TANZIA Rubani wa Ndege iliyotekwa 1982 kushinikiza Nyerere ajiuzulu afariki dunia

TANZIA Rubani wa Ndege iliyotekwa 1982 kushinikiza Nyerere ajiuzulu afariki dunia

Miaka yake ya mwisho akiwa hai alikuwa akishinda pale maeneo ya Pegeout karibu na ilipokuwa bushtrekker. Alikuwa mtu poa sana, akiniona lazima anisalimie.

Walikuwa members wa Gymkhana Club miaka ile, ndio wajanja wa mjini enzi za Nyerere anaondoka anaingia Mwinyi,

Alikuwepo mtu mmoja akifanya kazi habari Maelezo akiitwa Abdallah Ngororo, kila nikifuata bia za wazee Chinese au IFM usiku ninamkuta anapata kinywaji akiwa na hayati Jaji Mapigano, Profesa Shaba na wazee wengine wa mitaa ile.
Nimekukubali wewe ni wa wakati wetu. Umenikumbusha vituko vya Profesa Shaba hasa akisha piga vitu vyake. Mmoja ya wataalamu mahiri wa sekta ya afya kupata kutokea kwa wakati ule
 
Kuna dada mmoha ni mtoto wzo aliitwa Mage Mazula alikuwa mwimbaji wa bendi moja siikumbuki miaka ya 1994.

Kama sikosei ni Tanzanite band.
Alifanya kazi Serena Serengeti...mama yao alifanya kazi Esami
 
Familia ya Mazula ilikuwa familia rafiki sana na familia ya Mwalimu Nyerere.

Watoto wengi wa hii familia ni wasomi wakubwa wa enzi hizo
Issue siyo urafiki na Nyerere. Wakati ule tuliipenda nchi yetu na Nyerere alitulea kama watoto wake bila upendeleo na sisi tukashikamana. Wakati ule hakukuwa na faida au hasara kujuana na Mwalimu. Maendeleo yako darasani au kazini ndiyo yalikupandisha! Mimi nilikuwa mmoja wa watu tuliowapokea Captain Mazula na Mwamwaja pamoja na abiria wote pale uwanja wa ndege wa Stansted. Nakumbuka ule mshikamano uliokuwepo wake huo. RIP Captain Mazula.

Sent from my ONEPLUS A5000 using JamiiForums mobile app
 
Pilot training 200m TZS. Wanyonge piga keleleeeeeee!
 

Attachments

  • VID-20220701-WA0010.mp4
    575.6 KB
Nimekukubali wewe ni wa wakati wetu. Umenikumbusha vituko vya Profesa Shaba hasa akisha piga vitu vyake. Mmoja ya wataalamu mahiri wa sekta ya afya kupata kutokea kwa wakati ule
Alikuwa anakunywa Kilimanjaro Hotel ghorofa ya pili. Akishalewa anayeweza kumtoa sehemu nI marehemu mke wake tu. Alikuwa anaishi pale karibu na Ocean Road ambapo sasa hivi pamejengwa lile ghorofa refu.

Dr Hemish marehemu ni mtoto wake wa kiume, alikuwa na wa kike pia. Kwa sasa Profesa anaishi USA.
 
Mkuu Kamanda Moshi , enzi hizo mambo ya ufundi wa magari ni masingasinga, toka enzi za mashindano ya magari ya East Africa Safari Rally, mzungu Bert Sharkland wa Tanganyika Motors na singasinga Joginder Sing.
P
Safi sana. Umenikumbusha enzi za East Africa Safari RaIly nikosoma nilisubiri nje ya fence ya shule mpaka Shankland apite kwa mbwembwe na gati chafuuu, ila umekosea ni Bert Shankland.
 
Walikuwa ni mtu na kaka yake, na wote brand cars zao zilikuwa ni Volvo, enzi hiyo mawaziri gari zao zikiwa ni Pegeot 504 number zikiwa STC na STD!. Gari za polisi zilikuwa Landrover 109, na escort ya Nyerere ilikuwa Peogeot 404. Benzi yenyewe ya Nyerere naomba nisiseme, ila kulikuwa na mhindi tajiri kwa jina la Lord Rajipar, akaleta Benz kali kuliko ya Rais, S Class 500 miaka hiyo!. alitiwa ndani kwa uhujumu!.
Rip Capt. Mazula umetukumbusha mbali!.
P
Mhhh Paskali hii kesi ya Lord Rajpar inanikumbusha na inanipa majonzi kwani inanigusa sana kutokana na kuwa baba yangu mdogo (RIP) alikuwa mhusika kama mtumishi wa usalama kuishughulikia hii kesi, ilimpa hadi shinikizo.
 
Back
Top Bottom