google helper
JF-Expert Member
- Jun 11, 2013
- 9,623
- 13,759
AsanteROMAN ABRAMOVICH: MABILIONI YA DAMU, RISASI NA UMAFIA
SEHEMU YA 12
Mara ya mwisho nilieleza kuhusu vyombo vya habari vinavyomilikiwa na maoligarch wakiongozwa na Berezovsky walinyoanza kumkosoa Putin kwa lengo la kumuharibia kwa wananchi na hatimaye iwe rahisi kwao kumuondoa madarakani. Baada ya ukosoaji huu Putin kwenye moja ya hotuba zake aliwaambia wananchi kwamba kuna ‘genge’ la maoligarch wanaomiliki vyombo vya habari wanaendesha kampeni ya kumchafua kwa malengo yao ya kisiasa.
Unakumbuka nilieleza kwamba katika kipindi hiki Berezovsky alikuwa amejiingiza kwenye siasa. Alikuwa ni mwakilishi kwenye Bunge la Duma (GosDuma). Kwa hiyo madai haya ya Putin kwamba Berezovsky na wenzake wanamchafua kwa malengo ya kisiasa yalipata mashiko kwa sababu Berezovsky alikuwa ni mwanasiasa. Kwa hiyo wananchi waliona hii ilikuwa kama ni ‘move’ ya Berezovsky kuutaka urais wa Urusi. Wengi hawakupendezwa na hili maana walihisi huu haukuwa wakati sahihi kubadili Rais wa nchi kwa kuzingatia kwamba nchi ilikuwa kwenye mzozo mkubwa huko Chechenya na pia ulikuwa umepita muda mchache tu tangu kumbadilisha rais wa awali, Boris Yeltsin.
Ajabu ni kwamba baada ya hotuba hii ya Putin, safari hii sio tu kwamba Berezovsky alitumia vyombo vyake vya habari kumpinga Putin bali aliitisha mkutano na wanahabari na kumkosoa Putin na sera zake wazi wazi.
Putin na Abramovich hawakutaka kukurupuka kumshughulikia Berezovsky. Walikuwa na uwezo wa kutumia vyombo vya ulinzi kumkamata na kumtia gerezani Berezovsky lakini hii isingekuwa na ufanisi sana kwa sababu tatizo halikuwa Berezovsky peke yake bali ni yeye na genge lake. Na isingekuwa busara kuwakamata maoligarch wote na kuwatia gerezani kwani kutokana na ushawishi wao ingeweza kuzua taharuki kubwa kwenye nchi. Sasa wanafanyaje? Wamuache Berezovsky aendelee kutamba kwenye vyombo vya habari na kumchafua Rais?
Hapana… nyoka akiingia ndani ya shimo usizame na wewe kumfuata… msubiri juu. Hawezi kukaa shimoni milele… msubiri atokeze kichwa juu… mfyeke na upanga.
Usiwe na pupa,
Subiri…
Nilieleza kuhusu Badri Patarkatsishvili rafiki mkubwa wa Berezovsky ambaye alimletea Russia kusimamia Televisheni yake. Berezovsky na Badri walikuwa marafiki haswa lakini kulikuwa na mtu ambaye alikuwa rafiki mkubwa zaidi wa Berezovsky, rafiki wa kushibana haswa, rafiki wa damu haswa, mboni ya jicho kweli kweli ya Berezovsky. Huyu alikuwa anaitwa Nikolai Glushkov. Licha ya urafiki wao lakini pia walikuwa washirika wakubwa kwenye biashara.
Sasa turudi nyuma kidogo,
Pale Russia kuna shirika la ndege la umma linaitwa Aeroflot. Shirika hili ni moja ya mashirika kongwe zaidi ya ndege duniani. Mwaka 1995 Glushkov aliteuliwa kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Aeroflot. Baada ya mwaka mmoaja tangu kuteuliwa kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu kuna skandali kubwa aliibua japo haikufika kwa umma wakati ule lakini ilikuwa tafrani kubwa ndani ya ‘system’ ya serikali ya Russia.
Kipindi hicho ndani ya shirika kulitokea mkanganyiko mkubwa sana juu ya mapato ya shirika na matumizi yake. Glushkov akajipa jukumu la kuchimba ni nini hasa kilikuwa kinaendelea. Baada ya uchunguzi wake wa miezi kadhaa akang’amua kwamba fedha zote za shirika ambazo zilikuwa zinapatikana kutokana na mauzo ya tiketi ya ndege zilikuwa zinapelekwa kwenye zaidi ya akaunti 352 zilizotawanyika sehemu mbalimbali duniani. Akaja kugundua kuwa akaunti hizi zilikuwa zinatumiwana mashirika ya Usalama ya FSB, SVR na GRU kw ajili ya kugharamia shughuli za ujasusi nje ya Russia. Nilieleza kuhusu FSB, hawa wanahusika hasa na Couter-Intelligence na usalama wa ndani ya Russia na mipakani. SVR hawa wanahusika hasa na ujasusi nje ya Russia. GRU wao kwa kifupi twaweza kusema ni kama chombo cha intelijensia ya jeshi.
Glushkov akagundua kuwa pia waajiriwa 3,000 katiya waajiriwa wote 14,000 wa shirika la Aeroflot walikuwa ni mashushushu wa FSB, SVR na GRU.
Glushkov akakasirika na kuwaandikia barua vyombo hivyo vyote vya ujasusi. Katika barua hiyo kwanza aliwalalamikia vyombo hivyo kutumia rasilimali vya Aeroflot kwa shughuli zao za ujasusi bila ruhusa ya bodi ya Aeroflot wenyewe. Pili, aliwapa ‘bili’, Kiasi chote cha hela ambao mashirika ya ujasusi yalipokea kutoka Aeroflot na kuwataka warejeshe kwenye shirika.
Glushkov hakuishia hapo tu bali pia alihakikisha fedha zote ambazo zililipwa kwenye akaunti zile 352 ambazo zilikuwa bado hazijatolewa, utaratibu unafanyika akauti wakazi-freeze na kuhakikisha zinatolewa kwenye akaunti hizo. Makosa makubwa yalifanyika hapo…
Unaweza kujiuliza Glushkov aliwezaje kufanya haya dhidi ya shirika la ujasusi kama FSB, SVR na GRU? Lakini tukumbuke kwamba hii ilikuwa ni mwaka 1996 kwenye utawala wa Yeltsin ambapo maoligarch ndio walikuwa ‘wenye nchi’. Glushkov alikuwa anaweza kujitutumua na kufanya yote haya kwa mgongo wa oligarch Boris Berezovsky rafiki yake wa damu wa kufa na kuzikana.
Turudi tulipoishia…. Nyoka akiingia shimoni hatumfuati… tunasubiri atokeze kichwa nje tumfyeke.
Baada ya Berezovsky kuendelea kumkosoa kwa kutumia vyombo vyake vya habari… Abramovich akaja na mkakati wa kumdhibiti.
Abramovich akafukua kaburi skandali ile ya Nikolai Glushkov rafiki kipenzi wa Berezovsky. Jambo moja ambalo kipindi kile mwaka 1996 halikufuatiliwa kwa kina ilikuwa ni namna gani fedha zile zilizobakia kwenye akaunti 352 zilitolewa. Kwa sababu kipindi kile Abramovich alikuwa ni kipenzi pia cha Berezovsky kwa hiyo kuna siri nyingi alikuwa anazijua. Mojawapo ya siri hizi zilikuwa ni nini ambacho kilitokea kwenye fedha ambazo zilihamishwa kutoka kwenye akaunti zile 352.
Fedha zili kwa maelekezo ya Glushkanov zilihamishwa kutoka kwenye akaunti zile 352 za idara za ujasusi na zote kuwekwa akaunti ya kampuni iliyosajiliwa nchini uswisi inayoitwa Andava. Kampuni hii ya Andava ilikuwa inamilikiwa na watu wawili, Nikolai Glushkov na Berezovsky. Kwa maana nyingine ni kwamba Nikolai Glushkov na Berezovsky walikuwa wamejichukulia fedha za kampuni ya umma ya Aeroflot ambazo zilikuwa zimelengwa zitumiwe na FSB, SVR na GRU.
Hii ilikuwa silaha ya kwanza ya Abramvich kumshughulikia Berezovsky.
Polisi walimkamata Glushkov na kumfungulia mashtaka ya ubadhirifu wa mali za umma. Siku chache baada ya Glushkov kukamatwa Berezovsky alikimbia Russia na kuomba ukimbizi wa kisiasa nchini Uingereza kwa maana alijua kuwa yeye pia alihusika kwenye kosa hilo ambalo Glushkov alishtakiwa nalo.
Hii haikuwa muarobaini kamili wa kumshughulikia Berezovsky kwani japo alikimbilia Uingereza lakini bado alikuwa anamiliki kituo kile cha televisheni na kampuni nyingine kadhaa ambazo zilikuwa na ushawishi kiuchumi na kisiasa ndani ya Russia.
Abramovich akapiga hatua ya pili ya mkakati wake na kusafiri moja kwa moja hadi Uingereza ambako Berezovsky alikuwa amekimbilia…
Inaendelea usiku huu…
Habibu B. Anga "The Bold" - 0759181457
To Infinity and Beyond