Ruge na Makonda wanapataneje na vipi nyasi zilizoumia?

Ruge na Makonda wanapataneje na vipi nyasi zilizoumia?

Mleta mada unashangaa nini?! Kwani hujui kuwa mpatanishi mkubwa wa vita kati ya Israel na Palestine ni USA?!
Na unajua fika jinsi USA na Israel zinavyowiva..! But ndo hivyo USA ipo katikati ikijinasibu kama msuluhishi wa ugonvi huu wenye zaidi ya miaka 50!

Ukiangalia mzozo huu wa Palestine na Israel umeisha?! Jibu ni hapana...! Sasa kwann mzozo kati ya Ruge (CMG) na Paul Makonda uishe..?!

Akili kumkichwa..!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kumbe inawauma sana mpaka wamekaa kupanga mpango hiyo!!!!!! Ruge ni mtoto wa mjini na namuomba azidi kubanaaaaaaaa mpaka mtu atupe matokeo.
 
ruge akikbubari kifala fala hivi, sitizami tena runinga yao mimi spendagi ujina kbsa!

sasa usipoangalia TV yake yeye anaathirika nini? humu nina unatumia feki,TV hauangalii, hata ukifa wala hawatajua

kinachokuumiza ni chuki
 
Na Zawadi B Lupelo

Wanajamvi salamu mbele!
Nimeona katika mtandao wa YouTube kile kinachoitwa kupatanishwa kwa Makonda na Ruge na mpatanishaji akiwa ni Rais John Pombe Magufuli. Naomba niweke maoni yangu hapa Jf na maoni haya yasitafsiriwe kuwa ninapinga watu kupatana wala kuishi kwa amani zaidi kushirikiana.

Makonda na Ruge wamekuwa katika mtanziko na hali ya kutokuelewana kwa muda wa miezi kadhaa sasa chanzo kikubwa kikiwa ni kile kinachodaiwa kwamba Makonda alivamia kituo cha utangazaji cha clouds tv na kupora vifaa kadhaa vya ofisi. Makonda alikwisha kanusha kuvamia clouds media katika kipindi chake alichojiandalia StarTv na kudai kwamba yote aliyoyaongea Ruge ni uongo ametunga akaenda mbali zaidi kusema Ruge hajui kitu zaidi ya utunzi wa story za mapenzi (kifupi msanii).

Wahenga wanasema mafahari wawili wagombanapo ziumiazo ni nyasi katika vita hii nyasi hazikukosekana. Mh Waziri Nape Mnauye ni mmojawapo katika juhudi za kutafuta ukweli na pengine suluhu la swala la Clouds media na Makonda yalimkuta ya kumkuta akaumia.
Kuna vyombo mbalimbali vya habari, watu binafsi na taasisi zingine ambazo kwa kweli zilisikitishwa na na kitendo cha Makonda kuvamia kituo cha Clouds media na wakatoa msaada wa kulaani na zaidi vilisusia kuandika habari za Makonda na mbali na vitisho vilivyotolewa na Rais ( refer "watch it")

Kubwa zaidi ni TEF (Jukwaa la Wahariri) lilisimama kidete katika hili kuhakikisha haki inatendeka kwa clouds media.

Jambo Kubwa la kunote wakati yote haya yanatokea mpatanishi (Rais Magufuli) aliamua kuegemea upande mmoja hii haijawahi kuwa sifa ya msuluhishi mahali popote pale duniani. Msuluhishi anatakiwa kuwa impartial asiyeegemea upande wowote.

Magufuli alikwishatamka hadharani kwamba kinachoendelea kwenye mitandao (tuhuma dhidi ya Makonda) ni udaku na yeye hasikilizi udaku. Hakuishia hapo alienda mbele zaidi na kutangaza interest kuwa hatamtumbua Makonda wala hata fanya lolote lile. Kauli kama hii inadhihirisha alikubaliana na alichokifanya Makonda na wala hakua akijali lolote na huku ni kuegemea upande mmoja.

Leo hii Mbele ya hadhara mlolongo huu wa matukio unamalizwa kwa kushikana mikono watu wawili yaani Ruge na Makonda? Kweli kabisa bila maelezo yoyote?

Mpaka naandika haya kuna mambo yameishughulisha akili yangu kama ifuatavyo.

Kwanza, Rais Magufuli katika mgogoro huu hakupaswa kuwa msuluhishi kwani alishaonesha upande hii inayofanywa ni danganya toto kwa Ruge.

Pili, swala hili lilipaswa sasa lisiwe mikononi mwa Clouds media na Ruge tena maana lilikwishafika kwenye chombo kinachohusika na vyombo vya habari TEF.

Tatu, Ni lazima umma uambiwe wanachopatana Ruge na Makonda ni nini ni ishu ya uvamizi au walikwaruzana mambo mengine barabarani? Na kama ni ishu ya uvamizi lazima tujue kwanza ukweli ni nani mkosaji ambaye anaomba radhi ili asamehewe? Je wanasameheana kwamba walikoseana Ruge alikosa nini na Makonda alikosa nini? Isijekuwa anayesamehewa ni Ruge kwa kumsingizia Makonda.

Je kuanzia sasa Clouds media wataanza kurusha habari za Makonda vipi kuhusu TEF na washirika wao?.
Vipi kuhusu Nape Mnauye? Na wengine walioumia kama nyasi remedy yao ni ipi?

Unless tupate maelezo kuwa kuna mazungumzo ya siri ya kuwapatanisha na mwenye makosa amefahamika na ameomba msamaha kilichofanyika ni kizungumkuti tu na kuuziana mbuzi kwenye gunia.

Zawadi B. Lupelo


Sent using Jamii Forums mobile app

unahitaji uponyaji

TV ya Ruge ni ya binafsi, ugomvi wake na makonda ni wake na wao wanajuana. Makonda ni mwenyeji wa clouds, alikuwa anashinda pale anakula pale na kupiga story pale...swala la kuvamiwa mlivyolibeba kishabiki ndo aibu hizi


sasa mkuu unaandika nakala ndeeeefu, kana kwamba ugomvi ule unakuhusu !!!!


umejaa chuki,roho mbaya na una gubu....unakomaa kwenye keyboard eti unataka maelezo! mwenye TV kapanda pale na wameshikana mkono na alichofanya Magu ni ubaba/Fatherly action....wala sio eti aseme tatizo nini,

wewe ni nani nchi hii mpaka una demand maelezo, wenzako wanaoona aibu kama wewe wako kimya!
 
Kama account Ile ya Instagram ni ya Nape basi hata nusu kaputi haiwezi kusaidia kutuliza maumivu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ukweli Nape anaugulia maumivu yasiyoelezeka mkuu,hadi wakati mwingine namuhurumia kwasababu alikuwa upande wa haki wakati huo!

Lakini leo imeendelea imedhihirika wazi media zilipaswa kumsusia nani.

Kumsusa RC ni ile tu baba amekuudhi basi kwakuwa huwezi kumpiga baba unaenda kumtwanga mdogo wako!
 
unahitaji uponyaji

TV ya Ruge ni ya binafsi, ugomvi wake na makonda ni wake na wao wanajuana. Makonda ni mwenyeji wa clouds, alikuwa anashinda pale anakula pale na kupiga story pale...swala la kuvamiwa mlivyolibeba kishabiki ndo aibu hizi


sasa mkuu unaandika nakala ndeeeefu, kana kwamba ugomvi ule unakuhusu !!!!


umejaa chuki,roho mbaya na una gubu....unakomaa kwenye keyboard eti unataka maelezo! mwenye TV kapanda pale na wameshikana mkono na alichofanya Magu ni ubaba/Fatherly action....wala sio eti aseme tatizo nini,

wewe ni nani nchi hii mpaka una demand maelezo, wenzako wanaoona aibu kama wewe wako kimya!
Mkuu, wakati mwingine jitahidi kuweka mahaba yako kando ili kuuficha ujinga wako.

Hili swala lilikuwa ni kawaida kabisa kubebwa kwa uzito huo maana halikuwahi kutokea Tanzania na waliolibeba walifanya hivyo katika kutetea uhuru wa habari na wanahabari kwa ujumla..

Tv kuwa ya Ruge hakuwafanyi watu wakae kimya wasipaze sauti pale uhuru wa habari na wanahabari unapoingiliwa maana ile media nzima hafanyi kazi Ruge peke yake

Na kikubwa zaidi ni kwamba leo wote mliokuwa mnabeza lile tukio na kujificha nyuma ya vita dhidi ya bange mmevuliwa nguo rasmi na kwa aibu mnapaswa mjifiche na msionekane, JPM kutaka Ruge amsamehe RC ni kwamba ametambua ukubwa wa kosa alilofanya RC.

Kuombewa msamaha na rais sio kitu kidogo na wala hauombewi kwa kufanya kitu kidogo!
 
Makonda hana sifa za ukuu wa mkoa wa Dar. Namiss Ditopile sasa
 
Unaujiuliza maswali mengi.. hilo juu nenda polisi au mahakamani kama kuna mafaili au kupata namba za huko.

Hao wengine ndio waone kudandia issue kwa sabbau ya siasa zao wakifikiri walikuwa hawaonwi ndio wajifunze sasa. Sio kuingilia ya watu na kuwasukuma waweke yasiyo na hao TEF kufurahia kisa eti eanashilikiana na yule waziri aliyepita...kumbe wao mambo ya siasa kutaka kumshusha RC..

JPM hawamjui kuwa yupo dakika 5 mbele yao.

Hongera kwa marafiki kwa kushikana mikono leo. Wasipomrusha kutupa habari za Dar kwenye media zao.. basi wanajitakia wao ku...

Ila Makonda mnamoenda jamani leo amekuwa gumzo bab kubwaaaaaaaaa kama kawaida..

Makonda oyeeeeeee
naapa sijawahi kumuelewa huyu dada

be___blessed
 
huu ugomvi ulishakua solved, pale kwa stage ni kuonyesha tu watanzania kinachoendelea

be___blessed
 
History is a very good teacher "once a zero brain always a zero brain" Nimechoka aibu sana kudhani upo upatanishi hapo. Haupo bali ni usipomshika mkono unapimwa mkojo. Basi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom