Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Huyu jamaa nilifikiri ni very smart, lakini anaonekana ni mtupu. Hoja yake iko too personal, apologetic, imekaa kitoto na ni ya kutafuta mashabiki. Yaani hawa ndio wanaotafuna nchi yetu kweli watanzania tumelala!!!
 
Nakukubali Kubenea kwa misimamo yako isiyoyumba katika kutetea na kukemea maovu yanayofanywa na wanasiasa wenye lengo la kuchuma na si kuwahudumia wananchi.Naiona dhamira hiyo katika tahariri yako iliyosheheni maneno ya kushibisha.Naamini wana JF wengi tutakuunga mkono mpaka tuuone mwisho wake.RA anataka aonekane kama si miongoni mwetu,anataka aonekane ni raia 'special',anataka tuamini kitokacho kwake na vyombo vyake lukuki vya habari hataki tuamini asiyoyapenda anayoyaona yanamchafua.Naamini mwanahalisi inafanya kazi kwa kufuata maadili ya uandishi hivyo vitisho vyovyote vinavyotolewa na bwana mkubwa huyu havina lolote.
 
saaaaaaaaaaaaaaaaaafiiii saaaaaaaaaana spika,ilikuwa hakuna maana kumpa nafasi kuzungumza maneno ambayo ni utumbo mtupu,kwanza hayo maelezo ya rostam au kuna wengine pia wameshiriki ila rostam alitakiwa kuwa muwasilishaji maana kuna kauli zinawakilisha nafsi zaidi ya moja wakati muhusika ni yeye.Huyu jamaa hana jipya,angetueleza Richmond ni ya nani?mie naona maelezo yake ni kuwa anakubali richmond ni sehemu yake ila anamlalamikia mwakyembe kwa kutomsubiri arudi safari zake ili hamuhoji,yeye alishajulushwa kwa barua sasa ilikuwa ni jukumu lake kurejea ili atoe ushaidi wake,kuhusu madai yake kuwa kamati ya mwakyembe iliendelea na kazi zaidi ya wiki tatu baada ya muda halisi kuisha ni uzushi,mbona hajathibitisha katika maelezo yake?huyu jamaa anatapatapa tu.
 
Nadhani naweza kuungana na Spika kuwa ilikuwa ni upuuzi kuleta hoja kama hii kwenye bunge. Naona kama Spika alifanya jambo la maana!
kwel kabisa ule ni upuuzi mi wala sijui nini tulizani kuna kitu cha ajabu kumbe ujinga mtupu umeandikwa na washirika wake.
 
Mahakamani jama!!! Kwenye vyombo vya habari nini tena!!! Tuachie mahakama Kubenea au Aziz mkutane huko tutajua nani mkweli!!!

Kubenea: Ati ile kesi yako ni ya Nyumba nd*g* au ni ya Mafisadi? Which is which I'm confused bro.
 
mwanahalisi haliko update au ndio wameshughulika na kujiandaa kwa ajili ya mahakamani?
 
Hivi Rostam ana matatizo ya akili,Kwanini ametutusi watanzania..Rekodi ya kusema ukweli ameitoa wapi,ameshindwa kutuambia wamiliki wa RDc ni kina nani??Je ni mkweli huyu??

Lakini mkuu hii si ilikuwa kazi ya Kamati ya Mwakyembe au?
 
ebwana kubenea najua we ni mpitaji mzuri wa hapa jamvini,,tuko pamoja bro,,hakuna kulala
 
GT sasa njoo utetee msimamo wako na useme maneno yako y Kubenea kuchukua pesa .Kesha sema yeye hana pesa za kumpa Rostam ila anamkaribisha wakutane Mahakani.Mimi nitachanga hata kwa wa kuuza viatu .
 
GT sasa njoo utetee msimamo wako na useme maneno yako y Kubenea kuchukua pesa .Kesha sema yeye hana pesa za kumpa Rostam ila anamkaribisha wakutane Mahakani.Mimi nitachanga hata kwa wa kuuza viatu .

Unasutana mazee, nirimwerewa GT sio kwamba arikuwa anamtete RA isipokuwa alitaka ushahidi.

Akija atakuambia unaona sasa hakuna haja ya kuchanga kwa ajiri ya kesi, kwa maelerezo hayo hamuna kesi hapo! na akifungua kesi atakuwa kajingaanga kwa mafuta yake mwenyewe.
 
Ndio mbunge wa Igunga huyo jamani
Yaani yeye ndiye alionekana anafaa kuwawakilisha wananchi wa Igunga
Kweli kazi ipo, na ndi maana Mkubwa anashindwa kuchagua viongozi bora wa kufanya kazi na anaishilia kuchukua pumba kila siku maana watu wenyewe ndio hawa jamani!!

Huyu ndo mbuge mteule wa Igunga?Tena mjumbe wa kamati kuu ya sisiem!heri awe anatuma mapesa yake yanawawakilisha wananchi.
 
Kuna some few interesting things emerging from the content of Rostam's speech. Ni vigumu kuona haya ukiwa biased kwa kumwangilia Rostam badala ya kile alichowasilisha. Kwa mfano:

i) Rostam, pamoja na mambo mengine, anadai kwamba ripoti ya Mwakyembe "imepotosha na kupindisha mno hoja zinazohusu masuala ya fedha, uchumi na biashara". Sasa binafsi naona this is a very serious assertion na ninashangaa inawezekanaje spika hakutaka ufafanuzi kwa jinsi ambavyo kamati ilipotosha. Nafikiri kwamba Rostam alitakiwa atoe maelezo zaidi kuthibitisha jinsi ambavyo kamati ilipotosha mambo ya accounts.

ii) Even more glaring: je, ni kweli kwamba Kamati ya Mwakyembe iliendelea na muda baada ya deadline bila kibali cha spika? Na kama ni kweli iliendelea na muda, kwa au bila kibali cha spika, kwa nini Mwakyembe alikanusha bungeni? Kuna ubaya gani kujua ukweli kuhusu nani mwongo kati ya Mwakyembe na Rostam katika hili?

Bila kuyapatia majibu maswali kama haya, hili la Rostam litaendelea kubaki kuwa ni doa sio tu katika ripoti ya kamati hii bali pia katika utendaji wa bunge.

Kuna kitu cha kuchota kutoka kwenye haya maelezo kama mtu utaamua ku-focus kwenye content ya kile alichokisema kuliko personality ya aliyeyasema!
 
Duuhhh, sasa huyu Rostam naona anaanza kutuchanganya wananchi..!! Mara anang'ang'ania kusema ukweli, mara anageuka na kushitaki magazeti..!! Mbona anakuwa kigeugeu..?? Mimi naona kapoteza dira kama bunge lilivyokosa mwelekeo..!! Mwanahalisi juuuu, na akileta kujuana kwenye mahakama, wanawane, rusheni habari kama kawaida. Mpaka watanzania wote wafunguke macho. Kula ale, halafu kwenda kupunguza anaona shida.!!..!!..??
 
Back
Top Bottom