mkuu acha double standard, wewe unaita watu mpaka idiots kwa sababu hutaki hoja zao, sasa hapa mbona umegeuka tena?
Idiots ni kipaji na bahati nzuri na wewe una qualify hivyo na wewe unacho... hongera sana..
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
mkuu acha double standard, wewe unaita watu mpaka idiots kwa sababu hutaki hoja zao, sasa hapa mbona umegeuka tena?
Ukisoma post zangu a nyuma nilishawahi kusema kuwa wewe, mtu wa pwani na kibunango ni mtu mmoja na nikatoa hoja zangu ni kwa nini. Kwa hiyo sishangai kwa nini umeingilia ujumbe haraka haraka bila ya kuutafakari.
Ujumbe wangu kwa wewe na hao ndugu zako ni kwamba tunazikaribisha hoja zenu lakini at least ziwe na nguvu na research za kutosha. Lakini kama mkiendelea kukurupuka kama hivi na kuleta hoja za kishabiki tutawa-fire tu kama tulivyomfanyia baba yenu bungeni. Hapa JF haogopwi mtu hapa hasa watu wenye hoja nyepesi kama zenu. Nadhani itabidi kufanya IQ test kabla ya kupewa uwanachama hoja za kusema ccm ndicho chama imara bila ya kutuambia kuwa ni kwa nini ni imara hazina nafasi humu labda kwenye majukwaa.
Wasalimie pwani
Kanyaga twende mkuu Shalom, Jf haijawahi kupuungukiwa na vichwa, bravo mkuu strong point I hope imefika inakopelekwa!
Kwa hiyo post yako hapo juu hiyo IQ test wewe usha fail yaani yako imezidiwa na kidogo na ya kuku.
Kama Masatu = Mtu wa Pwani = Kibunango unahitaji kukumbiziwa mirembe haraka sana as the matter of urgency...
KUTOKA MAKTABA YA JAMBOFORUMS:MICHANGO YA BAADHI YA WANACHAMA KUHUSIANA NA HIYO HABARI:
Pressure on Kikwete to act on graft: Ernest Mpinganjira, Sunday Standard (Kenya) of October 14, 2007.
-----------------------------------------------------------------
Mtanzania: 15th October 2007, 10:53 AM
Huyu mwandishi anatumia ukweli kidogo kufanya madai ambayo
hana data za kuyathibitisha.
Article kama hii angeandika huku kwao wangemaliza mara moja.
Kwasababu anajua hatuna watu wa kukabiliana naye kwa hoja basi anaandika uchafu wowote aliowahi kuusikia karibuni bila kufanya uchunguzi wa kina.
-----------------------------------------------------------------
Halisi: 16th October 2007, 01:35 AM
Pamoja na kukosa baadhi ya facts ama kuwa nazo ambazo hazijafanyiwa kazi, lakini mwandishi anatupa picha moja mbaya sana kwamba kuna PENGO KUBWA KATIKA MEDIA ZA TANZANIA.
1. Media za Tanzania haziwezi moja kwa moja kumuandika Lowasa na Rostam Aziz, jambo ambalo mwandishi hapa kawaandika. Thisday wamejaribu naona wanabanwa sasa na mumeona Nguba katoa statement.
2. Media ya Tanzania imekua na woga na upenzi ambao hausaidii Taifa.
3. Media ya Tanzania haina umoja kwa mambo yanayogusa maslahi ya Taifa, habari ikiandikwa na gazeti moja mengine hayafuatilii kama ilivyo Kenya na Uganda.
--------------------------------------------------------------------------------
Dua: 16th October 2007, 01:45 AM
Brown envelopes zinafanya kazi.
Idiots ni kipaji na bahati nzuri na wewe una qualify hivyo na wewe unacho... hongera sana..
huenda ukawa unazungumza sana kishabiki, kuliko kuzungumza kiuhalisia.
CCM ni chama cha mapinduzi ni chama ambacho kinabadilika kutokana na hali na wakati na sio conservative.
Kunabadilika hasi na Chanya, kwa hili nakubaliana na wewe kuwa CCM inabadilika lakini in a negative way.
suala hili lililetwa bungeni na mbunge wa CCM Shekilengo na unajua ila mkuu akawa anatumia kutisha na mengine lkn chini kwa chini viongozi wakawa wanalizungumza.
Kwanini iwe chini kwa chini? Kama siyo Ufisadi mwingine. Wapinzani walilizungumza kwa uwazi na wanachi walio wengi hata sisi tulioko Sitalike, Mpanda tukalifahamu. Hivyo kwa kulizungumzia chini chini ilikuwa ishara nyingine ya kuficha ufisadi kwa gharama za wananchi.
na nnaamini kama si baraka za CCM hakuna lolote lingekuwa ila walifika pahala wakasema sawa ukweli uwe ukweli na tulifatilieni na aliehusika achukuliwe hatua.
Hii ni pressure kutoka kwa wanachi na siyo baraka za CCM kama unavyotaka kutafanya tuamini. Insingekuwa zomea zomea mikoni JK asingefanya lolote.
sikatai mchango wa upinzani upo tena mkubwa, lakini sio kujilabu na kutaka kuonesha kuwa wabunge wa CCM wamelala na wao ndio pekeee wenye uchungu wa nchi hii na wao pekee ndio waliofichua mambo hayo.
Wabunge wa CCM hawajalaa isipokuwa walikuwa macho kutetea Ufisadi, kwani huoni Zitto alivyotimuliwa bungeni katika scam ya Buzwagi?
ukweli utabakia wazi ndani ya CCM wako wengi kuliko upinzani wenye uchungu na nchi yao na wanaumia kuona wenzao wachache wanaharibu kwa maslahi ya nafsi zao.
Hakuna ukweli wowote, nchi imeingia mikataba mingapi ya kifisadi? Siku zote hizo wabunge wa CCM wenye uchungu si wangeachia ngazi?
CCm ni chama pekeee tanzania chenye utaratibu mzuri na sheria zilizonyooka, sio kama wapinzani wengi wanaganga njaa.
It is just a matter of time kabla hujaona CCM inasambaratika. CCM ilikomaa wakati wa CHama kimoja kwa sababu ya sintofahamu ya Wadanganyika na vilevile mawasiliano yalikuwa hafifu, yaani ili kupata habari za kitaifa mpaka mtu asome mzalendo, uhuru au asikilize Radio Tudanganyane Daima.Sasa hivi kuna namna nyingi ya kupata habari kitu ambacho ni mwiba kwa Sisiemu.
kweli una uchungu wa nchi baada ya kuhimiza wananchi kaitka maendeleo ww unawashawishi ktk mambo ambayo hayaleti faida yeyote ya nchi?
hivi upinzani hawawezi kuleta maendeleo hadi wawe na serikali?
Kuleta maendeleo kuna maana nyingi sana. lakini jukumu kubwa linabakia kuwa la Sirikali kwa sababu wao ni wanakusanya Kodi na kuratibu misaada na mikopo kutoka kwa Donors. Wapinzani wanapokemea ufisadi na kuokoa mamilioni ya shillingi huo ni mchango mkubwa wa maendeleo. Kama EL et al watafikishwa Kizimbani, Tanesco ikaokolewa na mzigo wa kulipa milioni 152 kwa siku gharama ya Umeme itapungua and as a result watu wanaojiri kwa kutegemea umeme wataongezeka. Lakini sifahamu wewe una-define vipi mchango wa kuleta maendeleo ya nchi.
hivi hamuwezi kuwahimiza alau kwa kuanzia wanachama wenu kusoma kwa bidii kujitolea wilaya zao kuboresha maendeleo yote yakiwemo ya elimu?
na kiteto mkishindwa mtasema watanzania hawana mwamko.
Sishangai kwa CCM kushinda Kiteto kwa sababu wanaweza kutumia Emilio Kibaki's style,kwa sababu TUME ni yao na wasimamizi ni wao.
kama kuna haja ya mabadiliko kuiondoa CCM basi mtanzania mbado hajajua ni chama kipi ambacho kinafaa kuiongoza Tanzania.
maana vyote ni vyama ambavyo havijawiva.
Heri kuongozwa na Chama chochote kile kuliko CCM iliyojaa ufisadi na wamewiva katika kubaka uchumi wa Taifa.
nnamalizia ktk vyama vya upinzani wako watu wachache makini na nnawakubali na kuwaheshimu lkn wengi wao wanafata mkumbo tu
Kikwete aanza kujuta
na Charles Mullinda
MTIRIRIKO wa matukio na kauli za Rais Jakaya Kikwete katika kipindi cha wiki moja iliyopita, vinaonyesha kuwa ameanza kujutia hatua ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, kujiuzulu wadhifa wake.
Tofauti na mtizamo wa awali uliokuwa ukionyesha kuwa Kikwete aliridhia kujiuzulu kwa Lowassa baada ya kutajwa kuwa mhusika mkuu katika kashfa ya Richmond, sasa imedhihirika kuwa alilazimika kukubaliana na uamuzi huo kwa vile hakuwa na njia nyingine ya kumnusuru.
Kikwete, ambaye alikuwa Dodoma kwa takriban wiki moja akikabiliana na misukosuko iliyokuwa ikiiandama serikali yake, alikuwa kimya kwa kipindi kirefu na hata kukataa kuonana na baadhi ya maswahiba wake baada ya Lowassa kujiuzulu na yeye kulazimika kulivunja baraza la mawaziri.
Hatua hiyo ya kukataa kuonana na baadhi ya watu wake wa karibu inaelezwa na wafuatiliaji wa mambo kuwa, ilitokana na mshtuko alioupata baada ya Lowassa, ambaye ni swahiba wake mkubwa katika maisha ya kawaida na hata ya kikazi, kuachia ngazi.
Wachambuzi wa masuala ya siasa wameeleza kuwa Kikwete sasa anakabiliwa na mtihani mgumu wa kurejesha umoja na mshikamano ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho yeye ni mwenyekiti wake, kufuatia kuibuka kwa mgawanyiko wa vigogo ndani ya chama hicho, uliosababishwa na kujiuzulu kwa Lowassa.
Tanzania Daima Jumapili ilidokezwa hivi karibuni na watu wa kuaminika kutoka ndani ya chama hicho kuwa kishindo cha kujiuzulu kwa Lowassa kimewagawa vigogo na makada maarufu wa CCM, jambo linalotishia uhai na uimara wake.
Mgawanyiko huo unamgusa pia Rais Kikwete, ambaye hotuba zake mbili alizozitoa baada ya kuapisha baraza lake jipya la mawaziri zinaonyesha kuwa hakubaliani moja kwa moja na ripoti ya Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mchakato wa zabuni ya uzalishaji umeme wa dharura, ulioipa ushindi Kampuni ya Richmond Development ya Marekani, iliyomtia matatani Lowassa.
Hili linapewa uzito na hatua ya Rais Kikwete kutowateua katika baraza lake jipya la mawaziri wajumbe wa Kamati ya Mwakyembe pamoja na wabunge wote wa CCM waliomshambulia Lowassa na wenzake waliotajwa ndani ya ripoti ya kamati hiyo.
Wadadisi wameeleza kuwa hatua hiyo inaonyesha jinsi ambavyo rais hakufurahishwa na namna kamati hiyo ilivyofanya kazi yake.
Sambamba na hayo, hatua ya Rais Kikwete kukiri kuwa kujiuzulu kwa Lowassa kulikuja wakati usiotarajiwa na kumwelezea kama ni kiongozi aliyelitumikia taifa hili kwa ujasiri na uzalendo mkubwa katika kipindi chote cha uongozi wake, licha ya kulazimika kuachia ngazi kwa tuhuma, kunaonyesha jinsi alivyosononeshwa na ulazima wa rafiki yake huyo kujiuzulu.
Wakati wabunge wengi waliojadili ripoti hiyo wakionyesha hasira dhidi ya Lowassa na wengine wakieleza kuwa anapaswa kufikishwa katika vyombo vya sheria na kutolipwa marupurupu ya uwaziri mkuu mstaafu, Rais Kikwete katika hotuba yake kwa taifa kupitia kwa wazee wa Dar es Salaam, alieleza kuwa anaamini Lowassa ameacha alama ya kudumu katika uongozi wake na kwamba yaliyotokea hadi kulazimika kujiuzulu ni ajali katika maisha ya kisiasa.
Kauli nyingine zinazoonyesha jinsi Rais Kikwete alivyosononeka, ni kukiri kuwa Lowassa, mtu aliyeongoza harakati za kuhakikisha kuwa Kikwete anakuwa rais wa nne wa Tanzania mwaka 2005 alikuwa na uhusiano naye kikazi na kimaisha kwa muda mrefu na kwamba kama mambo fulani fulani yangefanyika, basi yaliyotokea yasingefikia kuwa yalivyo.
Wakati hali ikiwa hivyo kwa upande wa Lowassa, hali pia si shwari kwa swahiba wake mwingine, Rostam Aziz, Mbunge wa Igunga, ambaye mbali na kutajwa katika kashfa ya Richmond pamoja na ile ya kuchotwa kwa mabilioni ya fedha kutoka Akaunti ya Malipo ya Nje (EPA) sasa anakabiliwa na kitimoto bungeni anakotakiwa kwenda kuthibitisha au kufuta kauli yake kuwa kamati iliendelea na kazi hata baada ya muda wake wa Desemba 30 kwisha.
Lakini kikubwa kinachoonekana kutishia sifa na heshima aliyonayo Rostam katika jamii ni madai ya kuhusishwa kwake katika kashfa ya EPA ambapo inadaiwa kuwa moja ya kampuni zilizochotewa fedha hizo ni Kagoda anayodaiwa kuimiliki.
Pamoja na kupenda kukaa mbali na vyombo vya habari, Rostam, mwanasiasa mwenye mvuto na ushawishi na pia anayeheshimika ndani ya CCM sasa alazimika kujitokeza mbele ya vyombo vya habari kuzungumzia tuhuma zinazoelekezwa kwake ili kuondoa picha mbaya inayoanza kujengaka dhidi yake.Iwapo kamati iliyoundwa na Rais Kikwete kuchunguza kampuni zilizotajwa kuhusika katika kashfa hiyo itamtaja kuhusika na Kagoda, mbali na kuchafua sifa yake, atachafua pia sifa ya Rais Kikwete, ikizingatiwa kuwa yeye ni mmoja wa wanamtandao walioshiriki kwa karibu kufadhili kampeni za CCM za mwaka 2005.
Kama ilivyokuwa kwa Lowassa, Rostam naye amekuwa akitajwa tajwa sana kuhusika katika kashfa hiyo kutokana na ukwasi wa kutisha alionao, unaodaiwa kutoendana na maelezo ya historia ya alikotokea kibiashara tangu wakati akiwa mfanyabiashara wa ngozi.
Wakati huo huo, fukuto la kashfa ya Richmond bado linaonekana kuwa bichi kutokana na kutofahamika, hasa kwa wamiliki wa kampuni hiyo na nguvu ilizonazo katika kunasa tenda kubwa kubwa za serikali licha ya sifa yake ya kutokuwa na uwezo wa kufanya kazi inazoomba.
Kushindwa kwa kamati teule ya Bunge iliyochunguza upatikanaji wa zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura kwa kampuni hiyo kubaini wamiliki wake, kumezidisha kuwapo wingu la mashaka dhidi ya baadhi ya vigogo kuhusika nayo.
Aidha, baadhi ya wachambuzi na wadadisi wameonyesha mashaka ya wazi kuhusu usiri unaoizunguka Richmond, wakirejea hatua ya Rais Kikwete kulazimika kuchomoa sehemu ya hotuba yake aliyoitoa kwa taifa Desemba mwaka 2006 iliyokuwa ikizungumzia masuala ya Richmond.
Na "nikiahidi kutofanya tena reaction ya JF, Slaa na wengine itakuwaje?!" Kikwete akipata ushauri wako utamvutia sana lakini atakuwa na mawswali kama hayo hapo juu. Atatamani mkutane ili umpe details zaidi na ikiwezekana umfanyie forecasts yatakoyojiri baada ya hapo.
tik tak tik tak.............