TANZIA Ruge Mutahaba afariki Dunia! Azikwa kishujaa kwao Kabale, Bukoba

TANZIA Ruge Mutahaba afariki Dunia! Azikwa kishujaa kwao Kabale, Bukoba

Kama zilivo desturi za kichaga na kihaya mara nyingi mtu mzima anapofariki msiba huwekwa nyumbani kwake, na Kama ni mtoto basi msiba huwa kwa wazazi wake, sijaelewa kwanini Kaká yetu mpendwa wameamua kupeleka msiba kwa baba na si kwake, au labda ni kutokana na ukubwa wa msiba wenyewe kwa wa Tanzania.

Mwenyezi Mungu amlaze mahali pema peponi
Hata kama ni mtu maarufu sio kila jambo lazima liwahusu jamani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ungewaza na kufikiri kabla ya kuweka hii mada
Amewaza vizuri tu.Yawezekana tumemuelewa kila mmoja kwa namna yake.Kwa Afrika(Tanzania) anapofariki mtu mzima tunategemea azikwe kwake au eneo lake la nyumba.Namaanisha kwamba msiba upokewe nyumbani kwake na shughuli zote za msiba zifanyike hapo kwake.Sina uhakika kwamba makabila yote huamini na kufuata utaratibu huo.
Huwa tunategemea anayezikwa nyumbani kwa wazazi ni yule ambaye bado ni mtoto kiumri au yule ambaye kwa sababu maalumu atazikwa huko kwa wazazi.Ni jambo la kuelimishana tu.Hata hivyo taratibu za misiba na mazishi zinaweza kuwa zinatofaitiana kutoka jamii moja hadi nyingine.
 
Kama zilivo desturi za kichaga na kihaya mara nyingi mtu mzima anapofariki msiba huwekwa nyumbani kwake, na Kama ni mtoto basi msiba huwa kwa wazazi wake, sijaelewa kwanini Kaká yetu mpendwa wameamua kupeleka msiba kwa baba na si kwake, au labda ni kutokana na ukubwa wa msiba wenyewe kwa wa Tanzania.

Mwenyezi Mungu amlaze mahali pema peponi
Mbona Watanzania tunakuwa na dukuduku ya kuzungumzia vitu ambavyo havina tija? Wewe yakuhusu nini wapi msiba unapofanyika kufuatana na maamuzi ya ndugu? Kama hapo kwake hapatoshi (ama kwa kukosa mtu wa kufuatilia shughuli yenyewe au kwa sababu nyingine yo yote) kwa baba yake ndiyo mahali mbadala kwani yeye ndiye amefiwa na mtoto.
 
Kama ni mtoto basi msiba huwa kwa wazazi wake.

Mwenyezi Mungu amlaze mahali pema peponi

Umesha jijibu mwenyewe.
Ila, ki-uhalisia, ni kweli ilitakiwa, msiba uwe kwake, lakini kwa vile tunaambiwa hakuwa na FAMILIA, ikimaanishwa MKE na WATOTO ambao angekuwa anaishi nao hapo nyumbani kwake. Pia, kama wazazi wake wasingekuwa nao wanaishi hapo karibu yake, basi msiba huo ungeanzia hapo nyumbani kwake, kisha kuelekea huko kwa wazazi wake, kama ingeamuliwa kwenda kuzika huko!
 
Kama zilivo desturi za kichaga na kihaya mara nyingi mtu mzima anapofariki msiba huwekwa nyumbani kwake, na Kama ni mtoto basi msiba huwa kwa wazazi wake, sijaelewa kwanini Kaká yetu mpendwa wameamua kupeleka msiba kwa baba na si kwake, au labda ni kutokana na ukubwa wa msiba wenyewe kwa wa Tanzania.

Mwenyezi Mungu amlaze mahali pema peponi
Kuna tatizo hapa ambalo hata mimi nimeliona.... Ukiangalia route ya msafara wa marehemu toka airport mpaka Lugalo hospital, hakuna panapoonesha msiba utaenda kwake

Jr[emoji769]
 
Amewaza vizuri tu.Yawezekana tumemuelewa kila mmoja kwa namna yake.Kwa Afrika(Tanzania) anapofariki mtu mzima tunategemea azikwe kwake au eneo lake la nyumba.Namaanisha kwamba msiba upokewe nyumbani kwake na shughuli zote za msiba zifanyike hapo kwake.Sina uhakika kwamba makabila yote huamini na kufuata utaratibu huo.
Huwa tunategemea anayezikwa nyumbani kwa wazazi ni yule ambaye bado ni mtoto kiumri au yule ambaye kwa sababu maalumu atazikwa huko kwa wazazi.Ni jambo la kuelimishana tu.Hata hivyo taratibu za misiba na mazishi zinaweza kuwa zinatofaitiana kutoka jamii moja hadi nyingine.
yaani unaweza kujenga au unakwako ila kama hauna ndoa bado ni mtoto kwa wazazi wako na bahati nzuri ana watoto na la kujiuliza kama hajafunga ndoa hiyo ibada itakuaje?
 
Kama mnavyojua Ruge Mutahaba ni mtoto wa Profesa Mutahaba wa Bukoba Vijijini, Tarafa ya Kiamutwara, Kata Karabagaine ,Kijiji Kabale, Kitongoji Kiziru -Muzira mbogo, Muhabarishaji yuko huko anatutumia updates moja kwa moja tunaweka hapa

Kwa wanaokaa maeneo ya Bukoba,
Eelekeo wa mazishi yatakapofanyika nyumbani kwao Mutahaba kama watokea mjini, Ni Barabara ya kibeta kama waelekea Muleba, ukifika Magoti Km 3 kutoka Bukoba mjini utakutana na Kibao cha Gereza Rwamulumba, unapita Itahwa, Karabagaine ndo unafika kabale/kiziru kwa mzee Mutahaba, ni km 8 kutoka bukoba mjini,

Wadau mbali mbali wa maeneo yanayopakana na mazishi yatakapofanyika wameshaanza kukusanyika wakitokea
Nsisha, Kangabushro, Itahwa, Magoti,Kitwe, Katoma,Itahwa na Rwamulumba ,

Maoni ya watu waliowengi wanasema kwamba ni kweli jamaa alikuwa maarufu ila hawakujua kama ni wa maeneo hayo, kwasababu ukilinganisha jina lake na maendeleo ya eneo lile ni kama vile hakutenda haki, japokuwa wanasahau kwamba Ruge alikuwa ni mtu wa masuala ya burudani tu na mtu mmoja hawei kuleta maendeleo ya wilaya nzima isipokuwa wa kulaumiwa kama kuna ishu ya kulaumu ni Mzee Mutahaba mwenyewe na maprofesa wanaomzunguka,

Kwa haraha haraka pale kuna maprofesa si chini ya wanne, kuna mabalozi waliowahi kuwa mabalozi na walioko ubalozini kama mabalozi sasa si chini ya watano,

Kuna watu wengi sana ambao kwa pamoja wangeweza kushirikiana kuleta kinachostahili,

kwa Bahati mbaya aliyesema hivyo ni kwa mshtuko wa kuona kumbe mtoto wa Mutahaba ni maarufu vile lakin kwa haraka haraka maendeleo wanayo japokuwa binadamu huwa hawaridhiki na kuna slogan imeshajengeka kwamba wahaya wanajenga kwingine siyo kwao,,

SALAAMU ZA RAMBI RAMBI TOKA KWA MKUU WA MKOA WA KAGERA KWENDA KWA FAMILIA YA MUTAHABA

WhatsApp Image 2019-03-01 at 11.07.01.jpeg


Maandalizi ya Nyumba ya Milele ya Marehemu Ruge Mutahaba

WhatsApp Image 2019-03-01 at 11.07.02.jpeg




WhatsApp Image 2019-03-01 at 11.07.03.jpeg



TAIFA LIMEPOTEZA MOJAWAPO YA VIJANA WAPAMBANAJI

UPDATES

HABARI: Msemaji wa familia ya Mutahaba, Kashasha amesema Rais John Magufuli ametoa ndege kwa ajili ya kusafirisha mwili wa Ruge Mutahaba na waombolezaji siku ya Jumapili kwenda Bukoba atapozikwa-MCL

MKUU WA MKOA AWASILI MSIBANI NA KUKUTANA NA KAMATI YA MSIBA

IMG_20190301_135026.png


Hapo Ni Mmiliki wa Shule ya Josiah Grils Bwana Ruga Masabala akisalimiana na Afande alifika Msibani

IMG_20190301_134943.png

Mwonekano wa Juu wa Nyumbani kijijini kwa Ruge Mutahaba
IMG_20190301_134848.png
IMG_20190301_134848.png



 
mtoto kwa wazazi ndo kwao in case kapatwa aliyopatwa ruge kwa mazingira aliyomo
 
Back
Top Bottom