Rukwa: Ujenzi wa mradi wa barabara ya Ntendo-Muze-Kilyamatundu (Km 179) kwa kiwango cha lami

Rukwa: Ujenzi wa mradi wa barabara ya Ntendo-Muze-Kilyamatundu (Km 179) kwa kiwango cha lami

Pfizer

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2021
Posts
590
Reaction score
807
Serikali ya Tanzania kupitia TANROADS inajenga mradi wa barabara ya Ntendo- Muze-Kilyamatundu (Km 179) mkoani Rukwa kwa kiwango cha lami.

Screenshot_20230430-205724.png


Akizungumza mara ya baada ya kutembelea mradi huo, unaojengwa na kampuni ya China Geo – Engineering
Corporation Ltd (CGC) leo Aprili 30-2023 Waziri Ujenzi na Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa amesema mradi huo unajengwa kwa awamu ambapo awamu ya kwanza ni ujenzi wa KM 25 kwa gharama ya Shilingi bilioni 45.299.

Screenshot_20230430-205706.png


Amesema Rais wa Tanzania Mheshimiwa Dkt Samia Suluhu Hassan anafanya kazi kubwa sana na mpaka sasa hakuna mradi wowote Nchini ambao umesimama kwa sababu Mkandarasi hajalipwa, wote wanalipwa kwa wakati na kazi kwenye miradi ya barabara na miradi mingine wanaendelea kulipwa.

Screenshot_20230430-210340.png


"Hivi karibuni Serikali kupitia TANROADS tunakwenda kusaini miradi ya EPC plus Finance, tutasaini zaidi ya kilometa 2000 kwa wakati mmoja, haijawahi kutokea tangu Nchi hii iundwe, wastani kwa mwaka tulikuwa tunasaini miradi ya kilometa 150/160 Tanzania nzima kwa upande wa barabara, lakini sasa tunakwenda kusaini Km 2000 kuunganisha mikoa yote, tuendelee kumpa ushirikiano Rais wetu na kuhakikisha miradi hii inakwenda vizuri" amesema Waziri Mbarawa.

Screenshot_20230430-205643.png


Akitoa taarifa fupi ya mradi Mtendaji Mkuu wa TANROADS Mhandisi Rogatus Mativila amesema Mradi huo unaanzia kwenye Kijiji cha Ntendo kwenye makutano ya barabara kuu ya Sumbawanga - Mpanda na barabara ya Mkoa ya Ntendo – Muze na kuishia Kijiji cha Kizungu.

Screenshot_20230430-210403.png


Amesema barabara hiyo inapita eneo lenye fursa mbalimbali za kiuchumi ikiwemo kilimo, ufugaji,uvuvi, uchimbaji madini (makaa ya mawe) na uchimbaji wa gesi na kwamba barabara hiyo inaunganisha mikoa ya Songwe, Rukwa na Katavi kupitia bonde la Ziwa Rukwa, ambayo ni maeneo muhimu kwa shughuli za Kilimo, Ufugaji na Uvuvi.

Screenshot_20230430-205621.png


Ameongeza kuwa ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa Kilomita 25, upana wa mita 9.5, mita 1.5 kila upande ni kwa ajili ya watembea kwa miguu na mita 6.5, kwa ajili ya magari na kwamba Utekelezaji wake umefikia asilimia 23.

Aidha muda wa mradi huo ambao ujenzi wake unajumuisha pia ujenzi wa makalavati makubwa 17 na makalavati madogo 43, ni miezi 18, umeanza tarehe 6 Juni 2022 na unategemewa kukamilika Disemba mwaka 2023.

1682877262428.jpg
 
Aiseee kwamba tunakopa Marekani afu twazipeleka China
 
Hivi karibuni Serikali kupitia TANROADS tunakwenda kusaini miradi ya EPC plus Finance, tutasaini zaidi ya kilometa 2000 kwa wakati mmoja, haijawahi kutokea tangu Nchi hii iundwe, wastani kwa mwaka tulikuwa tunasaini miradi ya kilometa 150/160 Tanzania nzima kwa upande wa barabara, lakini sasa tunakwenda kusaini Km 2000 kuunganisha mikoa yote, tuendelee kumpa ushirikiano Rais wetu na kuhakikisha miradi hii inakwenda vizuri" amesema Waziri Mbarawa.
Sisi makapuku tunampa ushirikiano mkubwa Sana huyo mama kwa kufanya kazi kwa nguvu zetu zote ili tupate mlo, maana mlo wetu unategemea juhudi zetu wenyewe. Msiompa ushirikiano ni nyie ambao milo yenu ipo tu hata msipofanya kazi kwa juhudi, mnaofisadi na kuiba pesa za misaada/mikopo, na kodi zetu kwa manufaa yenu binafsi. Laiti mngekuwa mnaishi kwa kufuata matamshi yenu hii nchi ingepiga hatua mbele haraka sana. Nyie wahuni, majizi, mafisadi, nk mnaturudisha nyuma.
 
Go mama Samia goooo!!!

Wkati haters wakiwa busy kulazimisha kulizima jjna lako na kulitukuza la mpendwa wao kila mara, we endelea kuwaumbua kwa vitendo tu bila neno lolote.......watakuja kukiri baadae huku wakilia kwa dhambi wanazozifanya sasa hivi.
 
Mama anafanya kazi, mikoa muhimu kuifungua kwa Sasa ni Rukwa, Katavi, na Kigoma. Rukwa na Katavi ni mikoa muhimu sana kwa chakula, ita stabilize bei sehemu nyingine za nchi.

Mama anafanya yote haya bila kelele.

Kazi iendelee.
Kazi zinaongea.
Kazi zinaonekana
 
Angekuwa ni yule mfu tungeona kwenye Tv kabeba nondo na nyundo na cement.

Mama kimya kimya!!!!
Nataman sana kumiliki mashamba rukwa
 
Ziambieni mamlaka hapo manispaa ziondoe hii aibu hapo mjini ... Hii ni takataka
Screenshot_20230501-084355_1.jpg
 
Angekuwa ni yule mfu tungeona kwenye Tv kabeba nondo na nyundo na cement.

Mama kimya kimya!!!!
Nataman sana kumiliki mashamba rukwa
Mama hana ujinga huo ,kwanza akitaka awe anazindua na kuweka mawe ya msingi Kila mradi hatiweza maana Kuna maelfu ya miradi Kila sekta na Kila Mkoa..

Sana sana hapo siku akija ziarani Rukwa labda aje kuifungua hiyo Barabara
 
Rukwa itafunguka kimaendeleo ikikamilika hiyo lami mpaka muze pia barabara ya lami kutoka Matai to Kasesya
Mzee haiishii Muze ila Kwa Sasa hiyo section ndio imeshaanza..
.Barabara nzima ni km 179 kutoka Sumbawanga/Ntendo-Muze-Ikemba-Kilyamatundu/Kamsamba(Rukwa/Songwe Border)
 
Back
Top Bottom