hizi zimhusuzo Samweli.

1 Samweli 28
14 Naye akamwuliza, Ni mfano wa nini? Akajibu, Ni mzee anazuka; naye amefunikwa vazi. Basi Sauli akatambua ya kwamba ndiye Samweli mwenyewe, akainama uso wake mpaka nchi, akasujudia.

15 Ndipo Samweli akamwambia Sauli, Mbona umenitaabisha mimi, hata kunipandisha juu? Sauli akajibu, Mimi nimetaabika sana; kwa kuwa hao Wafilisti wananifanyia vita, naye Mungu ameniacha; hanijibu tena, wala kwa manabii, wala kwa ndoto; kwa hiyo nimekuita wewe, ili wewe unijulishe nifanyeje.
 
Yooote hayo uliyoyaandika nisome andiko gani ili nielewe?
Uelewa wa hili haupo katika mstari mmoja bali kusudi lote la kuandikwa biblia. Soma biblia yote ukiwa umetulia na kumwomba roho wa Mungu akuongoze katika ufahamu/uelewa
 
Uelewa wa hili haupo katika mstari mmoja bali kusudi lote la kuandikwa biblia. Soma biblia yote ukiwa umetulia na kumwomba roho wa Mungu akuongoze katika ufahamu/uelewa
Biblia yote haizunzumzii kitu kimoja tu. Ina mambo mengi. Unaponiambie nisome biblia yote ni kukimbia wajibu wako wa kunifundisha.
Ndio maana Ufunuo wa Yohana hauzungumzi sawa na Injili ya Yohana.
 
Uelewa wa hili haupo katika mstari mmoja bali kusudi lote la kuandikwa biblia. Soma biblia yote ukiwa umetulia na kumwomba roho wa Mungu akuongoze katika ufahamu/uelewa
Mtu anapotaka kujua Yesu alizaliwa mji gani hawezi kusoma biblia yote.
 
Sasa hapo ndio ugumu wa biblia unapokuja. Yesu ni Mungu lakini Mungu huyo alikufa. Je alipokufa roho yake ilienda wapi?
Lakini kama ilivyoandikwa, mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu, mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao.

Inamaana kwamba kumpenda Mungu kunaendana sana na kutamani kujifunza kutoka kwake, kukubaliana na Neno Lake yaani inakupasa uamini pasipo kutilia shaka yoyote ile. [Hapa inakubidi ulazimishe akili zako za kibinadamu zikubaliane na kilichoandikwa]

Ndipo unaangaziwa mwanga wa kuyaelewa mambo ambayo akili ya kawaida ya kibinadamu ni ngumu kuyaelewa. Yaani kwa kifupi unavuviwa hali ya UFAHAMU wa kiroho.
 
Ni aghalabu sana kiongoz wa kiimani kuruhusu waumini na wasio waumini kuuliza maswali baada ya mada. Pengine utamaduni wa kuuliza maswali magumu ungekuwa ni Lazima, tusingeshuhudia utitiri wa madhehebu duniani, mengi yakiwa kwa maslahi ya viongozi wao.

Ni kiongoz mmoja tu (anayefahamika kwa sasa duniani) ambae ameenda mbali zaidi na kuruhusu maswali hata nje ya mada alizozungumzia na amekuwa akijibu kwa ufasaha na kutoa hata marejeo. Huyo Si mwingine bali ni Dr. Zakir Naik. katika video hii amejibu kuhusu kifo, kukata roho, roho ni nini na inaenda wapi baada ya kifo?


Ni aghalabu sana kiongoz wa kiimani kuruhusu waumini na wasio waumini kuuliza maswali baada ya mada. Pengine utamaduni wa kuuliza maswali magumu ungekuwa ni Lazima, tusingeshuhudia utitiri wa madhehebu duniani, mengi yakiwa kwa maslahi ya viongozi wao.

Ni kiongoz mmoja tu (anayefahamika kwa sasa duniani) ambae ameenda mbali zaidi na kuruhusu maswali hata nje ya mada alizozungumzia na amekuwa akijibu kwa ufasaha na kutoa hata marejeo. Huyo Si mwingine bali ni Dr. Zakir Naik. katika video hii amejibu kuhusu kifo, kukata roho, roho ni nini na inaenda wapi baada ya kifo?


This fellow is simply ignorant of many things, whetever he said about soul is stark nonsense. He is fallacious in his arguments. Quran is just a story book,
 
Biblia yote haizunzumzii kitu kimoja tu. Ina mambo mengi. Unaponiambie nisome biblia yote ni kukimbia wajibu wako wa kunifundisha.
Ndio maana Ufunuo wa Yohana hauzungumzi sawa na Injili ya Yohana.
.
Biblia inazungumzia kusudi lililoshikana nalo ni kuumbwa kwa ulimwengu na vyote vilivyomo, kuanguka kwa mtu/binadamu , ukombozi wa mtu alieanguka, njia Mungu alizo/anazopitia hata ukamilifu.

Mistari mingi ya biblia imelibeba/ficha hili kusudi ndio maana biblia haisomwi tu kama gazeti ila inasomwa ndani ya mstari kuweza kufunua kusudi la kuandikwa kwake.
 
Hao ni wanaomuelezea Mkuu.

Yesu hawezi kuwa Mungu Mkuu. Mimi mwenyewe ni Mkristo lakini napingana na hilo mpaka kifo.

Mtu kutenda miujiza hakumfanyi kuwa Mungu. Kuwa na mambo ya ajabu hakumfanyi kuwa Mungu.

Yesu ni Binadamu kama walivyowanadamu wengine.

Usipotoke.
Wewe ni mkristo wa dhehebu gani??
 
Roho ndio mtu mwenyewe halisi...Mwili ni kama jumba tu (housing) la roho ya binadamu..Mtu halisi yupo ndani ya mwili.
 
Binadamu anapokufa huenda kukusanywa na jamaa ya watu wake waliotangulia,,,mahali pa kusubiri katika ulimwengu usioonekana..Ona mfano wa Musa au Ndugu yake haruni....Torati 32:48-50
 
Ni aghalabu sana kiongoz wa kiimani kuruhusu waumini na wasio waumini kuuliza maswali baada ya mada. Pengine utamaduni wa kuuliza maswali magumu ungekuwa ni Lazima, tusingeshuhudia utitiri wa madhehebu duniani, mengi yakiwa kwa maslahi ya viongozi wao.

Ni kiongoz mmoja tu (anayefahamika kwa sasa duniani) ambae ameenda mbali zaidi na kuruhusu maswali hata nje ya mada alizozungumzia na amekuwa akijibu kwa ufasaha na kutoa hata marejeo. Huyo Si mwingine bali ni Dr. Zakir Naik. katika video hii amejibu kuhusu kifo, kukata roho, roho ni nini na inaenda wapi baada ya kifo?



Roho ni nguvu ya uhai ya viumbe hai. Kila kiumbe hai kina roho ya uhai na kinapokufa maana yake uhai katika huo mwili umetoweka.

Tofauti ya viumbe wengine wenye uhai na mtu ni moja kuu. Mtu ana nafsi na hii ndio utu yaani tabia ya Mungu ndani yake. Nafsi ni tabia ya roho ambayo ndio uungu. Wanyama na mimea wana roho ya uhai lakini hawana utu yaani nafsi.

Roho haifi ila huhama na mwili wa damu na nyama ulioachwa na roho hurudi mavumbini bali nafsi ya ule mwili humrudia muumba ambae ndie asili yake
 
Binadamu ana sehemu tatu,,MWILI,,NAFSI NA ROHO...Nafsi inajumuisha eneo lote la ufahamu(mawazo, maamuzi, dhamira na hisia) ila nafsi imefungamana na Roho ya binadamu.


Kitabu cha Ayubu 38:36
"Je! ni nani alietia hekima moyoni?
Au ni nani alietia ufahamu rohoni?" Wengi wametatanishwa na swala kwamba mawazo yanaanzia kichwani au moyoni?? Hata Albert Einstein nimemwona ktk utata huu..Binadamu yuko asilimia kubwa ktk roho.

Na yapo maisha mengine baada ya haya katika reality..
 
Back
Top Bottom