Roma na wenzake wapatikana, wapelekwa Kituo cha Polisi Oysterbay kisha Mwananyamala Hosp na kuachiwa

Roma na wenzake wapatikana, wapelekwa Kituo cha Polisi Oysterbay kisha Mwananyamala Hosp na kuachiwa

Atuambie kwanza kipi kilichomsukuma kutuambia jana kuwa Roma atapatkana kabla ya J2 yaani leo kama si kuwa alkuwa anajua aliko.
Akiniweka sawa hapo ndo ntampa hongera yangu
Roma kapatikana, ataelezea tukio zima
 
What about Ben Saa Nane jamani.
Wajaribu kuvaa viatu vya wazazi ndugu na jamaa zake wako ktk Hali gani mpaka sasa?
Serikali vyama vya siasa mashirika ya utetezi vyombo vya ulinzi na usalama tafadhali tusaidieni kumpata Ben na wengine wasio na majina wanaoendelea kutoweka
 
Attention yote ya mkutano wa N.ape imehamishiwa Osterbay, still bado CCM haitakosa washangiliaji wavivu kufikiri.. ili tukio lilikua na maana fulani wenye brain tu ndio wataelewa. shame
 
Huu ni usanii mtupu, ngoja tusubiri tutaujua tu ukweli....Roma kutekwa kwa sababu zipi haswa, labda atekwe na Wenzake waliotofautiana kwa mambo yao.
 
Ila mkumbuke kuwa bunge linaendelea maigizo kama haya yatakuwa mengi sana, pia nazani watakuwa walienda kumpiga bit hakuna kumshambulia serikali na gamba lake.
 
Msanii Roma Mkatoliki anadaiwa kupatikana na yupo Kituo cha Polisi Oysterbay jijini Dar.

Habari ya akina Roma kupatikana imethibitishwa na Mkurugenzi wa Tongwe Records J. Mada.

Bado hakuna maelezo ya kutosha kuhusiana na wapi walipokuwa na nani waliokuwa wamewashikilia. Kwa sasa wanadaiwa kuwepo kituoni hapo kwa taratibu za kipolisi kwa kuwa jalada la kupotea kwao lilifunguliwa hapo.

Kupatikana kwao kumefuatia wito mkubwa uliokuwa ukipaishwa na wasanii wenzake na mashabiki kuhusu kuachiliwa huru, ndani na nje ya mitandao ya kijamii.

Awali, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Kamishina Simon Sirro alisema bado walikuwa wakiendelea na upelelezi wa tukio la kupotea (kutekwa) kwa msanii Roma Mkatoliki na wenzake.

Taarifa zaidi zinafuata..

View attachment 492792
View attachment 492791
Inauma sana kuona wasanii wanapotezwa kiajabuajabu kwa sababu tu ya kusimamia ukweli kupitia kazi zao za sanaa. Wakati hizi sinema zikiendelea, tukumbuke kuwa katika uchaguzi mkuu uliopita wasanii walikomaa mwanzo mwisho. Hapa ndipo tunapojifunza kuwa urafiki na baadhi ya watu ni sawa kabisa na urafiki kati ya paka na panya. Aidha, matukio haya ya utekaji yanatukumbusha usemi usemao 'SHUKRANI ZA PUNDA NI MATEKE'. Tuwashukuru wasanii waliosimama kidete kudai kurudishwa kwa msanii mwenzao, vinginevyo tungeokota mzoga unaelea mtoni kwenye kiroba. Eee Mungu tusaidie sisi waja wako tunaopukutishwa kama majani ya kiangazi kila kukicha. Amina.
 
Atakuwa ameachiwa kwa makubaliano maalumu ya, "ukiulizwa never mention so and so, badala yake sema mlikuwa na wenzako msitu wa Mabwepande kutembelea location ya video yenu île ambayo mtafanya shooting lakini mkawa mmepotea ndani ya msitu, tutakulipa compasation ya Tshs......... else ukileta ubishi tutakutaja ktk orodha ya watumiaji na wauza ngada na unaweza kufungwa jela miezi sita bila kupitia mahakama yoyote !! "

By the way, inasemwa wakati anatekwa walikuwa studio wakijiandaa kurekodi nyimbo kadhaa.

Tunaweza kuzijua hizo nyimbo ambazo walikuwa wanajiaandaa kuzirekodi na maudhui yake ??

I think, from there twaweza kupata picha nani alihusika ktk kutaka "kuwapoteza " hawa vijana, je ni wale wasiotaka kukosolewa na kutaka kusifiwa tu ama ??
 
Hata mimi kwa kweli, watu hawatumii akili, wanapelekwa tu kama mahindi ya kuchoma
Msiofikiri kwa kutumia vichwa asanteni. Wasanii na ndugu wameitisha conf. wakamtuhumu huyo bosi wenu kuwa anajua mwenzao alipo, muda mfupi naye anajitokeza anasema kabla ya jumapili atakuwa amepatikana, inafika jumamosi(ambayo obviously ni kabla ya jumapili) Roma anapatikana. Inahtaji kiwango gani cha elimu kujumlisha moja na moja na kupata 2??
 
Kama Polisi wanasema hatujui na tunafanya uchunguzi..! Na Bashite ambaye si polisi anasema tutampata kabla ya Jumapili..! na leo ni Jumamosi na habari inasema amepatikana...! Kwa busara ya kawaida tu tutasema nini hapa?
Hapo kuna walakini
 
Msanii MTU wa kawaida tuu...wanatekwa machezaji na familia zao majuu uko sembuse bongo bhanaaa...
 
Back
Top Bottom