peno hasegawa
JF-Expert Member
- Feb 24, 2016
- 14,255
- 23,949
Aliyekuambia ni raia amekuzuga mkuuNaye ni mtanzania ana haki ya kutoa maoni, mbona mnakataa mawazo kinzani?
Kati ya majizi yanayojianda kunufaika na ufedhuri wa huu mkataba wa hovyo wa bandari, Rostam ndiye kiongozi wao. Ni swala la mda tu majina yatawekwa hadharani
Mfanyabiashara mkubwa nchini Rostam Aziz amezungumza na waandishi wa habari Juni 26, 2023 ambapo ameeleza mambo mbalimbali ikiwemo sakata la bandari ya Dar na kuhusika kwake kwenye uwekezaji huo mkubwa.
Mimi sijui wamekosania nini. Rostam anasema Dr. Slaa historia yake haimpi heshima wala uhalali wa kujifanya mzalendo. Siku zote anajijali yeye na tumbo lake.
Anaendelea...anasema aliacha utumishi wa Mungu kwa kuona maisha yake ni bora zaidi ya kumtumikia Mungu. Alijiunga na Chadema baada ya kukatwa CCM. Akajitoa Chadema baada ya kununuliwa na kupewa ubalozi. Anasema hana msaada kazi yake ni kupiga domo tu. Aiseee anamuita Kizabizabina ni mtu wa kuogopwa kama ukoma.
@Dr.W.P.Slaa tunasubiri majibu
My Take
CCM na Team ya Magufuli mje na nyinyi mtujibu mlimnunua Dr. Slaa kwa bei gani
Nasi tunavyo viambatanisho vyake ni suala la muda tu.Kati ya majizi yanayojianda kunufaika na ufedhuri wa huu mkataba wa hovyo wa bandari, Rostam ndiye kiongozi wao. Ni swala la mda tu majina yatawekwa hadharani
Aahaaaaaa,shikamoo Rostam
Mfanyabiashara mkubwa nchini Rostam Aziz amezungumza na waandishi wa habari Juni 26, 2023 ambapo ameeleza mambo mbalimbali ikiwemo sakata la bandari ya Dar na kuhusika kwake kwenye uwekezaji huo mkubwa.
---
Juzi katika mdahalo pale hoteli ya Serena nilisema kuwa sihusiki na hili jambo (mkataba wa bandari) kibiashara. Ningekuwa nahusika nisingekuwa jasiri wa kuyasema yale niliyoyasema katika mdahalo ule.
Unapohusika na jambo huwezi kulijadili, na pia huwezi kuwa na uwezo au neutrality (hali ya kutofungamana na upande wowote) ya kuzungumzia jambo lenyewe, hivyo ningekaa pembeni na kuacha wengine wajadili.
Mimi kama Rostam na kampuni zangu hatuhusiki na uwekezaji au utakaokuwa uwekezaji wa kampuni ya DP WORLD.
Mimi ni mfanyabiashara na nimewekeza ndani na nje ya nchi, na nimetangaza jina la Tanzania kote duniani kwa kuwavutia wawekezaji waje kuwekeza katika nchi yetu ili tuweze kupata ajira na tuimarisha uchumi wetu.
Watu wanapiga porojo na ninawapa changamoto waende mahakamani. Mimi ninaaminiwa na benki za ndani na za nje ndiyo maana wananikopesha,” amesema na kuongeza “Rais (John) Magufuli asigefungua viwanda vyangu kama mimi sio mfanyabiashara halali.
Mimi sifanyi kazi na serikali, huwezi kusikia Rostam anaomba tenda serikalini au anauza hata sindano serikalini. Mimi ni mfanyabiashara ninayefanya biashara na sekta binafsi ndio maana huwezi kunituhumu kuwa nimetoa rushwa au nimekula rushwa. Hayo maneno (ya Dkt. Slaa) ni ya uropokaji tu na yasiyifanyiwa utafiti.
Historia ya Dkt. Slaa haimpi heshima wala uhalali wa kujifanya eti yeye ni mtu wa kujali maslahi ya Watanzania. Siku zote amejijali yeye binafsi na maslahi yake binafsi.
Dkt. Slaa aliacha kazi ya utumishi wa Mungu kanisani baada ya utovu wa maadili kwa kuona maisha yake ni bora zaidi kuliko utumishi wa Mungu. Historia yake ni historia ya kukosa uaminifu an uadilifu.
Dkt. Slaa hakujiunga upinzani kutokana na imani yake kwa sababu jina lake lilikatwa alipogombea kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) na sababu iliyotolewa wakati wa kukatwa jina lake ni sababu ya kukosa uadilifu alipokuwa mtumishi wa Mungu kanisani.
---
My Take
CCM na Team ya Magufuli mje na nyinyi mtujibu mlimnunua Dr. Slaa kwa bei gani
Rostam amerudia tena enzi za Mengi? Si aliita siasa zetu ni uchwara akasusa na ubunge akakimbia? Nani kazitakasa siasa zetu hadi zikamvutia kurudi?Mfanyabiashara mkubwa nchini Rostam Aziz amezungumza na waandishi wa habari Juni 26, 2023 ambapo ameeleza mambo mbalimbali ikiwemo sakata la bandari ya Dar na kuhusika kwake kwenye uwekezaji huo mkubwa...
Rostam ana Cha kuonesha via makampuni yake,huyo Slaa ana kipi hasa?Wote ni wachumia tumbo..
Rostam ndio serikali. Kumbuka last moments za Jiwe pale Morogoro huyu na akina JK ni hatari sana.Hoja za Bandari, Dr Silaa alizielekeza serikalini.
Huyo Rostam anamjibu kama nani?
Kwahiyo kuna watu Dr slaa ni shujaa wao yaani!!!🤣🤣🤣🤣🤣🤣Asubirie mizinga na mabomu toka kwa Slaa..
Utawekwa ukweli kuhusu maskahi yake kwa DP workd atajuta kumsema
We subiria, unafikiri watampenda na aliwaita wao ni..oridha ya aibu?Kwahiyo kuna watu Dr slaa ni shujaa wao yaani!!!🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Hivi nyie vipusa na hohehahe mlitaka Dr Slaa afe kwa kumfia kengeza??? Mbona ni wajinga kiasi hiki??? DP World lazima apige mzigoDr slaa haaminiki ila kwenye maslahi ya nchi na kama hajalamba asali hua haongopi.
Halafu baadae akakimbilia huko huko🤣🤣🤣🤣We subiria, unafikiri watampenda na aliwaita wao ni..oridha ya aibu?
List of shame?