Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

RA Hafai hafai wal kamwe haitakii hii inchi mema.
Anachokifanya sasa ni kukazana kutafuta fedha za kurudishia alizotumia
2005 na kutafuta za kutumia 2010
 
Yale yale. Kuna mwaka tuliambiwa "nitapambana na rushwa kwa jitihada zangu zote.. Ikaundwa na tume, ilipotoa ripoti, tukaelezwa kuwa kuwachukulia hatua wala rushwa unahitajika ushahidi wa kutosha.
Wanaomtuhumu RA na wengine wajiandae kwa ushahidi, haya maneno maneno ya kila siku, hayatutasaidia sana kwa sababu hayawezi kumtia mtu yeyote hatiani
 
Kwa hili la ufisadi, msimsahau Mheshimiwa sana bw. Manji - Mbunge mtarajiwa wa Temeke 2010.
 
Boma,

Ikiwa haki yangu na usalama wangu hauwezi kulindwa na Serikali yangu kutokana na nguvu za giza ambazo zimejiingiza katika Serikali yetu, unatarajia kuwa nikienda mahakamani haki itatokea?

Mimi ninaushauri uende mahakamani ufungue KESI utapata watu wa kukuunga mkono usiogope UCHAWI kama kweli unaipenda TANZANIA na DECLARATION YAKO ITAKUWA NA MAANA SANA, otherwise, your declaration is null and void
 
boma,

Maneno ya mchungaji yanaweza kuwa ni marudio lakini kwako lakini si kwa kila mtu! So you dont have to be patronising here!

Wazo lingine, wale jamaa wa TPN wako wapi? Hii ndio nafasi yao ya kuitumia hiyo "P" au hao "professionals" zao kama vile wanasheria walioko katika Network na kuanza kufungua kesi. Ila, mahakama is not the only way to put him under pressure or make sure he faces justice.

kuandika tumeandika sana, kusema tumesema cha maana ni mahakamani tu na REV. KISHOKA AMETOA DECLARATION ambayo itakuwa na maana tu kama atakuwa bold kwenda mahakamani badala ya kuandika,
 
Na Padri Privatus Karugendo -MwanaHalisi

NINAANDIKA makala hii kwa uangalifu mkubwa. Kama itakuwa na harufu ya ubaguzi, basi itakuwa ni bahati mbaya na kusema ukweli itakuwa nje ya uwezo wangu.

Mimi ninaamini kwamba binadamu wote ni sawa. Na nimekuwa nikitetea haki za binadamu na kuwatetea Watanzania ambao wamekuwa wakinyoshewa kidole na kuitwa wahamiaji haramu.

Sipendi ubaguzi. Hivyo, ikitokea nikateleza kwenye makala hii, natanguliza kuomba msamaha!

Ninajua baadhi ya watu watashangaa kwa swali ninaloliuliza, maana Rostam Aziz anafahamika sana. Huyu ni tajiri mkubwa, ana makampuni mengi, hata New Habari Corporation ni mali yake.

Ni mfanyabiashara maarufu wa ngozi, ni mwana CCM mkereketwa wa hali ya juu. Ni mtu mwenye ndoa safi asiyefahamika kwa kufukuzana na vimwana (ni wachache sana wa namna yake, hivyo ni lazima ajulikane).

Ni Mbunge wa Igunga, ni rafiki wa karibu sana wa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edwrad Lowassa. Ni rafiki wa Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa; na ni swahiba wa karibu mno wa Rais Jakaya Kikwete, na ana uhusiano mkubwa na watu wengi maarufu nchini.

Kwa umaarufu huo, anafahamika Ngara hadi Mtwara, Bagamoyo hadi Kigoma. Ndiyo maana nimeanza kuwa kusema labda wapo watu watakaoshangaa swali langu.

Hata hivyo, swali langu hilo limechochewa na tamko lake mwenyewe alilotoa wakati anazungumza na waandishi wa habari kujitetea kwa mwaliko wake katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), usharika wa Kinondoni, Dar es Salaam, wiki chache zilizopita.

Kuna baadhi ya matamshi yake ambayo yamenifanya nijiulize, huyu ni nani? Nitayanukuu machache na kuyajadili hapa: “Katika kikundi hicho, wamo ambao hawaridhiki na nafasi za uongozi walizo nazo na ambao wamejenga chuki kwa kudhani na kujiaminisha kuwa labda mimi nilihusika kuwazuilia kujichukulia fursa za ufahari na hadhi wasizostahiki kwa vyeo vyao.”

Yeye ni nani kiasi afikiri watu wanawaza hivyo juu yake? Kwamba yeye anashiriki kupanga ni nafasi gani mtu achukue katika serikali? Yeye ni mshauri wa rais? Au urafiki wake unampatia nafasi ya kuingilia maamuzi mbalimbali katika serkali?

Katika kauli nyingine, anasema: “Nataka niweke jambo moja wazi, kwamba kama (Mchungaji Christopher) Mtikila angekuwa amenituhumu mimi tu, nisingeitisha mkutano huu. Nisingefanya hivyo kwa sababu hastahiki heshima ya kujibiwa na mimi.”

Matamshi kama haya yalinishutua na kunifanya nijiulize, huyu ni mtu gani anayejitukuza kiasi hiki? Ni mfalme wa nchi gani?

Huyu Rostam Aziz, ni nani ambaye watu wengine hawastahiki kujibiwa na yeye? Ni mtu gani huyu mwenye ubaguzi wa kupindukia? Ni mtu gani huyu mwenye dharau inayozidi mipaka?

Kama anabaguliwa Mchungaji Mtikila, ambaye ni kiongozi wa kanisa na chama cha siasa, watu wa kawaida watabaguliwa kiasi gani? Rostam anatoa wapi kiburi hiki? Ni kwa sababu ya utajiri wake? Ni kwa sababu ya ubunge wake?

Inashangaza sana jinsi Watanzania wanavyofumbia macho matukio kama haya. Huu ni wakati wa kusimama na kutetea heshima ya kila Mtanzania. Ni wakati wa kusimama na kusema: “Hapana!”

Tulidhalilishwa enzi zile za wakoloni na biashara ya utumwa, kwa nini tudhalilishwe leo ndani ya Tanzania huru? Huu ni wakati wa kuwakemea watu wa aina ya Rostam Azizi, wanaofikiri ni watu wa pekee kiasi cha kujikweza na kuwabagua baadhi ya watu.

Anatamba na kujigamba kwamba yeye ni mtu safi. Inawezekana mtu mwenye ubaguzi kama huu akawa safi? Mtu mwenye ubaguzi anakiuka haki za binadamu; na mtu yeyote anayekwenda kinyume cha haki za binadamu, hawezi kuwa mtu safi chini ya mbingu.

Hata akiwa na fedha nyingi kiasi cha kuweza kumgawia kila mtu, kama ni mbaguzi, hawezi kuwa safi. Hawezi!

Jambo jingine lililonishangaza sana kwenye tamko lake ni pale aliposema hivi: “ Mimi si miongoni mwa wale walioshindwa kutunza ndoa zao, na kutamani kuishi na wasichana wadogo ambao ni wa umri wa mabinti zao na wajukuu zao.”

Ujumbe huu ulimlenga nani? Na ujumbe huu unahusiana vipi na kitendo chake cha kwenda kujisafisha kule kanisani? Sitarajii kwamba alimlenga Mchungaji Mtikila. Tunamfahamu Mchungaji na mkewe. Si familia yenye kustahili kurushiwa maneno hayo.

Wale wanaomfahamu vizuri Rostam wanafikiri ujumbe kama huu angewapelekea rafiki zake wa karibu sana, anaowafahamu fika, na anaowatetea. Tunawafahamu.

Kwenye tamko lake, anatoa historia yenye uchungu, ambayo sifikiri kama kuna mtu anapenda kuikumbuka:- “Fedha zangu ni pato halali linalotokana na jasho langu kupitia biashara ambayo imekuwa ikiendeshwa na familia yangu tokea mwaka 1852 huko Tabora ilipoanzishwa na babu zangu”.

Wengi tunaifahamu vizuri historia. Ni biashara gani ya mwaka 1852 katika ardhi yetu ilikuwa halali? Tunaifahamu Tabora na historia ya watumwa na biashara ya pembe za ndovu. Ilikuwa biashara chafu kiasi kwamba mtu mchafu pekee ndiye anaweza kujivunia historia ya biashara hiyo.

Haiwezi kuwa tofauti na mikataba ya kidanganyifu ya Karl Peters na wenzake. Haiwezi kuwa tofauti na kile kilichotokea mwaka 1884-1885, kuigawa Afrika vipande vipande na kuitawala.

Ni biashara kama ile iliyoendeshwa na Wahindi, kununua mazao ya babu zetu kwa udanganyifu. Kwetu Kagera, kulikuwa na bakuli kubwa za Wahindi ya kununulia kahawa, ambazo zilipewa jina la “Balimanyaila.”

Maana yake ni kwamba, “itawachukua miaka mingi kugundua hila zetu.” Mabakuli haya yalibondwa bondwa kwenye pembe na kupanuliwa kiasi cha kumeza mabakuli ya kawaida kama mawili au matatu ya kahawa. Hivyo babu zetu waliuza matatu yaliyohesabika kuwa moja! Waliibiwa!

Anajigamba kwenye tamko lake, akisema: “Ili kutendeana haki basi, na kujua ukweli wa mambo natoa changamoto kwa yeyote mwenye ushahidi wa madai ya ufisadi dhidi yangu awasilishe ushahidi huo katika vyombo vya sheria.

Vinginevyo, ni afadhali wafunge midomo yao” Ni wazi kuwa Rostam Aziz anajua jinsi anavyofanya mambo yake kiujanja akishirikiana na Watanzania ‘aliowaweka mfukoni.’

Anasema ana watoto watatu anaowapenda na anapenda kuwalea kwa maadili mazuri. Je, watoto hao wanasomea kwenye Sekondari za Igunga, ambazo ameshiriki kuzijenga? Watoto hao wanashiriki maisha, na kuonja adha wanayoipata watoto wetu wa Kitanzania? Wanaishi wapi watoto hawa?

Je, kwa uzalendo alionao, anawasomesha watoto wake nje ya nchi?
Anasema:- “Kwa kumalizia, napenda Watanzania na waumini wa KKKT, waelewe kuwa nilikwenda katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Usharika wa Kinondoni, kwa mwaliko…”

Mbona inafahamika kwamba aliyekuwa amealikwa rasmi kwenye hafla hiyo ni Lowassa, ambaye baada ya kukataa mwaliko akawapendekezea mtu mwingine (Rostam) kwa vile aliaamini atawachangia fedha nyingi?

Kama, Rostam Aziz anataka tumwamini, mbona hasemi ukweli wote? Inasikitisha sana kwamba tamko la Rostam Azizi limejaa dharau na majigambo kama yale ya rafiki yake, Lowassa.

Inawezekana (hata hivyo, watu wanasema) kwamba tamko hilo liliandaliwa kwa kushauriana. Kila mtu ana namna yake ya kuandika. Hata akijificha namna gani, ni lazima atajifichua kwa kutumia baadhi ya maneno kama vile: “Ili kutendeana haki..”, “Hastahiki heshima..”, “Upande wa pili wa sarafu..” “Nataka niweke jambo moja wazi”, “Hii hali inayoshamiri hivi sasa ya kuviziana, kutungiana uongo na kutakiana mabaya..”.. maneno ambayo mara nyingi yamekuwa yakitumiwa na Lowassa, kwenye hotuba zake. Au Rostam aliibia staili hiyo?

Kimsingi, KKKT hawakuwa na kosa kumwalika Rostam Azizi, wala yeye hakuwa na kosa kwenda kule. Kosa alilisababisha mwenyewe alipoanza kujisifu mbele ya waumini, na kuzungumzia “usafi” wake, huku akiwarushia wengine makombora akiwa kanisani; na kulishukuru kanisa kwa kutambua “usafi” wake. Hapo ndipo mgogoro ulipoanzia.
 
Padri Karugendo,

Hili tulishalisemea toka zamani sana,ukiachilia mbali na hayo yote ya RA ila wewe kama mtu uliyesomea dini,naomba utuambie lego la kanisa kwa watu ambao waovu?Je tunawapokea na kuwakaribia au tunawatenga na kuwafukuza?

suala lingine ni hili la Mtikila,kila mtu yuko huru kuamua ajibizane na nani na sijibizane na nani,Mie nina uwezo wa kuamua tu kwamba sitaki kujibizana na Shalom kwa sababu zangu binafsi tu,au kubeza hoja za Mp,Naamua tu bila kuingiliwa na mtu mwingine.hilo alikuwa sahihi

Kuhusu suala la watu kutoridhika na nafasi zao,lina ukweli ndani yake na lilisababishwa na yeye kuwa karibu na Rais hivyo waliokosa walijua yeye ndiye alimshauri Raisi kuhsu hili.

Maendeleo ya Tanzania yanakuwa magumu kwa sababu ya kukosa sera zilizo bora na hayarudishwi nyuma na watu hata siku moja,ila ili uendelee unahitaji watu,siasa safi na utawala ulio bora.Tumekosa utawal ulio bora has akwa watendaji wengi wa serikali ambao wamaekuwa watumwa wa kukimbia 'workshop' na kuacha kubuni miradi ya maendeleo.

Mie nadhani kama tunaona RA ni mchafu,Yes i once said ni bora mwenye ushahidi aupeleke mahakamani
 
Biashara ya Jamaa ina Harufu ya Damu, Babu zetu watumwa(Roots, Kutakinte!). Inahitaji kususiwa, kuanzia vijijini hakuna kumuuzia ngozi mpaka mjini hakuna kusoma magazeti wala kuzipa tenda kampuni zake za ujenzi na zingine

Kuna mtu anaweza akatupa orodha ya Biashara za RA hapa.? Nimeshaanza "Movement" sifanyi biashara naye tena. Hata katika mtandao hakuna kusoma RAI/Mtanzania. Ile thread ya RA Tznian Axis of Evil ilienda wapi
 
Currently Active Users Viewing This Thread: 12 (5 members and 7 guests)
Halisi, gagnija, isayamwita, msaragambo, Tuandamane

IKO KAZI
 
Padri Karugendo,
Kwa nyakati tofauti nimekuwa nikilalamikia tabia ya baadhi ya waandishi wa habari kupotoka na kuacha kufanya kazi yao kwa kufuata misingi na miiko ya taalum yao. Inawezekana katika kufanya hivyo labda nilikuwa ninarejea makosa yanayofanywa pia na waandika habari (non-professional journalists). Sina hakika kama Padri Karugendo ni mwandika habari au ni mwandishi kweli aliyepitia labda pale Nyegezi au TSJ wakati huo.

Nikirejea katika thread hii ningependa Padri Karugendo atueleze ni nini hasa kilichomsukuma kuandika habari? pili, Je, maudhui katika makala yake yanamnufaisha vipi mwananchi wa kawaida? Ninaomba katika maelezo yake arejee ugomvi uliopo kati ya wamiliki wa Media House mbili za New Habari Corp. na Freemedia. Ninadariki kuyauliza haya kwa sababu kila kukicha nyie baadhi ya waandika habari mnaganga njaa zenu kwa kuleta habari zisizona manufaa kwa wananchi kwa lengo moja tu nalo ni kuwafurahisha mafahari wawili, mna mawazo yaliyo jela, hebu jikomboeni kifikra!!!!
 
Pundamilia,
Unataka tuamini kuwa source ya utajiri wa Rostam ni biashara ya babu zake? Hujamtendea haki Padre!
 
Pundamilia,
Unataka tuamini kuwa source ya utajiri wa Rostam ni biashara ya babu zake? Hujamtendea haki Padre!

Tusubiri kwanza majibu ya Padri Karugendo kama ambavyo nilivyouliza, then utakuwa na solid basis za kuchangia.
Natumaini kuwa umenielewa. Ahsante.
 
Mi nilishasema wazi kuwa Rostam inabidi kama mnamuona mchafu mlete ushahidi na sio kufikirika.

Padre, nikisema sina muda wa kujibizana nawe sina maana ni mbaguzi, naweza kuwa na maana kuwa nakuheshimu sana na sistahili kujibizana nawe. Najua umeenda shule ila uelee ku spin ni kazi ambayo wote tunaiweza.

Kuhusu biashara inawezekana imeanza mwaka 1450 acha aliyoitaja, uhalali au udhalimu wake inabidi ithibitishwe sio kuvamia na ku generalize. Padre umeenda shule vya kutosha kuelewa hilo. Hata Afrika kusini wakati wa ubaguzi kulikuwa na akina JOE SLOVO ambao walikuwa ni wazungu wanaosaidia weusi. Sio kila aliyekuwa muhindi au mwarabu alishiriki biashara chafu.

Kuhusu watu kufikiria kuwa amewakosesha vyeo. Mbona hilo ni so obvious? Hakuna ambaye hajui role ya Rostam kwenye kinyang'anyiro cha kiti cha urais wa Tanzania ndani ya CCM. Cha ajabu ni nini hapo?

Watoto wa Rostam wanasoma wapi?, unataka wasome Igunga?, najua huna watoto ila niambie ndugu zako waliopo mjini, wanawasomesha watoto wao Kanyigo mlikotokea? (sina maana unatoka kanyigo), mengine unatumia tu common sense ingawa sio always ni common.

Kweli kazi ya uandishi wa hizi makala ni rahisi sana. Unaweza kuandika tu ilimradi una spin mambo.

Ngoja nianze kuandika na kuwajibu hawa watanzania wenzetu, labda magazeti yenu yakatae, nitahakikisha natumia magazeti hayo hayo kujibia hoja.

Asanteni

Fairplayer
 
Padri kilicho zahir ya katika makala yako ni Ubaguzi,Chuki na Choyo hakuna hata dai moja ambalo umelitolea ushahidi.Tunahitaji makala zitakazo tuletea faida na sio kupoteza muda.
 
Wafuatao ndio walioteuliwa RASMI KWENYE KAMATI YA UCHAGUZI YA ccm 2005...Hawa hapo chini wanajuwa mengi sana tu...Wakiongozwa na RA...

Kamati ya Uchaguzi CCM

» KAMATI YA KURATIBU KAMPENI ZA CCM KITAIFA By Mike Mushi | Published 08/29/2005 | Kamati ya Uchaguzi CCM |

KAMATI YA KURATIBU KAMPENI ZA CCM KITAIFA

Kwa mujibu wa ibara ndogo ya 4 ya ibara ya 10 ya Katiba ya CCM (Toleo la Mei, 2005), moja kati ya kazi za Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM ni kusimamia Kampeni za Uchaguzi za Chama.

Kwa kuzingatia kuwa Kamati Kuu hufanya kazi zake kwa vikao ambavyo huchukua muda kufanyika, imeamua kuunda Kamati ya Kuratibu Kampeni za CCM Kitaifa ambayo itafanya kazi za siku kwa siku kwa niaba ya Kamati Kuu kwa kipindi chote cha Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005.

Katika kikao chake cha tarehe 29 Juni, 2005, Kamati Kuu iliwateua wafuatao kuwa wajumbe wa Kamati hiyo:-

1.Ndugu Philip J. MangulaMwenyekiti.

2.Brig. Gen (Mst.) Hassan Ngwilizi Mjumbe.

3.Ndugu Saleh Ramadhan FerouzMjumbe.

4.Ndugu Salome Joseph MbatiaMjumbe.

5.Ndugu Jackson MsomeMjumbe.

6.Ndugu Omar Ramadhan MapuriMjumbe.

7.Ndugu Kingunge NgombaleMwiruMjumbe

8.Ndugu Abdulrahman KinanaMjumbe

9.Ndugu Dr. Emmanuel NchimbiMjumbe

10.Ndugu Samia Suluhu HassanMjumbe

11.Ndugu Anna AbdallahMjumbe

12.Ndugu Ali Ameir MohamedMjumbe

13.Ndugu Rostam AzizMjumbe

14.Ndugu Mansoor Yusuf Himid Mjumbe

15.Ndugu Mohamed Aboud MohamedMjumbe

16.Ndugu Edward LowasaMjumbe

17.Ndugu Peter KisumoMjumbe

18.Ndugu Ferdinand RuhindaMjumbe

19.Ndugu Mohamed Abdulaziz Mjumbe

20.Ndugu Leila Nassor KhamisMjumbe

21.Ndugu Yusuf Mushi Mjumbe

22.Ndugu Sam MapandeMjumbe

printer version
 
Kati ya hao 22 hapo juu...Wako wakristo sita tu na mmoja anayeitwa Salome Mbatia keshakufa kiutatanishi(RIP)
Sasa wale waliokuwa wakileta uzushi wao na chuki dhidi ya wachagga...Huyo Yusuph Mushi awe mchagga asiwe mchagga...Na yeye si muislam?
ccm KUNA MAJAMBAZI NA MAGAIDI YANAENDESHA CHAMA CHENU NA MNATAKA KUTULETEA BALAA!

NB:Cha kushangaza ndugu zangu...Hii hapa ni ripoti ya Governor alternates ya ripoti kutoka Benki ya dunia ambapo Abdalah Kigoda alikuwa akijulikana kama Gavana na si Ballali...Hapa hakuhitaji maelelzo kweli?

http://www.worldbank.org/html/extpb/2004/Vol_2/PDF/WB%20Annual%20Report%202004.pdf
 
logopana.gif
Tanzania presidential candidate accused of receiving foreign funding
Dar es Salaam, Tanzania (PANA) - Tanzania's controversial opposition leader, the Reverend Christopher Mtikila alleged Friday that ruling Chama cha Mapinduzi (CCM) presidential candidate Jakaya Kikwete had used funds from Iran to defeat his opponents at the party's recent convention.

The Chairman of the Democratic Party claimed at a press conference that the Iranian government through Tanzanian MP Rostam Aziz, had funded Kikwete's campaign for over 10 years.

The press conference was held ahead of a meeting by eight opposition parties to plan a common strategy against the CCM in Tanzania's October elections.

Mtikila alleged that the Iranian government had set aside a substantial amount to prop presidential candidates in countries where the Asian country has economic interests.

Aziz, a Tanzanian of Iranian extraction is representing Igunga constituency in Tanzania's Union Parliament on the platform of the CCM.

Mtikila did not say how much Aziz had allegedly received from the Iranian government for Kikwete's presidential campaign, but cited Tanzania's uranium deposit as possible motivation for the alleged assistance.

He said the Iranian government could not have given Aziz money for nothing: "they must be harbouring interests in Tanzania."

This is the second time that Aziz, Kikwete's campaign manager, would be accused of securing foreign funds for Kikwete's presidential campaign.

Last April, London-based journal, Africa Confidential claimed that he had been given two million US dollars by the Oman government as campaign funds for Kikwete.

Kikwete, Tanzania's Foreign Affairs and International Co-operation Minister had vowed to sue the journal over the report, but since his nomination as CCM presidential candidate in May, he has said nothing about the report.

The London journal has challenged him to go to court insisting it has overwhelming evidence to back its claims.

There was no immediate reaction to Mtikila's allegations from either Aziz or Kikwete. Dar es Salaam - 16/09/2005
 
Back
Top Bottom