Mwana Mtoka Pabaya
JF-Expert Member
- Apr 22, 2012
- 15,118
- 16,485
Mkuu, Ronaldinho hakuwepo Barca wakati wa Pep Guardiola..!
Mtu huyu awapo uwanjani inaaminika Malaika huacha shughuli zao huko mbinguni na kumuangalia.
Ronaldinho WAS the best, Messi IS the best
Thread inasema Ronaldinho ALIKUWA zaidi ya Messi Barrcelona.
nauhakika Gaucho akianzisha Dini basi Companero lazima uwe muumini.
kwenye dini ya messi wewe ndio utamshikia chetezo.....sasa ubishi wa nini? unakuwa mbishi kama waha bana....wale wanabishana kwenye treni na behewa zima....
Masaa machache kabla ya 'La Pulga', yaani 'The Flea' ama 'Kiroboto' kama anavyojulikana Messi, kuvunja rekodi ya Muller ya kupachika mabao, veterani Ronaldinho amesikika akijipendekeza. Mkongwe huyo anayezidi kuisha na kusahaulika katika medani ya kabumbu ametumia ile janja Waingereza wanayoiita 'famous by association', yaani 'umaarufu kwa kuhusiana', kudai kuwa mrithi huyo ya Maradona ana nafasi muhimu moyoni mwake. Mchezaji huyo Zilipendwa ambaye matumaini yake ya kuonekana kwenye uwanja wa kihistoria wa Maracana mwaka 2014 kwenye kombe la dunia yanazidi kufifia kama mwanga wa kibatari kilichoisha mafuta licha ya kuteuliewa kwa kocha wake wa zamani, Big Phil, kuiongoza Selecao anataka walau akumbukwe na manazi wake kina Gang Chomba kwa kumpa pasi Messi siku alipofunga goli lake la kwanza. Eti yeye Gaucho alikuwepo siku ilipoanza safari ya kuelekea kwenye umaarufu ya mpiga chenga na mabao huyu machachari ambayo mchezaji mwenzake wa timu ya Barca, Gerald Pique, amekiri kuwa anacheza mpira usio wa asili ya kibinadamu. Hebu jisomee mwenyewe kujipendekeza huku:
As Messi closes in on Gerd Muller's record of 85 goals in a calendar year, Ronaldinho paid tribute to his former Barcelona team-mate. "For me Messi is the best in the world," he added. "For the last few years he has played at a level of football we have never seen before. "I'm very proud to speak of him, because I was there when he started off and now he is the best in the world, it makes me so happy. "The game I remember the most is when he scored his first goal, because it came from my pass and I remember this game most vividly because he was just getting started. "I had the chance to be there and live that moment. I'm very happy that his first professional goal came from a pass from me. Messi knows that there will always be a place in my heart for him" - Ronaldinho: Neymar will be the world's best - ESPN FC
Dinho ni mkali zaidi ya Messi, nadhani kwa miaka 20 iliyopita(1992-2012) wa kumlinganisha na Dinho ni Zizzou peke yake na sio huyu mtumia HGH.
Nakubalian na Elizabeth Dominic kwamba LM anabebwa sana na vyombo vya habari.
LM ana mkataba wa udhamini na Adidas, ambao wana mkataba pia na FIFA, kwa hiyo Adidas wanahakikisha wanatoa mchezaji bora ili kukuza biashara yao. Kwa sasa FIFA ya Blatter iko extremely corrupt. Kwa hiyo wachezaji wanaodhaminiwa na Nike, Puma na Reebok kushinda tuzo itakuwa sio rahisi.
Mkuu Kalumbesa, kuna takwimu umewawekea pale juu hakuna hata mmoja wao atakayezikanusha! Wanazipita kama hawazioni huku mioyoni mwao zinawachoma! Haahaaa, HAKUNA KAZI NGUMU KAMA KUPAMBANA NA UKWELI....Halafu hata huyo Dinho mwenyewe alishakubali Messi ni NOUUUUMAAAA!!!!!!!!!
Amekiri bila yeye binafsi kujijumuisha, huyu ni mtu mzima na busara zake, hawezi sema yeye ni zaidi ya Messi..! Ni juu yetu sisi tunaoijua soka tuchuja bumba na mchele..! Mess bado sana kumfikia Ronaldino Gaucho..! Tofauti ni kwamba Dhino alikaa kwenye peak muda mfupi ukilinganisha na haka ka-messi.! Pili barca ya ka-messi si ya Dhino, hii imekamilika hata wewe upewe team una uhakika wa vikombe na hutoadhirika kama Aserne WengerDa mnabishana hadi na wachezaji wenyewe ambao ndio wanapigia kura mchezaji bora - wamempigia kura mchezaji mwenzao Messi kwa miaka 4 mfululizo na Ronaldinho mwenye kakiri kuwa kiwango cha huyo dogo aliyemkabidhi mikoba Barca hakijawahi kuonekana kabla!
Mkuu Kalumbesa, kuna takwimu umewawekea pale juu hakuna hata mmoja wao atakayezikanusha! Wanazipita kama hawazioni huku mioyoni mwao zinawachoma! Haahaaa, HAKUNA KAZI NGUMU KAMA KUPAMBANA NA UKWELI....
Miaka inavyozidi kwenda ndo vipaji vya soka vinazidi kupotea!messi anaonekana mkali kwakuwa yupo katika era ambayo haina wanasoka wenye vipaji ndo maana mbio zao za kushindania yuko yeye na ronaldo tu....angalia ronaldinho gaucho jinsi alivyokuwa anapata ushindani na wenye vipaji vya ukweli!gaucho akiwa dimbani anaweza akajibadilisha akawa pima maji,mkandarasi,feni au mabeki wakijifanya wajanja akajigeuza maji hapo ndo hazuiliki!
Lakini hichi kibushuti kinacheza mpira na watu wa mpira wa Darasani na sio vipaji kwa sana...