Rostam Aziz: Sina uhusiano wowote, na sipendi kuhusishwa na mtu anayejiita Kigogo

Rostam Aziz: Sina uhusiano wowote, na sipendi kuhusishwa na mtu anayejiita Kigogo

figganigga

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
25,724
Reaction score
55,906
rostam-pic.jpg

Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni za Taifa Group, Rostam Azizi

TAARIFA KWA UMMA

MWENYEKITI Mtendaji wa Kampuni za Taifa Group, Rostam Azizi anapenda kuuhakikishia umma kwamba hana uhusiano wowote na asingependa kuhusishwa kwa namna yoyote na mtu anayejiita Kigogo katika mitandao ya kijamii.

Sambamba na hilo, ndugu Rostam hakubaliani na tuhuma kadha wa kadha zisizo za msingi wala ukweli ambazo huyu bwana amekuwa akizielekeza kwake binafsi na wakati mwingine kwa viongozi wa serikali na Watu wengine kadhaa.

Hatua ya mtu huyo, kufuatilia kazi za kampuni yetu ya Taifa Gas na wakati mwingine kupongeza utendaji wake kazi haipaswi kuonekana kwamba Taifa Gas inafahamiana naye au pengine kumtumia.

Ikumbukwe kwamba, wakati fulani mtu huyo huyo alipata kumjeruhi ndugu Rostam na mke wake wakati ule wa mlipuko wa COVID 19 kwa kuandika taarifa ambazo baadaye zilikuja kubainika hazikuwa na ukweli wowote.

Kwa sababu hiyo basi mwenyekiti wetu ndugu Rostam Azizi, anawasihi Watanzania wanaotumia na kufuatilia mitandao kuzingatia misingi ya utu, uwajibikaji na kuwa makini na yale wanayoandika au yanayoandikwa huko.

Pia kupuuzia uzushi na uongo unaoenezwa mitandaoni.
Mara kadhaa kumekuwa na taarifa katika mitandao za kuua na kufufua watu zinazotengenezwa mithili ya hadithi za kufikirika za Alfu Lela Ulela na wakati mwingine kuwatuhumu watu kwa wizi huku wengine wakitengenezwa waonekane ni malaika.

Haya ni mambo ya kukemea kwa nguvu zetu zote.

Imetolewa na
Ofisi ya Mwenyekiti Mtendaji
Taifa Group
Mei 5, 2023
Plot No. 77, Kipawa Kiwalani
Nyerere Road, P.O. Box 75627
Dar es Salaam Tanzania
 
Rostam anashindwa ongea na Persians wenzake au CIA wamdake Kigogo2014?
 
Huyu kigogo ni mythical person ambaye anatengenezwa na akitakiwa kujulikana atajulikana vizuri tu.

Me nadhani watu wengi wanatumia account yake na ndio maaana inakuwa ngumu kujua specifically ni nani haswa ni yeye.

Ila issue hii ni rahisi sana. Ukitaka kumkamata ni kwa kuwatambua watumiaji wote wa hii account na kuweza kujua wapo wapi na wanafanya nini.
 
Isije kuwa anajisingizia
kwa maana hz taarifa ndio nazisikia kwake🤔
 
Back
Top Bottom