Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

“Rostam Aziz alitakiwa atoe maelezo kuhusu uhusiano wake na Kampuni za Richmond na Dowans Holdings S.A, baada ya mashahidi kadhaa kudai kuwa ana uhusiano nazo.

“Aidha, alitakiwa aeleze kwa nini anwani ya barua pepe ya kampuni yake ya Caspian Construction Ltd, ilitumiwa na Dowans.”

Lakini alipoulizwa na Mtanzania jana, Rostam alisema yeye ana kampuni ya ukandarasi na amekuwa akifanya kazi na makampuni mbalimbali bila kujali mambo ya kisiasa.

“Mimi ni mkandarasi, nimefanya kazi na nitaendelea kufanya kazi na makampuni mengi, sina la kuficha katika hilo, kwani kila mtu anajua kampuni yangu,” alisema.

Sasa hapo ndiyo kajibu mapigo gani?.Huyu mtu siyo msafi ni mmoja wa mafisadi wakubwa na mtu wa karibu na JK. Si busara kwa Rostam Aziz kuendelea kushika nafasi katika serikali ya Tanzania kwa vile hayuko pale kwa ajili ya wananchi bali yuko pale kwa maslahi yake na wafanyabiashara wenzake wenye asili ya kiasia.

Ningeomba wanaJF kuweka mali zake hapa hadharani na kila aina ya biashara zake kwa kuwa magazeti mengi ameshayanunua.

-Wembe.
 
Sasa anaanza kuanzisha makampuni ya kutuibia wananchi wa kawaida, dawa yake ni moja tu, inafaa kurudishwa kwao.
Vinginevyo afuate sheria za nchi, UFISADI atafute sehemu za kuufanyia na siyo Tanzania.

Kwao ni wapi ndugu?
 
Sasa hapo ndiyo kajibu mapigo gani?.Huyu mtu siyo msafi ni mmoja wa mafisadi wakubwa na mtu wa karibu na JK.

Kuhusu ukaribu wake na JK sijui ila ninachojua kuwa alimwaga pesa nyingi CCM wakati wa kampeni ya u rais 2005...

Ningeomba wanaJF kuweka mali zake hapa hadharani na kila aina ya biashara zake kwa kuwa magazeti mengi ameshayanunua.

Huyu jamaa amenona hivi majuzi kama unakumbuka wa Chinese Delegation ilipokuja TZ alipewa contract ya ku supply ngozi China. ni contract kubwa ambayo,kama hakuwa very close na system,then sitegemei kuwa angepata.
Lakini ukiangalia the other side of coin,he is businessman na anatumia mapesa yake ku lobby hizi contract
 
Wakati bei ya Umeme imefikia kiasi kisicho kuwa cha kawaida naona bado kuna watu wanaleta mzaa.

Yaani watu wanasaini mikataba ya kutuuuza wananchi.

Mimi nafikiri kwa kuwa wabunge wametumwa na wananchi baada ya hapo wote waliohusika wafikishwe polisi mara moja wakiongozwa na Mkuu wao.

Huko ndiko waanze kusema jinsi wanavyoonewa.

Pia na wote walioimba wimbo ni wakati sasa wa kuwaita tena na kuwauliza kulikoni wimbo.

Nafikiri kamati ya Dr. Mwakyembe bado iendelee na Msabaa amesema atatoa ushirikiano nafikiri autoe Polisi.

Tunataka kujua milioni 152 analipwa nani?

Asije akawa analipwa Msabaa, Karamagi na Luwasa wakatuletea Mungiki-Tanzania.

-----------------------------------------------------Ninaunga mkono kauli yako kakindomaster. Hawa watu wote bwana isiishie tu eti kujiuzulu ndio basi...wafikishwe mbele ya vyombo vya sheria na kujibu mashtaka. mali zao zifilisiwe na pesa ipewe Tanesco waweze kuitumia ku-regulate bei ya umeme ishuke jamani.

Hawa mafisadi/conmen wanatakiwa wafikishwe mahali ambapo watajua Mtanzania wa kawaida, mlalahoi anaishije....can't afford to: buy LUKU, send his/her children to school, have 3-meals-a-day.
Wanatakiwa wafikishwe kwenye reality kama hii!
 
wengine wanaochangia kuiharibu nchi hii ni baadhi ya wahariri na waandishi wa habari!

Kimsingi rostam ni mtu mdogo sana, he s merely no body!!! lkn vyombo vya habari alivyovinunua vinampamba as if yuko maalum sana, tajiri sana nk, rostam ni dalali wa kawaida tu!! wala hana ujanja au elimu yoyote ya biashara!! tatizo ni wale anaokutana nao, they r very cheap!! ht lowassa na wengine wote!!

Mtu anapokosa integrity na kua cheap, ni jambo la kawaida kwake hata kunyang'anywa mke!! na asiseme lolote!!hana msimamo!!fedha haiwezi kukufanya uwe cheap! ni bora upotelee mbali, kabla mambo kukurudia.kama ilivyokuwa kwenye hili sakata la richmond.

Tuache bla bla tuwasaidie watu wa igunga, jimbo maskini kabisa ktk nchi hii, namna ya wao kumtoa rostam kwenye wadhifa alionao!! hapo tutajenga nchi, sio upuuzi huu tunaojadili hapa!

Truevoter
I feel you bro!.Ili tukusaidie na issue hii tunataka kujua kama wewe ni mmoja wa watu wa igunga . Tupe picha kamili tujue namna ya kugawana issue na kumla kabisa Rostam.
 
kwi kwi kwi
kwao ni Igunga ndugu yangu......

sio ukweli, kwao sio igunga Kwao ni Tora Bora Afghanistan,babu zake walifikia tu huko,unazania kwanini eneo linaitwa tabora?wazendo walishindwa kutaaamka Tora Bora(kwamfano kwa Mussa Hassan ambayo kwa sasa ni Msasani,Bush anatinga huku bongo mda sio mrefu labda anamhijia yeye(mungu tusadie)ampeleke guantanamo!!!!!!!
 
Ikulu: Richmond anaijua Rostam

· Ndiye aliyeileta nchini
· Lowassa alimuingiza


Na Saed Kubenea

KAMPUNI ya Richmond Devolvement Company (RDC), ni mali ya mfanyabiashara na mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, imefahamika.

Taarifa za kuaminika zinamtaja Rostam kuwa kinara mkuu katika Richmond; waziri mkuu "aliyeng'olewa na Bunge," Edward Lowassa, ‘aliingizwa na mwanasiasa huyo.'

Taarifa kutoka ndani ya Kamati ya Bunge iliyochunguza mkataba kati ya serikali na Richmond zinasema kwamba Mkurugenzi wa Mawasiliano, Ikulu, Salva Rweyemamu, ndiye aliyethibitishia Kamati kuhusu kuhusika kwa Rostam na Richmond.

Akizungumza 18 Desemba, 2007 katika kikao cha Kumi na Tano cha Kamati ya Bunge saa 10:23 jioni, Rweyamamu alilithibitishia Bunge kwamba anafahamu kampuni ya Richmond tangu Desemba 2006.

"...Mwaka jana, tuliombwa na watu wa Richmond, tuwasaidie katika ku-menage media katika matatizo yao kama yalivyokuwa na kwa kweli kazi hiyo tuliianza bila mkataba, tukaifanya," alisema.

Alisema wakati huo ofisi za kampuni hiyo zilikuwa katika jengo la Mkadamu House jijini Dar es Salaam; alitukutanishwa na Gire kwa ajili ya kufanikisha kazi hiyo.

"Mheshimiwa mwenyekiti… our main contact person alikuwa ni mtu mmoja anayeitwa Gire nafikiri ni Mohamed, sina uhakika na jina la kwanza," Salva alikiambia kikao cha Kamati ya Bunge.

Alisema, "Gire ndiye alikuwa representative wa Richmond hapa Dar es Salaam. … Gire alipewa namba yangu na rafiki yangu Rostam, I have that feeling. Kwa hiyo, baada ya hapo nikawa na-deal na Gire throughout."

Katika ushahidi wake huo uliochapishwa kuanzia ukurasa 955 hadi 964 katika kitabu cha Hansard za Bunge Sehemu ya Tatu, Salva anakiri kwamba Richmond ilikuwa ni kampuni ya kitapeli.

Ushahidi huo wa mkurugenzi wa mawasiliano wa Ikulu unathibitisha madai kwamba Richmond haikuwa kampuni ya Marekani, bali kikundi cha watu wa hapa nchini kilichokuwa na lengo la kukamua uchumi wa nchi.

Vilevile ushahidi huo unathibitisha kwamba wakubwa ndani ya serikali, akiwamo waziri mkuu aliyejiuzulu, Lowassa, alijua kila jambo kuhusu Richmond.

"Huu ni ushahidi mkubwa sana na ambao hauwezi kupuuzwa hata kidogo. Kwanza, ni kwa sababu, Salva ni swahiba mkubwa wa Rostam na ni mtu wa ikulu. Ushahidi wake, lazima uwe na ukweli," alisema mbunge mmoja wa CCM, juzi mjini Dodoma.

Wakati Salva akizungumza hayo, Rostam alikanusha kuifahamua kampuni hiyo, lakini alikiri kwamba alimtambulisha Salva kwa Gire.

"Mimi nawafahamu Dowans, si Richmond. Hawa nawafahamu kwa sababu kampuni yangu ya Caspian inafanya kazi pale," alisema Rostam mjini Dodoma.

Ushahidi wa Salva katika kamati unavunja minong'ono kwamba Kamati ya Mwakyembe iliwazushia Rostam na Lowassa kuhusu kuifahamu kampuni ya Richmond.

Ripoti ya Kamati Teule ya Bunge kuhusu mkataba kati ya serikali na kampuni ya kuzalisha umeme ya Richmond, iliwasilishwa bungeni Jumatano iliyopita na ilianza kujadiliwa Alhamisi, ambapo vigogo watatu wa ngazi ya juu katika serikali waliamua kuachia ngazi.

Vigogo walioachia ngazi ni Waziri Mkuu Edward Lowassa, Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na mtangulizi wake, Dk. Ibrahim Msabaha.

Kabla ya kuingia ikulu, Salva alifanya kazi katika kampuni G&S iliyokuwa inajihusisha na ushauri wa habari.

Huko alikuwa pamoja na mwandishi wa habari mwandamizi Gedion Shoo, ambaye kwa mujibu wa Salva bado anaendelea na kazi hiyo mpaka sasa.

"Hivi ninavyozungumza, sifahamu kama G&S wanaendelea na kazi hiyo, kwa sababu formally siko ndani ya G&S, nilijitoa baada ya kuanza shughuli yangu mpya. Siwezi kufanya kazi zote mbili," anafafanua Salva.

Akibanwa na mjumbe wa Kamati Injinia Stela Manyanya, Salva alisema, "…on one side, the company was not delivering on the other side, unapewa wewe jukumu la kuiambia media kusema hapa, hii delivery itakuja tu subirini wakati huo nchi iko kwenye matatizo makubwa sana. Matatizo ya giza."

Taarifa zinasema kujiuzulu kwa mawaziri hao kunafuatia shinikizo kubwa lililotokea ndani ya Kamati Kuu (CC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Imeelezwa kuwa baadhi ya wajumbe wa CC, walikuja juu, wakitaja majina na kushinikiza kwamba wote wanaotuhumiwa kwa ufisadi unaohusu Richmond na Akaunti ya Fedha za Nje (EPA) waachie ofisi za umma "na bila mjadala."

Imefahamika kwamba wajumbe waliokuwa wakishinikiza waliongozwa na Abdulrahaman Kinana na makamu mwenyekiti mstaafu wa CCM, John Malecela.

Bunge katika kikao chake kilichopita, liliunda Kamati teule kuchunguza mkataba kati ya serikali na kampuni ya Richmond.

Kamati hiyo iliongozwa na mbunge wa Kyela (CCM), Dk. Harrison Mwakyembe.
 
Salva alisema, “…on one side, the company was not delivering on the other side, unapewa wewe jukumu la kuiambia media kusema hapa, hii delivery itakuja tu subirini wakati huo nchi iko kwenye matatizo makubwa sana. Matatizo ya giza.”


This is very interesting, kwa hiyo huyu Salva, alipewa ukurugenzi Ikulu, huku rais akijua kuwa analo hili soo, maana nchi za wenzetu hii peke yake isingemruhusu kupewa hiyo kazi ya taifa, sasa sisi bongo vipi? Halafu hizi habari ndio zinatolewa public saa hizi? Salva anayesifia mtandao kila siku mbona hakusema haya mapema?
 
Hawa watu wanatu fool all along walikuwa wanajua kinachoendelea, mi naomba na ikulu iwe accountable with this all issue
 
naomba hicho kichwa ch ahabari kiwe hivi


RICHmond:Ikulu ya Rostam then nitaanza kuchangia kwanini Rostam wala hatishwi na haya mambo
 
This is very interesting, kwa hiyo huyu Salva, alipewa ukurugenzi Ikulu, huku rais akijua kuwa analo hili soo, maana nchi za wenzetu hii peke yake isingemruhusu kupewa hiyo kazi ya taifa, sasa sisi bongo vipi? Halafu hizi habari ndio zinatolewa public saa hizi? Salva anayesifia mtandao kila siku mbona hakusema haya mapema?

Nadhani hapa Salva tumsamehe kwa sababu kuu mbili:
1. Katika hiyo kampuni ya G&S, wao walikuwa wanafanya biashara ya media consultancy, na walipewa kazi hiyo ya kuishauri Richmond na media. Walifanya kazi hiyo kibiashara na hawakuiba cha mtu.
2. Alipotakiwa kutoa ushahidi kuhusu Richmond, alitoa ushirikiano kwa kuyasema anayoyajua.

Hii inaonesha ya kuwa Salva hayumo katika ufisadi huu. Ni kama hivi, ukiwa taxi driver na ukakodiwa na majambazi (bila kujua kuwa ni majambazi wametoka kupora), huwezi kuitwa nawe jambazi. Lakini ukiitwa kutoa ushahidi kuhusu hao abiria wako majambazi na ukakana ati huwajui, basi nawe utatuhumiwa pamoja nao. Ila ukitoa ushirikiano kuwa "mimi ninawakumbuka hawa jamaa, walinikodi kutoka Magomeni wakaniambia niwapeleke Tegeta, wakanilipa hela yangu nikawaacha huko Tegeta", basi huna kosa umetimiza wajibu wako. Naamini ndicho kilichotokea kwa Salva.
 
Reliable Sources Zinasema Kuwa ..hii Richmond Wote Walikuwepo[muungwana ,rostam,na Lowassa]...muanzilishi Rostam Na Ndie Aliyewauzia Wenzake Idea...

Muungwaana Alimuweka Rizwan Kama Msimamizi Wake Na Mwenzake Akamuweka Richard...rostam Alimuweka Mfanyakazi Wake Mmoja....

Muungwana Alishtuka Mapema Akaamua Kuuondoa Rizwan Haraka ....na Kipindi Hiki Ndipo Faili Lenye Majina Ya Wakurugenzi Lilipotea Brela....na Wala Halijapata Kuonekana...

lowassa Alichelewa Kushtuka ...na Wakati Anashtuka Na Kumuuandikia Muungwaana Kusudio La Kuachana Na Richmond...mwenzake Alishashtuka Kabla Na Lishaamua Richmond Imfie Lowassa Mkononi....aondoke...na Afe Kisiasa!!!..lakini Hata Hivyo Naye Lowassa Alishajitoa Ricmond Akamuachia Rostam..

Rostam Naye Ameshtuka Late Na Kuwapa Zigo Dowans ...lakini Bado Hawezi Kujitoa Dowans Kwa Kuwa Kila Mtu Anajua Ni Yake ..na Hata Vifaa Na Baadhi Ya Wafanyakazi Wametoka Caspian....

Hakuna Namna Ambayo Muungwana Naye Na Ikulu Yake Wanaweza Kujitenga Na Richmond...kwani Kama Hakuwa Na Nia Ya Kutumia Richmond Kama Mtaji Wa Kumuangamiza Lowassa...kama Rais Alikuwa Na Uwezo Toka Awali Wa Kuikataa Richmond ...baada Ya Kuwa Ameshtuka...tusingefika Huku....
 
Reliable Sources Zinasema Kuwa ..hii Richmond Wote Walikuwepo[muungwana ,rostam,na Lowassa]...muanzilishi Rostam Na Ndie Aliyewauzia Wenzake Idea...

Muungwaana Alimuweka Rizwan Kama Msimamizi Wake Na Mwenzake Akamuweka Richard...rostam Alimuweka Mfanyakazi Wake Mmoja....

Muungwana Alishtuka Mapema Akaamua Kuuondoa Rizwan Haraka ....na Kipindi Hiki Ndipo Faili Lenye Majina Ya Wakurugenzi Lilipotea Brela....na Wala Halijapata Kuonekana...

lowassa Alichelewa Kushtuka ...na Wakati Anashtuka Na Kumuuandikia Muungwaana Kusudio La Kuachana Na Richmond...mwenzake Alishashtuka Kabla Na Lishaamua Richmond Imfie Lowassa Mkononi....aondoke...na Afe Kisiasa!!!..lakini Hata Hivyo Naye Lowassa Alishajitoa Ricmond Akamuachia Rostam..

Rostam Naye Ameshtuka Late Na Kuwapa Zigo Dowans ...lakini Bado Hawezi Kujitoa Dowans Kwa Kuwa Kila Mtu Anajua Ni Yake ..na Hata Vifaa Na Baadhi Ya Wafanyakazi Wametoka Caspian....

Hakuna Namna Ambayo Muungwana Naye Na Ikulu Yake Wanaweza Kujitenga Na Richmond...kwani Kama Hakuwa Na Nia Ya Kutumia Richmond Kama Mtaji Wa Kumuangamiza Lowassa...kama Rais Alikuwa Na Uwezo Toka Awali Wa Kuikataa Richmond ...baada Ya Kuwa Ameshtuka...tusingefika Huku....

Mkuu Phil kama data zako hizi ni za kweli basi inabidi nifute kauli yangu ya kumtetea Salva hapo juu! Hatari kubwa hii!
 
Reliable Sources Zinasema Kuwa ..hii Richmond Wote Walikuwepo[muungwana ,rostam,na Lowassa]...muanzilishi Rostam Na Ndie Aliyewauzia Wenzake Idea...

Muungwaana Alimuweka Rizwan Kama Msimamizi Wake Na Mwenzake Akamuweka Richard...rostam Alimuweka Mfanyakazi Wake Mmoja....

Muungwana Alishtuka Mapema Akaamua Kuuondoa Rizwan Haraka ....na Kipindi Hiki Ndipo Faili Lenye Majina Ya Wakurugenzi Lilipotea Brela....na Wala Halijapata Kuonekana...

lowassa Alichelewa Kushtuka ...na Wakati Anashtuka Na Kumuuandikia Muungwaana Kusudio La Kuachana Na Richmond...mwenzake Alishashtuka Kabla Na Lishaamua Richmond Imfie Lowassa Mkononi....aondoke...na Afe Kisiasa!!!..lakini Hata Hivyo Naye Lowassa Alishajitoa Ricmond Akamuachia Rostam..

Rostam Naye Ameshtuka Late Na Kuwapa Zigo Dowans ...lakini Bado Hawezi Kujitoa Dowans Kwa Kuwa Kila Mtu Anajua Ni Yake ..na Hata Vifaa Na Baadhi Ya Wafanyakazi Wametoka Caspian....

Hakuna Namna Ambayo Muungwana Naye Na Ikulu Yake Wanaweza Kujitenga Na Richmond...kwani Kama Hakuwa Na Nia Ya Kutumia Richmond Kama Mtaji Wa Kumuangamiza Lowassa...kama Rais Alikuwa Na Uwezo Toka Awali Wa Kuikataa Richmond ...baada Ya Kuwa Ameshtuka...tusingefika Huku....

Baada ya kusanuka ndiyo maana Lowasa kaambiwa jiondoe mapema ili issue ife lakini wameishia bango sana Bungeni kwa kuwa sasa wengi wanataka jambo hili liende Mahakamani .Na huko tutasiia mengi na Muungwana sasa tutaona kama kweli issue itaenda mbele hakutakuwa na wa kubakia katika kutajwa sawa na BoT ambayo inataka kumezwa na Richmond lakini watu wanasema next ni BoT .
 
Tofauti kati ya data na majungu ni rahisi kuonekana.

Tazama hapa:
Akizungumza 18 Desemba, 2007 katika kikao cha Kumi na Tano cha Kamati ya Bunge saa 10:23 jioni, Rweyamamu alilithibitishia Bunge kwamba anafahamu kampuni ya Richmond tangu Desemba 2006.

Kisha soma hii:
Reliable Sources Zinasema Kuwa ..hii Richmond Wote Walikuwepo[muungwana ,rostam,na Lowassa]...

Hili ndilo linawapa heshima baadhi ya wana JF hapa. Anakuja na data: siku fulani, wakati fulani, mahala fulani kulitokea nini au kilisemwa kitu gani.

Sio kuja na 'inasemakana', 'habari za ndani'
'taarifa tulizo nazo' nk.

Kama una data mwaga vinginevyo kaa kimya uache wenye nazo watoe kuliko kuleta habari za kishabiki na majungu.
 
Reliable Sources Zinasema Kuwa ..hii Richmond Wote Walikuwepo[muungwana ,rostam,na Lowassa]...muanzilishi Rostam Na Ndie Aliyewauzia Wenzake Idea...

Muungwaana Alimuweka Rizwan Kama Msimamizi Wake Na Mwenzake Akamuweka Richard...rostam Alimuweka Mfanyakazi Wake Mmoja....

Muungwana Alishtuka Mapema Akaamua Kuuondoa Rizwan Haraka ....na Kipindi Hiki Ndipo Faili Lenye Majina Ya Wakurugenzi Lilipotea Brela....na Wala Halijapata Kuonekana...

lowassa Alichelewa Kushtuka ...na Wakati Anashtuka Na Kumuuandikia Muungwaana Kusudio La Kuachana Na Richmond...mwenzake Alishashtuka Kabla Na Lishaamua Richmond Imfie Lowassa Mkononi....aondoke...na Afe Kisiasa!!!..lakini Hata Hivyo Naye Lowassa Alishajitoa Ricmond Akamuachia Rostam..

Rostam Naye Ameshtuka Late Na Kuwapa Zigo Dowans ...lakini Bado Hawezi Kujitoa Dowans Kwa Kuwa Kila Mtu Anajua Ni Yake ..na Hata Vifaa Na Baadhi Ya Wafanyakazi Wametoka Caspian....

Hakuna Namna Ambayo Muungwana Naye Na Ikulu Yake Wanaweza Kujitenga Na Richmond...kwani Kama Hakuwa Na Nia Ya Kutumia Richmond Kama Mtaji Wa Kumuangamiza Lowassa...kama Rais Alikuwa Na Uwezo Toka Awali Wa Kuikataa Richmond ...baada Ya Kuwa Ameshtuka...tusingefika Huku....

Kaaazi kweli kweli, Mfamaji hakosi kutapatapa
Ni uhakika kwamba baada ya white head kuchota kodi zetu, yeye na wenzake wakaamua kucheza umafia wa karne kwa kumuhadaa Rizwani kununua hisa za Richimonduli na hili jukumu alipewa mtoto wa EL kumshawishi dogo aingie mtegoni, Na aliingizwa ktk panel baada ya hela kuyeyushwa ktk akaunti. Baadae muungwana aliposhtukia aligundua kuwa baadae atahusishwa kwani mwanae ni miongoni mwa wanahisa hivyo akaamua kureact ili kuwaumbua hawa matapeli peupe.
Hii habari ya Philemoni na dalili kuwa anamtetea EL kwa diplomasia ya hali ya juu.

White head amelikoroga na lazma anywe safari hii.
 
Mchungaji Kishoka tutafasirie maandiko:

"Hakuna ushkaji mkubwa kuliko huu, wa fisadi mmoja kuutema ulaji kwa ajili ya washkaji zake" (Richmonduli 8:18)

"Kwa maana jinsi hii Lowassa alimpenda JK, hata akautema u-PM, ili kila aliyerichimondi asilowaswe bali awe na ulaji wa milele" (Bangusilo 3:16)
 
Rostam Naye Ameshtuka Late Na Kuwapa Zigo Dowans ...lakini Bado Hawezi Kujitoa Dowans Kwa Kuwa Kila Mtu Anajua Ni Yake ..na Hata Vifaa Na Baadhi Ya Wafanyakazi Wametoka Caspian....


Mheshimiwa phillemon mikael..

Bila kuharibu mtiririko wa post zenu... nina angalizo moja! Caspian ni wajenzi kwa hivyo wao kuonekana kule Dowans ni jambo la kawaida kabisa... tujaribu kuleta lingine zaidi ya Hilo.
 
Back
Top Bottom