Rufaa dhidi ya African Lyon: Yanga kupewa alama zake 3 walizocheza dhidi ya African Lyon?

Rufaa dhidi ya African Lyon: Yanga kupewa alama zake 3 walizocheza dhidi ya African Lyon?

NAKUBALIANA NA WEWE ILA MWAKA JANA PIA MADRID ALIONDOLEWA COPA DE LA REY KWA KUMCHEZESHA INVALID PLAYER. KAMA KWELI WAPOKWE TU POINT ILA KAMA HAKUNA MAPOVU YASIENDELEE KUTOKA WATU WAPIGANE UWANJANI.
Naam!

Nadhani Yanga SC sio klabu ya kwanza kuikatia rufaa klabu pinzani.

Umeeleza vyema sana hapo kwa Real Madrid.
Kuenenda kinyume na Kanuni (Deliberately) si uungwana kabisa kwenye mchezo wa soka.

Acha vyombo husika vitoe hukumu! Chochote kitakacho amuliwa kulingana na Taratibu ndicho kitakachokuwa muafaka.
 
Ukiona timu inakimbilia rufaa ujue mpira umewashinda. TFF na hiyo timu yao wanatafuta kila njia watu washinde kwa pointi za mezani. Na hii sio mara ya kwanza walipotunguliwa na Stendi United walikata rufaa sijui iliishia wapi.Hiyo kamati ya masaa 72 huwa inakutana haraka kuamua kama suala lina maslahi na Yanga. Ndanda waliikatia rufaa Mbeya City mzunguko wa kwanza wa ligi kamati bado haijakaa. Kuna muda wa kufikisha pingamizi baada ya hapo kukiwa hamna pingamizi mchezaji anapewa leseni na kuruhusiwa kucheza.TFF na kamati zao itabidi wapindishe sheria kwani uwanjani fadhila hamna ndio maana marefa hawatoi penalti kwa timu fulani kama ilivyokuwa ada msimu uliopita.Mkwara wa Saanya umesaidia kwa kiasi fulani. Tunataka ushindi wa uwanjani ukitaka wa mezani kachezeni table tennis.
 
Ni milion 50 Mkuu
Nimecheka sana baada ya kunisawazisha hapo!

Shukran sana! Kumbe ni vimilioni 50/= si unajua tena vijipesa vyenyewe ni viduchu kiasi kwamba unashindwa kuvitofauyisha na vijipesa vinginevyo. [emoji23]
 
Kabla ya yote tuanze na lililoanza la Hassan Kessy ili huu mchezo usihitaji hasira. Mwambieni kocha wenu Rwanda Amina kwamba simba hatujaribiwi.


Salamu ziwafikie vyura wa jangwani.
 
Mechi hiyo sio ya mwisho!

Kizuri ni kwamba haujamalizana na Azam FC na haujamalizana na '' Mabingwa watetezi na wa kihistoria wa LigiKuu Tanzania bara".

Kwa hivyo endelea kujipa matumaini na faraja ila ndani ya nafsi yako naona moto wa kifuu ukiendelea kushika kasi... [emoji23]
Haituhusu tutawagonga tuu...[emoji350]
 
Mbao nao wafuate 50,000/- zao
Nikueleweshe tu Mkuu!

Hizo mil 50 ni adhabu ambayo haijahusisha mchezaji kuhusika kucheza mchezo wa ligi.

Kama mchezaji amehusika kucheza mchezo wa ligi wa adhabu ya kanuni huukumu na huko kwenye mchezo.

Zingatia 'nature' ya tukio la makosa!..
 
Hizi rufaa nyingine ni kama za Yahaya Jameh, walishindwa nini kufunga magoli uwanjani?
Hivi wangelishinda hiyo rufaa ingekatwa!?
Hata kama ya Yanga SC isingefika bila shaka ya MBAO FC ingefika tu....

Kama sio Mbao FC basi klabu yeyote huko mbeleni ingekata rufaa juu ya tukio hilo.

Kumbuka!

Kanuni ziongoze ligi, huku kila mtu akiwania alama 3. Ukizipata nje ya wigo wa kanuni yakupasa kuziridisha kure ambako zinatakiwa kuenda!
 
Nawaona wa kimataifa wakisogelea nafasi yao ya kila cku
Mkuu! Unakosea kidogo.


Usiseme tunasogea kwenye nafasi yetu.

sema tunarudi katika nafasi pendwa ya wananchi.

Kinachosegea kinaweza kisifike, ila kile kinachorudi ni lazima kiwasili pale kinapo rudi..
.. [emoji23]
 
Mkuu! Unakosea kidogo.


Usiseme tunasogea kwenye nafasi yetu.

sema tunarudi katika nafasi pendwa ya wananchi.

Kinachosegea kinaweza kisifike, ila kile kinachorudi ni lazima kiwasili pale kinapo rudi..
.. [emoji23]
[emoji23] ruvu shooting wanamtuhumu mchezaji wao mmoja kucheza chini ya kiwango!
 
Hata kama ya Yanga SC isingefika bila shaka ya MBAO FC ingefika tu....
Kama sio Mbao FC basi klabu yeyote huko mbeleni ingekata rufaa juu ya tukio hilo.
Kumbuka!
Kanuni ziongoze ligi, huku kila mtu akiwania alama 3. Ukizipata nje ya wigo wa kanuni yakupasa kuziridisha kure ambako zinatakiwa kuenda!
Kwa wenzetu mata nyingi utasikia kupigwa faini timu au wachezaji na hata marefa lakini wanajitahidi sana kuwa matokeo ya uwanjani yasiguswe na mtu!
 
wangeshinda wangeshtk nini?? naona simba wanawapeleka puta na wamebk kudai ushind wa mezan
Hatujawahi kuwa na hofu na wa Matopeni FC Mkuu!

Ile ni baiskeli ya barafu tu, ikitembea sana juani huwa inayeyuka na kupetelea pasipo julikana.

Umesahau yaliyotokea mwishoni mwa mzungu wa kwanza? naam! tarajia mengine.

Narudia tena:

Lengo la timu inapoingia uwanjani ni kupata alama 3.

Endapo kama imekosa alama 3 kwa kuchezewa rafu (kukiukwa kwa kanuni) basi inapasa adhabu ichukie nafasi yake.

Endapo ikipata alama 3. Sioni sababu ya kukata rufaa ikiwa hapo mbeleni itakatiwa tu rufaa na vilabu vinginevyo vishirikio ligi.

Sisi sio wasimamizi wa kanuni, ila pale zinapopindishwa dhidi yetu lazima tuinue vichwa.
 
Haituhusu tutawagonga tuu...[emoji350]
Mkuu bado umelala!?

Tangu lini unawaza kumfunga Yanga SC ([emoji23]). Mara ya mwisho unamfunga "Bingwa wa kihistoria wa LigiKuu Tanzania bara" ilikuwa mwaka gani?

Hebu taja mwaka tu?

Mwaka tu!

Mwaka.
 
Kabla ya yote tuanze na lililoanza la Hassan Kessy ili huu mchezo usihitaji hasira. Mwambieni kocha wenu Rwanda Amina kwamba simba hatujaribiwi.


Salamu ziwafikie vyura wa jangwani.
Sijakuelewa Mkuu!

Hebu jaribu kumuita shabiki mwenzako wa Matopeni FC ajaribu kunielezea hiko ulichokiandika.

Naona umeandika kwa mihemko ya kiwango cha PhD. [emoji23]
 
Nikueleweshe tu Mkuu!

Hizo mil 50 ni adhabu ambayo haijahusisha mchezaji kuhusika kucheza mchezo wa ligi.

Kama mchezaji amehusika kucheza mchezo wa ligi wa adhabu ya kanuni huukumu na huko kwenye mchezo.

Zingatia 'nature' ya tukio la makosa!..

naona na kessy alianza kuchezea yanga kabla ya hukumu kutolewa!
 
Yanga imeshawahi kukatwa points 3 mechi na Coastal union sababu ilimchezesha canavaro akiwa na kadi tatu za njano.. Wakatwe tu
 
Back
Top Bottom