Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

kahawa-1.jpg

Watadai barabara safi, hospital,mashule pamoja na huduma nyingi za jamii kwa mtaji wa kucheza bao na kunywa kahawa.
 
Mgaya Kingoba, Dodoma
Daily News; Saturday,April 12, 2008 @00:01


MAELEZO ya Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz (CCM) kuhusu kuhusishwa kwake na kashfa ya kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond sasa hayatawasilishwa bungeni, imefahamika.

Akizungumza mjini hapa jana, Spika wa Bunge, Samuel Sitta alisema Mbunge huyo wa Igunga hataweza kutoa maelezo yake tena kwa sababu Kanuni za Bunge zinamzuia kufanya hivyo. “Kanuni ya 54, kifungu kidogo cha nne, kinamzuia kufanya hivyo.

Kanuni inaeleza wazi kuwa jambo likishazungumzwa na kutolewa maamuzi haliwezi tena kuletwa hoja kuhusu jambo hilo,” alisema Sitta na kuongeza kuwa jana alikuwa anaandaa barua ya kumjibu Mbunge huyo.

Alisema kwa mujibu wa maelezo aliyoyasoma katika maandishi ya Rostam, anaona kuwa yatazua mjadala mwingine kwani itabidi Kamati Teule nayo ijibu; jambo alilosema itakuwa ni kuleta vurugu bungeni.

Kanuni ya 54, kifungu kidogo cha nne, inasomeka; “Hoja ambayo, kwa maoni ya Spika ina lengo la kutaka jambo ambalo lilikwisha kuamuliwa na Bunge katika kipindi kilichopita, halitakubaliwa na Spika isipokuwa tu kama ni hoja ya kutaka uamuzi wa Bunge uliokwisha kufanyika ubadilishwe.

Kanuni ya 54, kifungu kidogo cha nne, inasomeka; “Hoja ambayo, kwa maoni ya Spika ina lengo la kutaka jambo ambalo lilikwisha amuliwa na Bunge katika kipindi cha kumi na miwili iliyopita kabla ya kikao kinachoendelea lifikiriwe tena,
halitakubaliwa na Spika, isipokuwa tu kama ni hoja ya kutaka uamuzi wa Bunge uliokwisha fanyika ubadilishwe.

Awali akizungumza na gazeti hili, Rostam alisema kwamba anamsikiliza Spika kwa sababu anamheshimu, anakiheshimu chama chake; lakini alisisitiza pia kuwa hahusiki na suala la Richmond; kwa vielelezo na uthibitisho alionao.

Katika mkutano wa 10 wa Bunge, Februari mwaka huu, Sitta alisema kwamba Rostam atawasilisha maelezo yake kuhusiana na suala hilo baada ya kuhusishwa nalo, lakini hakuwapo bungeni wakati huo.

Kashfa ambayo Rostam alitaka kuizungumzia iliundiwa Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, ambayo iliwasilisha ripoti yake katika mkutano huo na kusababisha kujiuzulu kwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, kutokana na ofisi yake kuhusishwa nayo.

Mbali na Lowassa, mawaziri wawili, Dk. Ibrahim Msabaha (Ushirikiano wa Afrika Mashariki) na Nizar Karamagi (Nishati na Madini), walijiuzulu baada ya wao pia kudaiwa kuhusika katika kuibariki kampuni hiyo ambayo Kamati Teule ilidai ilikuwa ya kitapeli na yenye utata.

Akizungumza jana, Rostam alisema kinachofanyika ni mchezo wa kuigiza na kwamba yeye anamsikiliza Spika, anamheshimu; anasikiliza maelekezo ya chama chake na akapuuza watu wanaoeneza umbea kuwa chama kitamdhibiti.

“Mimi ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM. Nasikiliza maelekezo ya chama changu. Lakini pia mimi ni Mbunge niliyetokana na CCM. Mimi ni mtu mzito katika chama. Siwezi kudhibitiwa kwa umbea,” alisema.

Baada ya kuijadili ripoti ya Richmond, wabunge walitoa mapendekezo 23 ambayo yalipelekwa serikalini kwa nia ya kufanyiwa kazi. Tayari Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amesema yamekwisha kufanyiwa kazi na wanayo ripoti ya wataalamu iliyoyapitia mapendekezo hayo na kutoa ushauri.
 
Watadai barabara safi, hospital,mashule pamoja na huduma nyingi za jamii kwa mtaji wa kucheza bao na kunywa kahawa.



Namuona Magid Mjengwa yuko nao labda tumuulize sera ya washika zake alio kuwa nao walikuwa wanalong juu ya nini ? Hapa yaonekana ni maeneo ya iringa .
 
Just curious hivi kama Sitta alimwita kiongozi wa Serikali na kumwonyesha waraka huu, je aliwakilisha kwa Kiongozi wa Upinzani?

Kwa nini suala linalohusu maslahi ya Taifa lizimwe na kuzungumzwa kichama na si Kiserikali?

Kwa wale mliokuwa mnabisha wajibu wa Mwanachama wa CCM ni kwa CCM kwanza ndipo afikiria Taifa mnasemaje sasa?
 
How about this for Change:

Tuweke the 'alleged' ufisadi wa Rostam pembeni, halafu....

Tunajua Rostam anayo mapesa, haihitaji CCM ili apate mkate wake wa kila siku (ila labda kwa kuongeza uzito wa mkate huo. ila pengine CCM ndio inahitaji mapesa yake!

Sasa basi, katika hali hiyo Rostam ajitutumue na kuwaambia CCM kuwa liwalo na liwe, hata kama ni kumfukuza uanachama wamfukuze, lakini yeye anataka kusafisha jina lake kwa wananchi wake wa Igunga na waTanzania kwa ujumla - so he proceeds na kusema ukweli wake hadharani.

For one, mimi ntamheshimu sana kwa kitendo kama hicho, na utakuwa ni mfano mzuri wa kuigwa. Wananchi tutayapima maneno yake na hata pengine kumrudishia kiasi fulani cha heshima yake kama ukweli umo katika maneno hayo.

Jambo la kusikitisha, hakuna mtu, hata hao wanaojiita 'safi' ndani ya CCM walio tayari kuonyesha ujasiri wao.
 
Hivi kwa nini spika asiwe neutral? Kwani ni lazima Spika awe mjumbe wa cc na NEC ya CCM? Ingekuwa spika ni kutoka upinzani je hii "consultation" ingefanyika?
 
How about this for Change:

Tuweke the 'alleged' ufisadi wa Rostam pembeni, halafu....

Tunajua Rostam anayo mapesa, haihitaji CCM ili apate mkate wake wa kila siku (ila labda kwa kuongeza uzito wa mkate huo. ila pengine CCM ndio inahitaji mapesa yake!

Sasa basi, katika hali hiyo Rostam ajitutumue na kuwaambia CCM kuwa liwalo na liwe, hata kama ni kumfukuza uanachama wamfukuze, lakini yeye anataka kusafisha jina lake kwa wananchi wake wa Igunga na waTanzania kwa ujumla - so he proceeds na kusema ukweli wake hadharani.

For one, mimi ntamheshimu sana kwa kitendo kama hicho, na utakuwa ni mfano mzuri wa kuigwa. Wananchi tutayapima maneno yake na hata pengine kumrudishia kiasi fulani cha heshima yake kama ukweli umo katika maneno hayo.

Jambo la kusikitisha, hakuna mtu, hata hao wanaojiita 'safi' ndani ya CCM walio tayari kuonyesha ujasiri wao.

Ujasiri gani tena?? Hawa watu wapo hapo kwa ajili yao na familia zako..kwao huo ubunge uwaziri ni kama kazi nyingine yoyote tuu...hawajajenga kichwani kwamba ni kwa manufaa ya tanzania kwa ujumla..thats why inabidi kuwadhalilisha na kuweka ma scandal yao adharani wamejisahau sana hawa watu!! Too bad the average tanzanian voter doesnt understand all this.. :-(
 
Unajua kuna kiongozi mmoja mzito wa serikali aliwahi kusema in private kuwa "....mtandao wamelikoroga hilo ni lazima walinywe...",

According to the dataz, ni kwamba wakulu wengi wasio mtandao wameamua kuakaa pembeni na kuwaangalia mtandao wakilikoroga, sasa wanawasubiri walinywe, mimi ninajiuliza swali moja muhimu kwamba hwa wakulu wanaohusishwa na ufisadi, kila kukicha tuhuma mpya, sasa wanawezaje kufanya kazi za taifa kwa ufasaha na huku pia wakishughulikia utetezi wa ufisadi wao?

I mean hivi ni kweli Rostam, sasa hivi anao muda wa kushughulikia taifa na hizi tuhuma? Mimi nafikri wale wote wanaohusishwa na tuhuma za ufisadi, ni vyema wakaanza kujiweka pembeni na uongozi, na ni wakati muafaka wananchi tukaanza kudai na hiyo sheria kwenye katiba yetu ya jamhuri!
 
Baada ya Chenge kuapishwa kuwa Waziri baada ya mabadiliko ya hivi karibuni aliulizwa kwanini anafikiri Rais amemteua tena kuwa WAziri licha ya kugubikwa na tuhuma kadhaa za ufisadi. Jibu lake will be a classical example of "i dunno know"; yeye akasema "muulize Rais"... guess what happened after that..
 
Unajua kuna kiongozi mmoja mzito wa serikali aliwahi kusema in private kuwa "....mtandao wamelikoroga hilo ni lazima walinywe...",

According to the dataz, ni kwamba wakulu wengi wasio mtandao wameamua kuakaa pembeni na kuwaangalia mtandao wakilikoroga, sasa wanawasubiri walinywe, mimi ninajiuliza swali moja muhimu kwamba hwa wakulu wanaohusishwa na ufisadi, kila kukicha tuhuma mpya, sasa wanawezaje kufanya kazi za taifa kwa ufasaha na huku pia wakishughulikia utetezi wa ufisadi wao?

I mean hivi ni kweli Rostam, sasa hivi anao muda wa kushughulikia taifa na hizi tuhuma? Mimi nafikri wale wote wanaohusishwa na tuhuma za ufisadi, ni vyema wakaanza kujiweka pembeni na uongozi, na ni wakati muafaka wananchi tukaanza kudai na hiyo sheria kwenye katiba yetu ya jamhuri!


FMES,
Weekend hii imekuwa nzuri sana maana naona tunakubaliana kwenye karibu kila kitu. Serikali hivi sasa wanatumia muda wao mwingi kufukia shutuma zinazowakabili, tokea za Richmond, EPA, IMMMA connections, Radar na sasa hizi overseas account za akina Chenge n.k. Ni muhimu tukaungana wote kushutumu na kuwataka JK na timu yake waachie ngazi au bunge liwatimue.
 
Haihitaji ufahamu wa elimu rasmi kujua mchezo anaofanya rostam.huyu hana rekodi kabisa hata ya kusimama kuuliza swali la nyongeza bungeni tangu awe mbunge wa Igunga.ni mwoga kuongea hadharan! Kama hawez kusimama kuuliza maswali bungeni au hata kuzungumza kwenye vikao vya baraza la madiwan jimboni kwake sembuse kujibu tuhuma dhidi yake bungeni!! Tena za jinai! Hawezi.kajenga mazingira ya kuleta hofu juu ya alichotaka kusema ili hatimaye azuiwe kujieleza kama alivyotakiwa na bunge! Ni mpumbavu tu anaweza kusema namsikiliza spika na chama changu kuliko kupata nafasi ya kukanusha yale aliyotuhumiwa nayo mbele ya umma.kwa vile hata hao anaosema anawaheshimu wanawajibika kwa umma pia direct au indirectly! Heshima ipi ni bora ya spika na chama? au watu wa Igunga na watanzania wote waliompa hiyo dhamana aliyo nayo! Jambo hili liende mahakaman tu! Lakini ni dhahiri kabisa rostam hana sifa tena za kubaki kuwa kiongozi tanzania! Anaonekana laghai, tapeli na fisadi! Kwa vile profile yake yote ina walakin mkubwa, URAIA wake, ELIMU yake hata BIASHARA zake! ashukuru vile anaishi nchi isiyokuwa na uzalendo, watu ni mashabiki tu! na hata sheria zilizopo hazifuatwi! Lakini atabaki na natural dignity pale tu atazungumzia tuhuma za richmond dhidi yake kwa vielelezo siyo lazima bungeni! Hata ikibidi kuacha ubunge kwa gharama ya ukweli.
 
Haihitaji ufahamu wa elimu rasmi kujua mchezo anaofanya rostam.huyu hana rekodi kabisa hata ya kusimama kuuliza swali la nyongeza bungeni tangu awe mbunge wa Igunga.ni mwoga kuongea hadharan! Kama hawez kusimama kuuliza maswali bungeni au hata kuzungumza kwenye vikao vya baraza la madiwan jimboni kwake sembuse kujibu tuhuma dhidi yake bungeni!! Tena za jinai! Hawezi.kajenga mazingira ya kuleta hofu juu ya alichotaka kusema ili hatimaye azuiwe kujieleza kama alivyotakiwa na bunge! Ni mpumbavu tu anaweza kusema namsikiliza spika na chama changu kuliko kupata nafasi ya kukanusha yale aliyotuhumiwa nayo mbele ya umma.kwa vile hata hao anaosema anawaheshimu wanawajibika kwa umma pia direct au indirectly! Heshima ipi ni bora ya spika na chama? au watu wa Igunga na watanzania wote waliompa hiyo dhamana aliyo nayo! Jambo hili liende mahakaman tu! Lakini ni dhahiri kabisa rostam hana sifa tena za kubaki kuwa kiongozi tanzania! Anaonekana laghai, tapeli na fisadi! Kwa vile profile yake yote ina walakin mkubwa, URAIA wake, ELIMU yake hata BIASHARA zake! ashukuru vile anaishi nchi isiyokuwa na uzalendo, watu ni mashabiki tu! na hata sheria zilizopo hazifuatwi! Lakini atabaki na natural dignity pale tu atazungumzia tuhuma za richmond dhidi yake kwa vielelezo siyo lazima bungeni! Hata ikibidi kuacha ubunge kwa gharama ya ukweli.


Truevoter unapata shida na mtu kama Rostam .Hizi ni spinning kaka wacha kuumiza kichwa kabisa .Hawana lolote hawa .
 
Mpasuko bungeni

na Charles Mullinda
TAnzania Daima~Sauti ya Watu

SASA kuna kila dalili kuwa hatua ya Kamati ya Uongozi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumzuia Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, kuwasilisha maelezo yake binafsi bungeni ya kutetea hoja zake zote alizozitoa dhidi ya Kamati Teule iliyoongozwa na Dk. Harrison Mwakyembe, inaweza kuligawa Bunge.

Dalili hizo zimeanza kuonekana baada ya wabunge kuanza kuonyesha tofauti za wazi za msimamo kuhusu hatua hiyo, huku baadhi wakikubaliana nayo kwa maelezo kuwa ni kwa masilahi ya CCM na kulinda hadhi ya Bunge, na wengine wakionekana kuipinga.

Wabunge kadhaa waliozungumza na Tanzania Daima Jumapili walieleza kuwa, hatua hiyo ya kamati ya CCM inatoa picha kwamba sasa Bunge limeanza kuyumba na kutumika vibaya baada ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta, kuonyesha mwelekeo wa kuyumba.

Aidha, kundi hilo la wabunge limekwenda mbali zaidi na kueleza kuwa, hatua hiyo ya uongozi wa CCM ambao umekubaliwa pia na Sitta, unalenga kuficha siri ya mkakati uliotumika kuwaangusha baadhi ya mawaziri, akiwemo aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa kwa sababu za kisiasa kwa kutumia kashfa ya Richmond.

Kwa mujibu wa wabunge hao, hatua hiyo inathibitisha kuwepo kwa mkakati maalumu wa kuwanyamazisha ama kuwamaliza kisiasa baadhi ya wanasiasa, unaoendeshwa na kundi moja la wanasiasa ndani ya CCM kwa kutumia kivuli cha Bunge.

Habari zaidi zilizolifikia gazeti hili zinaeleza kuwa, baada ya kuvuja kwa habari kuwa Rostam amezuiwa kuwasilisha maelezo yake binafsi bungeni, baadhi ya wabunge wameanza kujipanga kumshinikiza Spika Sitta kutoa nafasi kwa mbunge huyo kutoa maelezo yake ili ukweli ufahamike.

Mbunge wa Karatu, Dk. Willibrod Slaa ambaye jana alizungumza na Tanzania Daima Jumapili kupitia simu yake ya kiganjani, alisema Bunge limeanza kupoteza mwelekeo na sasa linaelekea pabaya.

Dk. Slaa alieleza kushangazwa kwake na hatua ya Spika wa Bunge, kuanza kuwa na maamuzi ya kutatanisha, ambayo yanaonyesha dhahiri kuwagawa wabunge.

"Tunaelekea pabaya, Spika anashangaza, anaanza kuwa na maamuzi ya kutatanisha ambayo ni dhahiri yanawagawa wabunge. Rostam alitakiwa ndani ya Bunge na Spika mwenyewe kutoa maelezo ya kutetea hoja zake, leo anakuja na maelezo yanarudishwa kwenye Kamati ya CCM wakati wengine wanapelekwa kwenye Kamati ya Maadili!

"Tunarudi nyuma kwenye Bunge kuwa chombo cha CCM. Spika anakubali kutumika, tunajua aliitwa Butiama na kuagizwa mambo yote yanayohusu chama chao yajadiliwe kwanza ndani ya chama. Maagizo hayo yanadhihirishwa na hiki anachokifanya sasa," alisema Dk. Slaa mmoja wa wabunge makini na wenye msimamo thabiti katika masuala ya msingi.

Alisema ingawa Spika amekwishatamka kuwa ameacha kuhudhuria vikao vya chama chake, hilo halitoshi, anachotakiwa kufanya ni kuachia nyadhifa zote alizonazo katika CCM ili awe na uwezo wa kukataa kutumiwa na baadhi ya viongozi wa chama hicho.

Kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, Hamad Rashid (CUF) ambaye pia ni Mbunge wa Wawi, naye alisema Spika Sitta ameanza kuyumba na kueleza kuwa asidhani kwamba limekwisha kwa sababu anatarajia kulifufua tena kesho (Jumatatu) kwa kuomba mwongozo wa Spika kuhusu kanuni iliyotumika kumzuia Rostam kutoa maelezo yake kama alivyotakiwa katika kikao cha Bunge kilichopita.

Alisema hatua iliyofikiwa na Kamati ya Uongozi ya CCM dhidi ya Rostam si sahihi, kwa sababu inamnyima haki yake ya kikatiba, kisheria na kiraia ya kujitetea dhidi ya tuhuma alizoelekezewa, na pia ufafanuzi aliotakiwa kuutoa na Spika.

"Chombo kilichotoa uamuzi huo si cha kikatiba, hakihusiani na Bunge. Spika anapaswa alete hoja ya kumzuia Rostam bungeni na Bunge ndiyo liamue, anachoogopa ni nini? Nina shaka na maamuzi hayo.

"Hili halijaisha, Jumatatu (kesho) nitamuomba muongozo Spika kuhusu kanuni iliyotumika kumzuia Rostam, na ninamshauri arudi kwenye kanuni na hansard aache kuyumba," alisema Rashid ambaye anaheshimika kutokana na kuwa na misimamo isiyoyumba.

Mbunge mwingine aliyezungumzia suala hilo ni William Shelukindo (CCM) wa Bumbuli ambaye alisema uamuzi uliochukuliwa na kamati hiyo ya CCM ni sahihi kwa sababu, suala la kamati teule iliyochunguza Kashfa ya Richmond lilishamalizika baada ya kamati hiyo kukabidhi ripoti yake kwa Spika, hivyo haliwezi kujadiliwa tena.

Alisema anazifahamu vyema kanuni za Bunge kwa sababu ni mjumbe wa Kamati ya Kanuni za Bunge na kusisitiza kuwa, uamuzi huo wa kuzuiwa kwa Rostam kutoa maelezo yake ni sahihi.

"Mimi ni mjumbe wa Kamati ya Kanuni za Bunge, ninazifahamu vyema kanuni, hii Richmond basi jamani imekwishafika mwisho. Jambo likishapitishwa na Bunge haliwezi kurudishwa tena. Kamati teule haipo tena, ilishamaliza kazi zake, hivyo hata kama Rostam atasimama na kutoa maelezo yake, hakuna mtu wa kujibu. Labda Rostam kama bado anataka kulizungumzia hili alilete kwa njia nyingine, lakini hii ni wazi Spika hatamruhusu, na ni sahihi," alisema Shelukindo.
Kwa upande wake, Mbunge wa Kigoma Mjini, Peter Serukamba (CCM), alieleza kuwa jambo hilo ni zito, hivyo halipaswi kuongelewa ovyo ovyo.

Alisema binafsi hayuko tayari kulizungumzia, lakini kama litafikishwa bungeni wabunge wataonyesha msimamo wao.

Mwanasiasa mmoja aliyedai kutokuwa upande wowote katika suala hili alieleza kuwa, Spika Sitta ameonyesha wazi kulinda jambo fulani katika suala hili, kwa kutoa kauli zinazotafautiana kila anapokuwa akizungumzia au kuulizwa kuhusu Rostam kuwasilisha maelezo yake bungeni.

"Huyu mtu ni mwanasheria, amekaa bungeni siku nyingi, inawezekana kweli hajui vizuri kanuni za Bunge, mwanzo alitangaza bungeni kuwa Rostam anawajibika kuwasilisha maelezo yake binafsi kuhusu kile alichokisema bungeni katika kikao hiki cha Bunge.

"Muda umefika, ameulizwa na vyombo vya habari, mwanzo alisema amemzuia kwa sababu alitaka kuwasilisha maelezo hayo bila kumpelekea ayapitie na kwamba alimuagiza ayaandike ampelekee, ayasome ndipo amruhusu, baadaye kasema wataalamu wake wanayapitia, kisha ameibuka na hii mpya eti haruhusiwi kwa sababu kanuni za Bunge zinamzuia kuyawasilisha, huyu ni mtu wa kutilia shaka," alisema mwanasiasa huyo ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini.

Katika kipindi kisichozidi siku tano, Spika Sitta ametoa kauli kadhaa katika vyombo vya habari kuhusu Rostam kuwasilisha maelezo yake bungeni.

Jumatano wiki hii, alilieleza gazeti dada la Tanzania Daima kuwa, amemzuia Rostam kuwasilisha maelezo yake binafsi bungeni kwa sababu alikuwa hajatimiza masharti ya kanuni za Bunge.

Alisema mbunge huyo wa Igunga alikwenda ofisini kwake Jumatano ya wiki hii akiwa hajaandika maelezo yake na akiuliza ni lini atapangiwa kujieleza na ndipo yeye akamweleza kuwa, hawezi kumruhusu kusimama bungeni kuyawasilisha mpaka atakapoyaandika na kumkabidhi ili ayapitie kwanza.

Siku moja baadaye, Sitta alilieleza gazeti hili kuwa alikuwa ameshapokea maelezo ya Rostam na akayakabidhi kwa washauri wake kwa ajili ya kupitiwa na kupatiwa ushauri kabla ya kumpangia tarehe ya kuyawasilisha au la.

Aidha, siku hiyo hiyo, Sitta alikiri kuhusu uamuzi wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuitisha kikao cha Kamati ya Uongozi ya CCM kujadili masuala mbalimbali, likiwamo hilo la Rostam.

Taarifa ambazo Tanzania Daima ilizipata kutoka ndani ya kikao hicho, zilieleza kuhusu kufikiwa kwa uamuzi wa Rostam kuzuiwa kuwasilisha hoja yake na habari hiyo ikaandikwa katika toleo la jana gazeti hilo dada la hili.

Jana hiyo hiyo, Sitta alikaririwa na gazeti moja (si Tanzania Daima) la kila siku akieleza kuwa, alikuwa amemzuia Rostam kutoa maelezo yake kwa sababu maelezo aliyoyaandika yangeweza kusababisha vurugu bungeni.


Maoni ya Wasomaji
Maoni yanayotolewa na wasomaji wa safu hii ni ya kwao na sio maoni ya kampuni ya Freemedia Ltd. Aidha sio maoni ya mtunzi au mwandishi wa habari au makala husika hapo juu. Maoni haya hayajahakikiwa wala kuafikiwa na kampuni ya Freemedia Ltd.
Maoni 12 yameshatolewa. (Nawe toa maoni yako!)
eeh nashangaa haman bado maoni watanzania bado hamjaamka. nayi wa USA semeeni hili.

Ya kwangu mafupi ni haya; watanzania tupo kwenye njia panda ambayo inabidi tuamue kunyoa au kusuka.Namkumbuka mzee ruxa wakati ule alisema klorokwini ni chungu ila lazima tuimeze ii tupone malaria. Tukubali tukatae huu ndio muda rasmi wa wa kuweka mambo wazi Spika anajaribu kuzima moto kwa kufunika na nyasi kavu. Hii si sawa na ni hatari zaidi.Lowasa alijitoa kafara akijua itakuwa mwisho na watanzania wataridhika na kuiacha serikali kuendelea kula kimya kimya.Huu ulikuwa mtazamo mbovu wa jambo kubwa la kitaifa kama hili la maslahi ya taifa.
Ni vyema ROSTAM akaeleza alishiriki vipi na nani kuhujumu nchi yetu. CCM wasimpikie cha kusema kwani maswali yataendelea tu. pia MASABAHA naye aeleze kwa nini alijiuzulu na wengine wote ili tuamue cha kuwafanya sisi kama watanzania tunaobeba mizigo ya ufisadi.Iweje mtu aombe msamaha kama hana kosa? watuambie makosa yao wameyajua?
Huu uwe mwisho wa serikali ya siri siri has akuhusu maslahi ya taifa.WABINGE MUWE NA MSIMAMO ILI TUANZE UPYA . NI BORA SASA BUNGE LIKAVUNJWA NA TUANZE UPYA NA SERIKALI MPYA . HILI HALIKWEPEKI KWANI SASA MAMBO YA CCM HAYABEBEKI TENA.

HUU NI MTAZAMO WANGU.

na emmanuel , Sweden, - 13.04.08 @ 10:33 | #6294

Hivi hakuna njia yeyote ya kumtoa huyu spika wa Bunge na akachaguliwa mwingine? Watu wanaotaka kuiyumbisha nchi hii nimeshaamini ni huyu spika, huyu ataleta machafuzi makubwa katika nchi hii.
Hivi ninyi Wabunge mlimchagua kwa kufuata vigezo gani? Mbona hamna kitu ktk akili yake jamani!! anatuaabisha kabisa.
Mimi nahisi ktk ripoti ya Rostam, nafikiri Spika na Kikwete wake watakuwa wamehusishwa na hataki wajulikane.

na Amani, Yemeni, - 13.04.08 @ 10:55 | #6298

Kwanza huo mpasuko wa Bunge uundiwe serikali ya Mseto kama anayoitaka Seif Sharifu na ******* wenziwe.Pili mliambiwa zamani kuwa huyo Mwakiembe katumiwa kuwaumiza wengine kisiasa, hamkusikia na mlimpigia makofi kwa ripoti yake ya ki-aina-aina!
Mimi nahisi hii Tanzania yote imejaa mafisadi hata waandishi wa habari nao wamo kwani hawajui hata kupima mambo.Wao ni kuandika tu ili gazeti linunuliwe.
Kama kweli Rostam kazuiliwa basi wabunge wahoji hilo.Tumechoka na hizo kelele za kila siku. Nyote wezi nyie!

na ABDI JUMA IBRAHIM, Tanga, - 13.04.08 @ 11:28 | #6311

Jana nilisema huyu Spika mbali ya kuwa mwanasheria na mzoefu,maji yamemzidi,yamefika shingoni,amejitahidi kuficha na kudhibiti lakini wapi,sasa ndio kajichanganya kabisaaa na amedhihirisha alivyo na mapungufu makubwa,uwezo mdogo wa kuamua na kujua aseme nini kwa wakati upi,haswa kwenye mambo mazito ya kitaifa.

Baada ya Dr mwakyembe kuliomba bunge litake maelezo dhidi ya shutuma zilizotolewa na Rostam, Spika kwa kauli yake mwenyewe alimtaka Mbunge huyo(Rostam) kutoa maelezo, "la sivyo utakuwa umeridhalilisha bunge" alisema spika wetu.

Sasa nashangaa mtu huyo huyo anasema Rostam haruhusiwi kutoa ufafanuzi wa alichokisema.Hivi huyu ni spika kweli.Tatizo letu mtu akikaa serikalini kwa muda mrefu tunaona anafaa,ukweli kuhusu capability na uwezo wake mdogo wa kufikiri na kufanya maamuzi umeonekana(critical thinking and prompt decision making).

Sishangai,huyu Spika alipewa nafasi hiyo kama hatua ya CCM kujirudi,ni fadhila ya mpasuko wa kimtandao ndani ya Chama cha mapinduzi.hana uwezo,maamuzi yake hayaendeni na CV yake,kabakia kujigamba kama mwana ngonjera. Watanzania wa sasa hawataki porojo na majigambo,wanataka kazi na tija,wanaujua ukweli na wanataka bunge lisimame kwenye ukweli.

Kama ni kweli kuna hujuma zilikuwepo, kuwatenga baadhi ya wanamtandao tunataka tujue,si haki,na ni hatari kubwa kwa usalama wa nchi,ni kuidhalilisha hiyo demokrasia mnayoimba kila kukicha ,ripoti ya Dr Mwakyembe niliipenda sana na nafikiri ni ripoti ya kwanza nzuri,iliyotolewa na kamati lukuki zilizokwishaundwa hapo zamani.Lakini sitapenda watuhumiwa wazuiwe kutoa ukweli na kujitetea.Ndiyo! Rostam alikuwa akitafuta ushahidi kama kamati ilivyotafuta ushahihidi,Je? haki iko wapi? sheria iko wapi? narudia tena demokrasia tunayoimba kila siku iko wapi?

Huyu fisadi wa kihindi(nitabadilisha sifa yake nitakaporidhishwa na utetezi wake)apewe nafasi,tena ya kipekee.Penye ukweli huongo ujitenga.Tena ni wakati muafaka wa kujikaanga yeye mwenyewe kwa mafuta yake.

Kwa muono wangu kuna kitu kikubwa zaidi ya sisi tunavyofikiria.kuna siri kubwa inayofichwa,maadam,ndio kumekucha siri itavuja na hapo ndipo tutajua ukweli halisi wa sakata zima la ufisadi.

Eti wanalinda masilahi ya chama.Ufisadi ni kosa la jinai,ni kosa kwa jamhuri na si chama tawala.je siku CAFU au Chadema wakichukua nchi nao wachote uchumi wetu na wawafunge watu midomo eti ni kwa ajili ya masilahi ya chama.Kwanza mi sielewi masuala ya bunge chama kinaingia vipi.

Narudia kusema.Hiki chama cha mapinduzi hakina jipya,na natabiri mwisho wao unakaribia.Vitabu vyote vya dini vinasema Hata Mungu hapendi kuona watu wake wakiteseka kwa sababu ya watu wachache.Wezi, majangiri,wauaji,Kaeni chonjo,kwani mwenye nguvu anawaletea mtafaruko na mgongano ili wananchi wanaonyanyasika lakini wagumu wa kimaamuzi waamke,waone kwamba sasa basi,liwalo na liwe.Hakika mtaripa madhambi yenu hapa hapa,mmefanya kufuru kujitengenezea maisha ya peponi kwa mgongo(on expence of)wa wananchi fukara,sasa jehanam inanukia,itawakuta hapa hapa,masaki,osterbay,ocean road,upanga nk.

Hakika nchi itatamalaki,ukweli unaofichwa utakapokuwa wazi.nasema mtaficha sana lakini utatoka tu kwani upepo wa mageuzi umeanza, na umeanzia ndani,umeanzia chunguni,ukitoka utakwenda kwa wananchi,watu ambao siku zote mnawarubuni waendelee kunyanyasika,waendelee kutaabika.Hakika mlikuwa mkiwapa matumaini hewa.

Wakati wa kuwadanganya sasa utakwisha kwani wameujua ukweli.hapatakuwepo porojo za kasi mpya au kasi ndogo!hapatakuwepo na njozi za uchumi umepanda kwa kasi ya asilimia 6.1% wakati hali yao ya maisha inaendelea kudhorota!hapatakuwepo na kupaa au kushuka kwa ndege ya maendeleo!Nasema ni wakati huo hakutakuwepo na tupeni mda kidogo,tunajenga mikakati mipya.

Sijui sasa mtakuja na slogan(kauli mbiu) gani ili kuendelea kuwarubuni, kuwatia hofu na kuwajengea matumaini ya kufikirika hao wapiga kura.Hata mkija na " maendeleo ya sunami",Kasi ya upepo!maendeleo ya kimbunga!", nasema hakuna atakayewasikiliza.

Mimi sina chama na katika uongozi wa juu wa vyama vyote,sioni kiongozi wa kutukomboa.angalau naona mwanga kwa baadhi ya viongozi wa chini wa baadhi ya vyama vya upinzani.ndiyo! sioni wa kutuongoza na tunataka wa kutuongoza na kutukomboa, tunataka wa kufanya mageuzi makubwa ya kijamii na kiuchumi.Ebu angalia bahati waliyopata majirani zetu Rwanda.Hakika wamempata wa kuwakomboa,tunataka watu kama kagame,Kiongozi ambaye akiwa anakula, anafikiria maendeleo ya wananchi wake,akiwa amelala anaota njozi za kimaendeleo na anazitekeleza hata kama ni chungu kama chroloquine kwa viongozi wenzake,yeye cha kwanza ni maendeleo na maisha bora kwa wananchi wake.Hatutaki Raisi mtalii, kila kukicha yeye yuko ughaibuni.Ni wakati gani atakaa chini.atakaa kitako,kuona na kutafakari maisha ya anaowaongoza.ndio maana anaishia kupokea taarifa zilizotengenezwa kumridhisha,si wamekwisha jua ni mpokea taarifa.

Nasema,wananchi hawatataka mkwala na mbwembwe za kutembelea mawizarani.Eh!jamani,viongozi wetu kwa usanii kweli awajambo.uko ni kudhihirisha kuendeleza utalii,lakini huo nauhita utalii wa ndani.wananchi hawatataka hotuba za kila mwezi,hotuba zisizo na mantiki,hotuba za kuwapumbaza.kwani watakuwa wameujua ukweli,wameangaziwa mwanga mpya.

Nawaona(I can see)(I ENVISION) wananchi wakijutia makosa waliyokuwa wakiyafanya kwa miongo mingi.wakitaka mapinduzi sasa,wakitaka mapinduzi katika box la kura.Nawaona wananchi wasioambilika tena,hawaelewi la mkwezi au mgema au mpanda nazi,wananchi waliotayari kujitoa muhanga kwa ajili ya masilahi ya nchi yao.Hakika hayo ndio maono yangu na hayako mbali.ndio kwanza yananza kufukuta ndani ya chama cha wabadhirifu.kupitia kwa kinara wao Rostam na Lowassa.

Naona mpasuko mkubwa unaoambatana na anguko la dola linalotoa kishindo kikubwa.Hakika anguko la dola yenye nguvu kama ile ya kirumi.Ni suala la muda,labda dola ilyopo ifanye mapinduzi ya ndani,itubu,iwarudie ilyowakosea na kuwaambia sasa basi,hatuwaibii tena na mabilioni tuliyoiba haya hapa,chukueni.Najua hiyo ni ndoto na haiwezekani,kinachobakia ni kutimilika kwa ndoto yangu ya kwanza ya mapinduzi ya kifikra vichwani kwa walala hoi na hatimaye kwenye box la kura.

na romwald, USA, - 13.04.08 @ 11:37 | #6314

kama Lowasa,Karamagi, na Msabaha walijitetea, kwa nini huyu Rostam ambaye ni mtuhumiwa mkuu asijitetee?
Kwa nini tutoe uamuzi wa upande mmoja tu (uliotolewa na Kamati ya Mwakyembe) na upande mwingine hatujausikia utetezi wake? Hata mahakamani huwa wanasikiliza pande zote mbili. Sasa hii hali hii nfio inaitwa ni Udikteta ndugu yangu Sitta. Sitta sisi sio watoto na usitubuluzebuluze sisi tumechoka.

na jandu, msumbiji, - 13.04.08 @ 11:53 | #6320

Si haki hatakidogo kumyamazisha Rostam kutoa utetezi wake kwani huyu ndiye kinara wa ufisadi wote uliofanywa dhidi ya nchi yetu! Naamini utetezi wake kaandikiwa na washauri wake ambao nadhani watamuingiza matatani zaidi kuliko kumponya.Ujanja atakaotumia ni kutaka kuongopa kuwa kulikuwa na ripoti mbili moja ikiwa ni hiyo yeye na wenziwe wameighushi kuonesha kwamba kamati iliiandika baada ya muda wake kwa maelekezo ya spika!! Kote huko ni kutapatapa kwake na rafikiye Lowassa. Ukweli ni kwamba kama hivyo ndivyo mbona hakumpa rafikiye atumie ushahidi huo alipoitwa kujitetea? Mafisadi maji yamewafika shingoni waacheni wajizamishe wenyewe wao wakidhani wanajibu mapigo.

na Bulesi, Tanzania, - 13.04.08 @ 12:18 | #6323

JAMANI MUSISHANGAE YANAYOTOKEA CCM UKWELI NI KUWA SERIKALI BADO NI LOWASA ROSTAM NA KIKWETE:

Fukuto la fukuta, moshi wafoka, mapovu yanamwagika, CCM imefika njia panda! Ama isuke au inyoe!

Hili vurugu la Richmond, likizingirwa na BOT EPA, BOT CIS, BOT Minara, Rada, Kiwira, Buzwagi na moto kutoka Upinzani, unafanya mambo kadhaa tujiandee kutokea.
1. Wabunge ambao si mtandao, wenye uchungu wa kweli wa CCM, kuendelea kusulubisha viongozi wao na Serikali yao iwe wazi. Hawa wabunge, mwokozi wao na nguzo yao ni Wastaafu Malecela, Kawawa, Mwinyi, Salim na Msuya. Huku wako hawa walioshupalia RDC;-Mwakyembe, Kilango-Malecela, Seleli, Kimaro, n.k.
2. Team Mkapa; huku ni wale wajanja wa Che-Nkapa ambao bado wanatibu majeruhi ya mchakato wa kugombea Urais 2005 na kunyang'anywa tonge la Hatamu za Chama. Hapa kuna Mang'ula, Ngwilizi, Kigoda, Kinana, Warioba na Ruhinda. Katika kundi hili, pia wapo wale waliotajirika na mradi wa Ujasirimali Ikulu; Yona, Mramba, Mgonja, Mkono n.k.
3. Mtandao; Kundi hili lina majeruhi wengi kutokana na kuvunjwa kwa baraza la mwazirina mwegemeo wa kashfa za ufisadi kuwa kwenye shingo zao. Kundi hili, limegawanyika katika sura mbili;
1. Team Kikwete ambayo wamebakia Makamba, Chiligati, Membe, Migiro, Karume
2. Team Rostwassa(Rostam/Lowassa); Karamagi, Msabaha, Nchimbi, Apson, Meghji, Kamala, Masha Diallo, Chenge,
4. Wasiofungamana lakini wana nguvu na ni tishio; Pinda, Mwandosya, Sumaye, Balali, Salmin, Magufuli, Msekwa na Sitta.
Serikali mpya na baraza lake la mawaziri bado ni ya Kikwete Lowasa na Rostam.

Masha-Mambo ya ndani, bila Lowasa Bw. Mdogo Masha asingekuwa hapo alipo, ni lowasa aliyemshika mkono na kumwingiza kwenye siasa, kwani yeye Masha na Business partner wake Magai walikuwa private lawyers wa mamvi, na hata Magai aliwahi kupatiwa ujumbe wa bodi ndani ya city water wakati huo Lowasa ni waziri wa maji. Je unategemea Masha atasahau alikotoka kama JK asivyomtupa Hussein Mwinyi???? Hao polisi, Manumba na Magereza vyote viko chini ya Masha. Sasa je, nani atamkoma Nyani giradi????

Ngeleja-Nishati na Madini- Huyu alikuwa mwanasheria mkuu wa Vodacom Tanzania LTD ambako Rostam na lowasa wana hisa japo mamvi ni silent share holder. Ni Rostam aliyemshika mkono Ngeleja akagombee Sengerema na kumpatia fungu la kutosha ashinde. Na ndio maana ameachwa madini ili aendelee kulinda migodi ya Rostam. Hivyo tusitarajie mabadiliko makubwa.

Mkullo-fedha- Huyu akiwa mkurugenzi wa NPF sasa NSSF alichota mapesa kibao kumuunga mkono JK mwaka 1995, hivyo ni senior mwanamtandao. Na ndio maana Mkapa alipoingia madarakani akamtema NSSF.

Chenge- Miundombinu, JK hana namna, hampendi Chenge lakini anakuwa forced na Lowasa na Rostam. Mikataba yote kuanzia IPTL n.k imesainiwa wakati wa Chenge na yeye anaelewa nani ni nani katika hayo makampuni yanayozidi kuutafuna utajri wa taifa hili na kutuacha watanzania tukilalia chips kavu. Eti JK atamtosa Chenge! THUBUTU! Atasema kila kitu ! Na ndio maana wakamuwahi Salome mbatia wakamuua ili asiendelee kutoa siri kwa wapinzani kuhusiana na pesa za BOT, kwani yeye ndo alikuwa Mweka hazina mkuu wa chama wakati wa uchaguzi

Kutokana na kuwepo makundi haya makubwa na utata unaotambaa angani hasa baada ya Lowassa kuangushwa na minong'ono kuwa naye Lowassa no Rostam ana ushahidi wa kujikosha, linalobakia kwetu watazamaji ni kupima upepo na kuomba dua wapigane na wagawanyike ili tujue nani ni kwa manufaa ya Taifa na nani ni mnyonyaji.Kutokana na kuogopa kumwagiana radhi ndo maana wanaanza kudhibitiana.

CCM si salama, na hata kama wakitoka nje ya ukumbi wakiwa wamekumbatiana, tusiwaamini.Hivyo si shangai kwa CCM kutumia bunge kumzuia Rostam kuwasilisha hoja.

na kimla, Tanzania, - 13.04.08 @ 12:38 | #6331

mwanangu usiseme sana chama cha mafisadi(CCM) ukijui watampeleka sasa hivi marekani watufunge kamba anaumwa na hata hospitali atakayolazwa tusiambiwe.twende nao taratibu kwa tahadhari sasa hivi maji yako shingoni we uoni fisadi balali hadi leo wanasema hajulikani haliko,kaa chonjo mpenda nchi

na chapakazi, tanzania, - 13.04.08 @ 12:39 | #6332

hawa wabunge ameingia mkenge, Rostam hana lolote zaidi ya kuleta mhcngangyiko huu ambao hata vyama vya upinzani na waandishi wa habari wmeingia mkenge.

NI DHAIRI ROSTAM ALIJUA MAELEZE YAKE HAYATAKUBALIWA BUNGENI KWA MUJIBU WA KANUNI ZA BUNGE(58-59).JAMBO LIKISHAJADILIWA HARIRUHUSIWI TENA, HIZI KANUNI ZIMEWEKWA TANGU ROSTAM HAJAZALIWA NA ANALIFAHAMU HILO.

AMEFANYA MAKUSUDI KUTUNGA TAARIFA YAKE NA KUPELEKA KWA SPIKA AKIJUA WAZI ATANYIMWA KUONGEA, HII NI NJIA YAKE Y KUJISAFISHA NA AMEWAPATA WENGI.

MAFISADI WANA AKILI SANA, HAO LAO MOJA SITTA,ROSTAM KIKWETE, LOWASSA, MTAFUNGUKA MACHO LINI???

na Imani - 13.04.08 @ 13:07 | #6337

hapa kuna usanii mkubwa kuliko kawaida ndo maana nilisema sitta achunguzwe .huyu si msafi ni kinyonga na kamwe hakuna mtu wa akili timamu anayeweza kukubali kumdhamini kinyonga kwa sababu anabadilika rangi kwa kila wakati.
wakati wabunge wa Cuf walipotoka nje waliambiwa haya ni mmasuala ya chama kwa hiyo walipewa adhabu lakini leo kamati ya chama inamzuia rostamu kujitetea haya si masuala ya chama!!!
Nilisemaq rostamu asiitwe fisadi kabla ya kujitetea na kama watu wako makini watajua kuwa huyu bwana ana washauri makini na ndo maaana alitaka kusemaq bila kuandika maana angeropoka na sitta ni mjanja anajua ambachoi angesema ndo maaana kaytaka maandishi.
hapa hakuna mtu safi labda ummma tutumie nafasi hii kuyajua mengi katika kipindi hiki cha mpasuko.

na wilibroad peter, sweden(örebro), - 13.04.08 @ 13:25 | #6342

Kila mwamba ngoma, ngozi huvutia kwake. Sitta mambo yamemfika shingoni, ama atetee maslahi ta CCM au ya TAIFA. Ni wazi ameamua kutetea maslahi ya CCM, sasa kazi ni kwetu sisi wananchi nini tufanye.

Rostam ameshatengeneza penati-maguu 12, refa ni wabunge CCM, washika vibendera ni wabunge UPINZANI, watazamaji ni wananchi. Sasa refa akipendelea wananchi ni lazima tuingie uwanjani na kuchukua sheria mkononi.

Unyerere warudi tena BUNGENI. Mlilala hundingwandingwa, mwimacho hambiwi tule!!!!!!!!!!!!!!!

na Zawadi Ngoda, Dar es salaam/ Tanzania, - 13.04.08 @ 13:52 | #6349

Rostam pia anahusika kwenye kashfa ya uchotaji wa mabilioni ya shilingi pale Wizara ya Kilimo,kama ilivyoandikwa kwenye gazeti la MwanaHALISI,two weeks ago.Huyu mtu haridhiki! Kweli muonja asali haridhiki mara moja.But unfortunately mambo kama haya huwa hayawafikii wapiga kura mahalia,kwani huko vijijini kama Igunga huwa vyombo vingi vya habari huwa haviwafikii wananchi.Hata kama inatokea magazeti kuwa yanapelekwa huko,basi mabepari kama Rostam na Chenge huwa wanayanunua yote hata kabla hayajafika kwa wananchi.

Pia nashangazwa na ukimya wa serikali kuhusu huyu kupe Balali,je huo ugonjwa gani miezi yote hii?Au ana chronic terminal disease,(ingawa si vyema kuombea hivyo).Hapa kutakuwa na mchezo wa kijanja wa kumficha ili tusihoji,but serikali lazima itambue kuwa wananchi sasa wameamka,hatutasahau suala hili,tunajua anafichwa ili asiwataje wahusika wengine wa EPA.Mwalimu alipolazwa pale St Thomas tulikuwa tukipewa updates zake kila siku,sembuse huyu tapeli,"kuna siri gani kali" huko "sirikalini?"

na David, Dar, - 13.04.08 @ 14:12 | #6358
 
Rostam amejiandalia anguko la pili?



Ansbert Ngurumo



NILITARAJIA kwamba Kamati ya Uongozi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ingemfunga mdomo Mbunge wa Igunga, Rostam Azizi, ili asijitetee kuhusu alivyohusishwa na kashfa ya Richmond.


Ni kawaida ya kamati hii kuziba watu (wabunge wake) midomo wanapokaribia kuibua mambo mazito yatakayoivua nguo. Lakini yawezekana kwamba katika hili, sasa ndiyo inamzibua mdomo Rostam Azizi.

Rostam Azizi hakuzuka tu. Alijipanga na alidhamiria. Anaijua kamati hiyo, na amekuwa akiitumia kuziba mengine. Alijua analeta mambo mazito dhidi ya Bunge na CCM yake; na alifanya mikakati na wadau wenzake kabla ya kwenda bungeni.

Alijua waziri mkuu angeitisha kikao hicho kumdhibiti. Nimeshangaa kwamba amekubali kudhibitika!

Zaidi ya hayo alijua kwamba Spika wa Bunge, Samuel Sitta, asingeipokea na kuipitisha hoja yake moja kwa moja. Anajua madhara yake. Hata Sitta alijua kuwa Rostam Azizi anaandaa mashambulizi, kwani ni mwendelezo ule ule wa utetezi wa kambi ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, kujitetea na kusafisha majina yao.

Sitta alijua fika kuwa wanaosafisha majina yao ndio hao wanaosababisha kile alichokiita ‘siasa za maji taka,’ za kuibua kashfa zake.

Baadhi yetu tulishaonya kuwa suala hili la Richmond halikuwa la Lowassa na Rostam pekee; na kwamba haliwezi kwisha sasa. Tulisema pia kwamba kama Lowassa asingejiuzulu, tungejua mengi makubwa, iwapo wangeanza kutajana.

Lowassa alitunyima fursa hii. Alikataa kujitetea. Alikataa kusema anachokijua. Akajiuzulu. Naamini sasa kambi yake imejizatiti upya, na hoja zake zitapatikana katika utetezi wa Rostam Azizi.

Hapa katikati yametokea mengi ndani na nje ya CCM, ambayo hata Spika wa Bunge anayajua.

Kwanza, Rostam Azizi na Lowassa wamekuwa wakilalamika kwamba walihusishwa kimakosa. Alianza Lowassa, baadaye wakubwa wakamzima kama kibatari, baada ya kuona wana Monduli wamemwekea zulia jekundu!

Sasa ni zamu ya Rostam Azizi; na ujumbe wao ni ule ule. Napenda kusema kwamba si vema kuwaziba midomo. Waachwe waseme walichonacho. Wana haki ya kujitetea.

Imesemwa sana chini chini, sasa iachwe iwekwe wazi; kwani kina Rostam na Lowassa wanadai kamati ya Bunge iliyochunguza kashfa ya Richmond iliwaonea, na ilipewa maagizo maalumu; tena nje ya muda wake.

Katika hili, kambi hiyo inamtuhumu Spika wa Bunge moja kwa moja. Si siri kwamba wakati Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, anawasilisha ripoti ya kamati yake bungeni, na kutoa hitimisho lililolazimisha Baraza la Mawaziri kuvunjwa; tayari kambi ya Rostam na Lowassa ilikuwa na mafaili ya ripoti mbili mkononi.

Kwa mujibu wa kambi hiyo, ripoti ya kwanza ya kamati ya Bunge haikuwahusisha kabisa Rostam na Lowassa.

Wanadai kwamba ilipowasilishwa kwa Spika, akaikataa kwa maelezo kwamba Bunge lisingeweza kupokea ripoti ‘isiyokamilika.’

Ripoti ya pili, iliyowahusisha, ndiyo iliyowasilishwa bungeni; na wao wanadai ilitengenezwa ‘nje ya muda’ waliopewa, ikaongezewa vikolezo na ‘majina’ yaliyokusudiwa.

Haya ni madai ya kambi ya Rostam na Lowassa. Na ndipo hapa wanapoanzia kudai kwamba muda unaodaiwa kutumika kukamilisha ‘ripoti’ ya pili haukuwa rasmi!

Tuwaamini Rostam na Lowassa? Tuiamini ripoti ya kamati ya Bunge? Lakini hatuwezi kujibu vema maswali haya hadi kwanza utetezi wa Rostam uwasilishwe na usikilizwe.

Sana sana, kambi ya kina Rostam inatufanya tujiulize leo. Mbona wanataka kujitetea leo wakati walikuwa na muda wa kufanya hivyo na kutoa vielelezo wakati wa mjadala wa ripoti hiyo katika kikao kilichopita? Je, baada ya miezi miwili kupita, jamii itaamini maelezo wanayokuja nayo sasa? Utetezi wao utaaminika kwa Bunge na mamlaka nyingine zinazohusika? Utawasafisha?

Hata hivyo, habari za kuaminika zinasema kwamba muda huu waliopewa, umewasaidia kuwasilisha vema utetezi wao kwa Rais Jakaya Kikwete, kabla ya kuupeleka bungeni.

Ni wazi kwamba rais naye ni mhusika mkuu katika mradi wa Richmond tangu mwanzo, bali hapa katikati mawimbi ya kisiasa yalimzidi nguvu.

Na kwa kuzingatia ukaribu wa watatu hao (Kikwete, Lowassa na Rostam) kisiasa na kifamilia, rais amewasikiliza na kuahidi ‘kusaidia’ kuwasafisha. Kisichojulikana ni kama walidhani njia mwafaka ya kujisafisha ni kupitia bungeni.

Maana, ili wajisafishie bungeni, inabidi Bunge lifike mahali likiri kwamba liliwaonea. Maana yake, kamati ya Bunge ilikosea; hivyo hata mapendekezo iliyotoa, ambayo serikali iliahidi kuyatekeleza yalivyo, yasitishwe.

Je, watawala wako tayari kulidhalilisha Bunge kuwasafisha marafiki wa wakubwa? Lakini wengine wanasema katika siasa za Tanzania lolote linawezekana.

Kwa maana hiyo, yawezekana hata jitihada za sasa za kambi ya Rostam na Lowassa zina baraka kutoka juu. Maana baadhi ya wachunguzi na wafuatiliaji wa mambo wamegundua kuwa katika siku za karibuni, uhusiano kati ya Kikwete na Sitta umechafuka kwa sababu ya Richmond.

Niliandika suala hili kwa kifupi huko nyuma, kwamba sasa Kikwete ameogopa athari ya kujitenga na kina Lowassa na Rostam, kwa hiyo anawatafutia fursa wajisafishe; na kwamba ndiyo maana hata vikao vya CCM Butiama vilikwepa kabisa kuchukua hatua dhidi ya watuhumiwa wa ufisadi.

Hili liliwaudhi baadhi ya wajumbe; na liliwagawa wastaafu kila mtu akajitengenezea sababu ya kutokwenda Butiama.

Walitaka Kikwete achukue msimamo wa Bunge, asikilize maoni na hisia za wananchi juu ya ufisadi.

Alikataa, kwani alishapewa dozi ya ‘siri’ ambayo ilikuwa katika mafaili ya Rostam na Lowassa, akajua akiruhusu chama kiwaguse tu, watakitesa; maana wana mengi ya kuanika.

Lakini hili linawatia watawala katika mtihani mgumu. Yawezekana ni kweli kwamba hoja ya Rostam na Lowassa dhidi ya kamati ya Bunge ni kweli. Na kama ni kweli, hasira za rais dhidi ya Spika zitathibitishwa siku si nyingi.

Maana kama si kamati ya Bunge, Baraza la Mawaziri lisingevunjwa; rais asingeingizwa katika wakati mgumu unaotishia kukigawa chama chake na serikali yake.

Hata hivyo, itabidi achague moja; ama kuwasikiliza kina Rostam na Lowassa au kulisikiliza Bunge. Je, yuko tayari kutosa taasisi za utawala na kuwakumbatia marafiki? Yuko tayari kuliaibisha Bunge na kujenga heshima ya watu binafsi?

Lakini wapo watu wanaodhani kwamba lolote linawezekana. Wanaosema hivi wapo ndani ya mfumo wenyewe, na wanakumbuka kwamba miaka miwili iliyopita, Rais Kikwete alishauriwa na kuonywa kuhusu uhusiano wa serikali yake na Rostam.

Waliomuonya waliona mbali juu ya ukweli ambao sasa ndio umedhihirika. Walitaka ‘amshukuru’ Rostam kwa msaada wake kwao katika kampeni za urais, lakini asimweke karibu mno katika masuala ya utawala wa nchi.

Lakini Rais Kikwete alitaka kuwa muungwana kwa waliomsaidia. Ilifikia wakati, ingawa Rostam hakuwa serikalini, alikuwa akijihusisha moja kwa moja katika mipango ya serikali, hata katika mambo ambayo kimsingi yangefanywa na mawaziri.

Baadhi ya wanahabari wanakumbuka, na kumbukumbu bado zipo, kwamba hata baadhi ya taarifa za mikutano ya viongozi wa serikali na wanahabari kuhusu maamuzi kadhaa ‘mazuri’ kwa serikali zilitoka kwake kwenda vyumba vya habari.

Ajabu, zipo taarifa za baadhi ya mawaziri ambao walifanikiwa kirahisi kumfikia rais kupitia ‘nje ya serikali.’ Mtu mmoja aliyemuona kigogo mmoja wa usalama wa taifa ofisini kwa Rostam, tena wakijadili masuala ya taifa, aliwahi kudokeza kwamba sasa tunakoelekea ‘utabiri wa Nyerere unakaribia kutimia, Rostam ataiweka nchi mfukoni.’

Waliotaka kumtenga Rostam na Kikwete mwanzoni mwa utawala wa Awamu ya Nne, walijua kuwa Rostam ni mfanyabiashara mtafutaji na ana malengo mengi katika siasa, ambayo hawakutaka yamguse rais.

Kwa sababu hiyo, baadhi ya wanaojua vema uhusiano wake na Kikwete, waliokerwa na ukaribu wao huo, wanamuunga mkono mtu yeyote anayeweza kuwatenganisha – kwa masilahi ya taifa.

Sasa leo yanapoibuka masuala nyeti kama haya, ni dhahiri rais anakumbuka ushauri aliopewa akaupuuza. Lakini anaona pia amechelewa kumtema Rostam, maana tayari anajua mengi yanayoweza kumuangusha Kikwete mwenywe. Amfanyeje?

Inaonekana kwamba hata katika sakata hili la Richmond, kama madai ya kina Rostam ni kweli, Sitta alidhamiria kutimiza azima ya kuwatenganisha Rais Kikwete, Rostam na Lowassa, kwa sababu binafsi au hizo hizo zilizotajwa hapo juu. Kwa muda sasa amefanikiwa. Je, utengano huu utadumu hadi lini?

Jambo linalojulikana pande zote ni kwamba Kamati ya Mwakyembe haikukuta faili la usajili wa Richmond; ikahitimisha kwamba Richmond ni kampuni feki.

Lakini wajuzi wa mambo wanajua kwamba faili hilo lilikwapuliwa muda mfupi baada ya kamati ya Bunge kuundwa na kupewa hadidu za rejea.

Bahati nzuri, waliolipoteza wanajulikana, na walidhani wangetumia kumbukumbu hizo kuonyesha udhaifu wa kamati ya Bunge, kuwatetea waliohusishwa na kashfa; jambo ambalo sidhani kama litasaidia sasa.

Haya yote yakiibuka, Bunge litapaswa kujadili na hatimaye kujua nani aliiba faili la usajili wa Richmond, na alitaka kuficha nini!

Bahati nzuri nyingine ni kwamba wenye Richmond wanajulikana. Hata Rostam Azizi anawajua. Lakini sidhani kama kwa ukweli wote wa moyo wake, anaweza kuwataja bungeni, ingawa ana vielelezo vya kuwachoma wengine.

Katika hili, Rostam hana ujasiri wa kunywa sumu! Hawezi. Hatathubutu! Sana sana, atakachofanya ni kujaribu kuonyesha kwamba yeye hayumo.

Lakini lolote atakalosema Rostam sasa, likijadiliwa vema na hadharani, likachunguzwa kwa macho ya akili ya watu makini na wazalendo, litaivua nguo serikali na CCM.

Na kama linaivua nguo CCM ili wananchi wapone, kwanini Rostam anazuiwa kusema? Kwani CCM ni bora kuliko Watanzania? Kwani wizi wa wakubwa ni baraka kwa taifa?

Hii ni fursa nyingine kwa wananchi kujua makubwa zaidi kuhusu Richmond; si kwa kusikia tu hoja ya Rostam, bali kwa kuifanyia pia uchambuzi wa kina na kuona kilichomo na kinachokusudiwa.

**** mambo mawili hapa. Kwanza, hoja ya Rostam ina nia ya kufichua udhaifu fulani ambao anadhani utamsaidia kusafisha jina lake na la Lowassa. Pili, hoja hiyo hiyo itafichua kingine asichokusudia, ambacho kitamvua nguo yeye, Lowassa na Kikwete; CCM na serikali.

Hapo ndipo utamu ulipo; mtego ambao kamati ya CCM inakusudia kuuruka. Hilo la kwanza, linalenga kutoboa matundu kwenye nguzo ya Bunge, kuonyesha udhaifu wa Spika na kamati zake, na kuwajenga waliohusishwa na kashfa ya Richmond.

Spika yupo tayari kudhalilisha Bunge kwa ajili ya kuwajenga washindani wake? Hapa ndipo ulipo woga wa Spika. Je, rais atamtosa Spika katika hili?

Hili la pili ndilo linalomsumbua Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Ndio wasiwasi wa Kamati ya Uongozi ya CCM. Kwa sababu za kisiasa, ni wasiwasi wa Rais Kikwete pia. Sasa akae upande upi? Tusihukumu leo. Tusubiri.

Na inawezekana Rostam akafungwa mdono. Lakini je, Bunge litaikalia hoja yake hadi lini? Je, baada ya CCM kuingilia kati kumfunga mdomo asiliaibishe Bunge na CCM, ambalo Spika anaweza kulitumia kumnyima fursa ya kujieleza, Rostam atakuwa na ujasiri kama wa Dk. Willibrod Slaa, aliyechomoa hoja yake bungeni na kuimwaga hadharani?

Na je, hata akipewa muda atakuwa tayari kusema ukweli wote kuhusu Richmond na kujibu maswali yatokanayo? Kama ana uchungu na uwezo huo, kwa nini aliikwepa Kamati ya Mwakyembe, ndani ya muda iliopewa?

Mbona analeta utetezi wake nje ya muda wa kamati? Au aliamini kwa kuwa upotevu wa mafaili ‘kilikuwa kisiki tosha kwa kamati ya Bunge kuhitimisha kazi yake?’

Na je, anadhani iwapo Bunge litaruhusu hoja yake ijadiliwe kwa uwazi, hayatazuka mengine ambayo wajumbe wa kamati waliyafunika ili ‘mwanaharamu apite’ na ambayo wanaweza kuyaibua leo kudhoofisha kabisa utetezi wa Rostam? Je, yuko tayari kwa anguko la pili? Tunasubiri matokeo.

ansbertn@yahoo.com
+447847922762
www.ngurumo.blogspot.com
 
Rostam amejiandalia anguko la pili?



Ansbert Ngurumo



NILITARAJIA kwamba Kamati ya Uongozi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ingemfunga mdomo Mbunge wa Igunga, Rostam Azizi, ili asijitetee kuhusu alivyohusishwa na kashfa ya Richmond.


Ni kawaida ya kamati hii kuziba watu (wabunge wake) midomo wanapokaribia kuibua mambo mazito yatakayoivua nguo. Lakini yawezekana kwamba katika hili, sasa ndiyo inamzibua mdomo Rostam Azizi.

Rostam Azizi hakuzuka tu. Alijipanga na alidhamiria. Anaijua kamati hiyo, na amekuwa akiitumia kuziba mengine. Alijua analeta mambo mazito dhidi ya Bunge na CCM yake; na alifanya mikakati na wadau wenzake kabla ya kwenda bungeni.

Alijua waziri mkuu angeitisha kikao hicho kumdhibiti. Nimeshangaa kwamba amekubali kudhibitika!

Zaidi ya hayo alijua kwamba Spika wa Bunge, Samuel Sitta, asingeipokea na kuipitisha hoja yake moja kwa moja. Anajua madhara yake. Hata Sitta alijua kuwa Rostam Azizi anaandaa mashambulizi, kwani ni mwendelezo ule ule wa utetezi wa kambi ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, kujitetea na kusafisha majina yao.
Sitta alijua fika kuwa wanaosafisha majina yao ndio hao wanaosababisha kile alichokiita ‘siasa za maji taka,’ za kuibua kashfa zake.

Baadhi yetu tulishaonya kuwa suala hili la Richmond halikuwa la Lowassa na Rostam pekee; na kwamba haliwezi kwisha sasa. Tulisema pia kwamba kama Lowassa asingejiuzulu, tungejua mengi makubwa, iwapo wangeanza kutajana.

Lowassa alitunyima fursa hii. Alikataa kujitetea. Alikataa kusema anachokijua. Akajiuzulu. Naamini sasa kambi yake imejizatiti upya, na hoja zake zitapatikana katika utetezi wa Rostam Azizi.

Hapa katikati yametokea mengi ndani na nje ya CCM, ambayo hata Spika wa Bunge anayajua.

Kwanza, Rostam Azizi na Lowassa wamekuwa wakilalamika kwamba walihusishwa kimakosa. Alianza Lowassa, baadaye wakubwa wakamzima kama kibatari, baada ya kuona wana Monduli wamemwekea zulia jekundu!

Sasa ni zamu ya Rostam Azizi; na ujumbe wao ni ule ule. Napenda kusema kwamba si vema kuwaziba midomo. Waachwe waseme walichonacho. Wana haki ya kujitetea.

Imesemwa sana chini chini, sasa iachwe iwekwe wazi; kwani kina Rostam na Lowassa wanadai kamati ya Bunge iliyochunguza kashfa ya Richmond iliwaonea, na ilipewa maagizo maalumu; tena nje ya muda wake.

Katika hili, kambi hiyo inamtuhumu Spika wa Bunge moja kwa moja. Si siri kwamba wakati Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, anawasilisha ripoti ya kamati yake bungeni, na kutoa hitimisho lililolazimisha Baraza la Mawaziri kuvunjwa; tayari kambi ya Rostam na Lowassa ilikuwa na mafaili ya ripoti mbili mkononi.

Kwa mujibu wa kambi hiyo, ripoti ya kwanza ya kamati ya Bunge haikuwahusisha kabisa Rostam na Lowassa.

Wanadai kwamba ilipowasilishwa kwa Spika, akaikataa kwa maelezo kwamba Bunge lisingeweza kupokea ripoti ‘isiyokamilika.’

Ripoti ya pili, iliyowahusisha, ndiyo iliyowasilishwa bungeni; na wao wanadai ilitengenezwa ‘nje ya muda’ waliopewa, ikaongezewa vikolezo na ‘majina’ yaliyokusudiwa.

Haya ni madai ya kambi ya Rostam na Lowassa. Na ndipo hapa wanapoanzia kudai kwamba muda unaodaiwa kutumika kukamilisha ‘ripoti’ ya pili haukuwa rasmi!

Tuwaamini Rostam na Lowassa? Tuiamini ripoti ya kamati ya Bunge? Lakini hatuwezi kujibu vema maswali haya hadi kwanza utetezi wa Rostam uwasilishwe na usikilizwe.

Sana sana, kambi ya kina Rostam inatufanya tujiulize leo. Mbona wanataka kujitetea leo wakati walikuwa na muda wa kufanya hivyo na kutoa vielelezo wakati wa mjadala wa ripoti hiyo katika kikao kilichopita? Je, baada ya miezi miwili kupita, jamii itaamini maelezo wanayokuja nayo sasa? Utetezi wao utaaminika kwa Bunge na mamlaka nyingine zinazohusika? Utawasafisha?

Hata hivyo, habari za kuaminika zinasema kwamba muda huu waliopewa, umewasaidia kuwasilisha vema utetezi wao kwa Rais Jakaya Kikwete, kabla ya kuupeleka bungeni.

Ni wazi kwamba rais naye ni mhusika mkuu katika mradi wa Richmond tangu mwanzo, bali hapa katikati mawimbi ya kisiasa yalimzidi nguvu.

Na kwa kuzingatia ukaribu wa watatu hao (Kikwete, Lowassa na Rostam) kisiasa na kifamilia, rais amewasikiliza na kuahidi ‘kusaidia’ kuwasafisha. Kisichojulikana ni kama walidhani njia mwafaka ya kujisafisha ni kupitia bungeni.

Maana, ili wajisafishie bungeni, inabidi Bunge lifike mahali likiri kwamba liliwaonea. Maana yake, kamati ya Bunge ilikosea; hivyo hata mapendekezo iliyotoa, ambayo serikali iliahidi kuyatekeleza yalivyo, yasitishwe.

Je, watawala wako tayari kulidhalilisha Bunge kuwasafisha marafiki wa wakubwa? Lakini wengine wanasema katika siasa za Tanzania lolote linawezekana.

Kwa maana hiyo, yawezekana hata jitihada za sasa za kambi ya Rostam na Lowassa zina baraka kutoka juu. Maana baadhi ya wachunguzi na wafuatiliaji wa mambo wamegundua kuwa katika siku za karibuni, uhusiano kati ya Kikwete na Sitta umechafuka kwa sababu ya Richmond.

Niliandika suala hili kwa kifupi huko nyuma, kwamba sasa Kikwete ameogopa athari ya kujitenga na kina Lowassa na Rostam, kwa hiyo anawatafutia fursa wajisafishe; na kwamba ndiyo maana hata vikao vya CCM Butiama vilikwepa kabisa kuchukua hatua dhidi ya watuhumiwa wa ufisadi.

Hili liliwaudhi baadhi ya wajumbe; na liliwagawa wastaafu kila mtu akajitengenezea sababu ya kutokwenda Butiama.

Walitaka Kikwete achukue msimamo wa Bunge, asikilize maoni na hisia za wananchi juu ya ufisadi.

Alikataa, kwani alishapewa dozi ya ‘siri’ ambayo ilikuwa katika mafaili ya Rostam na Lowassa, akajua akiruhusu chama kiwaguse tu, watakitesa; maana wana mengi ya kuanika.

Lakini hili linawatia watawala katika mtihani mgumu. Yawezekana ni kweli kwamba hoja ya Rostam na Lowassa dhidi ya kamati ya Bunge ni kweli. Na kama ni kweli, hasira za rais dhidi ya Spika zitathibitishwa siku si nyingi.

Maana kama si kamati ya Bunge, Baraza la Mawaziri lisingevunjwa; rais asingeingizwa katika wakati mgumu unaotishia kukigawa chama chake na serikali yake.

Hata hivyo, itabidi achague moja; ama kuwasikiliza kina Rostam na Lowassa au kulisikiliza Bunge. Je, yuko tayari kutosa taasisi za utawala na kuwakumbatia marafiki? Yuko tayari kuliaibisha Bunge na kujenga heshima ya watu binafsi?

Lakini wapo watu wanaodhani kwamba lolote linawezekana. Wanaosema hivi wapo ndani ya mfumo wenyewe, na wanakumbuka kwamba miaka miwili iliyopita, Rais Kikwete alishauriwa na kuonywa kuhusu uhusiano wa serikali yake na Rostam.

Waliomuonya waliona mbali juu ya ukweli ambao sasa ndio umedhihirika. Walitaka ‘amshukuru’ Rostam kwa msaada wake kwao katika kampeni za urais, lakini asimweke karibu mno katika masuala ya utawala wa nchi.

Lakini Rais Kikwete alitaka kuwa muungwana kwa waliomsaidia. Ilifikia wakati, ingawa Rostam hakuwa serikalini, alikuwa akijihusisha moja kwa moja katika mipango ya serikali, hata katika mambo ambayo kimsingi yangefanywa na mawaziri.

Baadhi ya wanahabari wanakumbuka, na kumbukumbu bado zipo, kwamba hata baadhi ya taarifa za mikutano ya viongozi wa serikali na wanahabari kuhusu maamuzi kadhaa ‘mazuri’ kwa serikali zilitoka kwake kwenda vyumba vya habari.

Ajabu, zipo taarifa za baadhi ya mawaziri ambao walifanikiwa kirahisi kumfikia rais kupitia ‘nje ya serikali.’ Mtu mmoja aliyemuona kigogo mmoja wa usalama wa taifa ofisini kwa Rostam, tena wakijadili masuala ya taifa, aliwahi kudokeza kwamba sasa tunakoelekea ‘utabiri wa Nyerere unakaribia kutimia, Rostam ataiweka nchi mfukoni.’

Waliotaka kumtenga Rostam na Kikwete mwanzoni mwa utawala wa Awamu ya Nne, walijua kuwa Rostam ni mfanyabiashara mtafutaji na ana malengo mengi katika siasa, ambayo hawakutaka yamguse rais.

Kwa sababu hiyo, baadhi ya wanaojua vema uhusiano wake na Kikwete, waliokerwa na ukaribu wao huo, wanamuunga mkono mtu yeyote anayeweza kuwatenganisha – kwa masilahi ya taifa.

Sasa leo yanapoibuka masuala nyeti kama haya, ni dhahiri rais anakumbuka ushauri aliopewa akaupuuza. Lakini anaona pia amechelewa kumtema Rostam, maana tayari anajua mengi yanayoweza kumuangusha Kikwete mwenywe. Amfanyeje?

Inaonekana kwamba hata katika sakata hili la Richmond, kama madai ya kina Rostam ni kweli, Sitta alidhamiria kutimiza azima ya kuwatenganisha Rais Kikwete, Rostam na Lowassa, kwa sababu binafsi au hizo hizo zilizotajwa hapo juu. Kwa muda sasa amefanikiwa. Je, utengano huu utadumu hadi lini?

Jambo linalojulikana pande zote ni kwamba Kamati ya Mwakyembe haikukuta faili la usajili wa Richmond; ikahitimisha kwamba Richmond ni kampuni feki.

Lakini wajuzi wa mambo wanajua kwamba faili hilo lilikwapuliwa muda mfupi baada ya kamati ya Bunge kuundwa na kupewa hadidu za rejea.

Bahati nzuri, waliolipoteza wanajulikana, na walidhani wangetumia kumbukumbu hizo kuonyesha udhaifu wa kamati ya Bunge, kuwatetea waliohusishwa na kashfa; jambo ambalo sidhani kama litasaidia sasa.

Haya yote yakiibuka, Bunge litapaswa kujadili na hatimaye kujua nani aliiba faili la usajili wa Richmond, na alitaka kuficha nini!

Bahati nzuri nyingine ni kwamba wenye Richmond wanajulikana. Hata Rostam Azizi anawajua. Lakini sidhani kama kwa ukweli wote wa moyo wake, anaweza kuwataja bungeni, ingawa ana vielelezo vya kuwachoma wengine.

Katika hili, Rostam hana ujasiri wa kunywa sumu! Hawezi. Hatathubutu! Sana sana, atakachofanya ni kujaribu kuonyesha kwamba yeye hayumo.

Lakini lolote atakalosema Rostam sasa, likijadiliwa vema na hadharani, likachunguzwa kwa macho ya akili ya watu makini na wazalendo, litaivua nguo serikali na CCM.

Na kama linaivua nguo CCM ili wananchi wapone, kwanini Rostam anazuiwa kusema? Kwani CCM ni bora kuliko Watanzania? Kwani wizi wa wakubwa ni baraka kwa taifa?

Hii ni fursa nyingine kwa wananchi kujua makubwa zaidi kuhusu Richmond; si kwa kusikia tu hoja ya Rostam, bali kwa kuifanyia pia uchambuzi wa kina na kuona kilichomo na kinachokusudiwa.

**** mambo mawili hapa. Kwanza, hoja ya Rostam ina nia ya kufichua udhaifu fulani ambao anadhani utamsaidia kusafisha jina lake na la Lowassa. Pili, hoja hiyo hiyo itafichua kingine asichokusudia, ambacho kitamvua nguo yeye, Lowassa na Kikwete; CCM na serikali.

Hapo ndipo utamu ulipo; mtego ambao kamati ya CCM inakusudia kuuruka. Hilo la kwanza, linalenga kutoboa matundu kwenye nguzo ya Bunge, kuonyesha udhaifu wa Spika na kamati zake, na kuwajenga waliohusishwa na kashfa ya Richmond.

Spika yupo tayari kudhalilisha Bunge kwa ajili ya kuwajenga washindani wake? Hapa ndipo ulipo woga wa Spika. Je, rais atamtosa Spika katika hili?

Hili la pili ndilo linalomsumbua Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Ndio wasiwasi wa Kamati ya Uongozi ya CCM. Kwa sababu za kisiasa, ni wasiwasi wa Rais Kikwete pia. Sasa akae upande upi? Tusihukumu leo. Tusubiri.

Na inawezekana Rostam akafungwa mdono. Lakini je, Bunge litaikalia hoja yake hadi lini? Je, baada ya CCM kuingilia kati kumfunga mdomo asiliaibishe Bunge na CCM, ambalo Spika anaweza kulitumia kumnyima fursa ya kujieleza, Rostam atakuwa na ujasiri kama wa Dk. Willibrod Slaa, aliyechomoa hoja yake bungeni na kuimwaga hadharani?

Na je, hata akipewa muda atakuwa tayari kusema ukweli wote kuhusu Richmond na kujibu maswali yatokanayo? Kama ana uchungu na uwezo huo, kwa nini aliikwepa Kamati ya Mwakyembe, ndani ya muda iliopewa?

Mbona analeta utetezi wake nje ya muda wa kamati? Au aliamini kwa kuwa upotevu wa mafaili ‘kilikuwa kisiki tosha kwa kamati ya Bunge kuhitimisha kazi yake?’

Na je, anadhani iwapo Bunge litaruhusu hoja yake ijadiliwe kwa uwazi, hayatazuka mengine ambayo wajumbe wa kamati waliyafunika ili ‘mwanaharamu apite’ na ambayo wanaweza kuyaibua leo kudhoofisha kabisa utetezi wa Rostam? Je, yuko tayari kwa anguko la pili? Tunasubiri matokeo.

ansbertn@yahoo.com
+447847922762
www.ngurumo.blogspot.com

Kwa kweli mambo bado ni magumu sana Rostam kwa namna yoyote ile ameiweka Serikali mfukoni mwake pamoja na CCM yake Makala hii imenifanya niamini kuwa Rostam alikuwa na ajenda yake kuingia kwenye siasa.
Rostam ndio chimbuko la siasa za maji taka kwani yeye ni muasisi wa kundi la mtandao.
Rostam ndie ataefanikisha anguko la CCM
Rostam ndie aliyefanikisha kumweka JK madarakani na ndiye atakae sababisha JK atoke pale alipo sasa.
Rostam, Rostam, Rostam
Mfanyabiashara mkuwa mwenye hisa 30% Vodacom Tanzania Ltd, yeye kuonana na Rais, Mkuu wa Usalama wa Taifa na top wa serikali wala ahitaji appointment. allaa awaweke yeye walipo halafu aombe apontment uliona wapi?
 
Sokomoko aksante kwa habari hii...

Rostam Aziz kama walivyo watu wenye rangi isiyokuwa nyeusi kama yangu wanakuwa na kujiona wao ni miungu watu....

Alichotaka kuwasilisha bungeni ni nini? Au alitaka kusema CCM ilihitaji pesa 2005 ili ishinde?

Aibu kwa CCM na wahafidhina...
 
Kwa kweli mambo bado ni magumu sana Rostam kwa namna yoyote ile ameiweka Serikali mfukoni mwake pamoja na CCM yake Makala hii imenifanya niamini kuwa Rostam alikuwa na ajenda yake kuingia kwenye siasa.
Rostam ndio chimbuko la siasa za maji taka kwani yeye ni muasisi wa kundi la mtandao.
Rostam ndie ataefanikisha anguko la CCM
Rostam ndie aliyefanikisha kumweka JK madarakani na ndiye atakae sababisha JK atoke pale alipo sasa.
Rostam, Rostam, Rostam
Mfanyabiashara mkuwa mwenye hisa 30% Vodacom Tanzania Ltd, yeye kuonana na Rais, Mkuu wa Usalama wa Taifa na top wa serikali wala ahitaji appointment. allaa awaweke yeye walipo halafu aombe apontment uliona wapi?

Huyu Bwana amekosea kabisa kusoma nyakati!!! He is going down...and Kikweti kaa macho... utajikuta pasipo fikirika akilini mwako..Be worned!!!

Ni nyakati!!

Haziruhusu ufisadi!

Ni nguvu ya umma itakayofanya kweli itimie...!!

Sio serikali... !!

Sio chama fulani!!!

Vyote hivyo vimeshindwa ....porojo nyigi...!!!

Kwa mshangao siku moja asubuhi..alfajari asubuhi kabisa .... !!wananchi wa Tanzania watafanya kianchoitakiwa kifanyika...hapo hakuna kulindana...hapo hakuna ajali ya kisiasa...hapo patakuwa hapana kuwakiliswha misawaada...isiyo na kichwa wala miguu...hapo ni kumekucha...! Sio Rosta, wala Jk wala Lowasa..!!

But all this can be avoided kama Viongozi wetu wataamka na kuacha kuchezea mamlaka tuliyowapa!
 
Lunyungu, maneno gn hayo unayosema? Siumizi kichwa kusema hayo niliyosema, lengo ni kusema yanayotokea hayafai kufanywa na kiongozi mwadilifu hivyo hafai kubaki kiongozi wetu.kwa maneno yako kwa vile hawana lolote na ni spinners tuwaache wafanye watakavyo tusiumize vichwa.maneno ya kukata tamaa! sio wote tuko kama wewe! Mm naamin kuyasema mapungufu ni kati ya hatua za kuleta mabadiliko.acha maneno ya kukatisha watu tamaa. better u keep quite.halafu mm si kaka ni bibi.
 
Back
Top Bottom