Roman Abramovich: Utajiri wa Damu, Risasi na Umafia

Roman Abramovich: Utajiri wa Damu, Risasi na Umafia

Ongeza sauti kidogo mama..
The bold kawakimbia kama kawaida yake tuliopo kule group raha sana [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ubarikiwe sana mkuu... Waafrika tuna shida sana mahala fualani. Ni Mungu atusaidie tubadilike
Nimekua msomaji wa makala zako muda mrefu sana. Nikupongeze sana jamaa. Kuandika sio kazi rahisi hata kidogo. Kutafiti ni kazi kubwa kuliko kulima. Na ugumu zaidi, kueleza jambo likawa na taarifa zaidi kuliko mtu anavyoweza kuzipata katika dunia hii iliyojaa utandawazi. Kwenye jamii za wenzetu ungekua bilionea mkubwa, bahati mbaya jamii zetu zetu hizi ambazo hata kutoa ef 5 kwa mwezi mtu anaona ni kama anaibiwa, basi tunashukuru utaacha kumbukumbu ya maandishi haya, hata wajukuu zako watanufaika na maumivu ya kuacha usingizi na kukodoa macho kwenye makaratasi. KUDOS BRO.
 
Please kaka habib naomba uni tag ujawahi kunitag hata mara moja though najitahidi kukuomba , kazi nzuri sana .. nimesha tega alarm kabisa saa 2 kamili
 
Alijigamba kuwa anajua mambo sana ya usalama hapa EAC kikubwa anajipigia chapuo. Yeye alitakiwa kutoa afu sie wenyewe ndo tujaji jamaa anajua ama hajui.
Sema anabangaiza ya unga watoto waende chooni.
Huwa Niko sensitive sana na kauli za kunitoa Hela.yaani utakuja na lugha tamu ila mwishoni najua kuwa lengo lako mie nitoe Hela mfukoni nikupe.
Nishawahi kusema huyu ni kifaduro, hana lolote analojua story za usalama za vijiweni ndio anakuja kujitutumua humu ndani kwamba amebobea katika masuala ya intelligence, watu tunamuangalia na kubaki kucheka tu.

Njaa inamsumbua, fanyeni kumchangia hiyo elfu5, Akate kiu yake.
 
Hahahahaha pole endelea tu kulipia elfu tano tano mkuu nakumbuka niliwahi kuwepo kwenye group lake kama sio mwaka jana basi mwaka juzi hayo.na mie yalinikuta mpk nikajuta ratiba anaweka mwenyewe halafu anaivuruga ila ikifika mwisho wa mwezi ukifika anaibuka kusisitiza kulipia nilitoka nduki
Njaa mbaya sana Mkuu..
 
Hakuna shaka mkuu, leo nakutag
Saa mbili uwe hapa
Please kaka habib naomba uni tag ujawahi kunitag hata mara moja though najitahidi kukuomba , kazi nzuri sana .. nimesha tega alarm kabisa saa 2 kamili
 
Nina mwaka wa nne naandika hapa JF na kila makala its a nuclear bomb (inagusa watu).
Hakuna tusi ambalo sijatukanwa... so hakuna jipya mkuu labda wabuni tusi jipya... kama asemavyo Mhe. Joseph Haule.. "kipi sijasikia?"
Hata kama wanakushutumu, kuwa unacopy kutok google, ukweli kwamba you are talented. Upangiliwaji wa stori upo makini sana na umeenda ndani sana. AsanteTHE BOLD
 
ROMAN ABRAMOVICH: UTAJIRI EA DAMU, RISASI NA UMAFIA


SEHEMU YA KUMI


(Wale wote waliojipa mission ya kunitukana na kunikashifu kwenye comments nina neno moja kwenu… nyinyi ni wana wa Mungu na kwa sababu hiyo nawapenda sana)


Nilisema nitaeleza kidogo kuhusu Deripaska ambaye Abramovich alitambulishwa kwake na Berezovsky. Deripaska ni aina ya wasomi ambao wametumia taaluma yao vyema kujichumia utajiri. Tangu akiwa bado kijana mdogo tu Deripaska alikuwa na shauku kubwa mno ya kujisomea na kitu angalinacho hata sasa. Huyu bwana hata sasa ukifika ofisni kwake makau makuu ya Basic Elements jijini Moscow kwenye jengo hilo kuna kuta nyingi ambazo zina shelves za vitabu kuanzia chini mpaka juu. Deripaska alikuwa na kipawa kikubwa cha hisabati tangia utoto. Mwaka 1993 alihitimu chuo kikuu ‘with honors’ shahada ya fizikia kutoka Moscow State University. Miaka miwili baadae alihitimu shahada ya uzamili katika uchumi kutoka Plekhanov University of Economics.

Ndoto ya awali Deripaska ilikuwa ni kuwa msomi mbobezi kama ‘Theoretical physicist’. Lakini utakumbuka kwamba kipindi hiki ndicho ambacho Soviet Union ilidondoka. Hapo awali wanafunzi wote walikuwa wanasoma kwa udhamini wa serikali lakini baada ya Soviet Union kudondoka elimu ikawa ghali na serikali kuacha kugharamia masomo ya wanafunzi. Kwa hiyo kwa kijana kama Deripaska ambaye mwenyewe anasema kwamba hata hela ya kula ilikuwa ni tatizo kwake kipindi hicho hakukuwa na uhalisia wa yeye kuweza kugharamia masomo yake mwenyewe.

Lakini pia kipindi hiki kama tulivyoona awali kilikuwa ni kipindi chenye fursa nzuri kwa mtu kujilimbikizia utajiri. Kwa hiyo Deripaska akiwa na miaka 25 tu alishawishi wanasayasi wengine kadhaa manguli wa hesabu, fizikia na hata rocket science kuungana naye kuanzisha kampuni ya ‘ku-trade’ metals. Kampuni hii waliita VTK, na Deripaska ndiye alikuwa mwanahisa mkubwa kuzidi wenzake. Deripaska alikuwa ni moja ya watu wa mwanzo kabisa nchini Russia kutumia mifumo ya kisayansi na ‘systematics’ katika kutrade commodities. Unaweza kujiuliza namna gani anatumia sayansi kutrade commodities… binafsi huwa natrade currencies na huwa nawaambia watu ‘trading’ ni science and mathematics na ndio maana watu wengi hawako successful wakitaka kuwa traders… kwa nini? Kwa sababu sayanasi na hisabati sio kitu chepesi.
Uzuri ni kwamba Deripaska alikuwa ni nguli wa hisabati kwa hiyo VTK ilikuwa kwa haraka sana. Deripaska alikuwa ananunua commodities kwa bei ya chini ndani ya Urusi na kwenda kuziuza kwa bei ya juu kwenye soko la dunia.

Kwenye sehemu za mwanzo kabisa za makala hii nilieleza kwamba kipindi serikali ya Russia inabinafsisha viwanda na makampuni ya umma waligawa voucher kwa wananchi ili watumie voucher hizo kununua hisa kwenye makampuni ambayo yalikuwa yanabinafsishwa. Nilieleza kwamba kila mwananchi alipewa voucher ya Rubble 10,000 za Urusi. Kama ambavyo ilitokea hapa kwetu Tanzania wakulima walivyouza vocha za pembejeo za kilimo ndivyo ambavyo pia Warusi walivyouza voucher zao kwa matajiri. Deripaska ni moja ya matajiri hawa ambao waliwekeza hela ya kutosha kununua voucher kwa wananchi.

Kama mwaka mmoja tu baadae Deripaska alitumia voucher zote na faida yote aliyoipata kwenye kutrade commodities kununua hisa kwenye kiwanda cha Sayanogorsk Aluminium Smelter. Hiki ndicho kilikuwa kiwanda kikubwa zaidi cha uzalishanji aluminium nchini Rusia. Uwekezaji wake huu mkubwa ulimpatia hisa 20% za kiwanda hiki. Kwa wingi huu wa hisa ulimfanya Deripaska kuwa mwanahisa mkubwa zaidi nyuma ya serikali kwenye kiwanda hiki. Yaani mwenye hisa nyingi zaidi alikuwa serikali na yeye alikuwa namba mbili.

Kutokana na ushawishi huo mkubwa aliokuwa nao kwenye kiwanda cha Sayanogorsk Aluminium Smelter kwa sababu ya kuwa na hisa nyingi kuzidi mtu yeyote binafsi, mwaka 1994 Deripaska alifanya ushawishi kwa wanahisa wengine na kupewa Ukurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo. Nikukumbushe tu kwamba mwaka huo 1994 wakati anapewa ukurugenzi mkuu wa smelter kubwa zaidi nchini Russia alikuwa ana miaka 26 tu.

Miaka mitatu baadae yani mwaka 1997 Deripaska alianzisha Sibirsky Aluminium Group ambayo aliitumia kama kampuni mama ‘kuhold’ kampuni zake zote nyingine na shares zake zote kwenye makampuni mengine.

Kwa hiyo huyu ndiye mtu wa pili ambaye Berozovsky alimtambulisha Abramovich kwake.

Naweza kusema kwamba huyu pengine ndio alikuwa mtu muhimu zaidi kwa Abramovich kumfahamu labda nyuma ya Berozosky tu pekee. Licha ya umuhimu wake mkubwa ambao tutauona hivi punde lakini pia bwana huyu walikuwa na mengi ya kufanana. Ukipiga hesabu yako sawasawa utaona kwamba Abramovich alikuwa anamzidi mwaka mmoja tu Deripaska. Yaani kipindi kile Abrampvich anapewa Baraka na Putin kuingia kwenye biashara ya Aluminium akiwa na miaka 33, Deripaska alikuwa na miaka 32.

Wote wawili walikuwa ni vijana wadogo sana. Wote wawili wametokea kwenye maisha ya hali ya chini sana. Wote wawili wanajua namna ya kuishi kimkakati. Wote wawili walikuwa na ushawishi mkubwa sana. Abramovich kwenye system ya serikali na Deripaska kwenye ulimwengu hatari wa biashara ya Aluminium.
Wenye unyoya wa kufanana… huruka pamoja.

Nilieleza kwamba mwaka huo alipopewa Baraka na Putin kuingia kwenye biashara ya Aluminium, Abramovich alifungua kampuni iliyoitwa Millhouse Capital ambayo ilisajiliwa nchini Uingereza. Kampuni hii ilikuwa inatrade commodities. Tufahamu kwamba mpaka muda huu kampuni hii haikuwa lolote wala chochote. Haikuwa na ‘volumes’ kubwa kwenye kutrade hizo commodities wala assets za maana. Thamani pekee ya kampuni hii iliyokuwa nayo ni ile u kwamba inamilikiwa na Roman Abramovich.

Abramovich alipotambulishwa kwa Deripeska alikuwa na ombi moja tu kwake… waunganishe kampuni zao Millhouse Capital ya Abramovich na Sibirsky Aluminium Group ya Deripaska na iwe kampuni moja. Kwa umombo dili kama hii wanaita ‘merger’.
Unaweza kuona kwamba ombi hili lilikuwa ni la kijinga… Sibirsky Aluminium Group ilikuwa kwa muda huo ni kampuni kubwa sana ndani ya Russia inayomiliki smelters kadhaa kubwa kubwa ndani ya Russia na pia ilikuwa kampuni mama ya trading companies kama vile ile VTK ambayo deripaska aliinzisha na wanasayansi wenzake. Wakati ambapo Millhouse Capital ya Abramovich ilikuwa kama ni kampuni jina tu yenye ofisini bila mali kubwa kubwa kulinganisha na Sibirsky Aluminium Group.

Ajabu ni kwamba Deripaska hakusita hata kwa sekunde kukubali ombi hilo. Alikubali mara moja waunganishe kampuni hizo mbili kuwa moja ambayo watakuwa wanaimiliki wote.
Kwa nini akubali kirahisi hivi? Wendawazimu?... hapana, kama ilivyo kwa Abramovich ndivyo hivyo hivyo pia ilivyo kwa Deripaska… ni mtu wa mikakati. Anaiona miaka ishirini ijayo leo.

Kuna mambo mawili…

Thamani halisi ya kitu haitokani na hali yake ya sasa bali thamani yake ni ile ‘potential’ iliyonayo kuleta mafanikio huko mbeleni. Yaani kwamba tukiwaza kibiashara… kwa mfano utajiri au umasikini wa mtu haupimwi kwa kile alichonacho sasa bali ‘potential’ aliyonayo kupoteza zaidi au kuingiza zaidi kwa siku na miaka ijayo. Unaweza kuwa na milioni mia moja leo hii lakini kuna mtu akikuangalia anakuona masikini. Labda kwa namna fulani amegundua ndani ya miezi michache tu utazipoteza zote. Na unaweza kuwa na elufu kumi tu mfukoni na mtu mwingine akakuona tajiri kwa sababu anahisi potential uliyonayo mwakani tu unaweza kuwa na bilioni umelaza benki.

Napenda mifano hai, nitoe mfano mfupi halisi…
Mwaka 2008 nilikuwa na rafiki yangu tulikuwa darasa moja Tambaza High school. Huyu kwao walikuwa na haueni sana. Mzee wake alikuwa afisa mwandamizi wa serikali kwenye kitengo fulani. Alikuwa na safari za mara kwa mara nje ya nchi. Kuna safari moja aliporejea alimletea zawadi ya simu ya iPhone. Hiyo ni mwaka 2008 ambapo unaweza kutembea mjini kutwa nzima bila kuona mtu hata mmoja mwenye simu aina ya iPhone. Unaweza kupata picha ni kiasi gani yeye mwenyewe na sisi 'washkaji' zake tulikuwa ‘tunavimba’ shuleni… ndio hata sisi wapambe wake tulikuwa tunajiona kama simu yetu. Loooh.!!
Basi tukaanza ‘uzungu uzungu’ hivi… kutaka kujua mambo ambayo yanatrend huko duniani. Mara tukafahamu kuhusu facebook… hu ni mwaka 2008… sikumbuki kuwahi kumsikia mtu yeyote kabla akitaja facebook. Kilikuwa ni kitu kipya ambacho hapa nchini kilikuwa hakijulikani kabisa kabisa. Kipindi kile ‘chat rooms’ ndio zilikuwa maarufu sana hapa nchini. Pale shuleni kwetu ni ‘genge’ letu tu nadhani ndio ambao tulikuwa na akaunti za facebook na hata sisi ni baada ya kusikia ni kitu ‘hot’ huko duniani.

Kutokana na udadisi sikuishia tu kuitumia facebook bali nikaanza kuichimba. Ndio nikafahamu kuhusu mmiliki wake bwana Mark Zuckerberg na kipindi kile akisemwa kuwa ndio Bilionea kijana zaidi duniani akiwa na utajiri wa dola bilioni 2.4 akiwa na umri wa miaka 26 tu. Nikawa najiuliza sana… huyu mtu anawezaje kuwa tajiri mkubwa kiasi hicho wakati huduma hiyo tunaitumia bure? Kipindi kile facebook haikuwa na matangazo kama sasa na ilikuwq sehemu ya sera yao kutokuweka matangazo kwenye mtandao wao… hakukuwa na tangazo hata moja na wala walikuwa hawapokei matangazo. Na pia wala walikuwa hawajafanya ile IPO… ile kuirodhesha kwenye soko la hisa na kuanza kuuza shares kwa umma. Kipindi kile hata financial documents za kampuni zilikuwa zinaonyesha kwamba kwa mwaka wanapata zero revenue? Inakuwaje huyu mtu awe tajiri hivi? Hizi hela zinatoka wapi? Hawa wazungu wanatuzuga na uongo au nini?

Wewe unadhani hela za Mark zilikuwa zinatoka wapi kipindi kile? Kwa nini kipindi kile waseme ana utajiri wa dola bilioni 2.4?

Jawabu ni 'Speculation'… ‘potential’ ambayo watu wanaiona kwa kitu hicho kutengeneza faida kubwa kwa wakati ujao. Sikumbuki sawasawa lakini nadhani kipindi kile Facebook ilikuwa na watumiaji kama milioni 300 hivi duniani. Kwa hiyo kulikuwa na speculation kubwa kwamba hii kampuni siku yoyote ile ‘ita-boom’ na kuleta fedha nyingi. Na hii ndio ilikuwa inafanya thamani ya kampuni ya facebook kuwa kubwa na kumfanya Mark kuwa na utajiri wote ule. Lakini kiuhalisia kwa kipindi kile hawakuwa wanaingiza revenue hata kipande ukiachaa hela za investors.

Sasa hiki ndicho ambacho Deripaska alikuwa anakiona kwa Abramovich… potential. Potential gani? Abramovich alikuwa ni ‘mtoto’ pendwa wa Putin. Putin alikuwa anamuamini Abramovich kuzidi mtu yeyote yule. Kwa hiyo kama akiwa mmiliki mwenza wa kampuni moja na Abramovich, basi hakuna anga ambalo litawashinda kulivuka na wanaweza kutengeneza moja ya kampuni tajiri zaidi duniani.

Nilisema kuna mambo mawili… hiyo ilikuwa sababu ya kwanza. Sababu ya pili ilikuwa ya busara zaidi. Isingelikuwa busara kwake kumkatalia Abramovich kwasababu, ‘If Roman wants something… Roman gets something.!” Kama angemkatalia ofa hiyo Abramovich, basi Abramovich angetafuta namna nyingine ya kukipata kiwanda hicho na njia hiyo nyingine ingekuwa hasara kwa Deripaska. Abramovich ni aina ya watu ambao lazima wapate wanachokitaka… hakuna kiunzi ambacho atashindwa kukiruka.

Kwa hiyo wakaunganisha kampuni zao, Millhouse Capital na Sibirsky Aluminium Group na kuunda kampuni mpya inayoitwa RUSAL (siku hizi inaitwa United Company RUSAL).

RUSAL ilikuwa kwa haraka sana. Walichokuwa wanakifanya… walikuwa wananunua viwanda vingine na migodi ya boksiti ndani ya Russia na nchi jirani. Maoligarch ambao walikuwa wanamiliki viwanda hivyo na migodi ilikuwa ni eidha uwauzie RUSAL kiwanda chako kwa hiari au wakichukue kwa lazima. Ukikubali kuwauzia wanakulipa hela… ukikataa kuwauzia kesho kutwa tunaokota mwili wako jalalani.
Kuna ‘transcript’ za mahakamani kutoka Uingereza za mwaka 2010 ambapo Abramovich aliitwa kutoa ushahidi kwenye kesi fulani, anakiri kwamba hizi aluminium wars zilikuwa moto kweli kweli kiasi kwamba yeye binafsi anakumbuka kwa miaka ya 2000 na 2001 kwa wastani wa kila baada ya siku tatu ulikuwa unasikia mwii wa oligarch fulani umeokotwa.

Na hapa ndipo ambapo ulikuja umuhimu wa Badri Patarkatsishvili yule jamaa wa kwanza aliyetambulishhwa na Berezovsky. Unapojihusisha na sekta ambayo kila kukicha unasikia wenzako wanakufa lazima uwe na tahadhali makini haswa. Huyu Badri nilieleza kwamba alikuwa anajua kudili na Mafia.
Unapomwaga damu za wenzako lazima kuna marafiki zao na ndugu zao na hata wale wengine wanajihisi nao siku utawamaliza, wote hawa watajihami kwa kutaka kukumaliza wewe. Ilifika kipindi ndani ya Russia Abramovich alikuwa hawezi hata kuonekana hadharani… kila oligarch aliyekuwa bado hai alikuwa ameweka vijana kumuwinda na kutaka kumuua. Ndio hapa ambapo Abramovich ilimbidi kulipa zaidi ya dola milioni 500 kupitia kwa Badri kwenda kuhonga kila kikundi cha mafia ndani ya Russia ambacho kilitumwa kumuua yeye na kisha kuwapa agizo jipya wakawamalize wale ambao waliwatuma awali.

Nchi ilichafuka haswa kwa vifo vya maoligarch… lakini RUSAL ilizidi kupaa. Ndani ya miaka miwili tu walikuwa wana-control karibia migodi yote muhimu ya boksiti na viwanda vyote vikubwa vya Aluminium ndani ya Russia na nchi jirani. Kuanzia viwanda vya Armenal foil mill nchini Armenia mpaka Belaya Kalitva Metallurgical plant na Novokuznetsk aluminium smelter nchini Russia. Uje migodi ya boksiti ya Friguia bauxite na Alumina complex mpaka Kindia Company. RUSAL ilipaa juu kuwa moja ya kampuni kubwa zaidi ya uzalishaji wa aluminium duniani. Lakini hapana… Abramovich hakutaka kuwa ‘moja ya’ kampuni kubwa duniani. Alitaka kuwa kampuni kubwa zaidi duniani ya uzalishaji aluminium.

Afanyeje? Kulikuwa na ‘terget’ ya mwisho… Krasnoyarsk.

Kipindi hicho jimbo la Krasnoyarsk ndilo lilikuwa na hifadhi kubwa zaidi ya migodi ya boksiti. Sasa pale Krasnoyarsk kulikuwa na kiwanda cha aluminium kinachoitwa Krasnoyarsk Aluminium Smelter. Kiwanda hiki kilikuwa kinamilikiwa na oligarch anaitwa Anatoly Bykov. Huyu oligarch alikuwa ni kijana kama wao akina Abramovich japo alimzidi Abramovich miaka miwili kwa kuzaliwa. Kampuni yake ambayo ndiyo ilikuwa inamiliki Krasnoyarsk Aluminium Smelter kwa kipindi hicho iikuwa inashika nafasi ya pili nyuma ya RUSAL kwa uzalishaji Aluminium. Abramovich tayari alikuwa amemfuata na kumpa ofa mara kadhaa kuwauzia kampuni lakini Bykov alikataa. Mpaka muda huo alikuwa amefanikiwa kukwepa majaribio 26 ya kumuua.

Kwa hiyo huyu oligarch biashara alikuwa anaijua kama wao na uhuni wa kimafia pia alikuwa anaujua.

Kama Abramovich akifanikiwa kuchukua kiwanda hiki cha Krasnoyarsk Aluminium Smelter maana yake ni kwamba atafanikiwa kuifanya RUSAL kuwa kampuni kubwa zaidi ya uzalishaji aluminium duniani.

Lakini Bykov alikuwa amejiapiza kutowauzia kiwanda chake na majaribio ya kumtoa roho yalishindikana mara 26.
Abramovich si mtu wa kukubali kushindwa vita… “Roman wants something… Roman gets something.”

Alikuwa anahitaji mbinu mpya… Abramovich alijiapiza kuwa hataki tu kuwa na ‘moja ya’ kampuni kubwa zaidi duniani ya kuzalisha aluminium...alitaka kuwa na kampuni kubwa zaidi duniani ya kuzalisha aluminium.

Alikuwa anahitaji ‘kuchemsha muarobaini’ mpya wa kumnywesha Bykov.


Bold… Nitarejea.

To Infinty and Beyond
 
SEHEMU YA KUMI


Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi @Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu Debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM @Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu The Certified DON SINYORI mij addenbwii ONTARIO Kobe The Vein Mondray jaxonjaxon successor mzee wa liver sawariya Sitaki ukuda Domhome Mpatanishi MKANDAHARI mtugani wa wapi huyo wealthier cluecell Toyota escudo mgumu2 troublemaker Linamo shedede kamtu33 SteveMollel ngushi Donald stewart Mshuza2 Glycel mnonje Ochuanilove SingleFather Santi DEOD 360 ngushi anatory antony ukhuty chris van chicha auxillius Goma Son Hubeb pes KING DUBU VILLAIN mwayena donbeny Aleppo JipuKubwa shoo61 BOMBAY John mungo Nyakageni bato Dogo 1 sufra chamlungu painscott wegman Bravo Engliash MOSELBAY wa stendi FaizaFoxy bigmind cadabraa Internal Kelvin mwalukas mnonje Kelvin X Somoche Wgr30 Miiku Poise Jabman kalamuyamwalimu BOMBAY the say juxhb witnessj Gide MK Mmanyema mgogoone Mnongane Mandingo koncho77 afsa ngaboru Paradoxer Heavy Metal KIMBURU 06 Raaj kichekoh ngumba njeche kikale DullahTza Goodluck Mshana julius Darcy Denis Kasekenya mashonga kitalembwa Khaleed Shaban middle east SirChief jiwe jeusi Mkambarani mansakankanmusa gambada ynwa ney kush mossad 03 white wizard xtaper Mzigua90 Ollachuga Oc Gidbang Mateja M.G Yango jipu abaa4all DIBAJI Agenda1 Grahnman The MaskmaN Slim5 Xubzero agprogrammer JoJiPoJi Architectus blance86 Mamtolo monde arabe Ngao Ya Imani stardust JK naiman64 Dharra seledunga ABB SHAMMA Richard Waziri wa Kaskazini Mwinjuma1 Kanungila Karim baracuda Mwamba028 besaro Pyepyepye Bilionea Asigwa ibn Kiti Chema Tugas Royal Warrior mederii mmangO manzi james LIKUD adrenaline Royal Son Mhadzabe salaniatz Natasha Ismail jiwe jeusi chibalangunamchezo
John Mloy conjuget Van Pauser great G Mtoto wa nzi Zeus1 hindustan Sci-Fi MAN OF PEACE kashata emnly danny baraka bb MTOTELA kbosho TEMLO DA VINCA
 
Back
Top Bottom