Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Kama nilivyokwishasema ingawa ukweli huo unaogopwa, RA ni nguvu kubwa ambayo inahitaji umoja kuishinda. Ukisema RA unamgusa moja kwa moja Lowassa, Karamagi na Vijisenti ambao kwa pamoja wanamiliki sehemu kubwa ya media nchini na wanawaandishi wa habari na wahariri wao! Hivyo, bila kumsaidia Kubenea, bwana mdogo huyo ataenda na maji! Ijabu
 
Hebu tuangalie kilichoandikiwa na lugha iliyotumika:.

Ah kweli "the article is full of sweeping statements". Hii inaashiria kweli iliandikwa kukiwa na some elements of "jazba" ingawa sio kali kama zile "jazba za kipemba". This is no good for- a responsible journalism.
 
Tulisema hapa na tunasema tena Pinda na Spika mmepigwa bao la mwaka na Rostam.

Jamani tutoe pongezi mtu anapofanya jambo kwa kutumia akili ya hali ya juu. Rostam PR yake ni kiboko na kwa kweli ametuweza wote kwa sababu sasa na yeye atakuwa kwenye group la watu wanaoonewa na chama kwa kufungiwa kuongea kama Zitto.

...Yaani hapa nampa Rostam 5, na Bunge 0

Hakuna haja ya kuwapongeza mafisadi! RA apati sifa kwa vile amekuwa na uongo wa kueleza umma wa Tanzania!

Kwa heshima nyingi nakuomba moelex23 ufute kauli yako?
 
Ukifuatilia porojo za ugoni wa Kubenea na jinsi zinavyoungwa mkono na baadhi ya wanaJF, utaelewa kwa nini kila kiongozi sasa anataka kuwa na gazeti lake! Anaongoza RA ambaye mbali na Mtanzania, Rai, The African na Mwananchi (ambako ana shares), ameanzisha msururu wa vijigazeti vya udaku kumsafisha yeye na rafiki yake kipenzi Lowassa. Wanafuatia wengine: Diallo, Seif Khatib, Mbowe n.k. Sababu iko wazi: anzisha uongo wowote ule gazetini kwako, sehemu kubwa ya Watanzania watauamini bila tafakuri. Kubenea "mgoni", wataamini; Spika Sitta "kagushi risiti ya dawa", wataamini; Mwandosya "anataka Urais 2010", wataamini; Lowassa "kaonewa" licha ya kushindwa kujitetea Bungeni, wataamini; Lowassa "kaonewa" kwa kuwa ni "Mmasai" wa Monduli, wataamini; Msabaha "kaonewa" kwa kuwa ni Mwislamu, wataamini; Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge "ameiba" maji ya DAWASCO, wataamini n.k. Tumekosa utamaduni wa uchambuzi, wa kupembua taarifa ili kutenganisha pumba na mchele! Mafisadi wanataka tupoteze lengo, tuache kuwamulika tujishughulishe na porojo za ngono za Kubenea! Mafisadi wamejeruhiwa vibaya na taarifa ya Richmond ambayo imeandikwa kwa ustadi, ufasaha na umakini mkubwa, sasa wanataka tuelekeze macho kwenye porojo na risiti za hospitali na nyumba ndogo ya Spika! Hawataki tuendelee kuiangalia taarifa ya Kamati Teule, wanataka tujadili porojo za kitoto za Mwakyembe kuiba maji ya DAWASCO! Tunaomjua Mwakyembe kwa karibu tunawashangaa wanaoamini taarifa za washikaji wa Lowassa - CEO wa DAWASCO ni ndugu yake na Meneja Uhusiano ni Bibi yake (pengine wawe wameachana leo), na wote tulio kwenye media tunaliojua hilo! Wahariri, waandishi wote wa habari tumsaidie Kubenea kwa nguvu zetu zote ama sivyo kenda na maji huyo! Anapambana na nguvu kubwa! Ijabu
 
Ni afadhali wamfunuwe huo mdomo wake ili abwabwaje! Akifanya hiyo ataweza kumwaga MCHELE KWENYE KUKU WENGI.
Mpka sasa wote watuhumiwa hawajaweza kumwaga huo mchele.Kuna vitu vingine ni vya siri mno kwani wengine serikalini pia nao wamenyamaza kimya kama kwamba wamefungwa kauli.
WEKENI MAMBO WAZI HADHARANI.

AU MNATAKA rais Kikwete atunge tena TUME maalum ya ROSTAM !
 
Hamna lolote hapa,
Wote SPIKA,RA,SYSTEM,MWANAHALISI(Saidi Kubenea na wanzake)lao mmoja.
Kwenye ile Taarifa iliyo chwapishwa kwenye MWANAHALISI la jana hakukua nakitu cha SPIKA kumfungia RA kuzungumza.
i get this wield feeling kwamba bado tunaongopewa huu wote ni mpango hakukua na lolote kwenye ile taarifa ambayo supposely ilikua ya RA kwa SPIKA na BUnge na hayo matusi kwa DK.Mwakyembe hayakua moja kwa moja na kwa kuhesabu yapo kama matatu kama sio 4 na naomba niseme ni YAKUTENGENEZA.

w
Well,kwa mtazamo wangu Jamaa (Aliye juu i mean aliye juu kwenye Uongozi) ameamua kumrudishia HISA ZAKE ROSTAM ndio maan wakaamua kutu fix na hilo Mwanahalisi kama hivyo sivyo basi then we could have RA spred the beans.

MTAZAMO TU....!
 
Ni kitu gani kinachomfanya huyo jamaa (wa ngazi ya juu katika Uongozi) kumrudishia RA hisa zake?
Kuna fununu kwamba huyo RA si raia wa Tanzania kwa hivyo ilikuwaje awe na cheo cha UBUNGE?
Huku kuogopana na na kukingana (kirafiki) ndiko kunakoharibu maendeleo ya Tanzania.

WATAKINGANA MPAKA LINI? AKHERA!
 


Watu wenye fikra kama zako ndiyo wanaochangia kwa kiwango kikubwa kurudisha nyuma mapambano ya kifikra yanayotakiwa kuibadilisha Tanzania. Ni watu wanaowakilisha na kuitetea jamii ya kifisadi iendelee kunyonya jasho la masikini wa Tanzania. Nin watu wanaotumia vibaya uhuru wao wa kutoa mawazo kwa kufifisha mawazo chanya na kurutubisha mawazo hasi.

Katika mazingira ya giza na magumu kama haya, ni jambo la kushukuru kama kuna mtu anajaribu kuwasha hata mshumaa tu ili kupata mwanga japo hafifu. Mwanga huu unatuwezesha kutafuta swichi ya umeme kwa ajili ya mwanga mkali zaidi. Wewe unayewabeza wahariri wanapojaribu kufanya kazi yao, umefanya nini kikubwa katika kupambana na mafisadi zaidi ya wahariri hawa unaowaona hawana ubavu?
[/SIZE][/FONT]
Kama ufisadi ni huo waliofanya RA na Mkapa mimi kwangu nauita ufisadi endelevu kwa maana kuwa wamewekeza ndani ya nchi na watu wamepeta ajira,leo tunafaidika na bank m amabayoinalipa mishahara watoto wa walalahoi mizuri kuliko bank yeyote ndani ya nchi,kiwila mine imetoa ajira mpya zaidi ya mia tatu kwa watanzania,gazeti kubwa nchini la mwananchi limetoa ajira ngapi?habari corporation ilikuwa inakufa nasasakaifufua na wananchi wamepata ajira tena.Tunapinga tabia kama za kina mobutu au sani abacha ambao wanaweka mapesa nje ya tanzania.Kwa nchi yeyote ilioendelea hakuna namna unaweza pata maendeleo bila accumulation of capital.ulaya walitumia ukoloni.sisi tutpata wapi nchi ya kuinyonya,hivyo watu wenye akili kam RA wachukue hio bank kuu na kuwekeza...bravo Rostam Aziz,God bless u.
 
Kama ufisadi ni huo waliofanya RA na Mkapa mimi kwangu nauita ufisadi endelevu kwa maana kuwa wamewekeza ndani ya nchi na watu wamepeta ajira,leo tunafaidika na bank m amabayoinalipa mishahara watoto wa walalahoi mizuri kuliko bank yeyote ndani ya nchi,kiwila mine imetoa ajira mpya zaidi ya mia tatu kwa watanzania,gazeti kubwa nchini la mwananchi limetoa ajira ngapi?habari corporation ilikuwa inakufa nasasakaifufua na wananchi wamepata ajira tena.Tunapinga tabia kama za kina mobutu au sani abacha ambao wanaweka mapesa nje ya tanzania.Kwa nchi yeyote ilioendelea hakuna namna unaweza pata maendeleo bila accumulation of capital.ulaya walitumia ukoloni.sisi tutpata wapi nchi ya kuinyonya,hivyo watu wenye akili kam RA wachukue hio bank kuu na kuwekeza...bravo Rostam Aziz,God bless u.


Fisadi mkubwa,
Ufisadi ni ufisadi tu kwa sababu at the end of the day atakayelipia madhambi aliyoyafanya Mkapa na RA ni wewe, mimi, mjomba wangu, shangazi yangu na wote
ambao wameshindwa kupata matibabu stahili kwa sababu hela zetu zinakwenda kulipia riba kubwa ya madeni ambayo mafisadi hao wenzako wametuingizia. Huwezi ku- accumulate capital kwa migongo ya wakulima na wafanyikazi wa Tanzania. Huo ni uhaini. Na ningekuwa na mamlaka hao mashujaa wako unaowatetea ningewatia wote KITANZI!
 
Na ningekuwa na mamlaka hao mashujaa wako unaowatetea ningewatia wote KITANZI!

Mkuu Jasusi,

Heshima mbele mkuu, tupo ukurasa mmoja hapo!

By the way vipi huko anga zako huko nasikia kuna habari za kifo, vipi hizo?
 
Haya tena, yaelekea Rostam hakuwa na skadi la maelezo ya kuhatarisha maslahi ya CCM au SiriKali... kama isemavyo hapo chini


Rostam ajianika

· Hoja yake bungeni hii hapa
· Kibiliti kitupu, CCM watishiwa nyau
· Aishia kumtkana Dk. Mwakyembe


Na Saed Kubenea


CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kilitishiwa “nyau” na mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, na kikatishika. Alichotaka kukiwasilisha bungeni, hakikuwa na nguvu za kuadhirisha Bunge wala CCM, MwanaHALISI limegundua.

Kwa mujibu wa waraka wa Rostam ambao MwanaHALISI linao, hoja yake ilikuwa dhaifu, haikuwa na nguvu ya kulidhuru Bunge wala CCM.

Vile vile, Rostam ameshindwa kujiokoa na tuhuma kwamba anahusika na kampuni ya Richmond kwa sababu katika sehemu ya maandishi yake, ingawa anakiri kwamba haifahamu, anakiri kuwa alikuwa na maslahi ya kibiashara na kampuni ya Dowans iliyochukua kazi za Richmond iliyoshindwa kazi.

”Mheshimiwa Spika, hakuna hata mfanyakazi mmoja wa Caspian anayeifanyia kazi Dowans. Isipokuwa narejea tena maelezo niliyoyatoa katika mchango wangu kwamba watumishi wa kampuni yangu wanaweza kushirikiana na kampuni yoyoye ambayo kampuni yetu ina nia ya kufanya nayo biashara,” anasema katika hali ya kung’ang’ana.

Anasema, „„Na hilo lilifanyika kama ambavyo pia ni kweli kuwa kampuni ya Caspian ambayo mimi ni Mwenyekiti wake iliruhusu Dowans kutumia anuani ya posta na barua pepe yake kwa sababu tulikuwa tunatarajia kupata kazi ya ukandarasi wa ujenzi kutoka kwao, ambayo ndiyo biashara kuu ya kampuni ya Caspian.”

Anasema, „Mheshimiwa Spika, hiki si kioja kama ambavyo Mheshimiwa Mwakyembe na Kamati Teule alitaka ionekane. Ni taratibu za kawaida kabisa katika shughuli za biashara kuwa na kitu kinachoitwa “hospitality arrangement” yaani kupeana fursa za kutumia baadhi ya huduma baina ya kampuni zinazokusudia kufanya biashara au kupeana kazi.”

Anasema, „Hili linaweza likaonekana ni jambo kubwa la kuzua maswali kwa watu wasio na uelewa wa uendeshaji biashara lakini ni jambo la kawaida kabisa katika ulimwengu wa ushindani wa kibiashara ambapo kila kampuni inatafuta kandarasi kutoka kwa mwenzake.”


Licha ya kushindwa kujinasua, alitumia muda mwingi kumtuhumu Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mkataba kati ya serikali na Richmond, Dk. Harrison Mwakyembe, akimshambulia moja kwa moja na kumuita kwa majina kadhaa yasiyopendeza, na hivyo kuimaliza nguvu hoja yake mwenyewe.

Hoja ya Rostam haikuwasilishwa bungeni baada ya Spika wa Bunge, Samwel Sitta kuikataa kwa maelezo kwamba imejaa matusi na haikuwa na jipya.

Spika Sitta alisema kilichotaka kuwasilishwa na Rostam kilikuwa ni kile kile alichokitoa wakati alipochangia katika mjadala wa ripoti ya Kamati Teule.

Ni kutokana na hali hiyo, Spika Sitta aliamua kuwasilisha mbele ya Kamati ya Uongozi ya Wabunge wa CCM, hoja ya Rostam ili baada ya kuijadili, upatikane ufumbuzi.

Hatimaye, Kamati hiyo iliridhia maoni ya Sitta na kuamuru kuzuia hoja hiyo kuwasilishwa mbele ya Bunge. Uamuzi huo uliyoibua maswali mengi huku baadhi ya wabunge wakiona walinyimwa haki ya kupata kile Rostam alichotaka kuwasilisha.

Hata pale wabunge wa kambi ya upinzani, waliposimama bungeni kuomba mwongo wa Spika ili kupata kile kilichoandikwa na Rostam, wabunge wa CCM walikuja juu.

Anna Abdallah, akitetea uamuzi wa Kamati ya Uongozi ya CCM, alihoji, “ninyi mna maslahi gani na masuala ya wabunge wa CCM?”

Katika maelezo yake, Rostam amekana ushahidi uliotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano, Ikulu, Salva Rweyemamu. Alipohojiwa na Kamati Teule ya Bunge, Salva alisema ni yeye aliyemtambulisha kwa bosi wa Richmond.

Salva, aliyemtaja kama mwenye kampuni ya ushauri katika masuala ya habari (G&S Media Consultancy), amekaririwa katika ripoti ya Kamati ya Bunge akieleza kwamba alitambulishwa kwa Richmond na Rostam.

Rostam ametoa maelezo akisema ushahidi huo hauna nguvu kwa kuwa Salva “alidhani” kuwa yeye (Rostam) ndiye mwenye Richmond, akimaanisha kuwa Salva hakuwa na uhakika wa jambo hilo.

Katika hoja yake iliyozuiwa na CCM kuwasilishwa bungeni kikao kilichomalizika wiki iliyopita, Rostam ameshindwa kutoa vielelezo vya kuthibitisha madai aliyoyatoa kuwa Kamati Teule ya Bunge ya Mwenyekiti Mwakyembe, iliendelea kufanya kazi hata baada ya muda wake kwisha.

Waraka wa Rostam wa kurasa sita, haukueleza kwa namna yoyote ile mazingira ya kuthibitisha kwamba ni kweli kamati hiyo ilikuwa kazini baada ya 31 Desemba, siku iliyopangwa kuwa ya mwisho wa kazi kwa kamati hiyo.

Kitu ambacho Rostam amefanikiwa kukitetea ni kwamba hakuwepo nchini wakati alipoitwa na Kamati Teule, kwani amewasilisha pasipoti yake aliyodai ina mihuri ya Idara ya Uhamiaji inayoonyesha iligongwa wakati akitoka na kuingia nchini aliporejea kutoka likizoni nchini Uingereza.

“…kama nilivyoeleza katika mchango wangu wa maandishi, nilikuwa nje ya nchi kuanzia 17 Desemba, 2007 hadi 3 Januari, 2008. Nawasilisha kwako nakala ya photocopy ya Paspoti yangu ikiwa na mihuri ya Idara ya Uhamiaji inayoonyesha kutoka na kurejea kwangu hapa nchini kama kielelezo kinachothibitisha maelezo yangu hayo,” amesema.

Soma hoja kamili ya Rostam katika uk 12 wa gazeti hili.
 
Kwa mara nyingine tena CCM imeonyesha woga kuumbuka! Walitoka Butiama kwa mikogo, kumbe ni mafisi! ukweli ni vibaka watupu!

Kama kuna watakaodai wao ni CCM asili ni wapinga Ufisadi, basi nao waondoke na kuanzisha chama chao na kuwaachia mafisadi CCM koko!
Mkuu mbona unakosea tena!!!?? CCM mtu safi ni Mmoja tuu!!(Dr.).Na hata wao wanalijua hilo,hao wengine ni kina nani haswa?
**sanasana Mh.Shamsi Vuai Nahodha wa kulee upande wa pili.
 
Kila chama kina taratibu zake na wla sio pinda kama unavyodhani ccm inaongozwa na katiba yake hata jk hawezi kuamua mwenyewe ni kikao ndicho kinachoamua unafikiri ccm ni chama kama vyama vingine mtu yuko BWEJUU atakalo sema ndiyo chama kimesema Mzee mwanakijiji hebu wafafanulie hiyo ibala uliyonakili
 
Huyu Rostam ni gabachori na magabachori wengi wana matatizo ya pesa maana wana msemo wao unaosema "MALI BILA GENDO AWEZI KUWA MALI" kwa maana hiyo nafikiri jk alishauriwa vibaya kumuteua huyo gabachori na ndiyo maana alivyoona tume imeundwa akakimbilia uk kujificha na wala siyo kupuzika jk naomba uwe macho na hawa magabacholi
 
Duh hii kali eti 'hospitality' to share an email account...kweli he must think tanzanians are soooo stupid..ni ufinyu wa mawazo..it takes 20mins to set up ...@dowans.co.tz lol...naona ata kuiba nako wanabahatisha...Anyway ndo siasa zetu hizi...naona sasa tukubali matokeo tuu...
 
Fisadi anapoamua kupambana na washika kalamu nani mshindi??? Tusije kusikia mtu mzima yuko LUGALO???
 
Huyo ameshakuwa fisadi koko. Kuna msemo wa kiswahili usemao mfa maji haachi kutapatapa. Hiyo mitaji aliyoiwekeza Dubai kwa nini asingewekeza bongo? Sasa akianza kuchokoza watu watamuumbua mimi sitaki kumfanyia character assassination fisadi huyu hasha sisi tunahitaji kilichokuwa chetu kama watanzania.
 
We Fisadi Mtoto, mdogo, sijui kuna kitu gani ambacho wame-invest Tanzania ambacho kinaendelea vizuri? yaani mradi wowote ambao mafisadi wameanzisha na uko fresh kabisaa. Hawa jamaa walikuwa na Tamaa mbaya tuu, kila kitu walitaka wao na sasa yanawashinda. Mradi wa Richmond Ovyoo, Bandari ovyoo, Kiwira Ovyoo, na mengineyo. Yaani kwa kifupi ni tamaa tuu. Na hao wahindi waliowatumia hao viongozi wetu wako wapi sasa hivi, si ajabu wanakula kuku na wakati kina Mkapa kila mtu anawaponda sasa hivi. Kuna kitu kinaitwa "Common Sense" ambacho naona hao ndugu zangu hawana, wana tamaa tu.
Back to the Topic. Keep it up Kubenea, at the end the truth will prevail
 
Back
Top Bottom