RPC Mara: Kama kuna Mgambo wanaodai wanafanya kazi ya Polisi hao ni Wahalifu tu

RPC Mara: Kama kuna Mgambo wanaodai wanafanya kazi ya Polisi hao ni Wahalifu tu

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara limetoa ufafanuzi juu ya madai ya Polisi kuwatumia Mgambo katika shughuli zao

Awali, Mwanachama wa JamiiForums.com alidai Mgambo hao wamekuwa wakitumiwa usaidia shughuli za Kipolisi wamekuwa hawatendi haki kwa baadhi ya Wananchi pia akadai wanashirikiana na Whalifu wengine kufanya uhalifu.

Hoja ya Mdau hii hapa ~ OCD Bunda fanya uchunguzi wa kina juu ya mgambo wako, wanashirikiana na vibaka

Ufafanuzi wa Kamanda wa Polisi Mkoa (RPC) wa Mara, ACP Salim Morcase:
Siamini katika hayo madai ya huyo Mwananchi, kwa sababu simu yangu ni simu ya wananchi wote, kama angekuwa na jambo angenipigia kama ninavyopigiwa simu na Wananchi wengine.

Tuna weledi wa kutosha, tuna Askari wengi, shughuli zetu zote tunasimamia wenyewe. Yameshatoka maelekezo mbalimbali ya viongozi wetu, Jeshi la Polisi lipo vizuri kiweledi, hatutumii Mgambo yeyote, narudia hatutumii Mgambo yeyote kutekeleza majukumu yetu.

Shughuli zetu tunasimamia wenyewe, hao wanaojiita Magambo wanajipanga kazi wenyewe na ni sehemu ya Wahalifu kama walivyo wahalifu wengine.

Mwananchi yeyote kama ana jambo la ufafanuzi namba yangu ipo hewani, hata hapa ninavyoongea na wewe (Mei 5, 2024) nipo katika ukaguzi wa kata kwa kata, jambo hilo nikilipata na kuwabani wahusika hatua zitachukuliwa
 
RPC kazingua isee labda kama hajaelewa vema blames za watu,nchi nzima kumekuwa na utaratibu RASMI wa kuwatumia mgambo pale ambapo polisi wanakua wako Bize au kuna upungufu,mfano kwenye polisi kata haikosekani walau mgambo mmoja
Mi mwenyewe nashangaa,vituo vingi vina Askari wachache sana kwenye population kubwa ya wananchi,hawawezi kufanya kazi pekee yao ndio maana polisi jamii(community policing division) ni department yenye commissioner kwenye jeshi. Nimeshangaa sana.
 
Polisi wanategemea sana mgambo na polisi jamii kwenye kutekeleza majukumu yao,polisi hawatoshi nashangaa kuwakataa kiholela hivo kama polisi hawatoshi serikali iajiri polisi wa kutosha mgambo wakalime tu
 
Mi mwenyewe nashangaa,vituo vingi vina Askari wachache sana kwenye population kubwa ya wananchi,hawawezi kufanya kazi pekee yao ndio maana polisi jamii ni department yenye commissioner kwenye jeshi. Nimeshangaa sana.
Kuna mgambo kituo cha mabatini
Alikatwa mapanga mchana kweupe barabarani, na kijana aliyeamua kulipa kisasi cha kaka yake kusakiziwa kesi na huyo mgambo bahati mbaya mgambo hakufa ila aliambulia majeraha makubwa sana
Mgambo kwa kushirikiana na polisi wamekuwa majambazi yaliyohalalishwa na watawala
 
Mgambo wakalime au wafanye kazi zingine halali hawa mbwa kwa jina la mgambo wanashiriki dhuluma nyingi sana, kwa raia na ni vibaka wazuri sana kwa kushirikiana na polisi
Polisi wanawatuma mgambo mtaani wanajifanya ma imfomer kumbe wizi mtupu na dhuluma
 
Kuna mgambo kituo cha mabatini
Alikatwa mapanga mchana kweupe barabarani, na kijana aliyeamua kulipa kisasi cha kaka yake kusakiziwa kesi na huyo mgambo bahati mbaya mgambo hakufa ila aliambulia majeraha makubwa sana
Mgambo kwa kushirikiana na polisi wamekuwa majambazi yaliyohalalishwa na watawala
Pia kuna story za mgambo kushirikiana na polisi kutatua matatizo mbalimbali ya kiuhalifu katika eneo flani na kuleta ahueni na amani kwa wananchi kazi ambayo polisi peke yao walishindwa. Kila kitu chenye manufaa hakikosi watumishi chefuchefu.
 
Po
Kuanzia lini polisi akasema ukweli
Mbona huku mtaani kila kituo kina hao migambo wanashirikiana na hao polisi tena mpaka kwenye dori
Polisi wenyewe wengi ni wahuni, sijui CCP wanaenda kufundishwa uhuni!
 
Pia kuna story za mgambo kushirikiana na polisi kutatua matatizo mbalimbali ya kiuhalifu katika eneo flani na kuleta ahueni na amani kwa wananchi kazi ambayo polisi peke yao walishindwa. Kila kitu chenye manufaa hakikosi watumishi chefuchefu.
Nikuambie tu ukweli nilitokea kuwachukia polisi kuanzia mwaka 1967 hawa mbwa ndiyo chanzo cha kifo cha baba yangu mzazi kwa upumbavu wao na tamaa ya pesa ikapelekea baba yangu kusota mahabusu mwaka mzima
So nikimuona polisi najua ni walewale
 
Back
Top Bottom