Hahahaaa....... Najazilizia CV ya Dr Mwakyembe!
Kwa mtizamo wako huo, believe me, huhitaji kuona CV ya Harrison George Mwakyembe.
Dr. Mwakyembe ni kichwa cha kuotea mbali.
Hana elimu ya kuunga unga.
Kwenu ninyi wadogo yapo ambayo hamyajui.
Baada ya Azimio la Arusha na kuanzisha Jeshi la Kujenga Taifa, ilikuwa ni lazima kufanya kazi miaka 2 kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu.
Ulitolewa mwanya maalum wa kujiunga na mafunzo ya shahada ya Udaktari na Uhandisi tu kutokana na uhaba uliokuwepo kwa kada hizo mbili.
Wengine wote iliwalazimu kufanya kazi miaka 2 kabla ya kwenda University.
Harrison Mwakyembe alipelekwa kufanya kazi Chuo cha Uandishi wa Habari, TSJ, kama Mkufunzi, ambako aliamua kusoma Upaparazi, kabla ya kuanza kuufundisha.
Na huu ni ushahidi tosha kuwa alikuwa kichwa!
Lakini kwa kumalizia, SIASA ni mdudu wa ajabu ambao Mbunge Kasheku Msukuma ni super star kuliko msomi mwenye digrii 4.
Huku duniani, mwenye digrii 4 ni kibarua cha mwenye darasa la saba.
Dr. Mwakyembe aache ulimbukeni na atambue kuwa nje ya kufundisha vyuoni, digrii 4 hazina umuhimu wowote.