Rukwa: Watendaji Kata na Vijiji 93 watumia Milioni 162 za makusanyo ya Halmashauri kwa matumizi yao binafsi

Rukwa: Watendaji Kata na Vijiji 93 watumia Milioni 162 za makusanyo ya Halmashauri kwa matumizi yao binafsi

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
MKUU wa Wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa, Carlolius Misungwi, ametoa siku 16 kwa watendaji wa kata na vijiji kuhakikisha wanarejesha Sh. milioni 162 ambazo ni makusanyo ya halmashauri hiyo ambazo wanadaiwa kuzitumia kwa matumizi yao binafsi.

Amesema wakishindwa kurejesha fedha hizo, watakamatwa na Jeshi la Polisi kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.

Misungwi alitoa agizo hilo jana kwenye kiako cha Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo lililoketi kwa ajili ya kupitisha mpango na bajeti ya mwaka wa fedha wa 2021/22.

Alisema kuwa tangu halmashauri hiyo ilipoanza utaratibu wa kukusanya mapato kwa mashine za kielekroniki na kuyapeleka benki, watendaji hao wamekuwa na tabia ya kutopeleka fedha hizo benki, badala yake wamekuwa wakitumia fedha mbichi kwa matumizi yao binafsi.

Misungwi alisema katika halmashauri hiyo, watendaji 93 wametumia Sh. 162,742,350 (milioni 162.7), hivyo kuwataka wazirudishe kabla ya Februari 28, vinginevyo ataliagiza Jeshi la Polisi kumkamata kila mtendaji anayedaiwa.

"Ninaagiza kuanzia leo (jana) hadi Februari 28, kila mmoja arudishe kiasi cha fedha anazodaiwa, ikipita tarehe hiyo nitampa orodha OCD inayoonyesha kila mtendaji kiasi anachodaiwa na kijiji alichopo na nitamwagiza amkamate ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake," alionya.

Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo, Daud Sichone, alisema baraza linaunga mkono agizo la Mkuu wa Wilaya huyo kwa kuwa halipo tayari kuona watendaji wa serikali wanaongoza kuhujumu kodi za wananchi.

Alisema kuwa tangu mwaka 2017, fedha ambazo hazijapelekwa benki kutokana na makusanyo hayo ni Sh. milioni 300 na kwamba baadhi ya wadaiwa wameshastaafu, wengine wamefariki dunia na wengine kufukuzwa kazi kwa makosa mbalimbali.
 
Mshahara wa mtendaji wa kijiji 390K, acha wajilipe na wao ha ha ha.
 
Ndio maana mwenyekiti wao alikuwa analalamika kuwa wapinzani wanamchelewesha (kumbe walikuwa wanamchelewesha kuiba), maana alijua kuwa wapinzani hawangekubali wizi kama huo.
 
Amesema wakishindwa kurejesha fedha hizo, watakamatwa na Jeshi la Polisi kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.
Wangekuwa ni wa vyama vya upinzani wangeshakuwa ndan siku mingi, ila kwa kuwa ni wenzetu basi tunawapa muda wa kurejesha.
 
Wingi wa wapendwa wa kanda yetu ambao ni ma DC, RC, DAS, DED na RAS unafurahisha kwa kweli.
 
Mnataka watendaji wa vijiji wasihonge mapisi?

Waachane aisee!!

Nao wanapenda kupata sukari kama ya Zuchu.
 
Miongoni mwa halmashauri mbovu na za hovyohovyo ni pamoja na hiyo Kalambo.

Kuanzia mbunge wao mpaka hao vilaza madiwani hawajitambui.

Yanaleta ujinga ujinga tu badala ya kubuni vyanzo vingi vya mapato katika halmashauri.

Vivutio vya utalii vipo vya kutosha mfano Kalambo falls lkn hakuna juhudi zozote za kuitangaza na pia kutengeneza miundombinu rafiki ili kuweza kuwavutia watalii.
 
Ukiona mtu anashabikia CCM au ni kiongozi wa CCM jua anamaslai yake ndani.Hao ndio CCM mbele Kwa Kwa mbeke,
 
Kwa hesabu za haraka ni kila Mtendaji amekula almost 1,700,000 ambayo wakisema wakatwe kwenye mishahara yao itachukua miezi 12 kama watalipa shilingi 150,000 kwa mwezi.

Mtu amepiga hesabu miaka 6 ya JPM hajapata annual increment hivyo ameamua kujilipa.

Athari za mitano tena
 
Miongoni mwa halmashauri mbovu na za hovyohovyo ni pamoja na hiyo Kalambo.
Kuanzia mbunge wao mpaka hao vilaza madiwani hawajitambui.

Yanaleta ujinga ujinga tu badala ya kubuni vyanzo vingi vya mapato katika halmashauri.

Vivutio vya utalii vipo vya kutosha mfano Kalambo falls lkn hakuna juhudi zozote za kuitangaza na pia kutengeneza miundombinu rafiki ili kuweza kuwavutia watalii.
Watu wengine kama wewe ni mahodari wa kuropoka! Yaani kwa akili zako timamu kuna mtalii kutoka ng'ambo anaweza kufunga safari kuja kushangaa Kalambo falls? Vitu vingine mnavikuza bila uelewa mpana, Kalambo falls sana sana inawafaa ninyi wenyeji kwenda kufanya picnic.
 
Watu wengine kama wewe ni mahodari wa kuropoka! Yaani kwa akili zako timamu kuna mtalii kutoka ng'ambo anaweza kufunga safari kuja kushangaa Kalambo falls? Vitu vingine mnavikuza bila uelewa mpana, Kalambo falls sana sana inawafaa ninyi wenyeji kwenda kufanya picnic.
Huwa sibishani na nguruwe sawa
 
Ndio maana mwenyekiti wao alikuwa analalamika kuwa wapinzani wanamchelewesha (kumbe walikuwa wanamchelewesha kuiba), maana alijua kuwa wapinzani hawangekubali wizi kama huo.
Hahaha umeua
 
Iyo pesa ni mdogo sanaa maana hapo ni sawa kila myendaji kala shil Mil 1 tu
 
Back
Top Bottom