Rufaa dhidi ya African Lyon: Yanga kupewa alama zake 3 walizocheza dhidi ya African Lyon?

Rufaa dhidi ya African Lyon: Yanga kupewa alama zake 3 walizocheza dhidi ya African Lyon?

Imeiadhibu au imejivua lawama......sasa kama wameona kessy hakuwa na uhalali Yanga....na kutozwa milioni...hamsini.....hizo mechi alizocheza kessy Yanga zina uhalali gani.....!!??
Kosa la Yanga kuhusu Kessy ni kupeleka jina la Kessy Caf kama mchezaji wa yanga wakati kessy alikuwa bado hajamaliza mkataba wake simba. ila kessy kaanza kuichezea yanga katika ligi kuu vodacom baada ya kuisha mkataba na simba na alisainishwa mkataba na yanga baada ya mkataba na simba kuisha. Ndio maana yanga wakapigwa faini
 
Mkuu hujui au umesahau? Kessy alizuiliwa kucheza mpaka TFF walipomruhus u kucheza huku suala lake lina shughurikiwa ili kulinda kipaji chake.
Yaani ni shida sana hawa Jamaa! Sidhani kama amekuelewa vyema hapo.

Wao wana bifu na TFF kwenye kila jambo.

Hadi wanapofuka kwenye masuala ya msingi.
 
Yawapasa muwe mnazungumzia zile bao 6. Sio bao 5.

Kila mtu kamfunga mwenzake bao 5 kwa hivyo hakuna la kujiganga kuhusu hilo.

Anzeni kuzungumzia kuhusu bao 6...(Ili muonekane ndio mafanikio yenu makubwa sana dhidi ya Mabingwa wa kihistoria)

Usisahau "hata Real Madrid ameshawahi mfunga Barcelona bao 11 kwa 1"

Mafanikio ya Klabu hauahesabiwi na magoli Mangapi umemfunga mpinzani wako. Kama ingekuwa hivyo,,,, ningekuja na total goal ambazo nimekufunga na kujigamba nazo mida wote.
Ukizungumzia mafanikio vyura fc watasubiri sana kwa mnyama bro we kausha tu endelea kugoogle
 
Kosa la Yanga kuhusu Kessy ni kupeleka jina la Kessy Caf kama mchezaji wa yanga wakati kessy alikuwa bado hajamaliza mkataba wake simba. ila kessy kaanza kuichezea yanga katika ligi kuu vodacom baada ya kuisha mkataba na simba. Ndio maana yanga wakapigwa faini

Sasa kama mkataba wake na simba uliisha na akawa halali kuichezea Yanga...kwenye mechi z ligi kuu.....zinazotambuliwa na CAF.....iweje tena iwe kosa kwa kessy jina lake kupelekwa CAF....hali ya kuwa amekuwa akicheza kwenye ligi hiyo..ambayo CAF wanaitambua na mkataba wake na Simba ulikwa umekwisha.....!!??
 
Huyu jamaa kaanza kushabikia mpira kipindi cha Magu ndio maana ana google badala ya kutoa kumbukumbu kichwani
Umezungumzia kuhusu bao 5,nikakupa facts kuhusu bao 5.

Ungezungumzia kuhusu bao 6,ningekuja na hoja za bao 6.

Kunifunga bao 6 kwa mechi 1 sio historia kubwa sana ukilinganisha kutwaa Ubingwa mara 26 huku wewe umetwaa mara 18.

Haupaswi kujivunia rekodi za kipuuzi. Ndio maana mpaka leo huwezi msikia shabiki wa Real Madrid akijigamba mbele ya Shabiki wa Barcelona kuwa walishawahi wafunga bao 11 kwenye mchezo wa ligi july 1968.
 
Ndani ya saa 24 yatatoka Majibu ya Rufaa iliyokatwa na Mabingwa wa kihistoria wa LigiKuu Tanzania bara yaani Dar es Salaam Young Africans SC.

Kamati hiyo ndiyo yenyejukumu la kuamua kama Yanga inastahili alama mbili au kuendelea kuwa nyuma kwa alama nne kama ilivyokuwa sasa.
Klabu ya Yanga SC inaweza kupunguza gepu la alama 2 kati yake na wale waliowashikia nafasi yao, endapo tu itashinda rufaa yake iliyoikatia timu ya African Lyon, kwa kumchezesha mchezaji Venance Ludovic, huku akiwa hajakamilisha taratibu zake za uhamisho kutoka Mbao FC ya Mwanza.

Meneja wa Yanga Hafidhi, Salehe ameviambia vyombo vya habari, baada ya kupata taaarifa sahihi kuhusiana na mchezaji huyo waliamua kuwasilisha malalamiko yao kwa kamati ya rufaa iliyochini ya TFF, ili haki iweze kutendeka kama ambavyo sheria zinavyosema.

“Tulipata maelekezo ya kutosha na mchezaji huyo aliingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Awadhi Juma, na ndiyo alifunga bao la Lyon kabla ya sisi kusawazisha mchezaji huyo hajakamilisha taratibu zake za usajili kutoka Mbao na hata Mbao wenye wamemkatia rufaa,”amesema Hafidhi Afisa wa Yanga SC.

YANGA inaweza kukomboa pointi mbili ilizopoteza kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya African Lyon baada ya sare ya 1-1 Desemba 23, mwaka huu Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Kamati ya Saa 72, ambayo ndiyo inayosimamia ligi ya Vodacom inakutana leo na moja ya kesi ambazo itazisikiliza na kuzitolea maamuzi ni hiyo ya Yanga dhidi ya Lyon, kuhusiana na kumchezesha mchezaji huyo.

Lyon inadaiwa kukiuka taratibu za kumsajili mchezaji huyo kutoka timu ya Mwanza na rufaa mbili zimegongana mezani, moja ya Yanga na nyingine ya Mbao.

Klabu zote mbili Mbao na Yanga zinapinga Ludivic kuichezea Lyon akiwa mchezaji halali ya Mbao aliyoichezea mzunguko wa kwanza wa Ligi ya Vodacom Tanzania.

Kwa mujibu wa vielelezo vilivyowasilishwa na Mbao, inaonekana kabisa Ludovic alihamia Mbao kimakosa na akatumika kimakosa pia, hivyo Yanga inaweza kushinda rufaa hiyo na kuvuna pointi mbili zaidi.

Katika mchezo huo uliopigwa Desemba 23, kwenye uwanja wa Uhuru, timu hizi zilimaliza dakika 90, zikitoka sare kwa kufungana bao 1-1, na kupoteza malengo ya Yanga katika kuwafukuzia wapinzani wao Simba ambao walikuwa wanapishana kwa pointi mbili.

Endapo Yanga itashinda rufaa hiyo basi itafikisha pointi 42 na kupunguza gepu la pointi kati yao na Simba kutoka nne hadi mbili kama ilivyokuwa awali.
c69c4496bc50d5e4111d6912e5538140.jpg

-nawasilisha
Ndiyo maana sishabikii mpira Wa bongo,unachezwa mezani sii uwanjani
 
Kuna moja ya Kamati mule ndani inaongozwa na kiongozi wenu wa Klabu.

Hujawahi kusikia tukilalamika.
wewe uko wapi kwani maana naona kuna wekundu usoni mwako au ndio wale watz %
 
Poleni sana nyie ndala fc kushangilia kupata point 2 za mezani kwa ajili ya mchezaji wa Africa Lyon na mnajifanya kana kwamba mnasahau issue ya hasani kessi basi subirini nyie mpokwe point zote ambazo hasani kessi alicheza na zile alizokaa bench muone mtakuwa nafasi ya ngapi? Mnaposhangilia ya Ludovic mkumbuke na ya kessi pia
 
Sasa kama mkataba wake na simba uliisha na akawa halali kuichezea Yanga...kwenye mechi z ligi kuu.....zinazotambuliwa na CAF.....iweje tena iwe kosa kwa kessy jina lake kupelekwa CAF....hali ya kuwa amekuwa akicheza kwenye ligi hiyo..ambayo CAF wanaitambua na mkataba wake na Simba ulikwa umekwisha.....!!??
Mkuu hukuelewa, soma tena kwa utulivu
Yanga walipeleka jina kabla ya hata kumsainisha mkataba, wamemsainisha baada ya kessy kumalizika kwa mkataba wake simba.
 
Hili Swali Hakuna Mshabiki Wa Yanga Yoyote Anayeweza Kulijibu....
Kuna utofauti mkubwa sana kwenye hili:-



1. Kuingia mkataba na mchezaji ambaye hajamaliza mkataba na muajili wake aa awali (Muajili ambaye mchezaji hajafikia naye makubaliano ya kuvunja mkataba)
-Hoja ambayo imefikiwa muafaka wa malipo ya Mil 50.

2. Kuutumikia mkataba mpya ili hali ule wa zamani umefikia ukomo.
Kumbuka Kessy alianza kucheza baada ya kumapizika kwa muda wa ule mkataba wake wa awali
 
Hata hoja imeletwa kishabiki sana.
Mkuu

Hoja imeletwa kama taarifa kwa Mashabiki, wapenzi na wanachama wa Mabingwa watetezi wa kihistoria wa LigiKuu Tanzania bara yaani Dar es Salaam Young Africans SC.

Haijaja hapa ijadiliwe. Huu mjadala ni wa ziada tu.

Btw! Hakuna uzi wa kimichezo (haswa wa simba na yanga unao weza kuletwa bila kuwa na chembechembe za kishabiki.
 
Ujinga tu kutegemea za mezani
Ni kweli ukisemacho.

Ila hata wao walitaka ubingwa wa mezani baada ya kutaka Yanga SC ipunguzwe alama kwenye sakata la Kessy.

Si unakumbuka Mkuu?
( Maajabu ya Aden Rage)
 
Yawapasa muwe mnazungumzia zile bao 6. Sio bao 5.

Kila mtu kamfunga mwenzake bao 5 kwa hivyo hakuna la kujiganga kuhusu hilo.

Anzeni kuzungumzia kuhusu bao 6...(Ili muonekane ndio mafanikio yenu makubwa sana dhidi ya Mabingwa wa kihistoria)

Usisahau "hata Real Madrid ameshawahi mfunga Barcelona bao 11 kwa 1"

Mafanikio ya Klabu hauahesabiwi na magoli Mangapi umemfunga mpinzani wako. Kama ingekuwa hivyo,,,, ningekuja na total goal ambazo nimekufunga na kujigamba nazo mida wote.
Very logical
 
Poleni sana nyie ndala fc kushangilia kupata point 2 za mezani kwa ajili ya mchezaji wa Africa Lyon na mnajifanya kana kwamba mnasahau issue ya hasani kessi basi subirini nyie mpokwe point zote ambazo hasani kessi alicheza na zile alizokaa bench muone mtakuwa nafasi ya ngapi? Mnaposhangilia ya Ludovic mkumbuke na ya kessi pia

Mkuu unajisumbua bure....

Hawawezi kupokwa point hata moja bali wao ndio watakao ongezewa point hata kama ni za uzushi....kwa kuwa TFF ndio wameshaamua Yanga....awe bingwa ligi wa miaka yote....

Ndio maana haishangazi kukuta katika mechi ya Yanga mwamuzi anafungiwa kwa maamuzi mabovu.....huku waao wakiendelea kupeta....
 
Kuna utofauti mkubwa sana kwenye hili:-



1. Kuingia mkataba na mchezaji ambaye hajamaliza mkataba na muajili wake aa awali (Muajili ambaye mchezaji hajafikia naye makubaliano ya kuvunja mkataba)
-Hoja ambayo imefikiwa muafaka wa malipo ya Mil 50.

2. Kuutumikia mkataba mpya ili hali ule wa zamani umefikia ukomo.

Kumbuka Kessy alianza kucheza baada ya kumapizika kwa muda wa ule mkataba wake wa awali

HOMEWORK PLZ
 
YANGA KUVUNA PONTI ZA CHEE LEO KAMATI YA SAA 72
Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
YANGA inaweza kukomboa pointi mbili ilizopoteza kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya African Lyon baada ya sare ya 1-1 Desemba 23, mwaka huu Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Bin Zubeiry Sports - Online inafahamu kwamba Kamati ya Saa 72 ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inatarajiwa kukutana leo kujadili taarifa mbalimbali na kupitia rufaa – huku Yanga wakijiweka mkao wa kuvuna pointi za mezani.
Hiyo inafuatia rufaa yao waliyomkatia mchezaji wa Lyon, Venence Joseph Ludovic aliyefunga bao la Lyon katika sare hiyo ambaye inadaiwa ni mchezaji halali wa Mbao FC ya Mwanza.
MECHI%2B1.jpg

Venence Ludovic alichezea Mbao FC mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu

African Lyon inadaiwa kukiuka taratibu za kumsajili mchezaji huyo kutoka timu ya Mwanza na rufaa mbili zimegongana mezani Bodi, moja ya Yanga na nyingine ya Mbao.
Zote, Mbao na Yanga zinapinga Ludivic kuichezea Lyon akiwa mchezaji halali ya Mwanza ambayo aliichezea mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Kwa mujibu wa vielelezo vilivyowasilishwa na Mbao, inaonekana kabisa Ludovic alihamia Mbao kimakosa na akatumika kimakosa pia, hivyo Yanga inaweza kushinda rufaa hiyo na kuvuna pointi mbili zaidi.
Kamati pia leo itapitia Rufaa ya Ndanda FC dhidi ya wachezaji wa Simba kutoka Ghana, kipa Daniel Agyei na kiungo James Kotei ambao wanadaiwa kucheza mechi baina ya timu hizo wakiwa hawana vibali vya kufanya kazi nchini.
Kwa sasa inashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa pointi zake 40 baada ya kucheza mechi 18, nyuma ya Simba SC yenye pointi 44 za mechi 18 pia.
 
Back
Top Bottom