Habibu B. Anga
JF-Expert Member
- May 7, 2013
- 6,557
- 25,717
- Thread starter
- #861
ROMAN ABRAMOBICH: UTAJIRI WA DAMU, RISASI NA UMAFIA
SEHEMU YA TISA
MUHIMU: Kabla sijaenda kwenye mada nijibu swali ambalo naulizwa kila mara kwenye comments na PM ili iwe clear. Utaratibu wa kujiunga na 'familia' yangu kule whatsapp ni malipo ya shilingi elfu tano kwa mwezi. That's it.
And nimeweka namba yangu, kwa hiyo ni vyema unitumie meseji direct badala ya PM. Nafungua PM mara chache sana kwa hiyo unaweza kuona sijajibu meseji yako ukajiuliza huyu somo vipi tena. PM nyingi mno, zinanielemea kwa hiyo najikuta sifungui zote.
And hili ni suala la hiyari, kwa wenye kupenda wamekuja wale ambao wanahisi hawawezi basi tutakuwa tunaonana hapa jukwaani. Nadhali hii imekaa sawa, hakuna haja ya kufanya kuhusu hili. Limeisha…
Twende kwa Oligarch Abramovich….
Nimewahi kuonana na wasomaji wangu wachache sana wa makala na vitabu vyangu. Sababu kubwa ya kutoonana sana na watu ni kwa vile katika maisha ya kawaida huwa siongei kabisa japo ni msikilizaji mzuri sana. Tunaweza kukaa nikakusikiliza kwa masaa manne straight bila kuchoka wala wala ‘kuboreka’. Ubaya ni kwamba watu wengi wanategemea uwaeleze mengi na ubaya ni kwamba kwa asili huwa siongei ndio maana nachagua kuandika sana labda ‘ku-compasate’ energy ninayo-reserve kwa kutokuongea. Hii ni moja ya sababu kwa nini mara nyingi huwa sionani na watu… I’m not a good company kama unahitaji mtu wa ‘kupiga story’. Lakini sababu ya pili ni umri… wengi wana picha fulani kichwani ya muonekano au umri wa huyu muandishi ‘The Bold’. Wachache ambao nimekutana nao wote kitu kimoja huwa wanakisema ni kwamba kwa umri huu nilionao nawezaje kuandika vitu ambavyo naandika? Inawezekana wanasema hivyo as a compliment but it makes me feel very uncomfortable. Kwa hiyo napendelea kuendelea kujificha kwenye kichaka cha ‘The Bold.’
Kwa nini nasema haya… unapomsoma mtu kwa muda mrefu sana na mambo makubwa ambayo ameyafanya kuna wakati fulani unaanza kujenga picha ya nje ya uhalisia.
Kwa mfano, kwa vitu vyote hivi ambavyo Roman Abramovich amevifanya… kufikia hatua ya hadhi ya Oligarch, kulichachafya Bunge la Russia, kumuondoa Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali, kujimilikisha kampuni kubwa zaidi ya mafuta ya serikali, kumshawishi Rais Boris Yeltsin kuondoka madarakani na kumtengeneza Rais mpya Vladimir Putin… unaweza kudhani kwamba Abramovich ni lizee fulani hivi lililo zaliwa na kukulia kwenye ‘system’… lakini nikukummbushe kwamba mpaka siku ile mwaka 2000 mwezi May kipindi Putin anaapishwa kuwa rais mpya wa Russia… Roman Abramovich alikuwa ni kijana wa miaka thelathini na tatu tu. Niweke mkazo kwa namba… miaka 33.
Kwenye sehemu iliyopita nilieleza kwamba baada ya Abramovich kujihakikishia umilki wa Sibneft na kisha kumshawishi Rais Yeltsin kuachia ngazi na baadae kumfinyanga Putin na kumweka madarakani sasa uliwadia wakati wa kuingia katika ‘utukufu mpya’.
Nchi ya Urusi kwa miongo mingi sana imekuwa ndio nchi inayoongoza duniani kwa uzalishaji wa aluminium na hata matajiri wa kubwa wa Russia utajiri wao unatokana na aluminium, mafuta na gesi. Kwa hiyo sekta hii ya aluminium ni moja ya uti wa mgongo wa uchumi wa Russia.
Kwenye miaka ya tisini na mwanzoni mwa 2000 baada ya serikali kuanza ubinafsishaji holela wa mali za umma ushindani ulikuwa mkubwa haswa na Russia haijawahi kushuhudia vifo vingi vya watu mashuhuri kama kipindi hiki. Katika kipindi hiki zaidi ya matajiri mashuhuri 100 waliuwawa kinyama na miili yao kuokotwa barabarani.
Kipindi hiki kichungu kinakumbukwa kama wimbi la ‘Aluminium wars’. Nitaomba kuchambua kwa kuingia miguu miwili yote nukta kwa nukta ili kukielewa nini kilitokea kwa sababu tukiweza kuelewa vyema nini kilitokea ni rahisi zaidi kuielewa hata hii Russia ya sasa na mwelekeo wake wa kisiasa.
Ilikuwaje… tuanze kwenye mzizi.
Ukuaji wa sekta ya aluminium nchini Russia ni matokeo ya miaka mingi sana ya serikali ya nchi hiyo kuwekeza nguvu kubwa sana kwenye kuendeleza sekta hii. Kama haujafahamu, aluminium inachimbwa kutoka kwenye migodi ya boksiti (bauxite) na kisha kuchakatwa kuwa alumina (aluminium oxide). Alumina iko kama unga unga fulani hivi mwepe au mfano mzuri kama ‘snow’ hivi. Hii ndio hutumika kuzalisha aluminium. Sasa Russia ni moja kati ya nchi za kwanza kabisa kufanya bunifu za kuchakata boksiti mpaka kupata alumina. Gunduzi za mwanasayansi kama Beyer ambaye alikuwa raia wa Austria miaka ya 1889 akiwa anafanyakazi St. Petersburg’s katika kiwanda cha kemikali cha Tenteleev ambapo aligundua mbinu ya kuchakata alumina kutoka kwenye boksiti kwa kutumia alkali za kaustiki. Baadae gunduzi za watu kama Muller na Packard ambao waligundua uvunaji wa alumina kwa kuifanyia decomposition ya aluminium hydroxide na kisha kufanyia electrolysis. Katika lugha nyingine twaweza kusema kwamba warusi ndio ‘pioneers’ wa namna za uvunaji alumina kutoka kwenye migodi ya boksiti. Hata mapinduzi makubwa ya upatikanaji wa umeme wa uhakika nchini Russia ambayo yalitokea kwenye karne ya 20 kwa kiasi kikubwa kulitokana na uhitaji mkubwa wa viwanda vya kuzalisha aluminium na malengo ya nchi hiyo kutaka kuongeza uzalishaji kila mwaka.
Kwa hiyo sekta hii ya aluminium kwa miongo mingi nchini Russia imekuwa haraka na kuwa sehemu ya uti wa mgongo wa nchi.
Sasa kwenye miaka ya tisini kipindi ambapo serikali ilikuwa inahama kutoka kwenye ujamaa na kuingia kwenye ubepari na kubinafsisha mali za umma kuna jambo la kiuhini likafanyika. Wafanyabiashara ambao walikuwa wananunua viwanda vya aluminium wakatengeneza mgogoro wa kubuni kwamba kuna upungufu mkubwa wa malighafi ya alumina ndani ya Russia ambayo ndiyo inatumika kuzalisha aluminium. Kwa kuwa serikali ilikuwa mkononi mwa ma-oligarch wakashawishi kwamba serikali iondoe kodi kwenye uingizaji alumina kutoka nje ya Russia ili ‘kuboost’ tena uzalishaji wa aluminium. Serikali ikaondoa kodi kwenye malighafi za utengenezaji wa aluminium na pia kubadilisha mfumo wa kodi kwenye bidhaa za aluminum. Kwa hiyo biashara ya aluminium ambayo tayari ilikuwa na fursa ya kujenga utajiri, utamu wake ukaongezeka zaidi.
Ikafika kipindi kila oligarch alikuwa anataka kumiliki kiasi fulani cha sekta hii ya aluminium.
Ubaya ni kwamba mifumo ya umilikiwa viwanda hii ambayo ilikuwa inatumika ni kama ule ambao Abramovich aliuanzisha Russia namna ambavyo alikuwa anaimiliki Sibneft kupitia msululu wa ‘private trusts’ na makampuni yaliyosajiliwa kwenye sehemu zinazojulika kwa ukwepaji kodi kama vile Cyprus, Jersey, Canyon Islands na kadhalika. Yaani makampuni yalikuwa yanamilikiwa kwa mifumo complex kiasi kwamba huwezi kujua ni nani hasa ni mmiliki wa kampuni. Hii ikatoa mwanya wa watu kufanya ‘hostile takeovers’ za kihuni. Nilieleza hii uko mwanzoni. Tajiri anawalipa hela genge fulani la mafia. Wanakuja wanakuteka… unasainishwa nyaraka kwa nguvu, unauwawa kesho mwili wako unaokotwa vichakani uking’ong’wa na nzi.
Au mshindani wako unamtumia genge linampiga risasi mchana kweupe katikati ya mji.
Kilikuwa ni kipindi cha hatari kiasi hicho. Matajiri wakubwa zaidi ya mia moja waliuwawa kinyama na miili kutupwa mitaani.
Kipindi Putin anaingia madarakani May mwaka 2000 alikuta hizi ‘aluminium wars’ ziko kwenye kilele chake kabisa. Watu wanauwana kugombea rasilimali za nchi.
Kuna mambo mengi unaweza usikubaliane na Putin lakini suala moja lazima umpe heshima yake ni jinsi ambavyo anaipenda nchi yake. Putin alipoingia madarakani alikuwa na falsafa kwamba ndani ya Urusi ni ruksa kutumia fursa ya ubepari kutengeneza utajiri lakini malengo yako hayo ya kujitajirisha hakikisha hayaathiri nchi. Kwa hiyo hizi vita za kugombea viwanda vya aluminium na namna ambavyo kwa miaka mingi matajiri hawa walikuwa wameachwa kukwepa kodi ilikuwa inamkera haswa. Alikuwa anahitaji suluhisho….
Uzuri alikuwa na Roman Abramovich upande wake.
Nakumbuka siku ambayo Rais Donald Trump alipomteua mkwewe Jared Kushner kuwa mjumbe maalumu wa kusuluhisha mgogoro wa Palestine na Israel alisema kwamba, kama Kushner akishindwa kusuluhisha mgogoro huo hakuna ambaye atakuja kuweza. Unaweza kuhisi kwamba kauli hii ni ya kumkweza sana Kushner… lakini kwa watu ambao wanamfahamu Kushner watakueleza kwamba kauli ile ya Rais Trump ilikuwa na ukweli kwa silimia zote. Kushner ni moja ya wanamkakati bora zaidi dunia kuwahi kushuhudia.
Ndicho hiki ambacho pia Putin alikuwa anakiona kwa Abramovich… hakuna mzigo mzito unaoweza kumshinda ‘myamwezi’ huyu.
Baada ya Abramovich kupewa baraka na Putin kuingia kwenye sekta ya Aluminium kwanza kabisa akaanza kutengeneza mazingira mazuri kwa yeye kufanya kile ambacho alikuwaa anakikusudia. Masuala kadhaa…
Kwanza kabisa akafungua kampuni ya ku-trade commodities. Kampuni hii iliitwa Millhouse Capital na aliisajili London Uingereza. Kupitia kampuni hii alikuwa ana-trade commodities kama vile mafuta, Gold, Silver n.k. Lakini kampuni hii ilikuwa na malengo makubwa zaidi.
Abramovich alipoanza kujiingiza kwenye sekta ya aluminium kwanza kabisa alimuomba mentor wake bwana Berezovsky kumsaidia kwa ‘connection’ alizonazo kwenye ulimwengu huo wa hatari wa biashara ya aluminium. Kipindi hiki Berezovsky alikuwa amejiingiza kwenye siasa na alikuwa ni mwakilishi kwenye Bunge la GosDumas. Na kwa kipindi hicho ili ushinde kiti cha kisiasa nchini Russia lazima uwe na connections na makundi ya mafia kwa ajili ya protection na kuwafanyizia wapizani wako. Kwa hiyo Abramovich alikuwa anataka kutumia connection hizi za mentor wake.
Berezovsky alimsaidia kwa kumtambulisha kwa watu wawili ambao walikuja kugeuka kuwa muhimu sana kwenye maisha ya Abramovich mpaka leo hii…
Kwanza, tunakumbuka kwamba nilieleza kuwa wakati serikali ya Yeltsin inabinafsisha mali za umma hata televisheni ya taifa iliyoitwa Perviy Kanal (First Channel) nayo ilibinafsishwa na ambaye aliichukua alikuwa ni huyu Oligarch Boris Berezovsky. Sasa, baadae Berezovky allimuingiza Russia mtu anaitwa Badri Patarkatsishvili. Huyu alikuwa ni mfanyabiashra kutoka Georgia lakini ni myahudi wa Israel. Badri aliingizwa Russia na Berezovsky na kumpa jukumu la kuendesha kituo cha televisheni ambacho alikuwa amebinafsishiwa na serikali. Lakini uhalisia kamili ni kwamba Badri alikuwa anajua haswa namna ya 'kudili' na mafia na masuala ya 'underworld'. Kwa hiyo Badri alikuwa anahakikisha usalama wa Berezosky na pia kuhakikisha wapinzani wa Berezovky wanashughulikiwa ipasavyo.
Huyu ni mtu wa kwanza ambaye Abramovich alitambulishwa na mentor wake Berezovky. Kupitia mtu Abramovich alilipa zaidi ya Dola milioni 500 kwenda kwa mafia kupitia kwenye mikono ya Badri Patarkatsishvili. Kwa ajili ya nini? Nitaeleza…
Sasa ili kuelewa ni kwa namna gani Abramovich aliingia kwa kishindo kwenye sekta ya aluminium na ku-takeover tunapaswa kumchambua mtu wa pili ambaye Abramovich alitambulishwa na Berezovky.
Pale Russia kuna bwana mmoja anaitwa Oleg Deripaska. Katika enzi za utoto wake bwana huyu alikuwa ni wale aina za watoto ambao wazungu wanawaita 'prodigy'. Watoto wenye vipaji vya kupindukia kwenye suala fulani. Deripaska alikuwa ni prodigy wa hesabu na sayansi. Kabla sijaenda mbali kuna ‘pettern’ hapa nataka uione nitakuja kueleza huko mbele… Pattern ya kwanza ni Berezovsky mentor wa Abramovich nilieleza pale mwanzoni alikuwa ni Profesa wa Hisabati kabla ya kujiingiza kwenye biashara, lakini pia huyu Oleg Deripaska ambaye Abramovich alitambukishwa kwake naye alikuwa ni nguli wa Hisabati tangu utoto. Pattern ya pili ambayo nataka uione ni hawa watu watatu… Abramovich, Berezovsky na Badri Patarkatsishvili wote hawa wana asili ya Israel. Utanilewa hapo mbele kwa nini nime-highlight hayo mambo mawili.
Sasa ni namna gani huyu deripaska alimsaidia Abramovich kuingia kwenye biashara ya hatari ya Aluminium kwa kishindo… nitarudi kueleza.
Nitarejea maoligarch, see you soon…
The Bold - 0718 096 811
To Infinity and Beyond
SEHEMU YA TISA
MUHIMU: Kabla sijaenda kwenye mada nijibu swali ambalo naulizwa kila mara kwenye comments na PM ili iwe clear. Utaratibu wa kujiunga na 'familia' yangu kule whatsapp ni malipo ya shilingi elfu tano kwa mwezi. That's it.
And nimeweka namba yangu, kwa hiyo ni vyema unitumie meseji direct badala ya PM. Nafungua PM mara chache sana kwa hiyo unaweza kuona sijajibu meseji yako ukajiuliza huyu somo vipi tena. PM nyingi mno, zinanielemea kwa hiyo najikuta sifungui zote.
And hili ni suala la hiyari, kwa wenye kupenda wamekuja wale ambao wanahisi hawawezi basi tutakuwa tunaonana hapa jukwaani. Nadhali hii imekaa sawa, hakuna haja ya kufanya kuhusu hili. Limeisha…
Twende kwa Oligarch Abramovich….
Nimewahi kuonana na wasomaji wangu wachache sana wa makala na vitabu vyangu. Sababu kubwa ya kutoonana sana na watu ni kwa vile katika maisha ya kawaida huwa siongei kabisa japo ni msikilizaji mzuri sana. Tunaweza kukaa nikakusikiliza kwa masaa manne straight bila kuchoka wala wala ‘kuboreka’. Ubaya ni kwamba watu wengi wanategemea uwaeleze mengi na ubaya ni kwamba kwa asili huwa siongei ndio maana nachagua kuandika sana labda ‘ku-compasate’ energy ninayo-reserve kwa kutokuongea. Hii ni moja ya sababu kwa nini mara nyingi huwa sionani na watu… I’m not a good company kama unahitaji mtu wa ‘kupiga story’. Lakini sababu ya pili ni umri… wengi wana picha fulani kichwani ya muonekano au umri wa huyu muandishi ‘The Bold’. Wachache ambao nimekutana nao wote kitu kimoja huwa wanakisema ni kwamba kwa umri huu nilionao nawezaje kuandika vitu ambavyo naandika? Inawezekana wanasema hivyo as a compliment but it makes me feel very uncomfortable. Kwa hiyo napendelea kuendelea kujificha kwenye kichaka cha ‘The Bold.’
Kwa nini nasema haya… unapomsoma mtu kwa muda mrefu sana na mambo makubwa ambayo ameyafanya kuna wakati fulani unaanza kujenga picha ya nje ya uhalisia.
Kwa mfano, kwa vitu vyote hivi ambavyo Roman Abramovich amevifanya… kufikia hatua ya hadhi ya Oligarch, kulichachafya Bunge la Russia, kumuondoa Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali, kujimilikisha kampuni kubwa zaidi ya mafuta ya serikali, kumshawishi Rais Boris Yeltsin kuondoka madarakani na kumtengeneza Rais mpya Vladimir Putin… unaweza kudhani kwamba Abramovich ni lizee fulani hivi lililo zaliwa na kukulia kwenye ‘system’… lakini nikukummbushe kwamba mpaka siku ile mwaka 2000 mwezi May kipindi Putin anaapishwa kuwa rais mpya wa Russia… Roman Abramovich alikuwa ni kijana wa miaka thelathini na tatu tu. Niweke mkazo kwa namba… miaka 33.
Kwenye sehemu iliyopita nilieleza kwamba baada ya Abramovich kujihakikishia umilki wa Sibneft na kisha kumshawishi Rais Yeltsin kuachia ngazi na baadae kumfinyanga Putin na kumweka madarakani sasa uliwadia wakati wa kuingia katika ‘utukufu mpya’.
Nchi ya Urusi kwa miongo mingi sana imekuwa ndio nchi inayoongoza duniani kwa uzalishaji wa aluminium na hata matajiri wa kubwa wa Russia utajiri wao unatokana na aluminium, mafuta na gesi. Kwa hiyo sekta hii ya aluminium ni moja ya uti wa mgongo wa uchumi wa Russia.
Kwenye miaka ya tisini na mwanzoni mwa 2000 baada ya serikali kuanza ubinafsishaji holela wa mali za umma ushindani ulikuwa mkubwa haswa na Russia haijawahi kushuhudia vifo vingi vya watu mashuhuri kama kipindi hiki. Katika kipindi hiki zaidi ya matajiri mashuhuri 100 waliuwawa kinyama na miili yao kuokotwa barabarani.
Kipindi hiki kichungu kinakumbukwa kama wimbi la ‘Aluminium wars’. Nitaomba kuchambua kwa kuingia miguu miwili yote nukta kwa nukta ili kukielewa nini kilitokea kwa sababu tukiweza kuelewa vyema nini kilitokea ni rahisi zaidi kuielewa hata hii Russia ya sasa na mwelekeo wake wa kisiasa.
Ilikuwaje… tuanze kwenye mzizi.
Ukuaji wa sekta ya aluminium nchini Russia ni matokeo ya miaka mingi sana ya serikali ya nchi hiyo kuwekeza nguvu kubwa sana kwenye kuendeleza sekta hii. Kama haujafahamu, aluminium inachimbwa kutoka kwenye migodi ya boksiti (bauxite) na kisha kuchakatwa kuwa alumina (aluminium oxide). Alumina iko kama unga unga fulani hivi mwepe au mfano mzuri kama ‘snow’ hivi. Hii ndio hutumika kuzalisha aluminium. Sasa Russia ni moja kati ya nchi za kwanza kabisa kufanya bunifu za kuchakata boksiti mpaka kupata alumina. Gunduzi za mwanasayansi kama Beyer ambaye alikuwa raia wa Austria miaka ya 1889 akiwa anafanyakazi St. Petersburg’s katika kiwanda cha kemikali cha Tenteleev ambapo aligundua mbinu ya kuchakata alumina kutoka kwenye boksiti kwa kutumia alkali za kaustiki. Baadae gunduzi za watu kama Muller na Packard ambao waligundua uvunaji wa alumina kwa kuifanyia decomposition ya aluminium hydroxide na kisha kufanyia electrolysis. Katika lugha nyingine twaweza kusema kwamba warusi ndio ‘pioneers’ wa namna za uvunaji alumina kutoka kwenye migodi ya boksiti. Hata mapinduzi makubwa ya upatikanaji wa umeme wa uhakika nchini Russia ambayo yalitokea kwenye karne ya 20 kwa kiasi kikubwa kulitokana na uhitaji mkubwa wa viwanda vya kuzalisha aluminium na malengo ya nchi hiyo kutaka kuongeza uzalishaji kila mwaka.
Kwa hiyo sekta hii ya aluminium kwa miongo mingi nchini Russia imekuwa haraka na kuwa sehemu ya uti wa mgongo wa nchi.
Sasa kwenye miaka ya tisini kipindi ambapo serikali ilikuwa inahama kutoka kwenye ujamaa na kuingia kwenye ubepari na kubinafsisha mali za umma kuna jambo la kiuhini likafanyika. Wafanyabiashara ambao walikuwa wananunua viwanda vya aluminium wakatengeneza mgogoro wa kubuni kwamba kuna upungufu mkubwa wa malighafi ya alumina ndani ya Russia ambayo ndiyo inatumika kuzalisha aluminium. Kwa kuwa serikali ilikuwa mkononi mwa ma-oligarch wakashawishi kwamba serikali iondoe kodi kwenye uingizaji alumina kutoka nje ya Russia ili ‘kuboost’ tena uzalishaji wa aluminium. Serikali ikaondoa kodi kwenye malighafi za utengenezaji wa aluminium na pia kubadilisha mfumo wa kodi kwenye bidhaa za aluminum. Kwa hiyo biashara ya aluminium ambayo tayari ilikuwa na fursa ya kujenga utajiri, utamu wake ukaongezeka zaidi.
Ikafika kipindi kila oligarch alikuwa anataka kumiliki kiasi fulani cha sekta hii ya aluminium.
Ubaya ni kwamba mifumo ya umilikiwa viwanda hii ambayo ilikuwa inatumika ni kama ule ambao Abramovich aliuanzisha Russia namna ambavyo alikuwa anaimiliki Sibneft kupitia msululu wa ‘private trusts’ na makampuni yaliyosajiliwa kwenye sehemu zinazojulika kwa ukwepaji kodi kama vile Cyprus, Jersey, Canyon Islands na kadhalika. Yaani makampuni yalikuwa yanamilikiwa kwa mifumo complex kiasi kwamba huwezi kujua ni nani hasa ni mmiliki wa kampuni. Hii ikatoa mwanya wa watu kufanya ‘hostile takeovers’ za kihuni. Nilieleza hii uko mwanzoni. Tajiri anawalipa hela genge fulani la mafia. Wanakuja wanakuteka… unasainishwa nyaraka kwa nguvu, unauwawa kesho mwili wako unaokotwa vichakani uking’ong’wa na nzi.
Au mshindani wako unamtumia genge linampiga risasi mchana kweupe katikati ya mji.
Kilikuwa ni kipindi cha hatari kiasi hicho. Matajiri wakubwa zaidi ya mia moja waliuwawa kinyama na miili kutupwa mitaani.
Kipindi Putin anaingia madarakani May mwaka 2000 alikuta hizi ‘aluminium wars’ ziko kwenye kilele chake kabisa. Watu wanauwana kugombea rasilimali za nchi.
Kuna mambo mengi unaweza usikubaliane na Putin lakini suala moja lazima umpe heshima yake ni jinsi ambavyo anaipenda nchi yake. Putin alipoingia madarakani alikuwa na falsafa kwamba ndani ya Urusi ni ruksa kutumia fursa ya ubepari kutengeneza utajiri lakini malengo yako hayo ya kujitajirisha hakikisha hayaathiri nchi. Kwa hiyo hizi vita za kugombea viwanda vya aluminium na namna ambavyo kwa miaka mingi matajiri hawa walikuwa wameachwa kukwepa kodi ilikuwa inamkera haswa. Alikuwa anahitaji suluhisho….
Uzuri alikuwa na Roman Abramovich upande wake.
Nakumbuka siku ambayo Rais Donald Trump alipomteua mkwewe Jared Kushner kuwa mjumbe maalumu wa kusuluhisha mgogoro wa Palestine na Israel alisema kwamba, kama Kushner akishindwa kusuluhisha mgogoro huo hakuna ambaye atakuja kuweza. Unaweza kuhisi kwamba kauli hii ni ya kumkweza sana Kushner… lakini kwa watu ambao wanamfahamu Kushner watakueleza kwamba kauli ile ya Rais Trump ilikuwa na ukweli kwa silimia zote. Kushner ni moja ya wanamkakati bora zaidi dunia kuwahi kushuhudia.
Ndicho hiki ambacho pia Putin alikuwa anakiona kwa Abramovich… hakuna mzigo mzito unaoweza kumshinda ‘myamwezi’ huyu.
Baada ya Abramovich kupewa baraka na Putin kuingia kwenye sekta ya Aluminium kwanza kabisa akaanza kutengeneza mazingira mazuri kwa yeye kufanya kile ambacho alikuwaa anakikusudia. Masuala kadhaa…
Kwanza kabisa akafungua kampuni ya ku-trade commodities. Kampuni hii iliitwa Millhouse Capital na aliisajili London Uingereza. Kupitia kampuni hii alikuwa ana-trade commodities kama vile mafuta, Gold, Silver n.k. Lakini kampuni hii ilikuwa na malengo makubwa zaidi.
Abramovich alipoanza kujiingiza kwenye sekta ya aluminium kwanza kabisa alimuomba mentor wake bwana Berezovsky kumsaidia kwa ‘connection’ alizonazo kwenye ulimwengu huo wa hatari wa biashara ya aluminium. Kipindi hiki Berezovsky alikuwa amejiingiza kwenye siasa na alikuwa ni mwakilishi kwenye Bunge la GosDumas. Na kwa kipindi hicho ili ushinde kiti cha kisiasa nchini Russia lazima uwe na connections na makundi ya mafia kwa ajili ya protection na kuwafanyizia wapizani wako. Kwa hiyo Abramovich alikuwa anataka kutumia connection hizi za mentor wake.
Berezovsky alimsaidia kwa kumtambulisha kwa watu wawili ambao walikuja kugeuka kuwa muhimu sana kwenye maisha ya Abramovich mpaka leo hii…
Kwanza, tunakumbuka kwamba nilieleza kuwa wakati serikali ya Yeltsin inabinafsisha mali za umma hata televisheni ya taifa iliyoitwa Perviy Kanal (First Channel) nayo ilibinafsishwa na ambaye aliichukua alikuwa ni huyu Oligarch Boris Berezovsky. Sasa, baadae Berezovky allimuingiza Russia mtu anaitwa Badri Patarkatsishvili. Huyu alikuwa ni mfanyabiashra kutoka Georgia lakini ni myahudi wa Israel. Badri aliingizwa Russia na Berezovsky na kumpa jukumu la kuendesha kituo cha televisheni ambacho alikuwa amebinafsishiwa na serikali. Lakini uhalisia kamili ni kwamba Badri alikuwa anajua haswa namna ya 'kudili' na mafia na masuala ya 'underworld'. Kwa hiyo Badri alikuwa anahakikisha usalama wa Berezosky na pia kuhakikisha wapinzani wa Berezovky wanashughulikiwa ipasavyo.
Huyu ni mtu wa kwanza ambaye Abramovich alitambulishwa na mentor wake Berezovky. Kupitia mtu Abramovich alilipa zaidi ya Dola milioni 500 kwenda kwa mafia kupitia kwenye mikono ya Badri Patarkatsishvili. Kwa ajili ya nini? Nitaeleza…
Sasa ili kuelewa ni kwa namna gani Abramovich aliingia kwa kishindo kwenye sekta ya aluminium na ku-takeover tunapaswa kumchambua mtu wa pili ambaye Abramovich alitambulishwa na Berezovky.
Pale Russia kuna bwana mmoja anaitwa Oleg Deripaska. Katika enzi za utoto wake bwana huyu alikuwa ni wale aina za watoto ambao wazungu wanawaita 'prodigy'. Watoto wenye vipaji vya kupindukia kwenye suala fulani. Deripaska alikuwa ni prodigy wa hesabu na sayansi. Kabla sijaenda mbali kuna ‘pettern’ hapa nataka uione nitakuja kueleza huko mbele… Pattern ya kwanza ni Berezovsky mentor wa Abramovich nilieleza pale mwanzoni alikuwa ni Profesa wa Hisabati kabla ya kujiingiza kwenye biashara, lakini pia huyu Oleg Deripaska ambaye Abramovich alitambukishwa kwake naye alikuwa ni nguli wa Hisabati tangu utoto. Pattern ya pili ambayo nataka uione ni hawa watu watatu… Abramovich, Berezovsky na Badri Patarkatsishvili wote hawa wana asili ya Israel. Utanilewa hapo mbele kwa nini nime-highlight hayo mambo mawili.
Sasa ni namna gani huyu deripaska alimsaidia Abramovich kuingia kwenye biashara ya hatari ya Aluminium kwa kishindo… nitarudi kueleza.
Nitarejea maoligarch, see you soon…
The Bold - 0718 096 811
To Infinity and Beyond