RPC Mwanza naomba uingilie hili suala ili haki ipatikane

RPC Mwanza naomba uingilie hili suala ili haki ipatikane

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
8,734
Reaction score
5,750
Natoa ombi hili kwako maana wewe umekabidhiwa jukumu hili la kulinda usalama wa raia na mali zao kama kamanda wa mkoa.

Tukio hili baya lilitokea tar 26/10/2019 ndani ya ofisi ya kata ya Kahama wilaya ya ilemela Mkoa wa Mwanza. Watuhumiwa waliteswa na Mwanajeshi na Migambo kwa idhini ya Mtendaji wa kata na Mwenyekiti. Nzengo nzima iliona tukio hili na mmoja wa watuhumiwa akijulikana Omela alifariki.

Sasa imepita miezi mitatu hakuna hatua zozote ambazo zimechukuliwa. Watu waliofanya tukio hili wapo wanatamba mitaani tu.

Mke wa marehemu alifuatilia hadi kwa mkuu wa wilaya. DAS akampigia simu OCD Ilemela amsaidie ili wahusike wakamatwe lakini majibu aliyopata ni kuwa marehemu alikuwa jambazi na alipigwa na wananchi. Pia watafanya uchunguzi.

Kama alikuwa jambazi na alipigwa na wananchi wenye hasira kali tena kwenye mji wa watu.

Sasa kwa sababu kujichukulia sheria mkononi ni kosa hao, waliomuua mtuhumiwa wakamatwe. Mbona RPC mkoa magharibi Unguja alichukua hatua kwa askari aliyemuacha mtuhumiwa auliwe na wananchi wenye hasira kali na nini kinafanya hatua zisichukuliwe huko Mwanza.

N.B: Tanzania ni nchi yenye kufuata misingi ya sheria na utawala bora.Ibara ya katiba ya JMT 13(6) imeweka wazi jinsi haki watuhumiwa zinatakiwa kulindwa. Mahakama ndio chombo pekee cha kuwatia hatiani watuhumiwa.
 
Je marehemu alikua jambazi kweli au la!

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hapa kunamengi yamejificha chini ya kapeti hata mtoa maada hawezi jib ndio maana hata yeye anakomaa kama ni mwizi angelikamatwa na kupelekwa ktk vyombo vya sheria, ila mtoa maada atambue mazingra yanayofaa kumkamata mwiz na kumfikisha mahakamani.

Mfano, mwizi kaja nyumbani kwako kwa lengo la kupambana na wewe kivyovyote ushindwe kujichukulia sheria mkononi kwa kujihami et uogope nikimuua nitaambiwa nilijichukulia sheria mkononi.

Japo mm si mhukumu aliyetangulia mbele za haki ila kama kweli alikuwa mwizi basi mshahara wa dhambi ni mauti hakuna kitu kingine

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hapa kunamengi yamejificha chini ya kapeti hata mtoa maada hawezi jib ndio maana hata yeye anakomaa kama ni mwizi angelikamatwa na kupelekwa ktk vyombo vya sheria, ila mtoa maada atambue mazingra yanayofaa kumkamata mwiz na kumfikisha mahakamani. Mfano, mwizi kaja nyumbani kwako kwa lengo la kupambana na wewe kivyovyote ushindwe kujichukulia sheria mkononi kwa kujihami et uogope nikimuua nitaambiwa nilijichukulia sheria mkononi. japo mm si mhukumu aliyetangulia mbele za haki ila kama kweli alikuwa mwizi basi mshahara wa dhambi ni mauti hakuna kitu kingine

Sent using Jamii Forums mobile app
Yes, ni hvyo tu hamna namna hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe ndio unatakiwa uchunguzwe kweli kweli pengne alikuwa ni mshirika mwenzio hivyo kikosi kimepungukiwa nguvu kazi baada ya yeye kuondoka.

Sent using Jamii Forums mobile app

Kuwa na busara usiandike kitu kujifurahisha. Unajua alikamatwa vipi? Kwa kosa gani? Au unajua mimi nina shughuli gani? Mtu umempigia simu na Mwananchi wa kawaida aje ili kwenye mji wa mtu ili asaidie upelelezi anapelekwa ofisi ya kata anateswa na Mwanajeshi na migambo mpaka anakufa alafu hamna hata walichopata alafu wewe unamhukumu.Wewe ni Mahakama?

Alikamatwa anaiba? Alimatwa na mali ya huyo mwanajeshi? Mimi na zungumzia utendaji kazi kwa maadili na sheria zifuatwe. Alikamatwa kama mtuhumiwa alitakiwa apelekwe polisi kisha upelelezi ufanyike ithibitike kweli amefanya kosa hilo. Kisha apelekwe mahakamani.

Mimi sitetei wezi lakini kwa hili tukio sheria haikufuata mkondo wake. Tumia akili (common sense) yanaweza kukuta hata wewe.
 
Je marehemu alikua jambazi kweli au la!

Sent using Jamii Forums mobile app
Hilo ni suala amabalo mahakama ilipaswa kulithibitisha. Sio kutesa na kuua mtu kwenye ofisi ya kata ili aseme kama ameiba au hajaiba. Alipaswa apelekwe polisi upelelezi ufanyike alafu kama ni jambazi afungwe kwa mujibu wa sheria.sio kumtesa na kumuua.
 
Mkuu hapa kunamengi yamejificha chini ya kapeti hata mtoa maada hawezi jib ndio maana hata yeye anakomaa kama ni mwizi angelikamatwa na kupelekwa ktk vyombo vya sheria, ila mtoa maada atambue mazingra yanayofaa kumkamata mwiz na kumfikisha mahakamani.

Mfano, mwizi kaja nyumbani kwako kwa lengo la kupambana na wewe kivyovyote ushindwe kujichukulia sheria mkononi kwa kujihami et uogope nikimuua nitaambiwa nilijichukulia sheria mkononi.

Japo mm si mhukumu aliyetangulia mbele za haki ila kama kweli alikuwa mwizi basi mshahara wa dhambi ni mauti hakuna kitu kingine

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndugu yangu huyu jamaa hakukamatwa live anaiba. Kuna mtu alikutwa na milango ambayo inasadikiwa ni ya wizi. Yule aliyekamatwa alimtaja marehemu na marehemu alikuja nyumbani kwao. Hapo alikamatwa na Migambo .

Kuna Mwanajeshi alikuwa anadai ameibiwa Tv akasema huyu ndie mwizi wangu akaanza kumpiga akishirikiana na mgambo.Maana ofisi ya kata ilifungwa milango na madilisha. Watuhumiwa walikuwa wanne na bahati mbaya mmoja alifariki. Suala kubwa hapa ni watu kujishukulia sheria mkononi.

Nani anajua kama alikua mwizi? Huyu jamaa aliyefariki mimi simjui. Ila kwa kipigo kile hata kama ni wewe utakubali ili kunusuru maisha yako. Ofisi ya kata inakuwa na Magongo kwa ajiri ya kupigia watu? Chain za baiskeli? Sasa hizi polisi , mahakama na magereza za nini sasa?

Watuhumiwa walikuwa wanne na bahati mbaya huyu jamaa alikufa. Ila mimi siwezi sema alikuwa jambazi au la. Alitakiwa apelekwe polisi upelelezi ufanyike kisha kama ni jambazi apelekwe mahakamani.

Alafu kwanini waseme uongo kuwa alipigwa na wananchi?
 
Ndugu yangu huyu jamaa hakukamatwa live anaiba. Kuna mtu alikutwa na milango ambayo inasadikiwa ni ya wizi. Yule aliyekamatwa alimtaja marehemu na marehemu alikuja nyumbani kwao. Hapo alikamatwa na Migambo . Kuna Mwanajeshi alikuwa anadai ameibiwa Tv akasema huyu ndie mwizi wangu akaanza kumpiga akishirikiana na mgambo.Maana ofisi ya kata ilifungwa milango na madilisha. Watuhumiwa walikuwa wanne na bahati mbaya mmoja alifariki. Suala kubwa hapa ni watu kujishukulia sheria mkononi. Nani anajua kama alikua mwizi? Huyu jamaa aliyefariki mimi simjui. Ila kwa kipigo kile hata kama ni wewe utakubali ili kunusuru maisha yako. Ofisi ya kata inakuwa na Magongo kwa ajiri ya kupigia watu? Chain za baiskeli? Sasa hizi polisi , mahakama na magereza za nini sasa? Watuhumiwa walikuwa wanne na bahati mbaya huyu jamaa alikufa. Ila mimi siwezi sema alikuwa jambazi au la. Alitakiwa apelekwe polisi upelelezi ufanyike kisha kama ni jambazi apelekwe mahakani. Alafu kwa nini waseme uongo kuwa alipigwa na wananchi?
Kwenye awamu hii bora msahau kabisa hakuna lolote litakalofanyika sana sana mtakuwa mnazungushwa akili tu.
 
Kwenye awamu hii bora msahau kabisa hakuna lolote litakalofanyika sana sana mtakuwa mnazungushwa akili tu.
Mbona awamu hii kuna watu wamechukuliwa hatua kwa makosa kama haya. Mfano ni yule askari aliyefukuzwa kazi Zanzibar kwa kuruhusu mtuhumiwa auliwe. Suala la muhimu ni kufuatilia ili hatua zinazostahili zichukuliwe. Tutafuata ngazi zote husika mpaka mwisho ukweli ujulikane. Mpaka mh JPM tutafika.
 
Kuji
Yes, ni hvyo tu hamna namna hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
Kujihami sio kujichukulia sheria mkononi. Kujihami inaruhusiwa kisheria kabisa. Kwa hili tukio kuna ukiukwaji mkubwa wa sheria. Kwanza watuhumiwa walikamatwa na kuwekwa chini ya ulinzi ndani ya ofisi ya mtendaji wa kata. Pili mtendaji wa kata haruhusiwi kuhusika na makosa ya jinai. Tatu ofisi ya kata iligeuzwa kama mahakama na mwenyekiti alikuwepo. Nne watuhumiwa walipigwa na kuteswa ndani ya ofisi ya kata .Mmoja ndio alifariki ,kinachoshangaza ni hiyo kauli eti walipigwa na wananchi wenye hasira kali.
 
Acha kuingizia siasa zako za kipuuzi hapa... Kwan wangapi wamechukuliwa hatua awamu hii.
Endelea kudanganyika kuwa hatua zitachukuliwa labda kuhamishwa kituo tu!!!Wewe ndiye mpuuzi tu ebu niambie wale askari waliokamatwa kwenye kesi ya dhahabu za mamilion wako wapi kweli!!!! kesi yao iliishia wapi kweli!!! Hapo ndipo utajiona Mpuuzi kweli!!!!
 
Mbona awamu hii kuna watu wamechukuliwa hatua kwa makosa kama haya. Mfano ni yule askari aliyefukuzwa kazi Zanzibar kwa kuruhusu mtuhumiwa auliwe. Suala la muhimu ni kufuatilia ili hatua zinazostahili zichukuliwe. Tutafuata ngazi zote husika mpaka mwisho ukweli ujulikane. Mpaka mh JPM tutafika.
Mngekuwa mnamlalamiki wa chama cha Upinzani sawa leo hii haki ingetendeka lakini kwa hili Endeleeni kufatilia likipata ufumbuzi mtani-Tag.
 
Endelea kudanganyika kuwa hatua zitachukuliwa labda kuhamishwa kituo tu!!!Wewe ndiye mpuuzi tu ebu niambie wale askari waliokamatwa kwenye kesi ya dhahabu za mamilion wako wapi kweli!!!! kesi yao iliishia wapi kweli!!! Hapo ndipo utajiona Mpuuzi kweli!!!!
Wewe mpuuzi kwelikweli... Watakavyo mu approach raia wa kawaida na askari ni tofauti... Ila wote panga lazima lipite, hata kama ni kwa njia tofautitofauti.
 
Mngekuwa mnamlalamiki wa chama cha Upinzani sawa leo hii haki ingetendeka lakini kwa hili Endeleeni kufatilia likipata ufumbuzi mtani-Tag.
Kwa hiyo yule trafiki aliyemgonga mume wa yule mama kule kahama na JPM akatoa amri achukuliwe hatua ni wa kenya?
Pia hujui kuwa kama kuna uvunjaji wa sheria na ukiukwaji wa haki za binadamu kama mateso na mauaji hayo yaliyofanyika, mtu anaweza kwenda mahakama kuu kufungua kesi. Na hamna haja ya kukutag inaonekana ndio wale wale.
N.B watanzania sio wajinga .
 
Endelea kudanganyika kuwa hatua zitachukuliwa labda kuhamishwa kituo tu!!!Wewe ndiye mpuuzi tu ebu niambie wale askari waliokamatwa kwenye kesi ya dhahabu za mamilion wako wapi kweli!!!! kesi yao iliishia wapi kweli!!! Hapo ndipo utajiona Mpuuzi kweli!!!!
Kesi ya wizi wa dhahabu undani wake unaujua? Na kesi hiyo inafanana na hili tukio?
 
Kwa hiyo yule trafiki aliyemgonga mume wa yule mama kule kahama na JPM akatoa amri achukuliwe hatua ni wa kenya?
Pia hujui kuwa kama kuna uvunjaji wa sheria na ukiukwaji wa haki za binadamu kama mateso na mauaji hayo yaliyofanyika, mtu anaweza kwenda mahakama kuu kufungua kesi. Na hamna haja ya kukutag inaonekana ndio wale wale.
N.B watanzania sio wajinga .
Endelea kuishi kwa matumaini hiyo ilishatoka hairudi nyuma mkifanikiwa mtani-Tag!!!!
 
Back
Top Bottom