Roma Mkatoliki amwibua Mwakyembe, adai hana elimu ya kumshauri yeye mwenye digrii 4. Kama anapenda siasa aanzishe chama cha siasa

Roma Mkatoliki amwibua Mwakyembe, adai hana elimu ya kumshauri yeye mwenye digrii 4. Kama anapenda siasa aanzishe chama cha siasa

ROMA: KWETU BIMA YA AFYA NI BORA KULIKO IZO NDEGE.

"Yuda usimuharibie Dani ili umfurahishe Mtukufu, Sisi sote wanao kwa nini unampenda Yusuph.

Yakobo Baba Pesa Madaraka Umaarufu Ona umewapatia vijana wanakosa Hekima na Utu.

Wapunguzie Vifungo, Wafungwa wasio na hatia, Wengine walifata mkumbo kiukweli hawakuwa na Nia.

Nasikia Jimbo la Ubungo kuna mtu amelipania, Hizi tungo ni zaidi ya Waraka wa Waebrania.

Chama kilishawatimua Wanasiasa mlio wanunua, Yaani mnapiga Bomu Mochwari halafu mnajisifu mumeua !

Tuliombe Taifa tuwaombee Viongozi wetu, Nchi ina miiba sio tuwavishe viatu walioko peku.

Tusilete Uchama kwenye ishu za Kitaifa, Uongozi ni kuacha Alama Chanya na kuwajibika, Kutekana kuuana sio sifa ya Mtanganyika.

Hongera Baba kwa ukusanyaji wa Mapato Kedekede, ya kodi, Na Flyover ndo hizo kanyanga Twende, Kwetu Bima ya Afya ni Bora kuliko izo Ndege.

Atafanya yote Tumuombee yesu Nibebe, Watu wametumbuliwa kabla ya mwezi mmoja kustaafu, Walimu wamesahauliwa mapato yao, Halafu, Polisi mishahara yao hadi tuwapige tafu, boresha Mahospitalini tupunguze idadi ya Wafu."-Roma Mkatoliki.

#AnaitwaRoma..
Naomba kuwasilishaa wanazengo
 
"Kama msanii unang'ang'ana kuimba siasa na kukosoa serikali basi amua kuachana na muziki uanzishe chama cha siasa. Lakini kama unataka kupata maslahi kwenye muziki, basi nyimbo hizo hazilipi. Haiingii akilini nina shahada nne halafu msanii ambaye hajaenda hata shule anatunga nyimbo za kunikosoa. Wewe na darasa la nne lako sijui la 7 utanionya mimi mwenye degree nne na nimefundisha vyuo vikuu mbalimbali?" Dr.Harisson Mwakyembe (PhD), Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo.!
Kwa hiyo hata akikutwa kasahau kufunga zipu na hajavaa kaboka asiambiwe na ngumbaru aachwe tu kwa maana digrii nne zinaficha aibu!!!???
Ukiwa ccm bhana!!!
 
"Kama msanii unang'ang'ana kuimba siasa na kukosoa serikali basi amua kuachana na muziki uanzishe chama cha siasa. Lakini kama unataka kupata maslahi kwenye muziki, basi nyimbo hizo hazilipi. Haiingii akilini nina shahada nne halafu msanii ambaye hajaenda hata shule anatunga nyimbo za kunikosoa. Wewe na darasa la nne lako sijui la 7 utanionya mimi mwenye degree nne na nimefundisha vyuo vikuu mbalimbali?" Dr.Harisson Mwakyembe (PhD), Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo.!
Ndo ushamjibu hivyo
 
Roma arudi shule jamani

Mtu anaefundisha au aliwahi kufundisha chuo sio wa kumfananisha na alieishia darasa la saba jamani huo ni ukweli usiopingika

Mwakyembe alipasua GPA kubwa Bachelor akabakizwa kuwa mwanataaluma UDSM huwezi fananisha na Msanii yeyote hapa nchini

Mkuu, nadhani umeandika vitu ambavyo sio ukweli. Mh. Waziri alisoma Diploma ya Uandishi wa habari hapo University of dar es salaam mwaka 1977. Alianza kufundisha USDM 1984 kutokea kwenye nyazifa mbali mbali serikalini Na sio kwamba eti kwasababu alikuwa na uwezo mkubwa kiakili au GPA kubwa ndio sababu ya yeye kufundisha hapo UDSM. Pia ata elimu yake inamashaka sana, nadhani ameweza kufika hapo alipo kwasababu ya Siasa.

Asante
 
Ukiwa na PHD maana yake wewe ni mjuzi wa kitu kumoja tuuu, hapo ndiyo wasomi wetu wanakosea.
Kuona PHD ndiyo Unajua kila kitu ktk dunia Siyo sahihi hata kidogo.

Mkuu, sifa ya mtu mjinga siku zote "nikujikweza" kwamba anajua kila kitu na kuona watu wengine kwamba sio kitu. Kwenda shule na kupata certificates sio kipimo cha mtu kwamba ameelimika maana kuna factors nyingi zinaweza kusababisha mtu kufika hapo alipo. Kipimo pekee ni uwezo wa mtu kuonesha WISDOM( Busara) anapo zungumza ndio kipimo pekee chakutambua kama mtu ameelimika au lah.
 
Mwanamuziki ni mwanafasihi ni Kama mwandishi wa kazi za kifasihi anaweza kuandika au kuimba matatizo yanayoikumba Hadhira yake na kujaribu kutoa suluhisho kupitia kazi yake ya kifasihi.Mwambie huyo Dr ampe hai Farouk topan na Tamthiliya zake Aliyeonja Pepo na Mfalme Juha.
1573862906501.png
 
"Kama msanii unang'ang'ana kuimba siasa na kukosoa serikali basi amua kuachana na muziki uanzishe chama cha siasa. Lakini kama unataka kupata maslahi kwenye muziki, basi nyimbo hizo hazilipi. Haiingii akilini nina shahada nne halafu msanii ambaye hajaenda hata shule anatunga nyimbo za kunikosoa. Wewe na darasa la nne lako sijui la 7 utanionya mimi mwenye degree nne na nimefundisha vyuo vikuu mbalimbali?" Dr.Harisson Mwakyembe (PhD), Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo.!
Unaweza ukawa na degree 100 lakini you are useless kama Mwakyembe alivyo! Mwakyembe is useless. What matters is what you offer to the society! Roma is doing more good to the society compared to Mwakyembe!
 
Siku hizi degree ni mzigo na kupoteza muda tuu,
Hapa ni kudeal na kipaji ama kujiajiri ndo deal huyu mwakyembe ukimwambia ajiajiri atakufa na njaa na mtaji atafilisika


Ona mtoto wa tandale katoa ajira 200k huyo mwakyembe amemuajiri house boy and girl na dereva tuuu nyambafu
 
"Kama msanii unang'ang'ana kuimba siasa na kukosoa serikali basi amua kuachana na muziki uanzishe chama cha siasa. Lakini kama unataka kupata maslahi kwenye muziki, basi nyimbo hizo hazilipi. Haiingii akilini nina shahada nne halafu msanii ambaye hajaenda hata shule anatunga nyimbo za kunikosoa. Wewe na darasa la nne lako sijui la 7 utanionya mimi mwenye degree nne na nimefundisha vyuo vikuu mbalimbali?" Dr.Harisson Mwakyembe (PhD), Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo.!
Vidigrii vyake vinne havijamkomboa ndiyo maana anachokiweza ni upambe tu.
 
Roma arudi shule jamani

Mtu anaefundisha au aliwahi kufundisha chuo sio wa kumfananisha na alieishia darasa la saba jamani huo ni ukweli usiopingika

Mwakyembe alipasua GPA kubwa Bachelor akabakizwa kuwa mwanataaluma UDSM huwezi fananisha na Msanii yeyote hapa nchini
Sasa hiyo gpa yake inasaidia nn ?
 
huko alikokuwa anafundisha sindo wanapaita jalalani siku hizi[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28] halafu hizo degree nne sisi zinatudaidia nini mbona hazina msaada kwetu
 
"Kama msanii unang'ang'ana kuimba siasa na kukosoa serikali basi amua kuachana na muziki uanzishe chama cha siasa. Lakini kama unataka kupata maslahi kwenye muziki, basi nyimbo hizo hazilipi. Haiingii akilini nina shahada nne halafu msanii ambaye hajaenda hata shule anatunga nyimbo za kunikosoa. Wewe na darasa la nne lako sijui la 7 utanionya mimi mwenye degree nne na nimefundisha vyuo vikuu mbalimbali?" Dr.Harisson Mwakyembe (PhD), Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo.!
Awamu hii ina Rais wa aina yake.

Mwakyembe lazima atetee tumbo lake. Wameamrishwa. Suala likitokea lenye maudhui ya wizara zao, lazima wajitokeze kusema mfalme kavaa nguo tena anapendeza mno.

Yalimshinda Amos Makala kuhusu vitambulisho hewa vya kukusanya mapato. Kilichotokea na kutumbuliwa. Naamini ana amani ya moyo huko aliko.

Wengi wamebaki utumwani.
 
Back
Top Bottom