Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 9,189
- 16,128
Simulizi hizi unaweza kuzisoma Bure ndani ya app ya Maktaba Sauti. Ipo Playstore.
Huyu mzungu alizaliwa huko New Zealand. Baadaye akaja kuishi kwenye mapori ya mto Rufiji akiwa muwindaji. Majina yake mengine ni Mzee Rufiji au Mtawa maporini. Aliandika vitabu vinne vya kuchekesha sana juu ya maisha yake huko Maporini.
MZEE Rufiji au Baka (Barker) ametunga kitabu hiki kwa kutaka kuwafurahisha vijana. Vijana wa kimji na wa mashambani hamkosi mtakipenda sana kitabu hiki. Badala ya kwenda kilabuni ambako pengine upatikane na heka heka zisizo na maana, jisomee kitabu hiki, na vingine katika jamii hii vya huyu mzee ambaye si mwenyeji wa Afrika, lakini jinsi alivyo, tangu mwanzo wa tabia hata katika kuipenda kwake Afrika amekuwa naye Mwafrika mweupe.
Mimi ndiye Mzee Rufiji au Baka nijulikanaye sana karibu na watu wengi wa Afrika ya Mashariki, na pengi ulimwenguni kwa kazi yangu ya uwindaji. Nimepewa majina mengi na wenyeji wa Afrika niliopata kuishi nao katika taabu na raha. Nimepata kuitwa 'Bwana Ziraili' kwa jinsi nilivyozitoa roho za ndovu na wanyama wengi mwituni. Nimepata kuitwa 'Jitu Masoga' kwa masoga yangu, na majina mengi mengine; lakini lile langu la asili limeniselelea.
Vijana na mimi hufurahishana sana katika kila ninakotangatanga. Nawakumbuka wale watoto sita ambao habari zao niliziandika katika kitabu cha 'Masimulizi ya Mtawa Maporini: Kitabu cha Tatu' niliokwenda nao kuwinda hata tukatokewa na simba saba. Watoto hawa wa Kibantu waligeuza silaha kila walichokuwa nacho za kushambuliana na simba wale. Vitu vyenyewe walivyokuwa navyo vilikuwa ni machungwa, darubini, kofia, picha na birika.
Haya basi zisomeni wenyewe hadithi hizi zangu mie; natumaini hakuna atakayeanguka kutoka juu ya pikipiki kama alivyoanguka Mzungu mmoja rafiki yangu aliyezikumbuka hadithi zangu nilizomuhadithia alipokuwa akiendesha pikipiki na kucheka mpaka akaanguka.
MZEE 'RUFIJI'
Huyu mzungu alizaliwa huko New Zealand. Baadaye akaja kuishi kwenye mapori ya mto Rufiji akiwa muwindaji. Majina yake mengine ni Mzee Rufiji au Mtawa maporini. Aliandika vitabu vinne vya kuchekesha sana juu ya maisha yake huko Maporini.
Kitabu cha kwanza: Jinsi nilivyofika na Kukaa Afrika.
DIBAJI
DIBAJI
MZEE Rufiji au Baka (Barker) ametunga kitabu hiki kwa kutaka kuwafurahisha vijana. Vijana wa kimji na wa mashambani hamkosi mtakipenda sana kitabu hiki. Badala ya kwenda kilabuni ambako pengine upatikane na heka heka zisizo na maana, jisomee kitabu hiki, na vingine katika jamii hii vya huyu mzee ambaye si mwenyeji wa Afrika, lakini jinsi alivyo, tangu mwanzo wa tabia hata katika kuipenda kwake Afrika amekuwa naye Mwafrika mweupe.
Mimi ndiye Mzee Rufiji au Baka nijulikanaye sana karibu na watu wengi wa Afrika ya Mashariki, na pengi ulimwenguni kwa kazi yangu ya uwindaji. Nimepewa majina mengi na wenyeji wa Afrika niliopata kuishi nao katika taabu na raha. Nimepata kuitwa 'Bwana Ziraili' kwa jinsi nilivyozitoa roho za ndovu na wanyama wengi mwituni. Nimepata kuitwa 'Jitu Masoga' kwa masoga yangu, na majina mengi mengine; lakini lile langu la asili limeniselelea.
Vijana na mimi hufurahishana sana katika kila ninakotangatanga. Nawakumbuka wale watoto sita ambao habari zao niliziandika katika kitabu cha 'Masimulizi ya Mtawa Maporini: Kitabu cha Tatu' niliokwenda nao kuwinda hata tukatokewa na simba saba. Watoto hawa wa Kibantu waligeuza silaha kila walichokuwa nacho za kushambuliana na simba wale. Vitu vyenyewe walivyokuwa navyo vilikuwa ni machungwa, darubini, kofia, picha na birika.
Haya basi zisomeni wenyewe hadithi hizi zangu mie; natumaini hakuna atakayeanguka kutoka juu ya pikipiki kama alivyoanguka Mzungu mmoja rafiki yangu aliyezikumbuka hadithi zangu nilizomuhadithia alipokuwa akiendesha pikipiki na kucheka mpaka akaanguka.
MZEE 'RUFIJI'