Kuna some few interesting things emerging from the content of Rostam's speech. Ni vigumu kuona haya ukiwa biased kwa kumwangilia Rostam badala ya kile alichowasilisha. Kwa mfano:
i) Rostam, pamoja na mambo mengine, anadai kwamba ripoti ya Mwakyembe "imepotosha na kupindisha mno hoja zinazohusu masuala ya fedha, uchumi na biashara". Sasa binafsi naona this is a very serious assertion na ninashangaa inawezekanaje spika hakutaka ufafanuzi kwa jinsi ambavyo kamati ilipotosha. Nafikiri kwamba Rostam alitakiwa atoe maelezo zaidi kuthibitisha jinsi ambavyo kamati ilipotosha mambo ya accounts.
ii) Even more glaring: je, ni kweli kwamba Kamati ya Mwakyembe iliendelea na muda baada ya deadline bila kibali cha spika? Na kama ni kweli iliendelea na muda, kwa au bila kibali cha spika, kwa nini Mwakyembe alikanusha bungeni? Kuna ubaya gani kujua ukweli kuhusu nani mwongo kati ya Mwakyembe na Rostam katika hili?
Bila kuyapatia majibu maswali kama haya, hili la Rostam litaendelea kubaki kuwa ni doa sio tu katika ripoti ya kamati hii bali pia katika utendaji wa bunge.
Kuna kitu cha kuchota kutoka kwenye haya maelezo kama mtu utaamua ku-focus kwenye content ya kile alichokisema kuliko personality ya aliyeyasema!