RPC wa Dodoma, Afande Muroto aituhumu JamiiForums kwa kupotosha taarifa za kifo cha Sheikh Rashid Bura

RPC wa Dodoma, Afande Muroto aituhumu JamiiForums kwa kupotosha taarifa za kifo cha Sheikh Rashid Bura

Kumbe kamanda anatoa taarifa za kiuchunguzi sio taarifa za daktari aliyefanya postmortem? Hapa sasa nimeelewa. Taarifa hii ina ukakasi kwa sababu zifuatazo:
  1. Simu zake zote zilizimwa na nani?
  2. Kwanini Muroto asingesubiri taarifa ya Daktari badala ya kuropoka?
  3. Hilo la heart failure aliota au alioteshwa? Alifanya uchunguzi gani kujua kuwa ni heart failure na sio kitu kingine?
  4. Kulikuwa na haja gani ya kutoa tiketi aliyosafiria na kutaja namba ya gari na jina la kampuni inayomiliki gari hilo wakati havina uhusiano na kifo na hakufia ndani ya gari?
  5. Body language ya kamanda Muroto inaonesha wazi kuwa kuna jambo ovu anajaribu kuficha. Kwanini anaongea kwa kutojiamini?
Hapa lazima kuna kitu kiovu kinafichwa na Polisi kwa maslahi ya waovu.
 
Rais Magufuli aliwahi kuwaonya polisi kwa ujumbe huu hapa lakini hawataki kusikia. Sijui wanataka nini?
 
Gama,
Kukaa kimya kwenye Critical thinking ni kuharibu future ya taifa zima kwa ujumla.

Hoja inaweza iwe kweli au si kweli ila ikiumaaa saaana basi kuna namna, huwezi kuwa na taifa lenye vision linalotakiwa kuwa kimya muda woote nakuongea tu yale tu yanayotaka kusikiwa na watu fulani tuuuu.
 
[emoji134]‍♀️[emoji134]‍♀️[emoji134]‍♀️ imekula kwetu kwa kweli. Hakuna rangi tunaacha kuona msimu huu.
 
Hivi hawa wenzetu wamesahau kabisa juu ya uwepo wa Mungu!! Maisha ndio yameishia hapa?? Haya bwana, sisi tupo kama mashahidi wa haya yanayoendelea.
 
Lissu alipigwa risasi huko Dodoma, Lissu mwenyewe anasema siku ya shambulio lake polisi wa kwenye lango la kuingilia hapo kwenye makazi yao hawakuwepo. Sasa kama polisi hawakuwepo hapo kwenye lango na hakuna maelekezo yoyote yanayoeleweka, hapo unapata picha usalama hapo Dodoma upo kwa mtazamo gani kwa baadhi ya watu.
 
HIVI MNAJUA KUWA MUROTO NDIYE RPC BORA WA MAGU. ..

BAADA YA MUROTO NI MAMBOSASA.. . WANAFANYA KAZI NZURI SANA MBELE YA AMIRI JESHI...

SIRRO HAWEZI KUWAFANYA KITU OOTE HAO.. . NA WAO WANA UWEZO WA KUMVIMBIA SIRRO. .. KWA SABABU RAIS YUPO NYUMA YAO.. .
....na wewe upo mbele ya Rais !

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakusoma Pascal, unadhani Mystery amekosea kuliweka hivyo? Sisi ni binadamu kuna wakati huteleza. Tatizo la juzi sio kusifu bali ulimpa sifa asiyestahili bahati mbaya kama ujuavyo naye ana wapinzani wakutosha. Ndio maana wengine tunasema mahaba [yakizidi] hupofusha. Umesema "Tuwe wakweli, mazuri tusifu, mabaya tukosoe", nakubaliana nawe lakini kwenye ule uzi mazuri yale hayakuwa ya yule uliempa pongezi kana kwamba yeye ndiye aliye yaleta (causal attribution).
Kubali tu yaishe, dana dana za nini !?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sijawahi kuona jeshi la kipuuzi kama PT, hasa linapotokea jambo la mauaji ya kutatanisha kama haya ya Bura. Ikiwa serikal ilishatofautiana na CAG na Bura alihudhuria mkutano wake, kuna uwezekano mkubwa kuwa Bura aliuawa kwa sababu za kisiasa kama ilivyotokea kwa Tundu Lissu, Ben Saanane, Azory Gwanda na wahanga wengine ambao wameuawa kimya kimya na miili yao haijawahi kupatikana mpaka leo. Kwa mantiki hii, nawashauri wauaji wawe wanamtuma mtu mweledi kuongea na media, vinginevyo wataumbuka.
Watu wa mtaa wa Ufipa kwa kulazimisha, mpaka wana kera !

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom