Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Nungunungu,

Umestukia eeh kama hapa kuna usanii wa ki JF tu... unless tuna question hata credibility ya Mwakyembe then tunawez kununua wholesale hii story... to me is another day Kubenea at work!

By the way get well soon KUBENEA....
 
naomba hicho kichwa ch ahabari kiwe hivi


RICHmond:Ikulu ya Rostam then nitaanza kuchangia kwanini Rostam wala hatishwi na haya mambo

Kweli bwana hata mimi sasa naona IKULU NI YA ROSTAM NA WAHINDI WOTE
 
Inasemekana kuwa huyo mtoto wa JK ndie aliyekuwa shahidi katika mkataba wa kuhamisha shughuli za Richmond kwenda Dowans,akiwa kama mwanasheria kwenye kamapuni ya IMMMA.
 
Reliable Sources Zinasema Kuwa ..hii Richmond Wote Walikuwepo[muungwana ,rostam,na Lowassa]...muanzilishi Rostam Na Ndie Aliyewauzia Wenzake Idea...

Muungwaana Alimuweka Rizwan Kama Msimamizi Wake Na Mwenzake Akamuweka Richard...rostam Alimuweka Mfanyakazi Wake Mmoja....

Muungwana Alishtuka Mapema Akaamua Kuuondoa Rizwan Haraka ....na Kipindi Hiki Ndipo Faili Lenye Majina Ya Wakurugenzi Lilipotea Brela....na Wala Halijapata Kuonekana...

lowassa Alichelewa Kushtuka ...na Wakati Anashtuka Na Kumuuandikia Muungwaana Kusudio La Kuachana Na Richmond...mwenzake Alishashtuka Kabla Na Lishaamua Richmond Imfie Lowassa Mkononi....aondoke...na Afe Kisiasa!!!..lakini Hata Hivyo Naye Lowassa Alishajitoa Ricmond Akamuachia Rostam..

Rostam Naye Ameshtuka Late Na Kuwapa Zigo Dowans ...lakini Bado Hawezi Kujitoa Dowans Kwa Kuwa Kila Mtu Anajua Ni Yake ..na Hata Vifaa Na Baadhi Ya Wafanyakazi Wametoka Caspian....

Hakuna Namna Ambayo Muungwana Naye Na Ikulu Yake Wanaweza Kujitenga Na Richmond...kwani Kama Hakuwa Na Nia Ya Kutumia Richmond Kama Mtaji Wa Kumuangamiza Lowassa...kama Rais Alikuwa Na Uwezo Toka Awali Wa Kuikataa Richmond ...baada Ya Kuwa Ameshtuka...tusingefika Huku....

Mie Umenisikitisha sana,Kama unajua haya Kwanini haukwenda kutoa ushahidi katika Tume ya Mwakyembe?Mie nachofahamu walialikwa watanzania wote wanaojua kuhusu RDC na wakaenda.au na wewe ulikuwa pamoja na Lowassa??AU ulisubiri wakuuite baada ya ushaidi kutoka JF na Bungeni.?ndio maana Lowassa alisema amenowa..alikuwa ana akimaanisha ameonewa na watu kama wewe ambao mlikuwa mnajua dili lote na hamkusema chochote.

ila bado una muda wa kuwasilisha maoni yako kama wanvyofnya wabunge.Naomba umuandikie e-mail spika kupitia E-mail yake ssitta-at-parliament-dot-go-dot-tz kumwelezea hoja yako au Mheshimiwa slaa wslaa-at-parliament-dot-go-dot-tz !
 
Inasemekana kuwa huyo mtoto wa JK ndie aliyekuwa shahidi katika mkataba wa kuhamisha shughuli za Richmond kwenda Dowans,akiwa kama mwanasheria kwenye kamapuni ya IMMMA.
Dr. Ringo Tenga ndio alihusika na hiyo mikataba na wala si Ridhwani.Kwanza Ridhwani hajafaulu Mtihani wa kuwa Advocate.ni mwanasheria tu
 
Inasemekana kuwa huyo mtoto wa JK ndie aliyekuwa shahidi katika mkataba wa kuhamisha shughuli za Richmond kwenda Dowans,akiwa kama mwanasheria kwenye kamapuni ya IMMMA.

1. JF mnatisha!!! kwa hiyo hapo kumbe IMMMA ndiyo ndio shaidi sasa kwa nini huyo dogo unamuhisha? Yeye kama mfanyakazi ana tatizo gani?

2. Serikali inataka transfer mkataba kutoka Richmond kwenda Dowans, sasa hili hizi part mbili zisilalamikiane... basi kunakuwa na shahidi in this case IMMMA, sasa hapo tatizo liko wapi?

3. Kama nilivyosema mchawi wenu ni Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali period.
 
Mchungaji Kishoka tutafasirie maandiko:

"Hakuna ushkaji mkubwa kuliko huu, wa fisadi mmoja kuutema ulaji kwa ajili ya washkaji zake" (Richmonduli 8:18)

"Kwa maana jinsi hii Lowassa alimpenda JK, hata akautema u-PM, ili kila aliyerichimondi asilowaswe bali awe na ulaji wa milele" (Bangusilo 3:16)


yaaani teh teh he he he.

hii hap ya moto toka kwangu

"Kwa kujiuzuru kwake nasi tumepona" Kilongola 5:9
 
Jamani eeee ni wapi hii nchi inapelekwa na watu wachache?huyu salva huyu naye ikibidi anyongwe maana alijua kila kitu si angewapa tu waandishi wengine wasema /mi nachoka natamani mwl angefufuka leo awaone vijana wake mambo wanayofanya sasa.MMH NI KWELI MKUU WA KAYA ALIHUSIKA?
Baada ya kusanuka ndiyo maana Lowasa kaambiwa jiondoe mapema ili issue ife lakini wameishia bango sana Bungeni kwa kuwa sasa wengi wanataka jambo hili liende Mahakamani .Na huko tutasiia mengi na Muungwana sasa tutaona kama kweli issue itaenda mbele hakutakuwa na wa kubakia katika kutajwa sawa na BoT ambayo inataka kumezwa na Richmond lakini watu wanasema next ni BoT .
 
Kweli bwana hata mimi sasa naona IKULU NI YA ROSTAM NA WAHINDI WOTE
nDUGU TUANDAMANE WEWE HUKJUA TOKA ZAMANI HAYA?ILA MWISHO WA HAO WAHINDI UMEKARIBIA KABISA KAMA JINA LAKO TUTAANDAMANA KUCHUKUA MALI ZAO KOTE NCHINI
 
hivi kwanini tunashindwa kung'amua kuwa huu mchezo Kikwete mwenyewe alikuwepo all along, ndugu zangu watanzania tuache kumtukuza huyu rais kwanini baada ya kupata nguvu tusianze kuhoji haya mambo tusiache yatupite. Mara hongera rais hivi kwa akili rahisi hata kwa asiye msomi tunashindwa kuconnect dots nakuona ma villain halisi?
 
yaaani teh teh he he he.

hii hap ya moto toka kwangu
Teh teh LOWASSA akwaambia wenzIe nami nakwenda mtaani kuwaandalia makao ili nitakapo kuwepo nanyi muwepo,ili tume zikiundwa mjue muda wa mavuno ya mafisadi umewadia.kisha akapanda ikulu kuomba JK ASIMFILISI.KAMATI ya mwakyembe ikatokea na jeshi ikamwabia NITAKAEMBUSU HUYO NDIYE.....
 
"How Lowassa, former PM was involved in....."

"How Low-ass, a former PM was involved in ...."

Kosa la namna hii kwenye uandishi huitwaje? Maana mfuatano (sequence) wa herufi naona zote ni zilezile!
 
Teh teh LOWASSA akwaambia wenzIe nami nakwenda mtaani kuwaandalia makao ili nitakapo kuwepo nanyi muwepo,ili tume zikiundwa mjue muda wa mavuno ya mafisadi umewadia.kisha akapanda ikulu kuomba JK ASIMFILISI.KAMATI ya mwakyembe ikatokea na jeshi ikamwabia NITAKAEMBUSU HUYO NDIYE.....

ebwana hilo ndilo agano lao duuuuu
 
Ikulu: Richmond anaijua Rostam

· Ndiye aliyeileta nchini
· Lowassa alimuingiza


Na Saed Kubenea

KAMPUNI ya Richmond Devolvement Company (RDC), ni mali ya mfanyabiashara na mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, imefahamika.

Taarifa za kuaminika zinamtaja Rostam kuwa kinara mkuu katika Richmond; waziri mkuu “aliyeng’olewa na Bunge,” Edward Lowassa, ‘aliingizwa na mwanasiasa huyo.’

Taarifa kutoka ndani ya Kamati ya Bunge iliyochunguza mkataba kati ya serikali na Richmond zinasema kwamba Mkurugenzi wa Mawasiliano, Ikulu, Salva Rweyemamu, ndiye aliyethibitishia Kamati kuhusu kuhusika kwa Rostam na Richmond.

Akizungumza 18 Desemba, 2007 katika kikao cha Kumi na Tano cha Kamati ya Bunge saa 10:23 jioni, Rweyamamu alilithibitishia Bunge kwamba anafahamu kampuni ya Richmond tangu Desemba 2006.

“...Mwaka jana, tuliombwa na watu wa Richmond, tuwasaidie katika ku-menage media katika matatizo yao kama yalivyokuwa na kwa kweli kazi hiyo tuliianza bila mkataba, tukaifanya,” alisema.

Alisema wakati huo ofisi za kampuni hiyo zilikuwa katika jengo la Mkadamu House jijini Dar es Salaam; alitukutanishwa na Gire kwa ajili ya kufanikisha kazi hiyo.

“Mheshimiwa mwenyekiti… our main contact person alikuwa ni mtu mmoja anayeitwa Gire nafikiri ni Mohamed, sina uhakika na jina la kwanza,” Salva alikiambia kikao cha Kamati ya Bunge.

Alisema, “Gire ndiye alikuwa representative wa Richmond hapa Dar es Salaam. … Gire alipewa namba yangu na rafiki yangu Rostam, I have that feeling. Kwa hiyo, baada ya hapo nikawa na-deal na Gire throughout."

Katika ushahidi wake huo uliochapishwa kuanzia ukurasa 955 hadi 964 katika kitabu cha Hansard za Bunge Sehemu ya Tatu, Salva anakiri kwamba Richmond ilikuwa ni kampuni ya kitapeli.

Ushahidi huo wa mkurugenzi wa mawasiliano wa Ikulu unathibitisha madai kwamba Richmond haikuwa kampuni ya Marekani, bali kikundi cha watu wa hapa nchini kilichokuwa na lengo la kukamua uchumi wa nchi.

Vilevile ushahidi huo unathibitisha kwamba wakubwa ndani ya serikali, akiwamo waziri mkuu aliyejiuzulu, Lowassa, alijua kila jambo kuhusu Richmond.

“Huu ni ushahidi mkubwa sana na ambao hauwezi kupuuzwa hata kidogo. Kwanza, ni kwa sababu, Salva ni swahiba mkubwa wa Rostam na ni mtu wa ikulu. Ushahidi wake, lazima uwe na ukweli,” alisema mbunge mmoja wa CCM, juzi mjini Dodoma.

Wakati Salva akizungumza hayo, Rostam alikanusha kuifahamua kampuni hiyo, lakini alikiri kwamba alimtambulisha Salva kwa Gire.

“Mimi nawafahamu Dowans, si Richmond. Hawa nawafahamu kwa sababu kampuni yangu ya Caspian inafanya kazi pale,” alisema Rostam mjini Dodoma.

Ushahidi wa Salva katika kamati unavunja minong’ono kwamba Kamati ya Mwakyembe iliwazushia Rostam na Lowassa kuhusu kuifahamu kampuni ya Richmond.

Ripoti ya Kamati Teule ya Bunge kuhusu mkataba kati ya serikali na kampuni ya kuzalisha umeme ya Richmond, iliwasilishwa bungeni Jumatano iliyopita na ilianza kujadiliwa Alhamisi, ambapo vigogo watatu wa ngazi ya juu katika serikali waliamua kuachia ngazi.

Vigogo walioachia ngazi ni Waziri Mkuu Edward Lowassa, Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na mtangulizi wake, Dk. Ibrahim Msabaha.

Kabla ya kuingia ikulu, Salva alifanya kazi katika kampuni G&S iliyokuwa inajihusisha na ushauri wa habari.

Huko alikuwa pamoja na mwandishi wa habari mwandamizi Gedion Shoo, ambaye kwa mujibu wa Salva bado anaendelea na kazi hiyo mpaka sasa.

“Hivi ninavyozungumza, sifahamu kama G&S wanaendelea na kazi hiyo, kwa sababu formally siko ndani ya G&S, nilijitoa baada ya kuanza shughuli yangu mpya. Siwezi kufanya kazi zote mbili,” anafafanua Salva.

Akibanwa na mjumbe wa Kamati Injinia Stela Manyanya, Salva alisema, “…on one side, the company was not delivering on the other side, unapewa wewe jukumu la kuiambia media kusema hapa, hii delivery itakuja tu subirini wakati huo nchi iko kwenye matatizo makubwa sana. Matatizo ya giza.”

Taarifa zinasema kujiuzulu kwa mawaziri hao kunafuatia shinikizo kubwa lililotokea ndani ya Kamati Kuu (CC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Imeelezwa kuwa baadhi ya wajumbe wa CC, walikuja juu, wakitaja majina na kushinikiza kwamba wote wanaotuhumiwa kwa ufisadi unaohusu Richmond na Akaunti ya Fedha za Nje (EPA) waachie ofisi za umma “na bila mjadala.”

Imefahamika kwamba wajumbe waliokuwa wakishinikiza waliongozwa na Abdulrahaman Kinana na makamu mwenyekiti mstaafu wa CCM, John Malecela.

Bunge katika kikao chake kilichopita, liliunda Kamati teule kuchunguza mkataba kati ya serikali na kampuni ya Richmond.

Kamati hiyo iliongozwa na mbunge wa Kyela (CCM), Dk. Harrison Mwakyembe.

tik tak tik tak tik tak
 
Reliable Sources Zinasema Kuwa ..hii Richmond Wote Walikuwepo[muungwana ,rostam,na Lowassa]...muanzilishi Rostam Na Ndie Aliyewauzia Wenzake Idea...

Muungwaana Alimuweka Rizwan Kama Msimamizi Wake Na Mwenzake Akamuweka Richard...rostam Alimuweka Mfanyakazi Wake Mmoja....

Muungwana Alishtuka Mapema Akaamua Kuuondoa Rizwan Haraka ....na Kipindi Hiki Ndipo Faili Lenye Majina Ya Wakurugenzi Lilipotea Brela....na Wala Halijapata Kuonekana...

lowassa Alichelewa Kushtuka ...na Wakati Anashtuka Na Kumuuandikia Muungwaana Kusudio La Kuachana Na Richmond...mwenzake Alishashtuka Kabla Na Lishaamua Richmond Imfie Lowassa Mkononi....aondoke...na Afe Kisiasa!!!..lakini Hata Hivyo Naye Lowassa Alishajitoa Ricmond Akamuachia Rostam..

Rostam Naye Ameshtuka Late Na Kuwapa Zigo Dowans ...lakini Bado Hawezi Kujitoa Dowans Kwa Kuwa Kila Mtu Anajua Ni Yake ..na Hata Vifaa Na Baadhi Ya Wafanyakazi Wametoka Caspian....

Hakuna Namna Ambayo Muungwana Naye Na Ikulu Yake Wanaweza Kujitenga Na Richmond...kwani Kama Hakuwa Na Nia Ya Kutumia Richmond Kama Mtaji Wa Kumuangamiza Lowassa...kama Rais Alikuwa Na Uwezo Toka Awali Wa Kuikataa Richmond ...baada Ya Kuwa Ameshtuka...tusingefika Huku....

Hii Richmond imeanza kuwa kama watergate ya Marekani, inaanza na watu wa chini lakini taratibu inapanda levels za uongozi.

Ningemshauri Kikwete aje public haraka, awaeleze watanzania ukweli wote kuhusu yaliyotokea hapa na kama alihusika hivi basi aombe msamaha kisha aahidi kutofanya haya tena........

otherwise, tik tak tik tak tik tak..........
 
Mimi nafikiri hii issue yote inatakiwa kwenda mahakamani ni uhujumu uchumi.

Wa kwanza Lowassa
Wa pili Bangusilo
Wa tatu Karamagi
Wa nne Aziz

Wakifika huko watasaidia kuingiza wengine.

Nashukuru kwa bahadhi ya wabunge wanaotaka wanyanganywe passport hili wasitoroke. Lazima ifike wakati wawe wanachapwa kiboko kimoja kwa siku. Kwa muda wa mika angalau mitano.
 
Bado ninayaamini maneno ya Kubenea, kuwa Slava alijuwa kuhusu huu wizi, na aknyamaza kimyaa wakati wa uchaguzi wa rais alikuwa mstari wa mbele kuwatukana wagombea against mtandao, sasa kwenye hili la Richimonduli kwa nini asiwatukane aliowapigia debe kina Lowassa? Mkuu Ngurumo, siku huyu mkuu alipochaguliwa ulisema huyu ni kichwa nikakuambia huyu ni mnafiki unayaona sasa?

Wakuu mbona huu mjadala ni kichwa na umetolewa na mtu kichwa Kubenea, ambaye yaliyomkuta na kusema ukweli sasa hapa JF hayajatukuta? Majuzi tu wote hapa tulikuwa tunamlilia alipomwagiwa acid, leo amekuwa muongo maana hasemi tunayoyataka?

Kuna watu tena mnaheshimika katika kila ngazi za taifa letu, na wengine hapa tunakuja kujifunza, na kama ni worthy kujiunga na upande wa pili, sasa mnapowashusha hadhi kina Kubenea, sisi wengine itakuwaje? Wazee mbona mnatutisha?
 
Rostam Aziz akaangwa
Shadrack Sagati, Dodoma
Daily News; Friday,February 15, 2008 @00:01

BAADHI ya Wabunge wamependekeza Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz (CCM), achukuliwe hatua za kisheria kutokana na kutajwa kuwa ndiye mmiliki wa kampuni ya Richmond inayodaiwa kuihadaa Serikali katika makubaliano ya kuzalisha umeme wa dharura.

Wakichangia ripoti ya Kamati teule ya Bunge juu ya mkataba wa kuzalisha umeme wa dharura wa kampuni ya Richmond bungeni jana, wabunge hao walisema kitendo cha Mbunge huyo kugoma kwenda kutoa ushahidi katika kamati hiyo ni dharau kwa Bunge na kwa Spika aliyeiunda.

“Hatuwezi kuhoji kwa sasa kwamba Richmond ni ya akina nani. Ukweli uko wazi kuwa ni wale walioshinikiza kampuni hiyo ipewe mkataba,” alisema Mbunge wa Sikonge, Juma Mkumba (CCM).

Alisema Rostam katajwa kuwa na uhusiano na Richmond na pia anatajwa kuwa na uhusiano na kampuni ya Dowans inayoendesha shughuli za Richmond kwa sasa na akahoji kwa nini Mbunge huyo na Waziri wa zamani, Daniel Yona, wasichukuliwe hatua kwa kugoma kwenda kutoa ushahidi mbele ya kamati ya Bunge.

Alisema Rostam ni aibu kwa CCM, kwa vile ni Mbunge wa chama hicho na Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho na kuongeza kuwa baadhi ya wafanyabiashara wameingia kwenye siasa ili kuficha maovu yao.

Mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi (CCM), alisema ni vyema Rostam achukuliwe hatua, kwa vile ni kiongozi wa CCM na yuko kwenye Halmashauri na Kamati Kuu ya chama hicho. Alisema kitendo cha Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu, kunukuliwa akimtaja Rostam kuwa na uhusiano na Richmond ni ushahidi wa kutosha.

Alieleza kuwa kwa vile waliotajwa kuhusika katika mkataba huo ni viongozi wa serikali, Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) halina tena jukumu la kulipa fedha kwa Dowans na badala yake serikali. Hata hivyo, wakati suala hilo linajadiliwa jana, Rostam hakuwamo katika ukumbi wa Bunge.

Mbunge wa Kilindi, Beatrice Shelukindo, alisema kitendo cha mawaziri kujiuzulu kwa kuhusishwa na kashfa hiyo hakiwezi kupooza suala la Richmond na badala yake alitaka fedha zote ambazo zimelipwa kwa kampuni hiyo zirudishwe na wahusika wote, bila kujali vyeo, wafilisiwe.

Beatrice alisema kwamba tangu kutolewa kwa ripoti hiyo kuna baadhi ya watu wamekuwa wanatishiwa na akatoa mfano kuwa familia yake, yeye na mume wake, William Shelukindo, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uwekezaji na Biashara kutokana na kukazania suala hilo hadi likaundiwa tume, sasa wanatishiwa maisha.

“Mimi na Mzee Shelukindo tumeanza sasa kujihoji kuwa labda tuandike wosia tukabidhi kwa mwanasheria kutokana na hali hii ilivyo sasa, lakini hatuogopi maana tunatetea maslahi ya taifa,” alisema Beatrice. Alisema haogopi mtu, kwani anafahamu kuwa mlinzi pekee wa maisha ya mtu ni Mungu.

Kiongozi wa upinzani bungeni, Hamad Rashid (Wawi-CUF) alisema hakuna haja ya watu kuandamana kufurahia watu kujiuzulu, kwani bado Watanzania wengi wako kwenye matatizo na sehemu nyingi za Tanzania ziko gizani.

“Hakuna haja ya kuandamana eti kwa vile Rais amevunja Baraza. Watu wetu bado wanateseka. Mimi naomba wabunge wenzangu tuungane kudai mikataba yote ije bungeni,” alisema. Alisema serikali ina jukumu la kuishitaki Richmond irudishe fedha zote ambazo imelipwa wakati ni kampuni ya kitapeli na akapendekeza Tanesco iache kulipa fedha ambazo zinatokana na mkataba huo wa kitapeli badala yake serikali ilipe.

Mbunge wa Iramba Mashariki, Mgana Msindai (CCM), alihoji zinakokwenda fedha zinazolipwa kwa Dowans na kutaka malipo yote yasimamishwe. Alisema kama kuna Watanzania ambao wanahusika kuileta nchini au kutunga uongo ionekane ipo ni vyema wakafilisiwa na kufikishwa mahakamani.

“Sasa kusiwe na mchezo, nyie mawaziri mlioaminiwa na Rais chapeni kazi, lakini jifunzeni kwa wenzenu,” alisema Msindai ambaye katika hoja yake, pia alisisitiza Taasisi ya Kudhibiti na Kuzuia Rushwa (Takukuru) ifumuliwe na iundwe upya.

Grace Kiwelu (Viti Maalumu -Chadema) alipendekeza waliotajwa katika kashfa ya Richmond wanyang’anywe hati za kusafiria ili wasitoroke nchini wakati wakisubiri kufikishwa kwenye vyombo vya sheria na wanaolalamika kuwa hawakutendewa haki na Kamati ya Bunge waende mahakamani wakasikilizwe madai yao.

Mbunge wa Ubungo, Charles Keenja (CCM), ambaye aliwahi kuwa Waziri alisema hivi sasa kuna wimbi la watu kuiba fedha za umma kwa kutumia kalamu na kampuni hewa. Alitoa mwito kwa serikali kuhakikisha wanapambana na eneo hilo kama ilivyofanya kwa ujambazi.

Hoja hiyo itahitimishwa leo kwa mtoa hoja, Dk. Harrison Mwakyembe, kujibu yaliyoelezwa na wabunge. Baadaye Bunge litayajadili mapendekezo yaliyotolewa na Kamati na kuyaboresha kabla ya kupeleka maazimio Serikalini.







Wasemavyo wasomaji:
 

· Ndiye aliyeileta nchini
· Lowassa alimuingiza


Na Saed Kubenea

KAMPUNI ya Richmond Devolvement Company (RDC), ni mali ya mfanyabiashara na mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, imefahamika.

Taarifa za kuaminika zinamtaja Rostam kuwa kinara mkuu katika Richmond; waziri mkuu “aliyeng’olewa na Bunge,” Edward Lowassa, ‘aliingizwa na mwanasiasa huyo.’

Taarifa kutoka ndani ya Kamati ya Bunge iliyochunguza mkataba kati ya serikali na Richmond zinasema kwamba Mkurugenzi wa Mawasiliano, Ikulu, Salva Rweyemamu, ndiye aliyethibitishia Kamati kuhusu kuhusika kwa Rostam na Richmond.

Akizungumza 18 Desemba, 2007 katika kikao cha Kumi na Tano cha Kamati ya Bunge saa 10:23 jioni, Rweyamamu alilithibitishia Bunge kwamba anafahamu kampuni ya Richmond tangu Desemba 2006.

“...Mwaka jana, tuliombwa na watu wa Richmond, tuwasaidie katika ku-menage media katika matatizo yao kama yalivyokuwa na kwa kweli kazi hiyo tuliianza bila mkataba, tukaifanya,” alisema.

Alisema wakati huo ofisi za kampuni hiyo zilikuwa katika jengo la Mkadamu House jijini Dar es Salaam; alitukutanishwa na Gire kwa ajili ya kufanikisha kazi hiyo.

“Mheshimiwa mwenyekiti… our main contact person alikuwa ni mtu mmoja anayeitwa Gire nafikiri ni Mohamed, sina uhakika na jina la kwanza,” Salva alikiambia kikao cha Kamati ya Bunge.

Alisema, “Gire ndiye alikuwa representative wa Richmond hapa Dar es Salaam. … Gire alipewa namba yangu na rafiki yangu Rostam, I have that feeling. Kwa hiyo, baada ya hapo nikawa na-deal na Gire throughout."

Katika ushahidi wake huo uliochapishwa kuanzia ukurasa 955 hadi 964 katika kitabu cha Hansard za Bunge Sehemu ya Tatu, Salva anakiri kwamba Richmond ilikuwa ni kampuni ya kitapeli.

Ushahidi huo wa mkurugenzi wa mawasiliano wa Ikulu unathibitisha madai kwamba Richmond haikuwa kampuni ya Marekani, bali kikundi cha watu wa hapa nchini kilichokuwa na lengo la kukamua uchumi wa nchi.

Vilevile ushahidi huo unathibitisha kwamba wakubwa ndani ya serikali, akiwamo waziri mkuu aliyejiuzulu, Lowassa, alijua kila jambo kuhusu Richmond.

“Huu ni ushahidi mkubwa sana na ambao hauwezi kupuuzwa hata kidogo. Kwanza, ni kwa sababu, Salva ni swahiba mkubwa wa Rostam na ni mtu wa ikulu. Ushahidi wake, lazima uwe na ukweli,” alisema mbunge mmoja wa CCM, juzi mjini Dodoma.

Wakati Salva akizungumza hayo, Rostam alikanusha kuifahamua kampuni hiyo, lakini alikiri kwamba alimtambulisha Salva kwa Gire.

“Mimi nawafahamu Dowans, si Richmond. Hawa nawafahamu kwa sababu kampuni yangu ya Caspian inafanya kazi pale,” alisema Rostam mjini Dodoma.

Ushahidi wa Salva katika kamati unavunja minong’ono kwamba Kamati ya Mwakyembe iliwazushia Rostam na Lowassa kuhusu kuifahamu kampuni ya Richmond.

Ripoti ya Kamati Teule ya Bunge kuhusu mkataba kati ya serikali na kampuni ya kuzalisha umeme ya Richmond, iliwasilishwa bungeni Jumatano iliyopita na ilianza kujadiliwa Alhamisi, ambapo vigogo watatu wa ngazi ya juu katika serikali waliamua kuachia ngazi.

Vigogo walioachia ngazi ni Waziri Mkuu Edward Lowassa, Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na mtangulizi wake, Dk. Ibrahim Msabaha.

Kabla ya kuingia ikulu, Salva alifanya kazi katika kampuni G&S iliyokuwa inajihusisha na ushauri wa habari.

Huko alikuwa pamoja na mwandishi wa habari mwandamizi Gedion Shoo, ambaye kwa mujibu wa Salva bado anaendelea na kazi hiyo mpaka sasa.

“Hivi ninavyozungumza, sifahamu kama G&S wanaendelea na kazi hiyo, kwa sababu formally siko ndani ya G&S, nilijitoa baada ya kuanza shughuli yangu mpya. Siwezi kufanya kazi zote mbili,” anafafanua Salva.

Akibanwa na mjumbe wa Kamati Injinia Stela Manyanya, Salva alisema, “…on one side, the company was not delivering on the other side, unapewa wewe jukumu la kuiambia media kusema hapa, hii delivery itakuja tu subirini wakati huo nchi iko kwenye matatizo makubwa sana. Matatizo ya giza.”

Taarifa zinasema kujiuzulu kwa mawaziri hao kunafuatia shinikizo kubwa lililotokea ndani ya Kamati Kuu (CC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Imeelezwa kuwa baadhi ya wajumbe wa CC, walikuja juu, wakitaja majina na kushinikiza kwamba wote wanaotuhumiwa kwa ufisadi unaohusu Richmond na Akaunti ya Fedha za Nje (EPA) waachie ofisi za umma “na bila mjadala.”

Imefahamika kwamba wajumbe waliokuwa wakishinikiza waliongozwa na Abdulrahaman Kinana na makamu mwenyekiti mstaafu wa CCM, John Malecela.

Bunge katika kikao chake kilichopita, liliunda Kamati teule kuchunguza mkataba kati ya serikali na kampuni ya Richmond.

Kamati hiyo iliongozwa na mbunge wa Kyela (CCM), Dk. Harrison Mwakyembe.

Looking for last minute
 
Ni kwa nini huyu Rostam Aziz hakuwepo bungeni wakati anajua issue yake inajadiliwa? Bado analileltea bunge jeuri; bora bunge lenyewe lianze kumuadhibu then CCM wafuate(kama wana ubavu) halafu vyombo vya dola vichukue mkondo wake. siku zote hawa Watz wenye asili ya kiasia huwa sio wazalendo kabisa.
 
Back
Top Bottom