TANZIA Ruge Mutahaba afariki Dunia! Azikwa kishujaa kwao Kabale, Bukoba

Hahaaaaa Mayala, unachambua Kila kitu kutoka uchumi, siasa, jamii, sayansi etc.
 
Kwa la peponi HAKUNA ajuaye mkuu MAYALLA
 

Mkuu pamoja na hayo. Nadhani wewe sio mgeni wa Sheria na Utaratibu wa Kanisa Katoliki.
 
Mbona amependelewa sana kuzikwa na katekista, maana hua ni kimya kimya tu bila sala yoyote ile. Kwa kweli tulishukuru kanisa kwa heshima hiyo.
 
wafia dini mnafurahisha sana
Tena kuna wafia dini wa ajabu sana, Biblia zipo, maandiko yapo, mafundisho yapo, mfano mzuri ni kuhusu ibada za masanamu, watu wanawaaminia sana binaadamu, wanamtumikia shetani wakiaminishwa ni Mungu, bila wenyewe kujijua, sisi Wakatoliki tuliojitambua, tunamwelewa sana mtu kama Ruge kukataa ujinga ujinga fulani in the name of Catholic Church, zimewekwa sheria kibao ati usipofanya hivi, siku ukifa hatukuziki!.
Tena kitu cha ajabu ni wanafanya Cherry picking, kwa kuangalia status.
Angalieni msiba huu wa kigogo huyu walifanya nini na sikilizeni rais Magufuli alisema nini juu ya mtu huyu na bado alizikwa kwa heshima zote za kanisa, tena kwenye Hilo mimi meshauri
"Pongezi Rais Magufuli Kuwa Mkweli Daima. Tuanzishe Church of Africa, Tuoe Wake Wengi, Tuzae Watoto Wengi?" - JamiiForums
P
 
Mtu akiishakufa kinachotakiwa ni kuusitiri mwili kaburini. Kuna watu wanaamini uongo kuwa kwa maombi ya viongozi wa dini yanaweza kumuepusha marehemu na adhabu au mustakabali wa ama aende mbinguni au aende motoni. Mustakabali ni wapi mtu ataenda unajengwa mtu anapokuwa hai. Ukishakufa hizi nyingine ni mbwembwe tu.

Juu ya wafu huenda wapi baada ya kufa, jibu lake linatolewa na Yesu mwenyewe katika Yohana 5:28; “Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu.” Yesu hapa anasema watu waliokufa wanabakia hapo hapo walipofia (kama haikuwezekana kuwazika) ama wanabakia makaburini (kama iliwezekana kuwazika) hadi yeye mwenyewe atakaporudi, bila kujali kama wanastahili hukumu ama wanastahili uzima wa milele.

Hakuna kinachofanyika sasa kwa watu waliokufa. Wanapumzika wakisubiri kufufuliwa siku ya mwisho. Siku hiyo Mungu atakaposhuka maiti zote zitainuka na kutoka makaburini na watakaotangulia kutoka watakuwa wale wenye haki. “Wafu wako wataishi, maiti zangu zitafufuka; amkeni, kaimbeni, ninyi mnaokaa mavumbini, kwa maana umande wako ni kama umande wa mimea, nayo ardhi itawatoa waliokufa.” (Isaya 26:19) “Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.” (1 Wathesalonike 4:16)

Baada ya wenye haki kufufuliwa ndipo watafuatia waovu (au wale ambao hawakumwamini Yesu). Hawa watafufuliwa kwa ajili ya kupokea hukumu yao ambayo Yesu aliwalipia pale msalabani lakini hawakutaka kuipokea kwa imani. “. . . Wakati wa kufunuliwa kwake Bwana Yesu kutoka mbinguni pamoja na malaika wa uweza wake katika mwali wa moto; huku akiwalipiza kisasi wao wasiomjua Mungu, na wao wasioitii Injili ya Bwana wetu Yesu; watakaoadhibiwa kwa maangamizi ya milele, kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa nguvu zake.” (2 Wathesalonike 1:7-9). Sababu ya waovu kuangamizwa inatajwa hapa kuwa ni kutomjua Mungu, na kutotii injili ya Bwana Yesu.

Hakuna atakayeangamizwa kwa sababu ya uwingi wa dhambi zake maana Yesu alizilipia dhambi hizo pale msalabani.Kristo alikuja duniani kulipa adhabu ya kifo kile kitakachowapata watakaokataa kumwamini. Na kwa kuwa Mungu hana sera ya kulazimisha viumbe wake kukubali anachowafanyia atakubaliana na uchaguzi wao wa kutengwa naye milele kwa maangamizo yale makuu ingawa alilipa kila kitu kwa ajili yao.

Juu ya hoja kuwa wenye waliokufa wanaendelea kuishi katika mfumo fulani unaowawezesha kuwasiliana na walio hai au kujua kinachoendelea katika maisha ya wanadamu, Maandiko Matakatifu yanapinga dhana hiyo. “Kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote, wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahauliwa.” (Mhubiri 9:5). Na kwa kuwa Yesu alisema waliokufa wanaendelea kukaa makaburini hiyo inaondoa uwezekano wa wao kuendelea kuishi. Ili binadamu aweze kuishi kunatakiwa muunganiko wa vitu viwili; kiwiliwili na pumzi ya Mungu. “Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.” (Mwanzo 2:7). Kifo kinapotokea pumzi hutoka na kiwiliwili kukosa uhalali wa kuendelea kuishi. “Pumzi yake hutoka, huurudia udongo wake, Siku hiyo mawazo yake yapotea.” (Zaburi 146:4)

Dhana kuwaa mtu anapokufa anaendelea kuishi zinalenga kuwafariji wafiwa kwa kuwapunguzia uchungu, ama zinalenga kuwahadaa wanadamu. Maana wengine kwa kutumia dhana hizo wamewatoza wafiwa wakiwaahidi kuwaombea marehemu wao na kuwatoa sehemu ya mateso. Njia sahihi ya kukabili uchungu wa kuondokewa na marehemu ni kukubali kuwa amekufa na hajui lolote na Mungu ndiye atakayeamua pa kumweka siku hiyo ya mwisho anapokuja kuhukumu wanadamu.
 
Mkuu pamoja na hayo. Nadhani wewe sio mgeni wa Sheria na Utaratibu wa Kanisa Katoliki.
Yes mimi ni Mkatoliki die hard ambaye niko Ukatoliki not only kwa sababu nilizaliwa Katoliki, bali kwa uamuzi kubaki Mkatoliki, ila nyingi ya sheria za kanisa ni sheria za dunia hii sio sheria za Mungu.
P
 
kama alikuwa aendi kanisani wala kwenye jumuiya why azikwe kwa heshima ya kikatoliki??? ana watoto nje ya ndoa na pia pengine awajabatizwa why apewe asichostaili kama mkatoliki??
Dahh...

Ama hakika hatuna budi kubadili mienendo yetu WAROMA WAKATOLIKI ...
 
Kwa mara ya kwanza leo umeandika uharo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yes mimi ni Mkatoliki die hard ambaye niko Ukatoliki not only kwa sababu nilizaliwa Katoliki, bali kwa uamuzi kubaki Mkatoliki, ila nyingi ya sheria za kanisa ni sheria za dunia hii sio sheria za Mungu.
P
Peleka ushenzi huko.....Kuna mkatoliki mbumbumbu kama wewe!!! We nenda kakanyage mafuta huko...

Shwain
 
Nahisi kama ameonewa huruma flani

Kwa msimamo wa waroma ktk issue za Sacrament ..alipaswa kusindikizwa na mashairi ya Mpoto tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Yule katekista mpunga wa kutosha utakuwa ulisoma M pesa... Nyimbo zote waliimba wao wawili tu.
Mi hadi nikafikiri labda ni wa Anglican.
 
Unazungumzia ni heshima kwa Ruge au kwa waliobaki?

Kama ni heshima kwa marehemu Ruge mbona sasa hatoweza kujua kazikwa na nani hivyo hata haisaidii kwake.

Kama ni heshimu kwa waliobaki mbona haina maana yoyote kwao
...ni kama tu alivyosafirishwa kwa ndege. Angeweza kusafirishwa kwa lori.
....au kama alivyoagwa pale Karimjee, angeweza kuagwa pale Tandale kwa mfuga mbwa.
 
Asante Mkuu Pascal. Hili kanisa ni taasisi ya kibiashara na linafanya biashara na values zake ni mila na taratibu za kipagani za warumi. hivyo kama hukuwa mteja wake au mwanahisa wake watakubagua ile hatari. Halifuati biblia ,bali lina mafundisho yake ambayo ni kinyumbe na biblia. Mfano amri inayokataza kuchonga sanamu na kuziabudu wameiondoa kama ilivyo kwenye biblia na wakachukua ile ya kumi inayoongelea kuhusu kutamani wakaigawa zikawa amri mbili ,ili mradi idadi ya kumi itimie.
Huwa wanakiri hadharani kuwa muongozo wao siyo biblia tu ,bali wana mafundisho mengine au wana vyanzo vingine ya Imani.Lakini bado watu wanafikiri hili ni kanisa la kikristo.
Warumi walikuwa wanaua wakristo wa mwazoni, baadaye wakaona wanazidiwa, wakatumia kannuni inayosema '' if you can't fight them, join them''
Wakaamua kujiunga na Ukristo wa staili ya aina yake na mafundisho yake ya mila zao yakachukua nafasi ya biblia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…